22/08/2025
D Voice amewasiliha ombi kwa Baraza la Sanaa la Taifa (.tanzania) pamoja na viongozi wake, ikiwemo Dkt. Kedmon Mapana, Mtendaji Mkuu, na Gerson Msigwa, Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo, kuongeza vipengele muhimu kwenye tuzo za muziki, kufuatia ukuaji wa haraka wa muziki singeli nchini.
Kwenye chapisho lake la Instagram, ameomba tuzo tano mpya:
1. Best Singeli Writer – Tuzo ya mwandishi bora wa Singeli.
2. Best New Singeli Artist Award – Tuzo kwa msanii chipukizi wa Singeli.
3. Best Singeli Collaboration Song – Tuzo ya wimbo bora wa ushirikiano wa Singeli.
4. Best Singeli Video of the Year – Tuzo ya video bora ya Singeli kwa mwaka.
5. The Singeli Founder's Lifetime Achievement Award – Tuzo ya heshima ya maisha yote, ambayo D Voice anashauri iende kwa Legend Msagasumu, k**a heshima kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya Singeli.
Omba hili linaonyesha wazi hitaji la kutambulisha na kuthamini muziki wa Singeli. D Voice anasisitiza kuwa jamii ya Singeli, wasanii na mashabiki wake wanastahili heshima rasmi na kutambulika kupitia tuzo maalumu.
Powered By: