Sports Online

Sports Online Karibu kwenye ulimwengu wa burudani ya michezo! Tunakuletea habari, matokeo, na matukio moto kutoka ndani na nje ya uwanja. Usipitwe na chochote!
(1)

Ni kweli kiwango cha Elie Mpanzu kimeshuka?
07/10/2025

Ni kweli kiwango cha Elie Mpanzu kimeshuka?

Eng. Hersi Said aingia historia, ateuliwa kuwa Mjumbe wa K**ati ya Mashindano ya Vilabu vya Wanaume FIFARais wa Klabu ya...
07/10/2025

Eng. Hersi Said aingia historia, ateuliwa kuwa Mjumbe wa K**ati ya Mashindano ya Vilabu vya Wanaume FIFA

Rais wa Klabu ya Yanga SC, Injinia Hersi Said, ameteuliwa rasmi na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kuwa Mjumbe wa K**ati ya Mashindano yote ya Vilabu vya Wanaume Duniani kwa kipindi cha miaka minne (2025–2029).

Uteuzi huo, uliotangazwa na Baraza la FIFA tarehe 2 Oktoba 2025, unamfanya Eng. Hersi kuwa mtu wa kwanza kutoka Afrika Mashariki na Kati kuingia katika k**ati hiyo kubwa ya soka duniani.

Ni heshima kubwa kwa Tanzania na ukanda wa Afrika Mashariki, ikizingatiwa kwamba Eng. Hersi amekuwa kinara katika kusimamia maendeleo ya mpira wa miguu kupitia Yanga SC na michango yake mikubwa katika uongozi wa michezo barani Afrika.

✍️ Nasikia hata watani wao Yanga waliingilia dili la kumtaka kocha huyu raia wa Bulgaria. Maswali ni mengi. Kwanza kabis...
06/10/2025

✍️ Nasikia hata watani wao Yanga waliingilia dili la kumtaka kocha huyu raia wa Bulgaria. Maswali ni mengi. Kwanza kabisa hatuna mipango ya muda mrefu. Ina maana bila ya Simba kucheza na Gaborone United basi leo Pentev asingekuwa kocha wa Wekundu wa Msimbazi.
Ina maana kwamba bila ya Simba kucheza na Gaborone United, basi Yanga nao wasingemuona Pentev. Kwanini hatukumuona huyu kocha kabla ya mechi ya Gaborone United? Hapa ndio tunapogundua kwamba mpira wetu ni bora liende tu. Hatuna mipango ya muda mrefu.
Hatuandiki chini kinachopaswa kufanywa kwa msimu mzima. Kitu chochote kinaweza kutokea muda wowote. Hatuna mpango A wala B. Kila kitu kinaweza kutokea ghafla ghafla tu. Simulizi ya namna ambavyo kuna wachezaji wengi wamesajiliwa na timu hizi kwa sababu waliwahi kuzifunga. Basi. Sio kwamba walimchunguza mchezaji hapo awali, hapana! Ni kwa sababu amewafunga tu, lakini hakukuwa na uchunguzi yakinifu kuhusu mchezaji mwenyewe kabla ya pambano dhidi yake.
Ni hadithi ya Ditram Nchimbi pia. Aliwafunga Yanga mabao matatu na hapo hapo Yanga wakaanza kukimbizana na saini yake bila ya kujali kwamba mchezaji mwenyewe alikuwa hajawahi kufunga mabao zaidi ya kumi katika msimu mmoja. Alipotua Yanga mabosi ndio wakaanza kugundua upungufu mwingi kwake. K**a wangekuwa wamemchunguza awali si ajabu wasingemchukua kwa sababu tu alikuwa amewafunga mabao matatu katika mechi moja.
Kila la kheri kwa kocha mpya Msimbazi. Kitu kizuri kwa Simba ni kwamba wamemchukua mapema kabla ya msimu haujachanganya na atakuwa na muda mrefu wa kuwajua wachezaji wake kabla mambo hayajafika mbali.

Edo Kumwembe

06/10/2025

Faida wanayoipata Simba kwa kuchagua uwanja wa Meja Isamuhyo

06/10/2025

Simba Sc wamepatia sana, Yanga Sc kazi wanayo msimu huu pale KMC Complex

Weka maoni yako hapa ✍️
06/10/2025

Weka maoni yako hapa ✍️

🚨UPDATESHawa wapo kwenye rada za Yanga kuchukua nafasi ya Roman Folz (1) Nasreddine NabiKocha raia wa Tunisia, aliyewahi...
05/10/2025

🚨UPDATES

Hawa wapo kwenye rada za Yanga kuchukua nafasi ya Roman Folz

(1) Nasreddine Nabi
Kocha raia wa Tunisia, aliyewahi kuinoa Yanga SC na kuipa mafanikio makubwa ikiwemo mataji ya ligi na kufika fainali ya CAF Confederation Cup 2023. Anajulikana kwa nidhamu, mpira wa kisasa na kupanga timu kwa ufanisi mkubwa.

(2) Sead Ramović
Ni kocha na mchezaji wa zamani kutoka Ujerumani mwenye asili ya Bosnia

Kwa sasa ni kocha wa CR Belouizdad ya Algeria baada ya kuondoka Yanga msimu uliopita.

(3)Romuald Rakotondrabe
Kocha wa sasa wa timua ya taifa ya Madagascar (Barea). Ni mzawa wa Madagascar, amejijengea heshima kwa kuibua vipaji vya ndani na kuiongoza timu hiyo kuvunja rekodi kwenye AFCON. Anajulikana kwa mbinu za kujilinda na kutumia mashambulizi ya kushtukiza.

Nani achukue mikoba ya Roman Folz pale Yanga Sc

04/10/2025

Kumfungia mchezaji mechi 5 hatuusaidii mpira wetu

"Hasara ya kwanza tunakosa mashabiki, hasara ya pili tunakosa mapato na hasara ya tatu tunalipa faini ya USD 50,000. Vil...
26/09/2025

"Hasara ya kwanza tunakosa mashabiki, hasara ya pili tunakosa mapato na hasara ya tatu tunalipa faini ya USD 50,000. Vilevile tumepewa adhabu kutokana na mechi ya fainaili dhidi ya RS Berkane, huku vilevile tuliwasha fireworks.

Kwenye mechi ya fainali tumetozwa faini ya USD 35,000. Jumla Tumetoshwa USD 85,000 sawa na Tsh. 200 milioni."

"Tunacheza bila mashabiki kwenye mechi dhidi ya
Gaborone United pekee lakini sbaabu tumefanya makosa mfululizo CAF watakuwa makini na sisi kwelikweli sababu wanaona tunafanya vitendo ambavyo sio vya kiungwana hivyo watakuwa wanaangalia k**a Simba Sports Club tumebadilika. Ni lazima tuwe makini kwelikweli ili

kuwaonyesha kwamba tumejifunza na tumebadilika. Kuanzia hivi sasa tuchukue taswira mpya kwenye eneo la ushabiki."

"Wapo mashabiki ambao wametaka kuwa sehemu ya maumivu ambayo tunapitia klabu ya Simba na maumivu yenyewe ni faini ya Tsh. 212,500,000 sawa na USD 85,000. Kwa mapenzi yao mashabiki wameomba kuchangia faini ili kuipunguzia klabu mzigo na sisi
tumepokea na tumeridhia mashabiki wachangie"

Ahmed Ally

UPDATE🚨Sowah aanza rasmi Ligi Kuu akiwa na Simba SC baada ya kutokea Singida BS. Hii itakuwa mechi yake ya kwanza rasmi ...
25/09/2025

UPDATE🚨

Sowah aanza rasmi Ligi Kuu akiwa na Simba SC baada ya kutokea Singida BS.

Hii itakuwa mechi yake ya kwanza rasmi ndani ya jezi nyekundu za Msimbazi, akitarajiwa kuonyesha ubora wake na kuisaidia Simba katika mbio za ubingwa.

25/09/2025

Roman Folz anahitaji muda kidogo tu kupata kikosi, lakini timu iko vizuri sana

25/09/2025

Yanga wanatimu nzuri sana msimu huu

Address

Mazinde
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sports Online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sports Online:

Share