sallytv

sallytv Your go-to source for Breaking news, in-depth analysis, & Exclusive interviews, Sports, Business, Politics, and Entertainment.
📧:[email protected]

  Takribani wahamiaji 68 wamefariki dunia baada ya boti iliyokuwa imebeba takriban watu 150 kuzama katika pwani ya Yemen...
04/08/2025

Takribani wahamiaji 68 wamefariki dunia baada ya boti iliyokuwa imebeba takriban watu 150 kuzama katika pwani ya Yemen kufuatia hali mbaya ya hewa siku ya jana Jumapili, Agosti 3, 2025.

Chombo hicho kilizama katika jimbo la kusini mwa Yemen la Abyan, na miili 68 imepatikana, huku watu 12 wakiokolewa wakati wengine 74 wakiwa bado hawajapatikana.

Wengi wa waathiiriwa wanaaminika kuwa raia wa Ethiopiakwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji nchini Yemen (IOM), ambalo limelitaja tukio hilo kuwa la kuhuzunisha.

Yemen inasalia kuwa njia kuu ya wahamiaji kutoka Pembe ya Afrika wanaosafiri kwenda mataifa ya Ghuba ya Kiarabu kutafuta kazi, huku IOM ikikadiria kuwa mamia wamekufa au kupotea katika ajali k**a hizo katika miezi ya hivi karibuni.

Yemen ni nchi maarufu ambapo wahamiaji wengi waliokata tamaa wanaoelekea kaskazini mwa Saudi Arabia hupita ili kwenda kutafuta fursa bora zaidi za maisha.

  Mpenzi wa zamani wa rapa na mfanyabiashara Sean "Diddy" Combs, Gina Huynh, ambaye ametajwa k**a Mhusika Namba 3 katika...
04/08/2025

Mpenzi wa zamani wa rapa na mfanyabiashara Sean "Diddy" Combs, Gina Huynh, ambaye ametajwa k**a Mhusika Namba 3 katika kesi ya shirikisho inayomkabili Diddy, ameandika barua maalum kwa jaji akiunga mkono ombi la Diddy kupewa dhamana ili asubiri hukumu akiwa nje ya gereza.

Kwa mujibu wa nyaraka mpya za kisheria zilizopatikana na TMZ, Gina anasema amemfahamu Diddy kwa muda mrefu na anamchukulia k**a mtu wa familia, mfano wa baba na mfanyabiashara mwenye maono – si mhalifu k**a anavyodaiwa.

Katika barua hiyo, Gina anakumbuka changamoto na mafanikio ya uhusiano wao wa awali, lakini anasisitiza kuwa kila mara Diddy alipofanya makosa, alikuwa tayari kukiri na alijitahidi kubadilika na kufanya maamuzi bora zaidi baadaye.

Anaeleza kuwa kufikia mwisho wa uhusiano wao, Diddy alikuwa amebadilika na kuwa mtu mwenye upendo, uvumilivu na upole – tabia ambazo zilitofautiana kabisa na mwenendo wake wa awali.

Barua hiyo ni sehemu ya juhudi za timu ya Diddy kushawishi mahak**a kumruhusu kusubiri kesi akiwa nje kwa dhamana.

  Baada ya msimu wa kiwango cha juu akiwa na Pyramids FC, mshambuliaji Fiston Mayele   DR Congo jana ametwaa rasmi Tuzo ...
04/08/2025

Baada ya msimu wa kiwango cha juu akiwa na Pyramids FC, mshambuliaji Fiston Mayele DR Congo jana ametwaa rasmi Tuzo ya Mchezaji Bora wa Msimu wa Ligi kuu ya Misri, Mayele alicheza michezo 23 na kufunga Mabao 8 akisaidia kutungeneza magoli 2.

Fiston aling’ara akiwa na AS Vita Club ya DRC miaka kadhaa badaye akatua Tanzania na kung’aa kwa kiwango cha juu akiwa na Yanga SC, ambako alishinda mataji ya ndani na kufika fainali ya Kombe la Shirikisho CAF 2023.

Msimu wa 2023/24 alijiunga na Pyramids FC ya Misri na kuendelea kuwa tishio langoni akifunga mabao muhimu 6 kwenye michezo 10 na kusaidia timu kutwaa ubingwa.

Mayele si tu mfungaji, bali ni kiongozi, mpambanaji na nembo ya mafanikio ya wachezaji bora wa Afrika.

  Mchezaji mkongwe wa Simba SC, Mzamiru Yassin, amefichua kuwa ana mpango wa kuanza kusomea ukocha wakati akiendelea kui...
04/08/2025

Mchezaji mkongwe wa Simba SC, Mzamiru Yassin, amefichua kuwa ana mpango wa kuanza kusomea ukocha wakati akiendelea kuitumikia klabu hiyo kubwa nchini.

Mzamiru ambaye amekuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Simba kwa miaka kadhaa, amesema kuwa huu ni wakati sahihi wa kuanza kujiandaa kwa maisha ya baada ya soka, huku akitumia uzoefu wake mkubwa uwanjani k**a msingi wa mafanikio ya baadaye akiwa k**a kocha.

“Nina malengo ya kujiandaa mapema. Mpira ni maisha mafupi, hivyo ni muhimu kuweka msingi wa baadae,” alisema Mzamiru kwa ufupi.

Taarifa hizi zimepokelewa kwa mtazamo chanya na mashabiki wa Simba, wengi wakiona ni hatua nzuri kwa mchezaji huyo ambaye amekuwa mfano wa nidhamu na kujituma ndani ya uwanja.

Endapo atafanikiwa kufanikisha ndoto yake hiyo, Mzamiru anaweza kuwa miongoni mwa wachezaji wachache wa kizazi chake wanaoingia kwenye fani ya ukocha wakiwa bado wanacheza, jambo linaloonyesha ukomavu na maono ya mbali.

____✍️ "Dickson Mashulano"

  Kuongea wakati wa kuangalia movie ni tabia inayokera na kuvunja utaratibu wa kawaida wa kijamii. Watu wengi huona hili...
04/08/2025

Kuongea wakati wa kuangalia movie ni tabia inayokera na kuvunja utaratibu wa kawaida wa kijamii. Watu wengi huona hili k**a kukosa adabu, kwa sababu sinema ni uzoefu wa pamoja unaohitaji utulivu na heshima kwa wengine.

Utafiti mmoja uliochapishwa kwenye Psychological Science unaonesha kuwa watu wanaokiuka kanuni za kijamii huonekana kuwa si waadilifu, hawaaminiki, na hawajali wengine. Ingawa utafiti huo haukuzungumzia sinema moja kwa moja, unasaidia kuelewa kwa nini mtu anayepiga kelele au kuongea hovyo wakati wa movie huonekana k**a mbinafsi au mwenye tabia za kujikweza.

Kwa upande mwingine, wataalamu wa afya ya akili wanasema kuwa mara nyingine tabia ya kuongea hovyo katika mazingira yanayohitaji utulivu—k**a sinema—inaweza kuwa ishara ya matatizo fulani ya kisaikolojia k**a vile ukosefu wa uwezo wa kujizuia (impulsivity), matatizo ya umakini (k**a ADHD), au kutotambua mipaka ya kijamii, jambo linaloweza kuhusiana na hali k**a autism au matatizo ya tabia.

Kwa hiyo, wakati mwingine si tu kukera, bali inaweza kuwa kiashiria cha mtu anayehitaji msaada wa kitaalamu wa afya ya akili.

  Msanii wa Bongo Fleva   ameweka wazi kuwa kwasasa yeye ndio msanii namba moja Tanzania kwasasa na hii ni kwa mujibu wa...
03/08/2025

Msanii wa Bongo Fleva ameweka wazi kuwa kwasasa yeye ndio msanii namba moja Tanzania kwasasa na hii ni kwa mujibu wa namba anazopata kwenye sehemu za kusikilizia muziki pamoja na nyimbo zake zinavyovuma mitaani

ameeleza hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram huku akisema kuwa anayebisha ajitokeze.

⬇️Fungua comment kuona zaidi. (📸:Mbosso IG)

  Mchezo wa Kundi B uliowakutanisha Madagascar na Mauritania umehitimishwa kwa sare ya bila kufungana (0-0), matokeo amb...
03/08/2025

Mchezo wa Kundi B uliowakutanisha Madagascar na Mauritania umehitimishwa kwa sare ya bila kufungana (0-0), matokeo ambayo yamezifanya timu zote mbili kugawana pointi moja kila moja.

Matokeo haya yanaendelea kuwanufaisha Tanzania, ambayo inaendelea kusalia kileleni mwa kundi hilo ikiwa na alama 3, kufuatia ushindi wao wa 2-0 dhidi ya Burkina Faso hapo jana.

FT: Madagascar 0-0 Mauritania

  Mtoto wa kiume aitwaye Thaddeus Daniel Pierce amezaliwa huko Ohio tarehe 26 Julai, 2025, akiwa mtoto anayejulikana kuw...
03/08/2025

Mtoto wa kiume aitwaye Thaddeus Daniel Pierce amezaliwa huko Ohio tarehe 26 Julai, 2025, akiwa mtoto anayejulikana kuwa amezaliwa kutoka kwa kiinitete kilichohifadhiwa kwa muda mrefu zaidi kuwahi kurekodiwa—takriban miaka 31.

Kiinitete hicho kiligandishwa mwezi Mei mwaka 1994 na kiliwekwa kwenye hifadhi hadi Lindsey na Tim Pierce walipokichukua kwa njia ya uasili wa kiinitete, baada ya kupitia changamoto za kupata mtoto kwa kipindi cha miaka saba. Awali, kiinitete hicho kiliumbwa na Linda Archerd, ambaye aliamua kuchangia viinitete visivyotumika baada ya kupata mtoto mmoja kupitia njia ya IVF (In Vitro Fertilization).

Kisa hiki kinaonyesha mafanikio ya teknolojia ya kugandisha viinitete kwa muda mrefu, pamoja na ongezeko la matumizi ya uasili wa kiinitete k**a njia mbadala ya kupata watoto kwa familia zinazokumbwa na ugumba.

  Klabu ya Yanga imekamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji Mohamed Doumbia (26), anayejulikana kwa jina la utani “Midf...
03/08/2025

Klabu ya Yanga imekamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji Mohamed Doumbia (26), anayejulikana kwa jina la utani “Midfield Pimper” kutokana na uwezo wake mkubwa wa kucheza katika maeneo finyu, kupiga mashuti ya mbali kwa usahihi, na akili ya kutengeneza nafasi kwa wachezaji wenzake.

Doumbia, ambaye anaweza kucheza k**a kiungo wa kati namba 8 na pia k**a kiungo mshambuliaji namba 10, amejiunga na Yanga akitokea FC Slovan Liberec ya Jamhuri ya Czech. Huu ni usajili uliokuwa ukihusishwa na Yanga tangu mwezi Mei, na sasa umekamilika rasmi.

Miongoni mwa wachezaji wapya waliojiunga na kikosi cha Yanga msimu huu ni pamoja na Balla Conte, Kouma, Ecua, Zimbwe, Chikola na Boyeli. Hata hivyo, kwa mtazamo binafsi, Doumbia anaonekana kuwa usajili bora zaidi kutokana na mchanganyiko wa kasi, nguvu na akili anayoionyesha uwanjani.

Katika soka la kisasa, kiungo mwenye uwezo wa kupiga mashuti ya mbali kwa usahihi ni hazina adimu, na Doumbia anaonekana kuwa mmoja wao – jamaa anapiga sana "screamers"! Bila shaka, makipa wa Ligi Kuu Tanzania Bara (NBC Premier League) wataanza kuwa makini na jina lake.

Balaa jingine rasmi limetua Jangwani.

  Rapa maarufu Soulja Boy amek**atwa na polisi mjini Los Angeles baada ya kusimamishwa kwenye ukaguzi wa kawaida wa bara...
03/08/2025

Rapa maarufu Soulja Boy amek**atwa na polisi mjini Los Angeles baada ya kusimamishwa kwenye ukaguzi wa kawaida wa barabarani.

Taarifa zinaeleza kuwa msanii huyo alikuwa abiria ndani ya gari lililosimamishwa, na alik**atwa kwa tuhuma za kuwa mhalifu anayemiliki silaha ya moto kinyume cha sheria.

📺:TmZ, 📸: Getty Images

  Timu ya Taifa ya Morocco imefanikiwa kuondoka na alama zote tatu baada ya kuwashushia Angola kichapo cha magoli 2-0 na...
03/08/2025

Timu ya Taifa ya Morocco imefanikiwa kuondoka na alama zote tatu baada ya kuwashushia Angola kichapo cha magoli 2-0 na kuishusha timu ya Taifa ya Kenya kileleni mwa Kundi A.

FT: Morocco 2-0 Angola
29’ Riahi I.
81’ Quinito (OG)

MSIMAMO WA KUNDI A:
1. Morocco 3 Pts
2. Kenya 3 Pts
3. Zambia 0 Pts
4. DR Congo 0 Pts
5. Angola 0 Pts

  Niseme kwa ujumla hii ni famila yetu, ni familia imara sana sio família dhaifu, familia hii imekuwa na mafanikio maku...
03/08/2025

Niseme kwa ujumla hii ni famila yetu, ni familia imara sana sio família dhaifu, familia hii imekuwa na mafanikio makubwa kwa mikaa minne iliyopita na tunashukuru kwa kila mafankio.

Lakini niwambie tu hii imeishabaki kuwa
historia, sasa ni msimu mpya na wote tunazianza mbio kwenye mstari mmoja, idadi ya magoli tuliyofunga, idadi ya
suruhu na idada ya magoli tuliyofungwa yote yamepita sasa tunaenda kuikabli changamoto mpya.

Yote haya yamesemwa na Rais wa Yanga Eng Hersi Said leo katika senina ya utamvulisho kwa wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wa klabu hiyo.

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when sallytv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share