BINGO_onlinetz

BINGO_onlinetz Official page ya BINGO TV
email [email protected]

16/01/2026

Mchambuzi wa masuala ya nchini Philipo Mwakibinga amewataka Watanzania kuwapuuza baadhi ya wanaharakati wa mitandaoni wenye nia ovu wanaoeneza uzushi kuwa Rais wa Jamhuri ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan ana migogoro ya ndani na wasaidizi wake.

Akizungumza na Waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam Mwakibinga amewataja wanaharakati hao ni Maria Sarungi, Sativa na wengineo na nia yao ni kusambaza ajenda za uzushi na hatakubali hali hii iendelee.

Mwakibinga amewataka Watanzania kuwa makini na taarifa wanazokutana nazo mitandaoni akiwataka kupuuza kabisa madai yanayosambazwa na baadhi ya wanaharakati wa mitandao ya kijamii wenye nia zisizo njema na watasimama kidete kukemea hali hiyo.

14/01/2026

TUSIKAIMISHE JUKUMU LA MALEZI, WAZAZI TUWAJIBIKE- KAFULAMA

Tunapoendelea na mwaka mpya wa 2026, rai imetolewa kwa wazazi na walezi kutokaimisha jukumu la malezi ya watoto wao kwa watu wengine na badala yake watenge muda wa kulea na kukuza watoto wao katika misingi na tamaduni zinazokubalika ili kuondokana na kadhia kadhaa za uduni wa malezi ikiwemo tabia ovu na tamaduni za kigeni ambazo zimekuwa zikiathiri jamii na Taifa kwa ujumla.

Rai hiyo imetolewa na Bi. Grace Kafulama, Mkazi wa Kigoma, wakati akizungumza nasi kuhusu umuhimu wa malezi ya wazazi kwa watoto k**a msingi wa amani na usalama ndani ya jamii na Taifa kwa ujumla, akisema masuala hayo huanza ndani ya familia zinazowajibika vyema katika malezi ya watoto hao.

Bi. Kafulama amesisitiza kuwa malezi kwa watoto si kugharamia mahitaji ya mtoto peke yake, bali ni pamoja na kuzungumza na watoto, kuwafundisha na kuwaelekeza kuhusiana na masuala mema, akisema jukumu hilo ni la kila mzazi na mlezi k**a ilivyokuwa zamani.

“Kwasasa tupo kwenye jamii ambayo tunashuhudia baadhi ya watoto wakifanya mambo ya ajabu na kwasababu si mtoto wako unaamua kumuacha kwamba atajua mwenyewe. Tusimame kutimiza wajibu wetu, wewe mzazi ni balozi wa kwanza wa kukemea, kuonya na kuelimisha juu ya matendo mema na kuwatengenezea mazingira bora ya kesho, hakuna Waziri ama serikali itakayomtengeneza mtoto k**a sisi jamii na wazazi hatutawajibika vyema.” Amesema Bi. Kafulama.

Katika hatua nyingine, Bi. Kafulama amezungumzia pia chanzi cha vurugu za wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, akisema kwa kiasi kikubwa matukio yale yamesababishwa na kudhorota kwa malezi ya Vijana nchini, akisema ikiwa kila mzazi atawajibika vyema ni aghalabu kwa wananchi kushiriki katika kuharibu amani ya Tanzania.

14/01/2026

VIJANA TUNA DENI KWA RAIS SAMIA, “ANATUJALI NA KUTUPENDA”- KHALIFA

Watanzania wamempongeza na kumshuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya ulinzi na usalama Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ujasiri na uimaraka wake katika kulinda na kuitunza amani ya Tanzania kwa kusimama kidete katika kutatua kero za wananchi na kuwaletea maendeleo watanzania.

Pongezi hizo zimetolewa na Wakazi wa Mkoa wa Arusha akiwemo Bw. Hussein Khalifa, Mkazi wa Arusha Mjini, wakati akieleza kuhusu hatua mbalimbali za maendeleo zilizofikiwa kwenye Uongozi wa Rais Samia, wakati huu ambapo tunaelekea kuadhimisha siku 100 tangu kuapishwa kwake kuiongoza Tanzania kwa awamu ya pili.

“Mimi namsifu Amiri Jeshi wetu Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwanza kwenye amani, ambayo imeendelea kuwa tunu ya Tanzania kiasi cha kusifika kote duniani na kuwa kimbilio la waliokosa makazi. Amekuwa Rais Jasiri pia na Rais wa kutumainiwa kiasi cha kuwa Mama yetu wa Taifa ambapo kwa ujasiri na ushupavu wake amani imeendelea kutawala nchini.” Amesema Bw. Khalifa.

Akisisisita kuwa Vijana wanalo deni kwa Rais Samia Khalifa amezungumzia pia mageuzi makubwa ya Vijana kupewa kipaumbele katika serikali ya Dkt. Samia kwa kuunda Wizara maalumu ya Vijana, akisema Rais Samia tangu kupatikana kwa uhuru wa Tanzania, ndiye kiongozi pekee aliyetoa fursa ya Wizara kwa Vijana ili Vijana kuweza kutatuliwa changamoto zao kikamilifu chini ya Ofisi ya Rais.

Dakika ya 105+ Baada ya kumaliza dakika 90 Azam FC 0:0 Young Africans Sports Club
13/01/2026

Dakika ya 105+ Baada ya kumaliza dakika 90

Azam FC 0:0 Young Africans Sports Club

Nani mwingine ameachwa?
12/01/2026

Nani mwingine ameachwa?

11/01/2026

Lucy Antony Michael (35), Mkazi wa Yombo Dovya, Mtaa wa Makangarawe, Wilayani Temeke, Dar es Salaam amevamiwa na watu wasiojulikana akiwa anatoka nyumbani kwake, ambapo watu hao walimpiga na kumshambulia maeneo mbalimbali ya mwili wake

Lucy ambaye ni miongoni mwa watu waliojitambulisha kuwa ni Waumini wa Kanisa Katoliki walioenda kwenye Ubalozi wa Vatican, uliopo hapa nchini kwaajili ya kupeleka barua ya malalamiko juu ya mwenendo wa baadhi ya viongozi wa Kanisa hilo hivi karibuni, amesema kabla ya kuvamiwa na kushambuliwa kwake kwa siku kadhaa amekuwa kwenye misukosuko ya kupokea simu na kutumiwa sms za kejeli, matusi na wengine kumtishia maisha

Akizungumza na Waandishi wa Habari akiwa nyumbani kwake leo, Jumapili Januari 11.2026, Lucy amehusianisha kushambuliwa kwake na maoni aliyotoa mbele ya Wanahabari kuhusiana na mwenendo wa baadhi ya viongozi wa Kanisa Katoliki, jambo ambalo ameeleza kuwa amelifanya kwa nia njema ya kujenga iliyolenga kuwarejesha viongozi hao kwenye mstari, maoni ambayo yamepokelewa kwa hisia hasi kwa baadhi watu kwenye jamii

Aidha, bada ya kushambuliwa Lucy amefikisha malalamiko yake kwenye Kituo cha Polisi Makangarawe na kupewa RB No. MAR/RB/49/2026

Shuhuda wa tukio hilo Sabina Michael, Mjumbe wa Serikali ya Mtaa Ashura Salum na Daud Leonard ambaye ni mmoja wa waumini wanaosali pamoja na Lucy, kwa nyakati tofauti wameeleza kusikitishwa na tukio hilo sambamba na kuziomba mamlaka husika kuchukua hatua stahiki kwa wote waliohusika, huku pia wakiomba kuimarishiwa zaidi usalama mtaani kwao kwani matukio ya aina hiyo yanaweza kusababisha wasiwasi kwa jamii.

10/01/2026

Video mpya na picha kutoka kwa msanii Nandy huku akijiita Kibonge kwenye video akiwa amejirekodi kwenye kioo usiku wa kuamkia leo, Una maoni gani kuhusu muonekano mpya wa Nandy baada ya kunenepa?

Sponsored by

10/01/2026

Jamaa unampa marks ngapi eti

POLISI YACHUKUWA HATUA KWA MATUKIO MATATU YA VIFO, LIPO LA ALIYEJINYONGA MAHABUSU.Jeshi la Polisi limetangaza kumshikili...
08/01/2026

POLISI YACHUKUWA HATUA KWA MATUKIO MATATU YA VIFO, LIPO LA ALIYEJINYONGA MAHABUSU.

Jeshi la Polisi limetangaza kumshikilia askari mmoja wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Rufiji kwa tuhuma za kumpiga risasi Shaban Said Luluba, Mkazi wa Kijiji cha Nyamwage Wilayani Rufiji na kupelekea kupoteza maisha wakati akifanya uk**ataji Januari 08, 2025.

Taarifa iliyotolewa kwa Vyombo vya habari na Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania
Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) David Misime imesema Uchunguzi unaendelea kuhusu tukio hilo na endapo itabainika kuna uzembe au matumizi zaidi ya nguvu hatua nyingine za kisheria zitachukuliwa dhidi ya askari huyo.

Misime pia amesema Jeshi hilo linafanya uchunguzi wa matukio ya vifo vilivyotokea kwa nyakati tofauti Tarime/Rorya pamoja na Jijini Arusha ikiwemo tukio la kifo cha Dickson Tadeus Joseph, mkazi wa Rebu Senta Wilayani Tarime kilichotokea Januari 01, 2026 huko katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime.

“Baada ya kutokea kifo hicho, Jeshi la Polisi limepokea barua ya malalamiko kuwa, kifo hicho hakikutokana na Dickson Tadeus Joseph (marehemu) kuanguka katika eneo la Mtaa wa Serengeti wakati akikimbia k**a ilivyo elezwa awali bali kimesabababishwa na Askari Polisi.” Amesema Misime.

Kulingana na Polisi, uchunguzi wa kina umeanza kuhusu tukio hilo na kulingana na ushahidi kutoka kwa watu walioshuhudia, ikibainika kuna Askari aliyehusika hatua stahiki kwa mujibu wa sheria zitachukuliwa dhidi yake.

Misime amezungumzia pia taarifa ya Viollete Uwumuhoza, Raia wa Rwanda ambaye alijinyonga Januari 07, 2026 akiwa mahabusu ya Polisi Jijini Arusha, alikokuwa akishiliwa kwa kosa la kuingia na kuishi nchini kinyume cha Sheria ambapo uchunguzi wa kina unaohusisha uchunguzi wa kisayansi na wa haraka unaendelea kuhusiana na tukio hilo.

07/01/2026

Watanzania wamehimiza kuwa makini na wanaojiita wanaharakati nchini, akitahadharisha uwepo wa baadhi ya makundi yenye sababu nyingine na dhamira ya kueneza chuki kwa watanzania kwa kutumia kivuli cha uanaharakati wa masuala mbalimbali katika jamii.

Wito huo umebainishwa na Mchambuzi wa masuala ya siasa nchini Tanzania Bw. Rajab Said Nyangasa wakati akizungumza kwenye kipindi cha “Watu na stori” kinachorushwa na runinga ya Mtandaoni Jijini Dar Es Salaam, akisema hilo ndilo tatizo kubwa katika kizazi cha leo ikiwa ni pamoja na wengi kuamini zaidi upande wa kwanza kuzungumza hata ikiwa wanachozungumza hakina ukweli na uhalisi.

“Tunayo shida, na shida yetu kwenye kizazi cha leo ni kuwa zikisimama pande mbili, ya kweli na ya uongo ni kuwa pande itakayokuwa ya kwanza kuzungumza itaaminika maradufu sasa kuna watu wanatumia muavuli wa uanaharakati kutimiza nia mbaya na kukuza uadui na bahati mbaya ubaya huu ukienda kwa jamii, jamii mara nyingi haina muda wa kuangalia kinachosemwa na watu hawa wanaojiita wanaojiita wanaharakati ni kweli ama si kweli “ amesema Bw. Nyangasa.

Nyangasa ameeleza kuwa watu hao ndio sababu ya baadhi ya changamoto nyingi za kijamii nchini, kauli ambayo imekuja siku chache mara baada ya mfululizo wa shutuma ambazo zimekuwa zikielekezwa kwa baadhi ya watu ambao wamekuwa sababu ya kuhamasisha matukio ya uvunjifu wa amani nchini pamoja na kueneza chuki kwa watanzania dhidi ya Viongozi wa serikali ya awamu ya sita.

Address

Kinondoni B
Dar Es Salaam

Telephone

+255768108051

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BINGO_onlinetz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share