22/04/2026
MTOTO AIBIWA, AKUTWA AMETELEKEZWA MAKABURINI
Na Ally Mandai.
Mtoto mwenye umri wa miaka mitatu na miezi kumi wa jinsia ya k**e aliripotiwa na mama yake kuwa ameibiwa kwa kubebwa kwenye pikipiki na mtu asiyejulikana katika eneo la Kona ya Bwiru, Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza amepatikana baada ya kuokotwa na Wasamaria wema.
Taarifa ya leo Aprili 21, 2026 iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza imeeleza kuwa mnamo Aprili 18 mama mzazi wa mtoto huyo aitwaye Neema Julius Sesela, mwenye umri wa miaka 19, mama lishe na mkazi wa mtaa wa Nyampala โBโ, Kata ya Nyamanoro, Wilaya ya Ilemela aliripoti katika Kituo cha Polisi Kirumba kuibiwa kwa mtoto huyo ambaye jina lake linahifadhiwa kwa sababu za kisheria.
Tukio hilo lilitokea Aprili 18, 2026 mtaa wa Barabara ya Vumbi, Kona ya Bwiru, Wilaya ya Ilemela wakati mama huyo akiwa katika shughuli zake, aligundua kuwa mtoto ameibiwa na mtu huyo aliyeondoka naye kwa kutumia usafiri wa pikipiki ambayo hata hivyo namba zake za usajili hazijafahamika.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo uchunguzi wa tukio hilo ulianza mara moja kwa kuwahoji watu mbalimbali wenye ufahamu kuhusu tukio hilo ambapo mkazi mmoja wa eneo hilo aliweza kutoa โCCTV footageโ iliyoonesha mtu mmoja wa jinsia ya kiume akitoka katika eneo la tukio akiwa amempakia mtoto huyo kwenye pikipiki, ingawa namba zake za usajili hazikuweza kuonekana vizuri.
Mnamo Aprili 20, 2026 majira ya saa 3:30 usiku taarifa zilipatikana kuwa mtoto huyo alitelekezwa kwenye makaburi ya Nyasaka yaliyopo Wilayani Ilemela kabla ya kuokotwa na Wasamaria wema na kumpeleka kwa mwenyekiti wa mtaa.
Jeshi la Polisi lilipata taarifa na kufika kwa ajili ya uchunguzi zaidi ambapo wazazi wa mtoto huyo na baba mzazi aitwaye Mwankunja Edward (30) fundi seremala, wote wakazi wa Ghana, mtaa wa Nyampala โBโ, Wilaya ya Ilemela, wamemtambua mtoto huyo kuwa ni mtoto wao huku uchunguzi wa afya ya mtoto ukiendelea kufanywa katika hospitali husika. ๐ญ๐ญ๐ญ
usisahau Kuni follow Easo TV