27/05/2025
💔💔💔NILIMUAMINI KUPITA KIASI💔💔💔
Nilikuwa nampenda sana . Alikuja k**a malaika, akajifanya mwenye upendo na huruma. Alinitumia meseji kila asubuhi, akanifanya nihisi k**a mimi ni mtu wa pekee duniani.
Tulikaa miezi mitatu kwenye mahusiano, kila siku nikimpigia, nikimtumia vocha, hata pesa kidogo alizokuwa anaomba. Nilikuwa tayari kufanya lolote kwa ajili yake. Nilikuwa kipofu wa mapenzi.
Lakini nilianza kuona mabadiliko. Simu zikawa hazipokelewi haraka, meseji hazijibiwi k**a awali. Siku moja rafiki yangu alinipigia na kuniambia, “Kaka, huyo Amina niliwaona na jamaa mwingine wakitoka hotelini.”
Nilivunjika moyo. Nilipomuuliza, alikataa kila kitu kwa ujasiri. Lakini siku chache baadaye, alinitumia meseji: *"Samahani, nilikupenda lakini moyo wangu haukuwa wako peke yako."*
Nilikaa kimya, nikagundua kuwa sio kila anayekuja na tabasamu anamaanisha. Mapenzi ya kweli yanajengwa na ukweli, sio maneno matamu tu.
Baada ya ujumbe wake wa mwisho, sikuandika tena. Nilikaa kimya, nikamwachia nafasi. Nilijifunza kitu kikubwa—sio kila anayekupigia kila siku anakupenda kweli, na sio kila anayepuuza simu yako yuko bize.
Nilianza kujijenga, nikaweka nguvu zangu kwa familia na ndoto zangu. Nilipojifunza kujithamini, ndipo nikaelewa thamani yangu haipaswi kutegemea mtu mwingine
K**a unapiga simu au kutuma meseji na mtu anapuuza mara kwa mara bila sababu ya msingi:
-👉*Usijishushe:* Thamani yako haitegemei majibu ya mtu.
👉Toa nafasi:* Ukiona hujibiwi, kaa kimya. Asiyekutafuta hana nafasi ya kukupoteza
👉Jithamini:* Weka muda wako kwa watu wanaokuthamini kweli.
👉Usilazimishe:* Mapenzi ya kweli hayaombwi wala hayaombi nafasi. Yanajitokeza.
đź’ĄWewe ni wa thamani, na anayekustahili atakuonesha wazi bila kujificha.