01/06/2026
Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Bwana Sisty Nyahoza, leo Juni 1, 2026, amefanya ziara ya katika Makao Makuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) yaliyopo Edwin Mtei House, Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Katika ziara hiyo, Bwana Nyahoza akiwa na ujumbe alioambatana nao, amepokelewa na kufanya kikao cha ndani na viongozi wakuu wa chama hicho wakiongozwa na Katibu Mkuu, John Mnyika.
____
Fuatilia kwenye YouTube Channel na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Makala, Michezo, Burudani, Uchambuzi na Mahojiano.