Taimediatz

Taimediatz Habari za ukweli na uhakika ndani na nje ya Tanzania kwa wakati sahihi.

26/12/2025

Naibu Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesema Watanzania wameahidi kutoa shilingi milioni 100, kwa kila goli watakalofunga dhidi ya Uganda kwenye mchezo unaotarajiwa kuchezwa kesho Disemba 27,2025 nchini Morocco.

Makonda ameyasema hayo Leo Disemba 26,2025 Akiongea na wachezaji wa Taifa Stars kuelekea mchezo huo.

✍🏿
πŸ¦…

  Waziri wa Afya, Mohammed Nchengerwa, ameagiza uchunguzi wa haraka katika Hospitali ya Rufaa Mkoa ya Temeke, ili kubani...
26/12/2025

Waziri wa Afya, Mohammed Nchengerwa, ameagiza uchunguzi wa haraka katika Hospitali ya Rufaa Mkoa ya Temeke, ili kubani chanzo cha kuzimwa kwa mashine za X-ray na vitendo vya Rushwa vinavyoendelea katika Hospitali hiyo.

Gaia hilo limekuja siku chache baada ya taarifa kusambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu utendaji usiridhisha katika Hospitali ya Temeke, ikiwemo kuzimwa kwa mashine ya X-ray ambapo ufuatiliaji wa Siri wa Waziri wa Afya umebaini uwepo wa rushwa za waziwazi bila uoga.

✍🏿
πŸ¦…

26/12/2025

Msanii wa maigizo wa miaka mingi Elizabeth Michael, maarufu K**a Lulu, ameonesha namna sikukuu yake iliyoenda akiwa na watoto wake akilazimika kuingia kwenye michezo ya watoto.

Lulu amesambaza video hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram namna anafurahia na watoto wake.

✍🏿
πŸ¦…

26/12/2025

Nabii Ebo Noah, anayejulikana na wafuasi wake k**a β€œnabii” nchini Ghana, aliyetabiri mwisho wa Dunia utakuwa Disemba 25,2025 amesema kuwa baada ya maombi na kufunga kwa siku 21, alimwomba Mungu kuahirisha siku ya mwisho wa dunia na kudai kuwa ombi hilo lilikubaliwa.

Usiku wa kuamkia leo, Ebo Noah alijitokeza hadharani katika show ya King Sarks, ambapo aliwataka wananchi kuendelea kusherehekea sikukuu ya Krismasi, akisisitiza kuwa hakuna tukio lolote litakalotokea.

✍🏿
πŸ¦…

  Msanii maarufu wa Nigeria, Simisola Bolatito Kosoko maarufu kwa jina  anatarajia kupata mtoto wa pili na mume wake amb...
26/12/2025

Msanii maarufu wa Nigeria, Simisola Bolatito Kosoko maarufu kwa jina anatarajia kupata mtoto wa pili na mume wake ambaye pia ni Msanii mwenzie Adekunle Almoruf Kosoko maarufu kwa jina la Adekunle Gold.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram msanii Simi amesema picha akiwa na familia yake zinazoonesha kuwa wanatarajia kupata mtoto wa pili na kuacha ujumbe kwa mashabiki zake.
β€œMerry Christmas from the Kosokos πŸŽ„ All our love to you and we thank you for all your love to us”, aliandika Simi.

✍🏿
πŸ¦…

25/12/2025

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Jabiri Makame, amewezesha kijana mmoja kurejeshewa pikipiki yake iliyokuwa ikishikiliwa na mkandarasi aliyekuwa akijenga barabara mkoani humo, baada ya kushikiliwa kwa madai ya kupita katika barabara iliyodaiwa kuwa hairuhusiwi.

Kijana huyo akiwasilisha malalamiko yake mbele ya Mkuu wa Mkoa, amesema tukio hilo lilitokea tarehe 26 Julai, alipokutana na vijana wanne waliomsimamisha na kudai kuwa amepita katika barabara isiyoruhusiwa. Alieleza kuwa waliitaka faini ya shilingi laki moja na nusu, kisha wakachukua pikipiki yake na kuondoka nayo bila kumweleza ilikopelekwa.

Akijibu hoja hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Songwe alionyesha kushangazwa na kitendo cha kushikiliwa kwa pikipiki kwa muda mrefu bila maelezo ya kisheria, akisisitiza kuwa pikipiki hiyo irejeshwe mara moja.

β€œMimi nataka nione pikipiki ile hapa. K**a kuna uharibifu uliofanywa na hiyo pikipiki aje kuniambia. Lakini haiwezekani mtu akae na pikipiki ya mwananchi.

✍🏿
πŸ¦…

25/12/2025

Nabii wa Ghana anayejitambulisha kwa jina la Ebo Noah amedai kuwa Mungu ameahirisha uharibifu wa dunia kwa mafuriko, akieleza kuwa hatua hiyo imetokana na maombi na kuombea yaliyofanywa na watumishi wa Mungu.

Kupitia video iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, Ebo Noah amesema kuwa baada ya kufanya maombi makali, alipata maono mapya aliyodai kuwa ya kiungu. Katika maono hayo, alisema aliona idadi kubwa ya watu kutoka ndani na nje ya Ghana wakikusanyika ili kuingia kwenye safina aliyodai kuwa ameijenga.

Kwa mujibu wa Ebo Noah, safina hiyo haikuweza kuwachukua watu wote waliokusanyika, hali iliyomsababisha kuendelea kuombea ili suluhisho lipatikane.

Amedai kuwa baada ya kuomba pamoja na watu aliowataja k**a β€œwatumishi wakuu wa Mungu,” Mungu alitoa muda zaidi ili safina nyingine zijengwe kwa ajili ya kuwahifadhi watu wote.

Kauli hiyo imezua mjadala mpana kwenye mitandao ya kijamii, huku baadhi ya wananchi wakitaka uthibitisho wa madai hayo na wengine wakiyachukulia k**a ujumbe wa kiimani.

✍🏿
πŸ¦…

25/12/2025

Leo Disemba 25,2025 ikiwa Tanzania inaungana na Mataifa mengine duniani kuadhimisha Sikukuu ya kuzaliwa kwa Kristo Yesu, mitaa ya kuanzia Mbezi Beach Tangu Bovu hadi Kawe , kumeonekana kutulia kwa kiasi kikubwa wanachi wameonekana kutoka nyumba za ibada huku wengine wakiendelea na shughuli zao za kila siku.

✍🏿
πŸ¦…

  Watu watano wamefariki dunia baada ya Helkopta ya kampuni ya uokoaji yaKiliMediaur Aviation kupata ajali maeneo ya kat...
24/12/2025

Watu watano wamefariki dunia baada ya Helkopta ya kampuni ya uokoaji ya
KiliMediaur Aviation kupata ajali maeneo ya kati ya Kibo na Barafu Camp katika Mlima Kilimanjaro.

K**anda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, leo Desemba 24, saa 11:30 ikiwa inatoka kuchukua wagonjwa wa kampuni ya Utalii
BobyCamping.
β€œNi kweli kuna ajali ya helkopta ya kampuni ya uokoaji ya KiliMediar na waliofariki ni wageni wawili, guide (muongoza watalii) mmoja, rubani na daktari, taarifa zaidi zitapatikana kesh asubuhi,” amesema k**anda Maigwa.

Taarifa kutoka eneo la tukio ambazo bado hazijathibitishwa
zinaeleza kuwa baada ya helikopta hiyo kuanguka ililipuka moto na kusambaratika huku jitihada za uokoaji zikifanyika.

Eneo la Kibo Hut na Barafu Camp ni urefu wa kati ya mita 4,670 na meta 4,700 kutoka usawa wa bahari.

✍🏿
πŸ¦…

24/12/2025

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, ameziagiza Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kuwasha mitambo yote ili kuondoa mgao wa maji kwa wakazi wa Dar es Salaam na Pwani, kufuatia kuongezeka kwa kiwango cha maji katika Mto Ruvu baada ya mvua takribani milimita 50 kunyesha katika safu za milima ya Uluguru, mkoani Morogoro.

Aweso ametoa maelekezo hayo mara baada ya kufika katika Mtambo wa Maji wa Ruvu Chini, uliopo Bagamoyo mkoani Pwani, ambako alishuhudia Mto Ruvu ukirejea kwenye hali yake ya kawaida baada ya kipindi cha kupungua kwa kina cha maji.

Kuhusu malalamiko ya wananchi kubambikiziwa bili za maji licha ya kutopata huduma hiyo, Waziri Aweso ameielekeza DAWASA kufanya uchunguzi wa kina na kuchukua hatua stahiki dhidi ya watakaobainika kuhusika.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Bonde la Wami-Ruvu, Mhandisi Elibariki Mmassi, ameeleza kuhusu kiwango cha mvua
kilichorekodiwa pamoja na hatua za udhibiti wa uchepushaji wa
maji ya Mto Ruvu, akisema kuwa bodi inaendelea kufuatilia kwa ukaribu kuhakikisha vyanzo vya maji vinatunzwa ipasavyo.

✍🏿
πŸ¦…

24/12/2025

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba, ameagiza watumishi wa Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), waliohusika na ubadhirifu wa fedha kiasi cha Sh bilioni 2.5 wafukuzwe kazi mara moja, akisisitiza kuwa Serikali haitavumilia matumizi mabaya ya fedha za umma.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo Disemba 24, 2025 alipofanya ziara ya kukagua utendaji kazi wa kivuko eneo la Kigamboni, Dar es Salaam, ambapo ameeleza kuwa vitendo vya ubadhirifu vimekuwa chanzo cha kudorora kwa huduma za usafiri wa vivuko na kuongeza gharama zisizo za lazima kwa Serikali.

β€œWatu wasioweza kujirekebisha ni lazima warekebishwe. Kumekuwepo na matumizi mabaya ya madaraka na fedha, hali ambayo haiwezi kuvumiliwa,” amesema Dk Mwigulu.

Pia Dkt.Mwigulu amebainisha kuwa kwa sasa matengenezo yamesimama kwa baadhi ya vivuko kutokana na madeni ya takribani Sh milioni 800, huku taarifa za kifedha zikionesha baadhi ya watumishi wa TEMESA wamehusika na ubadhirifu wa Sh bilioni 2.5.


Waziri Mkuu ameonya kuwa endapo hatua kali hazitachukuliwa, serikali itaingia kwenye gharama kubwa za matengenezo ya vivuko chakavu badala ya kununua vivuko vipya, hali itakayoongeza mzigo kwa wananchi na kuathiri utoaji wa huduma.

✍🏿
πŸ¦…

24/12/2025

Kazini kwa Mwamposa kuna kazi, muumini aomba Mzungu aliyemchumu amuoe kwani anataka kuolewa na mtu kutoka nje ya Tanzania.

✍🏿
πŸ¦…

Address

Mwenge
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Taimediatz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share