BINGO_onlinetz

  • Home
  • BINGO_onlinetz

BINGO_onlinetz Official page ya BINGO TV
email [email protected]

CHINI YA RAIS SAMIA KIASI CHA MIKOPO KWA WAJASIRIAMALI CHAONGEZEKAChini ya Rais Samia kiasi cha mikopo ya Wajasiriamali ...
13/07/2025

CHINI YA RAIS SAMIA KIASI CHA MIKOPO KWA WAJASIRIAMALI CHAONGEZEKA

Chini ya Rais Samia kiasi cha mikopo ya Wajasiriamali chaongezeka kutoka TZS7Trilioni hadi TZS14Trilioni Wakati Rais Samia Suluhu anaingia madarakani Wajasiliamali waliopewa mikopo binafsi (Personal loans ),thamani ya mikopo hiyo ilifikia jumla ya TZS 7Trilioni miaka minne baadae mikopo hii imefikia jumla ya TZS 14Trilioni sawa na ongezeko la TZS7Trilioni au 100% pia ni ongezeko la mara mbili, haya ni matokeo ya Uongozi wenye maono wa Rais Samia Suluhu Hassan unaotambua nafasi ya wajasilimali wadogo na wakati, ambao idadi yao ni 90% ya biashara zote duniani, wakichangia 50% ya ajira na karibu asilimia 70% ya uchumi wa dunia ( kwa mujibu wa Ripoti ya Hali ya Uchumi (2024)

Ibrahim Traoré anakataa mwaliko wa kutembelea Marekani, akithibitisha kwamba kwa sasa anashughulika na kuwahudumia watu ...
12/07/2025

Ibrahim Traoré anakataa mwaliko wa kutembelea Marekani, akithibitisha kwamba kwa sasa anashughulika na kuwahudumia watu wa Burkina Faso na hana muda wa masuala ya kidiplomasia.

Mbunge wa Jimbo la Kisesa anayemaliza muda wake Luhaga Mpina huenda safari yake ya kuwawakilisha wananchi wa Kisesa ikaf...
12/07/2025

Mbunge wa Jimbo la Kisesa anayemaliza muda wake Luhaga Mpina huenda safari yake ya kuwawakilisha wananchi wa Kisesa ikafikia tamati ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwaka huu baada ya vikao vya mchujo kwa ngazi ya wilaya ya Meatu na mkoa wake wa Simiyu kumtupa nje ya mbio za kuwania kuteuliwa na CCM kupeperusha bendera kwenye nafasi ya ubunge katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu.

Mpina Mbunge machachari ndani na nje ya Bunge aliyejipatia umaarufu kwenye takribani miaka mitano sasa kwa kuibana serikali ndani ya Bunge na hata nje ya Bunge kwa hoja mbalimbali amekumbana na rungu la chama chake ngazi ya wilaya na mkoa baada ya vikao vya Kamati ya Siasa ya CCM wilaya ya Meatu kumtupa nje kwa kutopendekeza jina lake.

maamuzi ambayo yamebarikiwa na chama ngazi ya mkoa hivyo sasa nafasi ya mwisho ya yeye kupenya jina lake kwa ajili ya kwenda kwenye mchakato wa kura za maoni ikibakia vikao vya ngazi ya taifa kwa maana ya Kamati Kuu ambayo imepewa mamlaka ya kufanya uteuzi wa mwisho.

Katika jimbo hilo, wagombea waliokuwa wakichuana katika hatua ya awali walifikia 14, lakini kupitia kikao cha wilaya na mkoa, majina yaliyopendekezwa ni Sitta Risinge, M***a Mbuga, na Silinde Gumada.

Full video & story ipo Youtube

Sponsored by Wanauza na Kununua Magari Tz.



12/07/2025

Msanii Akiwasha Kwenye Tour Yake Iloyopewa Jina La ambapo ameanzia nchini Na Huo Ni Mwanzo Tu.

Full video & story ipo Youtube

Sponsored by Wanauza na Kununua Magari Tz.



Miradi ya kilimo chini ya Rais Samia imezalisha ajiramara arobaini ya zilizokuwepo mwaka 2020Miradi ya kilimo iliyosajil...
12/07/2025

Miradi ya kilimo chini ya Rais Samia imezalisha ajira
mara arobaini ya zilizokuwepo mwaka 2020
Miradi ya kilimo iliyosajiliwa katika kituo cha uwekezaji TIC ilizalisha ajira 2,516 mwaka 2020 ambapo mwaka 2024 imezalisha ajira 123,720, hili ni ongezeko la ajira 123,244 ambazo ni mara arobaini na nane ya idadi za ajira zilizozalishwa kutokana na uwekezaji uliofanyika mwaka huo.

Sera nzuri za kiuchumi na mazingira mazuri ya kiuwekezaji, vimechochea katika ongezeko hili ambapo watanzania wanaendelea kunufaika na miradi hii 237 yenye thamani $687.2milioni sawa na TZS1.8Trilioni, Ajira hizi zimetokana na shughuli zifuatazo,

i Ajira za moja kwa moja mashambani
ii Viwanda vya uchakataji
iii Usafirishaji
iv Ajira za ofisini

Rais Samia na ajira 500,000 sekta ya SanaaMwaka 2020 jumla ya idadi ya wasanii waliosajiliwa na baraza la sanaa BASATA n...
11/07/2025

Rais Samia na ajira 500,000 sekta ya Sanaa

Mwaka 2020 jumla ya idadi ya wasanii waliosajiliwa na baraza la sanaa BASATA na kurasimisha kazi zao ilikua ni 377 ambapo miongoni mwao kulikua na wasanii 34 wa ufundi, 172 wa maonesho na 171 kutoka tasnia ya muziki.

Baada ya Rais Samia kuingia madarakani idadi hii imeongezeka na kufikia jumla ya wasanii waliosajiliwa kufikia 992 ambapo miongoni mwao kuna na wasanii wa ufundi 169, maonesho 260 na muziki 563. Ongezeko hili ni sawa na tofauti ya jumla ya wasanii 615 ambayo ni mara mbili ya idadi ya
wasanii wote waliosajiliwa na BASATA kwa mwaka 2020.

Ongezeko hili la usajili na urasimishaji wa kazi za sanaa limechochewa na sababu nyingi ikiwemo uboreshaji wa mifumo ambayo inafanya wasanii
kunufaika na kazi zao, uanzishwaji wa mfuko wa sanaa na utamaduni ambao mpaka kufikia mwezi februari 2025 umefanikiwa na kutoa mikopo
yenye thamani ya TZS5.35bn kwa miradi 359 ya Sanaa iliyozalisha jumla ya ajira 497,213 ikiwemo miradi ya muziki 78, filamu 90, maonesho 65, ufundi
103 na lugha na fasihi 23. Hiki ndicho kinawafanya wasanii wampende zaidi Rais Samia na Serikali yake.
Pamoja na hayo, Sekta ya muziki imepata mikopo yenye thamani ya TZS1.3bn kwa miradi 78, sekta ya filamu imepata mikopo yenye thamani ya TZS1.33bn kwa miradi 90, sekta ya sanaa za ufundi imepata mikopo yenye thamani ya TZS1.6bn kwa miradi 103 na sanaa za maonesho imepata mikopo ya TZS759.1milioni kwa miradi 65. Mifumo iliyoboreshwa pia imepelekea kiasi cha mirabaha kilichogawiwa kwa wasanii waliosajiliwa COSOTA kuongezeka kutoka Shilingi milioni 245 hadi Shilingi milioni 687.7 kwa mwaka 2025

Kiungo staa wa   Hotspur, Pape Matar   amelipa pesa kugharimia umeme wa kijiji kizima huko kwao Senegal. Staa huyo wa Sp...
10/07/2025

Kiungo staa wa Hotspur, Pape Matar amelipa pesa kugharimia umeme wa kijiji kizima huko kwao Senegal. Staa huyo wa Spurs ametumia mamilioni ya pauni kulipia huduma za umeme katika kijiji cha Fayako huko Senegal.

alirejea kijijini Fayako, mahali ambako wazazi wake walitokea na kuwasaidia kulipia gharama za huduma ya umeme.

Alisema wakati alipotembelea Fayako, kisiwa kidogo kilichopo umbali wa maili 100 kutoka mji mkuu wa Senegal, Dakar: “Utaratibu unaendelea kuhusiana na huduma ya umeme. Nina hakika si muda mrefu, Fayako itapendeza k**a watu wake wanavyopendeza. Nakipenda kijiji hiki na najivunia.”

Sambamba na kusaidia kulipia gharama za umeme, Sarr alichangia pia vifaa vya elimu k**a laptop, printa na paneli za umeme wa jua katika shule za kijijini hapo.

Alitoa pia vifaa vya ujenzi kwa ajili ya utanuzi wa kituo cha afya kwenye kijiji hicho. Sarr ameamua kufuata nyayo za shujaa wake, staa wa zamani wa Liverpool, Sadio Mane, ambaye alichangia Pauni 500,000 (Sh 1.8Bilioni) kujenga hospitali kwenye mji wa kwao huko Bambali, Senegal.

Full video & story ipo Youtube
_
Sponsored by Wanauza na Kununua Magari Tz.


Msanii  Tayari Amewasili Bodi Ya Filamu Kuitika Wito Baada Ya Kuitajika Afike Leo Saa Nane Mchana.Full video & story ipo...
10/07/2025

Msanii Tayari Amewasili Bodi Ya Filamu Kuitika Wito Baada Ya Kuitajika Afike Leo Saa Nane Mchana.

Full video & story ipo Youtube
_
Sponsored by Wanauza na Kununua Magari Tz.


Mwanasoka Luka Modrić, mwenye umri wa miaka 39, atahama klabu ya   rasmi baada ya Kombe la Klabu Duniani, k**a alivyoele...
10/07/2025

Mwanasoka Luka Modrić, mwenye umri wa miaka 39, atahama klabu ya rasmi baada ya Kombe la Klabu Duniani, k**a alivyoeleza kocha mpya wa , Massimiliano Allegri.  

Amekubali mkataba wa mwaka mmoja wa kuchezwa AC Milan, hadi Juni 2026, na kuna chaguo la kuongeza mwaka mwingine.

Uhamisho huu umethibitishwa zaidi na Mkurugenzi wa Michezo wa AC Milan, Igli Tare, pamoja na Fabrizio Romano.

Rekodi Kuu na Mafanikio ya Modrić kwa Madrid,Alijiunga na Real Madrid mwaka 2012, akicheza mechi karibu 597 na kufunga magoli 43.

Amefanikiwa kunyakua jumla ya mataji 28 ikiwemo UEFA Champions League 6 mara, La Liga 4, Copa del Rey, UEFA Super Cup, na Klabu la Dunia (Club World Cup).

Full video & story ipo Youtube
_
Sponsored by Wanauza na Kununua Magari Tz.


Kesi namba 8323/2025 ya mgawanyo wa rasilimali za Chama cha Demokrasia na Maendeleo iliyokuwa inaendelea katika Mahak**a...
10/07/2025

Kesi namba 8323/2025 ya mgawanyo wa rasilimali za Chama cha Demokrasia na Maendeleo iliyokuwa inaendelea katika Mahak**a Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Dar Es Salaam, imeahirishwa mpaka Jumatatu ya tarehe 14, Julai 2025 saa nne asubuhi.

Ahirisho hili limekuja baada ya mawakili wa upande wa waleta maombi kuiomba mahak**a kupata muda wa kwenda kuisoma na kutafakari barua iliyopelekwa mahak**ani hapo na upande wa wajibu maombi (Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa CHADEMA na Katibu Mkuu).

Wakili wa wajibu maombi Mpale Mpoki aliieleza Mahak**a kuwa wateja wake waliandika barua kwenda kwa Naibu Msajili wa Mahak**a kuomba na kutaka Jaji Hamidu Mwanga ajitoe kusikiliza kesi namba 8323/2025.

Wakili Mpoki ameileza mahak**a kuwa walichelewa kuupatia upande wa waleta maombo nakala ya barua kutokana na kwamba barua hiyo ilikuwa ni ya mahak**a tu hivyo hawakufahamu k**a upande wa waleta maombi wanapaswa kuapatiwa nakala ngumu.

Hata hivyo kuahirishwa kwa shauri hilo kunaathiri maombi yaliyowasilishwa mahak**ani na upande wa CHADEMA ya kuiomba mahak**a kufuta uamuzi alioutoa Jaji Mwanga Juni 10, juu ya kusimamishwa kwa shughuli za CHADEMA.

Full video & story ipo Youtube
_
Sponsored by Wanauza na Kununua Magari Tz.


10/07/2025

Rais wa Marekani Donald Trump ameeleza kuwa Urusi ilifanya mashambulizi makubwa ya ndege zisizo na rubani dhidi ya Ukraine saa chache tu baada ya kauli yake ya Kuahidi uungaji mkono zaidi wa kijeshi kwa Kyiv na kumshutumu mwenzake wa Urusi Vladimir Putin kwa kutoa maneno makali juu ya mazungumzo ya amani.

Mpaka sasa taarifa zinaeleza kuwa ni mtu mmoja aliuawa.

Full video & story ipo Youtube

Sponsored by Wanauza na Kununua Magari Tz.

na maafisa wa Ukraine.

Address


Telephone

+255768108051

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BINGO_onlinetz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share