Tanzania Ya Samia

  • Home
  • Tanzania Ya Samia

Tanzania Ya Samia 🔥 Powered by youth. Inspired by Mama Samia.
💪 Digital force for truth, change & national pride.
✊️The Pride Of CCM & President Samia💚💛.

Our Services are | TRAVEL| TOUR| RENTAL| BOOKINGS| AIR TICKETING. In Partnership with SEMPA EXPERTS (Tours & Car Rental)

KILA MTU ANAISHABIKIA* *CCM* *KWA STYLE YAKE*Kitu muhimu wananchi wanachopaswa kufahamu ni kuwa huu ni mwaka wa uchaguzi...
19/07/2025

KILA MTU ANAISHABIKIA* *CCM* *KWA STYLE YAKE*

Kitu muhimu wananchi wanachopaswa kufahamu ni kuwa huu ni mwaka wa uchaguzi; kelele, mivutano na shutuma zisizo na maana ni sehemu ya maisha.

Hakika katika jicho la tatu; jicho la kutulia na kutumia akili nyingi - ni wazi Upizani dhidi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) umezidi kuzikwa.

Leo wapizani hawapigi tena kelele za No Reforms No Election, leo wapizani wameungana na kushangilia kelele za Balozi Kada wa CCM Ndugu Humphrey Polepole, anayelia na Chama chake Chama Cha Mapinduzi. Anacholilia yeye mwenyewe ndiye anayejua.

Ukimsiliza Ndg. Polepole halili ujenzi wa Taifa hili, haangazii miradi iliyokamilishwa na inayoendelea, haangazii uchumi na uboreshwaji wa miundombinu mbalimbali, hatuambii juu ya elimu bure na mikopo ya elimu ya juu kufika kwa wakati kwa wanafunzi.

Ndugu Polepole ameridhika na utendeji kazi wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Jemedari Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ngazi za kitaifa, bila shaka hana kesi ya maendelo bali ana kesi ya yanayoendelea ndani ya chama chake.

Watu wa 'Reform' pasipo kujigundua wameingia kwenye mtego na kushangilia pale Ndugu Polepole anapolia kuimarisha siasa za ndani ya CCM, kuimarisha maadili ya CCM na yale yaliyo ndani ya CCM anayoona yanahitaji kurekebishwa. Pasipo kujitambua 'Reform' wanaungana kuijenga CCM; hii ndio nguvu ya CCM.

Kelele zote zimekufa za Mahakamani na 'Reform' kelele utakazozisikia sasa ni CCM. Hii pia ukiangalia kwa Ndugu Askofu Gwajima utaiona upepo wa kelele ni wa kichama na si kitaifa. Leo hii wote tunapambana na Katiba ya CCM, hakika Wahenga hawakukosea waliposema CCM BABA LAO, wamefanikiwa KUZIMA ZOTE NA KUWASHA MOSHI WAKIJANI masikio macho harakati zote zinaangazia CHAMA TAWALA WAKIELEKEA OKTOBA KUTIKI ✅.

The Diplomat_Tz 🇹🇿 .
🇹🇿
🧭
🔨


🌍✨ UZINDUZI WA DIRA YA TAIFA 2050 ✨🌍Leo Tanzania imeandika ukurasa mpya wa matumaini na mwelekeo! 🇹🇿Kupitia Dira ya Taif...
17/07/2025

🌍✨ UZINDUZI WA DIRA YA TAIFA 2050 ✨🌍
Leo Tanzania imeandika ukurasa mpya wa matumaini na mwelekeo! 🇹🇿
Kupitia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050, tunaweka msingi wa kujenga taifa jumuishi, imara, shindani na endelevu kwa vizazi vijavyo.

📌 Kaulimbiu: “Tanzania Tunayoitaka: Jumuishi, Imara, Shindani na Endelevu”
📌 Misingi ya Dira:
✅ Uchumi wa kisasa unaotegemea viwanda na ubunifu
✅ Uwekezaji kwa watu – elimu, afya, ajira
✅ Utawala bora, haki na amani
✅ Uhifadhi wa mazingira na ustahimilivu wa tabianchi

🔥 Dira ya 2050 si ndoto – ni mwongozo wa hatua!
Tuanze leo kujenga Tanzania ya kesho kwa mshikamano, maarifa, na maadili.

📣 Tanzania ya 2050 ni yetu sote – vijana, wazee, wanawake, wanaume – wote tunahitajika! .
🇹🇿
🧭
🔨


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mwenyekiti Mstaafu wa Chadema Mhe...
17/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mwenyekiti Mstaafu wa Chadema Mhe. Freeman Mbowe mara baada ya kuzindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC) Jijini Dodoma tarehe 17 Julai, 2025. .
🇹🇿
🧭
🔨


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi pamoja na wageni mbalimbali k...
17/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi pamoja na wageni mbalimbali kabla ya kuzindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC) Jijini Dodoma tarehe 17 Julai, 2025. .
🇹🇿
🧭
🔨


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akionesha nakala za vitabu vya Dira ya Taifa ya M...
17/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akionesha nakala za vitabu vya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 mara baada ya uzinduzi katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC) Jijini Dodoma tarehe 17 Julai, 2025. .
🇹🇿
🧭
🔨


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika ...
17/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC) Jijini Dodoma tarehe 17 Julai, 2025. .
🇹🇿
🧭
🔨


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya heshima na shukrani kutoka kwa W...
17/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya heshima na shukrani kutoka kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Profesa Kitila Alexander Mkumbo kwenye hafla ya uzinduzi wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC) Jijini Dodoma tarehe 17 Julai, 2025. .
🇹🇿
🧭
🔨


Viongozi pamoja na wageni mbalimbali wakiwa kwenye kwenye hafla ya uzinduzi wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 iliyofany...
17/07/2025

Viongozi pamoja na wageni mbalimbali wakiwa kwenye kwenye hafla ya uzinduzi wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC) Jijini Dodoma tarehe 17 Julai, 2025. .
🇹🇿
🧭
🔨


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na viongozi mbalimbali kwenye hafla ...
17/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na viongozi mbalimbali kwenye hafla ya uzinduzi wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC) Jijini Dodoma tarehe 17 Julai, 2025. .
🇹🇿
🧭
🔨


UTAWALA • AMANI • USALAMA • UTULIVUHaya siyo maneno ya kawaida — ni misingi muhimu inayobeba ndoto ya Tanzania tunayoita...
17/07/2025

UTAWALA • AMANI • USALAMA • UTULIVU

Haya siyo maneno ya kawaida — ni misingi muhimu inayobeba ndoto ya Tanzania tunayoitaka ifikapo 2025.
Ni dira ya taifa letu kuelekea kwenye maendeleo jumuishi na ya kudumu.

🇹🇿 Utawala bora unaleta uwajibikaji.
🕊️ Amani ni msingi wa mshikamano wetu.
🛡️ Usalama unatulinda sisi na mali zetu.
🌿 Utulivu hutuwezesha kupiga hatua bila kuyumba.

Kwa pamoja, haya ndiyo yanayojenga mazingira ya taifa imara, linalojali watu wake na linaloweka mbele maslahi ya wote.

Dira ya Taifa 2025 si ndoto tu — ni mwongozo wa sasa kwa Tanzania yenye haki, ustawi, na matumaini. .
🇹🇿
🧭
🔨


Fuatilia matangazo ya moja kwa moja kupitia Akaunti zetu za Instagram: ikulu_mawasiliano, Facebook: Ikulu Tanzania Faceb...
17/07/2025

Fuatilia matangazo ya moja kwa moja kupitia Akaunti zetu za Instagram: ikulu_mawasiliano, Facebook: Ikulu Tanzania Facebook fanpage: Ikulu Mawasiliano, Twitter: ikulu_Tanzania Youtube Channel: Ikulu Tanzania na Tovuti: www.ikulu.go.tz .
🇹🇿
🧭
🔨


Tanzania Mpya, Dira Mpya 🇹🇿Ili kufikia taifa jumuishi lenye ustawi, haki na linalojitegemea, tunasimama juu ya NGUZO TAT...
17/07/2025

Tanzania Mpya, Dira Mpya 🇹🇿

Ili kufikia taifa jumuishi lenye ustawi, haki na linalojitegemea, tunasimama juu ya NGUZO TATU kuu za mageuzi:

1️⃣ Uchumi Imara, Jumuishi na Shindani – Uchumi unaogusa maisha ya kila mmoja, unaotoa fursa sawa kwa wote.

2️⃣ Uwezo wa Watu na Maendeleo ya Jamii – Elimu bora, afya imara, usawa na jamii inayojali.

3️⃣ Uhifadhi wa Mazingira na Ustahimilivu wa Tabianchi – Kulinda ardhi yetu, maji yetu na hewa yetu kwa kizazi cha leo na kesho.

🇹🇿 Kwa pamoja, tunaijenga Tanzania tunayoitaka – yenye maendeleo endelevu na watu waliowezeshwa. .
🇹🇿
🧭
🔨


Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzania Ya Samia posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Tanzania Ya Samia:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share