BINGO_onlinetz

BINGO_onlinetz Official page ya BINGO TV
email [email protected]

Wekeni ushabiki Pembeni nani Kabaruza leo😂
12/09/2025

Wekeni ushabiki Pembeni nani Kabaruza leo😂

12/09/2025

WASANII WA MAMA ONGEA NA MWANAO NA LAMATA VILLAGE WAWA KIVUTIO KAMPENI ZA DKT. SAMIA

Wasanii kutoka makundi mawili maarufu nchini, Mama Ongea na Mwanao na Lamata Village wakiongozwa na na wamegeuka kivutio katika Kampeni za Mgombea Urais Kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi kubwa wanayoifanya mikoani.

Wasanii hao kila wanakopita wanaibua shangwe kubwa sana kutoka kwa wafuasi na pale wanapopanda jukwaani kumuombea kura Dkt. Samia Suluhu basi Wananchi wengi wanawaahidi kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan mwezi Oktoba.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Askofu Mkuu wa Jimbo K...
12/09/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Tabora Kardinali Protase Rugambwa pamoja na Baba Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo hilo Mhashamu Baba Askofu Paul Ruzoka, Ikulu Ndogo ya Tabora tarehe 12 Septemba, 2025. Pamoja na mambo mengine pia Maaskofu hao walimuombea Rais Dkt. Samia ambaye anagombea nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).

DKT. SAMIA: KILA MKAZI WA URAMBO ATAONA MAENDELEO HALISIMgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama C...
11/09/2025

DKT. SAMIA: KILA MKAZI WA URAMBO ATAONA MAENDELEO HALISI

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kuendeleza maendeleo katika Wilaya ya Urambo kupitia miradi mikubwa ya afya, elimu, maji, kilimo, na miundombinu.

Akizungumza katika kampeni za uchaguzi mkuu wa 2025, Dkt. Samia amebainisha kwamba ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri umekamilika na huduma za matibabu zimeimarika, ikiwemo huduma 32 muhimu za afya. Aidha, miundombinu ya elimu inaendelea kuboreshwa kwa ujenzi wa vyumba 350 vya madarasa ya shule za msingi na sekondari, pamoja na Shule ya Msingi yenye mtaala wa Kiingereza. Pia, Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kimepangwa kujengwa ili kukuza ufundi stadi miongoni mwa vijana.

Dkt. Samia ameongeza kuwa huduma za maji safi na salama zinaendelea kupanuliwa kupitia miradi ya upatikanaji na usambazaji wa maji, ikiwemo upanuzi wa mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria na uchimbaji wa visima vipya. Aidha, katika sekta ya kilimo, kuimarika kwa upatikanaji wa mbolea ya ruzuku kunatarajiwa kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara.

Kuhusiana na miundombinu, Dkt. Samia ameahidi ujenzi wa barabara za lami, matengenezo ya barabara za changarawe, ujenzi wa soko la kisasa, bwawa na skimu za umwagiliaji, pamoja na hoteli ya kisasa na vibanda vya stendi kuu ya mabasi. Ahadi hizi ni sehemu ya mpango wa maendeleo unaolenga kuinua kipato cha wananchi na kuboresha maisha yao kwa ujumla.

DKT. SAMIA: TUTAIMARISHA BEI YA MAZAO NA KUBORESHA UFUGAJI IGUNGAMgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. S...
10/09/2025

DKT. SAMIA: TUTAIMARISHA BEI YA MAZAO NA KUBORESHA UFUGAJI IGUNGA

Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Septemba 10, 2025, ameahidi kuendelea kuimarisha sekta ya kilimo na ufugaji mkoani Tabora, akibainisha kuwa lengo ni kumkomboa mkulima na mfugaji kwa kuhakikisha mazao na mifugo vinanufaisha wananchi kiuchumi.

Akizungumza mbele ya maelfu ya wananchi wa Wilaya ya Igunga, Dkt. Samia amesema tayari Serikali imesambaza tani 176 za mbolea ya ruzuku na matrekta zaidi ya 30 kwa wakulima wa eneo hilo.

Aidha, amebainisha kuwa iwapo atapewa ridhaa ya kuongoza awamu ijayo, ataendeleza mikakati ya kutoa pembejeo za kilimo kwa wakulima ili kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi.

Katika sekta ya ufugaji, Dkt. Samia ameahidi kutenga maeneo maalum ya malisho na maji kwa mifugo, sambamba na kutoa ruzuku za chanjo kwa wafugaji, lengo likiwa ni kuhakikisha mifugo kutoka Tanzania inatambulika kimataifa, hasa kibiashara, kwa kuzingatia ubora wa afya ya mifugo.

SAMIA AAPA KUIPANDISHA IGUNGA VIWANGO: HOSPITALI, MAJI NA BARABARA KWA WANANCHIMgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM...
10/09/2025

SAMIA AAPA KUIPANDISHA IGUNGA VIWANGO: HOSPITALI, MAJI NA BARABARA KWA WANANCHI

Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewahamasisha wananchi wa Igunga kuunga mkono utekelezaji wa Ilani ya CCM 2025, akisisitiza mafanikio yaliyopatikana na kutoa ahadi mpya za maendeleo zinazolenga kuboresha maisha ya kila mwananchi.

Dkt. Samia alisema wilaya ya Igunga imepata mafanikio makubwa katika sekta ya afya, ikiwemo ukarabati wa Hospitali ya Halmashauri na kukamilika kwa ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi, jambo lililoleta huduma bora kwa wagonjwa. Katika sekta ya elimu, idadi ya shule za msingi na sekondari imeongezeka, huku Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Stadi (VETA) kikiwa ni jukwaa muhimu la kuwajengea vijana ujuzi wa kiufundi na stadi za maisha.

Sekta ya kilimo na biashara imeimarishwa kwa ongezeko la uzalishaji wa mazao ya chakula, upatikanaji wa mbolea na kuendelezwa kwa viumbeaji na uzalishaji wa vifaranga vya samaki. Aidha, mtandao wa barabara mjini na vijijini umeboreshwa, kurahisisha usafirishaji wa wananchi na bidhaa zao, jambo linaloongeza mapato na fursa za biashara.

Baada ya kufafanua mafanikio, Dkt. Samia alitoa ahadi zinazolenga kusukuma mbele maendeleo. Ahadi hizo ni pamoja na ujenzi wa vituo viwili vya afya Uswaya na Kining’inila, ukamilishaji wa maboma ya madarasa 180 katika shule za msingi, maboma ya maabara 20 katika shule za sekondari, na nyumba 37 za walimu.

Zaidi ya hayo, Dkt. Samia aliahidi ujenzi wa mabwawa na skimu katika vijiji vya Igurubi, Buhekela, Simbo, Itumba, Mwamapuli, Mwalunili, Makomelo na Mwashiku, pamoja na ujenzi wa Soko Kuu la wafanyabiashara wadogo na wakubwa, kuboresha maeneo ya uwekezaji, na kukamilisha maboma ya majosho 15 pamoja na mabirika ya kunyweshea mifuko 3.

Katika sekta ya michezo, ujenzi wa kiwanja cha michezo cha Halmashauri na jengo jipya la ofisi za Halmashauri unaendelea, kuimarisha burudani, michezo na utendaji bora wa utawala

Watoto wetu wanastahili shule bora, vijana wanastahili ajira, wakulima wanastahili tija – CCM inaleta yote haya
09/09/2025

Watoto wetu wanastahili shule bora, vijana wanastahili ajira, wakulima wanastahili tija – CCM inaleta yote haya




Kufatia ajali aliyopata  akiwa location  ameibuka na Kudai Uchafuni wanataka kumtoa kafara hivyo awahi akafanyie dua kwa...
09/09/2025

Kufatia ajali aliyopata akiwa location ameibuka na Kudai Uchafuni wanataka kumtoa kafara hivyo awahi akafanyie dua kwasababu alishaoteshwa.

PICHA:Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan k...
09/09/2025

PICHA:Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Matukio tofauti ya picha alipozungumza na Umati wa Wananchi wa Wilaya ya Bahi Mkoani Dodoma waliofurika Barabarani kumlaki wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu akiwa njiani kuelekea Mkoa wa Singida leo Septemba 09, 2025.

Mgombea wa Nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt....
06/09/2025

Mgombea wa Nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Mafinga katika muendelezo wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu kwa Chama hicho mkoani Iringa tarehe 06 Septemba, 2025.

Address

Kinondoni B
Dar Es Salaam

Telephone

+255768108051

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BINGO_onlinetz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share