URT Updates

URT Updates Updates from the United Republic of Tanzania

22/09/2025

Maadhimisho ya siku Faru Duniani ambapo leo tarehe 22 Septemba 2025 Maafisa na Askari wa Hifadhi ya Ngorongoro kwa kushirikiana na Jeshi la ...

22/09/2025

World's News Updates

17/09/2025

World's News Updates

TANZANIA, UK TO EXPLORE BILATERAL CLIMATE AND RENEWABLE ENERGY COOPERATIONMinister for Foreign Affairs and East African ...
12/09/2025

TANZANIA, UK TO EXPLORE BILATERAL CLIMATE AND RENEWABLE ENERGY COOPERATION

Minister for Foreign Affairs and East African Cooperation Amb. Mahmood Thabit Kombo, met with UK Minister for Climate Hon. Katie White OBE (MP) at Whitehall in London and discussed opportunities for strengthened bilateral cooperation on climate action, renewable energy, and conservation.

During the meeting held on September 10,2025 Minister Kombo highlighted Tanzania’s commitment to clean cooking, renewable energy, forestry, and marine conservation and shared achievements such as the distribution of 300,000 clean cookstoves reducing firewood use by 48% and construction of Tanzania’s largely hydropower-based energy system, which has a surplus capacity of 4,000 MW compared to 1,900 MW demand.

Minister Kombo emphasized that Tanzania is ready to lead regionally in renewable energy, forestry, and clean cooking while seeking equitable and sustainable partnerships.

On her side Minister Hon. Katie White reaffirmed UK commitment to support Tanzania’s climate and energy priorities, signaling a strengthened collaboration between the two nations.

She expressed strong support for Tanzania’s initiatives and proposed deeper engagement through technical assistance, financing mechanisms, and coordinated participation in global climate platforms such as COP30 and the United Nations General Assembly.

At the end of the meeting, both sides identified potential areas for collaboration including technical and financial support for clean cooking, forestry initiatives, sustainable timber and furniture production, waste management and recycling, energy grid improvements, and participation in carbon markets. Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation Climate Change Commission PH World Climate change Organisation - WCCO Climate Reality Ministry of Climate Change, Govt of Pakistan Ofisi ya Makamu wa Rais

TANZANIA YAORODHESHWA KATIKA NCHI ZINAZOTAZAMIWA KUFUZU KUTOKA NCHI MASIKININa. Peter Haule na Joseph Mahumi, WF, Dodoma...
10/09/2025

TANZANIA YAORODHESHWA KATIKA NCHI ZINAZOTAZAMIWA KUFUZU KUTOKA NCHI MASIKINI

Na. Peter Haule na Joseph Mahumi, WF, Dodoma

Tanzania imeorodheshwa na Kamati ya Sera za Maendeleo ya Umoja wa Mataifa, kuwa miongoni mwa nchi zinazotazamiwa kufuzu kutoka katika kundi la nchi masikini (Least Developed Countries) kwenda nchi inayoendelea.

Hayo yamebainishwa jijini Dodoma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, wakati wa Mkutano wa Awali wa tathmini ya nchi kutoka nchi maskini kwenda nchi inayoendelea inayofanywa na Umoja wa Mataifa (UN) kupitia Shirika lake la Biashara na Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNCTAD).

Dkt. Mwamba alisema hatua hiyo imetokana na Tanzania kupiga hatua kubwa katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika kipindi cha miongo miwili iliyopita kupitia uthabiti wa Sera za uchumi zilizosababisha kukua kwa uchumi kwa wastani wa asilimia 6.2 kati ya mwaka 2000 na 2024.

“Pato la mtu kwa mwaka limeongezeka kutoka dola za Marekani 453 mwaka 2000 hadi dola 1,277 kwa mwaka 2023, kiwango cha umasikini uliokithiri kimepungua kutoka asilimia 36 mwaka 2000 hadi asilimia 26 mwaka 2024 kutokana na utekelezaji makini wa sera za fedha na ongezeko la mikopo kwa sekta binafsi”, alisema Dkt. Mwamba.

Dkt. Mwamba alisema kuwa Mfumuko wa bei umeendelea kudhibitiwa na kubaki kwenye tarakimu moja hali iliyoimarisha uthabiti wa uchumi na kuongeza uwezo wa wananchi kukabiliana na gharama za maisha.

Alisema kuwa kumekuwa na uwekezaji wa kimkakati hususani katika miundombinu ya nishati kupitia utekelezaji wa mradi wa kufua umeme wa Julius Nyerere Hydropower ambao ni mradi mkubwa wa kitaifa wa ujenzi na uzalishaji wa umeme.

Alisema kuwa upo mradi wa usafiri wa abiria na mizigo kati ya Dar es Salaam – Morogoro hadi Dodoma kupitia Reli ya Kisasa ya Standard Gauge Railway (SGR) na pia miradi ya maboresho katika sekta ya elimu na huduma za afya.

Vilevile alisema kuwa maboresho katika elimu na huduma za afya pamoja na mkazo katika viwanda na ajira yamechangia katika kufikia vigezo vinavyowezesha nchi kuondolewa kwenye kundi la nchi maskini. UN Trade and Development UNCTAD statistics United Nations Ikulu Mawasiliano

RAIS SAMIA APONGEZWA KWA KUTOA AJIRA MALIASILI NA UTALIINa Sixmund Begashe, MwanzaRais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameponge...
10/09/2025

RAIS SAMIA APONGEZWA KWA KUTOA AJIRA MALIASILI NA UTALII

Na Sixmund Begashe, Mwanza

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutoa fursa ya ajira kwa vijana waliohitimu vyuo vilivyopo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii.

Pongezi hizo zimetolewa na Naibu Katibu Mkuu (Uhifadhi) wa Wizara hiyo, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba, katika mahafali ya 61 ya Taasisi ya Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi (PWTI), yaliyofanyika jijini Mwanza mwishoni mwa wiki.

CP Wakulyamba amesema chuo hicho kimeendelea kuwa chachu ya mafanikio ya uhifadhi nchini kwa kutoa wataalamu mahiri wa wanyamapori, mazingira na utalii, jambo linaloiwezesha serikali kutoa kipaumbele katika ajira.

“Pamoja na serikali kuwa mwajiri mkuu, bado ni changamoto kutosheleza mahitaji ya soko la ajira. Natoa rai kwa sekta binafsi inayojihusisha na uhifadhi wa misitu, wanyamapori na biashara zinazohusiana na utalii, kutoa nafasi kwa vijana hawa ili kuongeza tija na kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira,” amesema.

Vilevile, amewataka wahitimu kutumia ujuzi walioupata kwa maslahi ya Taifa.

Naye, Mkurugenzi wa Kitengo cha Utafiti na Mafunzo wa wizara hiyo, Dkt. Edward Kohi, alisema wizara itaendelea kufanya tafiti ili kubaini hali ya ajira kwa wahitimu wa vyuo vyote vinavyosimamiwa na Maliasili.

Aidha, Mwenyekiti wa Bodi ya Magavana ya PWTI, Prof. Agnes Sirima, ameahidi kuendeleza ushirikiano na wizara katika kuinua uwezo wa taasisi hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa ya uongozi wa chuo hicho, kozi ndefu zilianza Oktoba 3, 2024, zikihusisha wanachuo 446 wa mwaka wa masomo 2024/25, ambapo wanawake walikuwa 124 (sawa na asilimia 27.64) na wanaume 322 (sawa na asilimia 72.36) na wahitimu waliofanikiwa kuhitimu mwaka huu ni 313.

Timu ya Netiboli ya Maliasili Yatinga Nusu Fainali SHIMIWINa John Bera, MwanzaTimu ya netiboli ya Wizara ya Maliasili na...
10/09/2025

Timu ya Netiboli ya Maliasili Yatinga Nusu Fainali SHIMIWI

Na John Bera, Mwanza

Timu ya netiboli ya Wizara ya Maliasili na Utalii imeandika historia leo, Septemba 10, 2025, baada ya kufuzu kwa mara ya kwanza hatua ya nusu fainali ya Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI), yanayoendelea jijini Mwanza.

Timu hiyo ilijihakikishia nafasi hiyo muhimu baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 35–31 dhidi ya timu ya Wizara ya Elimu katika mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa. Ushindi huu unaiweka Maliasili kwenye nafasi ya kipekee, ikiwa ni mara ya kwanza kufuzu hatua hiyo tangu kuanza kwa mashindano hayo.

Kocha wa timu hiyo, Bi. Rehema Kapela, ameipongeza timu hiyo kwa juhudi, ari na nidhamu waliyoionesha, akisema wana matumaini makubwa ya kufika fainali na hata kutwaa ubingwa.

"Ni siku ya kihistoria kwetu kufuzu nusu fainali. Tumefanya kazi kwa bidii na tunafurahia kufika hapa. Tunatumai kushinda tena na kufika fainali kwa sababu ari ya kufika huko tunayo," alisema Bi. Rehema.

Naye mchezaji wa timu hiyo, Neema Nkya, ameeleza imani kubwa aliyonayo kwa timu yao huku akimpongeza kocha wao kwa mafunzo bora yaliyowafikisha hatua hiyo.

Kwa upande wake, Kaimu Mratibu wa 'Maliasili Sport Club', Bw. George Rwezaura amewapongeza wachezaji kwa mafanikio hayo na kusisitiza kuwa hatua hiyo ya kihistoria ni ya kupongezwa na chachu kubwa kushinda nusu fainali na fainali.

"Hongereni sana wachezaji wetu. Mnaipeperusha vyema bendera ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Tunawapongeza sana kwa kuingia nusu fainali; hili ni jambo kubwa na la kihistoria," amesema George.

Mchezo huo wa kusisimua ulihudhuriwa na mashabiki pamoja na viongozi kutoka Shirikisho la Michezo la SHIMIWI. Kwa upande wa Wizara ya Maliasili na Utalii, miongoni mwa waliokuwepo kushuhudia mchezo huo ni Mkurugenzi Msaidizi wa Sehemu ya Utawala, ambaye pia ni Mratibu wa Michezo wa Wizara, Bi. Violeth Mlinga.

WAZIRI KOMBO AWASILI NCHINI UINGEREZA KWA ZIARA RASMIWaziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balo...
08/09/2025

WAZIRI KOMBO AWASILI NCHINI UINGEREZA KWA ZIARA RASMI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahamoud Thabit Kombo, amewasili nchini Uingereza kwa ziara rasmi inayotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 8 hadi 12 Septemba, 2025.

Lengo la ziara hiyo ni kuimarisha uhusiano bora na wa kihistoria kati ya Tanzania na Uingereza.

Wakati wa ziara hiyo, Mheshimiwa Kombo atamwakilisha Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, k**a Mgeni Rasmi katika ufunguzi wa kituo kipya cha Masuala ya Kimataifa cha *ODI Global* utakaofanyika Westminster, London, tarehe 9 Septemba 2025.

Akiwa London, Mheshimiwa Waziri Kombo pia atashiriki katika mfululizo wa vikao vya viongozi waandamizi wa Serikali ya Uingereza, Waziri anayeshughulikia masuala ya Afrika; pamoja na Waziri anayeshughulikia Masuala ya Tabianchi.

Katika hatua nyingine ya kuimarisha ushirikiano wa kimataifa, Waziri Kombo atakutana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Mhe. Shirley Ayorkor Botchwey, na Katibu Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Bahari (IMO), Mheshimiwa Arsenio Dominguez.

Aidha Waziri Kombo atafanya vikao na taasisi muhimu za Uingereza za fedha za maendeleo na uwekezaji, ikiwemo British International Investment (BII) na UK Export Finance (UKEF), pamoja na wawakilishi wa King’s Foundation
k**a juhudi za kuboresha ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Uingereza ambao ni msingi mkuu wa sera ya mambo ya nje ya Tanzania.

Ili kuimarisha zaidi ushirikiano wa kiuchumi, Waziri Kombo atashiriki pia katika meza ya majadiliano ya kibiashara na makampuni teule ya Uingereza kwa ajili ya kubaini fursa katika biashara, uwekezaji, nishati safi, miundombinu, na sekta nyingine za kipaumbele. Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation

Dkt. Salem Al-Junaibi na Ujumbe wake Awasili nchini kwa Ziara ya KibiasharaMwenyekiti wa Chama cha Biashara na Viwanda c...
07/09/2025

Dkt. Salem Al-Junaibi na Ujumbe wake Awasili nchini kwa Ziara ya Kibiashara

Mwenyekiti wa Chama cha Biashara na Viwanda cha Oman Dkt. Salem Al-Junaibi (Mb) na ujumbe wa Wafanyabiashara wa Oman, amewasili nchini leo, tarehe 7 Septemba 2025, kwa ziara ya siku tano, kuangazia fursa za uwekezaji na biashara za Tanzania, katika sekta mbalimbali.

Mara baada ya kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dkt. Al-Junaibi na ujumbe wake, alipokelewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Twaibu, pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Abdalah Kilima.
Viongozi wengine waliompokea ni Naibu Balozi wa Oman nchini Tanzania, Rashid Al Mandhir, pamoja na maafisa waandamizi wa Serikali na Sekta binafsi.

Katika ziara yao, Dkt. Al-Junaibi na ujumbe wake wanatarajiwa kukutana na viongozi wa Serikali pamoja na taasisi mbalimbali za umma na binafsi, zikiwemo Tume ya Ushindani (FCC), Kiwanda cha Nyama – Kibaha, Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA), KAMAKA, TISEZA, BRELA, TANTRADE, TBS, TIRDO na Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC).

Aidha, ujumbe huo pia utatembelea Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Wakala wa Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), pamoja na Bodi ya Chai Tanzania (TTB).

Vilevile ujumbe huo pia utashiriki katika mazungumzo na Makatibu Wakuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Nishati, pamoja na Ofisi ya Rais – Kazi, Uchumi na Uwekezaji. Katika mikutano hiyo, pande hizo mbili pia zitasaini mikataba mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Oman.

Dkt. Al-Junaibi na ujumbe wake pia watatembelea Zanzibar ambako watakutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa ZIPA, ZNCC, pamoja na kutembelea Eneo Maalum la Uchumi Zanzibar.

Mbali na mazungumzo hayo na Serikali ya Tanzania Bara na Zanzibar, ujumbe huo wa wafanyabiashara wa Oman pia utafanya mawasilisho kuhusu hali ya biashara na viwanda nchini Oman, pamoja na fursa mbalimbali za ushirikiano wa kibiashara kati ya Oman na Tanzania.

Ziara hiyo ya Dkt. Al-Junaibi na ujumbe wake inatarajiwa kukamilika tarehe 12 Septemba, 2025, kabla ya kurejea nchini Oman. Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation

Wanamichezo wa Maliasili Sports Club watakiwa kujituma na kudumisha nidhamu kwenye mashindano ya SHIMIWI - MwanzaNa John...
06/09/2025

Wanamichezo wa Maliasili Sports Club watakiwa kujituma na kudumisha nidhamu kwenye mashindano ya SHIMIWI - Mwanza

Na John Bera, Mwanza

Uongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii umewataka wanamichezo wanaoiwakilisha Wizara hiyo katika mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) 2025 kuzingatia nidhamu ya hali ya juu wanapotekeleza majukumu yao ya kimichezo.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Mwanza na Mkurugenzi Msaidizi wa Sehemu ya Utawala katika Wizara hiyo ambaye pia ni Mratibu wa Michezo Wizarani, Bi. Violeth Mlinga, wakati akizungumza na wachezaji wa Maliasili Sports Club mara baada ya mazoezi ya asubuhi.

Bi. Mlinga amesema kuwa nidhamu ni nguzo muhimu katika Utumishi wa Umma na ndio msingi wa mafanikio ya kila mtumishi.

"Zingatieni sana nidhamu katika kila kitu, ikiwa ni wakati wa mazoezi, mashindano, pamoja na nje ya uwanja. Nidhamu ni chanzo kikuu cha mafanikio kwa mtumishi wa Umma," alisema Bi. Mlinga.

Aidha, amewahimiza wachezaji hao kujituma na kucheza kwa bidii, akisema juhudi zao zitaisaidia Wizara kuibuka na ushindi na hatimaye kusaidia juhudi za kuutangaza Utalii wa ndani na nje ya nchi.

"Tukumbuke kuwa tumekuja kupambana. Lengo ni kuiletea Wizara ushindi. Hivyo hakikisheni mnapambana kwa nguvu zote ili kuipa Wizara mafanikio, ambayo yatachochea pia utangazaji wa utalii wetu," aliongeza.

Kwa upande wake, Katibu wa Maliasili Sports Club, Bw. Patrick Kutondolana, akizungumza kwa niaba ya wachezaji, alisema mashindano ya mwaka huu yana ushindani mkubwa, lakini timu zinaendelea kujiandaa kwa bidii kuhakikisha zinaleta ushindi.

"Mashindano ni magumu, lakini tumejipanga vizuri. Tutaendelea kujituma kwa bidii ili kuiwakilisha vyema Wizara na kuhakikisha tunachangia katika kutangaza utalii wa Tanzania." alisema Bw. Kutondolana.

WAZIRI KOMBO ATUA JIJINI ARUSHA KUUNGANA NA MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI KUSHIRIKI MKUTANO WA...
06/09/2025

WAZIRI KOMBO ATUA JIJINI ARUSHA KUUNGANA NA MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI KUSHIRIKI MKUTANO WA 35 WA BARAZA LA KISEKTA LA MAWAZIRI LA JUMUIYA HIYO.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb), amewasili Jijini Arusha na kuongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa 35 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,

Mkutano huo unaofanyika katika ngazi tatu tofauti, umeanza rasmi tarehe 31 Agosti hadi tarehe 02 Septemba, 2025 kwa ngazi ya Wataalam, baada ya hapo ukaendelea kwa ngazi ya Makatibu Wakuu tarehe 03 hadi 04 Septemba, 2025 na hii leo unaingia katika awamu ya tatu ya ngazi ya Mawaziri, ambapo unatarajiwa kuchukua siku mbili, tarehe 05 hadi 06 Septemba, 2025.

Mawaziri wanaoshiriki mkutano huu ni Mawaziri wote wa Mambo ya Nje wanaoshughulikia masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoka nchi zote wanachama wa Jumuiya hiyo.

Baraza hili la Mawaziri la Kisekta la Jumjuiya, leo linapokea na kujadili taarifa mbalimbali zilizoanza kujadiliwa katika ngazi ya Wataalam na Makatibu Wakuu, zikiwemo taarifa za Utekelezaji wa Maamuzi na Maelekezo yaliyopita ya Baraza la Kisekta lililopita, Rasimu ya Mkakati wa Saba (7) wa Maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dira ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Mwaka 2050, Mkakati wa Mageuzi ya Kidigitali wa Mwaka 2025 - 2030, Maandalizi ya Sera ya Lugha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Kalenda ya Majukumu ya Jumuiya kwa kipindi cha mwezi Julai hadi Desemba, 2025 na hatua iliyofikiwa katika uondoaji wa vikwazo visivyo vya kiforodha Katika Jumuiya, na hatua iliyofikiwa katika masuala ya Kisiasa ya Nchi Wanachama wa Jumuiya hiyo ya Afrika Mashariki.

Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ni Jumuiya ya nchi nane za Kanda ya Maziwa Makuu ya Afrika ikijumuisha Jamhuri ya Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Jamhuri ya Kenya, Jamhuri ya Rwanda, Jamhuri ya Shirikisho la Somalia, Jamhuri ya Sudan Kusini, Jamhuri ya Uganda na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ikumbukwe kwamba lengo kuu la Jumuiya hii ni kukuza ushirikiano wa kikanda katika nyanja mbalimbali ikiwemo biashara, forodha na ushirikiano wa kisiasa. Jumuiya hii ilianzishwa awali mwaka 1967, lakini kutokana na tofauti za kisiasa ilivunjika mwaka 1977 kabla ya kufufuliwa rasmi mwaka 1999 kwa kutiwa Saini kwa Mkataba mpya.

Tangu kufufuliwa kwake, Jumuiya ya Afrika Mashariki imeanzisha hatua mbalimbali muhimu za ujumuishaji, ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa Umoja wa Forodha mwaka 2005, Soko la Pamoja mwaka 2010, na juhudi zinazoendelea kuelekea Muungano wa Fedha. Jumuiya hiyo pia imekuwa ikifanya kazi ya kuoanisha sera katika sekta k**a usafiri, afya, elimu, na nishati. Ikiwa na jumla ya watu wanaozidi milioni 300 na msisitizo wa pamoja juu ya maendeleo ya kikanda, EAC ina nafasi inayoongezeka katika masuala ya bara na inachukuliwa k**a mfano wa ushirikiano wa kikanda barani Afrika. Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation

29/08/2025

World's News Updates

Address

Dar Es Salaam
14112

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when URT Updates posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share