Taimediatz

Taimediatz Habari za ukweli na uhakika ndani na nje ya Tanzania kwa wakati sahihi.

16/09/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amewatakia kila la heri wachezaji na mashabiki wa timu za Simba na Yanga kuelekea mchezo wao wa Fainali ya Ngao ya Jamii utakaochezwa leo tarehe 16 Septemba, 2025 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.



  Masista wanne Wakarmeli Wamisionari wa Mtakatifu Theresia wa Mtoto Yesu, na Dereva wao, wamefariki kwa ajali ya gari i...
16/09/2025

Masista wanne Wakarmeli Wamisionari wa Mtakatifu Theresia wa Mtoto Yesu, na Dereva wao, wamefariki kwa ajali ya gari iliyotokea katika eneo la Bukumbi, mkoani Mwanza, walipokuwa wakielekea uwanja wa Ndege, baada ya gari yao kugongana uso kwa uso na Lori majira ya saa5 usiku wa jana Septemba 15,2025.

Waliofariki ni, Sr. Lilian Kapongo (55), Mama Mkuu wa Shirika, Sr. Nerina Simeon (60), Katibu Mkuu wa Shirika na raia wa Italia, Sr. Damaris Matheka (51), Mkuu wa shule ya sekondari ya wasichana Bukumbi, Sr. Stellamaris Muthini (48), mtawa raia wa Kenya, Boniface Msonola (53), Dereva.

Masista hawa walienda jimboni (Kahama) kwa ajili ya Nadhiri za Daima za wenzao watatu, katika adhimisho lililofanyika siku ya Jumamosi. Jana asubuhi walianza safari kutokea Kahama kuelekea Mwanza kabla ya kurudi Dar es Salaam. Majira ya saa 5 usiku, wakiwa wanatokea kwenye Jumuiya yao Bukumbi - Mwanza kuelekea Uwanja wa Ndege, wakapata ajali na kufariki dunia.

Mtu pekee aliyenusurika na mauti katika ajali hiyo ni Sr. Pauline Mipata (20), Matron wa shule ya wasichana Bukumbi, ambaye hata hivyo amejeruhiwa vibaya na kwa sasa yupo chumba cha wagonjwa mahututi katika Hospitali ya Bugando.



16/09/2025
16/09/2025

Kaimu Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika, anaelezea sababu zilizopelekea kuwatoa katika chumba cha Mahak**a, mapema mara baada ya Kesi ya Uhaini ya Mwenyekiti wao Tundu Lissu, kuanza na kupelekea kesi hiyo kusimama kwa muda.



  Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Tundu Lissu amegoma kuendelea na kesi ya uhaini inayomkabili (kutokana na ratiba ya leo) h...
16/09/2025

Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Tundu Lissu amegoma kuendelea na kesi ya uhaini inayomkabili (kutokana na ratiba ya leo) hadi hapo hoja yake aliyoiwasilisha Mahak**ani hapo itakapotolewa uamuzi na jopo la Majaji watatu wanaosikiliza kesi hiyo wakiongozwa na Jaji Danstan Ndunguru

Baada ya Majaji kuingia kwenye chumba namba moja kwa ajili ya kuanza kusikiliza kesi hiyo kwa mujibu wa ratiba ya leo, Jumanne Septemba 16.2025, Lissu amewaeleza Majaji hao kuwa alipoingia kwenye chumba cha Mahak**a hajawakuta wafuasi wake na kwamba amepata taarifa kuwa wamegoma kutokana na baadhi ya wanachama wenzao kuzuiliwa kuingia Mahak**ani na maafisa wa Jeshi la Polisi wanaotekeleza amri ya ZCO,

Kutokana na hoja hiyo, Lissu ameomba Mahak**a kutoa muongozo wake wa haraka na kuhoji inawezekanaje ZCO anaawafukuza watu Mahak**ani na Mahak**a iko kimya?, pia amesema Majaji pekee ndio wenye mamlaka ya kutoa amri yoyote Mahak**ani sasa inawezekanaje mtu mwingine anatoa amri ndani ya viunga vya Mahak**a, amri ambazo pia zinakinzana na sheria na taratibu?

Baada ya kuwasilisha hoja hiyo, Lissu aliieleza Mahak**a kuwa hawezi kuendelea na kesi hadi suala hilo litolewe muongozo na Mahak**a, na kwamba hadi wafuasi wake waruhusiwe kuingia Mahak**ani

Baada ya kuwasilishwa kwa hoja hiyo, Wakili wa Serikali Mkuu Nassor Katuga aliiomba Mahak**a kuendelea ratiba ya usikilizwaji wa kesi kutokana na kwamba suala analowasilisha Lissu halina uhalisia, lakini pia Katuga amesema wafuasi hao walikuwepo kwenye chumba cha Mahak**a na wametoka muda mfupi kabla ya kesi kuanza



16/09/2025

Wanachama wa CHADEMA, wamesusia Kesi na kutoka kwenye chumba cha Mahak**a baada ya baadhi ya wanachama wenzao kuzuiwa kuingia Mahak**ani wakati Kesi ya Uhaini inayomkabili mwenyekiti wao Tundu Lissu ikiwa inaendelea Mahak**a Kuu Masjala ndogo ya Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika akizungumza na wanahabari leo, Jumanne Septemba 16.2025 amesema kuanzia mapema asubuhi ya leo mamia ya wanachama wao wamezuiliwa na Polisi kuingia Mahak**ani wakielezwa kuwa chumba cha Mahak**a namba moja ambacho kesi ya Lissu inafanyika kimejaa

Hata hivyo Mnyika amedai kuwa jambo hilo halina uhalisia kwakuwa chumba hicho hakijajaa na kwamba hata watu waliokuwepo kwenye chumba hicho wengi wao amedai kuwa ni askari waliovaa kiraia

Kufutia hilo, imeelezwa kuwa licha ya viongozi na makada wao kugomea kesi hiyo lakini bado wataendelea kubaki kwenye viunga vya Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam (lakini si kwenye chumba namba moja ambacho kesi ya Lissu inaendelea) ili kuona hatua za mwisho zitafikiwaje kwakuwa kwa sasa viongozi wa CHADEMA wakiongozwa na Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara Amani Golugwa wanaendelea na jitihada za kuwasiliana na uongozi wa Mahak**a kwa hatua zaidi

Sambamba na hilo, kupitia kwa Mawakili wanaomsaidia Tundu Lissu wamemfikishia taarifa hiyo mshtakiwa mwenyewe ili kabla ya kuendelea na ratiba yoyote iliyoko mbele yake leo awasilishe hilo Mahak**ani.



16/09/2025

Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro, limemk**ata mtu mmoja ka tuhuma za kumfanyia ukatili mfanyakazi wa kazi za ndani.

Tukio hilo limetokea baada ya picha mjongeo kusambaa kwenye mitandao ya kijamii kumuonesha mwanamke mmoja akiwa amejeruhiwa na baada ya uchunguzi wa awali ikaonekana amefanyiwa ukatili huo na waajiri wake.



  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaama Mhe Albert Chalamila alipotembelea soko la Kawe ambalo limeungua moto usiku wa kuamkia ...
15/09/2025

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaama Mhe Albert Chalamila alipotembelea soko la Kawe ambalo limeungua moto usiku wa kuamkia leo Septemba 15,2025 kuwafariji wafanyabiashara waliopoteza mali zao kutokana na ajali hiyo ambapo ameelekeza Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kutoa kiasi cha shilingi milioni miamoja k**a mkono wa pole

Akizungumza mara baada ya kutembelea soko hilo lililoteketea kwa moto kwenye eneo la kawe jijini Dar es aalaam RC Chalamila pamoja na kufikisha salam za pole kutoka kwa Rais Dkt Samia amesema soko hilo sasa litajengwa na Serikali kwa ubora na kwa haraka ili wafanyabiashara waendelee na biashara na kwamba kwa sasa wafanyabiashara wapelekwe eneo la viwanja vya shirika la nyumba NHC Tanganyika Perkas

Aidha RC Chalamila ameelekeza kuandaliwa takwimu za wafanyabiashara kwenye masoko yote ili yanapotokea majanga kuwe na takwimu sahihi za waathirika ambapo kwa soko hilo la Kawe kulikua na takribani wafanyabiashara elfu moja walioathitika hivyo ametaka Manispaa ya kinondoni kutoa milioni miamoja ya pole mapema Septemba 16, 2025

Kwa upande wake Katibu wa wafanyabiashara wa soko la Kawe Ndg Silvester Chidego ameshukuru Serikali kwa kutoa faraja kwa wafanyabiashara na kwamba fedha hizo milioni miamoja watazigawa kwa wafanyabiashara wote huku mmoja wa wazee wafanyabiashara wa soko hilo akiomba wadau kujitokeza kuwawezesha wafanyabiashara huku akitoa tahadhari kwa vibaka walioiba bidhaa za wafanyabiashara kuwa kuna dua maalum itasomwa

Soko hilo la kawe limeungua usiku wa Septemba 15, 2025 hivyo kuamkia Septemba 16, 2025 RC Chalamila ameagiza k**ati ya kuchunguza chanzo cha moto huo iwe imeundwa na ifanye kazi yake mara moja.


15/09/2025

Mwanasheria wa (CHADEMA) Wakili Dkt. Rugemeleza Nshala amesema baada ya mapingamizi yaliyokuwa yamewekwa na Mwenyekiti wa chama hicho Taifa Tundu Lissu dhidi ya Jamhuri katika kesi ya uhaini inayomkabili inayoendelea kwenye Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam kutupiliwa mbali, Mawakili wake sasa wanafikiria kuchukua hatua zaidi kuhusiana na hilo.

Akizungumza na wanahabari kwenye viunga vya Mahak**a hiyo leo, Jumatatu Septemba 15.2025, Wakili Dkt. Nshala amesema kwa sasa mtuhumiwa amesomewa mashtaka lakini hajajibu 'ndio' au 'hapana' badala yake ameomba kutoa maelezo yanayoonesha mapungufu yaliyopo kwenye hati ya mashtaka.



15/09/2025

Jeshi laPolisi kanda maalum ya dar es Salaam, limesema tukio lililotokea asubuhi ya leo katika viunga vya nje ya Mahak**a kuu lilikuwa Polisi wakituliza vurugu zilizokuwa zinafanywa na baadhi ya wanachama wa CHADEMA.

Akitoa taarifa hiyo Kamanda wa Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro, amesema kundi la Wanachama wa CHADEMA baada ya ukumbi uliokuwa unatumiwa kwenye kesi ya Tundu Lissu kujaa na hivyo baadhi ya wafuasi hao waliokuwa nje ya Mahak**a walianzisha fujo na kujaribu kuwashabulia askari ambao walijihami na kutuliza fujo hizo haraka.

Jeshi la Polisi linatoa wito kuwa kitendo chochote cha kuwachokoza askari kitashughulikiwa haraka na kuyarejesha mazingira ya usalama kwenye eneo husika haraka kwa kadiri inavyowezekana.



  Chama cha ACT-Wazalendo kimepinga na hakikubaliani na uamuzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) wa kumwondoa Mgo...
15/09/2025

Chama cha ACT-Wazalendo kimepinga na hakikubaliani na uamuzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) wa kumwondoa Mgombea Urais wa Tanzania kupitia chama hicho, Luhaga Mpina kwa kuwa uamuzi huo haujazingatia misingi ya sheria.

Chama hicho kimesema INEC imefanya maamuzi kwa kutumia uamuzi wa Msajili wa Vyama vya Siasa ambao chama hicho kimeukatia rufaa Mahak**a Kuu, hivyo haikupaswa kutoa uamuzi ikiwa jambo hilo bado lipo mahak**ani.

✍🏿

**akuu

15/09/2025

Tazama namna ambavyo Jeshi la Polisi nchini Tanzania, walivyowadhibiti wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), leo katika viunga vya Mahak**a Kuu masjala ndogo ya Dar es Salaam, wakati wakisubiri kuingia Mahak**ani kwa ajili ya kusikiliza kesi ya Mwenyekiti wao Tundu Lissu, anayekabiliwa na kesi ya Uhaini.

Polisi walionekana kutumia nguvu kwa ajili ya kuwatawanya wafuasi wa Chama hicho waliokuwa wamejitokeza kwa wingi tangu saa12 asubuhi ya leo Septemba 15, 2025.

✍🏿

**akuu

Address

Mwenge
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Taimediatz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share