21/05/2026
YALIYO KIKI ✍️
Mimi ni mwanamke Umri wangu ni miaka 36 Sasa, Niko kwenye ndoa huu ni mwaka wa kumi, tuna Watoto watatu Mimi na mume wangu.
Dada yangu, iko hivi kuanzia mwezi wa pili mwaka huu mume wangu aliacha kunigusa Wala akawa hataki kushiriki tendo la ndoa, Yani ilifikia hatua mpaka nimlazimishe ndo tuna fanya na nisipo taka Mimi yeye akawa hawezi Kunihitaji kabisa na tukawa tuna weza maliza mwezi bila kufanya kitu ambacho ni tofauti na alivyo kuwa nyuma.
Tumeendelea na hiyo hali ya Kusumbuana sana kwenye tendo ila mwisho siku juzi jumatatu aliona anifungukie kweli, aliniita akaniambia yeye Kwa Sasa hana hisia na Mimi na hawezi kuwa na hisia juu yangu tena, akaniomba nitafute mwanaume mwingine ila nisitoke hapa nyumbani niendelee kulea watoto.
Dada nililia sana, nikamwuliza nini Sababu ya yeye kukosa hisia na mimi, anacho nijibu ni kuwa hata yeye haelewi ila tu imetokea tu Hana hisia na Mimi za kufanya tendo.
Lakini kwenye masuala ya Matumizi na Huduma zote anatoa, na Kila ninacho hitaji ananipatia ila changamoto tu ndo hiyo, na Ili kunithibitishia ana maanisha kweli kahamia chumba kingine, kanunua kitanda, Tv na Kila kitu kaamua kunipisha chumbani.
Ukweli Mimi sielewi kinacho endelea Kwa mume wangu na sija mwambia mtu yeyote, naomba unipostie nipate ushauri kwenye hiki kitu nahisi kuchanganyikiwa.