Aq Online Tv

Aq Online Tv Tufuate kwaajili ya kupata chakula cha imani yako.

22/07/2025

Wakati watu wengine wakiwa wamewasahau na kuwaacha waendelee kukumbwa na kadhia ya vita, njaa pamoja kiu. Lakini Sheikh Abdul-Qadir Al-Jahdhamy hajazisahau familia zilizopo Gaza, Palestine. Kila siku amekuwa akipeleka misaada mbalimbali ikiwemo vyakula, maji, mavazi, fedha, mahema na kila msaada ambao wanaouhitajia amekuwa akiwafikia kupitia taasisi yake ya Alwadoud Charitable Organization . Familia hizi zimebeba picha yake Sheikh Abdul-Qadir na kuendelea kumshukuru kwa yale ya Kheir ambayo amekuwa akiwafanyia kila siku.

22/07/2025

Ila Bi Aisha alikuwa na wivu ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ Tuambie wewe ukilala na mkeo, umetakiwa uamke utoke, Je utamuamsha mkeo au utamuacha alale?

22/07/2025

Mtu akipanda kitandani anapanda na Tasbihi, kweli?? ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ Mas'hafu kitandani kweli Masheikh? ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

21/07/2025

Huyu ni mtu ambae kimuonekano alionekana k**a ni mwendawazimu au asiyekuwa na akili sawasawa, akawa anatolewa katika eneo hilo, Sheikh akamzuia aliyekuwa anamtoa, amuache palepale. Basi huyu mtu ilifikia hatua hadi ya kulia kwa kuhisi upekee aliopewa na Sheikh kwa kuwekewa hadi mkono kichwani kwake.

21/07/2025

Zaidi ya mataifa 22 ya kiislamu, hayaoni yanayoendelea Ghaza kwa miaka na miaka? Je, wameamua kuwaacha waendelee kuangamizwa? ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ

19/07/2025

Umekuja duniani hauna kitu, na utaondoka hauna kitu

๐—™๐—ถ๐˜€๐˜๐—ผ๐—ป ๐— ๐—ฎ๐˜†๐—ฒ๐—น๐—ฒ ๐—”๐—ฏ๐—ฎ๐—ฑ๐—ถ๐—น๐—ถ ๐——๐—ถ๐—ป๐—ถ, ๐—”๐˜„๐—ฎ ๐— ๐˜‚๐—ถ๐˜€๐—น๐—ฎ๐—บ๐˜‚ โ€“ ๐—๐—ถ๐—ป๐—ฎ ๐—๐—ถ๐—ฝ๐˜†๐—ฎ ๐—ป๐—ถ '๐— ๐—ฎ๐—ต๐—บ๐—ผ๐˜‚๐—ฑ'Mshambuliaji hatari wa kimataifa kutoka Jamhuri ya Kid...
16/07/2025

๐—™๐—ถ๐˜€๐˜๐—ผ๐—ป ๐— ๐—ฎ๐˜†๐—ฒ๐—น๐—ฒ ๐—”๐—ฏ๐—ฎ๐—ฑ๐—ถ๐—น๐—ถ ๐——๐—ถ๐—ป๐—ถ, ๐—”๐˜„๐—ฎ ๐— ๐˜‚๐—ถ๐˜€๐—น๐—ฎ๐—บ๐˜‚ โ€“ ๐—๐—ถ๐—ป๐—ฎ ๐—๐—ถ๐—ฝ๐˜†๐—ฎ ๐—ป๐—ถ '๐— ๐—ฎ๐—ต๐—บ๐—ผ๐˜‚๐—ฑ'

Mshambuliaji hatari wa kimataifa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Fiston Kalala Mayele, ameripotiwa kubadili dini na kujiunga rasmi na dini ya Kiislamu. Taarifa hizi ambazo kwa sasa zinaendelea kusambaa katika mitandao mbalimbali ya habari za michezo, zimepokelewa kwa hisia tofauti na mashabiki wa soka barani Afrika, hususan mashabiki wa zamani wa Yanga SC ambao bado wana kumbukumbu ya mchango wake mkubwa ndani ya klabu hiyo ya Tanzania.

Kwa mujibu wa ripoti kutoka kwa mwandishi maarufu wa michezo wa nchini Misri, Amr El Dardir, Mayele aliamua kubadili dini yake na kuingia katika Uislamu, akichagua jina jipya la Kiislamu Mahmoud Mayele. Inadaiwa kuwa safari yake ya kiroho ilivutwa zaidi na wachezaji wenzake ndani ya klabu yake ya sasa ya Pyramids FC ya Misri, akiwemo Ramadan Sobhi na Karim Hafez, ambao walikuwa bega kwa bega naye katika hatua hiyo muhimu ya maisha yake.

Taarifa zinaeleza kuwa mabadiliko haya yalifanyika wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, kipindi ambacho Waislamu kote duniani hujikita katika ibada na tafakari ya kina kuhusu maisha na imani yao. Hata hivyo, mpaka sasa Mayele mwenyewe hajatoa tamko rasmi hadharani, wala klabu ya Pyramids haijathibitisha au kutoa taarifa ya moja kwa moja kuhusu suala hilo.

Mashabiki wengi wameonesha mshik**ano na heshima kwa mchezaji huyo, wakiamini kuwa kila mtu ana haki ya kufanya maamuzi ya kiimani kulingana na safari yake ya kiroho. Wengine wamepongeza hatua hiyo k**a ishara ya unyenyekevu, utulivu wa kiroho, na kuimarika kwa uhusiano wake binafsi na Mungu.

Mayele, ambaye alitamba vikali akiwa na klabu ya Yanga SC kwa kufunga mabao mengi muhimu na kusaidia timu hiyo kutwaa mataji kadhaa, hivi sasa anachezea klabu ya Pyramids FC nchini Misri, akiwakilisha vilivyo bara la Afrika katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.

KADHI MKUU WA KENYA, SHEIKH ATHMAN ABDULHALIM HUSSEIN AFARIKI DUNIAJamii ya Waislamu nchini Kenya na Afrika Mashariki kw...
10/07/2025

KADHI MKUU WA KENYA, SHEIKH ATHMAN ABDULHALIM HUSSEIN AFARIKI DUNIA

Jamii ya Waislamu nchini Kenya na Afrika Mashariki kwa ujumla imetikiswa na taarifa za msiba wa ghafla wa Kadhi Mkuu wa Kenya, Sheikh Athman Abdulhalim Hussein, aliyeaga dunia asubuhi ya leo akiwa nyumbani kwake katika eneo la Tudor, Mombasa.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Imam wa Msikiti wa Jamia, Sheikh Jamaludin Osman, Kadhi Mkuu alifariki dunia mapema leo na mazishi yake yanatarajiwa kufanyika Mombasa baada ya Sala ya Alasiri, kwa mujibu wa taratibu za dini ya Kiislamu.

โ€œHakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu na hakika kwake tutarejea. Ninasikitika kuwajulisha kuwa Kadhi wetu Mkuu, Sheikh Abdulhalim Hussein, ameaga dunia asubuhi ya leo akiwa nyumbani kwake hapa Mombasa,โ€ alisema Sheikh Jamaludin.

ASSALAAMU ALAIKUM WARAHMATULLAH WABARAKAATUHBaraza Kuu la Wanawake wa Kiislam Tanzania, Mkoa wa Dar es Salaam, linayo fu...
04/07/2025

ASSALAAMU ALAIKUM WARAHMATULLAH WABARAKAATUH

Baraza Kuu la Wanawake wa Kiislam Tanzania, Mkoa wa Dar es Salaam, linayo furaha kuwaalika kina mama na mabinti wote katika Mhadhara mkubwa, utakaoongozwa na Sheikh Hassan Ahmed kutoka Malindi, Kenya ๐Ÿ•Œ

๐Ÿ—“๏ธ Tarehe: Ijumaa, Julai 4, 2025
๐Ÿ•“ Muda: Baada ya alasiri
๐Ÿ“ Mahali: Masjid Taqwa - Ilala Bungoni, Dar es Salaam

Katika mhadhara huu tutapata:
โœจ Mawaidha yenye kugusa nyoyo
๐Ÿ“– Elimu juu ya nafasi ya mwanamke katika Uislam
๐Ÿคฒ Dua na nasaha kutoka kwa mgeni maalum
๐Ÿค Fursa ya kuungana na akina mama wenzetu kwa ajili ya kumcha Allah

๐Ÿง•๐Ÿฝ Tukio hili ni mahsusi kwa kina mama na mabinti wa Kiislam, hivyo usikose!

๐Ÿ“ž Kwa maelezo zaidi wasiliana na:
Ukht Fatma Mdidi โ€“ โ˜Ž๏ธ +255 715 860 120

โžก๏ธ Wote mnakaribishwa kwa moyo mkunjufu!

TANICE WAFANYA DUA YA KULIOMBEA TAIFA LEO TAREHE 29-06-2025Taasisi ya Tanzania Annujum Islamic Center (TANICE) leo tareh...
29/06/2025

TANICE WAFANYA DUA YA KULIOMBEA TAIFA LEO TAREHE 29-06-2025

Taasisi ya Tanzania Annujum Islamic Center (TANICE) leo tarehe 29 Juni 2025 imeendesha dua maalum ya kuliombea Taifa, katika kituo chao cha mafunzo kilichopo Temeke, Dar es Salaam. Hii ni mara ya tatu mfululizo kwa taasisi hiyo kuandaa tukio hili kila mwaka k**a sehemu ya utamaduni wao wa kuombea amani, mshik**ano na maendeleo ya nchi.

Hafla hiyo imehudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini, wanajamii na wawakilishi wa mashirika mbalimbali. Miongoni mwa wageni mashuhuri ni aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Diaspora Tanzania, Mhe. Lee Saydou Kiwool.

Tukio hilo limeambatana na hotuba za hamasa, mawaidha ya kiroho na sala za pamoja, likiwa ni kielelezo cha mshik**ano wa kidini katika kulijenga Taifa lenye maadili na matumaini.

๐——๐—ธ๐˜. ๐— ๐˜„๐—ถ๐—ป๐˜†๐—ถ ๐—”๐˜‡๐—ถ๐—ป๐—ฑ๐˜‚๐—ฎ ๐—ž๐—ฎ๐—บ๐—ฎ๐˜๐—ถ ๐— ๐—ฎ๐—ฎ๐—น๐˜‚๐—บ ๐˜†๐—ฎ ๐—ž๐˜‚๐˜€๐—ถ๐—บ๐—ฎ๐—บ๐—ถ๐—ฎ ๐— ๐—ฎ๐—ฑ๐—ฟ๐—ฎ๐˜€๐—ฎ ๐—ญ๐—ฎ๐—ป๐˜‡๐—ถ๐—ฏ๐—ฎ๐—ฟRais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mh...
28/06/2025

๐——๐—ธ๐˜. ๐— ๐˜„๐—ถ๐—ป๐˜†๐—ถ ๐—”๐˜‡๐—ถ๐—ป๐—ฑ๐˜‚๐—ฎ ๐—ž๐—ฎ๐—บ๐—ฎ๐˜๐—ถ ๐— ๐—ฎ๐—ฎ๐—น๐˜‚๐—บ ๐˜†๐—ฎ ๐—ž๐˜‚๐˜€๐—ถ๐—บ๐—ฎ๐—บ๐—ถ๐—ฎ ๐— ๐—ฎ๐—ฑ๐—ฟ๐—ฎ๐˜€๐—ฎ ๐—ญ๐—ฎ๐—ป๐˜‡๐—ถ๐—ฏ๐—ฎ๐—ฟ

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameongoza hafla ya uzinduzi wa Kamati ya Kitaifa itakayoshughulikia usimamizi wa Madrasa katika visiwa vya Zanzibar.

Uzinduzi huo umefanyika tarehe 26 Juni 2025 katika viunga vya Afisi ya M***i Mkuu wa Zanzibar iliyopo Mazizini, Mkoa wa Mjini Magharibi, sambamba na hafla ya dhifa ya chakula cha mchana kuadhimisha kuingia kwa mwaka mpya wa Kiislamu 1447 Hijria.

Katika hotuba yake, Dkt. Mwinyi alibainisha kuwa madrasa nyingi zimekuwa zikikabiliwa na changamoto za muda mrefu, ikiwemo mazingira duni ya kujifunzia na maslahi hafifu kwa walimu. Kupitia k**ati hiyo mpya, Serikali inalenga kuweka mikakati madhubuti ya kuboresha hali hiyo.

Aidha, Rais aliitaka Kamati hiyo kuandaa mpango kazi wenye bajeti ya utekelezaji sambamba na mbinu za kutafuta rasilimali fedha, ili kuhakikisha uboreshaji wa madrasa unaenda sambamba na mahitaji halisi ya jamii.

Pia alielezea kuridhishwa kwake na maendeleo ya taasisi za Kiislamu visiwani humo, hasa katika kupunguza migogoro ya kidini na kuboresha huduma. Aliitolea pongezi Afisi ya M***i Mkuu kwa ujenzi wa jengo jipya, akieleza kuwa litasaidia kuinua kiwango cha utoaji huduma.

Katika maelezo yake kwa viongozi wa dini na wananchi, Rais Dkt. Mwinyi aliwasisitiza umuhimu wa kuiombea nchi amani na utulivu, hasa kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Katika tukio hilo, alimkabidhi rasmi M***i Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Saleh Omar Kaabi, Hadidu Rejea za Kamati husika kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu yake.

Katika kuhitimisha siku hiyo, Rais Dkt. Mwinyi alishiriki ibada ya pamoja na waumini wa Kiislamu katika Msikiti wa Jammiu Zinjibar, uliopo Kiembe Samaki, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislamu.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Aq Online Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Aq Online Tv:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share