Sisi Ni Habari

Sisi Ni Habari For all your favourite news

Kutana na  Fatuma Makongoro Itutu ambaye watanzania wengi humfahamu k**a BI MWENDANi Bibi wa wajukuu wanne na vitukuu sa...
27/10/2025

Kutana na Fatuma Makongoro Itutu ambaye watanzania wengi humfahamu k**a BI MWENDA

Ni Bibi wa wajukuu wanne na vitukuu saba ambaye anatoka kwenye familia ya machifu huko Mkoani Mara ambaye akiwa darasa la nne alihamishwa na kuendelea na masomo yake shule ya msingi Kinondoni Mkoani Dar es salaam.

Mwaka 1998 ndipo alipoingia rasmi kwenye tasnia ya filamu na kuanzia kuigiza rasmi na jina la Bi Mwenda alipewa kwenye moja ya filamu alizoigiza na kundi la sanaa la Kaole akiigiza k**a mwanamke mchawi aliyekuwa akimloga mke Mwenzake.

Na baada ya jina hilo la Bi Mwenda kuwa maarufu mpaka Leo limekuwa ndilo jina lake maarufu na watanzania walio wengi wamekuwa wakimchukulia k**a mama wa Ubwaya Ubwela yaani mchawi na mwanamke mwenye roho mbaya lakini katika maisha ya kawaida ni mwanamke wa kawaida asiye mchawi wala kuwa na roho mbaya.

Hata hivyo kupitia simulizi yake ambayo Bi Mwenda ameitoa katika kipindi cha Alama kinachorushwa na Sinema zetu ya Azam tv anasema aliwahi kuvamiwa na kupigwa na wanawake wawili katika maeneo ya Ilala Bungoni na baadaye Kariakoo akituhumiwa kuwa mchawi na mtu mwenye roho mbaya Kutokana na watu hao kumuona kwenye tv akiloga 🤣🤣

Bi Mwenda anaendelea kusema kuwa hata waigizaji wa mikoani wakiandaa script za filamu zao kwenye sehemu ya mama mchawi huwa wanamtafuta yeye ili akaigize kwenye nafasi hiyo😄

Dr. Nandipha : Ndege Mjanja hunaswa na tundu bovu-3Nandipha alikuwa kwenye penzi zito na Thabo Bester. Historia ya Thabo...
27/10/2025

Dr. Nandipha : Ndege Mjanja hunaswa na tundu bovu-3

Nandipha alikuwa kwenye penzi zito na Thabo Bester. Historia ya Thabo Bester haiko wazi sana. Ambacho kiko wazi ni kwamba Bester alikuwa binadamu. Alizaliwa na mwanamke. Mama yake anaitwa Maria Mabaso. Alizaliwa huko Soweto. Mama yake hakuwa na maisha mazuri alikuwa anafanya vibarua vya kulima. Bester hakuwa na hata cheti cha kuzaliwa. Makuzi yake hayako wazi sana. Lakini mara kadhaa Bester alikumbwa na shutuma za ulaghai na udanganyifu katika umri mdogo. Bester alikuwa tapeli. Akiwa na miaka 19 Bester alifungwa miaka miwili gerezani kutokana na makosa ya ulaghai.

Ukweli ni kwamba, malezi ya Nandipha na Bester yalikuwa ardhi na mbingu. Wakati mwingine watoto waliolelewa vizuri k**a Nandipha huwa wanakosa kuzijua kanuni za kitaa. Hawa ni rahisi kudanganyika kwa sababu wanafikiri kwamba duniani watu wote ni wema k**a walivyokuwa wazazi wao. Mitaa ina kanuni zake. Kanuni zake hazifundishwi chuo Kikuu. Nandipha hakuyajua haya.

Bester kwake mtaa ndio ulikuwa nyumbani kwake. Yeye toka anazaliwa alijua aishi namna gani aweze kusurvive mtaani. Bester alikuwa anajifanya wakala na anawasaidia wanawake ambao walikuwa wana ndoto ya kufanya kazi ya urembo kutimiza ndoto zao. Bester alikuwa anawaaminisha kwamba yeye alikuwa anazijua njia za kuwafanya wafike wanapotaka kufika. Wanawake walimwamini. Kila walipokuwa wanakutana nae, Bester aliwabaka na kisha kuwaibia simu la laptop na kuwatishia kisu.

Bester hakuishikia kuwabaka tu, mwaka 2011 Bester alimuua kikatili aliyekuwa mpenzi wake Nomfundo Tyhulu. Nomfundo alikuwa bado mdogo sana. Wakati anafariki alikuwa na umri wa miaka 27.

Nomfundo na Bester walikuwa wamejuana miezi 8 tu. Walikuwa hawaishi pamoja. Nomfundo alikuwa anaishi Johannesburg wakati Bester Durban. Siku moja Nomfundo akampigia simu Bester, akamwambia amepata ajira mpya. Bester akamdanganya kwamba anataka apige picha. Wakaenda Capetown. Hiyo ilikuwa tarehe 19 September 2011. Wakafikia hotel inaitwa One&Only. Hii ni hotel ya Nyota 5 ambayo gharama ya chumba si chini ya Shilingi Milioni 1.5. Wakaa hapo siku 2.

Siku ya tatu wakahamia hotel nyingine. Nomfundo akagundua kwamba..!

Itaendelea... Ijumaa !

Dr. Nandipha : Ndege Mjanja hunaswa na tundu bovu-4

Siku ya tatu wakahamia hotel nyingine. Nomfundo akagundua kwamba kumbe Bester bado alikuwa na mahusiano na mpenzi wake wa zamani. Tena walikuwa wanapasha kiporo k**a kawaida. Hii ilimuumiza Nomfundo ambaye alikuwa ana amini Bester ni wake tu. Siku nzima walikuwa wanazozana. Baada ya kuzozama wakaenda kulala. Hiyo ilikuwa ni tarehe 21 September mwaka 2011.

Tarehe 22 September 2011.
Saa 8 usiku Nomfundo anashtuka usingizini. Anakuta Bester akiwa amesima huku amemnyooshea kisu. “Lete simu na lap yako hapo”. Bester anaamrisha. Maskini wakati Nomfundo hajajua afanye nini, Bester anashusha kisu na kumdunga Nomfundo kifuani. Nomfundo anapapatika huku damu zikiruka mithili ya kuku wa Krismasi. Bester akamfunga Nomfundo mikono nyuma kwa kutumia t-shirt, kisha akamwamuru atoe password ya laptop. Masaa matano baadae Bester akaondoka na kumwacha. Bester akamwambia mhudumu wa guest kwamba, Nomfundo alikuwa amelala, asimsumbue labda atamwamsha kuanzia saa 8 mchana. Kumbe Nomfundo alikuwa tayari amekufa.

Ilipofika saa 3 usiku wahudumu wakaenda kumgongea Nomfundo. Maskini Nomfundo wa watu alikuwa amekufa tayari. Damu zilikuwa zimetapakaa karibu chumba kizima.

Ilikuwa ngumu kumk**ata Bester. Kwa sababu Facebook alikuwa na zaidi ya akaunti 13 huku akitumia majina tofauti. Hii ndio sababu aliitwa Mbakaji wa Facebook. Siku anak**atwa alikutwa na line za simu 100. Baada ya kuk**atwa. Bester akikiri kwa kinywa chake ni yeye ndie aliyemuua Nomfundo. Bester akahukumiwa kifungo cha maisha gerezani.

Akiwa gerezani, Bester akaanzisha mahusiano na Dr. Nandipha Magudumana...

Itaendelea...

Dr. Nandipha : Ndege Mjanja hunaswa na tundu bovu-5

Simu ya mume wa Nandipha ilikuwa inaita. Kuangalia ni namba mpya. Akapokea.
“Habari shemeji,” kumbe ni kaka yake Nandipha alikuwa amepiga.
“Salama” mume wa Nandipha akajibu
“Shemeji Nandipha amek**atwa”
“Nandipha ndio nani” mume wa Nandipha akauliza k**a ndio kwanza analisikia jina hilo kwa mara yako.
“Nandipha Magudumana, mkeo, mama wa watoto wako humjui shemeji” kaka yake akajibu.
“Huyo mtu mimi simjui wala sijawahi hata kumsikia. Utakuwa umekosea namba”, mume wa Nandipha akakata simu kabisa.

Pengine ningekuwa hata mimi ningemkana mchana kweupe. Mwanamke umemuoa, ukazaa nae. Leo anaondoka na kwenda kutangatanga kisha ndugu zake wanakupigia simu. K**a sio kumkana basi ningekemea pepo. Pepo tokaaa.

Haiko wazi sana Nandipha na Bester walijuanaje. Lakini mahusiano yao yanapamba moto kuanzia mwaka 2017. Lakini walikutanaje?

Inadaiwa kwamba, Nandipha na Bester walijuana toka mwaka 2006 katika chuo Kikuu cha Witwatersrand. Inaamika Bester alikuwa akiendesha matamasha ya mambo ya urembo na mitindo. Nandipha alikuwa mmojawapo wa mabinti waliokuwa wakishiriki katika matamasha hayo. Miaka ikaenda wakiwa wanawasilina. Ilipofika mwaka 2011 wakapotezana. Baada ya hapo Nandipha akaolewa na kupata watoto.

Mwaka 2016 Nandipha na Bester wakaanza kuwasiliana tena. Nandipha akaanza kumtembelea gerezani mara kwa mara. Penzi likakolea. Nandipha akawa haambiliki tena. Nandipha akawa anafanya anachoambiwa na Bester. Mwaka 2020, Nandipha akawasilisha nyaraka kwamba alikuwa amechumbiwa na Bester. Hii ilikuwa k**a mkosi kwake kwani mwaka 2021 Nandipha akafungiwa kutibu..!

Itaendelea...!

Dr. Nandipha: Ndege Mjanja hunaswa na tundu bovu-6

7 April 2023, Arusha Tanzania

Sasa haikuwa siri tena kwamba Bester hakufa gerezani. Ilikuwa wazi Nandipha ndie aliyemsaidia Bester kutoroka gerezani. Habari hizi zilikuwa wazi kwa kila mtu. Bester na Nandipha walijua kwamba walikuwa wanatafutwa. Sasa wakae Afrika Kusini wanafanya nini. Uamuzi ulikuwa mmoja tu. Kutoroka.!?

Polisi walishtuka kwamba tayari Nandipha na Bester walikuwa hawako tena Afrika Kusini. Gari waliyotumia ilikutwa imetelekezwa kwenye mpaka wa Msumbiji na Afrika Kusini. Tayari Bester na Nandipha walikuwa Dar es Salaam Tanzania. Huko Nandipha alikuwa anavaa juba na kujifunika gubi gubi. Bester nae alikuwa anavaa nguo za kuficha uso. Hata hivyo Dar es Salaam ilikuwa ni njia ya mpito tu.

Tarehe 7, April Saa 11 alfajiri polisi wa Tanzania, wakiwa na polisi wa Interpol walikuwa wameizunguka Hotel moja maarufu jijini Arusha. “Tunamtaka mteja aliyelala chumba namba 44”. Hayo yalikuwa ni maneno ya polisi kwa mhudumu wa hotel hiyo. “Wameondoka k**a dakika 10 zilizopita”, mhudumu akawajibu na kuwaacha polisi wanaangaliana. Sasa watakuwa wanakwenda wapi. Nairobi ndio kituo kilichokuwa kinafuata.

Polisi wakajiongeza. Mbio mbio mpaka kwenye kizuizi cha barabarani kuelekea mpaka wa Namanga. Ikapita gari ya kwanza, ikapita gari ya pili. Hatimaye ikasimamishwa gari moja iliyokuwa spidi. Shusha vioo. Polisi mmoja akaita kwa kujiamini. Bester umekwisha. Bester akashukta. Wamenijuaje. “Mko chini ya Ulinzi”. Hapo wakak**atwa Bester akiwa na Dr. Nandipha pamoja na mtu mwingine raia wa Msumbiji.

Afrika Kusini ikapigwa na butwaa, imevichukua vyombo vya nchi hiyo miezi 11 kubaini Bester katoroka, lakini imewachukua siku 2 tu polisi wa Tanzania kumk**ata Bester na washirika wake. Huo ndio ukweli. Bester alikuwa tayari amek**atwa. Hiyo ilikuwa ni siku ya Ijumaa. Kifuatacho. Warudishwe Afrika Kusini kujibu mashtaka yaliyokuwa yanawakabili.

Siku 6 baadae,Bester na Nandipha walikuwa Afrika Kusini na kisha kusomewa mashtaka. Nandipha na Bester bado wako gerezani huko Afrika Kusini. Kesi yao itaanza kusikilizwa mwezi Novemba. Kwa sasa kuna habari kwamba huko gerezani Nandipha ana mimba ya miezi 5..!

Mwisho

Dr. Nandipha : Ndege Mjanja hunaswa na tundu bovu-2Jamii na dunia ikaamini Bester aliungua moto. Hatorudi tena mshenzi y...
26/10/2025

Dr. Nandipha : Ndege Mjanja hunaswa na tundu bovu-2

Jamii na dunia ikaamini Bester aliungua moto. Hatorudi tena mshenzi yule. Kwa matendo yake pengine mwili wake ulikuwa unateketea katika moto wa milele Jehenamu.
Huku nje Nandipha na Bester wakala maisha. Nandipha akaondoka kwa mume wake na watoto wake wawili. K**a Nandipha hayupo nyumbani, Bester anakwenda kuwachuku watoto shule.

Nandipha akamtambulisha Bester kwa baadhi ya marafiki zake na ndugu k**a mbia mwenzake. Mfanyabiashara maarufu kutoka Marekani. Akawaambia jina lake anaitwa TK Nkwana. Wenye akili wakajua wale walikuwa wapenzi.

Baadae ikabainika kwamba, siku selo ya Bester inawaka moto kamera za gereza zilizimwa na siku moja kabla kamera zilikuwa zimefunikwa. Hii ikaleta mashaka. Mamlaka zikafikiria kwamba pengine maofisa wa Magereza wamehusika kumuua Bester. Wakaomba taarifa ya uchunguzi wa mwili wa Bester. Taarifa ya madaktari ikaeleza kwamba, mwili ule ulikutwa fuvu la kichwa limepasuka na marehemu hakufariki kwa moto. Mtu aliyekufa kwa moto moshi huwa unakutwa kwenye mapafu. Wakapima DNA ya Bester na ya Mama yake, hazikuendana. Mungu wangu. Huyu hakuwa Bester. Bester yuko wapi sasa. Magazeti yakaandika. Bester katoroka gerezani.

Miezi 11 baada ya selo ya Bester kuteketea, Magazeti yakaanza kupata taarifa kutoka kwa raia wema. Gazeti moja likatumiwa picha ya Bester na Nandipha wakiwa wanafanya manunuzi katika duka la Woolworths huko Sandton City. Akili zikafunguka zaidi. Kumbe Bester yupo na anaishi na Nandipha.

Nandipha anaishi na mbakaji. Anaishi na mfungwa. Majina yake ya kuzaliwa kabisa ni Nandipha Sekeleni. Alizaliwa mwaka 1989 huko Eastern Cape na kukulia Port Edward huko KwaZulu-Natal. Inaandikwa Nandipha alikuwa daktari Bingwa wa Upasuaji, lakini hainyeshi alisoma wapi. Isipokuwa Nandipha alisoma degree yake ya kwanza ya udaktari wa binadamu katika chuo Kikuu cha Witwatersrand, huko Johannesburg. Alihitimu mwaka 2013. Mwaka huo huo Nandipha alifunga ndoa na aliyekuwa mume wake Dr Mkhuseli Magudumana. Katika ndoa yao Mungu akawajaalia watoto wawili, Aziza na Ayana. Mwaka 2017, Nandipha alianzisha clinic yake iliyokuwa inajishughulisha na maswala ya urembo....!

Itaendelea..

Dr. Nandipha : Ndege Mjanja hunaswa na tundu bovu-1Mwaka 2023 dunia nzima iligeukia jiji la Arusha. Hapo walik**atwa Tha...
25/10/2025

Dr. Nandipha : Ndege Mjanja hunaswa na tundu bovu-1

Mwaka 2023 dunia nzima iligeukia jiji la Arusha. Hapo walik**atwa Thabo Bester na Dr. Nandipha Magudumana. Wote raia wa Afrika Kusini. Thabo Bester alikuwa anatumikia kifungo cha maisha gerezani baada ya kupatikana na hatia ya makosa ya mauaji na ubakaji. Kila nikiwaza kisa cha Nandipha na Bester naamini ama kweli ndege mjanja hunaswa na tundu bovu. Nandipha daktari wa binadamu, mama wa watoto wawili, mke wa mtu ilikuwaje akanasa penzi zito na mwendawazimu k**a Thabo Bester. Je ni uchawi. Je ni ujinga tu ama Bester alikuwa na uwezo mkubwa wa kusahiwishi mtu yeyote akaingia kwenye njia zake. Mimi sijui.

Siku Bester anapelekwa gerezani, polisi waliwaambia maafisa wa Magereza kwamba. Bester alikuwa mtu mwenye ushawishi mkubwa. Wakawaonya kwamba wasimpe nafasi ya kumsikiliza. Ukimsikiliza Bester umekwisha. Hawakusikia. Siku zikaenda. Wakaingia kwenye mfumo wa Bester. Dokta Nandipha akanasa na kuwa mfungwa wa fikra wa Bester. Askari Magereza wakageuka wafungwa pia wa Bester. Kwa hawa maofisa wa Serikali sidhani k**a ni maneno tu ya Bester pekee ndio yaliyowavuta. Pengine na hongo ya pesa. Kwenye udhia penyeza rupia.

Bado haijajulikana vizuri Nandipha na Bester walijuanaje. Wengine wanasema Nandipha walikuwa chuo kimoja baadae Bester akahama chuo. Lakini hakuna ushahidi kwamba Bester aliwahi kusoma chuo Kikuu cha Witwatersrand. Mapenzi yao yalikuwa motomoto toka mwaka 2017, wakati huo tayari Bester alikuwa anatumikia kifungo cha maisha gerezani. Nandipha akawa hashikiki tena. Mke wa mtu na mama wa watoto wawili alikuwa kwenye penzi zito na muuaji. Hakika makaratasi sio akili.

Nandipha na Bester wakasuka mpango. Iwe isiwe lazima Bester atoke gerezani. Nandipha akaenda katika Mortuary moja akachukua mwili wa mzee mmoja akadai ni wa baba yake. Mwili ule ulikutwa umetupwa mtoni siku chache baadae. Akaenda tena akachukua mwili wa mtu mwingine akadai ilikuwa maiti ya kaka wa rafiki yake anataka kwenda kuzika. Akapewa maiti ya kijana wa makamo. Nandipha akaukabidhi mwili kwa askari magereza. Usiku wake selo ya Bester ikawaka moto. Dunia ikatangaziwa, Mbakaji na Muuzaji Thabo Bester alikuwa amefariki!

Itaendelea

"Niwambie hata hao wanaotengeneza akaunti zao feki wanahisi wamejificha , hauwezi kujificha. Hivi vifaa vya elektroniki ...
24/10/2025

"Niwambie hata hao wanaotengeneza akaunti zao feki wanahisi wamejificha , hauwezi kujificha. Hivi vifaa vya elektroniki vimetufanya hata siri zetu ziwe tu hadharani. Kwahiyo wengine tuna picha zao hata mimi kwenye gari pale ninazo nikiona mtu naangalia hivi siyo yule anayetafutwa?

Na siku hiyo k**a wewe unayeanzisha maandamano tukiwa na picha yako tukikuona ndiye huyu, hata k**a ulikuwa unapita tu lazima tukuk**ate Si ulishatenda kosa?! Tutakuk**ata. Kwahiyo wasifikiri k**a wapo salama sana hata k**a hawajaandamana" Asema Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, DCP David Misime kuhusu hali ya usalama nchini kuelekea kipindi cha Uchaguzi Mkuu akifanya kipindi FM

24/10/2025

JK NA HAYATI MAGUFULI WALIPOFANYA UKAGUZI,UJENZI BARABARA YA MWENDO KASI MWAKA 2014

Rais wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikagua ujenzi wa barabara ya mabasi yaendayo kasi (DART) eneo la Kimara Mwisho jijini Dar mnamo Mei 29, 2014, akiongozana na aliyekuwa Waziri wa Ujenzi wakati huo, Dkt John Pombe Magufuli.

Ziara hiyo ililenga kukagua maendeleo ya mradi huo mkubwa wa usafiri wa umma uliobuniwa ili kuboresha hali ya usafiri jijini ili kupunguza msongamano wa magari.

Video na IssaMichuzi

https://habari101tz.blogspot.com/2025/10/tma-yatoa-taarifa-juu-ya-uwepo-wa.html
23/10/2025

https://habari101tz.blogspot.com/2025/10/tma-yatoa-taarifa-juu-ya-uwepo-wa.html

Dar es Salaam - Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inatoa taarifa ya uwepo na mwenendo wa Kimbunga “CHENGE” katika Bahari ya Hindi, Kaskazini Mashariki mwa Kisiwa cha Madagascar umbali wa takribani kilometa 2400 kutoka Mashariki mwa pwani ya Mtwara.Kimbunga “CHENGE” kilianza kujitengenez...

22/10/2025

Mama Amina k**a Kila mtu anamuweza hivi ona alivyompa Diamond amri na Mondi akatii amri🤣🤣🤣

Address

UBUNGO, RIVERSIDE
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sisi Ni Habari posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share