Simulizi na Sauti

Simulizi na Sauti Welcome to Simulizi na Sauti, an online content company founded on May 31, 2017, by Fredrick Bundala. Follow our page for accurate and engaging stories

We deliver high-quality news, entertainment, and lifestyle content.

Rayvanny amedhihirisha kwa nguvu kwamba ni moja ya mastaa wakubwa wa Bongo Fleva barani Afrika. Data mpya za streaming z...
22/08/2025

Rayvanny amedhihirisha kwa nguvu kwamba ni moja ya mastaa wakubwa wa Bongo Fleva barani Afrika. Data mpya za streaming zinaonyesha kwamba msanii huyu yupo kwenye nafasi ya tano barani Afrika kwa wasikilizaji milioni 50.9, jambo ambalo ni la kushangaza na la kujivunia kwa Tanzania.

Wasanii Watano Wa Afrika Wenye Wasikilizaji Wengi YouTube Music.

Moliya: 424M

Rema: 328M

Ckay: 98.2M

Tyla: 62.2M

Rayvanny: 50.9M

Hii inamaanisha Rayvanny amepita mastaa wakubwa wa Nigeria k**a Davido (44.1M), Ayra Starr (29.6M), Burna Boy (21.5M), na Wizkid (19.2M), akithibitisha kwamba Bongo Fleva inayo nguvu barani Afrika.

Wasanii 10 Wa Bongo Fleva Wenye Wasikilizaji Wengi YouTube Music

1.Rayvanny: 50.9M

2.Diamond Platnumz: 9.04M

3.Marioo: 7.08M

4.Mbosso: 6.89M

5.Jux: 6.69M

6.Harmonize: 6.19M

7.Zuchu: 4.7M

8.Jay Melody: 3.29M

9.Alikiba: 2.99M

10.Darassa: 2.67M

Rayvanny anaongoza kwa tofauti kubwa, akionyesha kuwa yeye ndiye mlinda mlango wa Bongo Fleva kimataifa kwa sasa. Zuchu anasimama kwenye orodha hii akiwa MSANII pekee wa k**e.

Kwanini hii ina maana?

1. Rayvanny anaoeperusha bendera ya Tanzania kwenye soko la kimataifa.

2. Monthly audience kubwa inahusiana moja kwa moja na urahisi wa yeye kuuza zaidi muziki wake, ushirikiano zaidi, na kutambuliwa kimataifa.

3. Gap kubwa kati ya Rayvanny na wasanii wengine inaibua mjadala mpya: Je, “Crown ya Digital King” Tanzania sasa iko mikononi mwa Rayvanny?

Yammi ameachia rasmi EP yake mpya iitwayo "After All," huku akipata sapoti kubwa kutoka kwa supastaa Nandy.Nandy alitumi...
22/08/2025

Yammi ameachia rasmi EP yake mpya iitwayo "After All," huku akipata sapoti kubwa kutoka kwa supastaa Nandy.
Nandy alitumia ukurasa wake wa Instagram kushea taarifa za EP hiyo iliyoachiwa leo Agosti 22, na kumpongeza Yammi kwa mafanikio hayo. Kitendo hiki kimepokelewa kwa hisia chanya na mashabiki wengi.

Sapoti hii ya Nandy inachukuliwa k**a ishara ya amani, kwani hapo mwanzo Yammi alikuwa chini ya usimamizi wake, na mwisho wa mahusiano yao ya kikazi ulikuchukuliwa kwa mitazamo tofauti. Uungaji mkono huu unaonyesha kwamba uhusiano wao umeimarika na wameweka tofauti zao pembeni.

Powered By:

D Voice amewasiliha ombi kwa Baraza la Sanaa la Taifa (.tanzania) pamoja na viongozi wake, ikiwemo Dkt. Kedmon Mapana, M...
22/08/2025

D Voice amewasiliha ombi kwa Baraza la Sanaa la Taifa (.tanzania) pamoja na viongozi wake, ikiwemo Dkt. Kedmon Mapana, Mtendaji Mkuu, na Gerson Msigwa, Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo, kuongeza vipengele muhimu kwenye tuzo za muziki, kufuatia ukuaji wa haraka wa muziki singeli nchini.

Kwenye chapisho lake la Instagram, ameomba tuzo tano mpya:

1. Best Singeli Writer – Tuzo ya mwandishi bora wa Singeli.

2. Best New Singeli Artist Award – Tuzo kwa msanii chipukizi wa Singeli.

3. Best Singeli Collaboration Song – Tuzo ya wimbo bora wa ushirikiano wa Singeli.

4. Best Singeli Video of the Year – Tuzo ya video bora ya Singeli kwa mwaka.

5. The Singeli Founder's Lifetime Achievement Award – Tuzo ya heshima ya maisha yote, ambayo D Voice anashauri iende kwa Legend Msagasumu, k**a heshima kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya Singeli.

Omba hili linaonyesha wazi hitaji la kutambulisha na kuthamini muziki wa Singeli. D Voice anasisitiza kuwa jamii ya Singeli, wasanii na mashabiki wake wanastahili heshima rasmi na kutambulika kupitia tuzo maalumu.
Powered By:

Akaunti za Instagram za mastaa maarufu k**a Future, Adele, Tyla, na Michael Jackson zilidukuliwa na wahalifu mtandaoni. ...
22/08/2025

Akaunti za Instagram za mastaa maarufu k**a Future, Adele, Tyla, na Michael Jackson zilidukuliwa na wahalifu mtandaoni. Akaunti hizi zilitumika kuchapisha picha za Future akiwa ameshikilia sarafu ya dhahabu iliyoandikwa “FREEBANDZ”, ikiwa na maandishi ya ajabu na linki zisizo za kawaida, jambo lililosababisha mashaka na taharuki kwa mashabiki. Machapisho hayo yalifutwa ndani ya dakika 20, lakini tayari yalikuwa yamesambaa.

Ni muhimu kuelewa kwamba Freebandz ni jina la lebo ya muziki iliyoanzishwa na Future mwaka 2011, inayohusiana na kazi zake za muziki kupitia Epic Records na Sony Music. Hata hivyo, sarafu ya crypto iitwayo “FREEBANDZ” haijathibitishwa kuwa na uhusiano wowote na Future na inahusiana na uwezekano wa utapeli mtandaoni (scam) unaotumia majina ya mastaa kuvutia wawekezaji.

Mashabiki wanashauriwa kuepuka kubonyeza linki zozote au kuwekeza jwenye sarafu hii na kuthibitisha taarifa kupitia vyanzo rasmi ili kuepuka kupoteza fedha. Tukio hili linaonyesha jinsi wahalifu wanavyotumia mastaa maarufu kutangaza bidhaa za uwongo mtandaoni.

Serikali ya India imepitisha sheria mpya inayopiga marufuku kubet mtandaoni na michezo yote ya kubashiri inayohusisha fe...
22/08/2025

Serikali ya India imepitisha sheria mpya inayopiga marufuku kubet mtandaoni na michezo yote ya kubashiri inayohusisha fedha halisi. Hatua hii inalenga kuzuia uraibu wa k**ari, udanganyifu, na hasara kubwa za kifedha ambazo zimekuwa zikiongezeka kila mwaka.

Sheria hiyo, Promotion and Regulation of Online Gaming Act, 2025, pia inakataza matangazo ya betting na njia za malipo kwa huduma hizo. Wanaokiuka marufuku watakabiliwa na adhabu kali, ikiwemo faini kubwa na kifungo jela.

Makampuni makubwa k**a Dream11 na MPL ambayo yalitegemea sekta ya betting sasa yako hatarini kufungwa, hali ambayo inaweza kusababisha kupotea kwa ajira nyingi. Hata hivyo, michezo ya e-sports na ile ya ujuzi itaruhusiwa kuendelea chini ya usimamizi na leseni maalum kutoka Tume ya Michezo ya Mtandaoni (NOGC).

Serikali ya India imesisitiza kuwa marufuku ya kubet ni muhimu kulinda vijana dhidi ya uraibu unaoweza kuleta madhara makubwa kuliko hata dawa za kulevya.
Powered By:

Israel imetishia kwamba Gaza City inaweza kufutwa kwenye ramani endapo Hamas haitasalimisha silaha zake zote na kuwaachi...
22/08/2025

Israel imetishia kwamba Gaza City inaweza kufutwa kwenye ramani endapo Hamas haitasalimisha silaha zake zote na kuwaachia huru mateka walioko mikononi mwao. Hatua hii imekuja wakati ambapo Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu ameridhia mipango ya kijeshi ya kuishambulia Gaza City, eneo linalotajwa kuwa ngome kuu ya Hamas.

Wakati huo huo, Hamas imekubali pendekezo lililopendekezwa na Misri na Qatar la kusitisha mapigano kwa siku 60 na kufanya ubadilishanaji wa mateka na wafungwa kwa awamu. Hata hivyo, Israel imekataa mpango huo wa sehemu, ikisisitiza kwamba Hamas lazima ijisalimishe kabisa na kuachia mateka wote bila masharti.

Mvutano huu unaibua hofu kubwa ya athari za kibinadamu, huku jumuiya ya kimataifa ikizidisha shinikizo la kuhitajika kwa makubaliano ya kusitisha vita ili kuokoa maisha ya raia.
Powered By:

Yammi ametangaza rasmi orodha ya nyimbo zitakazopatikana kwenye EP yake mpya yenye jina After All. Hii ni EP yake ya pil...
21/08/2025

Yammi ametangaza rasmi orodha ya nyimbo zitakazopatikana kwenye EP yake mpya yenye jina After All. Hii ni EP yake ya pili baada ya Three Hearts, na imebeba jumla ya nyimbo sita (6) zinazotarajiwa kumuweka kwenye ramani kubwa zaidi ya muziki wa Bongo Fleva. ndiye msanii peke aliyeshirikishwa kwenye

Watayarishaji (Producers) walioandaa muziki wa After All ni; Trone, na

EP ya After All inatarajiwa kutoa mwelekeo mpya wa sauti na simulizi za maisha, huku ikithibitisha nafasi ya k**a mmoja wa wasanii wa k**e wanaojitahidi kupambania nafasi zao kwenye muziki wenye ushindani mkubwa. Powered By:

Rayvanny  anaendelea kuweka rekodi mpya, safari hii kupitia wimbo wake mpya wa kimataifa, "Oh Mama! TETEMA," ambao amewa...
21/08/2025

Rayvanny anaendelea kuweka rekodi mpya, safari hii kupitia wimbo wake mpya wa kimataifa, "Oh Mama! TETEMA," ambao amewashirikisha wasanii wakubwa k**a Nora Fatehi, Vishal Mishra na Shreya Ghoshal.

Mafanikio makubwa ya wimbo huu yamejidhihirisha kwenye mitandao ya kijamii, ambapo sauti ya wimbo huo imetumiwa kwenye Reels zaidi ya 500,000 kwenye mtandao wa Instagram. Kupitia akaunti yake ya Instagram, Rayvanny alionyesha furaha yake na kustaajabu, akisema "REELS 500K HAIJAWAHI TOKEA," akimaanisha kwamba hii ni mara ya kwanza kwake kufikia idadi kubwa kiasi hicho ya video zilizotumia wimbo wake.

Mafanikio haya yanathibitisha umaarufu na ushawishi wa Rayvanny kwenye soko la muziki la kimataifa, huku wimbo huu ukiendelea kuwa maarufu na kuonyesha utawala wake kwenye majukwaa ya kidijitali k**a YouTube Music na Spotify, ambako Rayvanny anaongoza kwa mamilioni ya wasikilizaji wa mwezi. Powered By:

Address

Salasala
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Simulizi na Sauti posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share