24/12/2025
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, ameziagiza Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kuwasha mitambo yote ili kuondoa mgao wa maji kwa wakazi wa Dar es Salaam na Pwani, kufuatia kuongezeka kwa kiwango cha maji katika Mto Ruvu baada ya mvua takribani milimita 50 kunyesha katika safu za milima ya Uluguru, mkoani Morogoro.
Aweso ametoa maelekezo hayo mara baada ya kufika katika Mtambo wa Maji wa Ruvu Chini, uliopo Bagamoyo mkoani Pwani, ambako alishuhudia Mto Ruvu ukirejea kwenye hali yake ya kawaida baada ya kipindi cha kupungua kwa kina cha maji.
Kuhusu malalamiko ya wananchi kubambikiziwa bili za maji licha ya kutopata huduma hiyo, Waziri Aweso ameielekeza DAWASA kufanya uchunguzi wa kina na kuchukua hatua stahiki dhidi ya watakaobainika kuhusika.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Bonde la Wami-Ruvu, Mhandisi Elibariki Mmassi, ameeleza kuhusu kiwango cha mvua
kilichorekodiwa pamoja na hatua za udhibiti wa uchepushaji wa
maji ya Mto Ruvu, akisema kuwa bodi inaendelea kufuatilia kwa ukaribu kuhakikisha vyanzo vya maji vinatunzwa ipasavyo.
βπΏ
π¦