Ummu Muhammâd

Ummu Muhammâd I love everyone

26/08/2025

Alikuwa akitoka nyumbani huku akiacha wosia mmoja kwa mkewe: alisema
“Mke wangu iwapo nitapatwa na jambo, au nikichelewa, na mkihitaji kitu…baasi piga simu namba hii.”

Mkewe akamuuliza: “Namba ya nani hii?”
Akasema kwa utulivu: “Namba ya ndugu yangu.”

Akaona ajabu; maana anamfahamu vyema mume wake kuwa hana ndugu, lakini akatikisa kichwa na akaendelea kimya na mume akaondoka.

Siku zikapita. Mume akatoweka wiki nzima, jambo lisilo desturi yake.
Vitu vya nyumbani vikaanza kuisha kidogo kidogo, hadi makabati yakawa matupu.
Mama akachoka na hofu ikamzidia. Watoto wakawa wanalia kwa njaa kali, naye hakuwa na chochote cha kuwatuliza nacho watoto.

Alijaribu kumpigia mumewe mara nyingi. Simu ilikuwa imezimwa au haipatikani.
Na mambo yalipozidi kuwa mabaya, alikumbuka wasia wa mume wake.
Akachukua simu na kupiga namba ile.

Akapokea mwanaume kwa sauti yenye ya kuchoshwa, kana kwamba alikuwa na tatizo kazini:
Akasema,
“Ni nani anayepiga?”

Yule mke akasema huku akilia: “Watoto wangu wamechoka kwa njaa kwa siku kadhaa, na hatujapata habari yoyote kuhusu mume wangu Muhammad. Aliniacha na wasia kuwa tukihitaji kitu nikupigie, na akasema wewe ni ndugu yake… nami najua hana ndugu.”

Akamjibu akiwa na hasira na kukerwa: “kata simu mama”
Lakini kabla hajakata simu, ghafla sauti ya maneno ya mwanaume yakaingia yenye ukali wa kutaka kujua jambo zaidi:
“Subiri mama! Umesema Muhammad? Muhammad yupi?”

Akasema kwa majonzi: “Mume wangu, Muhammad bin …” (akamtaja kwa jina kamili).

Kimya kikarefuka upande wa pili, kisha sauti ikabadilika ghafla, ikawa yenye hofu na mshtuko: Yule mwanaume akasema...
“Wewe ni mke wa Muhammad?! Subiri hapo, usiweke mbali simu!”

Moyo wa mama ulishikwa na mshangao.

Dakika chache baadaye, mlango wa nyumba yake ukagongwa kwa nguvu. Alipofungua, akakuta kundi la watu wakishikilia mifuko ya chakula, nguo na pesa. Nyuma yao akiwa amesimama yule mwanaume aliyepokea simu.

Yule mwanaume akamwendea mama yule huku machozi yakimtiririka: akisema
“Samahani dada yangu… Muhammad si ndugu yangu wa damu, bali ni ndugu yangu katika dini na ktk mema. Yeye kila mwezi alikuwa akinipatia kiasi cha pesa, akiniusia akisema kwamba: ‘Iwapo siku moja sitakuwepo, na familia yangu ikihitaji msaada, basi wewe ndiye ndugu niliyewaachia familia yangu.’”

Mwanamke akabaki kustaajabu, machozi yakitiririka.

Mwanaume akaendelea:
“Nilidhani amekusahau… kumbe alikuwa anakuamini na akaniachia dhamana. Nimekosea kwa sauti yangu mbaya niliyokujibu nayo, lakini kuanzia leo mimi ndiye ndugu yenu, na nyumba yenu haitakosa riziki.”

Watoto wakakimbia wakishika mikono ya wale waliobeba chakula, wakicheka huku machozi ya mama yao yakibubujika kwa furaha.

✨ Funzo:
Wema wa kweli ni kuacha nyuma amana na msaada kwa familia, si kwa maneno tu bali kwa vitendo. Muhammad alijua thamani ya ndugu wa kweli, hata k**a si wa damu.

✍️Kujiandaa na maisha – Mume alitambua kuwa maisha yanaweza kubadilika ghafla, akawaacha mke na watoto wake na wasia wa msaada. Hii ni funzo kwetu tuwe na mipango ya kuwalinda wategemezi wetu.

✍️Undugu wa Kiislamu – Hata k**a si ndugu wa damu, undugu wa imani na wema una thamani kubwa. Muhammad alimchagua mtu wa amana na kumwita ndugu.

👉Msaada kwa wakati wa dhiki – Wema wa kweli huonekana wakati wa shida. Ndugu huyo alipobadilika na kuwasaidia familia, alidhihirisha thamani ya undugu wa Kiislamu.

🫵Kutokudharau maombi ya wenye shida – Mwanzo aliongea kwa kero, lakini alipofahamu ukweli alibadilika. Funzo ni tusidharau kilio cha mhitaji, huenda ndani yake kuna uokovu wetu.

🤝Kuwajibika kwa familia – Kila mtu anapaswa kuwaza mustakabali wa familia yake hata endapo atapatwa na kifo au matatizo.

💫Mali bora ni mali inayotumika kwa wema Muhammad hakuridhika kufaidika peke yake, bali alitumia riziki yake kuandaa msaada kwa familia yake.

Endelea kufuatilia ukurasa wangu
Hakikisha umebofya jina la Sufian Mzimbiri ili uweze kuni follow na kujifunza mengi zaidi.

20/08/2025

Yaa rabbi nakuomba uwape
Afya njema wapendwa wetu waishi kwa furaha na amani 🙏
Uwapunguzie mitihan yaa rabbi 🙏

14/08/2025

Naomba mnishauri Chochote

09/08/2025
31/07/2025

ROHO KABLA HAIJATOKA ANAJILAUMU

Kisa cha msafiri aliyekutana na mitihani mitatu ktk safari yake na akaishinda na kuja kujilaumu sana siku anakata roho.

Imesimuliwa kwamba mtu mmoja aliyekuwa mwema alikuwa ktk saqaratul mauti na akawa hatamki ispokuwa maneno matatu.

1.MTIHANI WA KWANZA ULOMFIKA.
Alisafiripo bwana mmoja aliyekuwa mwema safari ndefu yenye misukosuko na majaribu mbali mbali,

Wakati akiwa katikati ya safari yake ndefu, akiwa yuwapita njiani mara akaskia mtu yuapiga makelele, akastaajabu kwamba inawezekanaje mtu kupiga makelele ilhali maeneo haya nimaporini hakuna hata mtu anayeishi!!

Ndipo Akasimama akasikiliza kwamakini akaisikia sauti inakotokea, hapo akataka kuendelea na safari yake, lakini moyo ukakataa kwenda akaweka begi lake chini

Ndipo akaanza kufuatilia ile sauti ya mtu anayepiga makelele niwapi inatokea, akafuata mpaka akafika,

Alipofika karibu anamkuta mtu yumo ndani ya chaka au kichaka amejificha humo lakini cha kushangaza mtu yule yuko uchi wa hana nguo hata moja,

Baasi msafiri yule alikuwa na mashuka mawili moja jipya na jingine chakavu ndipo akampatia bwana yule shuka yake ilochakaa na kuacha shuka lake jipya ndani ya begi lake,
Yule bwana alipopewa lile shuka akashukuru sana akajifunika na akatoka ndani ya lile chaka

Na msafiri yule baada ya hapo akaendelea na safari yake..........................

2.MTIHANI WA PILI ULOMFIKA,
Mara baada kashaamsaidia yule bwana aliyekuwa uchi akaendelea na safari yake,

Akiwa anaendelea na msafara wake Alipofika mbele akakutana na mtu mwingine njiani yualia, akamuuliza unalia nini akasema nina njaa Kali sana nina siku kadhaa sijala

Yule msafiri akasimama akatizama ndani ya begi lake anao mkate mmoja mzima na mwingine aliula alibakisha nusu

Akatoa ile nusu ya mkate na akampa yule mtu mwenye njaa kali ilomfanya ashindwe mpaka kutembea,
Alipompa alipokula akapata nguvu ndipo nayeye akaendelea na msafara wake, na msafiri yule akaendelea na safari yake,

3.MTIHANI WA TATU ULOMPATA,

Baada ya pale alipokuwa sasa kashaakutana na mitihani miwili na ameishinda baasi unakuja MTIHANI wa tatu,

Njiani yuakutana tena na kiwete, hawezi kutembea ana tambaa, na anataka awahi swala ya ijumaa kwa jamaa msikitini, na msikiti nao uko mbali kidogo.

Yule bwana akaweka begi lake vizuri begani na akambeba mgongoni,
Yule kiwete akapanda mgongoni yule msafiri akasimamisha safari yake kwa muda ili kumfikisha yule kiwete msikitini aiwahi swala,

Akaenda huku kambeba mgongoni, akafika na akamfikisha kiwete yule msikitini na ndipo alipomfikisha akarudi kuendelea na safari yake

Baasi mitihani yote hiyo MITATU akawa ameifaulu, akasafiri mpaka akafika anakoenda,

Lakini haukupita muda mrefu sana
Bwana yule msafiri yakamjia mauti,

Lakini sasa wakati wa kukata roho, akiwa katika sakaratul mauti, ule uchungu wa kukata roho
Akawa yuatabasamu lakini huku anajilaumu sana

Walikuwopo baadhi ya watu wakati bwana yule akiwa yuko ktk sakaratul mauti,

Lakini chakustaajabisha na kilichowastaajabisha watu waliokuwepo sehemu ile walimshuhudia msafiri yule akiwa yuko katika hali ya tabasamu na Mara akihuzunika

Kwasababu wakati mtu akifa Allah humletea mtu k**a darubini akimuonyesha huko aendako kwamba kukoje

Baasi bwana yule Alikuwa nik**a mtu ametizama sehemu lakini kile anachokiona hakuna mwingine anayeweza kuona akiwa ktk tabasam zuri.

Msafiri yule akawa ana nadi kwa kusema maneno haya akirudia kila neno Mara tatu tatu

Akisema

ليته كان جديدا
ليته كان كاملا
ليته كان بعيدا

Laitahu kaana jadiinan ×3
Laytahu kaana kaamilan ×3
Laytahu kaana baiidan ×3

Baasi akawa yuandelea kunadi mwenyewe maneno hayo huku roho inachukuliwa taratibu, mpaka akafikia mwisho wa kunadi na hapo roho ikatoweka,.

Akazikwa bwana yule
Siku zilipopita mmoja miongoni mwa watu wema akamuona bwana yule msafiri ktk ndoto akamuuliza kuhusiana na yale maneno aliyokuwa akiyasema wakati anakata roho

Ndipo yule msafiri akawa anamueleza yule mtu mwema kuhusiana na yale yaliyojiri siku anakata roho

Kulipokucha yule mtu mwema akawasimulia watu juu ya yale aliyoyaona ktk ndoto ambayo yalijitokeza ktk siku ya kukata roho yule msafiri akiwaambia

Bwana huyo alisafir siku moja na akakutana na mitihani MITATU na akaweza kuifaulu sasa maneno hayo aloyasema yanasadifu fraha aliyokuwa nayo pale alipo onyeshwa pepo yake ilivyokuwa nzuri na kubwa ambayo kaandaliwa na tafsiri yake nik**a ifuatavyo

Ama kuhusu Yale maneno hake yamwanzo aliposema
ليته كان جديدا
Laitahuu kaana jadiidan,
(Laiti lingelikuwa ni jipya)
Lilikuwa ni shuka
Hapo alikuwa akizungumzia shuka alilotoa kumpa yule msafiri akijilaumu mara baada yakuonyeshwa pepo yake ilivyokuwa kubwa kwaajili yakutoa shuka tena chakavu, sasa anajiuliza mwenyewe nakujilaumu kwamba je hilo ni chakavu je angempa yule bwana lile shuka jipya hiyo pepo ingekuwaje k**a shuka chakavu lenyewe pepo yake kubwa namna hii!.?

Na ama kuhusu tafsiri ya maneno yale aliposema
ليته كان كاملا
Laytahu kaana kaamilan
(Laiti ungelikuwa ni mzima)
Huo ni mkate........
Hapo nipale alipokutana nayule bwana mwenye njaa Kali na akampa kipande cha mkate
Sasa ameonyeshwa ukubwa na uzuri wa pepo yake hapo akiwa anakata roho ndio maana mkamuona anajilaumu kwamba uzuri na ukubwa wote huo wa pepo nikwaajili ya kipandetu cha mkate je sasa ningempa ule mkate mzima,
hiyo pepo yangu ingekuwa nzuri na kubwa kiasi gani k**a kipandetu pepo yake ni nzuri na kubwa kiasi hiki!!!

Ama kuhusu tafsir ya maneno yake aliposema
ليته كان بعيدا
Laytahu kaana baiidan
(Laiti ile sehemu ingelikuwa mbali)
Ule msikiti......
Ambapo pale alipokutana na yule kilema akambeba kumfikisha msikitini ndipo Allah anamuonyesha malipo yake nayo ni pepo ya juu nzuri na kubwa
Sasa bwana yule anajuta na kusikitika na kujilaumu kwamba hayo nimalipo ya sehemu ile tena yenye umbali mdogotu sasa je ile sehemu ingekuwa mbali au
Vipi sasa ingekuwaje hiyo pepo yangu kwa uzuri k**a ile sehemu ingelikuwa ni mbali zaidi ya pale ingekuwa pepo yangu ni nzuri na kubwa kiasi gani k**a kijisehemutu kile malipoyake nipepo yanamna hii!!?

Naam nadhani hapo ndipo mwisho wa kisa cha bwana huyu
Bila shaka k**a umesoma kwa utulivu umepata mazingatio makubwatu

Ambayo miongoni mwayo ni

1.Amali yoyote ile utendayo ijapo kuwa ndogo kiasi gani Allah anaiona na malipoyake utakuja yaona siku hiyo ikifika

2.Ukitoa au kutenda kidogo pia utakuja kujuta kwamba kwanini nisingetoa kingi, au nisingefanya makubwa zaidi na zaidi!!
Utaishia kulalama lakini muda ndo ushaafika haicheleweshwi japo sekunde.

Follow ukurasa huu wa Sufian Mzimbiri ujifunze zaidi

28/07/2025

Maisha ya Ajabu, Mauti ya Ajabu ❤️❤️❤️
Takriban miaka 40 iliyopita, mzee huyu aliingia msikitini 🕌 kabla ya swala na akamwambia Imam:
"K**a nisipohudhuria swala mbili za jamaa mfululizo msikitini, basi ujue kuwa nimekufa ⚰️ nyumbani kwangu."

Mzee alipoona uso wa Imam umejaa mshangao, mzee alifafanua kuwa hana watoto na mke wake tayari amefariki.

Tangu siku hiyo, Sheikh hakuwahi kukosa swala hata moja msikitini kwa kipindi cha miaka 4️⃣0️⃣, achilia mbali swala mbili mfululizo.
Mnamo Julai 2019, mzee alifariki wakati wa swala ya Ijumaa ndani ya msikiti, na kila mtu alishuhudia mauti yake. ❤️❤️❤️

Allah atupe mwisho mwema, aamiin

18/07/2025

One
Day
Yes utatoboa
Tu inshaallah 🙏🥰

18/07/2025

Dada ukiwa unajistiri na kujiheshimu hakuna atakaye

Kuchezeaa

17/05/2025

Simba baba lao
hata iweje

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ummu Muhammâd posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share