04/06/2026
Benki ya CRDB kupitia CRDB Foundation, imeahidi kutoa zawadi zaidi ya shilingi milioni 100, kwa ajili ya mashindano ya Ndondo Cup kwa mwaka 2026, ikiwa ni msimu wa 13 tangu kuanzishwa kwake.
Zawadi hizo shilingi milioni 30, kwa mshindi wa kwanza, milioni 15 kwa mshindi wa pili , zawadi za milioni 100, pamoja na shilingi 100,000/- kwa mchezaji bora na shabiki bora kwenye kila mechi.
Akiongea wakati wa uzinduzi wa mashindano hayo ( Imbeju ndondo cup 2026), kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Saad Mtambule, ameipongeza Benki hiyo kwa kuendelea kuunga mkono bunifu mbalimbali za vijana nchini.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa CRDB Foundation, TullyEsther Mwambapa, amesema anataka kuona kijana atakayeshiriki Imbeju Ndondo Cup , anatoka hapo akiwa si mchezaji tu bali akiwa na maarifa zaidi, maono makubwa na fursa za kufanikiwa kimaisha.
✍🏿