Khidma TV

Khidma TV KHIDMA ONLINE TV, CHANNEL YA KIISLAMU KWA MAWAIDHA ZAIDI TEMBELEA YOUTUBE +255 752 950 350
(1)

21/07/2025

Tusimwachie shetani taifa la tanzania isitokee wengine wakawazunguka wengine Mungu atakaa pembeni na shetani ataachukua hatamu yake.

SHEKH ALHAD M***A SALUM AMFANYIA WALIMA MWANAE HAFLA HIYO ILIKUA YA HESHIMA SANA  KWA KUHUDHURIWA NA VIONGOZI KIBAO. Wak...
21/07/2025

SHEKH ALHAD M***A SALUM AMFANYIA WALIMA MWANAE HAFLA HIYO ILIKUA YA HESHIMA SANA KWA KUHUDHURIWA NA VIONGOZI KIBAO. Wakiongozwa na M***i wa Tanzania Sheikh Dr. Abubakar Zebeir Bin Ally

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mardhiano na Aman Tanzania (JMAT) Dk Alhad M***a Salum jumapili ya tarehe 20,07,2025 aliliteka jiji la Dar es salaam baada ya kufanya hafla nzito na yenye hadhi kubwa sana ktk ukumbi wa Dyccc Temeke Jijini Dar katika walima wa mwanae islah aliyefunga ndoa weki iliyopita nchini Kenya

Walima hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Dyccc Changombe na kunogeshwa na uwepo wa Mashekh tofauti na Viongozi wa dini zingine mbalimbali wakiwa wamejumuika kwa utulivu wa hali ya juu sana .

Tunamuombea bwana harusi na bibi harusi Mola awabariki katika ndoa yao awakinge na husda awape kizazi chema.

21/07/2025

Taasisi ya Al-Hikma Foundation jana Julai 20, 2025 imehitimisha rasmi zoezi la kuwafanyia tohara watoto katika zahanati ya Vingunguti, jijini Dar es Salaam, ambapo jumla ya watoto 85 walifanyiwa tohara, na hivyo kufikisha idadi ya watoto 1,800 walionufaika na huduma hiyo tangu kuanza kwa zoezi hilo katika mkoa wa Dar es salaam.

Zoezi hilo lilifanyika na Al-hikma Foundation chini ya usimamizi wa Sheikh Nurdin Kishki, likiwa na lengo la kusaidia jamii hasa familia zenye kipato cha chini kwa kuwapatia huduma hiyo muhimu ya afya bila malipo.

TOHARA KWA WATOTO 1,800 JIJINI DAR ES SALAAMTaasisi ya Al-Hikma Foundation jana Julai 20, 2025 imehitimisha rasmi zoezi ...
21/07/2025

TOHARA KWA WATOTO 1,800 JIJINI DAR ES SALAAM

Taasisi ya Al-Hikma Foundation jana Julai 20, 2025 imehitimisha rasmi zoezi la kuwafanyia tohara watoto katika zahanati ya Vingunguti, jijini Dar es Salaam, ambapo jumla ya watoto 85 walifanyiwa tohara, na hivyo kufikisha idadi ya watoto 1,800 walionufaika na huduma hiyo tangu kuanza kwa zoezi hilo katika mkoa wa Dar es salaam.

Zoezi hilo lilifanyika na Al-hikma Foundation chini ya usimamizi wa Sheikh Nurdin Kishki, likiwa na lengo la kusaidia jamii hasa familia zenye kipato cha chini kwa kuwapatia huduma hiyo muhimu ya afya bila malipo.

Akizungumza wakati wa hafla ya kuhitimisha zoezi hilo, Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mhe. Omary Kumbilamoto, ambaye alikuwa mgeni rasmi, aliipongeza Al-Hikma Foundation kwa kutimiza kwa vitendo ahadi yao ya kuunga mkono jitihada za serikali katika kuboresha afya ya watoto.

"Nawapongeza sana Al-Hikma Foundation chini ya Sheikh Nurdin Kishki kwa moyo wao wa kujitolea na kwa kufanikisha tohara kwa watoto 1,800. Hii ni hatua kubwa ya kuimarisha afya ya jamii yetu na kupunguza maambukizi ya magonjwa mbalimbali yanayoweza kuzuilika," alisema Meya Kumbilamoto.

Aidha, Sheikh Nurdin Kishki aliwahimiza wadau wengine kuiga mfano wa Al-Hikma kwa kusaidia jamii katika maeneo mbalimbali ya huduma za kijamii, hususan sekta ya afya, elimu na ustawi wa watoto.

Taasisi ya Al-Hikma Foundation imekuwa ikitekeleza miradi mbalimbali ya kijamii ikiwemo kufungisha ndoa kwa mabachela, tohara za bure, misaada kwa yatima na elimu kwa jamii, ikiwa ni sehemu ya mchango wake kwa maendeleo ya taifa.

Al-Hikma Foundation Watimiza ahadi ya kuwafanyia sunna au tohara watoto 1800 bure.Taasisi ya Al-Hikma Foundation chini y...
21/07/2025

Al-Hikma Foundation Watimiza ahadi ya kuwafanyia sunna au tohara watoto 1800 bure.

Taasisi ya Al-Hikma Foundation chini ya Mkurugenzi Sheikh Nurdeen Kishki mnamo tarehe 16/03/2025 ndani ya Uwanja wa Mkapa Katika Mashindano Makubwa Zaidi ya Qur'an Tukufu ya Mabara Yote Ulimwenguni ilitoka ahadi ya kuwafanyia tohara watoto 1000 ikiwa ni mmoja kati ya sapraizi zilizo tolewa.

Katika kufanikisha ahadi hiyo taasisi ya Al-hikma ilishirikiana na Serikali pamoja na TAASISI YA AFYA YA KIISLAAM YA SUNSHINE MUSLIM VOLUNTEERS (SMV) Tarehe 26/04/2025 zowezo hilo lilianza rasmi katika Kituo cha Afya Yombo mwitikio ulikua ni mkubwa wazazi walijitokeza kwa wingi jambo ambalo iliilazimu taasisi ya Alhikma chini ya Mkurugenzi wake Sheikh Nurdeen Kishki kuongezaa idadi kutoka watoto 1000 mpaka watoto 1800 ambapo licha ya ongezeko hilo bado kuna wengi hawajafikiwa na hudma hiyo.

Jumapili ya tarehe 20/07/2025 zoezi hilo limefungwa rasmi katika Zahanati ya Vingunguti chini ya Sheikh Nurdeen Kishki mgeni rasmi katika tukio hilo alikua ni Mhe, Omary Kumbilamoto meya wa jiji la Dar es salaam

20/07/2025

Masheikh na wazee zetu walimsaidia Mwalim Nyerere kupata uhuru tuitunze amani tulio achwa na wazee wetu yasije tufika ya wenzetu Ruwanda.

20/07/2025

Matatizo ya maisha yako yapo katika maswali haya jibu maswali haya kisha anza leo.

20/07/2025

Masharifu wa kenya wanalia juu ya amani wakenya wanajidai wao ndio wenye akiliza zaidi sasa mbona wanaivuruga nchi yao.

19/07/2025

Kuna watu wanaleta uchochezi nchini mwetu uchochezi ni kazi ya shetani na wachoche ni mashetani.

Sheikh. Nurdeen Kishki aliongea hayo katika khutuba ya ijumaa yenye anuwani ya wajibu wa kila musilamu juu ya nchi yake khutuba hiyo aliitoa msikiti wa mtoto kariakoo.

Kusijikiza khutuba yote tembelea YouTube channel yetu ya KhidmaTV.

19/07/2025

Usiende mpigia mtu kura eti amekupa elfu 50,000 ukifanya hivyo utakua umeuza miaka 5 ijayo kila mwaka umeuza kwa elfu 10000.

19/07/2025

Itikia dua ukiwa na yakini kua Allah atakujibu AmiinYaarab

Kusifiwa kwa zama zetu hizi baadhi ya watu usipo wasifia unaweza kukosa msaada kabisa na wakati mwengine wanakodi watu k...
19/07/2025

Kusifiwa kwa zama zetu hizi baadhi ya watu usipo wasifia unaweza kukosa msaada kabisa na wakati mwengine wanakodi watu kwaajili ya kumsifia yeye.

Dini ya uislamu haikuacha kitu usipenda kusifiwa na watu lakini pale ikibidi umesifiwa basi soma dua hi.👇

Ewe Allah usinichukulie kwa yale wanayoyasema na unisahemehe kwa wasiyoyajua na unifanye bora kuliko wanavyofikiria. 😊

Dua hiyo ndani yake kuna funzo la kujishusha na kujiona wewe sio kitu mbele ya wengine na mbele ya Allah na hivyo Mola akujalie kwa yale wanayoyasema yawe ya kweli kwako.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Khidma TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Khidma TV:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share