03/06/2026
Bunge la Jamhuri ya Zimbabwe limepitisha hatua yake ya kwanza ya usomaji bungeni kwa muswada tata ambao unaweza kuongeza muda wa muhula wa Urais na Ubunge kutoka miaka mitano hadi saba katika sheria inayolenga kurekebisha katiba Pia muswada huo unalenga kubadilisha mfumo wa uchaguzi wa rais, ambapo badala ya kura ya moja kwa moja ya wananchi, bunge litakuwa na mamlaka ya kumchagua kiongozi wa nchi ambapo Ibara zenye utata zaidi zinapendekeza kuruhusu Rais Mnangagwa na wabunge kusalia ofisini hadi 2030 Marekebisho yaliyopendekezwa yamesababisha ghadhabu kwa wananchi na yanakabiliwa na changamoto kadhaa za kisheria. Wakosoaji wakiwemo Chama cha Wanasheria nchini humo wanasema mapendekezo hayo yanadhoofisha taasisi za kidemokrasia na kulimbikiza madaraka kwa rais. Makanisa makubwa na mashirika ya haki za binadamu wanasema mabadiliko hayo ni kinyume na katiba na yanahitaji kura ya maoni. Muswada huo Utasomwa mara ya pili Jumatano wakati wabunge watakapojadili uhalali wa marekebisho zaidi ya kumi na utahitaji angalau theluthi mbili ya kura katika Mabunge yote mawili ili kupitishwa.