Khidma TV

Khidma TV KHIDMA ONLINE TV, CHANNEL YA KIISLAMU KWA MAWAIDHA ZAIDI TEMBELEA YOUTUBE +255 752 950 350
(1)

27/07/2025

Kabla hujalala soma ayatul kursi utalala na ulinzi wa Allah na shetani hatokusogelea.

27/07/2025

Toba iliyokubaliwa.

Muhadhara wa kina mama.Fatilia muhadhara hu wa kina mama unaoendelea hivi sasa kupitia YouTube Channel ya KHIDMA TV muha...
27/07/2025

Muhadhara wa kina mama.

Fatilia muhadhara hu wa kina mama unaoendelea hivi sasa kupitia YouTube Channel ya KHIDMA TV muhadhara hu unaadaliwa na taasisi ya Faraja Islamic Foundation.

Watoa mada katika muhadhara huo ni.
Sheikh Ramadhan Kwangaya, Mada yake ni Usidharau dhambi yoyote.

Sheikh. Mohammed Mwelekwa - Mada. Uislamu na uzazi wa mpango.

Dr. Zakiyya Ally Kilima - Mada. Changamoto zitokanazo na ujauzito na uzazi.

Usipitwe na mada hizo ingia YouTube Channel ya KHIDMA TV muhadhara upo Mubashara.

Rais Emmanuel Macron. Ufaransa kulitambua rasmi taifa la Palestina mwezi Septemba jambo ambalo litalifanya kuwa taifa la...
27/07/2025

Rais Emmanuel Macron. Ufaransa kulitambua rasmi taifa la Palestina mwezi Septemba jambo ambalo litalifanya kuwa taifa la kwanza la G7 kufanya hivyo.

Katika chapisho kwenye mtandao wa X, Macron alisema tangazo hilo rasmi litatolewa katika kikao cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa huko New York.

Lenye uhitaji mkubwa hii leo ni kukomeshwa kwa vita huko Gaza na raia waokolewe. Amani inawezekana kufikiwa. Tunahitaji usitishaji mapigano mara moja, kuachiliwa kwa mateka wote, na msaada mkubwa wa kibinadamu kwa watu wa Gaza, aliandika.

Maafisa wa Palestina walifurahishwa na uamuzi wa Macron, huku Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akisema hatua hiyo "inaunga mkono ugaidi" kufuatia shambulio la Hamas la tarehe 7 Oktoba 2023 nchini Israel.

Katika chapisho lake kwenye ntandai wa X siku ya Alhamisi, Macron aliandika: "Mkweli kwa ahadi yake ya kihistoria kwa haki na amani ya kudumu katika Mashariki ya Kati, nimeamua kuwa Ufaransa itatambua Jimbo la Palestina.

"Lazima pia tuhakikishe kuondolewa kwa Hamas, na kulinda na kuijenga upya Gaza.

"Mwishowe, ni lazima tujenge Taifa la Palestina, tuhakikishe uwepo wake, na pia kuhakikisha kwa kukubali kuondolewa kwa jeshi na kuitambua kikamilifu Israel, kunachangia usalama wa wote Mashariki ya Kati. Hakuna njia mbadala."

Macron pia aliambatanisha barua kwa Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina Mahmoud Abbas kuthibitisha uamuzi wake huo.

TANZANIA katika kuunga mkono harakati za Ukombozi, kutetea utu, usawa na haki za Binadamu - ni nchi ambayo misingi ya kuundwa kwake ni uwepo wa Taifa Huru la Palestina tangu zama za Serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya Uongozi wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Yasser Arafat wa PLO ambaye Tanzania ilikuwa ni nyumbani kwake. Tanzania imesimama na Wapalestina katika kudai haki ya kuwa na taifa lao na kuweza kujiendesha k**a Binadamu wenye uhuru wa kuamua mambo yao ya msingi. Kuna kipindi katikati palikuwa na wingu baya, lakini limepita kwa haraka ni safari ndefu sana iliyojaa majasho, machozi, damu, machungu, maumivu na gharama kubwa ya maisha - tunalitakia kila la heri Taifa Huru la Palestina

WITO tunatoa wito kwa mataifa na watu wote duniani wafanye hima kulitambua Taifa Huru la Palestina kwa lengo la kuleta amani ya kudumu Mashariki ya Kati, ulimwengu umechoka kila kukicha kusikia mauaji na unyama usimithilika ukitendeka katika eneo hilo la sayari ya dunia.

27/07/2025

Waislamu tuache kulalamika na kujirudisha nyuma ukijidhalilisha watu wataendelea kukudhalilisha.

26/07/2025

Mwenye kusoma ayatul kursi kila baada ya swala yeye na kuingia peponi kinachomzui ni kufa tu.

26/07/2025

Wanangu nikifa msinizike nichomeni moto alafu majivu kayatupeni baharini.

Je watoto watalazimika kutekeleze wosia wa baba yao?Katika mafundisho ya uislamu mtu akifariki azikwe chini ya ardhi.Pia...
26/07/2025

Je watoto watalazimika kutekeleze wosia wa baba yao?

Katika mafundisho ya uislamu mtu akifariki azikwe chini ya ardhi.

Pia katika mafundisho ya uislamu wosia wa mzazi una nafasi kubwa kwa wale walio achiwa wosia.

Mzazi katoa wosia kwa watoto wake nikifa msinizike nichomeni moto na kisha majivu mkatupe baharini. je watoto watekeleze wosia wa baba yao?

Tuambie katika comment, k**a huna jibu endelea kubakia katika mitandao ya Khidma TV tutawaletea majibu.

26/07/2025

Kuna maeneo usithubutu kumtaja kwa ubaya Sheikh Walid utapigwa na wale wanao mpenda.

26/07/2025

Ngumu kumeza, je unajua kua dhambi zako zinaweza kukupeleka Poponi badala ya kwenda motoni? sharti ni mmoja tu fanya hili leo.

Rais wa Zanzibar Dr. Hussein Ali Mwinyi. Ijumaa ya leo amejumuika na waumini wa dini ya Kiislamu Msikiti wa Ijumaa wa Su...
25/07/2025

Rais wa Zanzibar Dr. Hussein Ali Mwinyi. Ijumaa ya leo amejumuika na waumini wa dini ya Kiislamu Msikiti wa Ijumaa wa Sunni Muslim Jamaat Dodoma.

Katika salamu alizotoa baada ya swala ya Ijumaa amewakumbusha waumini wa kuwa amani ni nyenzo muhimu ya ustawi wa kila sekta katika nchi, hivyo ni wajibu wa kila mmoja kuilinda na kuidumisha, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.

Kwa mnasaba huo, Viongozi wa Dini, Wanahabari na Wanasiasa ni miongoni mwa watu wenye ushawishi mkubwa katika jamii, hivyo wana wajibu wa kuwa mstari wa mbele katika kueneza ujumbe wa amani na mshik**ano.

Rais Dr. Hussein Ali Mwinyi amekua na utamaduni wa kujumuika na waumini katika swala za ijumaa na nyeginezo jambo ambalo ni nadra kuliona kwa viongozi wa juu wa nchi katika dunia ya sasa. Mola amuhifadhi na amfanyie wepesi katika majukumu yake.

25/07/2025

Kuna mwanandoa hivi sasa yupo tayar atoe kila kitu ili avunje ndoa yake ndoa nyingi zipo hatarini.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Khidma TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Khidma TV:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share