Modc News

Modc News Kwa Habari za Michezo na Burudani, Uchumi na Biashara, Siasa na uchambuzi wa kina kutoka Pande zote za Dunia.

06/06/2026

Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba


06/06/2026

: Katika ziara ya Waziri Mkuu wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, inayoendelea mkoani Iringa ndani ya Jimbo la Isimani, mwananchi mmoja amejitokeza hadharani kueleza malalamiko yake mbele ya kiongozi huyo, akidai kuwa mtu aliyemtaja kwa jina la Paulo anadaiwa kumtorosha mtoto wake.

Akizungumza mbele ya Waziri Mkuu, mwananchi huyo alisema, “Waziri Mkuu, Paulo amemtorosha mtoto wangu,” huku akieleza kuwa hadi sasa hajui alipo mtoto huyo na kwamba suala hilo linafahamika na Afande Mwakagenda.

Baada ya kusikiliza malalamiko hayo, Dkt. Mwigulu aliomba ufafanuzi wa tukio hilo kutoka kwa vyombo vya usalama kwa kusema, “Afande, tuambie kuhusu hili,” ili kupata maelezo zaidi kuhusu madai hayo.


06/06/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba Ameyasema hayo Juni 5, 2026 wakati akizungumza na wakazi wa Isimani, Mkoani Iringa.

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu yupo mkoani Iringa kwa Ziara ya kikazi.


06/06/2026

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, amewataka viongozi wa Jiji la Dar es Salaam kuwa mfano bora katika utunzaji wa mazingira ili kuhakikisha jiji hilo linaendelea kuwa safi na kuvutia wageni pamoja na wawekezaji wanaoingia nchini kupitia mkoa huo.

Mpogolo ametoa kauli hiyo wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ngazi ya Mkoa wa Dar es Salaam, yaliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Manispaa ya Ilala. Amesema usafi wa mazingira ni msingi muhimu wa maendeleo endelevu na taswira nzuri ya jiji.

Ameeleza kuwa viongozi wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha wananchi kushiriki shughuli za utunzaji wa mazingira, ikiwemo usimamizi wa taka na usafi wa maeneo ya makazi na biashara, ili kudumisha hadhi ya Dar es Salaam k**a kitovu cha biashara nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Kajenjere Mathewe, Andrew, amesema utunzaji wa mazingira unatoa fursa mbalimbali za kiuchumi, ikiwemo ajira kwa vijana kupitia shughuli za ukusanyaji, uchakataji na usimamizi wa taka zinazozalishwa katika jiji.

Andrew ameongeza kuwa kila mwananchi ana wajibu wa kutunza mazingira kwa kuwa ni urithi muhimu kutoka kwa watangulizi wa taifa. Amesisitiza kuwa ushiriki wa pamoja katika kulinda mazingira utachangia kuifanya Dar es Salaam kuwa safi, salama na yenye maendeleo endelevu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.


06/06/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kuwa yeye ni mpole sana isipokuwa anachukizwa sana na uonevu unaofanywa na baadhi ya watumishi wa serikali kwa wananchi.

Ametoa kauli hiyo baada ya kusikika kwa kauli inayosema kuwa 'huyu ni zaidi ya Magufuli'


06/06/2026

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kusimamia utoaji wa haki kwa wananchi na kuimarisha uwajibikaji kwa watumishi wa umma ili kuhakikisha huduma za Serikali zinatolewa kwa ufanisi, kwa wakati na kwa kuzingatia maslahi ya wananchi.

Amesema hayo leo Ijumaa, Juni 5, 2026 alipokuwa akizungumza na kusikiliza kero za wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa katika Jimbo la Isimani mkoani Iringa katika viwanja vya Isimani tarafani.

Dkt. Mwigulu amesema haki za wananchi hazipaswi kucheleweshwa wala kunyimwa kwa sababu yoyote na kusisitiza kuwa kila anayestahili haki yake anapaswa kuipata kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.

“Haki si hisani. Tunataka anayestahili haki apewe haki yake. Serikali haitavumilia vitendo vya kupora au kuchelewesha haki za wananchi kwa sababu yoyote ile,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amesema watumishi wa umma wanapaswa kutambua kuwa nafasi walizonazo ni dhamana ya kuwatumikia wananchi na kwamba huduma zinazoweza kutolewa kwa siku hiyo zinapaswa kutolewa bila kuwazungusha wananchi.

“Linaloweza kufanyika leo lifanyike leo. Wananchi wanapofika katika ofisi za umma wanapaswa kuhudumiwa kwa heshima, haraka na kwa ufanisi,” amesema.

Pia amesema Serikali itaendelea kuchukua hatua kali dhidi ya watumishi watakaobainika kushindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo, hususan wale wanaokwaza utoaji wa huduma na matumizi sahihi ya rasilimali za umma.

Waziri Mkuu amesema uwajibikaji, uadilifu na utoaji wa huduma bora ni msingi muhimu wa kujenga imani ya wananchi kwa Serikali na kuhakikisha maendeleo yanawafikia wananchi wote.

Kadhalika, amewahakikishia wananchi wa Isimani kuwa Serikali itaendelea kutekeleza ahadi zilizotolewa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na miradi ya maendeleo iliyopo kwenye Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa lengo la kuboresha maisha ya wananchi.


06/06/2026

Mwenezi wa taifa ndugu kenan kihongozi akiwa anendelea na ziara zake zinazoendelea nchi nzima
Akiwa katika mkoa wa Arusha ndugu Kenan amemsifu mwenezi wa mkoa ndugu Saipulaini huo kuwa ni mfano wa kiigwa kwa viongozi wadogo ambao wanafanya kazi nzuri na iliotukuka

Aidha kenan amesema kuwa ccm inawalea wanachama wake wakiwa bado wadogo na ndio maana wakipewa nafasi yoyote ya uwongozi ndani ya. chama na nje ya chama wanakuwa wanafanya vizuri na hiyo ndio utafauti kati ya chama Ccm na vyama vingine vya siasa


06/06/2026

Makamu wa Rais Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amekoshwa na uwezo wa mtoto huyu mdogo akisema kuwa anauwezo wa kuchukua jimbo na kumuondoa mbunge anayeonekana kuwa hatoshi.


06/06/2026

Makamu wa Rais Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akieleza jitihada zilizofanyika ili kumpata Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, awe mgeni rasmi kwenye Madhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayofanyika Juni 5, 2026, lakini Juhudi hizo ziligonga mwamba kutokana na ugumu wa ratiba zake.


🤝🇹🇿 Mwigulu Nchemba akisalimiana na Mbunge wa Isimani Bungeni DodomaWaziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwig...
05/06/2026

🤝🇹🇿 Mwigulu Nchemba akisalimiana na Mbunge wa Isimani Bungeni Dodoma

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwigulu Nchemba, amesalimiana na Mbunge mpya wa Jimbo la Isimani, Emmanuela Mtatifikolo, wakati wa vikao vya Bunge jijini Dodoma.

Katika tukio hilo la Juni 5, 2026, Kulia ni Mbunge wa Iringa Mjini, Fadhili Ngajilo

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Modc News posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share