Saa 24

Saa 24 Welcome to Masaa 24. Official page for Tanzanian Media blog. Live Local and International News | Updates | Politics | Sports | Intertainment.

16/03/2026

Msanii wa muziki A.K.A London Boy anaelezea jinsi Nyarugusu town ilivyojengeka.

16/03/2026

Katika kuelekea kuhitimisha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, tunakumbushwa kuwa na kiasi, hasa katika unywaji maji kwani maji yanaweza kuwa sumu.

Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi alizungumza haya Machi 2, 2026 katika Msikiti wa Mtoro, katika Mazungumzo ya Busati la Mtoro

Video: Dua TV

#

15/03/2026

Sauti hii umeisikia wapi?

Huyu ni dada Mary Chizi mwenye sauti maarufu zaidi katika ulimwengu wa watumia simu za mkononi.

06/03/2026

Mafuriko makubwa yameharibu mali na miundombinu mbalimbali katika jiji la Nairobi kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha tangia mapema hapo jana.

Mpaka sasa haijajulikana ukubwa halisi wa hasara iliyosababishwa na mafuriko hayo ingawa serikali ya Kenya imeripotiwa kuagiza jeshi la Ulinzi, The Kenya Defence Forces (KDF) kusaidia na shughuli za uokoaji katika kipindi hiki cha dharura.

Video Credit: nicki bigfish

03/03/2026

Mwanamke mmoja nchini Kenya ameingia matatani baada ya kutuhumiwa kumuuzia mzazi dawa ya ngozi badala ya dawa ya macho, ili akampake mtoto wa mzazi huyo kwenye macho mara tano kwa siku, kitendo ambacho kimwpelekea upofu kwa mtoto huyo.

Katika tamko lililotolewa na Chama cha Wafamasia nchini Kenya (Pharmaceutical Society of Kenya) Rais wa Chama hicho Wairimu Njuki amesema mtuhumiwa huyo ambaye video yake imesambaa mtandaoni, siyo mwanachama wao, na amewaasa waKenya kuwa makini na watumishi wanaojitambulisha kuwa wafamasia.

03/03/2026

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Robert Chalamila akizungumzia tatizo la foleni mkoani humo.

02/03/2026

Mwanamke mmoja wa ki Israel aliyejulikana kwa jina la mtandaoni Noya Zion amelazimika kutoa tamko baada ya kuona picha yake katika kituo kimoja cha habari nchini Izraeli k**a mmoja kati ya waliofariki duni katika maandamano yanayoendelea nchini Iran.

Video za dada huyo zilisambaa mitandaoni hasa baada ya kuonekana kuwa ni kitendo kinachojirudiq mara kadhaa.

‎Kamishna Turk alisema hatua iliyochukuliwa na Tanzania kuanzisha Tume ya kuchunguza kilichojiri Oktoba 29, k**a hatua m...
27/02/2026

‎Kamishna Turk alisema hatua iliyochukuliwa na Tanzania kuanzisha Tume ya kuchunguza kilichojiri Oktoba 29, k**a hatua muhimu inayojali haki za binadamu.

‎Kamishna Turk alisema hatua iliyochukuliwa na Tanzania kuanzisha Tume ya kuchunguza kilichojiri Oktoba 29, k**a hatua muhimu inayojali haki za binadamu .

27/02/2026

Kutana na jeshi mahiri linaloulinda msikiti mtakatifu wa Makkah na mahujaji wanaozuru kuhiji katika msikiti huo.

Jeshi hili la ki Saudi linatumia vifaa vya hali ya juu ikiwemo kamera zenye uwezo wa kutambua matukio mbalimbali kutokea angani.

27/02/2026

Kundi kubwa la nzige limeonekana kuvmia maeneo ya kati ya Mauritania na Morocco likihatibu mazao na kuzua taharuki miongoni mwa watu.

Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa FAO, nzige hao ambao wameanza kuvuka kuelekea visiwa vya Canary nchini Hispania wanasemekana kusababishwa na joto kali lililosababisha uwepo wa masalia ya nzige hao.
Video: Accuweather

26/02/2026

Rais Salva Kiir Mayardit mwenye Makamu wa Rais watano. Je wajua ni kwa nini?

Katika South Sudan, tangu Februari 2020, nchi imekuwa na makamu watano wa rais chini ya serikali ya umoja inayoongozwa na Rais Salva Kiir Mayardit. Hii ni matokeo ya mkataba wa amani wa mwaka 2018 uliolenga kumaliza vita vya ndani vya muda mrefu na kuleta muundo wa ushirikiano wa vyama mbalimbali vya kisiasa. 

Hawa ndio makamu watano wa rais walioteuliwa:
• Riek Machar – Makamu wa Kwanza na kiongozi wa upande wa upinzani (SPLM-IO). 
• James Wani Igga – Makamu wa Pili (Chama Tawala).
• Taban Deng G*i – Makamu wa Tatu (Chama Tawala).
• Rebecca Nyandeng Garang – Makamu wa Nne, mwanachama wa kundi la Former Detainees. 
• Hussein Abdelbagi / Josephine Lagu – Makamu wa Tano, aliyechaguliwa kupitia South Sudan Opposition Alliance. 

Rais Kiir alianzisha muundo huu wa makamu wengi wa rais kubadili siasa za nchi zilizoharibika na vita, kwa kushirikisha makundi yote makubwa ya kisiasa serikalini.

Je ulijua hili?

Address

62 Mindu Street, Upanga
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Saa 24 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share