Taimediatz

Taimediatz Habari saa 24/7
K**a una habari au Tangazo njoo Dm
Email: [email protected]

05/06/2026

Inawezekana msanii akiiona hii video anaweza kujikataa au kusema hii ni Ai.

Kwenye show yake iliyofanyika Mkoani Mwanza Alikiba alisema kuwa atatoa ngoma moja tu lakini mpaka sasa ameshatoa ngoma mbili ni takribani siku 61 toka atoe kauli hiyo.

Unafikiri nini kimembadilisha Alikiba hadi kutoa ngoma mbili katika kipindi cha muda mfupi hivi?

✍🏿

05/06/2026

Mchumba wa marehemu mwanamitandao wa Marekani, Ashly Robinson maarufu k**a Ashlee Jenae, Joe McCann, amevunja ukimya wake baada ya Jeshi la Polisi Zanzibar kutangaza kukamilika kwa uchunguzi wa kifo cha mpenzi wake na kubaini kuwa hahusiki kwa namna yoyote na tukio hilo.

Katika taarifa yake, McCann alisema kuwa ingawa matokeo ya uchunguzi yameweka wazi ukweli kuhusu kifo cha Ashly, hayapunguzi maumivu anayopitia kutokana na kumpoteza mtu aliyempenda. Alitumia methali ya Kiswahili inayosema, “Moyo ni k**a msitu, huwezi kuona yaliyomo ndani yake,” akieleza kuwa bado anaendelea kuomboleza msiba huo mkubwa.

✍🏿

04/06/2026

Benki ya CRDB kupitia CRDB Foundation, imeahidi kutoa zawadi zaidi ya shilingi milioni 100, kwa ajili ya mashindano ya Ndondo Cup kwa mwaka 2026, ikiwa ni msimu wa 13 tangu kuanzishwa kwake.

Zawadi hizo shilingi milioni 30, kwa mshindi wa kwanza, milioni 15 kwa mshindi wa pili , zawadi za milioni 100, pamoja na shilingi 100,000/- kwa mchezaji bora na shabiki bora kwenye kila mechi.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa mashindano hayo ( Imbeju ndondo cup 2026), kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Saad Mtambule, ameipongeza Benki hiyo kwa kuendelea kuunga mkono bunifu mbalimbali za vijana nchini.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa CRDB Foundation, TullyEsther Mwambapa, amesema anataka kuona kijana atakayeshiriki Imbeju Ndondo Cup , anatoka hapo akiwa si mchezaji tu bali akiwa na maarifa zaidi, maono makubwa na fursa za kufanikiwa kimaisha.

✍🏿

04/06/2026

Jeshi la Polisi visiwani Zanzibar limesema kifo cha Mwanamtandao wa Marekani, Ashly Robinson maarufu k**a 'Ashlee Jenae' kimetokana na kujinyonga kwasababu ya msongo wa mawazo.

Kauli ya Polisi inakuja ikiwa ni siku 57 zimepita tangu Ashlee kukutwa katika chumba chake cha Hoteli Visiwani humo, Aprili 8, 2026 akiwa amejinyonga.

Akitoa ufafanuzi leo Juni 4, 2026 kuhusu uchunguzi uliobainika kwenye tukio hilo, Naibu Kamishna wa Polisi Zanzibar ambae pia ni Naibu Kamishna wa Makosa ya Upepelezi Zanzibar, Zubeir Chembere amesema hakuna aliyebainika kumuua Ashlee zaidi ya kujinyonga kwa sababu ya msongo wa mawazo.

Chembere amesema uchunguzi ulibaini kwenye simu yake kulikua na jumbe zilizokuwa zikiashiria kutaka kujiua ikiwemo Ashlee kuiuliza Akili Mnemba (Chart GPT) kuhusu dawa kiasi gani anaweza kutumia ili kujitoa uhai wake.

Ashlee alienda Zanzibar akiwa na mumewe mtarajiwa Joe McCann.

✍🏿

04/06/2026

Mwanafalsafa wa Pan -African kutoka nchini Zimbabwe, Joshua Maponga, ameishauri Serikali ya Tanzania, kufungia usajili baadhi ya mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo yanahusishwa na kufadhili baadhi ya makundi ya watu waliochochea vurugu za wakati na baada ya uchaguzi 2025.

Maponga ameyasema hayo Leo Juni 4,2026 wakati anaongea na waandishi wa habari kuhusu ushiriki wa waandishi wa habari wa Tanzania kutoandika chochote kilichosababisha matukio ya Oktoba 29,2025 na siku zilizofuata .

Aidha ameshauri waandishi wa habari wa Tanzania, kufanya habari za kiuchunguzi kwenye mashirika hayo ili waone namna wamekuwa wakipokea fedha huku wakifanya mambo ya kishetani nyuma yake.

✍🏿

04/06/2026

Mwandishi wa habari kutoka nchini Nigeria, David Hundeyin, amesema vyombo vya habari vya CNN na BBC, ni vyombo vya Serikali ya Marekani ndio maana huwa wanawekeza kufanya habari za machafuko kuhusu Afrika huku wakiwa na ajenda fulani itakayowanufaisha siku za mbeleni.

Hundeyin ameyasema hayo Leo wakati anaongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusu makala ya machafuko yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 nchini Tanzania, na kusema kuwa vyombo vya CNN na BBC , vilifanya makala vikiwa na lengo fulani K**a zilivyofanya kwa mataifa mengine baadae vikanufaika.

Aidha amesema hakuna Taifa nje ya Afrika linaloweza kuwa na uchungu na nchi yako isipokuwa wewe mwenyewe hivyo tusikubali kuingia kwenye machafuko kwa maslahi ya makundi fulani ya watu.

✍🏿

03/06/2026

Benki ya CRDB, imezindua kampeni ya Kopa Kimpango wako, itakayowawezesha Watumishi wa umma kukopa hadi shilingi milioni 300 ndani ya saa 24, huku riba ikiwa imeshuka kutoka 17% hadi 16%.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo , Mkuu wa kitengo cha wateja binafsi, Stephen Adili, amesema mkopo huo hautahitaji kufika kwenye tawi la CRDB, bali kupitia mtandao unaweza kumaliza kila kitu kupitia mfumo wa ESS.

Aidha Adili amesema mkopo huo unaweza kulipwa hadi kwa kipindi cha 12 badala ya miaka 10 ilivyokuwa kwenye mikopo ya awali .

✍🏿

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Matukio tofauti ya Picha alipopokelewa na...
03/06/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Matukio tofauti ya Picha alipopokelewa na Mwenyeji wake Rais wa Shirikisho la Urusi Mhe. Vladimir Putin alipowasili Ikulu ya Jijini Moscow Leo Juni 03,2026.

✍🏿

03/06/2026

UKWELI WA MATUKIO YA OKTOBA

03/06/2026

K**anda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Muliro Jumanne Muliro amewapongeza Wakaguzi na Askari wa vyeo mbalimbali 32 waliofanya vizuri zaidi katika utendaji kazi za Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam.

Pongezi hizo zimetolewa leo Juni 02, 2026 katika viwanja vya bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay Kinondoni ambapo K**anda Muliro alimwakilisha Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Camillus Wambura ikiwa ni sehemu kutambua mchango wa askari hao katika kazi za Polisi.

Aidha, K**anda Muliro amewataka Maofisa, Wakaguzi na Askari wa vyeo mbalimbali kuendelea kutekeleza majukumu yao ya kusimamia sheria za nchi kwa kuzingatia sheria, nidhamu, weledi na ujasiri.

✍🏿

Address

Mwenge
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Taimediatz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share