Simulizi na Sauti

  • Home
  • Simulizi na Sauti

Simulizi na Sauti Welcome to Simulizi na Sauti, an online content company founded on May 31, 2017, by Fredrick Bundala. Follow our page for accurate and engaging stories

We deliver high-quality news, entertainment, and lifestyle content.

Billnass na Nandy sio tu wanandoa na wasanii wakubwa, bali pia ni wazazi wa mtoto wao wa k**e, Naya. Kwa sasa, jina la b...
25/07/2025

Billnass na Nandy sio tu wanandoa na wasanii wakubwa, bali pia ni wazazi wa mtoto wao wa k**e, Naya. Kwa sasa, jina la binti yao limegeuka kuwa sehemu ya ubunifu wa sanaa yao. Kwenye wimbo mpya wa Billnass How Come, anasikika akisema “Baba Naya, usiniguse” – kauli inayotafsiriwa k**a ujumbe wa kujiamini, kuwatahadhalisha watu kujiweka mbali na yeye, na kusonga mbele bila kuyumbishwa.

Nandy naye amejumuisha kauli ya “Mama Naya, usiniguse” kwenye wimbo wake mpya Tonge Nyama, akionyesha kuwa jina la Naya limekuwa nembo mpya katika muziki wake.

Ubunifu huu umeleta utambulisho wa kifamilia kwenye kazi zao, ukionyesha namna wanavyotumia maisha yao binafsi kuwaburudisha mashabiki kwa njia ya muziki.

Tuseme matamasha mawili makubwa ya muziki yameandaliwa siku moja, muda mmoja lakini maeneo tofauti.👉 Mbosso anapiga shoo...
25/07/2025

Tuseme matamasha mawili makubwa ya muziki yameandaliwa siku moja, muda mmoja lakini maeneo tofauti.
👉 Mbosso anapiga shoo akiwa na hit yake kali 'Pawa'
👉 Wakati huohuo, Marioo anatumbuiza kwa mara ya kwanza wimbo wake mpya 'Mvua'

Wewe k**a shabiki wa Bongo Fleva, ungetoka nyumbani kwenda kumuangalia nani?

Tangu Vita ya Pili ya Dunia, Japan imekuwa ikihesabiwa k**a moja ya nchi salama zaidi kwa wawekezaji duniani, hasa kutok...
25/07/2025

Tangu Vita ya Pili ya Dunia, Japan imekuwa ikihesabiwa k**a moja ya nchi salama zaidi kwa wawekezaji duniani, hasa kutokana na utulivu wake wa kisiasa chini ya utawala wa chama cha LDP. Hata hivyo, hali imebadilika baada ya uchaguzi wa Julai 2025 ambapo muungano wa LDP na Komeito umepoteza wingi wa kura kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1955.

Kupanda kwa umaarufu wa vyama vya upinzani, hasa vile vya siasa kali k**a Sanseito, kumewatia hofu wawekezaji wa kimataifa. Vyama hivi vinasukuma ajenda za kupunguza kodi, kuongeza matumizi ya kijamii, na kupunguza uwekezaji wa kigeni—suala linalotia wasiwasi kuhusu uthabiti wa bajeti ya taifa hilo lenye deni kubwa.

Matokeo ya kisiasa yameanza kuathiri masoko: Yen imeanza kuwa na mabadiliko ya thamani yasiyotabirika, huku riba ya hati fungani za serikali (JGBs) hasa za muda mrefu ikipanda. Wawekezaji wa kimataifa na makampuni ya uwekezaji yameanza kuwa makini zaidi na soko la Japan, wakihofia mkwamo wa sera na mabadiliko yasiyotabirika.

Kwa sasa, wataalamu wanashauri wawekezaji kuwa na mikakati ya tahadhari zaidi, wakichambua kwa makini sekta salama k**a vile huduma za jamii, na kupunguza utegemezi wa yen k**a kinga ya kiuchumi. Hadhi ya Japan k**a ngome salama inatajwa kuingia mashakani, na soko linahitaji uangalizi wa karibu zaidi kuliko ilivyowahi kuwa hapo mwanzo

Afisa Mkuu Mtendaji wa kampuni ya teknolojia Astronomer, Andy Byron, na Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu, Kristin Cabot,...
25/07/2025

Afisa Mkuu Mtendaji wa kampuni ya teknolojia Astronomer, Andy Byron, na Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu, Kristin Cabot, wamejiuzulu baada ya kuonekana kwenye video wakikumbatiana kwenye tamasha la Coldplay lililofanyika Massachusetts, Marekani, tarehe 16 Julai 2025.

Tukio hilo liliwavutia watazamaji wengi baada ya kuonyeshwa kwenye "Kiss Cam," huku msanii Chris Martin akitania jukwaani kwamba "Wameamua kuonyesha upendo hadharani." Video hiyo ilisambaa sana mtandaoni na kusababisha uchunguzi wa ndani wa kampuni.

Baada ya shinikizo la umma na uchunguzi huo, Byron alitangaza kujiuzulu Julai 19, na Cabot alifuatia kujiuzulu ifikapo Julai 24. Nafasi ya uongozi kwa sasa inashikiliwa na Pete DeJoy k**a kaimu Mkurugenzi Mtendaji.

Kupitia ukurasa wake wa LinkedIn, Astronomer ilikanusha taarifa kuwa Byron alitoa tamko lolote kuhusiana na tukio hilo, ikisisitiza kwamba ripoti zilizodai hivyo ni za uongo. Kampuni pia ilieleza kuwa mtu wa tatu aliyekuwa katika video hiyo alitambuliwa kimakosa.

Astronomer imesisitiza kuwa viongozi wake wanatakiwa kuwa mfano wa maadili ya kazi na uwajibikaji. Tukio hili limeibua mjadala mkubwa kuhusu mipaka ya mahusiano kazini na athari za mitandao ya kijamii katika maisha ya kitaaluma ya watu binafsi.

Baada ya mapumziko mafupi kufuatia sherehe ya kifahari ya harusi yao ya  , Jux na mkewe Priscilla wamechukua tena jukwaa...
24/07/2025

Baada ya mapumziko mafupi kufuatia sherehe ya kifahari ya harusi yao ya , Jux na mkewe Priscilla wamechukua tena jukwaa la Instagram kwa kishindo, safari hii wakitangaza habari njema, ujio wa mtoto wao wa kwanza.

Kupitia picha za kuvutia za ujauzito (baby bump), Priscilla anaonekana akipendeza na kung’aa akiwa na tumbo lake kubwa wazi huku Jux akionekana naye akishiriki kwa upendo katika picha hizo.

Kwa picha hizi, ni sahihi kusema tujiandae na Baby Shower ya taifa.

'Nikisema 2025 huu ndio wimbo wa Afrika  Mashariki uliopewa sikio duniani… ntakua nimekosea?! 😜🌍🔥’ – Rayvanny atamba kuh...
24/07/2025

'Nikisema 2025 huu ndio wimbo wa Afrika Mashariki uliopewa sikio duniani… ntakua nimekosea?! 😜🌍🔥’ – Rayvanny atamba kuhusu akimshirikisha Diamond Platnumz. -

Shirikisho la Muziki Tanzania (SHIMUTA) limetoa pongezi za dhati kwa COSOTA kwa hatua ya kihistoria ya kuipa Society of ...
24/07/2025

Shirikisho la Muziki Tanzania (SHIMUTA) limetoa pongezi za dhati kwa COSOTA kwa hatua ya kihistoria ya kuipa Society of Music Advocacy (SOMA) leseni rasmi ya kukusanya mirabaha ya wasanii.

Kupitia Rais wake Addo November Mwasongwe, SHIMUTA imesema kuwa hatua hiyo ni ushindi mkubwa kwa tasnia ya muziki nchini, hasa kwa kuwa imeweka msingi wa kulinda haki za wasanii kwa njia ya kisheria na kitaalamu.

SOMA, inayojumuisha wadau muhimu k**a na mtayarishaji , imepewa jukumu hilo kubwa kwa matarajio ya kuleta uadilifu, uwazi, na maendeleo katika maisha ya wanamuziki wa Tanzania.

SHIMUTA imesisitiza imani yao kwa .tanzania na kuitakia mafanikio katika utekelezaji wa majukumu yake mapya.

Kwa niaba ya wasanii na wadau wa muziki, SHIMUTA imesema: “Hongereni sana na SOMA, huu ni mwanzo mpya kwa muziki wa Tanzania.”
Powered By: &

Lebo ya Bad Nation kwa kushirikiana na ukurasa wa MariooNews, wamemuita Marioo kuwa “Human Artificial Intelligence (HAI)...
24/07/2025

Lebo ya Bad Nation kwa kushirikiana na ukurasa wa MariooNews, wamemuita Marioo kuwa “Human Artificial Intelligence (HAI)”, wakimaanisha kuwa uwezo wake wa kutoa hit baada ya hit unakaribia ule wa mashine yenye akili bandia. Kauli hii inaibua mjadala k**a hii ni sifa inayostahili au ni majigambo ya kimkakati?

Kwa upande mmoja, kauli hii ina uzito wa kweli. Marioo ameendelea kutuonyesha maajabu katika kutoa nyimbo zinazoshika chati. Kuanzia Hakuna Matata, Nairobi, Mi Amor, hadi Mvua na Ha Ha Ha — ambazo kwa sasa zinatawala namba 1 na 2 kwenye YouTube Tanzania — ameonyesha kuwa ana mfumo wa ubunifu wa hali ya juu usioyumba. K**a kweli tungelilinganisha na mashine ya kisasa, basi ni ile inayoweza kutambua ladha ya soko, hisia za mashabiki, na mwelekeo wa muziki wa Bongo fleva kwa wakati mmoja.

Hata hivyo, si vyema kupuuza ukweli kwamba mafanikio ya yamechangiwa pia na juhudi binafsi, timu yake, watayarishaji k**a , , pamoja na uongozi wa Bad Nation. Hii inaonesha kuwa "HAI" ni zaidi ya sifa, ni mkakati wa kuimarisha brand yake kimataifa, hasa kipindi hiki ambapo nyimbo zake zinatembea kila kona ya Tanzania na nje ya mipaka.

Kumuita “HAI” ni njia ya kuelezea ubora wake kisanii kwa lugha ya kiteknolojia. Inavutia, inaburudisha, na inaongeza uzito kwenye simulizi ya mafanikio yake.

Ndege ya abiria aina ya Antonov An‑24 iliyokuwa ikisafirisha watu 49, wakiwemo watoto watano, imeanguka karibu na mji wa...
24/07/2025

Ndege ya abiria aina ya Antonov An‑24 iliyokuwa ikisafirisha watu 49, wakiwemo watoto watano, imeanguka karibu na mji wa Tynda, Mashariki ya Mbali mwa Urusi, Alhamisi tarehe 24 Julai 2025. Ndege hiyo ya Angara Airlines ilikuwa ikitokea Blagoveshchensk kuelekea Tynda na ilipata ajali wakati wa jaribio la pili la kutua katikati ya hali ya hewa mbaya.

Wataalamu wa uokoaji waligundua mabaki ya ndege hiyo yakiwa yanawaka moto katika msitu mnene, takribani kilomita 15 kusini mwa Tynda, bila dalili za manusura. Ripoti zinaeleza kuwa ndege hiyo ilitengenezwa mwaka 1976 na imekuwa ikitumika licha ya changamoto za upatikanaji wa vipuri kutokana na vikwazo vya kimataifa.

Uchunguzi wa awali unaonesha huenda ajali ilisababishwa na hitilafu ya kibinadamu au matatizo ya kiufundi. Serikali ya Urusi imeanzisha uchunguzi wa kina kuhusu tukio hili, huku Rais Vladimir Putin akiwa tayari amepewa taarifa.

Ajali hii imezua maswali kuhusu usalama wa ndege kongwe zinazotumika maeneo ya mbali ya Urusi yenye hali ngumu za kijiografia na hewa.

Baada ya mafanikio makubwa ya EP yake mpya Room Number 3, msanii wa Bongo Fleva, , ametwngaza rasmi ziara ya ndani ya nc...
24/07/2025

Baada ya mafanikio makubwa ya EP yake mpya Room Number 3, msanii wa Bongo Fleva, , ametwngaza rasmi ziara ya ndani ya nchi kwa lengo la kuusogeza muziki wake kwa mashaabiki walio nje ya Dar Es Salaam.

Ziara hii itampitisha kwenye mikoa mbalimbali ya Tanzania, ikimpa fursa ya kuungana na mashabiki wake ana kwa ana, huku akitumbuiza nyimbo zinazotikisa chati k**a "Pawa", na "Aviola".

Kwa sasa, EP yake imeshika nafasi ya kwanza kwenye Apple Music na Boomplay Tanzania, huku nyimbo nne zikiingia kwenye Top 5 ya nyimbo 100 bora nchini. Hali hii inayochochea hamu kubwa kwa mashabiki wanaosubiri kwa hamu kumuona Mbosso jukwaani.

Kwa ziara hii, Mbosso anathibitisha kuwa Bongo Fleva bado ina nguvu kubwa ndani ya ardhi yake.

Sekta ya kilimo mkoani Geita ina mchango mkubwa katika pato la mkoa, ikichangia takribani asilimia 70 ya mapato yote ya ...
24/07/2025

Sekta ya kilimo mkoani Geita ina mchango mkubwa katika pato la mkoa, ikichangia takribani asilimia 70 ya mapato yote ya ndani, huku shughuli nyingine za kiuchumi zikichangia asilimia 30. Miongoni mwa mazao ya biashara yenye uzito mkubwa ni zao la pamba, ambalo limeendelea kuwa chanzo kikuu cha kipato kwa wakulima wengi wa mkoa huo.

Takwimu zinaonyesha ongezeko kubwa la uzalishaji wa zao hilo, kutoka tani 9,309 mwaka 2021 hadi kufikia tani 19,632 mwaka 2025. Aidha, upatikanaji wa mbolea ya ruzuku umechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza matumizi ya pembejeo miongoni mwa wakulima, jambo lililosaidia kuboresha uzalishaji kwa hekta.

Katika kipindi hicho, matumizi ya mbolea kwa hekta yameongezeka kutoka kilo 19 hadi kilo 24, hali inayoashiria uhitaji wa mifumo bora ya pembejeo, masoko ya uhakika, na miundombinu ya kuchakata mazao ili kuongeza thamani kabla ya kuuza.

Kwa muktadha huo, mkoa wa Geita unabeba fursa lukuki kwa wawekezaji katika sekta ya kilimo, hususan kwa wanaotaka kuwekeza katika kilimo cha pamba, usindikaji, na teknolojia ya kuongeza tija kwa wakulima. Ukuaji huu unatoa mazingira rafiki kwa ubia kati ya wakulima na sekta binafsi kwa lengo la kuinua uchumi wa eneo na taifa kwa ujumla.

Unataka nyumba ya ndoto yako?, Wafuate

Harmonize ameonyesha studio yake ya kurekodia kupitia ukurasa wake wa Instagram na kudai kuwa ni studio bora zaidi nchin...
24/07/2025

Harmonize ameonyesha studio yake ya kurekodia kupitia ukurasa wake wa Instagram na kudai kuwa ni studio bora zaidi nchini. Katika picha aliyoichapisha, mtayarishaji maarufu Cukie Dady anaonekana akifanya kazi mbele ya vifaa vya kisasa, huku Harmonize akiandika:

"Best kitchen 🍳👨‍🍳 in the game. This is my house and who you see is . Album mood 🎶💿"

Kauli hiyo inaashiria kuwa Harmonize anajivunia kuwa na studio ya kiwango cha juu, anayoitumia kutengeneza albamu yake mpya. Kwa kutumia neno "kitchen" k**a lugha ya mtaani kwa studio, Harmonize amesisitiza ubunifu na ubora wa mazingira yake ya kazi, akijitangaza k**a mmoja wa wasanii waliowekeza zaidi kwenye muziki wao.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Simulizi na Sauti posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share