HOT MEDIA

HOT MEDIA Entertainment/Lifestyle
Hot media | Sport news | Breaking news
Link in our Bio📌
HOT MEDIA 👇👇👇
htt

17/01/2026

Klabu ya Sima Sc imemtangaza rasmi mchezaji mpya kiungo mshambuliaji Libasse Gueye leo January 17 2026.

Huyu ndiyo mchezaji mpya wa simba.
17/01/2026

Huyu ndiyo mchezaji mpya wa simba.

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, ameongoza kwa kishindo katika uchaguzi wa urais uliofanyika Alhamisi, akiwa mbali mbele...
17/01/2026

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, ameongoza kwa kishindo katika uchaguzi wa urais uliofanyika Alhamisi, akiwa mbali mbele ya mpinzani wake mkuu Bobi Wine, ambaye chama chake tayari kimeanza kuhoji uhalali wa matokeo.

Takwimu zilizopo hadi sasa zinaonesha Museveni akiwa na asilimia 75 ya kura, huku Wine akiwa na asilimia 21, kwa mujibu wa matokeo kutoka asilimia 70 ya vituo vya kupigia kura.

Chama cha Wine kilisema kwenye mitandao ya kijamii kuwa helikopta ilitua katika eneo la nyumba yake jijini Kampala na kwamba “alichukuliwa kwa nguvu na kupelekwa kusikojulikana.”

Mtandao wa intaneti umezimwa, jambo linalofanya iwe vigumu kuthibitisha madai hayo. Polisi wa eneo hilo waliiambia BBC kuwa hawakuwa na taarifa zozote kuhusu tukio hilo.

Hapo awali, Wine alisema kuwa amewekwa chini ya kizuizi cha nyumbani, huku vikosi vya usalama vikizingira makazi yake.

Katika hatua hiyo, msemaji wa polisi Kituuma Rusoke aliliambia shirika la utangazaji la ndani NBS kwamba k**a mgombea urais, Wine alikuwa “mtu wa kuangaliwa”, na akaongeza kuwa uwepo mkubwa wa usalama kuzunguka nyumba yake ulikuwa kwa usalama wake mwenyewe.

Baadhi ya waandishi wa habari wa ndani walisema kuwa vikosi vya usalama vilikuwa vimewazuia kufika nyumbani kwa kiongozi huyo wa upinzani katika eneo la Magere, jijini Kampala.

Wine pia aliwaambia wafuasi wake wapuuze “matokeo ya uongo” yaliyotangazwa, akisema kuwa mamlaka “zinaiba kura”. Hakutoa ushahidi wowote kuhusu madai yake, na mamlaka husika hazijajibu tuhuma hizo.

Takribani wafuasi saba wa upinzani nchini Uganda wameuawa katika vurugu zilizotokea usiku kucha katika mazingira yanayoz...
16/01/2026

Takribani wafuasi saba wa upinzani nchini Uganda wameuawa katika vurugu zilizotokea usiku kucha katika mazingira yanayozua mabishano makubwa ya kisiasa, wakati Rais Yoweri Museveni akiongoza kwa kiwango kikubwa katika matokeo ya awali ya uchaguzi wa urais uliofanyika Alhamisi.

Kwa mujibu wa upinzani, wafuasi wao walishambuliwa na vikosi vya usalama walipokuwa wamekusanyika katika makazi ya mbunge wa upinzani Muwanga Kivumbi huko Butambala, takribani kilomita 55 kusini-magharibi mwa mji mkuu Kampala.

Hata hivyo, polisi wamekanusha madai hayo na badala yake kuilaumu upinzani kwa kuchochea vurugu.

Tume ya Uchaguzi ilitangaza Ijumaa mchana kuwa, kwa kuzingatia matokeo kutoka asilimia 60 ya vituo vya kupigia kura, Rais Museveni alikuwa anaongoza kwa asilimia 75 ya kura zote zilizohesabiwa, akifuatiwa na kiongozi wa upinzani Bobi Wine kwa asilimia 21.

Akizungumza na shirika la habari la AFP, Mbunge Muwanga Kivumbi alisema askari na polisi walifyatua gesi ya kutoa machozi na baadaye risasi za moto dhidi ya mamia ya watu waliokuwa wakifuatilia matokeo ya awali katika makazi yake.

Alidai kuwa watu kumi waliuawa ndani ya nyumba yake.

Madai hayo yalithibitishwa na mwanaharakati wa haki za binadamu, Agather Atuhaire, katika mazungumzo na shirika la habari la Reuters.

Hata hivyo, msemaji wa polisi wa eneo hilo, Lydia Tumushabe, amepinga kauli hizo akisisitiza kuwa polisi walilazimika kutumia nguvu kwa kujilinda baada ya kile alichokitaja k**a shambulio la “kundi la wahuni wa chama cha NUP” dhidi ya kituo cha polisi, pamoja na mpango wa kuvamia kituo cha kujumlisha kura.

Alidai kuwa washambuliaji walikuwa wamejihami kwa mapanga, mashoka na vifaa vya kuwasha moto, na kwamba angalau watu saba walipoteza maisha.

Wakati huohuo, waandishi kadhaa wa habari wa ndani wameripoti kuzuiwa na vikosi vya usalama kufika katika makazi ya kiongozi wa upinzani Bobi Wine, yaliyoko eneo la Magere, Kampala.

Chama cha NUP kilidai kupitia mtandao wa X kuwa maafisa wa usalama walivuka uzio wa makazi hayo kinyume cha sheria na kuanza kuweka mahema ndani ya kiwanja chake.

Kwa upande wake, msemaji wa polisi Kituuma Rusoke aliambia kituo cha televisheni cha NBS kuwa Bobi Wine, k**a mgombea wa urais, alikuwa “mtu wa kuzingatiwa,” akiongeza kuwa uwepo mkubwa wa vikosi vya usalama katika eneo la makazi yake ulikuwa ni kwa lengo la kuhakikisha usalama wake binafsi.

Tukio hili limeongeza mvutano wa kisiasa nchini Uganda, huku mashirika ya haki za binadamu na wadau wa demokrasia wakitaka uchunguzi huru na wa haraka kuhusu vifo na matumizi ya nguvu katika kipindi cha uchaguzi.

Kuminywa kwa huduma za intaneti kunakotekelezwa na serikali za Iran na Uganda kumezalisha shinikizo kwa raia wao kutafut...
16/01/2026

Kuminywa kwa huduma za intaneti kunakotekelezwa na serikali za Iran na Uganda kumezalisha shinikizo kwa raia wao kutafuta mbinu mbadala za mawasiliano, hali iliyochangia kuongezeka kwa matumizi ya mtandao wa Bitchat.

Mtandao huo, unaomilikiwa na mwanzilishi mwenza wa Twitter, Jack Dorsey, hauhitaji intaneti wala kadi ya simu ili kuwaunganisha watumiaji.

Badala yake, unatumia teknolojia ya Bluetooth kuruhusu ujumbe kusambazwa kutoka simu moja hadi nyingine hadi kufikia mlengwa anayekusudiwa.

Bitchat ilizinduliwa rasmi mwezi Julai 2025 na imekuwa suluhisho muhimu katika maeneo yasiyo na mawimbi ya intaneti au katika nchi ambako serikali zimezuia au kudhibiti upatikanaji wa huduma hiyo.

Mwaka huu pekee, programu hiyo imepakuliwa mara 28,000, idadi inayoashiria kukumbatiwa kwa kiwango kikubwa na watumiaji.

Nchini Uganda, kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu, kiongozi wa upinzani Robert Kyagulanyi, maarufu k**a Bobi Wine, aliwahimiza wafuasi wake kupakua Bitchat, akionya kuwa hatua ya serikali ya kuminyia intaneti ingewanyima fursa ya kufuatilia matokeo ya uchaguzi na maendeleo ya kisiasa kwa wakati.

Vilevile, Bitchat imepata umaarufu mkubwa miongoni mwa waandamanaji nchini Iran, ambako serikali imekuwa ikikata au kudhibiti intaneti ili kudhibiti maandamano yaliyoendelea kwa zaidi ya wiki moja.

Katika mazingira hayo, programu hiyo imekuwa nyenzo muhimu ya mawasiliano na uratibu miongoni mwa waandamanaji.

Kwa ujumla, mwenendo wa kuminywa kwa intaneti unaendelea kuongezeka duniani.

Kwa mujibu wa ripoti za mashirika ya haki za kidijitali Access Now na KeepItOn Coalition, visa 296 vya kufungiwa au kudhibitiwa kwa intaneti vilirekodiwa katika mataifa 54 mwaka 2024, ongezeko kubwa ikilinganishwa na visa 78 vilivyoripotiwa mwaka 2016.

16/01/2026

Hili kwasasa limekuwa wimbo kwa simba mpaka sasa bado haijulikani ni maamuzi gani yatafanyika katika klabu ya simba.

16/01/2026

SIMBA ANAONA ILI ANAENUNUA NI YANGA

K**a kweli hili ni tatizo

16/01/2026

UCHEZAJI WA STRICKERS NI MUHIMU KUUJUWA ILI UJUWE JINSI YA KUMTUMIA.

16/01/2026

Ivi ni kweli Selemani ni mchezaji mzuri zaidi ya Dube.?

Nyumba ya mgombea urais wa NUP, Robert Kyagulanyi, imezingirwa, kwa mujibu wa maafisa wa NUP.''Nyumba ya Bobi Wine imezi...
16/01/2026

Nyumba ya mgombea urais wa NUP, Robert Kyagulanyi, imezingirwa, kwa mujibu wa maafisa wa NUP.

''Nyumba ya Bobi Wine imezingirwa tangu jana jioni, hawezi kuwasiliana na mawakala wake wa uchaguzi. Iwapo amefanya kosa anapaswa kushtakiwa,kufikishwa mahak**ani na utaratibu wa kesi uanze kulingana na sheria. Nyumba yake haijarasimishwa kuwa ni kizuizi'' anasema Mweka hazina wa NUP, Benjamin Katana.

Hata hivyo, msemaji wa polisi Kituuma Rosoke amewaambia wanahabari kuwa hana ufahamu kuwa Kyagulanyi amezuiwa k**a inavyodaiwa na chama chake.

Mnamo mwaka 2021, katika uchaguzi mkuu Bobi Wine alishikiliwa na majeshi nyumbani kwake. Aliibuka wa pili na kura asilimia 35%. Ni hatua hiyo ambayo Marekani waliikemea wakitaja uchaguzi haukuwa wa hakina wazi, dai ambalo mamlaka za Uganda zilikanusha.

Haya yanajiri, huku matokeo ya uchaguzi mkuu yakiendelea kutangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Uganda, ikimuonyesha Museveni anaongoza kwa asilimia 76 ya kura zilizohesabiwa kutoka vituo vya kupigia kura 22,758.

Kwa mujibu wa mato

Shirika la haki za binadamu, Human Rights Defender, limeonyesha wasiwasi mkubwa kuhusu uwazi wa matokeo ya awali ya ucha...
16/01/2026

Shirika la haki za binadamu, Human Rights Defender, limeonyesha wasiwasi mkubwa kuhusu uwazi wa matokeo ya awali ya uchaguzi wa urais.

Kwenye taarifa yake ya mtandao wa X, Human Rights Defender imeeleza:

“Ukosefu wa ufuatiliaji na kutokueleza ni wilaya zipi matokeo yanatoka unasababisha wasiwasi mkubwa na unachochea madai ya hila ya kisiasa. Tunawataka waangalizi wa uchaguzi kuhakikisha wanarekodi na kuripoti kila tukio la ukosefu wa utaratibu kwa wakati halisi.”

Kwa mujibu wa tume ya uchaguzi Uganda EC Yoweri Museveni anaongoza kwa asilimia 76%.

Iwapo Museveni atashinda aitakuwa ni muhula wa saba akiwa madarakani. Inaaminika kuwa anapendelea mtoto wake wa kiume ambaye ni mkuu wa majeshi Uganda Muhoozi Kainerugaba kumrithi, hata hivyo alikana kuwa anamfunza mikoba ya uongozi.

Matokeo ya Urais kutangazwa Jumamosi ya tarehe 16 Januari 2026.

16/01/2026

Kuhusu poshy Queen na harmonize ukweli ni huu.

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

09:00 - 17:00

Telephone

+255717876945

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when HOT MEDIA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share