Bongo Fasta

Bongo Fasta Ukurasa rasmi wa chaneli ya YouTube iitwayo Bongo Fasta.

14/09/2025

Anguko la Justin Bieber Linalowaliza Wengi

13/09/2025

Kila Mtu alidhani Huyu ni SHUGA DADI" Wake, walipojua ukweli kila mtu alishanga

12/09/2025

Ulishawahi kusikia kuhusu 50 Cent kununua Jumba la kifahari la Mike Tyson?

Hebu Funguka
13/09/2024

Hebu Funguka

13/09/2024

Leo siku ya tarehe 13 september ni kumbukumbu ya kifo cha mwanamuziki wa kufoka foka kutoka nchini marekani, tupac shakur,kilichotokea mwaka 1996 baada ya nyota huyo kushambuliwa kwa risasi akiwa kwenye gari na bosi wake.

Tukio la kushambuliwa kwa tupac, lilitokea mnamo tarehe 7 september 1996 huko jijini las vegas nchini marekani, wakati tupac akiwa ndani ya gari nyeusi aina ya BMW, yeye na boss wake suge knights. Wawili hao walikuwa wametoka kwenye pambano la ngumi la mike Tyson lililofanyika katika ukumbi wa MGM Grand.

Wakiwa katika mataa, gari nyeupe aina ya Cadillac ilisimama pembeni yao, upande ambao tupac alikuwa amekaa katika siti ya abiria, ghafla mtu kutoka kwenye gari hiyo alianza kufyatua risasi, ambazo zilimpata Tupac sehemu kadhaa za mwili.

Tupac alipelekwa hospitali ambako madaktari walijaribu kuokoa uhai wake kwa siku sita. Lakini hatimae siku ya tarehe 13 september 1996, tupac alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 25 tu.

Kifo cha tupac kiliacha maswali mengi na nadharia za mbalimbali huku baadhi wakidai nyota huyo hakufa, bali alighushi kifo chake, na ya kwamba yuko hai mafichoni na siku moja atarudi, lakini mpaka leo, miaka 28 imepita Tupac hajawahi kurudi, lakini jina na kazi zake, bado zinaishi.

12/09/2024

Usifanye mchezo na Mbwa wa vikosi vya usalama.

Hebu tuambie kidogo 😂😂😂😂
12/09/2024

Hebu tuambie kidogo 😂😂😂😂

Siku k**a ya leo miaka 32 iliyopita, Mae C. Jameson, aliweka rekodi ya kuwa mwanamke wa kwanza mwenye asili ya Africa kw...
12/09/2024

Siku k**a ya leo miaka 32 iliyopita, Mae C. Jameson, aliweka rekodi ya kuwa mwanamke wa kwanza mwenye asili ya Africa kwenda angani (Space).

Mae Jameson alizaliwa tarehe 17 october mwaka 1956 Alabama nchini Marekani. Tangu akiwa mtoto mdogo alitamani sana kuwa mwanasayansi.

Anaeleza kuwa tamanio lake la kwenda angani, lilizaliwa baada ya kutazama filamu za Star Trek hasa baada ya kumuona muigizaji Uhura, ambae alikuwa mwanamke mwenye asili ya afrika, akiigiza filamu inayohusu safari za angani.

Mwaka 1992 Mae alikaa angani kwa siku 8, huku akifanya tafiti mbalimbali, na hiyo kumfanya kuwa mwanamke wa kwanza mweusi, kufanya safari ya angani.

Mwanamke huyu kwa sasa ana umri wa miaka 67 na anauwezo wa kuongea lugha kadhaa ikiwemo kiswahili

11/09/2024

Habari, Karibu katika ukurasa rasmi wa Bongo Fasta. Hapa utajifunza kuhusu mambo mengi yanayoshangaza na kuzua gumzo ulimwenguni. usisite kuwasiliana nasi kwa njia tulizoainisha katika wasifu wa ukurasa huu.

Sasa Twende kazi

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bongo Fasta posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share