sallytv

sallytv Your go-to source for Breaking news, in-depth analysis, & Exclusive interviews, Sports, Business, Politics, and Entertainment.
📧:[email protected]

04/10/2025

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limesema kuwa kumekuwepo na ongezeko la watu wanaotumia mitandao ya kijamii kuchapisha maudhui yanayochochea kuliingiza jeshi hilo katika mambo ya kisiasa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Kanali Bernard Masala Mlunga baadhi ya hoja hizo zinatolewa na watu waliopo katika mazingira ya kijeshi, wengine wakijinasibisha na JWTZ bila uhalali, na baadhi yao ni wale walioachishwa jeshi kutokana na tabia na mwenendo usiofaa au kujihusisha na siasa na uanaharakati.

JWTZ limeeleza kuwa linaendelea kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uaminifu, utii na uhodari, likizingatia kiapo chake.

04/10/2025

Meneja wa Simba Dimitar Pantev akiwasili Uwanja wa ndege wa kimataifa Mwalimu Julias Nyerere jijini Dar es Salaam tayari kwa kukamilisha taratibu za kusaini mkataba na uongozi wa klabu hiyo, sambamba na kujiunga benchi la ufundi na wachezaji.

📺:Mwanaspoti

  Scout wa Simba SC, Mels Daalder amejiuzulu nafasi yake ndani ya klabu hiyo, Mels Daalder amejiuzulu kwasababu haioni n...
04/10/2025

Scout wa Simba SC, Mels Daalder amejiuzulu nafasi yake ndani ya klabu hiyo, Mels Daalder amejiuzulu kwasababu haioni nafasi yake ndani ya Simba Sports Club kwa namna yoyote ile.

Mels amefanya maamuzi hayo kwasababu mambo mengi ya eneo lake yanafanyika bila yeye kushirikishwa na kupelekeshwa kufanya vitu anavyoona si sahihi.

04/10/2025

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza jumla ya kilogramu 4,402.02 za dawa za kulevya katika Kiwanda cha Saruji cha Twiga, kilichopo Wazo, jijini Dar es Salaam.

Dawa zilizoteketezwa ni pamoja na kilogramu 2,168.18 za methamphetamine, kilogramu 1,064.29 za he**in, gramu 326.95 za co***ne, kilogramu 515.48 za bangi na kilogramu 653.74 za mirungi.

Dawa hizo zilihifadhiwa k**a vielelezo vya mashauri mbalimbali yaliyopo mahak**ani, ambapo baadhi ya mashauri bado yanaendelea kusikilizwa huku mengine yakiwa tayari yametolewa hukumu.

Credit: Global TV

  Star wa muziki kutoka Nchini   ameendelea kuandika historia kimataifa baada ya kutajwa na jarida maarufu la muziki Bil...
04/10/2025

Star wa muziki kutoka Nchini ameendelea kuandika historia kimataifa baada ya kutajwa na jarida maarufu la muziki Billboard kwenye orodha ya “September Reggae/Dancehall Fresh Picks of the Month”.

Billboard imeorodhesha nyimbo 10 mpya za reggae, dancehall na soca zinazotakiwa kusikilizwa, zikijumuisha majina makubwa k**a Prince Swanny, Skillibeng & Vybz Kartel, Chronic Law, pamoja na Zuchu.

Zuchu ametajwa kupitia wimbo wake “Amanda (Remix)” aliomshirikisha rapa maarufu wa jamaica , hatua inayompa nafasi kubwa zaidi ya kuonekana kwenye ramani ya muziki duniani.

Powered by Magari ARENA

  📉 Netflix yapoteza thamani ya zaidi ya $20 Bilioni baada ya Elon Musk kuanzisha kampeni kali kwenye ukurasa wake wa X ...
04/10/2025

📉 Netflix yapoteza thamani ya zaidi ya $20 Bilioni baada ya Elon Musk kuanzisha kampeni kali kwenye ukurasa wake wa X (zamani Twitter) akihimiza wazazi kufuta usajili wa Netflix kwa ajili ya “afya ya watoto wao”.

Musk aliandika ujumbe wenye maneno: “Cancel Netflix for the health of your kids”, huku akishiriki picha inayoonesha Netflix ikihusishwa na ajenda ya “Transgender Woke Agenda”.

Baada ya kauli hiyo, mjadala mkubwa umeibuka mitandaoni kuhusu ushawishi wa Elon Musk na nafasi ya Netflix katika mijadala ya kijamii.

Powered by Magari ARENA/ 📸:Getty Images

  Mabosi wa Simba wamemalizana na kocha Dimitar Pantev (49) na muda wowote leo atatua jijini Dar es Salaam kuanza kukino...
04/10/2025

Mabosi wa Simba wamemalizana na kocha Dimitar Pantev (49) na muda wowote leo atatua jijini Dar es Salaam kuanza kukinoa kikosi ambacho kitarejea mazoezini Jumatatu.

Dimitar aliyekuwa kiungo enzi za uchezaji wake, alizaliwa Juni 26, 1976 kabla ya kustaafu kucheza, ni mmoja ya makocha waliochora tattoo nyingi mwilini mwake akipendelea kuvaa hereni katika masikio yote na alianza kazi ya ukocha kwa timu za vijana katika Jiji la Varna ambalo ni la tatu kwa ukubwa huko nyumbani Bulgria, wakati wa msimu wa 2008-09 alikuwa msaidizi wa Dobrudzha Dobrich.

Kocha huyo mwenye Leseni ya UEFA A, alifanya kazi k**a kocha mkuu wa Vladislav Varna na Shabla ya Bulgaria. Wakati wa miaka yake sita na klabu hiyo alitwaa mataji matano mfululizo ya Ligi Kuu ya Bulgarian Premiere Futsal. Agosti 31, 2015, Dimitar aliteuliwa kuwa kocha wa Spartak Varna, akiiongoza klabu hiyo kupanda hadi Ligi ya Tatu 2016.

Hakuishia hapo Julai 2022, Dimitar aliteuliwa kocha wa Victoria United huko Cameroon, alishinda Ligi ya Mkoa wa Kusini Magharibi.

Machi 21, 2024, Dimitar alirudi Victoria United, baadaye aliongoza Victoria kwa taji lao la kwanza la Elite One katika historia ya klabu ikitwaa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Cameroon.

Huku Januari 23, 2025, Dimitar aliteuliwa k**a kocha wa Gaborone United, akiiongoza timu hiyo kutwaa taji la Ligi Kuu ya Botswana katika msimu wa kwanza katika klabu hiyo.

Dimitar ana uzoefu na soka la Afrika, ni muumini wa kucheza soka la kushambulia na kuzuia huku akipenda kumiliki mchezo k**a ilivyo falsafa ya Simba.

✍️| "Dickson Mashulano"

Powered by Magari ARENA

  Muigizaji na mwimbaji wa R&B, Tyrese Gibson, anayejulikana kwa nyimbo zake za mapenzi na nafasi yake kwenye filamu za ...
04/10/2025

Muigizaji na mwimbaji wa R&B, Tyrese Gibson, anayejulikana kwa nyimbo zake za mapenzi na nafasi yake kwenye filamu za Fast & Furious, amejikuta mikononi mwa polisi wiki hii.

Kwa mujibu wa TMZ, Tyrese amek**atwa mapema.leo Ijumaa asubuhi jijini Atlanta akishutumiwa kwa kosa la ukatili wa wanyama" Cruelty to Animals" baada ya mbwa wake aina ya Cane Corso kumshambulia na kumuua mbwa wa jirani mwezi uliopita.

Taarifa kutoka kaunti ya Fulton zinaonyesha kuwa Tyrese alijisalimisha katika gereza la kaunti hiyo saa 11:59 alfajiri. Hata hivyo, aliachiwa huru muda mfupi baadaye baada ya kulipia dhamana ya dola 20,000 sawa na Tsh Milioni 54.

📺: TmZ/ 📸:Getty Images

04/10/2025

Wazee wa Kuzoom Mmeona Nini⁉️👀

  Mchezaji wa klabu ya Young Africans, Ibrahim Abdullah, amefungiwa kutocheza mechi tano (5) baada ya kosa la kumkanyaga...
04/10/2025

Mchezaji wa klabu ya Young Africans, Ibrahim Abdullah, amefungiwa kutocheza mechi tano (5) baada ya kosa la kumkanyaga kwa makusudi mchezaji wa Mbeya City, Ibrahim Ame, katika mchezo wa Ligi Kuu uliomalizika kwa sare ya bila kufungana (0-0) kati ya Mbeya City FC dhidi ya Young Africans SC.

Kitendo hicho kilitafsiriwa k**a rafu mbaya iliyoweza kuhatarisha usalama wa mchezaji aliyekanyagwa. Adhabu hiyo imetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 41:21 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji.

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when sallytv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share