AV MEDIA TZ

AV MEDIA TZ Your number one source of all the Entertainment News, Music, Gossips & an Audiovisual.

29/07/2025

Mke wa Jux, Priscilla ambaye anatarajia mtoto hivi karibuni, akifurahia safari yake ya ujauzito!.

Timu ya Simba SC imetangaza rasmi kuingia mkataba mkubwa wa udhamini na kampuni ya kimataifa ya betting, Betway, wenye t...
29/07/2025

Timu ya Simba SC imetangaza rasmi kuingia mkataba mkubwa wa udhamini na kampuni ya kimataifa ya betting, Betway, wenye thamani ya Sh20 bilioni kwa kipindi cha miaka mitatu.

Kupitia mkataba huo, Betway inakuwa mdhamini mkuu mpya wa klabu hiyo kubwa Afrika Mashariki na Kati.

Mtendaji Mkuu wa Simba, Zubeda Sakuru amesema kuwa udhamini huo utakuwa na faida kubwa kwa klabu hiyo.

“Mkataba ambao tumeingia unakwenda kuleta mapinduzi kwenye mchezo wa soka hapa Tanzania na unakwenda kuongezea nguvu dhamira ya Simba kuwa klabu namba moja barani Afrika”.

“Udhamini huu ambao thamani yake ni Bilioni 20 kwa miaka mitatu, unaonyesha namna Simba imedhamiria kuleta mabadiliko ya kuwa klabu kubwa,” amesema Zubeda.

29/07/2025

Ni Diamond Platnumz na Zuchu!.

Mshindi wa Grammy kutoka Afrika Kusini, Tyla ameonesha kukoshwa mno na kile ambacho Wizkid amekuwa akikifanya kwenye muz...
29/07/2025

Mshindi wa Grammy kutoka Afrika Kusini, Tyla ameonesha kukoshwa mno na kile ambacho Wizkid amekuwa akikifanya kwenye muziki kwa miaka zaidi ya 10 sasa.

Tyla akiongea na Kiss Xtra ya Uingereza, alimuelezea Wizkid k**a nguli wa muziki wa Afrika ambaye amekuwa akipambana kuupeleka muziki wa Afrika kimataifa.

29/07/2025

Mke wa Jux, Priscilla pamoja na Mama yake mzazi Ojo katika moja ya sherehe hivi majuzi.

Hatimaye Mr. Blue ametunukiwa tuzo yake ya kwanza kabisa kwenye taaluma yake ya muziki kupitia Entertainment Arts Excell...
29/07/2025

Hatimaye Mr. Blue ametunukiwa tuzo yake ya kwanza kabisa kwenye taaluma yake ya muziki kupitia Entertainment Arts Excellence Awards (EAEA) 2025, akitambuliwa k**a Living Legend of the Year.

Mr. Blue alianza muziki miaka ya 2000 akiwa kijana mdogo na amebaki kuwa mmoja wa wasanii waliotoa mchango mkubwa kwenye ukuaji wa muziki wa Bongofeva.

29/07/2025

Mastaa wa Bongofleva, Nandy, Zuchu, Diamond Platnumz na Billnass wakiwa studio kwa S2kizzy pale Pluto Republic.

29/07/2025

Mwimbaji wa Bongofleva, Diamond Platnumz akifurahia baada ya Baba Levo kupitishwa na CCM kuwa miongoni mwa wagombea Ubunge ndani ya Chama hicho jimbo la Kigoma Mjini.

28/07/2025

Rapa wa Marekani, Kendrick Lamar katika show yake huko Lisbon, Ureno.

Mwanamuziki wa Bongofleva, Jux na mkewe Priscilla kutokea nchini Nigeria wanatarajia kupata mtoto wao wa kwanza muda sio...
25/07/2025

Mwanamuziki wa Bongofleva, Jux na mkewe Priscilla kutokea nchini Nigeria wanatarajia kupata mtoto wao wa kwanza muda sio mrefu.

Ikumbukwe Februari ndipo Jux alifunga ndoa na mpenzi wake kutokea Nigeria, Priscilla ambaye waliweka wazi uhusiano wao mnamo Julai 2024.

Tazama picha zaidi kwenye comments.

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma (Mwana FA), leo amekutana na kufanya kikao maal...
22/07/2025

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma (Mwana FA), leo amekutana na kufanya kikao maalum cha usuluhishi kati ya msanii wa muziki wa kizazi kipya, Billnass, na msambazaji wa kazi za muziki, Mx Carter.

Kikao hicho kimefanyika kufuatia malalamiko ya hadharani yaliyotolewa na Billnass kupitia mitandao ya kijamii, ambapo alieleza kutoridhishwa na namna kazi zake zinavyosambazwa na kutopata faida inayostahili kupitia majukwaa ya kidigitali.

Malalamiko hayo yamezua mjadala mpana kuhusu maslahi ya wasanii na usimamizi wa haki zao za kazi za sanaa.

Katika kikao hicho, Naibu Waziri amesikiliza pande zote mbili na kutoa mwongozo wa kisheria na kiutawala kwa lengo la kuhakikisha haki na maslahi ya msanii yanalindwa bila kuvunja mikataba iliyopo.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa mawasiliano ya moja kwa moja kati ya wasanii na wasambazaji, pamoja na kuhimiza matumizi ya mifumo rasmi ya usambazaji inayohakikisha uwazi wa mapato.

“Kama Wizara, tutaendelea kuwa sehemu ya kutafuta suluhu kwa changamoto za wasanii wetu, lakini pia ni jukumu la pande zote kuhakikisha mikataba inazingatia haki na uwiano wa mapato,” alisema Mhe. Mwinjuma.

Kikao hicho pia kimehudhuriwa na maafisa kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), pamoja na COSOTA, ili kuhakikisha suluhu ya kudumu inapatikana kwa misingi ya haki na uwazi.

Hii ni hatua muhimu katika kulinda hadhi ya msanii wa Kitanzania na kuimarisha tasnia ya muziki nchini.

Mwimbaji wa Bongofleva kutokea WCB Wasafi, Diamond Platnumz amesema alikataa ofa ya kusaini na Roc Nation ambayo ilikuwa...
21/07/2025

Mwimbaji wa Bongofleva kutokea WCB Wasafi, Diamond Platnumz amesema alikataa ofa ya kusaini na Roc Nation ambayo ilikuwa na kitita cha Sh675 milioni.

Diamond amesema baada hapo, ndipo akaenda kusaini Warner Music kwa Sh13.5 bilioni, ofa ambayo aliona ni nzuri kwake.

Kauli ya Diamond inakuja baada ya mdau mmoja wa JamiiForums kuhoji kwanini wasanii wa Tanzania hawasainiwi na lebo kubwa za muziki duniani.

Address

Mbezi Beach
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AV MEDIA TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to AV MEDIA TZ:

Share