16/07/2025
๐๐ถ๐๐๐ผ๐ป ๐ ๐ฎ๐๐ฒ๐น๐ฒ ๐๐ฏ๐ฎ๐ฑ๐ถ๐น๐ถ ๐๐ถ๐ป๐ถ, ๐๐๐ฎ ๐ ๐๐ถ๐๐น๐ฎ๐บ๐ โ ๐๐ถ๐ป๐ฎ ๐๐ถ๐ฝ๐๐ฎ ๐ป๐ถ '๐ ๐ฎ๐ต๐บ๐ผ๐๐ฑ'
Mshambuliaji hatari wa kimataifa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Fiston Kalala Mayele, ameripotiwa kubadili dini na kujiunga rasmi na dini ya Kiislamu. Taarifa hizi ambazo kwa sasa zinaendelea kusambaa katika mitandao mbalimbali ya habari za michezo, zimepokelewa kwa hisia tofauti na mashabiki wa soka barani Afrika, hususan mashabiki wa zamani wa Yanga SC ambao bado wana kumbukumbu ya mchango wake mkubwa ndani ya klabu hiyo ya Tanzania.
Kwa mujibu wa ripoti kutoka kwa mwandishi maarufu wa michezo wa nchini Misri, Amr El Dardir, Mayele aliamua kubadili dini yake na kuingia katika Uislamu, akichagua jina jipya la Kiislamu Mahmoud Mayele. Inadaiwa kuwa safari yake ya kiroho ilivutwa zaidi na wachezaji wenzake ndani ya klabu yake ya sasa ya Pyramids FC ya Misri, akiwemo Ramadan Sobhi na Karim Hafez, ambao walikuwa bega kwa bega naye katika hatua hiyo muhimu ya maisha yake.
Taarifa zinaeleza kuwa mabadiliko haya yalifanyika wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, kipindi ambacho Waislamu kote duniani hujikita katika ibada na tafakari ya kina kuhusu maisha na imani yao. Hata hivyo, mpaka sasa Mayele mwenyewe hajatoa tamko rasmi hadharani, wala klabu ya Pyramids haijathibitisha au kutoa taarifa ya moja kwa moja kuhusu suala hilo.
Mashabiki wengi wameonesha mshik**ano na heshima kwa mchezaji huyo, wakiamini kuwa kila mtu ana haki ya kufanya maamuzi ya kiimani kulingana na safari yake ya kiroho. Wengine wamepongeza hatua hiyo k**a ishara ya unyenyekevu, utulivu wa kiroho, na kuimarika kwa uhusiano wake binafsi na Mungu.
Mayele, ambaye alitamba vikali akiwa na klabu ya Yanga SC kwa kufunga mabao mengi muhimu na kusaidia timu hiyo kutwaa mataji kadhaa, hivi sasa anachezea klabu ya Pyramids FC nchini Misri, akiwakilisha vilivyo bara la Afrika katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.