Mpogo da Swaggz

Mpogo da Swaggz Film & Music Videos Director
Musician | Voiceover artist
From East Africa Tanzania 🇹🇿

MSAGASUMU AFARIKI KWA AJALI DODOMAMchezaji wa zamani wa soka Tanzania SELEMANİ MSAGASUMU amefariki kwa ajali usiku wa ku...
03/07/2025

MSAGASUMU AFARIKI KWA AJALI DODOMA

Mchezaji wa zamani wa soka Tanzania SELEMANİ MSAGASUMU amefariki kwa ajali usiku wa kuamkia leo tarehe 3 Julai 2025. Msagasumu alikuwa anaendesha pikipiki ambayo iligongana na gari na kupelekea umauti wake papo hapo, Dereva wa gari anashikiliwa na Polisi ilihali mwili wa marehemu ukiwa hospitali ya Mkoa. Katika uhai wake Msagasumu amewahi kuzichezea timu kadhaa ikiwemo CDA ya Dodoma (Watoto wa Nyumbani) lakini alikuwemo kwenye timu ya Taifa ya vijana U20 (Ngorongoro Heroes) mwaka 1999 .

SISI NI WA ALLAH NA HAKIKA KWAKE NI MAREJEO YETU.

Pumzika Sele mpaka wakati mwingine!

Kikosi Cha Mnyama dhidi ya JKT
05/05/2025

Kikosi Cha Mnyama dhidi ya JKT

Klabu ya Simba Sc imetoa taarifa kuhusu Mlinda mlango wao Aishi Manula kuwa ameshindwa kuendelea na safari baada ya kupa...
04/12/2024

Klabu ya Simba Sc imetoa taarifa kuhusu Mlinda mlango wao Aishi Manula kuwa ameshindwa kuendelea na safari baada ya kupata hitilafu ya kiafya dakika chache kabla ya kuanza safari ya kuelekea nchini Algeria tukiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.

19/11/2024
19/11/2024

Mtoto Kautaka🤣🤣

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akielekea kwenye Kikao cha Baraza la Mawaziri kili...
25/10/2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akielekea kwenye Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika katika Ikulu ndogo ya Tunguu Zanzibar tarehe 25 Oktoba, 2024.

23/10/2024

Watu hawapendi amani kabisa🤣🤣

Mazishi ya Mpendwa wetu Yusuph Abdallah Kaimu (PEMBE) yatafanyika leo saa Saba mchana YOMBO DOVYA - Panda gari za kwenda...
21/10/2024

Mazishi ya Mpendwa wetu Yusuph Abdallah Kaimu (PEMBE) yatafanyika leo saa Saba mchana YOMBO DOVYA - Panda gari za kwenda BUZA Waambie wakushushe kituo kinaitwa Chama au Shule uliza Msibani kwa PEMBE au hata kwa Natasha ni jirani na ulipo Msiba - Ukija na usafiri wako baada ya kutoka kituo cha Davis Corner unavuka reli unapandisha kilima ukikimaliza ndio unafika kituo cha Chama au Shule - Tujitokeze kwa wingi tumsindikize mwenzetu kila nafsi itaonja umauti - INNAH LILLAH WAINNAILAIHI RAJIUN -

14/10/2024

SIMBA 🦁 🔥🙌 Akikiwasha kwenye Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru pamoja na kumbukizi ya miaka 25 ya Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza leo 14 Oktoba, 2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Kiongozi wa mb...
14/10/2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Kiongozi wa mbio hizo Ndugu Godfrey Eliakim Mzava kwenye Kilele cha Maadhimisho Mbio za Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza tarehe 14 Oktoba, 2024.

Mwanamke anayefahamika k**a Joyce Ojala (32) ambaye ni mkazi wa Matalawe mjini Njombe anashikiliwa na Polisi kwa kosa la...
12/10/2024

Mwanamke anayefahamika k**a Joyce Ojala (32) ambaye ni mkazi wa Matalawe mjini Njombe anashikiliwa na Polisi kwa kosa la kutoa taarifa za uongo kuwa ametekwa na watu wasiojulikana ili kufanikisha kumrudisha mumewe Mfaume Mzee (37) aliyekuwa mkoani Ruvuma akifanya shughuli za madini kwa zaidi ya miezi sita.

K**anda wa Polisi mkoa wa Njombe Mahamoud Banga akizungumza na
vyombo vya habari amethibitishwa kushikiliwa kwa mwanamke huyo
aliyekutwa amekaa kwenye ofisi ya fundi kuchonga mjini humo.

"Mama huyu alitoa taarifa kwa mume wake kwamba ametekwa na watu
wasiojulikana na mume wake anahitajika aje kwasababu amekuwa
akijihusisha na vitendo vya uhusiano na wanawake ambao ni wake za watu
kwa hiyo wamemteka ili mume wake aweze kuja yeye mwenyewe, lakini
baada ya kutoa taarifa katika jeshi la Polisi wakati wa ufuatiliaji tulibaini
kwamba huyu mama alikuwa amejiteka yeye mwenyewe kwa wivu wa
mapenzi", amesenma K**anda Banga.

Banga amesema mwanamke huyo amekuwa akizungumza na mumewe
mara nyingi lakini amekuwa akiambiwa bado ana shughuli nyingi jambo
lilifanya mwanamke huyo kutumia mbinu hiyo iliyosababisha mume wake
kurudi haraka lakini Polisi wamebaini kuwa mwanamke alidanganya ili
mwanaume aweze kurudi kumpa stahiki yake.

Watu wengi wanaamini kwamba makaburini ndipo mizimu na mashetani wanaishi lakini sivyo K**a wanavyofikiria, mizimu Inawe...
12/10/2024

Watu wengi wanaamini kwamba makaburini ndipo mizimu na mashetani wanaishi lakini sivyo K**a wanavyofikiria, mizimu Inaweza kuishi na wewe ndani ya nyumba yako.

Ukweli ni kwamba Makaburini ni sehemu salama kuwaepuka mizimu wakati wa usiku, kwasababu usiku Kuna nafasi kubwa kwa mizimu kuwepo chumbani kwako tofauti na Makaburini.

Kwahiyo k**a unasumbuliwa na mizimu siku mojamoja uwe unaenda makaburini kulala ili upate usingizi mzuri.

Wangapi Mpo Tayari ☺️

Mpogo✍️

Address

Dar Es Salaam

Website

http://www.gmail.com/mustaphampogotz

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mpogo da Swaggz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mpogo da Swaggz:

Share