SocialLink Media

SocialLink Media Media House
content creator
based in Tanzania

22/05/2026

Nyota wa zamani wa Klabu ya Manchester United na timu ya Taifa ya Uingereza, Rio Ferdinand aomdoka Tanzania.

22/05/2026

Umati wenye hasira umechoma moto sehemu ya hospitali inayowahudumia wagonjwa wa Ebola mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kufuatia tukio la familia na marafiki wa kijana aliyefariki kuvamia hospitali hiyo na kuchukua mwili wake kwa nguvu kwa ajili ya mazishi.

Kwa mujibu wa taarifa, watu hao walianza kurusha mawe na kuchoma mahema yaliyokuwa yakitumika k**a wodi za kuwahifadhi wagonjwa waliotengwa, hatua iliyosababisha taharuki kubwa katika eneo hilo.

Mamlaka za afya zinasisitiza kuwa miili ya watu waliokufa kutokana na Ebola huwa na hatari kubwa ya kueneza ugonjwa huo, hivyo taratibu maalum za mazishi salama hufuata ili kuzuia maambukizi zaidi.

Tukio hilo limetokea katika hospitali ya Rwampara, iliyoko karibu na mji wa Bunia katika jimbo la Ituri, ambako visa vingi vya Ebola vimeripotiwa.

Kutokana na hali hiyo, wahudumu wa afya wamelazimika kuwekwa chini ya ulinzi wa jeshi huku polisi wakijaribu kurejesha utulivu.

Inaelezwa kuwa kijana huyo alikuwa maarufu katika jamii, jambo lililochangia hasira za wananchi ambao bado wana uelewa mdogo kuhusu hatari ya ugonjwa wa Ebola.

22/05/2026

Wajuzi wa mambo mtuambie.

22/05/2026

Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Bw. Lazaro Twange ameeleza kutoridhishwa na kasi ya mkandarasi anayetekeleza mradi wa maboresho ya Kituo cha Kufua Umeme cha Hale kutokana na kuchelewa kukamilika kwa Mradi huo ulioanza kutekelezwa tangu mwaka 2022.

Bw. Twange ameyasema hayo leo Aprili 22, 2026 wakati wa ziara yake ya ukaguzi katika mradi wa Hale pamoja na mradi wa usafishaji wa bwawa la Mto Pangani iliyopo katika Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga ambapo amemtaka mkandarasi wa Mradi wa Hale kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi huo ikiwa ni pamoja na kuongeza wafanyakazi pamoja na muda wa kufanya kazi ili ukamilike kwa wakati.

“Siridhishwi sana na mwenendo wake. Mkandarasi amewahi kuomba nyongeza ya muda mara mbili na nimepata taarifa kuwa yuko kwenye hatua za kuomba nyongeza nyingine ya tatu. Ndio maana nimekuja kuona kuna nini,” amesema Bw. Twange.

Amesema mradi huo una maeneo saba ya utekelezaji ambapo maeneo mawili tayari yamekamilika huku mengine yakiendelea na utekelezaji.

“Nimezungumza na msimamizi wa mradi, mhandisi mshauri pamoja na mkandarasi na nimewaelekeza wakae pamoja kuhakikisha ifikapo mwisho wa mwezi Julai mradi huu uwe umekamilika,” amesema Bw. Twange

Aidha, kuhusu mradi wa usafishaji wa bwawa la Pangani, Bw. Twange amesema matarajio ya TANESCO ni kuhakikisha kazi hiyo inakamilika ndani ya muda uliopangwa ili kuepusha changamoto zinazoweza kujitokeza wakati wa msimu wa mvua.

“Matarajio yetu ni kutoupitiliza mwaka mmoja ili tumalize kabla ya msimu unaokuja wa mvua,” ameongeza.

Katika hatua nyingine, Bw. Twange amesema TANESCO kwa sasa inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ya umeme nchini yenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni 13.4.

Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Mradi wa Hale Mha. Kulwa Byemelo amesema maagizo yaliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji yatatekelezwa ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati.

“Mradi huu utakapokamilika utaimarisha upatikanaji wa umeme katika wilaya mbalimbali zinazochukua umeme kutoka

22/05/2026

Rio ameyasema hayo leo Mei 22, 2026 Jijini Dar es salaam, wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu ziara yake Nchini, ambapo pia ameshukuru kupewa heshima ya kuwa Balozi wa Utalii wa Tanzania na kusema anatazamia mambo makubwa kupitia nafasi hiyo.

Aidha, Rio amesema Vyombo vya Habari vimezungumza mengi kuhusu ujio wake Nchini, akieleza kuwa ametembelea maeneo mengi Barani Afrika na ataendelea kufanya hivyo, huku akisisitiza kuwa hakuna Mtu mwenye mamlaka ya kumwambia nini afanye au asifanye.

Rio ameongeza kuwa dhamira kubwa ya ujio wake Tanzania ni kuhamasisha Vijana kupitia mchezo wa Soka ambao ndio anaoupenda zaidi

22/05/2026

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amewajibu wale wanahoji kwanini Mchezaji wa zamani wa Timu ya Taifa ya Uingereza Rio Ferdinand,hajachapisha kitu chochote Kwenye mitandao ya kijamii Tokea aje Tanzania.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Mei 22, 20206, Jijini Dar es salaam, Makonda amesema amemuomba asichapishe kwa sasa kuwa yupo Tanzania, akieleza kuwa hilo sio jambo muhimu ikilinganishwa na kazi aliyo nayo ya kuinua vipaji vya Vijana wa Kitanzania.

“Wakati mwingine tunapenda kubeza mambo lakini hatujui nguvu kubwa inayofanywa na Viongozi wetu kufanikisha hayo mambo, ajenda kubwa ilikuwa ni kwanini Rio hajapost kwenye Akaunti yake kuwa yupo Tanzania na Watu wakawa wanamfuatilia kuona ataweka post gani ili waamini yupo Tanzania.” Amesema Makonda

Aidha, ameongeza kuwa mara nyingi Watu hujikita kwenye Mitandao ya Kijamii badala ya kuangalia manufaa ya muda mrefu yanayoweza kupatikana kupitia ushirikiano k**a huo.

22/05/2026

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeiagiza Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia Wakala wa Vipimo (WMA) kuanza kuhakiki vipimo vinavyotumika katika huduma za muda wa maongezi na bando za intaneti ili kuhakikisha wananchi wanapata thamani halisi ya fedha wanazolipia.

Kauli hiyo imetolewa leo Ijumaa Mei 22, 2026 na Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Mjini, Mariam Ditopile, wakati akiwasilisha taarifa ya Kamati kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa mwaka wa fedha 2025/2026 pamoja na maoni ya Kamati kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

Katika taarifa hiyo, Kamati imeeleza kuwa kumekuwepo na malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu uhalisia wa matumizi ya huduma za muda wa maongezi na bando za intaneti wanazonunua kutoka kwa kampuni mbalimbali za mawasiliano.

Kutokana na hali hiyo, Kamati imeishauri Serikali kuhakikisha Wakala wa Vipimo (WMA) unaanza rasmi jukumu la kuhakiki usahihi wa vipimo vinavyotumika katika huduma hizo ili kuimarisha uwazi na kulinda maslahi ya watumiaji.

Kamati imeeleza kuwa hatua hiyo itasaidia kuhakikisha wananchi wanapata huduma zinazolingana na gharama wanazolipia sambamba na kuongeza uwajibikaji kwa watoa huduma za mawasiliano nchini.

21/05/2026

Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuonesha usikivu mkubwa kwa wananchi wa mikoa ya Kusini kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo iliyokuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu. Nape ameyasema hayo leo Alhamisi Mei 21, 2026, dakika chache kabla ya upigaji kura wa Bajeti ya Wizara ya Ujenzi bungeni jijini Dodoma.

Akizungumza bungeni, Nape amesema kuwa, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mtama pamoja na wananchi wa mikoa ya Lindi na Mtwara, anasimama kuishukuru Serikali kwa namna ilivyokuwa sikivu katika kushughulikia changamoto na mahitaji ya wananchi wa Kusini.

“Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mtama na wananchi wa mikoa ya Lindi na Mtwara nasimama hapa kuishukuru sana Serikali sikivu ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kusikia na kuwa sikivu na kututendea mema watu wa Kusini,” alisema Nape.

Ameeleza kuwa Serikali imefanikiwa kushughulikia mambo mbalimbali muhimu yaliyokuwa ni kilio cha wananchi wa maeneo hayo ikiwemo sekta ya korosho, gesi, maendeleo ya Bandari ya Uvuvi pamoja na utekelezaji wa miradi ya elimu na afya.

Mbunge huyo pia amesema, wananchi wa Kusini wamefarijika baada ya Serikali kutoa uhakika wa ujenzi wa Barabara ya Dar es Salaam – Lindi – Mtwara kwa kiwango kinachoridhisha, jambo ambalo litasaidia kukuza uchumi na kurahisisha shughuli za usafirishaji katika ukanda huo.

Aidha, Nape ametumia nafasi hiyo kumshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Serikali yake pamoja na Waziri wa Ujenzi kwa juhudi kubwa wanazoendelea kuzifanya katika kuwaletea maendeleo wananchi wa Kusini mwa Tanzania.

21/05/2026

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, M***a Azzan Zungu amesema viongozi wa Wizara ya Ujenzi wanafanya kazi kubwa na nzuri katika utekelezaji wa majukumu yao.

Akizungumza mara baada ya Bunge kupitisha bajeti hiyo jijini Dodoma, Spika Zungu amempongeza Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, Naibu Waziri Mhandisi Godfrey Kasekenya, Katibu Mkuu pamoja na wataalamu wote wa Wizara hiyo wakiwemo wataalamu wa TANROADS na taasisi nyingine zilizo chini ya Wizara kwa kazi nzuri wanayoifanya katika sekta ya miundombinu nchini.

“Mambo hapa bungeni yamekwenda kwa uhalisia na hoja, na Serikali imejibu kwa hoja. Wabunge na wananchi wameridhika,” alisema Spika Zungu.

Mapema jana Mei 20, 2026 Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega aliwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka wa fedha 2026/2027 ambapo imeomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi 2,564,441,414,000 kwa ajili ya matumizi ya kawaida pamoja na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Akiwasilisha bajeti hiyo, Waziri Ulega alisema kuwa fedha hizo zinalenga kuimarisha utekelezaji wa miradi ya miundombinu nchini hususan katika sekta ya barabara ili kuongeza ufanisi wa usafirishaji na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Kwa mujibu wa makadirio hayo, kati ya fedha zilizoombwa, Shilingi 97,104,935,000 zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya Wizara na taasisi zake, huku Shilingi 2,467,336,479,000 zikielekezwa katika miradi ya maendeleo.

Aidha, kati ya fedha za matumizi ya kawaida, Shilingi 92,209,218,000 ni kwa ajili ya mishahara ya watumishi na Shilingi 4,895,717,000 zimetengwa kwa matumizi mengineyo ya uendeshaji wa shughuli za kila siku.

Kwa upande wa bajeti ya maendeleo, fedha za ndani zimepangwa kuwa Shilingi 1,544,872,147,000 huku fedha za nje zikiwa Shilingi 922,464,332,000. Fedha za ndani zinajumuisha Shilingi 1,047,405,500,000 kutoka Mfuko wa Barabara pamoja na Shilingi 497,466,647,000 kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali.

21/05/2026

Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuonesha dhamira kubwa katika maendeleo ya miundombinu kwa kusaini mikataba takribani 80 yenye thamani ya shilingi trilioni 6 ambayo ipo kwenye hatua mbalimbali za utekelezaji (pipe line).

Ulega amesema hayo leo Alhamisi Mei 21, 2026 wakati akihitimisha hoja ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni.

Amssema katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wa Awamu ya Sita, Rais Samia ameendelea kufanya mageuzi makubwa kwenye sekta ya ujenzi kwa kujenga madaraja pamoja na kilometa 1,495 za barabara za lami nchini kote.

“Katika miaka hii mitano, pamoja na mambo yote ambayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameyafanya kwenye madaraja, kilometa 1495 za lami zilizojengwa ndani ya uongozi wa Awamu ya Sita nchi nzima, pia utaona kwamba amesaini mikataba takribani 80 yenye thamani ya takribani shilingi trilioni 6 ambayo ipo katika pipe line,” alisema Ulega.

Amesema hatua hiyo inaonesha commitment (dhamira ya dhati) kubwa ya Rais Samia katika kuhakikisha taifa linafikia malengo ya maendeleo kupitia uwekezaji mkubwa wa miundombinu ya barabara na madaraja.

Kufuatia hayo, Mhe. Ulega ameeleza kuwa, hatua hiyo inaonesha wazi ni nini Rais Samia anakusudia na wapi anataka kulifikisha taifa hili.

21/05/2026

Mbunge wa Jimbo la Itigi, Yohana Msita amesema wananchi wa jimbo hilo wanamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya barabara kwa kiwango cha lami, akieleza kuwa maendeleo hayo yameleta mabadiliko makubwa katika eneo hilo.

Akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi Bungeni jijini Dodoma leo Alhamisi Mei 21, 2026, Msita amesema Itigi Mjini sasa ina kilometa 10 za barabara za lami, jambo ambalo hapo awali lilionekana kuwa ndoto kwa wananchi wa eneo hilo.

“Mimi namshukuru sana Rais Samia kwa namna ambavyo ametukumbuka watu wa Jimbo la Itigi. Leo hii Itigi Mjini tuna kilometa 10 za lami, jambo ambalo hapo nyuma lilikuwa hadithi,” alisema Msita.

Mbunge huyo amesema serikali kupitia Wizara ya Ujenzi imefanya kazi kubwa katika utekelezaji wa miradi ya miundombinu, huku akieleza kuwa uwekezaji mkubwa wa fedha uliofanyika katika jimbo hilo ni ushahidi wa dhamira ya serikali kuwaletea wananchi maendeleo.

“Nawashukuru Rais na Waziri wa Ujenzi kwa kazi kubwa iliyofanyika, mabilioni ya fedha yamelala pale Itigi. Nishukuru, kwani nisiposhukuru nitajifunza roho mbaya ikizingatiwa mimi ni kijana,” alisema.

Aidha, Msita amesema ujenzi wa barabara ya Noranga hadi Itigi yenye urefu wa kilometa 25 katika barabara kuu inayokwenda Rungwa hadi Makongorosi umekamilika, huku mkandarasi akiendelea na kazi za mwisho za kumalizia mradi huo.

“Tayari kilometa 25 zimekamilika, na mkandarasi sasa anafanya finishing kumalizia barabara hiyo. Tunashukuru sana,” alisema.

Amesema wananchi wa Itigi wanaunga mkono juhudi za serikali katika ujenzi na matengenezo ya barabara, akibainisha kuwa barabara ya Mkiwa–Itigi–Rungwa–Makongorosi yenye urefu wa takribani kilometa 356 ni muhimu kwa uchumi wa maeneo mbalimbali pamoja na shughuli za kijamii na kisiasa za jimbo hilo.

Kwa mujibu wa Msita, barabara hiyo inaunganisha mikoa ya Singida, Tabora, Katavi, Songwe na Mbeya, hivyo kukamilika kwake kwa kiwango cha lami kutasaidia kukuza uchumi wa taifa na kurahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa.

Address

Sinza Mori
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SocialLink Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share