Muvi za kijanja

Muvi za kijanja Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Muvi za kijanja, Digital creator, Dar es Salaam.

👉mzigo unahusu kampuni Moja inayomilikiwa na nyamela mmoja kwa jina la Mr blutKampuni yake inaandamwa na skendo za mauwa...
02/10/2024

👉mzigo unahusu kampuni Moja inayomilikiwa na nyamela mmoja kwa jina la Mr blut

Kampuni yake inaandamwa na skendo za mauwaji ya wafanyakazi wake pindi wanapokaribia kustaafu,Lakini hamna ushahidi wa kumfunga

Hufanya mauwaji hayo ili kiinua mgongo Cha wafanyakazi hao kibaki mikononi mwake kwa maslahi yake mwenyewe

Kazi hii ya mauwaji na kupoteza ushahidi wa mauwaji ilikuwa ikifanywa na mtu wake Mzee Duncan almaarufu black kaiser

Baada ya Dancan kufanya kazi hiyo ya mauwaji kwa miaka mingi na yeye pia muda wake wa kustaafu ukawadia na yeye pia wakapanga kumletea Ile Ile michezo

Hapa ndipo unatimia ule msemo usemao ukiuwa kwa upanga na wewe utakufa kwa upanga

Zilipobaki siku 14 Ili astaafu alipewa mission ya mwisho,Wakiwa na dhumuni kwamba baada ya kufanya mission hiyo na yeye wamletee huo huo mchezo waliofanyiwa wafanyakazi wengine

Hivyo kikaagizwa kikosi kipya Cha wauwaji wachanga ili wakadeal na kumpoteza Mzee Duncan

Bila kujua kwamba kakwepa mishale mingi kipindi cha ujana wake mpaka kufikia umri huo wa kustaafu,hivyo ana mafunzo na mbinu nyingi za kudeal na hao watoto walioanza kazi majuzi

Hapo ndipo alienda kuwaonyesha yeye ni mafia zaidi yao,uzee wake si kizuizi Cha yeye kushindwa kuwapelekea moto na kuwachezesha sindimba.✍️

Ni single movie,ipo iliyo tafsiriwa na ambayo haijatafsiriwa,Bei sh 1000 tunatuma Whatsapp na telegram 0742932384,pia tuna group la movie na season telegram, link ipo sehem ya comment.👇

Michael Dudikoff alipitia njia fupi na thabiti kutoka kuwa mtu asiyejulikana hadi kuwa nyota wa filamu za mapigano. Akiw...
19/09/2024

Michael Dudikoff alipitia njia fupi na thabiti kutoka kuwa mtu asiyejulikana hadi kuwa nyota wa filamu za mapigano. Akiwa anafanya kazi ya kuhudumia wateja kwenye mgahawa, aligunduliwa na mhariri wa jarida la mitindo la Esquire, Max Evans, ambaye alimshauri kujaribu kuwa mwanamitindo.

Maonesho ya mitindo ya mavazi yalimpeleka kwenye matangazo ya picha, ambayo hatimaye yalifungua mlango wa uigizaji kupitia matangazo ya kibiashara kwa wateja wakubwa k**a Coppertone na Stridex.

Hatua iliyofuata ilikuwa uigizaji kwenye televisheni; alionekana kwenye kipindi cha vichekesho kiitwacho Happy Days.

Baada ya kucheza nafasi ndogo kwenye vipindi vya televisheni (k**a vichekesho vya NBC Gimme a Break!) na filamu (k**a filamu ya kisayansi ya TRON), Dudikoff alipata nafasi ya kuwa mhusika mkuu ambayo anajulikana zaidi, Pvt. Joe Armstrong, katika filamu ya American Ninja.

Mbali hili tambala alitamba na filamu k**a Avenging Force, Platoon Leader na River of Death.

Dudikoff amemuoa Belle Dudikoff, na wanandoa hawa wana watoto wawili pamoja. Licha ya umaarufu wake, Dudikoff ameweza kudumisha maisha ya familia yenye usawa na anabaki kujitolea kwao.

Baada ya kuwa na kazi zenye mafanikio katika tasnia ya burudani, Dudikoff alitangaza kustaafu kutoka kwenye uigizaji.

Hivi Bado mnaamini bongo movie inazinguwa vijana wadogo Sasa wanaibeba hivyo ,hivyo inabidi tumsahau kanumba maisha ya b...
19/09/2024

Hivi Bado mnaamini bongo movie inazinguwa vijana wadogo Sasa wanaibeba hivyo ,hivyo inabidi tumsahau kanumba maisha ya bongo movie yasonge RK Mzee wa wrong house na huku sasa anaichanganya sukari ndani ya SIRI YA HUBA🔥🔥

14/09/2024

👉Katika kusheherekea siku yake ya kuzaliwa ya kutimiza miaka 75 Mzee Charles Abernathy aliwaita watoto wake wote wanne ili ajumuike nao katika siku yake hiyo muhimu

Wanae wote waliitikia mualiko na kufika katika jengo la baba yao la kifahari aliyekuwa kajaaliwa Kuwa na utajiri mkubwa,Lakini miongoni mwa kijana wake kwa jina la Grew alifika na mkewe Hannah

Jambo la Mwanae kufika na mkewe halikuwafurahisha baadhi ya ndugu maana mualiko ulikuwa unawahusu watoto tu,maana Baba yao alikuwa na agenda ya sili dhidi Yao

Baada ya muda kidogo baba yao aliwaambia kwamba kawaita nyumbani kwake siku hiyo kwa sababu usiku huo anapaswa kuuwawa,hivyo basi alimpa bibie Hannah nafasi ya kuondoka ili msala huo wakabiliane nao ndugu tu,Lakini bibie akagoma🤔

Hivyo basi lengo la wito huo kwa wanae ni kuhakikiaha kwamba usiku huo anapaswa kuuwawa hivyo wanapaswa wafanye juu chini wazuie baba yao asiuwawe 😱

Watoto walidhani masihara,baadae akawaambia kwamba wakifanikiwa kumlinda dhidi ya watu wanaotaka kumuuwa usiku huo basi atawalithisha mali zake zote😍

Na iwapo wakishindwa kumlinda baba yao dhidi ya kifo basi utajiri wake wote utagawiwa katika vituo vya misaada ikiwemo vituo vya watoto yatima

kuonyesha kwamba haleti masihara alimuamuru mtu wake wa karibu afunge milango yote kwa nje Kisha wasubiri kizaa zaa kitakachokuja usiku

Eeh bhana kumbe utajiri wote aliokuwa nao Mzee aliupata kwa njia za haramu za kishirikina(k**a freemason) na wanae hawakujua na mkataba wake na mashetani ilikuwa kwamba akifikisha miaka 75 basi ndio siku yake ya mwisho😔

kwahiyo Mzee akaona si mbaya kizaa zaa hicho kikimkuta yeye na wanae usiku huo wa birthday yake maana wote wamekula huo utajiri haramu🤣oyaah ni bonge Moja la horror muvi,humo ndani Kuna kizaa zaa Cha maana bibie Hannah alijuta kuingilia mambo ya kifamilia🤣

Mzigo ninao Whatsapp na telegram 0742932384, iliyo tafsiriwa na ambayo haijatafsiriwa Bei sh 1000.✍️

Digital creator

14/09/2024

👉Chuoni na mashuleni huwa Kuna Ile pisi kali ambayo Kila mwanaume rijali anatamani Kuwa nayo,hichi ndicho kilichomkuta mwamba Nick baada ya kumuelewa mwanachuo mwenzie bibie Christina

Shida ni kwamba bibie Christina Yupo matawi ya juu hapo chuoni kuanzia swaga,pia ni mtoto wa kishua na pesa ipo,Lakini mtaalam wetu Nick yeye swaga ziro kuanzia tembea yake,ongea yake pia kutupia code kali hajui

Hivyo basi hali hiyo ilimnyima ujasiri Nick na wanachuo wengine wa kiume wenye swaga ziro kushusha nyavu kwa bibie

Kuna siku bibie Christina alichukua gari ya mama yake aliyekuwa kasafiri na kwenda kupiga nayo misele hadi maeneo ya chuoni kwao,bahati mbaya alipata ajali,hivyo Ili kuuwa Soo pindi mama yake atakaporudi alitaka kufix hitilafu iliyojitikeza katika gari hiyo

Hivyo ikabidi atafute mafundi chuoni hapo maana kulikuwa na kitengo Cha ufundi magari,bad News akaambiwa gari lake ili liwe sawa matengenezo yatagharimu muda wa wiki mbili,wakati bibie anataka zoezi hilo likamilike kwa muda wa siku chache maana mama yake karibu anarudi

Good news kwenye kitengo hicho Cha garage alikuwepo pia kijana asiye na swaga Nick ,akaona hiyo ndio fursa ya Kuwa karibu na bibie,hivyo akamwambia bibie gari lake atalitengeneza kabla ya hizo wiki mbili,lakini kwa sharti Moja tu,waigize k**a Wapenzi chuoni hapo kwa muda wa wiki mbili

Bibie akaona fresh tu,Si kuigiza tu bila kurusha roho hamna Shida, ila kutokana na muonekano wa Nick kuanzia uvaaji,mtindo wa nywele na ongea yake bibie aliona jamaa anamuaibisha chuoni hapo

Hivyo akaanza kumbadirisha kuanzia kwa kumtafutia pamba kali,kuchange mtindo wa nywele n.k,Ili wafanane,eeh bhana baada ya bibie kumgharamia mshkaji nyota kali na uhandsome wa jamaa uliofichika awali ukaanza kuonekana chuoni hapo

Ghafla akawa staa kuliko bibie,madem wa chuoni hapo waliomuona k**a rofa wakawa wanang'ang'ania Kuwa nae,too bad hata bibie Christina alijikuta tayari moyo wake umeangukia kwa Nick ambaye hivi Sasa Kawa staa kuliko bibie,na hana habari tena na bibie Christina

Bibie akawa hazingatiwi tena too bad Nick akaanza kutoka na pisi nyingine akiwemo rafiki wa karibu wa christine wakati huo bibie Christina alikuwa ameanza kumpenda Nick kikweli kweli si maigizo tena🤔mapenzi hayajaribiwi🤣

Ni single movie, tunayo Whatsapp na telegram 0742932384, ipo iliyo tafsiriwa na ambayo haijatafsiriwa Bei sh 1000.✍️

Digital creator

Movie inaañza nchini india mwana anaenjoy maisha ya kijijini ya amani na familia yake yani mama yake pamoja na mkewe lak...
13/09/2024

Movie inaañza nchini india mwana anaenjoy maisha ya kijijini ya amani na familia yake yani mama yake pamoja na mkewe lakini ataingia tamaa kwenda kutafuta maisha nje ya india na kudondokea nchini saudia ili akafanye kazi na pesa atume nyumbani sasa movie ndo inaanza je atafanikiwa kufika saudia ?

NB Wale wanao penda kuangalia movie uku wanafuta machozi😂 ndio kazi yenu moja ya movie kali za drama za asia za mwaka2024🔥

Makadirio ya Filamu Bora zaidi za Muda wote;1. The Godfather (1972)2. The Shawshank Redemption (1994)3. Schindler's List...
13/09/2024

Makadirio ya Filamu Bora zaidi za Muda wote;

1. The Godfather (1972)
2. The Shawshank Redemption (1994)
3. Schindler's List (1993)
4. Raging Bull (1980)
5. Casablanca (1942)
6. Citizen Kane (1941)
7. Gone with the Wind (1939)
8. The Wizard of Oz (1939)
9. One Flew Over the Cuckoo's Nest (1975)
10. Lawrence of Arabia (1962)
11. Pulp Fiction (1994)
12. The Good, the Bad and the Ugly (1966)
13. Fight Club (1999)
14. Forrest Gump (1994)
15. The Matrix (1999)
16. Goodfellas (1990)
17. Star Wars: Episode V - The Empire Strikes Back (1980)
18. The Lord of the Rings: The Return of the King (2003)
19. Inception (2010)
20. Apocalypse Now (1979)
21. 12 Angry Men (1957)
22. Psycho (1960)
23. The Lord of the Rings: The Fellowship of the Ring (2001)
24. Back to the Future (1985)
25. The Dark Knight (2008)
26. The Lord of the Rings: The Two Towers (2002)
27. It's a Wonderful Life (1946)
28. Raiders of the Lost Ark (1981)
29. Gladiator (2000)
30. The Silence of the Lambs (1991)
31. Saving Private Ryan (1998)
32. Terminator

Tama Riyadi, kwenye jengo lenye urefu wa ghorofa ishirini, akiwa kaweka watu wake kila chumba..Humo ni umafia tu, kubaka...
13/09/2024

Tama Riyadi, kwenye jengo lenye urefu wa ghorofa ishirini, akiwa kaweka watu wake kila chumba..

Humo ni umafia tu, kubaka, kulala, kula unga, kutengeneza bangi, kupakia madawa, na kila aina ya uharifu..

Ni genge la waharifu wenye roho za kinyama kwenye miili yao, kwao damu sio tatizo kubwa hata kidogo..

Yoyote ataeingia kwenye himaya yao, ni k**a ametia saini, kwenye mkataba rasmi wa kifo chake..

Sio raia sio polisi, hakuna anaepaswa kuingia ndani ya jengo hili, na kuhitaji mazungumzo ya kuwaweka chini ya ulinzi..

Anaitwa Rama, Rookie Office, akiwa na kundi la watu zaidi ya 20 nyuma na mbele yake, walifika kwenye himaya ya Tama Riyadi..

Lengo likiwa waondoke nae akiwa hai au maiti, haijalishi watakutana na nini, walikula kiapo cha kuondoka na mtuhumiwa wao..

Ilikuwa rahisi?, hapana, Tama Riyadi analindwa na watu wenye kila aina ya silaha mikononi..

Kumfikia yeye ni kuhitaji kuionesha Dunia, kuwa hakuna linaloshindikana chini ya ardhi hii..

Kumaliza korido zote, inabidi umalizane na waliotangulia, ili umfikie Tama kwenye kiti chake cha kuzunguka..

Sio rahisi, lakini sio haiwezekanai, Rama na kundi lake walifika, na walionana na kila waliemtarajia..

Ni giza la khofu na mashaka ya kutupwa, ndani ya hilo jengo, maaskari walibaki wachache sana..

Walitakaiwa kuzinusuru roho zao, ili wapate cha kubadithia huko nje kwenye familia zao..

Ilitembea panga mpaka giza linaingia, Rama alipoona wamebaki wachache, akatakiwa ajisalimishe..

Kwake hilo ni tusi, akafungua ukurasa mzito wa kifo na uhai, kile kitabu cha ngumi za Waindonesia, Panchak Sirat Style...

Aliona bora arudishwe maiti, kuliko kujipeleka kwenye mikono ya Tama Riyadi, mwanaume akafunga vidonda, akasema liwalo na liwe..

Ilipigwa ngumi ya karne, alikutana na mnyama Mad Dogo, Yayan Ruhian, chuma ikala chuma..

Nani atoke akiwa mzima, kwenye jengo lile la kifo na uhai?, movie yangu bora ya action ya muda wote!..

Wenzetu wana mitindo yao ya kupigana, ambayo ndio imewapa majina makubwa na pesa nyingi..Mtu k**a Jackie Chan, yeye ni b...
13/09/2024

Wenzetu wana mitindo yao ya kupigana, ambayo ndio imewapa majina makubwa na pesa nyingi..

Mtu k**a Jackie Chan, yeye ni bingwa kweli wa Taekwondo, Judo na kung fu..

Mtu k**a Jet lee, bingwa haswa wa Tai chi, na Jeet Kun do fighting style, huku akipiga pia kung fu..

Donnie Yen the master, yeye ni mwalimu wa Wing chun, Wushu, kung fu, na Kick boxing..

Na Idol wake mkubwa ni Bruce Lee, ndio maana kwa walioangalia The New Big Boss, mule Don alipiga kila kitu k**a Bruce..

K**a ilivyo kwa Thailand na Tony Jaa wao na Dan Chupong, kule mapigo ni Muai Thai, unapigwa unavunjwa, hadi Moi hawakutibu..

Halafu kule Indonesia kuna Panchak Sirat, ndio kung fu ya kule, na alieileta kwenye screen kikamilifu ni Iko Uwais..

K**a umeangalia zile Raid zote mbili, na ndio aina ya mtindo anaopigana, utagundua hiyo Panchak Sirat, ni mapigo ya moto wa kuotea mbali..

Lakini mnajua kuwa Iko Uwais ni Starring, ila kuna mtu hamuwezi, au tuseme huyo mtu ni mwalimu haswa wa hilo pigo..

Anaitwa Yayan Ruhiyan, huyo hapo kwenye hiyo picha, huyo ni mkufunzi haswa wa hilo pigo la Panchak Sirat..

Utamuona kwenye A boy kills the world, Raid 1 & 2, Beyond Skyline, na kwenye Merantau, akiwa tena na Iko Uwais..

Msela anapiga hadi anakera, kufa kwake ni kugumu kuliko kawaida, ana pumzi, ana nguvu, ana speed, na anapiga sehemu muhimu tu..

Ukijua starring wako anaemda kukutana na Mad Dog Yayan Ruhian, jiandae kumuonea huruma hadi mwisho..

Sisi wapenda ngumi, kumuangalia Mad dog ni starehe yetu, kwa sababu hachoshi hata kidogo..

Nani hamjui balaa lake, tuanzie hapo kwanza😃..

13/09/2024

Leo nawapa single hizi Bora za mwaka huu 2024

1. Dead Hand 2024

2. Under Paris 2024

3. Furiosa A mad max saga 2024

4. Mr 9 Do our Die 2024

5. La capitano 2024

6. City Hunter 2024

7. The beekeeper 2024

8. Badland Hunter 2024

9. Darkness of man 2024

10. Hellhound 2024

11. Cash out 2024

12. Abigail 2024

13. Life After fighting 2024

14. Trash 2024

15. Alienoid The Return to the future 2024

16.. Dune part two 2024

17. Cristimas Bloody 2024

18. Aquiet place day one 2024

19. Caught in time 2024

20. Code.8 part TWO 2024

KAZITAFUTE HIZO BADAE UJE UNAMBIE HAPA😎

Hollywood wanajitahid sana kwenye horror movie         Kwa muda mrefu since 1990 mpk sasa wanajitahidi sana      Ila kwa...
13/09/2024

Hollywood wanajitahid sana kwenye horror movie
Kwa muda mrefu since 1990 mpk sasa wanajitahidi sana
Ila kwa maono ya mbele INDONESIA Wanakuja kasi sana kwenye horror japokuwa hawana manjonjo mengi sana kwenye muvi zao ila Jina HORROR MOVIES wanalitetendea haki sana
Yn muvi zao zinatisha haswa ukiona cover photo ya movie ukienda ndani na uhalisia unaupata hvhv yn wanakuja kasi sana
KM UMEKUWA ADICTED NA HORROR MUV NA UNAKOSA ULE MSISIMKO WA HALISI NOW ANZA KUFATILIA ---INDONESIA HORROR MOVIES
HIZO
SIJJIN_-
KAFIR_-
MUNAFIK
_-PAMAL_-
KULTUS IBILIS
_MANGARIB na nyingnezo nying

😺Rasmi movie mpya ya Akshay Kumar na muongozaji Priyadarshan ya kutisha na comedy itaitwa Bhooth Bangla..!
13/09/2024

😺Rasmi movie mpya ya Akshay Kumar na muongozaji Priyadarshan ya kutisha na comedy itaitwa Bhooth Bangla..!

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Muvi za kijanja posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share