03/06/2026
Ni rasmi sasa Sir Idris Elba! Jumanne tarehe 2 Juni 2026, King Charles III alimvisha heshima ya kifalme mwigizaji, mwanaharakati na mwanamuziki Idris Elba katika hafla ya investiture iliyofanyika Windsor Castle, kwa kutambua huduma zake kwa vijana, heshima iliyotangazwa awali kwenye Orodha ya Heshima za Mwaka Mpya 2026.
Elba, 53, mzaliwa wa Hackney kwa baba Msierraleone na mama Mghana, alianza safari yake baada ya kupata £1,500 kutoka Prince’s Trust akiwa na miaka 18, fedha iliyompeleka National Youth Music Theatre; leo ni balozi wa The King’s Trust.
Pamoja na mkewe Sabrina, mwaka 2022 walianzisha Elba Hope Foundation, wakijikita kwenye elimu, ajira za vijana na maendeleo endelevu. Wawili hao wamesaidia kukusanya zaidi ya $1.75 bilioni dhidi ya umaskini vijijini, $2 milioni kwa mfuko wa COVID-19, na $6 milioni za unafuu wa deni kwa Somalia.
IkFied.com