Bongo Daily

Bongo Daily Tanzania News Updates

27/03/2026

MH SAMIA NI RAIS JASIRI NA ANALIPENDA TAIFA LETU

ZIARA YA MWENEZI MULEBA KAGERA

26/03/2026

TUMEMPOTEZA KIONGOZI ALIYETUMIKIA TAIFA MH WILLIAM LUKUVI

LEMA AIBUA MJADALA MKALI: KAULI ZAKE ZA ELIMU JUMUISHI ZATAFSIRIWA KUUNGA MKONO MASUALA YA LGBTQ+Mjumbe wa Kamati Kuu ya...
20/03/2026

LEMA AIBUA MJADALA MKALI: KAULI ZAKE ZA ELIMU JUMUISHI ZATAFSIRIWA KUUNGA MKONO MASUALA YA LGBTQ+

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Lema, ameibua mjadala mkali baada ya kauli zake kuhusu umuhimu wa elimu jumuishi mashuleni kutafsiriwa na baadhi ya wananchi k**a ishara ya kuunga mkono masuala ya ushoga (LGBTQ+).

Akizungumza katika kikao na vijana na wadau wa elimu, Lema alisisitiza kuwa ni muhimu kwa wanafunzi kupata uelewa mpana wa masuala ya kijamii, ikiwemo tofauti za kimtazamo na maisha ya watu mbalimbali duniani. Kauli hiyo imechukuliwa kwa mitazamo tofauti, huku baadhi wakidai kuwa inafungua mlango wa kufundisha na kukubali ushoga mashuleni.

“Tunapaswa kujenga kizazi kinachoelewa dunia ya sasa na kuheshimu tofauti za watu,” alinukuliwa Lema, kauli ambayo imezua tafsiri mseto katika jamii.

Wapo wanaomuunga mkono wakisema kuwa anasisitiza elimu na uelewa tu, lakini pia wapo wanaopinga wakidai kuwa kauli hiyo ni sawa na kuhalalisha ushoga kupitia mfumo wa elimu.

Kwa upande wa CHADEMA, baadhi ya wanachama wameeleza kuwa msimamo huo unalenga haki, usawa na kupunguza ubaguzi, huku wakisisitiza kuwa elimu jumuishi haimaanishi kuhamasisha mwenendo wowote bali kuelewesha jamii.

Hata hivyo, viongozi wa dini na baadhi ya wazazi wameonyesha wasiwasi mkubwa, wakitaka ufafanuzi zaidi juu ya mipaka ya elimu hiyo na namna itakavyolinda maadili ya Kitanzania.

Mjadala huu umeendelea kushika kasi mitandaoni, huku ukigawanya maoni ya wananchi kati ya wanaounga mkono mabadiliko ya elimu na wale wanaotetea maadili ya jadi.

Je, hii ni hatua ya kuelekea elimu ya kisasa au ni changamoto kwa maadili ya jamii? Mjadala bado unaendelea.

12/03/2026

MWANZA TULINDE AMANI YETU

MWENEZI KENANI AKIONGEA NA WANANCHI WA MWANZA

MWENEZI WA CCM TAIFA AKIWA KIKAO CHA MASHINA NYAMAGANA MWANZAKatibu wa NEC Itikadi Uenezi na Mafunzo  wa CCM ameendelea ...
12/03/2026

MWENEZI WA CCM TAIFA AKIWA KIKAO CHA MASHINA NYAMAGANA MWANZA

Katibu wa NEC Itikadi Uenezi na Mafunzo wa CCM ameendelea na ziara ya kikazi Mkoani mwanza.

Leo mkutano wa hadhara utafanyiak viwanja vya furahisha mwanza.

MWENEZI CCM TAIFA APOKELEWA WILAYA YA MAGU - MWANZAZIARA YA KIKAZI INAANZA MKOA WA MWANZA
10/03/2026

MWENEZI CCM TAIFA APOKELEWA WILAYA YA MAGU - MWANZA

ZIARA YA KIKAZI INAANZA MKOA WA MWANZA

09/03/2026

BARIADI - SIMIYU

Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Kenan Kihongosi ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi kuhakikisha wafanyabiashara waliokuwa wakifanya biashara katika eneo la Soko Kuu la Bariadi wanapewa kipaumbele mara baada ya kukamilika kwa ujenzi wa soko hilo.

Kihongosi ametoa maelekezo hayo leo Machi 9, 2026 alipokagua ujenzi wa soko hilo linalojengwa eneo la Sima Wilayani Bariadi Mkoa wa Simiyu.

Katika ziara hiyo, amemuagiza pia mkandarasi kuongeza kasi ya ujenzi na kuhakikisha mradi unakamilika ndani ya muda wa mkataba ifikapo Februari 3, 2027.

Kwa mujibu wa taarifa ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, ujenzi wa soko hilo unaogharimu zaidi ya Sh bilioni 26.5 umefikia asilimia 25 na unahusisha pia ujenzi wa barabara za lami zenye urefu wa kilomita 8.6 pamoja na majengo ya ofisi.

Soko hilo litakapokamilika litakuwa na maduka 251, vizimba 592, vizimba vya samaki 64 pamoja na maeneo ya mama lishe na baba lishe, maegesho ya magari na miundombinu mingine ya kisasa kwa ajili ya kuboresha shughuli za biashara wilayani humo.

TAARIFA MUHIMUKumekuwa na taarifa kwamba kuna mtu au watu wanatumia namba 0651 451 946 yenye usajili wa Goodluck Richard...
08/03/2026

TAARIFA MUHIMU

Kumekuwa na taarifa kwamba kuna mtu au watu wanatumia namba 0651 451 946 yenye usajili wa Goodluck Richard Kazeze kujitambulisha kwa majina au nafasi ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM.

Tunapenda kuufahamisha umma kuwa namba hiyo inatumiwa na watu wasio sahihi kwa malengo ya utapeli. Mtu yeyote anayepokea simu au ujumbe kutoka namba hiyo akidai kuwa kiongozi au kuomba fedha anapaswa kutambua kuwa hivyo ni vitendo vya Utapeli na kuwa makini.

Naomba wananchi na wanachama wote wasitoe fedha wala kufanya makubaliano yoyote kupitia namba hiyo, na badala yake wathibitishe taarifa kupitia njia rasmi za mawasiliano.

Tafadhali puuzeni na toa taarifa kwa mamlaka husika endapo mtapokea mawasiliano ya aina hiyo.

Asante kwa Ushirikiano. Kidumu Chama Cha Mapinduzi.

08/03/2026

KENAN ATOA ONYO KALI KWA VIONGOZI WANAOTUMIA VIBAYA MADARAKA

Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Kenan Kihongosi, ametoa onyo kali kwa baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali wanaotumia vibaya madaraka yao kwa kuwanyanyasa na kuwadhulumu wananchi wa hali ya chini.

Kihongosi alitoa onyo hilo wakati wa mwendelezo wa ziara yake ya uimarishaji wa Chama katika Mkoa wa Simiyu, ambapo leo ni siku ya pili ya ziara hiyo baada ya kumalizika kwa ziara ya Mkoa wa Shinyanga.

Katika ziara hiyo pia alisikiliza kero za wananchi na kutoa maelekezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Itilima kufuatilia na kushughulikia haraka malalamiko ya mwananchi aliyedai kudhulumiwa ardhi yake, licha ya kushinda kesi mahak**ani.

Amesisitiza kuwa viongozi wanapaswa kutumia madaraka waliyopewa kuwatumikia wananchi kwa haki na uadilifu badala ya kuwanyanyasa au kuwadhulumu.

CCM: UHAI WA CHAMA NI WANACHAMA WAKEItilima: Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema uhai wa chama cha siasa unategemea wingi...
08/03/2026

CCM: UHAI WA CHAMA NI WANACHAMA WAKE

Itilima: Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema uhai wa chama cha siasa unategemea wingi wa wanachama wake.

Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Kenani Kihongosi ameeleza hayo leo Machi 8,2026 alipotembelea na kuhudhuria kikao cha Shina namba moja Tawi la Nkoma B Kata ya Nkoma wilayani Itilima mkoani Simiyu.

Lengo likiwa ni kukagua uhai wa chama, akieleza kuwa uhai wa CCM upo katika mashina yake. Wakati Kihongosi akisikiliza ajenda za kikao hiko walieleza kuwa kuna wanachama ambao wataka kujiunga na chama lakini bado hawajajiandikisha.

Kihongosi alisema shina hilo ni la mfano akieleza kuwa wanachama hao wapya wapokelewa haraka iwezekanavyo kwani uhai wa chama ni wanachama wake.

“Katika taarifa mmesema kuna wanachama wapya mnataka kuwapokea, jambo hilo kuna mjumbe amesema hapa kwamba wapokelewe na sisi tunasema mwapokee kwa sababu hai wa chama na wanachama wake,” amesema kihongosi.

Ameongeza: “Kwa hiyo k**a kuna wanachama wanataka kujiunga na chama chama mapinduzi tunawakaribisha kwa mikono miwili chama chama mapinduzi kinaendelea kufanya usajili na kinaendelea kuchukua makombe ya ushindi kila wakati”.

08/03/2026

Leo tunaadhimisha Siku ya Wanawake Duniani – siku ya kutambua nguvu, mchango na uongozi wa mwanamke katika kujenga familia, jamii na Taifa.

Chama Cha Mapinduzi kinaamini kuwa mwanamke ni nguzo muhimu ya maendeleo ya Tanzania. Tunawaalika wanawake wote pamoja na wananchi kwa ujumla kuendelea kushirikiana, kuungana na kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa Taifa letu.

Tunasimama pamoja kuhamasisha usawa, fursa na uwezeshaji wa wanawake katika kila sekta ya maisha. Mwanamke akisimama imara, Taifa nalo linasimama imara.

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema maendeleo ya kweli yanahitaji vitendo na imedhihirisha hivyo kupitia utekelezaji wa y...
05/03/2026

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema maendeleo ya kweli yanahitaji vitendo na imedhihirisha hivyo kupitia utekelezaji wa yale yote waliyoyaeleza katika Ilani ya uchaguzi 2025/30.

Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi an Mafunzo wa CCM Taifa, Kenani Kihongozi ameeleza hayo leo Machi 5,2026 alipotembelea mradi wa kufua umeme wa jua (REA) katika kijiji cha Kayenze Kata Ya Ukune Halmashauri ya Ushetu, Wilaya ya Kahama,Mkoani Shinyanga.

Imeelezwa kuwa mradi huo umekamilika ndani ya kipindi cha mwaka mmoja na umegharimu kiasi cha Sh bilioni 11.6 na unachangia megawati tano katika gridi ya taifa, na unahusisha ushirikiano katika ya serikali na mwekezaji ambaye ni kampuni ya kichina.

Akizungumza baada ya kutembelea mradi huo Kihongosi amesema CCM k**a ilivyoahidi kwenye ilani maendeleo yaliyosemwa yatafika katika kila maeneo yaliyokusudiwa akieleza kuwa miaka mitano hadi 10 iliyopita umeme haukuwepo kwenye vijiji lakini leo kila kijiji kina umeme.

“Leo hapa tumepata taarifa kwamba vijiji na vitongoji 136 wakandarasi wapo saiti vimebaki vijiji k**a 100 na kidogo ambavyo kabla ya mwaka 2030 au 2029 serikali za mitaa maana yake vitongoji vyote vitawaka umeme, wasije watu wakawaambia hakuna kilichofanyika,” amesema Kihongosi.

Ameongeza kuwa yaliyofanyika yapo na yanaonekana, hivyo wananchi wasipotoshwe kuambiwa hakuna kilichofanyika akisisitiza katika maendeleo ya kweli hayahitaji propaganda bali vitendo.

“Kwenye kujenga uchumi au maisha au mafanikio hatuhitaji maneno tunahitaji vitendo na ndo k**a hizi sola zipo hapaa, zahanati inajengwa itakabidhiwa muda si mrefu, kuanza matumizi ya nishati safi na mengineyo,” amesisitiza Kihongosi.

Akitoa taarifa Mkandarasi wa Mradi huo, Adrian Simaimoto amesema mradi huo umeanza kujengwa Septemba 2024 na kukamilika Agosti 2025 na unajengwa na kampuni ya kichina.

Address

Ubungo Kibangu
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bongo Daily posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share