Dost Media Tz

Dost Media Tz We aim to tell a story that matters

Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed, ametangaza kukamilika kwa bwawa la umeme lenye utata linalojengwa kwenye Mto Nile, ...
04/07/2025

Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed, ametangaza kukamilika kwa bwawa la umeme lenye utata linalojengwa kwenye Mto Nile, na kusema kuwa hatua hiyo ni mafanikio makubwa kwa taifa lake licha ya mvutano wa muda mrefu na mataifa jirani, hususan Misri na Sudan.

Akihutubia wabunge jijini Addis Ababa hapo jana, Abiy alisema serikali yake inaandaa uzinduzi rasmi wa mradi huo mkubwa wa umeme unaofahamika k**a Grand Ethiopian Renaissance Dam (GERD) mnamo mwezi Septemba. Bwawa hilo, ambalo ujenzi wake ulianza mwaka 2011, limeigharimu Ethiopia takribani dola bilioni nne na linatajwa kuwa mradi mkubwa zaidi wa nishati barani Afrika.

Licha ya mvutano wa muda mrefu kuhusu mgao wa maji ya Mto Nile, Abiy alisisitiza kuwa maendeleo ya Ethiopia hayataleta madhara kwa mataifa jirani. "Tunaamini kuwa maendeleo ya taifa moja hayapaswi kuwa mzigo kwa mwingine. Maendeleo ya Ethiopia ni kwa ajili ya ustawi wa wote," alieleza Abiy mbele ya Bunge.

Kwa miaka kadhaa, Ethiopia na Misri zimekuwa katika mvutano mkali kuhusu bwawa hilo, ambapo Misri imekuwa ikieleza hofu zake kuwa mradi huo unaweza kupunguza kiwango cha maji ya Mto Nile inayokitegemea kwa asilimia kubwa kwa matumizi ya nyumbani, kilimo na viwanda. Sudan pia imekuwa na mashaka kuhusu athari za kiusalama na kiikolojia zitakazotokana na mradi huo.

Tangazo la kukamilika kwa bwawa hilo linaashiria mwanzo mpya wa mwelekeo wa kisiasa, kiuchumi na kidiplomasia katika ukanda huo wa Afrika Mashariki na Kaskazini. Macho sasa yanaelekezwa kwenye uzinduzi rasmi wa mradi huo na mazungumzo ya kidiplomasia yatakayofuata kati ya Ethiopia, Misri na Sudan.

Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed, ametangaza kukamilika kwa bwawa la umeme lenye utata linalojengwa kwenye Mto Nile, na kusema kuwa hatua hiyo ni mafaniki...

Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ameiamuru nchi hiyo kusitisha ushirikiano wake na Shirika la Kimataifa la Kudhibiti Ngu...
03/07/2025

Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ameiamuru nchi hiyo kusitisha ushirikiano wake na Shirika la Kimataifa la Kudhibiti Nguvu za Atomiki (IAEA) kufuatia mashambulizi yaliyofanywa na Marekani dhidi ya vinu vya nyuklia vya taifa hilo. Hatua hii inakuja siku chache tu baada ya Bunge la Iran kupitisha muswada unaositisha rasmi ushirikiano wa kidiplomasia na kiufundi na shirika hilo linalosimamia matumizi salama ya nishati ya atomiki duniani.

Mpaka sasa, haijafahamika wazi hatua hiyo ya Iran itaathiri vipi shughuli za IAEA nchini humo, hasa ikizingatiwa kuwa shirika hilo limekuwa likihusika kwa karibu na ufuatiliaji wa mpango wa nyuklia wa Iran kwa miaka kadhaa. IAEA yenyewe haijatoa tamko lolote kuhusu tangazo hilo la Tehran. Hata hivyo, hatua hii inaashiria kuzorota zaidi kwa uhusiano kati ya Iran na jumuiya ya kimataifa, hasa Marekani, ikichukuliwa kuwa uamuzi huo umetangazwa katika kipindi cha mvutano mkali wa kijeshi na kisiasa.

Akizungumza baada ya kutoa agizo hilo, Rais Pezeshkian alisisitiza kuwa Iran haina budi kuchukua hatua za kulinda uhuru wake wa kisayansi na kisiasa. "Hatutaendelea kushirikiana na shirika ambalo halikuweza kuzuia mashambulizi dhidi ya haki yetu ya msingi ya kuwa na teknolojia ya nyuklia kwa matumizi ya amani," alisema Pezeshkian, akitoa ujumbe mzito wa kukosoa kile alichokiita "ubaguzi wa kimataifa dhidi ya Iran".

Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ameiamuru nchi hiyo kusitisha ushirikiano wake na Shirika la Kima...

Katika kongamano kubwa linalofanyika Seville, nchini Uhispania, zaidi ya mataifa 100 yameahidi kushirikiana kutafuta sul...
02/07/2025

Katika kongamano kubwa linalofanyika Seville, nchini Uhispania, zaidi ya mataifa 100 yameahidi kushirikiana kutafuta suluhisho la kudumu kwa tatizo la mzigo wa deni linaloendelea kuyakandamiza mataifa yanayoendelea. Wataalamu, viongozi wa kisiasa na wachumi kutoka pande zote za dunia wameelezea wasiwasi wao kuwa hali hiyo ni “bomu linalosubiri kulipuka,” huku kila nchi ikijaribu kusawazisha matarajio na uwezo wake katika kuchangia mabadiliko. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, aliwaambia wajumbe wa kongamano hilo kwamba: “Mzigo wa madeni unaulemaza ulimwengu unaoendelea,” akisisitiza kuwa sasa ni wakati wa hatua za pamoja katika kuyasaidia mataifa masikini kujinasua katika lindi hilo la kiuchumi.

Takwimu zilizowasilishwa kwenye kongamano hilo zimeonyesha jinsi hali inavyozidi kuwa mbaya. Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, deni la nje la nchi masikini zaidi duniani limeongezeka zaidi ya mara tatu katika kipindi cha miaka 15, huku mataifa hayo yakilazimika kulipa zaidi ya dola trilioni 1.4 kila mwaka kwa wakopeshaji. Hali hiyo imezifanya nchi nyingi kutumia fedha nyingi zaidi kwenye malipo ya riba kuliko katika huduma muhimu k**a afya. Ripoti iliyoandaliwa kwa maagizo ya hayati Papa Francis na kusimamiwa na mshindi wa Tuzo ya Nobel, Joseph Stiglitz, imeeleza kuwa “zaidi ya watu bilioni tatu wanaishi katika nchi ambazo hulipa fedha nyingi kwenye riba kuliko zinazoingizwa kwenye sekta ya afya.”

Ahadi za kusaidia hazikuishia kwenye maneno tu. Uhispania, mwenyeji wa kongamano hilo, imejitokeza kuonyesha mfano kwa kuahidi kupeleka dola bilioni 1.9 zaidi kwa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), ikiwa ni sehemu ya juhudi za kusaidia nchi zinazoendelea.

Kiongozi wa Kenya, Rais William Ruto na mwenzake wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, waliungana katika kutoa wito wa mageuzi ya haraka katika mfumo wa kifedha wa kimataifa ili kutatua mzunguko wa madeni na ukosefu wa usawa wa kifedha duniani. Waraka wa pamoja uliopitishwa na washiriki unashauri kuwepo kwa vifungu vipya vya mikopo vitakavyoruhusu nchi kusitisha urejeshaji wa mikopo kwa muda wakati zinapokumbwa na majanga k**a vile mafuriko, njaa au matetemeko ya ardhi.

Uchaguzi Mkuu 2025: Moto Waendelea Kuwaka!Hali ya siasa nchini imechangamka huku vigogo wa zamani, wanahabari, wajasiria...
01/07/2025

Uchaguzi Mkuu 2025: Moto Waendelea Kuwaka!

Hali ya siasa nchini imechangamka huku vigogo wa zamani, wanahabari, wajasiriamali na vijana wa UVCCM wakijitokeza kwa kasi kuchukua fomu za kugombea ubunge na udiwani kupitia CCM.

Kutoka kwa Ester Bulaya hadi Paul Makonda, kutoka kwa wanahabari k**a Baruan Muhuza, Salim Kikeke hadi viongozi wa UVCCM, CCM ya 2025 ni mchanganyiko wa uzoefu, ujana na ushawishi mpya. Je, unadhani nani atapita?

Kusoma zaidi makala haya bonyeza kiungo hapa chini



https://dostmedia.co.tz/majimboni-kumewaka-moto-watia-nia-waongezeka-ccm/

Zaidi ya watu milioni 14 duniani kote wako katika hatari ya kufariki dunia kufikia mwaka 2030, kufuatia uamuzi wa Mareka...
01/07/2025

Zaidi ya watu milioni 14 duniani kote wako katika hatari ya kufariki dunia kufikia mwaka 2030, kufuatia uamuzi wa Marekani chini ya utawala wa Rais Donald Trump kupunguza msaada wa kibinadamu kwa nchi zinazoendelea. Takwimu hizi zimetolewa katika utafiti mpya uliotangazwa leo na jarida la tiba la Lancet, likionyesha hali ya kutisha inayoikumba sekta ya misaada ya kimataifa.

Kati ya watu wanaotajwa kuwa hatarini, theluthi moja ni watoto wadogo, jambo linalozua hofu kubwa kwa mustakabali wa kizazi kijacho katika nchi maskini. Utafiti huo wa kimataifa unaonyesha kuwa kati ya mwaka 2001 hadi 2021, ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID) ulisaidia kuzuia vifo vya watu milioni 91 katika mataifa yanayoendelea.

Hata hivyo, hali hiyo imebadilika kufuatia hatua ya Trump kurejea madarakani mwezi Januari na kupunguza kwa kiasi kikubwa mgao wa misaada. Kabla ya hatua hiyo, USAID ilikuwa ikichangia zaidi ya asilimia 40 ya misaada ya kibinadamu duniani.

Utafiti huo umetolewa wakati viongozi wa kimataifa na wadau wa sekta binafsi wakikutana nchini Uhispania kwa ajili ya kujadili njia za kuimarisha misaada ya kimataifa, huku wakikabiliana na changamoto za kupungua kwa rasilimali na kuongezeka kwa mahitaji ya kibinadamu.

Zaidi ya watu milioni 14 duniani kote wako katika hatari ya kufariki dunia kufikia mwaka 2030, kufuatia uamuzi wa Marekani chini ya utawala wa Rais Donald Tr...

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amefutilia mbali uwezekano wa kurejea kwenye meza ya mazungumzo na Marek...
01/07/2025

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amefutilia mbali uwezekano wa kurejea kwenye meza ya mazungumzo na Marekani katika siku za karibuni, akisisitiza kuwa Tehran inahitaji hakikisho thabiti kuwa haitashambuliwa tena.

Katika mahojiano maalum na kituo cha habari cha CBS Evening News ya Marekani, Araghchi alijibu matamshi ya Rais Donald Trump aliyedokeza kuwa kuna uwezekano wa kurejea kwa mazungumzo ya nyuklia kati ya mataifa hayo mawili mapema wiki hii. Hata hivyo, Araghchi alisema licha ya mlango wa diplomasia kubaki wazi, Iran bado inahitaji muda zaidi na dhamana ya usalama.

Kauli hii imekuja kufuatia mashambulizi ya kijeshi yaliyotekelezwa na Israel dhidi ya maeneo ya nyuklia na miundombinu ya kijeshi ya Iran, ambapo Marekani pia ilishiriki kwa kushambulia maeneo matatu muhimu ya nyuklia: Fordo, Natanz na Isfahan mnamo Juni 21.

Mgogoro huu unaendelea kuzua wasiwasi mkubwa wa kiusalama katika ukanda wa Mashariki ya Kati, huku majaribio ya kidiplomasia yakisuasua, na hatma ya makubaliano ya nyuklia baina ya Marekani na Iran ikisalia katika mashaka.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amefutilia mbali uwezekano wa kurejea kwenye meza ya mazungumzo na Marekani katika siku za karibuni, akisisit...

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akipanda mti wa kumbukumbu pamoja na Rais wa Burundi, Évari...
28/06/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akipanda mti wa kumbukumbu pamoja na Rais wa Burundi, Évariste Ndayishimiye kabla ya ufunguzi wa Kiwanda cha mbolea cha ITRACOM Fertilizers Limited kilichopo Nala, Jijini Dodoma, tarehe 28 Juni, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akipanda mti wa kumbukumbu pamoja na Rais wa Burundi, ...
28/06/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akipanda mti wa kumbukumbu pamoja na Rais wa Burundi, Évariste Ndayishimiye kabla ya ufunguzi wa Kiwanda cha mbolea cha ITRACOM Fertilizers Limited kilichopo Nala, Jijini Dodoma, tarehe 28 Juni, 2025.

Mjumbe wa NEC, Richard Kasesela amechukua fomu kuwania ubunge jimbo la Rungwe lililopo mkoani Mbeya leo Juni 28, 2025.Ji...
28/06/2025

Mjumbe wa NEC, Richard Kasesela amechukua fomu kuwania ubunge jimbo la Rungwe lililopo mkoani Mbeya leo Juni 28, 2025.

Jimbo hilo ambalo linaongozwa na Mbunge Anton Mwantona hadi sasa huku likitajwa kunyemelewa na Gwamaka Mwafwenga aliyekuwa mkurugenzi wa NEMC, yupo pia Eliud Mwaiteleke, Aliko Mwaiteleke na wengine.

Mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi Mch. Peter Msigwa amekuwa mwanachama wa Kwanza wa Chama hicho Iringa Mjini kujitokeza ...
28/06/2025

Mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi Mch. Peter Msigwa amekuwa mwanachama wa Kwanza wa Chama hicho Iringa Mjini kujitokeza na kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa na Chama chake kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Iringa Mjini.

Msigwa, Mwanasiasa wa zamani wa Chadema na Mbunge wa Jimbo hilo kwa kipindi cha Miaka kumi kupitia Chadema, mapema mwaka huu ndipo alipojiunga na CCM na kupokelewa na Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Katibu Mkuu Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ambaye pia ni Mgombea mwenza wa Rais Samia katika uchaguzi wa mwezi Oktoba.

Kuingia kwenye Kinyang'anyiro hicho kwa Mch. Msigwa kumeibua ushindani mwingine mkubwa kwenye Jimbo hilo kati yake na Mbunge wa sasa Mhe. Jesca Msambatavangu, ambaye ameongoza kwa kipindi kimoja na akitangaza kutetea nafasi yake tena.

Nukuu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan Leo Juni 27, 2025 wakati akihitimisha shughul...
27/06/2025

Nukuu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan Leo Juni 27, 2025 wakati akihitimisha shughuli za Bunge la 12.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Juni 27, 2025, amehitimisha rasmi shughuli za Bun...
27/06/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Juni 27, 2025, amehitimisha rasmi shughuli za Bunge la 12, ambalo linatarajiwa kuvunjwa rasmi Agosti 3, 2025.

Akihutubia wabunge katika hotuba yake, Rais Samia ameeleza mafanikio ambayo yamepatikana, hatua zilizopigwa, na mwelekeo wa maendeleo ya Tanzania na kubainisha mamlaka aliyonayo chini ya Ibara ya 90, kifungu kidogo cha pili cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.

"Kwa mamlaka niliyonayo chini ya ibara ya 90 ya kifungu kidogo cha pili ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, sasa ninayo heshima kutamka shughuli za Bunge la 12 zimehitimishwa leo, na Bunge litavunjwa rasmi tarehe 3, Agosti 2025," amesema Rais Samia.

Bunge la 12 lilifunguliwa rasmi Novemba 13, 2020, na Rais wa Awamu ya Tano, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli. Baada ya kifo cha Hayati Rais Magufuli, Rais Samia alilihutubia Bunge hilo kwa mara ya kwanza mnamo Aprili 22, 2021.

Address

Mbezi Beach
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dost Media Tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share