Modc News

Modc News MODC News inakusogezea mchanganyiko wa habari kutoka duniani kote kiganjani kwako

๐ŸŒ๐Ÿ† WACHEZAJI WA KIAFRIKA WANAOCHEZA EPL WATAKAOONDOKA VILABUNI KWAO NA KWENDA AFCON:Sunderland โ€” 6๐Ÿ‡ฒ๐Ÿ‡ฆ Chemsdine Talbi๐Ÿ‡ธ๐Ÿ‡ณ H...
13/12/2025

๐ŸŒ๐Ÿ† WACHEZAJI WA KIAFRIKA WANAOCHEZA EPL WATAKAOONDOKA VILABUNI KWAO NA KWENDA AFCON:

Sunderland โ€” 6
๐Ÿ‡ฒ๐Ÿ‡ฆ Chemsdine Talbi
๐Ÿ‡ธ๐Ÿ‡ณ Habib Diarra
๐Ÿ‡ฒ๐Ÿ‡ฟ Reinildo
๐Ÿ‡ง๐Ÿ‡ซ Bertrand Traorรฉ
๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฉ Arthur Masuaku
๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฉ Noah Sadiki

Manchester United โ€” 3
๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฒ Bryan Mbeumo
๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฎ Amad Diallo
๐Ÿ‡ฒ๐Ÿ‡ฆ Noussair Mazraoui

Fulham โ€” 3
๐Ÿ‡ณ๐Ÿ‡ฌ Alex Iwobi
๐Ÿ‡ณ๐Ÿ‡ฌ Calvin Bassey
๐Ÿ‡ณ๐Ÿ‡ฌ Samuel Chukwueze

Burnley โ€” 3
๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฉ Axel Tuanzebe
๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡ฆ Lyle Foster
๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ณ Hannibal Mejbri

Nottingham Forest โ€” 2
๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฎ Ibrahim Sangarรฉ
๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฎ W***y Boly

Everton โ€” 2
๐Ÿ‡ธ๐Ÿ‡ณ Iliman Ndiaye
๐Ÿ‡ธ๐Ÿ‡ณ Idrissa Gueye

Brentford โ€” 2
๐Ÿ‡ง๐Ÿ‡ซ Dango Ouattara
๐Ÿ‡ณ๐Ÿ‡ฌ Frank Onyeka

Manchester City โ€” 2
๐Ÿ‡ช๐Ÿ‡ฌ Omar Marmoush
๐Ÿ‡ฉ๐Ÿ‡ฟ Rayan Aรฏt-Nouri

Tottenham Hotspur โ€” 2
๐Ÿ‡ธ๐Ÿ‡ณ Pape Matar Sarr
๐Ÿ‡ฒ๐Ÿ‡ฑ Yves Bissouma

West Ham United โ€” 2
๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฉ Aaron Wan-Bissaka
๐Ÿ‡ธ๐Ÿ‡ณ El Hadji Malick Diouf

Wolves โ€” 2
๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡ผ Tawanda Chirewa
๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฎ Emmanuel Agbadou

Brighton & Hove Albion โ€” 2
๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฒ Carlos Baleba

Crystal Palace โ€” 1
๐Ÿ‡ธ๐Ÿ‡ณ Ismaรฏla Sarr

SANAMU KUBWA YA LIONEL MESSI YAJENGWA INDIA!Katika hatua ya kushangaza na ya heshima kubwa kwa mchezaji bora duniani, sa...
13/12/2025

SANAMU KUBWA YA LIONEL MESSI YAJENGWA INDIA!

Katika hatua ya kushangaza na ya heshima kubwa kwa mchezaji bora duniani, sanamu mpya ya Lionel Messi imejengwa mjini Kolkata, India

Urefu wa sanamu hiyo unakadiriwa kuwa futi 70 (takriban mita 21)!
๐Ÿ† Messi anaonekana akiwa ameshikilia Kombe la Dunia, tukio ambalo linaendelea kuenziwa tangu Argentina ilipotwaa taji hilo 2022.

Mashabiki wa soka nchini India, hasa Bengal, wamekuwa wakimpenda Messi kwa miaka mingi, na sanamu hii ni ishara ya mapenzi hayo makubwa.

TANZIA๐Ÿ˜ญ๐ŸšจTaarifa za awali kutoka DRC ni kwamba Chico Ushindi Wakubanza mshambuliaji wa zamani wa Tp Mazembe na Young Afri...
13/12/2025

TANZIA๐Ÿ˜ญ

๐ŸšจTaarifa za awali kutoka DRC ni kwamba Chico Ushindi Wakubanza mshambuliaji wa zamani wa Tp Mazembe na Young Africans amefariki dunia.

Taarifa kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
13/12/2025

Taarifa kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Kocha mkuu wa Yanga, Pedro Goncalves amekingalia kikosi cha timu hiyo kilivyo kwa sasa, kisha kuuambia uongozi wa klabu ...
13/12/2025

Kocha mkuu wa Yanga, Pedro Goncalves amekingalia kikosi cha timu hiyo kilivyo kwa sasa, kisha kuuambia uongozi wa klabu hiyo, umletee mashine mpya tatu amalize kazi.
Mabosi wa Yanga wamepokea ripoti ya kwanza ya Pedro baada ya kukisimamia kikosi hicho katika mechi sita za mashindano zikiwemo mbili za Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi na nne za Ligi Kuu Bara, zilizotosha kumpa picha ya wapi anataka kuiboresha mara michuano ikirudia tena
Taarifa kutoka kwa mabosi wa Yanga ni kwamba, Pedro ametaka kutafutiwa kiungo mkabaji mwenye ubora mkubwa, japo amesisitiza Duke Abuya amefanya kazi bora eneo hilo lakini anataka kumhamisha. Ripoti ya Mreno huyo inasema, endapo atapata kiungo huyo mkabaji basi Abuya atahamishwa nafasi akisogezwa juu, hatua ambayo itaifanya Yanga kuwa na ubora mkubwa eneo la katikati kutokana na uwezo wa Mkenya huyo sambamba na kiungo atakayekuja.
Ripoti hiyo pia inahitaji kiungo mshambuliaji, yaani namba 10 na bado Pedro haridhishwi saana na watu alionao eneo hilo huku akionyesha hataki kutumia fundi Pacome Zouzoua eneo hilo. Pedro ameonyesha anataka kumtumia Zouzoua k**a kiungo wa pembeni akitokea kushoto akicheza eneo nusu (half space) jukumu litakalomfanya kuwa hatari zaidi mbele ya lango la mpinzani na kuinufaisha Yanga kuliko ilivyo sasa akiwa amefunga mabao mawili na asisti mbili vilevile.
Akili hiyo ya Pedro ya kutaka namba 10 inawaweka mtegoni Mamadou Doumbia na Lassine Kouma ambao walikuwa wanapewa nafasi kwa nyakati tofauti kucheza nafasi hiyo, licha ya Ecua Celestine naye kuwa mchezaji wa nafasi hiyo, japo kwa sasa anachezeshwa pembeni k**a winga.
Kocha huyo Mreno pia anataka kutafutiwa winga mmoja mwenye ubora mkubwa atakayeongeza nguvu ya kuzalisha mashambulizi kutokea pembeni.

๐Ÿšฉ ORODHA YA TIMU ZITAKAZO SHIRIKI MAPINDUZI CUP MSIMU WA 2025/26Mashindano ya Mapinduzi Cup yatafanyika kuanzia Desemba ...
13/12/2025

๐Ÿšฉ ORODHA YA TIMU ZITAKAZO SHIRIKI MAPINDUZI CUP MSIMU WA 2025/26

Mashindano ya Mapinduzi Cup yatafanyika kuanzia Desemba 29, 2025 hadi Januari 13, 2026, yakishirikisha jumla ya timu nane zifuatazo:

๐ŸŸAzam FC

๐ŸŸFufuni FC

๐ŸŸYoung Africans SC (Yanga)

๐ŸŸMlandege

๐ŸŸURA FC

๐ŸŸSimba SC

๐ŸŸKVZ FC

๐ŸŸSingida Black Stars

Mashindano yanatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa huku vigogo wa soka wakipambana kutwaa ubingwa.

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema imefuatilia makala iliyochapishwa muda mfupi uliopita na chombo cha ...
21/11/2025

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema imefuatilia makala iliyochapishwa muda mfupi uliopita na chombo cha habari cha CNN kuhusu matukio ya tarehe 29 Oktoba, 2025 na siku zilizofuata.

Taarifa ya leo Novemba 21, 2025 iliyotolewa na Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa imesema โ€œTunachambua na kuhakiki maudhui yaliyomo katika makala hiyo na tamko la Serikali litakuja baada ya kukamilika kwa uhakiki huo.โ€

Mapema leo Novemba 21, 2025, CNN ilitoa ripoti ya uchunguzi wake wa kina ambapo imedai imebaini ushahidi unaoonyesha kuwa Polisi wa Tanzania walitumia risasi kuwashambulia na kuwaua waandamanaji waliokuwa wakipinga Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29.

Ripoti hiyo ya CNN ikiongozwa na mwandishi Larry Madowo imedai imeufanya uchunguzi huo kwa uchambuzi wa forensic, ikiwemo muunganiko wa video, picha za maeneo ya tukio, na picha za satelaiti.

Na hii ndio jezi namba tatu ya Yanga SC ambayo wataitumia katika mechi zake za Ligi ya Mabingwa msimu huu.We umeipenda J...
19/11/2025

Na hii ndio jezi namba tatu ya Yanga SC ambayo wataitumia katika mechi zake za Ligi ya Mabingwa msimu huu.

We umeipenda Jezi namba ngapi????


Hii ndio jezi ya Ugenini ya Yanga SC msimu huu kwenye michuano ya Kimataifa. Mnaipa alama ngapi!?
19/11/2025

Hii ndio jezi ya Ugenini ya Yanga SC msimu huu kwenye michuano ya Kimataifa.

Mnaipa alama ngapi!?

Jezi za Yanga ambazo zitatumika msimu katika mashindano ya Caf Champions League. Hii ni Jezi za nyumbaniHapo Vipi Wananc...
19/11/2025

Jezi za Yanga ambazo zitatumika msimu katika mashindano ya Caf Champions League.

Hii ni Jezi za nyumbani

Hapo Vipi Wananchii?

18/11/2025

Hii hapa Orodha kamili ya balaza la mawaziri katika kipindi cha pili katika awamu ya sita chini ya Rais Samia, Makonda yumo

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Modc News posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share