Pambazuko

Pambazuko Linasambazwa bure kupitia Mtandao wa WhatsApp. Kila mtu anaombwa kusambaza bila ubaguzi.

Pambazuko ni gazeti la lugha adhimu ya Kiswahili linalosambazwa kila Jumatatu na timu ya wahariri kutoka nchi mbalimbali; Tanzania, Kenya, Uganda, DR Congo na Rwanda.

Time flies! It is 29 years together!
30/12/2024

Time flies! It is 29 years together!

Kila heri kwa wasomaji wetu, wanasafu, waandishi wa habari na wajuvi pamoja na wanaojifunza Kiswahili kupitia gazeti la ...
24/12/2024

Kila heri kwa wasomaji wetu, wanasafu, waandishi wa habari na wajuvi pamoja na wanaojifunza Kiswahili kupitia gazeti la Pambazuko.

Hapi, Makalla, Mongella waula CCMNa Mwandishi WETUCHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimemkumbuka Ally Hapi na kumpa nafasi ya ku...
03/04/2024

Hapi, Makalla, Mongella waula CCM

Na Mwandishi WETU

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimemkumbuka Ally Hapi na kumpa nafasi ya kuwa mtendaji mkuu wa jumuia yake ya wazazi.

Hapi ambaye baada ya kunyofolewa kwenye dhamana ya ukuu wa mkoa wa Iringa, aliamua kuwa mkulina na muuza nyanya, kazi ambayo anaonekana kuifurahia zaidi, maana "hakukauka" kwenye mitandao ya jamii - hasa Facebook na Instagram, kuonesha mafanikio yake.

Katika kikao chake cha halmashauri kuu ya chama hicho, kilichofanyika leo, Ikulu, Dar es Salaam, Amos Makalla na John Mongella, ambao waliokuwa wakuu wa mikoa kabla ya kutangazwa kuondolewa juzi, sasa wamepata uteuzi.

Soma taarifa ya chama hicho tawala hapa.

Siku 10 zatosha kuingia Ikulu. Rais mpya Senegal aapaNa Mwandishi WETUMUNGU akiamua jambo lake kwa yeyote, hakuna wa kuz...
02/04/2024

Siku 10 zatosha kuingia Ikulu. Rais mpya Senegal aapa
Na Mwandishi WETU
MUNGU akiamua jambo lake kwa yeyote, hakuna wa kuzuia; siyo nguvu za dola, fedha, hila, ujambazi wala dhamana.
Hiyo imedhihirika leo baada ya Bassirou Faye, mwenye miaka 44, kuapishwa kuwa rais wa tano wa Senegal. Nchi hiyo ilipata uhuru wake mwaka 1960.
Rais huyo mpya wa Senegal, anaweka historia ya kuwa kiongozi mwenye umri mdogo zaidi kupata kutokea kwenye nchi hiyo ambayo imekuwa ikigubikwa na machafuko, hasa vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Faye katika harakati zake za kuingia Ikulu, “amepigwa figisu” kila mahali, ikiwamo kufungwa na kusingiziwa makosa ya uhaini na ugaidi.
Kinachoshangaza, Faye anakalia kiti cha kuongoza Senegal, baada ya kufanya kampeni kwa siku 10, tena akiwa anatokea gerezani, alikowekwa na utawala uliopita.
Faye, mwenye wake wawili, aliapishwa mapema leo katika Mji wa Diamniadio, ambao uko nje kidogo ya Jiji la Dakar.
Katika hotuba yake fupi baada ya kuapishwa, Faye aliahidi kuiunganisha nchi hiyo kwa kuwa na amani, kuzika ubaguzi wa kiitikadi na imani na zaidi sana kuhakikisha maisha ya wananchi yanakuwa nafuu.

Mke aua mume kwa kumchoma ‘kisu’Na Mwandishi WETUMAISHA sasa yamebadilika na matukio ya kutisha yahakita vichwa vya haba...
02/04/2024

Mke aua mume kwa kumchoma ‘kisu’
Na Mwandishi WETU
MAISHA sasa yamebadilika na matukio ya kutisha yahakita vichwa vya habari kila uchao.
Tukio jingine la kutisha limetokea leo asubuhi katika mji mdogo wa Kibara, wilayani Bunda, Mara baada ya mke kumuua mumewe kwa kumchoma ma kitu chenye ncha kali kifuani. Kitu hicho kinadaiwa kuwa kisu.
Habari ambazo Pambazuko limezipata mapema leo zinaeleza kuwa aliyeuawa ni Ofisa Kilimo wa Kata ya Neruma wilayani Bunda, Julius Rubambi ambaye ana umri wa miaka 38.
Pambazuko limeelezwa kuwa mke wa Julius aitwaye Elizabeth Stephen mwenye miaka 30, alimchoma mumewe kisu kifuani baada ya kutokea ugomvi kati yao.
Inaelezwa kuwa mke na mume walikuwa na ugomvi ambapo walipigana baada ya kushindwa kuelewana kuhusu jambo ambalo bado vyombo vya usalama na gazeti hili vinafuatilia.
Elizaberth naye amelazwa katika Hospitali ya Kibara akiendelea na matibabu baada ya kupata majeraha kutokana na kioigo cha mumewe, Julius.
Pambazuko linafuatilia kwa karibu na linaendelea kuchunguza kupata kilichosababisha ugomvi kati yao.
Usiache ku – like na ku- comment kwenye ukurasa huu wa Facebook na waeleze wenzako wafuatilie habari kupitia hapa.

02/04/2024

Gazeti lako la Pambazuko halikuwa hewani Jumatatu hii kutokana na sababu za kiufundi. Tuonane wiki Jumatatu ijayo - Mhariri

Simba ina nafasi, Yanga inawezaNa Mwandishi WETUMAMBO sasa yamebadilika na “meza ya historia imepinduliwa” baada ya timu...
02/04/2024

Simba ina nafasi, Yanga inaweza

Na Mwandishi WETU

MAMBO sasa yamebadilika na “meza ya historia imepinduliwa” baada ya timu za soka za Tanzania kuweza “kuwavimbia” na hata kuwafunga Waarabu.

Timu kutoka Misri, Tunisia, Algeria na Morocco, zilikuwa na uhakika wa kuzifunga timu za Tanzania na hazikuwa na hofu yoyote; iwe ndani ya nchi zao au zinazpokuwa Dar es Salaam.

Miongo k**a miwili iliyopita timu kutoka nchi hizo za Kiarabu, ambayo ilipangwa kucheza na timu yoyote ya Tanzania, ingeweza kufika Dar es Salaam asubuhi ya siku ya mechi, jioni ikacheza na usiku huohuo ikaondoka kurudi kwao, huku ikiwa imepata ushindi mkubwa.

Hata hivyo, mambo yamekuwa tofauti sana na sasa Waarabu wanacheza na timu za Tanzania, wanakuwa na adabu.

Ipo mifano mingi, lakini moja ni mechi ya kwanza na robo fainali ya Klabu Bingwa Afrika mwishoni mwa wiki iliyopita – Machi 29, timu bora Afrika wakati huu, Al Ahly ya Misri, ililazimika kuja na karibu kila kitu wanachokihitaji kwa ajili ya maandalizi ya mechi yake dhidi ya Simba.

Tena walikuja siku kadhaa kabla ya siku ya mechi. Lakini Al Ahly, ambayo inahesabika kuwa ni timu bora Afrika, iliambulia ushindi mwembamba wa goli moja tu na huo ukiwa ni ushindi wa kwanza wa timu hiyo katika Uwanja wa Benjamin Mkapa katika miaka ya hivi karibuni.

Takriban miaka mitano, Al Ahly walikuwa hawajawahi kupata ushindi katika uwanja huo.

Wakati huohuo, Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini nayo imekiona cha moto juzi – Jumamosi, Machi 30, baada ya kutumia maarifa yao yote, lakini wakaambulia suluhu wakicheza na Yanga katika mchezo mwingine wa robo fainali ya Klabu Bingwa Afrika.

Kabla ya mchezo huo, watu wengi waliaminishwa, kupitia uchambuzi uliojikita katika rekodi za timu hiyo katika miaka ya hivi karibuni, kuwa itapata ushindi mbele ya Yanga. Lakini hali haikuwa hivyo.

Orodha ya wachezaji wa mechi hiyo ilipotolewa, Yanga ikiwa haina wachezaji wake muhimu kadhaa, wengi wakaamini kuwa kipigo kwa Yanga hakiepukiki.

Lakini Yanga ilifanikiwa kuibana Mamelodo na kutoka nayo suluhu na kuwaacha watu wengi na mshangao.

Mechi hizi mbili za robo fainali ya Klabu Bingwa Barani Afrika zimetuacha funzo kubwa.

Kuwa mechi mbili za robo fainali zimechezwa Dar es Salaam zikihusisha timu za Tanzania na hii inamaanisha kuwa Tanzania imeingiza timu mbili katika hatua hiyo kubwa ya mashindano makubwa Afrika.
Katika nchi zote zilizoshiriki mashindano hayo tangu awali hakuna nchi yoyote ambayo imefanikiwa kuingiza timu mbili katika hatua hiyo isipokuwa Tanzania.

Na matokeo ya mechi za kwanza yanaonesha kuwa Simba na Yanga hazikufika katika hatua hiyo kwa kubahatisha.

Hali hii inaweza isishangaze sana kwa Simba ambayo katika kipindi kifupi imefanikiwa kufika mara tano katika mashindano ya Afrika, ikifanya hivyo mara nne katika mashindano ya Klabu Bingwa na mara moja katika Kombe la Shirikisho.

Yanga ilianza kuonesha mabadiliko mwaka jana ambapo ilifanikiwa kufika katika fainali za Kombe la Shirikisho kwa kutolewa kwa kanuni ya goli la ugenini.

Historia inaonesha kuwa katika miaka ya hivi karibuni, Simba imeingia robo fainali ya mashindano ya Afrika mara tano na mwaka jana Yanga ilifika fainali.

Ingawa historia haichezi mpira, lakini ni muhimu kukubali kuwa historia inajengwa na uhalisia. Hivyo, uhalisia ni kuwa viwango vya kucheza vya Simba na Yanga vimeimarika katika miaka ya hivi karibuni.

Hivyo, ingawa baadhi ya watu wameshaikatia tamaa Simba baada ya kufungwa goli moja Dar es Salaam, lakini uhalisia unaonesha kuwa timu hiyo bado ina nafasi ya kuitoa Al Ahly na kusonga mbele katika mashindanipo hayo.

Aidha, suluhu iliyoipata Yanga mbele ya Mamelodi huku ikipungukiwa na wachezaji wake muhimu, inadhihirisha kuwa timu hiyo inaweza kuitoa Mamelodi katika mechi ya marudiano itakayofanyika Aprili 5 huko Afrika Kusini.

Viwango
Lakini kwa ujumla ukiangalia timu zilizoingia kwenye hatua ya robo fainali ya mashindano ya Klabu Bingwa Afrika msimu huu, utabaini kuwa hali ya mchezo wa soka katika eneo la Afrika Mashariki na Kusini imeboreka kwa kiasi kikubwa.

Kati ya timu nane zilizoingia katika hatua hiyo, tano zinatoka katika ukanda wa SADC. Timu hizo ni Yanga na Simba kutoka Tanzania, Mamelod ya Afrika Kusini, TP Mazembe ya DRC na Atletco de Angola kutoka Angola.

Kuna timu moja tu kutoka Afrika Magharibi na Afrika Kaskazini imetoa timu mbili.

Miaka kadhaa iliyopita hakuna mtu alitarajia hali k**a hiyo. Ukiacha TP Mazembe, hakuna timu nyingine iliyokuwa inajitutumua kufika hatua hiyo kutoka eneo la SADC mpaka pale Mamelodi nayo ilipojiingiza kwa kasi kwenye soka la Afrika. Sasa hivi Simba na Yanga nazo zimeingia huko.

Hii inaonesha kuwa ule utawala wa soka kwa nchi za kaskazini na magharibi mwa Afrika, sasa mzani umegeuka.

Imepatikana sasa hivi kutoka Ikulu.Mabadiliko Baraza la Mawaziri na kuhamishwa ama kutenguliwa kwa watendaji wa serikali...
30/03/2024

Imepatikana sasa hivi kutoka Ikulu.

Mabadiliko Baraza la Mawaziri na kuhamishwa ama kutenguliwa kwa watendaji wa serikali anayoongoza Rais Samia Suluhu Hassan.

Aliyefungwa miaka 23 kwa ujangili atoroka Mwandishi WETUMFUNGWA Amos Bernard Mtinange, maarufu kwa jina la Meja,  aliyek...
27/03/2024

Aliyefungwa miaka 23 kwa ujangili atoroka
Mwandishi WETU
MFUNGWA Amos Bernard Mtinange, maarufu kwa jina la Meja, aliyekuwa anatumikia kifungo cha 23 kwa ujangili, ametoroka akiwa chini ya ulinzi, wilayani Babati, Manyara, Pambazuko linaeleza.
Mfungwa huyo ametoroka akiwa katika shamba la Magereza akifanya kazi chini ya usimamizi wa askari wenye silaha.
Alihukumiwa kifungo hicho Novemba mwaka Jana.
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Manyara (RPO), Solomon Mwambingu amethibitisha tukio hilo jana na kusema – “kweli Meja ametoroka.”
"Tunazo hizo taarifa na suala hili linafanyiwa kazi, " amesema mkuu huyo wa Magereza, huku akigoma kueleza mazingira ya Meja kutoroka.
Meja anadaiwa kutoroka Alhamisi ya wiki iliyopita akiwa na mfungwa mwingine ambaye alik**atwa na askari wa Magereza siku hiyohiyo.

Tukemee ufisadi ndani ya familia kwanzaNa Frt. Benedict Msoffe,Roma, ItaliaJAMII ndiyo hazina ya nchi. Kutoka humo nchi ...
27/03/2024

Tukemee ufisadi ndani ya familia kwanza

Na Frt. Benedict Msoffe,
Roma, Italia

JAMII ndiyo hazina ya nchi. Kutoka humo nchi hupata viongozi wa kisiasa na hata wa kidini, wataalamu, wafanyakazi, wazazi, vijana na kila aina ya raia itakayokuwa nao.
Manazuoni Abraham J. Heschel, mwenye asili ya Uyahudi na mchambuzi, anaeleza kazi ya manabii katika kitabu chake, “The Prophets.”.
Uchambuzi wake unaangazia hasa hali ya kijamii na kisiasa ya Israeli wakati wa unabii wa manabii wa kwanza kuweka kazi zao katika maandishi (Amos, Hosea, Isaya na Mika).
Mmoja wa manabii hao ambaye unabii wake ulitawaliwa na hisia kali za kukemea na kuonya dhidi ya uasi wa watu alikuwa Hosea.
Katika mambo mengi, Nabii Hosea alipigia kelele ufisadi.
Kwa Hosea, ufisadi ni ishara ya kwamba jamii nzima imeoza kabisa kuanzia katika “mizizi hadi matawi.”
Hosea alionya kuwa ufisadi haukuwa tu katika mahali pa juu, bali kila mtu katika nafasi yake alitekeleza ulaghai uliokuwa ukijidhihirisha kwa namna tofauti-tofauti.
Ni k**a inavyoonekana leo, ambapo watoto na vijana kidogo kidogo hujifunza kutokana na uhusiano ndani ya familia, kutokuaminina, kutokuwepo uadilifu na kuwajibika.
Na hapo endapo ndani kuna shida, basi watoto hujifunza mambo mabaya.
Hii hukumbusha habari ya miaka kadhaa iliyopita wakati wa mazishi ya Askofu Anthony Mayala wa Jimbo Katoliki Mwanza. Katika ibada ya mazishi yake walikusanyika watu wa kila hadhi.
Walikuwepo viongozi wa serikali pamoja na dini na katika salamu kadhaa, wengi waliopata nafasi walimzungumzia Askofu Mayalla kwamba alikuwa akikemea ufisadi kwa nguvu zake zote.
Ibada iliadhimishwa na Kardinali Pengo ambaye pamoja na mengine yote, aligusia vita dhidi ya ufisadi katika mahubiri yake.
Aliwauliza waliokuwa wamehudhuria swali; “tunapokemea sana ufisadi ni kwanini tunafanya hivyo?” Je! Ni kwa sababu tunauchukia kabisa ufisadi kwa moyo wetu wote. Je, tukipewa sasa hivi nafasi waliyonayo hao wanaofanya ufisadi ufisadi, utakoma?
Maswali hayo ya Pengo yanagusa kabisa jamii, ambayo ukiangalia wengi wanaopinga ufisadi kwa maneno makali, endapo watapata nasi, wanaweza kuwa vinara wa ufisadi.
Mifano ipo mingi yenye kuonesha jamii, inaweza kuwa sehemu kubwa ya kuubeba ufisadi, hata k**a inaonekana ikiupinga hadharani.
Kipo kisa kinachobeba taswira hii ambacho kinasimuliwa na Biblia. Katika kile kisa cha mwanamke mzinifu aliyefikishwa mbele ya Yesu katika Injili (rej. Yohane 8:1 – 11).
Wanajamii wale walimk**ata mwanamke kwa kumtuhumu dhambi, na kumpeleka kwa Yesu ili akahukumiwe, na walikuwa tayari na mawe kwa ajili ya kumpiga hadi kufa endapo Yesu atatamka hukumu.
Basi, wakamkabidhi kwa Yesu, walitengeneza duara huku tayari kwa kumpiga mawe, Yesu, akawasikiliza, baadaye akainama kuandika kitu ardhini.
Alipomaliza kuandika, akawauliza – “ nani asiyekuwa na dhambi kati yenu ili awe wa kwanza kurusha jiwe kumpiga mwanamke.”
Badala ya kujibiwa, wanaume wote waliomleta mwanamke yule “waliyeyuka” na kutokomea na ndipo Yesu akatamka kwa mwanamke; “nenda zako, usitende dhambi tena.”

Waandishi wawili wafariki ajaliniNa Mwandishi WETUTASNIA  ya habari Tanzania, imepata pigo kubwa kwa waandishi wawili wa...
26/03/2024

Waandishi wawili wafariki ajalini
Na Mwandishi WETU
TASNIA ya habari Tanzania, imepata pigo kubwa kwa waandishi wawili wanaofanya kazi Mkoa wa Lindi kufariki dunia kwa ajali ya gari.
Pambazuko ambalo lilifika Kijiji cha Nyamwage, Pwani ilikotoea ajali hiyo, saa 8:35, lilielezwa na watu waliowahi eneo hilo kuwa ajali hiyo ilitokea majira ya saa 7 usiku wa kuamikia leo – Machi 26.
Waandishi waliopoteza maisha ni Josephine Kibiriti wa kampuni ya Sahara Media group (StarTV), na Abdalah Nanda wa Channel Ten.
Inaelezwa kuwa waandishi hao wa habari walikuwa wakitokea Dar es Saalam walikoalikwa kikazi na walikuwa wakirejea eneo lao la akazi, Lindi.
Taarifa kutoka Jeshi la Polisi – mkoa wa kikazi wa Rufiji, zinaeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni gari walilokuwa wakisafiria kugongana na lori.
Miili ya waandishi hao imehifadhiwa Kituo cha Afyà Ikwiriri.
Gazeti la Pambazuko linatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa waandishi hao na kuwatakia pumziko la amani.

Sasa kila goli Simba, Yanga 10m/-Na Mwandishi WETUTIMU mbili za Tanzania, Simba na Yanga ambazo zinashiriki robo fainali...
26/03/2024

Sasa kila goli Simba, Yanga 10m/-
Na Mwandishi WETU
TIMU mbili za Tanzania, Simba na Yanga ambazo zinashiriki robo fainaliza Klabu Bingwa Afrika, sasa zishindwe zenyewe tu; kwani zina kila sababu ya kushinda mechi zao na kusonga mbele hatua ya nusu fainali.
Ukiacha hamasa inayoongozwa na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ambaye ameahidi kulipa shilingi milioni 10 kwa kila goli litakalofungwa, pia mashabiki, wapenzi wa soka wanaonekana kujawa hamasa kushabikia timu hizo.
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Damas Ndumbaro amesema Simba na Yanga zina kila sababu ya kushinda ili kuendelea na hatua ya nusu fainali na hatimaye kuchukua kombe hilo maarufu zaidi Afrika na lenye heshima kwenye medani za kimataifa.
“Mnaona kabisa Mama yetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongeza dau hilo ili timu zetu mbili ziweze kufanya vizuri na zipate mafanikio zaidi, tumeziambia timu zote mbili zishirikiane na serikali katika kipindi hiki ili kupata mafanikio,” ameongeza waziri huyo.
Pambazuko limearifiwa kuwa serikali pia itagharimia tiketi za ndege kwa timu hizo kusafiri kwenda kucheza nje ya Dar es Salaam.
Simba inatarajiwa kucheza dhidi ya Al Ahly ya Misri katika mchezo utakaofanyika Machi 29,2024, huku Yanga akijiandaa kuvaana na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini katika mchezo utafanyika siku inayofuata - Machi 30, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dare es Salaam.
Gazeti la Pambazuko linazitakia kila heri timu hizo kubwa Tanzania ushindi ili ziweze kusonga mbele na kuiletea sifa Tanzania na wana Afrika Mashariki.

Address

Sandary Hospital Building
Dar Es Salaam
12145

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Pambazuko posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share