Dost Media Tz

Dost Media Tz We aim to tell a story that matters

25/08/2025

Tanzania imeanza ujenzi wa maabara kubwa na ya kisasa ya uchunguzi wa sampuli za madini, ambayo itakuwa kubwa kuliko zote katika nchi za Afrika Mashariki na Kati. Maabara hii itatoa huduma za kimaabara kwa ubora wa hali ya juu na kwa haraka kwa wadau wa sekta ya madini nchini.

Hayo yameelezwa leo na Waziri wa Madini, Mh. Anthony Mavunde, wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa maabara hiyo katika eneo la Kizota, Jijini Dodoma.

“Tunamshukuru Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa kinara wa mageuzi makubwa katika sekta ya madini na kwa kuandika historia ya ujenzi wa maabara hii ya kisasa, miaka 100 tangu kuanzishwa kwa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) mwaka 1925.

Leo tunaandika historia kwa kuanza ujenzi wa maabara kubwa itakayokuwa na mitambo na vifaa vya kisasa vinavyotoa huduma za kimaabara ndani na nje ya nchi. Hii itakuwa ni ukombozi mkubwa kwa wadau wa sekta ya madini kupata taarifa sahihi za kimaabara kwa wakati na zenye ubora wa hali ya juu. Ni imani yangu maabara hii itachochea ukuaji na maendeleo ya sekta ya madini,” alisema Mavunde.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST), Dkt. Notka Huruma Batenze, amesema maabara hii ya kisasa ya uchunguzi wa sampuli za madini italeta tija kubwa kwa wadau wa sekta ya madini na kurahisisha upatikanaji wa huduma hii muhimu kwa maendeleo ya sekta ya madini.

Gharama za ujenzi wa maabara hii zinakadiriwa kufikia shilingi bilioni 14.3, huku muda wa kukamilisha ujenzi ukikadiria kuwa siku 690.

Takribani watu 20, wakiwemo waandishi wa habari watano wa vyombo vya kimataifa, wameuawa katika shambulio la anga la Isr...
25/08/2025

Takribani watu 20, wakiwemo waandishi wa habari watano wa vyombo vya kimataifa, wameuawa katika shambulio la anga la Israel katika Hospitali ya Nasser, Gaza Kusini. Miongoni mwa waliopoteza maisha ni mpiga picha wa Reuters Husam al-Masri na mwandishi huru wa Associated Press, Mariam Dagga. Waandishi wengine ni Mohammed Salameh wa Al Jazeera na mpiga picha Muath Abu Taha na Ahmed Abu Aziz.

Mashuhuda wamesema shambulio la kwanza liliua kadhaa, kisha shambulio la pili likalenga waokoaji waliokuwa wakihudumia majeruhi. Video kutoka eneo la tukio zinaonyesha hali ya taharuki, moshi ukifuka juu ya jengo la hospitali huku waathirika wakikimbia kuokoa maisha yao. Jeshi la Israel limesema linachunguza tukio hilo, likisisitiza kuwa “halilengi waandishi wa habari moja kwa moja”.

Shambulio hili linakuja wiki mbili baada ya waandishi sita, wakiwemo wanne wa Al Jazeera, kuuawa karibu na Hospitali ya al-Shifa mjini Gaza.

Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa imelilaani tukio hilo na kulitaja k**a ukiukaji mkubwa wa sheria za kimataifa, huku Kamati ya Kulinda Waandishi wa Habari (CPJ) ikitaka Israel ithibitishe madai yake dhidi ya waandishi wanaolengwa.

__________________________
Fuatilia  kwenye YouTube Channel   na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

25/08/2025

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema elimu ya watu wazima sio tu elimu ya masomo ya kawaida, bali ni zana muhimu ya maendeleo endelevu, kwani inachangia kipato, ustawi wa kijamii, afya na ushiriki wa kiraia na kuongeza kuwa uzoefu duniani unaonesha kwamba elimu ya watu wazima ni chombo muhimu cha maendeleo ya kijamii, kiuchumi na binafsi.

Amesema hayo leo Jumatatu (Agosti 25, 2025) alipofungua kongamano la kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima inayofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

“Elimu si tukio la muda bali ni safari endelevu ya kujifunza katika maisha yote, elimu ya Watu wazima si kwa ajili ya watu wazima pekee, bali hata kundi la vijana wanaweza kujiunga na kunufaika na program mbalimbali za ujuzi zinazotolewa na taasisi hiyo”.

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Serikali inatambua kwamba katika kipindi cha nusu karne iliyopita, Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima imepiga hatua kubwa na kutoa mchango wa kipekee katika maendeleo ya Taifa.

“Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima imekuwa ikishauri Serikali kwenye maeneo ya kisera na kitaalamu katika masuala ya elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi iliyosaidia kuwafikia Watanzania wengi zaidi waliokuwa hawajapata fursa ya elimu ya msingi”.

Mheshimiwa Majaliwa ameielekeza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kuhakikisha wanaongeza wigo wa upatikanaji wa elimu ya watu wazima ikiwemo kuwafikia makundi yote nchini hasa maeneo yaliyo pembezoni na yenye changamoto za kijamii na kijiografia.

Pia, ameiagiza Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kwa kushirikiana na wadau waendelee kufanya tafiti za mara kwa mara kuhusiana na elimu ya watu wazima ili kubaini changamoto zinazojitokeza na kuandaa suluhisho bunifu linaloendana na mahitaji halisi ya jamii.

__________________________
Fuatilia kwenye YouTube Channel na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

25/08/2025

Kassim Majaliwa amesema elimu ya watu wazima sio tu elimu ya masomo ya kawaida, bali ni zana muhimu ya maendeleo endelevu, kwani inachangia kipato, ustawi wa kijamii, afya na ushiriki wa kiraia na kuongeza kuwa uzoefu duniani unaonesha kwamba elimu ya watu wazima ni chombo muhimu cha maendeleo ya kijamii, kiuchumi na binafsi.

Amesema hayo leo Jumatatu (Agosti 25, 2025) alipofungua kongamano la kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima inayofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

“Elimu si tukio la muda bali ni safari endelevu ya kujifunza katika maisha yote, elimu ya Watu wazima si kwa ajili ya watu wazima pekee, bali hata kundi la vijana wanaweza kujiunga na kunufaika na program mbalimbali za ujuzi zinazotolewa na taasisi hiyo”.

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Serikali inatambua kwamba katika kipindi cha nusu karne iliyopita, Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima imepiga hatua kubwa na kutoa mchango wa kipekee katika maendeleo ya Taifa.

“Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima imekuwa ikishauri Serikali kwenye maeneo ya kisera na kitaalamu katika masuala ya elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi iliyosaidia kuwafikia Watanzania wengi zaidi waliokuwa hawajapata fursa ya elimu ya msingi”.

Mheshimiwa Majaliwa ameielekeza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kuhakikisha wanaongeza wigo wa upatikanaji wa elimu ya watu wazima ikiwemo kuwafikia makundi yote nchini hasa maeneo yaliyo pembezoni na yenye changamoto za kijamii na kijiografia.

Pia, ameiagiza Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kwa kushirikiana na wadau waendelee kufanya tafiti za mara kwa mara kuhusiana na elimu ya watu wazima ili kubaini changamoto zinazojitokeza na kuandaa suluhisho bunifu linaloendana na mahitaji halisi ya jamii.
__________________________
Fuatilia kwenye YouTube Channel na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

25/08/2025

Mashambulizi ya Israel yaliupiga mji mkuu wa Yemen, Sanaa, tarehe 24 Agosti 2025 na kusababisha vifo vya watu sita na majeruhi 86. Jeshi la Israel lilisema liliwalenga wapiganaji wa Houthi kwa kushambulia maeneo ya kijeshi karibu na Ikulu, vituo viwili vya umeme na ghala la mafuta. Hatua hiyo ilikuwa jibu kwa mashambulizi ya mara kwa mara ya makombora na droni za Houthi kuelekea Israel, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono Wapalestina katika vita vya Gaza.

Mzozo kati ya Israel na Houthi unachimbuka kutoka vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Yemen vilivyoanza 2014, ambapo harakati ya kundi hilo, lenye uhusiano wa karibu na Iran, ilitwaa mji mkuu Sanaa. Tangu kuzuka kwa vita vya Gaza Oktoba 2023, Wahouthi wameongeza mashambulizi ya makombora na droni dhidi ya Israel na kushambulia meli katika Bahari Nyekundu, wakisema wanapigania Wapalestina. Hatua hii imepanua mzozo wa Yemen hadi Mashariki ya Kati kwa upana zaidi.

Israel imejibu mara kadhaa kwa mashambulizi ya anga dhidi ya Yemen, ikiharibu bandari, viwanja vya ndege, na miundombinu ya mafuta. Katika matukio kadhaa, Houthi walirusha makombora yaliyofika maeneo ya Tel Aviv na Ben Gurion Airport, jambo lililolazimisha Israel kuongeza ulinzi wake wa anga na kushirikiana na Marekani kulinda njia za biashara baharini. Hatua hizi zimeonyesha jinsi mzozo wa Yemen unavyochangia kutikisa usalama wa kikanda na kimataifa.

Athari za mzozo huu ni kubwa: raia wa Yemen wanaendelea kuathirika kwa vifo, majeruhi na uharibifu wa miundombinu muhimu, wakati njia za biashara kupitia Bahari Nyekundu zimevurugwa na kuongeza gharama za usafirishaji duniani. Mashambulizi haya yameongeza hofu ya kuenea zaidi kwa vita katika Mashariki ya Kati na kuongeza shinikizo kwa jumuiya ya kimataifa kutafuta suluhisho la kidiplomasia, lakini sisi k**a Afrika tutaathirika vipi k**a mzozo huu ukiendelea kutanuka Zaidi siku za usoni?
__________________________
Fuatilia kwenye YouTube Channel na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuwa Serikali itaendelea kuu...
25/08/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za kuwaandaa vijana wengi zaidi wa Zanzibar kuwa wataalamu wa elimu ya anga.

Dkt. Mwinyi ameyasema hayo alipokutana na wanafunzi watano waliochaguliwa kutembelea makao makuu ya NASA yaliyopo Washington D.C., Marekani, pamoja na kushiriki katika mashindano ya NASA International Space Apps Challenge 2025 yatakayofanyika jijini Ibra, Oman. Mkutano huo umefanyika Ikulu Zanzibar leo tarehe 25 Agosti 2025.

Fursa hiyo imetokana na uwezo mkubwa waliouonesha waliposhiriki katika programu ya Kimataifa ya IASC (International Astronomical Search Collaboration) inayohusu uvumbuzi wa asteroids kwa kushirikiana na NASA (National Aeronautics and Space Administration) ya Marekani.

Jumla ya wanafunzi 22 kutoka Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Karume, Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar na Chuo Kikuu cha Abdulrahman Al-Sumait ambao walishiriki kwa utambulisho wa Zanzibar Space Team na kufanikiwa kugundua asteroids mpya kupitia picha za anga zinazotumwa na NASA kwa programu ya Astrometrica.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Khamis Abdulla Said, amewataja Majid Khalfan Omar, Nadhifa Mashaka na Is-haka Harith Salim kuwa watatembelea makao makuu ya NASA nchini Marekani, huku Mulhat Abdallah na Feisal Issa Minchoum wanatarajiwa kuhudhuria Hackathon nchini Oman.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya Royal Astronomy and Space Society, Bi. Amina Ahmad, amesema wanakusudia kuanzisha utalii wa anga Zanzibar pamoja na kuzindua programu maalum za mafunzo kwa wanafunzi kutoka skuli mbalimbali ili kujifunza taaluma hiyo.

Zoezi zima limeratibiwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa kushirikiana na asasi ya kiraia ya Royal Astronomy and Space Society .a.s.s_tz na Eng. Abdulwahab Al Busaidi kutoka Oman Astronomical and Space Society.

Katika ziara hiyo inayotarajiwa kuanza Oktoba 2025, wanafunzi watapewa mafunzo kuhusu sayansi ya anga, uvumbuzi na teknolojia mbalimbali zitakazowawezesha kuimarika kitaalamu na kitaaluma.

__________________________
Fuatilia  na tembelea website www.dostmedia.co.tz

Msanii wa muziki wa bongo fleva nchini Tanzania Juma@jux amefanikiwa kupata mtoto wake wa kwanza wa kiume na mke wake pr...
25/08/2025

Msanii wa muziki wa bongo fleva nchini Tanzania Juma@jux amefanikiwa kupata mtoto wake wa kwanza wa kiume na mke wake priscy ambaye pia ni msanii wa huko nchini Nigeria.

Mtoto huyo amepewa jina la Raheem Mkambala ambapo hadi sasa amevuna followers 136K ndani ya masaa kadhaa kwenye ukurasa wake wa Instagram kukiwa na post moja.

Mama mzazi wa priscy kupitia mtandao wa instagram, ametoa pongezi kwa binti yake na kumtakia kila la kheri katika malezi ya mtoto wake huyo wa pekee.

Jux na Priscy walifunga ndoa yao ya kifahari na iliyozua gumzo duniani miezi kadhaa iliyopita na kuwa mke na mume halali na hatimaye kwa sasa wanaenda kuanza ukurasa wao mpya wa kuwa baba na mama kupitia mtoto wao huyo Raheem.
__________________________
Fuatilia  kwenye YouTube Channel   na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

25/08/2025

Msanii wa Bongo Fleva amesambaza tabasamu kwa kuwapa zawadi wanafunzi na mwalimu walioimba nyimbo yake ya k**a njia ya kujifunza shuleni.

Mbosso kupitia video ambayo amepakia kwenye mtandao wa Instagram ameandika "Takribani Kilometa 298 na zaidi kutoka Dar Es Salaam hadi kufika Wilaya ya Muheza ( Muheza Mjini ) hazikutosha kumfikia Mwalimu Wetu wa .

Ikatulazimu tena kuzitafuna Kilometa zaidi ya 40 Kuelekea Juu Kabisa Milimani Katika Kijiji Cha KAZITA ili tuweze Kumfikia Mwalimu JAO MABRUCK KALESI na Wanafunzi Wa Shule Ya Msingi KAZITA.

Lengo ni kuthamini na kuwafikiashia Pongezi na Zawadi k**a Mrejesho wa Shukrani kwa Kuufanya Wimbo Wetu Wa kuwa Sehemu ya Hamasa ya kufundishia wanafunzi na kuwatia Moyo Kwenye Masomo Yao Wimbo huu wa uliobadirishwa kuwa wimbo wa Shule Sasa tumeshuhudia ukitumika na Walimu mbalimbali kufundishia wanafunzi na kuwapa hamasa ya Ufaulu kwenye Masomo Yao.

Pongezi Nyingi Zikufikie Mwalimu KALESI .kalesi na Wanafunzi wote wa Shule Ya Msingi KAZITA kwa Ubunifu huu na Mungu Awabariki Sana.
_______________
Fuatilia kwenye YouTube Channel na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

25/08/2025

Aliyekuwa Mbunge wa Tanga Mjini, Ummy Mwalimu, amewataka wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Tanga kuheshimu maamuzi yaliyofanywa na Halmashauri Kuu ya CCM ya kumteua Kassim Amari Mbaraka kuwa mgombea wa jimbo hilo katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Akizungumza na waandishi wa habarileo Agosti 25, 2025 jijini Dar es Salaam,Ummy amesisitiza kumuunga mkono mgombea huyo na kuondoa makundi ndani ya chama ili kuhakikisha CCM inaibuka na ushindi.

“Pale ambapo chama tayari kimefanya maamuzi ya kumteua mtu kuwa mgombea wa CCM katika uchaguzi, wajibu wetu sisi sote ni kuheshimu uamuzi huo, Ninawaomba sana ndugu zangu kumuunga mkono ndugu yetu Kassim Amari Mbaraka ambaye ameteuliwa na chama chetu kuwa mgombea wetu wa Jimbo la Tanga Mjini.” Amesema Mwalimu.

Kauli hiyo ya Ummy Mwalimu inakuja baada ya wanachama wa CCM Tanga, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Tawi la Chungurira, Mwinyi Zahoro Bakari, kuandamana kupinga uamuzi wa kumteua Mbaraka, hasa ikizingatiwa kuwa Ummy aliongoza kwa kura nyingi katika kura za maoni zilizofanyika Agosti 4, 2025.

Katika kura za maoni Ummy alishika nafasi ya kwanza akipata kura 5,750 kati ya kura halali 10,176. Aliyeshika nafasi ya tatu, Kassim Mbaraka (Makubel) alipata kura 80 na ndiyo amepitishwa na chama hicho kupeperusha bendera ya Jimbo hilo.
__________________________
Fuatilia kwenye YouTube Channel na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

Klabu ya Olympique Marseille wameanza mazungumzo ya awali na Real Madrid kwa lengo la kumsajili kiungo wa kati Dani Ceba...
25/08/2025

Klabu ya Olympique Marseille wameanza mazungumzo ya awali na Real Madrid kwa lengo la kumsajili kiungo wa kati Dani Ceballos.

Klabu hiyo ya Ufaransa inamsaka Ceballos kwa mkopo, huku wakiwa na mpango wa kumnunua kabisa mwishoni mwa msimu, Kutokana na dili hilo Real Madrid tayari wana masharti yao maalum na pili, maamuzi ya mwisho yatategemea Ceballos mwenyewe k**a atakubali kujiunga na Marseille.

Ceballos amekuwa na muda mgumu kupata nafasi ya kudumu katika kikosi cha Real Madrid kinachonolewa na Xabi Alonso huku inatajwa kujiunga na Marseille k**a njia nzuri ya kupata muda zaidi wa kucheza na kurudisha makali yake.
______________________
Fuatilia  kwenye YouTube Channel   na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

Msanii wa Muziki, Ciara kutoka nchini Marekani ameachia kolabo yake na Msaniii wa Tanzania diamond platnumz ikiwa na Jin...
25/08/2025

Msanii wa Muziki, Ciara kutoka nchini Marekani ameachia kolabo yake na Msaniii wa Tanzania diamond platnumz ikiwa na Jina La ‘Low’ ambayo inapatikana kwenye Deluxe Album yake ya ‘Cici’.

Tasnia ya muziki wa Tanzania inakua na kuvuka mipaka kutokana na kolabo hiyo ambapo Ciara ni mmoja wa wasanii wakubwa duniani walioweka rekodi mbalimbali kubwa kwenye Muziki wa R&B na Pop.

Hii sio kolabo ya mara ya kwanza kwa Msanii Diamond P kufanya kwani tayari amefanya na wasanii wakubwa wa kimataifa akiwa k**a Omarion, Neyo, na Rick Ross, jambo linaloonyesha wazi heshima na mafanikio ya muziki wa Bongo Fleva ulimwenguni.
__________________
Fuatilia  kwenye YouTube Channel   na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amewapongez...
25/08/2025

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amewapongeza wanachama wote wa chama hicho walioteuliwa kugombea nafasi za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani katika Uchaguzi Mkuu Mwaka huu Oktoba 29.

Rais samia kupitia mtandao wa Instagram ametoa pongezi hizo kwa kuandika  "Ninawapongeza wanachama wote wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walioteuliwa kugombea nafasi za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani "

 "Ninawatakia kila la kheri katika maandalizi ya safari yenu ya kwenda kuomba ridhaa ya wananchi kupitia sanduku la kura, kwenye Uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba 2025 " Ameongeza Rais Samia.

Rais Samia amehitimisha kwa kuwaombea Mwenyezi Mungu awatangulie, awaongoze na kuwafanikisha kupata ushindi kwenye nafasi hizo.
_________________
Fuatilia  kwenye YouTube Channel   na tembelea website www.dostmedia.co.tz kwa Habari, Michezo, Makala na Uchambuzi.

Address

Mbezi Beach
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dost Media Tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Dost Media Tz:

Share