URT Updates

URT Updates Updates from the United Republic of Tanzania

Prof. Mfaransa Aja na Kitabu: Aiambia Dunia Kutalii Tanzania ni TibaNa Mwandishi Wetu Paris, UfaransaWaziri wa Maliasili...
09/07/2025

Prof. Mfaransa Aja na Kitabu: Aiambia Dunia Kutalii Tanzania ni Tiba

Na Mwandishi Wetu Paris, Ufaransa

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana, akiwa nchini Ufaransa jana Julai 8, 2025 amekutana na Mwandishi wa kitabu cha "Tanzano-Therapie", Prof. Chantal Henry ambaye ni Mkufunzi Mwandamizi katika Chuo Kikuu cha Paris East Creteil (UPEC) na mtaalamu wa magonjwa ya afya akili nchini Ufaransa.

Prof. Huyo ameandika Kitabu hicho kinachozungumzia kwa undani jinsi mtu anavyoweza kupona changamoto za saikolojia ya akili na kuhuishwa kisaikolojia kwa kutembelea maeneo ya hifadhi na kuangalia wanyama na vitu vya asili utafiti uliofanywa nchini Tanzania.

“Nilitembelea maeneo mengi ya kiutalii Tanzania hasa Hifadhi za Serengeti, Ngorongoro mpaka kule Gombe-Mahale nikiwa na familia kisha nikarudi k**a mtafiti ambapo nilishiriki mimi mwenye na kuona tiba hiyo lakini pia nimefanya mahijiano na watalii wengi.

“Nikahitimidha kwamba utalii wa kwenda maeneo hayo ya Tanzania unatoa tiba kwa mtu mwenye hatua mbalimbali za magonjwa ya akili na hata saikolojia ya kawaida. Tanzania ni tiba na nimekuwa nikizunguka maeneo mengi huku Ulaya kulisema hilo na watu wameitikia kuja Tanzania,” alisema Prof. Chantal.

Akizungumza mara baada ya mazungumzo na Profesa huyo kuhusu kitabu hicho kilichoandikwa kwa lugha ya Kifaransa, Waziri Pindi amesema kitabu hicho kitaendeleza kuitangaza Tanzania na kuunga mkono kazi kubwa anayoifanya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika sekta ya utalii kupitia filamu ya “Tanzania: The Royal Tour” na “Amazing Tanzania.”

Profesa Chantal akifundisha Chuo Kikuu cha East Central Paris na akiwa pia na kliniki ya kutibu watu wenye changamoto ya afya ya akili, amechapisha maandiko zaidi ya 300 ikiwemo makala mashuhuri ya “Don't Forget the Benefits of Empathy”

Naye Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi amesema wana mshawishi Profesa huyo Kitabu hicho kitatafsiriwe pia katika lugha mbalimbali ili watalii kutoka maeneo yote duniani waweze kukisoma na kuelewa ikiwemo Kiingereza na Kiswahili.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Bw. Ali Mwadini ambaye ameeleza kuwa tayari kitabu hicho kwa mara ya kwanza kilizinduliwa Ubalozini hapo Juni mwaka huu.

Waziri Chana na ujumbe wake wapo mjini Paris kuhudhuria Mkutano wa 47 wa Kamati ya Urithi wa Dunia ya Unesco ambapo taarifa mbalimbali za hali ya uhifadhi wa maeneo ya wanyamapori na malikale zikiwemo za Tanzania, zitawasilishwa. FRANCE 24 English France tv Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation Ikulu Mawasiliano Branding Tanzania Ngorongoro Conservation Area Authority

Balozi Shaibu M***a ampokea Waziri wa Mambo ya Nje wa Cyprus Mhe. Constantinos Kombos Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mam...
09/07/2025

Balozi Shaibu M***a ampokea Waziri wa Mambo ya Nje wa Cyprus Mhe. Constantinos Kombos

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashaririki Mhe. Balozi Shaib M***a amempokea Waziri wa Mambo ya Nje wa Cyrus Mhe. Constantinos Kombos, katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar Es Salaam ambaye amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu.

Mhe M***a aliambatama na Mkurugenzi wa Ulaya na Amerika Mhe. Balozi Swahiba Mndeme na Maafisa Wandamizi wa Wizara.

Kwa upande wake Mhe. Kombos ameambatana na ujumbe wa watu sita kutoka katika Wizara yake, Mabalozi na wawakilishi kutoka Idara Siasa na Afrika.

Ziara ya Mhe. Kombos ya tarehe 8-10 Julai, 2025 inalenga kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na kikanda na Tanzania, ili kuleta maendeleo ya wananchi wa pande hizo mbili.

Akiwa nchini, Mhe. Kombos atakutana Viongozi wa Kitaifa, na kufanya mazungumzo na Mhe. Waziri-NJE Mhe Balozi Mahmoud Thabit Kombo.

Aidha, atashiriki mkutano wa pande mbili kati ya Tanzania na Cyprus, atatia saini hati za makubaliano ya ushirikiano kuhusu Mashauriano ya Kisiasa na ile ya ushirikiano katika masuala ya Mabaharia.

Mhe. Kombos pia atashiriki katika majadiliano ya meza ya pamoja kati ya Jumuiya ya Biashara ya Ulaya na Tanzania Chambers of Commerce. Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation European Commission

Waziri Kombo ashiriki Kongamano la Diplomasia ya AfyaWaziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mah...
09/07/2025

Waziri Kombo ashiriki Kongamano la Diplomasia ya Afya

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) ameshiriki Kongamano kuhusu Kukuza Huduma za Afya Ulimwenguni kupitia Diplomasia lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi, Muhimbili (MUHAS) jijini Dar es Salaaam Julai 8, 2025.

Waziri Kombo ameeleza kuwa Sera ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001 toleo la mwaka 2024 iliyozinduliwa tarehe 19 Mei, 2025 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ilienda sambamba na uzinduzi wa Kitabu cha Mwongozo wa Diplomasia ya Uchumi kinachoeleza utekelezaji wa Diplomasia katika sekta mbalimbali ikiwemo ya afya.

Ameeleza kufurahishwa na wanafunzi wa MUHAS kwa kujipambanua mapema katika diplomasia ya afya kwani Tanzania sasa imekuwa kivutio kwa wengine kuja nchini kupata huduma mbalimbali za afya.

Hatua hii imesaidia kupunguza gharama ya kupeleka wagonjwa kutibiwa nje ya nchi. Hivyo, Kongamano hilo limelenga kuieleza Afrika na Dunia kuwa Muhimbili ipo tayari kuwahudumia kwa huduma bora na utaalamu wa hali ya juu.

Aidha, katika muendelezo wa kutekeleza Sera ya Mambo ya Nje kwa vitendo, Wizara pia ilishiriki mwaliko wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwenye kongamano lililofanyika mwezi Juni 2025, Dodoma kwa lengo la kutangaza fursa mbalimbali zilizopo mkoani humo ikiwemo huduma ya afya, elimu, biashara, uwekezaji na utalii kwa Mabalozi wote wanaowakilisha nchini. Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation

Wizara ya Fedha imeendelea kupongezwa kwa utoaji wa elimu yenye uhalisia na maisha ya wananchi katika masuala ya fedha n...
07/07/2025

Wizara ya Fedha imeendelea kupongezwa kwa utoaji wa elimu yenye uhalisia na maisha ya wananchi katika masuala ya fedha na uchumi kwa kutumia fursa zilizopo na matumizi bora ya fedha katika kuchochea maendeleo.

Hayo yameelezwa na ujumbe wa Shirika la World Vision Tanzania Mkoa wa Tanga wa mradi wa utunzaji mazingira, ukiongozwa na Bw. Swalehe Mwachuo, ulipotembelea Banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Sabasaba, Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.

Bw. Mwachuo alisema kuwa wamevutiwa na elimu kuhusu Sera za Fedha na elimu ya huduma ndogo ya fedha ambayo inauhalisia kwa wajumbe wengi wa mradi huo na maeneo walikotoka.

Alisema kuwa, ujumbe uliotembelea Banda la Wizara ya Fedha umetoka Mkoani Tanga katika Wilaya za Mkinga, Pangani, Handeni na Kilindi ambao umekuja kupata elimu ya kazi zinazofanywa na Wizara ya Fedha hususani zilizo na manufaa ya moja kwa moja kwa wajumbe hao.

Alisema wajumbe hao watapeleka taarifa kwa wananchi wengine kuhusu Sera za fedha na namna ya kuepukana na mikopo umiza, kukopa kwa malengo na kutotumia fedha za mikopo kwenye matumizi yasiyo na faida.

Bw. Mwachuo alisema kuwa wamejifunza kuwa fedha za mkopo sio za mkopaji bali faida ndio ya mkopaji hivyo ni vema kutumia fedha ya mkopo kuzalisha ili kupata faida.

Wataalamu kutoka Wizara ya Fedha kupitia Idara na Vitengo lakini pia Taasisi zilizo chini ya Wizara, wanaendelea kuwakaribisha watanzania kufika katika Banda la Wizara hiyo ili waweze kuwahudumia. Wizara ya Fedha

05/07/2025

*Khadija Kopa&Jay Melody kunogesha Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 50 ya Uhuru wa Comoro*

Malkia wa Taarab,Bi Khadija Kopa ni miongoni mwa wasanii walioalikwa kunogesha sherehe za miaka 50 ya uhuru wa Comoro zinazotarajiwa kufanyika kesho Jumapili tarehe 6 Julai ambapo amealikwa pia Msanii wa Kizazi Kipya Jay Melody.Mgeni Rasmi katika Sherehe hizo ni Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Wasanii wa Tanzania wana mvuto mkubwa katika jamii ya Wacomoro.Bi Khadija Kopa na Jay Melody walipata fursa ya kumtembelea Balozi wa Tanzania,Saidi Yakubu.

30/06/2025

pia unaweza kutoa maoni yako kuhusu blog hii

Wanafunzi Kutoka Qatar Watembelea Tanzania, Wafanya Ziara ya Kujifunza na UtaliiMoshi, Tanzania – Wanafunzi zaidi ya kum...
26/06/2025

Wanafunzi Kutoka Qatar Watembelea Tanzania, Wafanya Ziara ya Kujifunza na Utalii

Moshi, Tanzania – Wanafunzi zaidi ya kumi kutoka Doha, nchini Qatar, wakiambatana na walimu na baadhi ya wazazi wao, wametembelea vivutio mbalimbali vya utalii nchini Tanzania ikiwa ni sehemu ya kujifunza na kujionea utajiri wa maliasili uliopo nchini.

Katika ziara hiyo iliyopewa jina la “Thedi Kilimanjaro Expedition”, wanafunzi hao walipata fursa ya kupanda Mlima Kilimanjaro, kutembelea maporomoko ya maji, pamoja na hifadhi mbalimbali za wanyamapori. Wameeleza kuvutiwa na mandhari ya kuvutia ya Tanzania na kuahidi kuwa mabalozi wazuri wa kuitangaza nchi hiyo k**a kivutio cha utalii pindi watakaporejea nchini kwao.

Ziara hiyo imeratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ya Tanzania, ikiwa ni sehemu ya juhudi za serikali kutangaza utalii wa Tanzania katika soko la kimataifa, hususan nchini Qatar, ambayo ina nafasi kubwa ya kukuza sekta hiyo kupitia usafiri wa kimataifa.

Godwin Kiegeko, Afisa wa Mambo ya Nje kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, amesema ujio wa wanafunzi hao utakuwa kichocheo cha wageni wengine wengi kuitembelea Tanzania, hasa vijana kutoka mataifa ya Kiarabu.

Kwa upande wake, Afisa Utalii Mkuu kutoka Bodi ya Utalii Tanzania, Ester Solomoni, amesema kuwa kupitia ziara hiyo, soko la utalii wa Tanzania nchini Qatar litazidi kukua, na hivyo kusaidia kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea Tanzania kila mwaka.

Abrahamani Saidi, mmoja wa wakufunzi waliowasindikiza wanafunzi hao, amesema kupanda Mlima Kilimanjaro ilikuwa ni fursa ya kipekee kwa wanafunzi wao. Wamejifunza kuhusu jiografia, ikolojia na pia umuhimu wa uhifadhi wa mazingira. Pia wameweza kuona utofauti mkubwa wa kijiografia na tamaduni baina ya Tanzania na Qatar.

Nao wanafunzi kutoka nchi hiyo wakaelezea mazingira na waliyojifunza na kujivunia walipotembelea Mlima Kilimanjaro:
• Abdalla Mufta, mwanafunzi kutoka Qatar
• Dima, mwanafunzi kutoka Qatar
• Yusuph Sahala, mwanafunzi kutoka Qatar

Ziara hiyo imeacha alama kubwa kwa washiriki na kuonyesha nafasi ya Tanzania k**a kituo muhimu cha utalii wa kielimu na kiutamaduni katika ukanda wa Afrika Mashariki. Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation Qatar Charity قطر الخيرية

25/06/2025

pia unaweza kutoa maoni yako kuhusu blog hii

SERIKALI YAWAREJESHA WATANZANIA 42 KUTOKA NCHINI IRAN NA ISRAEL.Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanikiwa ...
25/06/2025

SERIKALI YAWAREJESHA WATANZANIA 42 KUTOKA NCHINI IRAN NA ISRAEL.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanikiwa kuwarejesha salama nchini Watanzania 42 kutoka nchini Israel na Iran kufuatia vita vilivyokuwa vikiendelea baina ya mataifa hayo mawili.

Akizungumza mara baada ya kuwapokea Watanzania hao kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samwel Shelukindo amesema zoezi la kuwarejesha Watanzania wote salama nchini ni utekelezaji wa agizo maalumu la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuhakikisha kwamba Watanzania wote waliopo katika mataifa hayo mawili wanarejeshwa nchini salama.

Aidha Balozi Shelukindo amesema leo juni 25, 2025 wameingia Watanzania makundi mawili, kundi moja liliwasili mchana wa leo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Aman Karume na kwamba gharama zote za kuwarejesha Watanzania hao zimegharamiwa na serikali na kuongeza kuwa Watanzania wengine kutokea nchini Iran wanatarajiwa kuwasili nchini kesho Juni 26, 2025.

Balozi Shelukindo pia kupitia hadhara hiyo, ametoa rai kwa Watanzania wote kuhakikisha kwamba tunaendelea kuilinda tunu yetu ya utulivu na amani k**a ambavyo Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anavyotuasa mara kwa mara.

Akizungumza katika mapokezi hayo, mmoja kati ya wanafunzi waliokuwa wanasoma nchini Israel Bi. Neema Dasina amesema hali ya usalama nchini Israel ilikuwa mbaya kufuatia milipuko ya mabomu ya mara kwa mara isipokuwa kupitia maelekezo mahususi kutoka kwa ubalozi wa Tanzania nchini humo na ule wa nchini Misri, huku akiishukuru serikali na Mhe. Rais Samia kwa kwa ujumla jinsi ambavyo wameonyesha thamani ya Watanzania hasa katika kipindi hiki cha hatari iliyokuwa mbele yao.

Mama mzazi wa mmoja wa vijana waliorejea salama kwa niaba ya wazazi wengine Bi. Asela Luena, ameishukuru serikali ya Mhe. Rais Samia kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa juhudi za dhati za kuwapigania watoto wao, na kuhakikisha kwamba wanarejea salama na kuungana na familia zao.

“baada ya kupata taarifa za hali ya usalama nchini Israel hatukulala usingizi, niliwasiliana na binti yangu, aliniambia mama usiwe na wasiwasi kwasababu sisi wote tupo kwenye mikono salama, serikali imeingilia kati na kila kitu tunafanyiwa na serikali, kwakweli sisi wazazi tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Samia kwa upendo wake wa dhati kwa taifa letu, tumefarijika sana k**a familia lakini k**a taifa hii ni heshima kubwa duniani” alimalizia mama Asela Luena.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imefikia uamuzi huo wa kuwarejesha Watanzania wote waliopo katika mataifa ya Israel na Iran kufuatia mapigano yaliyozuka baina ya mataifa hayo mawili, japokuwa siku chache zilizopita zilitolewa taarifa za kumaliza vita hivyo vilivyodumu kwa takribani siku kumi na mbili mfululizo.

Viongozi wengine walioambatana na Katibu Mkuu Balozi. Dkt. Samwel Shelukindo katika mapokezi hayo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, ni pamoja na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mindi Kasiga. Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation Msemaji Mkuu wa Serikali Ikulu Mawasiliano Branding Tanzania Israel Defense Forces

WIZARA YA FEDHA YATOA ELIMU YA USIMAMIZI WA MNYORORO WA UGAVI KWA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARIKamishna wa Idara ya Sera...
17/06/2025

WIZARA YA FEDHA YATOA ELIMU YA USIMAMIZI WA MNYORORO WA UGAVI KWA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI

Kamishna wa Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma, Wizara ya Fedha, Dkt. Frederick Mwakibinga, akizungumza wakati wa Mafunzo kwa Wahariri Vyombo vya Habari kuhusu masuala ya usimamizi wa mnyororo wa ugavi katika sekta ya umma, yaliyoandaliwa na Wizara ya Fedha, katika ukumbi wa Nane Nane, Mkoani Morogoro, ambapo aliwaomba wahariri hao kutumia kalamu zao, sauti, picha, na majukwaa mbalimbali ya vyombo vya habari, kutoa elimu kuhusu nafasi na mchango wa mnyororo wa ugavi katika maendeleo ya Taifa itafanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Tanzania na Misri kupanua wigo wa ushirikianoWaziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Mahmo...
19/03/2025

Tanzania na Misri kupanua wigo wa ushirikiano

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) wamekutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje, Uhamiaji na Wamisri Waishio Nje wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Mheshimiwa Dkt. Badr Abdelatty, katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada ya mazungumzo yao, Waziri Kombo ameeleza kuwa Tanzania na Misri zimejidhatiti kuimarisha ushirikiano wa uwili kwa manufaa ya kiuchumi ya pande zote mbili.

Waziri Kombo ameeleza kuwa Ujenzi wa Mradi wa Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere ni kielelezo cha uhusiano imara wa nchi hizi mbili. Pamoja na hayo, amesisitiza kuendeleza ushirikiano katika utekelezaji wa miradi mingine ya kimkakati na kimaendeleo.

Waziri Kombo ameongeza kuwa lipo dirisha la kuongeza wigo wa ushirikiano kibiashara na uwekezaji katika sekta ya uvuvi, bidhaa za chakula na kilimo, utalii, huduma za bandari pamoja na sekta ya usafirishaji ambapo amelikaribisha Shirika la Ndege la Misri (Egypt Air) kuongeza safari zake nchini.
“Takwimu za biashara kati ya Tanzania na Misri zimekuwa zikiongezeka, ambapo thamani ya biashara zimeongezeka kutoka Tsh bilioni 84.3 mwaka 2019 hadi Tsh bilioni 142 mwaka 2023. Hii ni hali ya kutia moyo, lakini wote tumekubaliana kuwa fursa za ukuaji ni kubwa zaidi, na tunahitaji kufanya zaidi ili ukuaji huo uendelee.”

Aidha, Waziri Kombo amewasihi Watanzania kuchangamkia fursa za mafunzo katika kada mbalimbali zikiwemo udaktari na kilimo ambazo zimekuwa zikitolewa na Serikali ya Misri.

Kwa upande wake, Mheshimiwa Dkt. Abdelatty amesema kuwa sasa ni wakati wa Tanzania na Misri kuongeza nguvu kukuza ushirikiano katika biashara na uwekezaji akieleza kuwa Misri iko tayari kushirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya miundombinu ikiwemo reli, barabara, na bandari.

Tanzania ni uti wa mgongo wa mazao ya chakula kwa nchi nyingi za Afrika na hivyo, Misri ingependa kuwa miongoni mwa nchi zinazoagiza mazao ya chakula kutoka Tanzania.

Aidha, Waziri Dkt. Abdelatty amesisitiza suala la matumizi mazuri ya maji ya Mto Nile pamoja na kushirikiana na Tanzania na nchi nyingine zote zenye vyanzo vya maji jumuishi katika kutunza vyanzo hivyo kwa faida ya vizazi vijavyo.

Misri inashika nafasi ya 8 katika uwekezaji hapa nchini, na uwekezaji wa Misri unafikia kiasi cha dola za Marekani bilioni 1.37, na kuchangia kutoa ajira kwa Watanzania wapatao 3,776. Branding Tanzania Ikulu Mawasiliano Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation Clouds Media Tanzania

Address

Dar Es Salaam
14112

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when URT Updates posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share