Saa 24

Saa 24 Welcome to Masaa 24. Official page for Tanzanian Media blog. Live Local and International News | Updates | Politics | Sports | Intertainment.

30/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Akizungumza na Wananchi wa Namtumbo Baada ya Kuzindua Kiwanda cha Majaribio cha Uchenjuaji wa Madini ya Urani Namtumbo Ruvuma, leo tarehe 30 Julai, 2025.

Kibonzo Cha Siku ✍️ na
29/07/2025

Kibonzo Cha Siku ✍️ na

Katika taarifa rasmi iliyotolewa katika Ofisi za  Makao Makuu, imebainishwa baadhi ya majina yaliyopita kugombea nafasi ...
29/07/2025

Katika taarifa rasmi iliyotolewa katika Ofisi za Makao Makuu, imebainishwa baadhi ya majina yaliyopita kugombea nafasi za ubunge na uwakilishi watakaoingia katika mchujo wa kura za maoni, kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba 2025, na kuacha baadhi ya wagombea maarufu k**a aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Bumbuli, January Makamba; Mtangazaji Maarufu, Burton Mwemba (Mwijaku), aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo, na wengine wengi.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele azindua rasmi wa kalenda ya uchaguzi...
26/07/2025

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele azindua rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 Jijini Dodoma Julai 26,2025.

Waziri wa ,  ameonyesha kuridhishwa na utekelezaji wa mradi wa maji unaojengwa kwa gharama ya Dola za Kimarekani milioni...
26/07/2025

Waziri wa , ameonyesha kuridhishwa na utekelezaji wa mradi wa maji unaojengwa kwa gharama ya Dola za Kimarekani milioni 53, ambao hadi sasa umefikia asilimia 68 ya ujenzi wake.

Akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo uliopo juu ya milima ya Mtaa wa Kagera, katika Halmashauri ya Manispaa ya Geita Waziri Aweso amesema dhamira ya serikali ni kuhakikisha kuwa wakazi wa mji wa Geita wanapata huduma ya maji ya uhakika na ya kutosha.

26/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi
CCM Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Akishiriki Mkutano Mkuu Maalumy CCM kwa Njia ya Mtandao White house -Dodoma, leo tarehe 26 Julai, 2025

Jeshi la Tanzania Immigration Services Department Uhamiaji mkoani Geita limewak**ata jumla ya watu 54 raia wa kigeni kut...
24/07/2025

Jeshi la Tanzania Immigration Services Department Uhamiaji mkoani Geita limewak**ata jumla ya watu 54 raia wa kigeni kutoka nchi za Burundi, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kwa tuhuma za kuishi nchini kinyume cha sheria, bila kuwa na vibali halali vinavyowaruhusu kuendelea kuwepo ndani ya mipaka ya Tanzania.

Jeshi la Uhamiaji mkoani Geita limewak**ata jumla ya watu 54 raia wa kigeni kwa tuhuma za kuishi nchini kinyume cha sheria.

Kuanzia tarehe 25 Julai 2025, hatua kali za kudhibiti upatikanaji wa maudhui ya ngono mtandaoni nchini Uingereza zitaanz...
18/07/2025

Kuanzia tarehe 25 Julai 2025, hatua kali za kudhibiti upatikanaji wa maudhui ya ngono mtandaoni nchini Uingereza zitaanza rasmi kutekelezwa; lengo likiwa ni kulinda watoto na vijana dhidi ya maudhui hatarishi.

Mamlaka ya udhibiti wa mawasiliano nchini humo, Ofcom, imetangaza orodha ya tovuti 13 kubwa za ngono ambazo zimekubali kuanza kutumia mifumo ya uhakiki wa umri kabla ya tarehe hiyo.

Unafikiriaje hatua hii?

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, ameshiriki uzinduzi wa Dira ya Maend...
17/07/2025

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, ameshiriki uzinduzi wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2050 uliofanyika leo, Julai 17, 2025, jijini Dodoma.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya uzinduzi huo, amesema kuwa akiwa Mwenyekiti wa CHADEMA kabla ya kustaafu, chama chake kilishiriki kikamilifu katika kutoa maoni na mawazo kwa ajili ya maandalizi ya Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, ameshiriki uzinduzi wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2050.

17/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Akizindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Dodoma Tanzania leo tarehe 17 Julai,2025.

Ripoti ya takwimu ya sekta ya Mawasiliano ya robo mwaka iliyoishia Juni 2025 imeonesha kuwa kumekuwa na ongezeko la lain...
16/07/2025

Ripoti ya takwimu ya sekta ya Mawasiliano ya robo mwaka iliyoishia Juni 2025 imeonesha kuwa kumekuwa na ongezeko la laini za simu kutoka laini milioni 90.4 Machi 2025 hadi kufikia laini milioni 92.7 Juni 2025 sawa na ongezeko la asilimia 2.6.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo inaonesha kuwa mkoa wa Dar unaongoza kwa kuwa na laini milioni 17.01, Mwanza ilishika nafasi ya pili kwa kuwa na laini milioni 6.14 na arusha ikishika nafasi ya tatu kwa kuwa na laini milioni 5.58.

Maendeleo hayo yanaonesha mwelekeo chanya wa sekta ya Mawasiliano unaotokana na usimamizi thabiti wa sekta unaofanya na serikali ya awamu ya sita kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

Tembelea tovuti ya (www.tcra.go.tz), au kupitia kiunganisho https://bit.ly/44tXbii ilikupitia ripoti kamili ya takwimu ya sekta ya Mawasiliano (Aprili - Juni 2025).

Address

62 Mindu Street, Upanga
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Saa 24 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share