Dost Media Tz

Dost Media Tz We aim to tell a story that matters

18/10/2025

Wanafunzi kisiwani Zanzibar nao wameitaka serikali ijayo kuhakikisha wanajifunza katika mazingira salama na yenye ustawi, wakisisitiza umuhimu wa kuwa na madarasa bora, chakula shuleni, na usalama wa wanafunzi.

Wamesema kuwa ingawa baadhi ya shule ziko katika hali nzuri, nyingine bado zinakabiliwa na changamoto za miundombinu duni na mazingira hatarishi ambayo yanadhoofisha ari ya kujifunza.

Kadri uchaguzi mkuu unavyokaribia, walimu na wanafunzi Zanzibar wamekuwa wakitoa sauti zao zenye matumaini na matarajio kwa serikali ijayo — wakitaka elimu iwe miongoni mwa maeneo yatakayopewa kipaumbele cha juu kwa ajili ya ustawi wa taifa.

_____________
Fuatilia kwenye YouTube Channel na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

17/10/2025

Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, (CHADEMA), Tundu Lissu amemuwekea Mapingamizi shahidi wa tatu wa Jamhuri Samweli Elibariki Kaaya ambaye ni Mkaguzi wa Jeshi la Polisi kuhusu kupokelewa vielelezo ikiwemo Flash Disk na vingine katika kesi yake ya Uhaini ambayo imeendelea kusikilizwa Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Oktoba 17, 2025, Nje ya Viunga vya Mahak**a hiyo, Mkurugenzi wa Sheria CHADEMA, Wakili Gastoni Garubindi amethibitisha mapingamizi hayo ambapo ametaja sababu alizowasilisha Tundu Lissu kuhusu Mapingamizi yake dhidi ya Shahidi huyo.

Wakili Garubindi amesema sababu ya kwanza ni kwamba vielelezo ambavyo shahidi aliomba vipokelewa Mahak**a Kuu havikusomwa awali katika Mahak**a ya Kisutu ambayo ilianza kusikiliza kesi hiyo ambapo Lissu ameiambia Mahak**a kuwa havina uhalali wa kupokelewa huku akitaja Sababu ya pili kwamba ya kisheria kuhusu uhalali wa shahidi kutoa vielelezo hivyo, akidai kuwa hana mamlaka ya kuwasilisha vielelezo hivyo.

Sababu ya tatu inahusu mnyororo wa namna ushahidi huo ulivyopatikana hadi hatua ya kuufikisha Mahak**ani (chain of custody) na kisha sababu ya nne ni kwamba kabla ya shahidi kuomba kutoa ushahidi huo, alitakiwa kwanza kuwasilisha ripoti ya uchunguzi alioufanya.

Kesi hiyo inatarajiwa kuendelea siku ya Junatatu Oktoba 20 ambapo upande wa Jamhuri watatoa majibu ya Mapingamizi ya Lissu na kisha Mahak**a itatoa uamuzi kuhusu mapingamizi hayo.
_____________
Fuatilia kwenye YouTube Channel na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

17/10/2025

Mchezaji wa klabu ya Namungo Fc, Lukindo ameweka bayana kuwa mchezaji anayemvutia na anayemfuatilia zaidi kwenye mchezo wa soka ni Ronaldo pamoja na Mbappe.

Full Video inapatikana You tube ya

17/10/2025

Mchezaji wa Namungo FC anayefahamika k**a Frank amejibu maswali mbalimbali aliyoulizwa na Mchezaji mwenzake Lukindo na kuwatoa hofu mashabiki zake kuwa wakae tayari mambo mazuri yanakuja.

Full Video inapatikana You Tube ya

17/10/2025

Mchezaji wa Namungo FC, Pius Buswita amethibitisha kuwa ni kweli kwenye mchezo wa soka kunakuwa na uchawi kutokana na matukio mbalimbali ambaye yeye aliwahi kukutana nayo.

Full Video on you tube ya Dost media.

17/10/2025

Walimu kutoka maeneo mbalimbali ya Zanzibar wamewataka viongozi watakaochaguliwa kuipa kipaumbele sekta ya elimu kwa kuboresha miundombinu ya shule na huduma za usafiri, ili kuweka mazingira bora kwa walimu na wanafunzi.

Wamesema kuwa licha ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika miaka mitano iliyopita kuweka mkakati wa kujenga shule za kisasa zenye ghorofa, bado yapo maeneo ambayo hayajafikiwa na mpango huo, hali inayosababisha changamoto katika ufundishaji na ujifunzaji.

_____________
Fuatilia kwenye YouTube Channel na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

17/10/2025

Mratibu wa kituo cha Walimu Zanzibar, Mwalimu Daudi Mohammed, ameeleza hali halisi inayowakabili walimu katika jimbo hilo, akisisitiza umuhimu wa maboresho katika miundombinu ya elimu na teknolojia ya kufundishia.
Akizungumza na Dost Media, Mwalimu Daudi amesema walimu wanakabiliana na changamoto za kuendana na maendeleo ya teknolojia katika ufundishaji, hivyo ametoa wito wa kuimarishwa kwa mifumo ya TEHAMA katika shule zote kisiwani humo.
Ameongeza kuwa ushirikiano wa karibu kati ya viongozi na walimu utakuwa nguzo muhimu katika kuinua kiwango cha elimu Zanzibar.

Zikiwa zimesalia siku 11 kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025, unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, walimu wamekuwa sehemu ya sauti zinazotoa maoni kuhusu mustakabali wa elimu nchini.

_____________
Fuatilia kwenye YouTube Channel na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

17/10/2025

Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu imewataka Waajiri Sekta Binafsi kuzingatia kima kipya cha chini cha mshahara ambacho kimepanda kwa wastani wa asilimia 33.4. kutoka shilingi 275,060 hadi shilingi 358,322 na kitaanza kutumika rasmi Januari 1, 2026.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Oktoba 17, 2025, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete, amesema wataendelea kufuatilia utekelezaji wa kima hicho na hawatosita kuchukua hatua kwa waajiri ambao watakaidi kutekeleza amri hiyo.

“Aidha ofisi yangu itaendelea kufatilia kwa karibu utekelezaji wa amri hii, kutoa elimu kwa waajiri na wafanyakazi pamoja na kufanya tathimini ya mara kwa mara ili kuhakikisha utekelezaji wake unafanyika kikamilifu," Amesema Waziri Ridhiwan.
_____________
Fuatilia   kwenye YouTube Channel   na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

     

17/10/2025

Zanzibar ni kisiwa ambacho kimepiga hatua kubwa katika maendeleo ya sekta ya Elimu ndani ya kipindi cha miaka mitano iliyopita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Hussein Ali Hassan Mwinyi.

Hata hivyo, pamoja na mafanikio hayo, bado kuna maeneo kadhaa ambayo hayajafikiwa ipasavyo, hususan katika baadhi ya majimbo ya Unguja.

Tumezuru kisiwa hiki na kuzungumza na wananchi, watumishi pamoja na wadau wa sekta ya elimu ili kufahamu matarajio yao kwa uongozi ujao, hususan kuhusu mustakabali wa elimu Zanzibar na changamoto wanazokutana nazo katika maeneo wanayofanyia kazi au wanayohudumia.

_____________
Fuatilia kwenye YouTube Channel na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

Dost Media kwenye Namungo Fc ‘Media Day’ Leo Ijumaa, Oktoba 17, 2025. _____________Fuatilia   kwenye YouTube Channel   n...
17/10/2025

Dost Media kwenye Namungo Fc ‘Media Day’ Leo Ijumaa, Oktoba 17, 2025.

_____________
Fuatilia   kwenye YouTube Channel   na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

    

Address

Mbezi Beach
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dost Media Tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Dost Media Tz:

Share