EXA MEDIA

EXA MEDIA Media

18/06/2025
18/06/2025

Sabri ni mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji mwenye maono wa Sabri knows Enterprises, kampuni inayoongoza katika kuendele...
17/06/2025

Sabri ni mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji mwenye maono wa Sabri knows Enterprises, kampuni inayoongoza katika kuendeleza uchumi wa buluu. Akiwa na uzoefu wa miaka minne, Sabri ameiongoza kampuni hiyo kuzalisha bidhaa bunifu za baharini zinazounga mkono uendelevu wa mazingira na ukuaji wa uchumi. Kutokana na mchango wake mkubwa, Sabri ameteuliwa kuwania Tuzo ya Vijana ya Biashara na Uwekezaji Afrika Mashariki ya mwaka 2025. Kupitia uongozi wake, Sabri Nose Enterprises inaendelea kuwa na mchango mkubwa katika tasnia na jamii kwa ujumla.

:🇬🇧 Jude Bellingham📍 Kiungo – Real Madrid & Uingereza🗓️ Alizaliwa: 29 Juni 2003📍 Stourbridge, EnglandJude Bellingham ali...
22/05/2025

:

🇬🇧 Jude Bellingham
📍 Kiungo – Real Madrid & Uingereza
🗓️ Alizaliwa: 29 Juni 2003
📍 Stourbridge, England

Jude Bellingham alianza kucheza soka akiwa na umri mdogo katika Birmingham City, ambapo alifanya historia kuwa mchezaji mdogo zaidi kuwahi kuchezea timu hiyo ya wakubwa. Akiwa na miaka 17, alijiunga na Borussia Dortmund ya Ujerumani na kuonyesha kiwango cha juu sana.

Mnamo mwaka 2023, alijiunga na Real Madrid, moja ya vilabu vikubwa zaidi duniani. Akiwa Madrid, ameibuka kuwa kiungo bora kabisa, akishinda tuzo ya Mchezaji Bora wa La Liga na UEFA Champions League msimu wa 2023/24. 🎖️

⚽ Ametajwa kuwa mchezaji bora duniani kwa sasa na ana thamani ya juu zaidi sokoni.
🔥 Ana umri mdogo lakini tayari ni gwiji anayepanda kwa kasi!

“Kila safari huanza na mwisho wake. Leo hatuagi tu mchezaji, tunaaga kiongozi, moyo wa timu, na kiungo aliyebadilisha hi...
21/05/2025

“Kila safari huanza na mwisho wake. Leo hatuagi tu mchezaji, tunaaga kiongozi, moyo wa timu, na kiungo aliyebadilisha historia ya Yanga SC – Stephane Aziz Ki.

Tangu alipotua Jangwani mwaka 2021, Aziz Ki hakuwa tu mchezaji wa kawaida. Aligeuka kuwa injini ya kikosi, akichora ramani ya kila mchezo kwa akili, maono na miguu yake ya dhahabu. Amecheza mechi 114 ndani ya jezi ya kijani na njano, akatufungia mabao 54 na kutoa pasi 32 zilizobeba furaha ya mashabiki kote nchini.

Msimu wa 2023/2024 ulikuwa wa kipekee – alipachika mabao 21 na kutwaa kiatu cha dhahabu k**a mfungaji bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Hakusimama hapo. Aliwaongoza Wananchi hadi fainali ya Kombe la Shirikisho la CAF, akifunga penalti muhimu zilizopeleka timu kwenye historia. Hakika, alikuwa jemedari wa vita uwanjani.

Leo tunaaga – si kwa huzuni pekee, bali kwa heshima. Kwa moyo mkunjufu tunamtakia kila la heri huko Morocco alipokamilisha uhamisho wake kwenda Wydad Athletic Club. Ni wakati wake sasa kung’ara kwenye anga la kimataifa, akiwa balozi wa Yanga, Tanzania, na soka la Afrika Mashariki.

Tunajua kuwa Aziz Ki atabaki kuwa sehemu ya historia yetu – historia iliyoandikwa kwa jasho, mapenzi, na ushindi.

Asante kwa kila dakika uliyoivaa jezi ya Wananchi. Asante kwa kutufundisha maana ya mapambano, uongozi, na kujituma. Safari yako haijaisha – bali imebadili njia. Na sisi tutaendelea kuwa mashabiki wako, popote ulipo.

Safari njema Ki. Utakumbukwa daima.

💚💛

Fainali ya CAF Champions League Kuanza kwa Moto Jumamosi! 🔥⚽Jumamosi hii kwenye Uwanja wa Loftus, mabingwa wa Afrika Kus...
20/05/2025

Fainali ya CAF Champions League Kuanza kwa Moto Jumamosi! 🔥⚽

Jumamosi hii kwenye Uwanja wa Loftus, mabingwa wa Afrika Kusini Mamelodi Sundowns wataikaribisha Pyramids FC ya Misri katika mechi ya kwanza ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika. 🇿🇦🆚🇪🇬

📍 Dimba: Loftus Versfeld Stadium
⏰ Muda: Saa 4:00 usiku (10:00 jioni EAT)
📺 Live: Azam Sports 1 HD

Ni wakati wa vigogo wa Afrika kupimana ubavu – Shalulile na Sundowns au Mayele na Pyramids, nani ataanza kunusa harufu ya ubingwa? 🏆

🇹🇿 Historia Fupi ya Tanzania1. Kabla ya Ukoloni (Hadi karne ya 19) • Eneo la Tanzania lilikuwa na jamii mbalimbali za Ki...
20/05/2025

🇹🇿 Historia Fupi ya Tanzania

1. Kabla ya Ukoloni (Hadi karne ya 19)
• Eneo la Tanzania lilikuwa na jamii mbalimbali za Kiafrika zilizojihusisha na kilimo, uvuvi, na biashara.
• Pwani ya Tanzania (hasa Kilwa, Bagamoyo, Zanzibar) ilikuwa kitovu cha biashara ya pembe za ndovu, dhahabu na watumwa – hasa kupitia Waarabu na Waswahili.
• Wafanyabiashara wa Kiarabu, Kihindi, na Wazungu walifika kupitia Bahari ya Hindi.

2. Enzi ya Ukoloni
• 1880s–1919: Eneo la Tanganyika lilikoloniwa na Wajerumani, likijulikana k**a German East Africa.
• 1919–1961: Baada ya Vita ya Kwanza ya Dunia, Uingereza ilichukua Tanganyika kutoka kwa Wajerumani kupitia Mamlaka ya Baraza la Mataifa (League of Nations).
• Zanzibar: Ilikuwa chini ya utawala wa Waarabu wa Oman kwa muda mrefu hadi kuwa koloni la Kiingereza mwaka 1890 (protectorate).

3. Uhuru
• Tanganyika ilipata uhuru: Desemba 9, 1961 chini ya Julius Kambarage Nyerere.
• Zanzibar ilipata uhuru: Desemba 10, 1963, lakini mapinduzi yakafuata Januari 12, 1964, yakiiondoa sultani madarakani.

4. Muungano wa Tanzania
• Aprili 26, 1964, Tanganyika na Zanzibar ziliungana kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
• Muungano huu uliweka msingi wa taifa moja lenye serikali mbili: ya Muungano na ya Mapinduzi Zanzibar.

5. Ujamaa na Kujitegemea
• Nyerere alianzisha sera ya Ujamaa (socialism) mwaka 1967 kupitia Azimio la Arusha.
• Lengo lilikuwa kuleta usawa, maendeleo ya pamoja, na kujitegemea kiuchumi, ingawa baadaye ilikumbwa na changamoto nyingi.

6. Mabadiliko ya Kisiasa na Kiuchumi
• Mwaka 1985, Ali Hassan Mwinyi alichukua uongozi kutoka kwa Nyerere.
• Miaka ya 1990s, Tanzania ilianza mabadiliko ya kisiasa kutoka mfumo wa chama kimoja hadi vyama vingi (1992).
• Pia ilianza mageuzi ya kiuchumi kuelekea soko huria.

7. Tanzania ya Kisasa
• Tangu wakati huo, nchi imeendelea kubadilika kidemokrasia na kiuchumi.
• Marais waliowahi kuongoza ni pamoja na:
• Julius Nyerere (1964–1985)
• Ali Hassan Mwinyi (1985–1995)
• Benjamin Mkapa (1995–2005)
• Jakaya Kikwete (2005–2015)
• John Magufuli (2015–2021)
• Samia Suluhu Hassan (2021–sasa) – Rais wa kwanza mwanamke nchini.

JKT Queens Watwaa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara 2024/25Timu ya soka ya JKT Queens imetwaa ubingwa wa Lig...
20/05/2025

JKT Queens Watwaa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara 2024/25

Timu ya soka ya JKT Queens imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara msimu wa 2024/25 baada ya ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Gets Program. Ushindi huo umeiwezesha JKT Queens kutwaa taji hilo kwa tofauti ya mabao 20, licha ya kuwa na alama sawa na Simba Queens waliomaliza ligi katika nafasi ya pili.

Kwa ushindi huo, JKT Queens wameweka rekodi ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Wanawake mara tano—idadi kubwa zaidi ya ubingwa kuwahi kufikiwa na timu yoyote. Simba Queens wanashika nafasi ya pili katika rekodi ya jumla ya mataji, wakiwa na mara nne.

Katika msimamo wa mwisho wa ligi, JKT Queens na Simba Queens walimaliza wakiwa na alama 47 kila mmoja baada ya michezo 18, lakini JKT Queens waliongoza kwa tofauti ya mabao. Nafasi ya tatu ilichukuliwa na Yanga Princes waliomaliza na alama 37, huku Mashujaa Queens wakifunga orodha ya ‘top four’ kwa alama 31 baada ya michezo 18.

Matokeo ya Mechi za Mwisho:
• Gets Program 0–5 JKT Queens
• Alliance Girls 0–2 Simba Queens
• Yanga Princes 2–2 Ceasiaa Queens
• Mashujaa Queens 3–1 Bunda Queens

Freeman Mbowe Afunguka Sababu ya Ukimya Wake Baada ya Uchaguzi Mkuu 2025Dar es Salaam – Mwenyekiti wa zamani wa chama ch...
20/05/2025

Freeman Mbowe Afunguka Sababu ya Ukimya Wake Baada ya Uchaguzi Mkuu 2025

Dar es Salaam – Mwenyekiti wa zamani wa chama cha upinzani CHADEMA, Freeman Mbowe, amevunja ukimya na kueleza sababu ya kutokuzungumza hadharani tangu Uchaguzi Mkuu wa Januari 22, 2025 ulipomalizika.

Mbowe ameeleza kuwa kwa sasa si nafasi yake tena kutoa matamko kuhusu masuala ya chama, kwani mamlaka yapo mikononi mwa viongozi waliopo madarakani.

“Wanaotakiwa kuzungumza kwa sasa ni viongozi waliokabidhiwa mamlaka na chama,” alisema kwa kifupi.

Akizungumza na JamiiForums.com tarehe 19 Mei 2025, Mbowe alijibu swali la kwanini amekuwa kimya kwa muda mrefu kwa kusema:

“Niseme nini my brother!? Wasemao ni wenye mamlaka… wasije wakadai tunawashawashwa.”

Kauli hii imekuja siku moja tu baada ya Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Pwani, Boniface Jacob “Boni Yai”, kutangaza kuwa hana mpango wowote wa kuhama chama. Katika tamko lake la Mei 18, 2025, Boni Yai alieleza kuwa anahisi baadhi ya makada wanaoihama CHADEMA wakitaja jina la Mbowe, hawajatumwa na mwanasiasa huyo.

Address

KIJICHI
Dar Es Salaam
15129

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when EXA MEDIA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share