18/10/2025
Wanafunzi kisiwani Zanzibar nao wameitaka serikali ijayo kuhakikisha wanajifunza katika mazingira salama na yenye ustawi, wakisisitiza umuhimu wa kuwa na madarasa bora, chakula shuleni, na usalama wa wanafunzi.
Wamesema kuwa ingawa baadhi ya shule ziko katika hali nzuri, nyingine bado zinakabiliwa na changamoto za miundombinu duni na mazingira hatarishi ambayo yanadhoofisha ari ya kujifunza.
Kadri uchaguzi mkuu unavyokaribia, walimu na wanafunzi Zanzibar wamekuwa wakitoa sauti zao zenye matumaini na matarajio kwa serikali ijayo — wakitaka elimu iwe miongoni mwa maeneo yatakayopewa kipaumbele cha juu kwa ajili ya ustawi wa taifa.
_____________
Fuatilia kwenye YouTube Channel na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.