DIRA YA LEO

DIRA YA LEO Politics | Social | Economics | Sports | Entertainment; Accurate news at the right time.

14/05/2026

Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam imesema kichwa cha mwanafunzi wa IFM kimepatikana kwa mganga wa kienyeji maeneo ya Kitunda kibeberu Dar.

CNN Inaripoti mkutano wa kwanza wa rais wa Marekani Donald Trump na rais wa China Xi Jinping umefanyika huku pakiwa na p...
14/05/2026

CNN Inaripoti mkutano wa kwanza wa rais wa Marekani Donald Trump na rais wa China Xi Jinping umefanyika huku pakiwa na picha ya wanaume tu bila mwanamke yoyote kwenye meza hio kubwa ya mazungumzo, wanasema 'Inaonekana hakuna mwanamke hata mmoja aliyehusika katika mazungumzo hayo, kwa upande wa Marekani au China, Wanawake hawana uwakilishi katika ngazi za juu za serikali huko Beijing na Washington, Sio Marekani wala China ambayo imewahi kuwa na kiongozi wa k**e. Unafikiri ni kwanini?

08/05/2026

Wenyeviti 56 wa Serikali za Mitaa kutoka Jimbo la Segerea wametambulishwa Bungeni baada ya kualikwa na Mbunge wa Jimbo hilo, Agnesta Lambert Kaiza (CHAUMA), huku viongozi hao wote wakitokana na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

07/05/2026

Mbunge wa Jimbo la Segerea, Agnesta Lambert Kaiza, ameendelea kuwasemea wananchi wa jimbo lake baada ya kuishukuru serikali kwa utekelezaji wa miradi ya maji inayolenga kupunguza changamoto ya upatikanaji wa huduma hiyo katika kata za Kimanga, Kisukuru na Segerea.

Kiongozi mkuu wa Iran, Ayatollah Mojtaba Khamenei, ameapa kulinda uwezo wa nyuklia na makombora ya taifa hilo licha ya s...
01/05/2026

Kiongozi mkuu wa Iran, Ayatollah Mojtaba Khamenei, ameapa kulinda uwezo wa nyuklia na makombora ya taifa hilo licha ya shinikizo kutoka Marekani.

Akizungumza kupitia televisheni ya serikali, alikosoa uwepo wa Marekani katika Ghuba ya Uajemi na kusema mabadiliko mapya yanaandikwa katika historia ya eneo hilo.

Aliongeza kuwa Wairani milioni tisini wanachukulia maendeleo ya kisayansi na kiteknolojia, ikiwemo nyuklia, k**a sehemu ya utambulisho wa taifa lao.

Iran’s Supreme Leader, Mojtaba Khamenei, has vowed to safeguard the country’s nuclear and missile capabilities despite pressure from the United States.

Speaking on state television, he criticized the U.S. presence in the Persian Gulf and said that a new chapter is being written in the region’s history.

He added that Iran’s population of 90 million views scientific and technological advancement—including nuclear development—as a key part of their national identity.

Rais wa Marekani, Donald Trump, amezua mjadala baada ya kupendekeza kuwa wagombea wote wa nafasi za urais na makamu wa r...
01/05/2026

Rais wa Marekani, Donald Trump, amezua mjadala baada ya kupendekeza kuwa wagombea wote wa nafasi za urais na makamu wa rais nchini humo wanapaswa kufanyiwa vipimo maalum vya utambuzi wa akili (cognitive tests) kabla ya kuruhusiwa kuingia kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi.

Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mtandao wake wa Truth Social, Trump amesema hatua hiyo ingeweza kusaidia kuhakikisha viongozi wanaochaguliwa wanakuwa na uwezo kamili wa kiakili, jambo ambalo kwa maoni yake lingeleta ufanisi zaidi katika uongozi wa nchi.

Katika ujumbe huo, Trump aliwataja baadhi ya viongozi waliopita akiwemo Barack Obama na Joe Biden, akidai kuwa mfumo huo ungezuia kuchaguliwa kwa viongozi ambao, kwa mtazamo wake, hawakufaa.Aidha, Trump alieleza kuwa yeye binafsi aliwahi kufanya vipimo hivyo mara tatu wakati wa urais wake na kufaulu kwa kiwango cha juu, akisisitiza kuwa mafanikio hayo ni nadra kupatikana kulingana na madaktari.

Kauli hiyo imeibua mijadala mitandaoni na katika duru za kisiasa, Wengi wakisema jambo hilo linaweza kutumika kisiasa au kubagua baadhi ya wagombea.

U.S. President Donald Trump has sparked debate after suggesting that all candidates running for president and vice president in the United States should undergo special cognitive tests before being allowed to participate in elections.

In a message posted on his social media platform Truth Social, Trump said the move could help ensure that elected leaders are mentally fit, which, in his view, would lead to more effective governance.

In the same message, Trump mentioned some former leaders, including Barack Obama and Joe Biden, claiming that such a system would prevent the election of leaders whom he believes were unfit for office.

He also stated that he personally took such cognitive tests three times during his presidency and performed at a very high level, emphasizing that such results are rare according to doctors.

The remarks have triggered widespread debate online and within political circles, with many arguing that such a requirement could be used for political purposes or to discriminate against certain candidates.

27/04/2026

Trump alivyoondolewa ukumbini baada ya kunusurika kupigwa risasi kwenye mkutano Washington

26/04/2026

"Mimi ni Mbunge ninayetoka na Chama cha Upinzani lakini ninaamini katika harakati anazofanya Rais Dkt. Samia kwa ajili ya watanzania" Mbunge wa Jimbo la Segerea, Agnesta Lambert.

Amesema hayo leo alipozungumza katika mkutano wa hadhara wa Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba alioufanya kwenye uwanja wa shule ya msingi Msimbazi jijini Dar es Salaam leo Aprili 26, 2026

  Waziri wa Ulinzi wa Mali, Jenerali Sadio Camara, ameripotiwa kuuawa kufuatia mashambulizi makubwa na ya kuratibiwa yal...
26/04/2026

Waziri wa Ulinzi wa Mali, Jenerali Sadio Camara, ameripotiwa kuuawa kufuatia mashambulizi makubwa na ya kuratibiwa yaliyolenga vituo vya kijeshi katika maeneo mbalimbali nchini humo, kwa mujibu wa vyanzo vilivyoizungumza na Al Jazeera.

Taarifa hizo zimekuja baada ya makundi yenye silaha, yanayohusishwa na mtandao wa Al-Qaeda pamoja na waasi wa Tuareg, kushambulia kwa wakati mmoja mji mkuu Bamako, Kati pamoja na miji mingine ya kimkakati, hali iliyosababisha taharuki kubwa ndani ya serikali ya kijeshi ya Mali.

Jenerali Camara alikuwa mmoja wa viongozi wakuu wa utawala wa kijeshi uliotwaa madaraka kupitia mapinduzi ya mwaka 2020 na 2021, hivyo kifo chake kinatajwa kuwa pigo kubwa kwa uongozi wa nchi hiyo unaokabiliwa na ukosefu wa usalama unaozidi kuongezeka.

Ripoti zinaeleza kuwa nyumba yake ililengwa moja kwa moja wakati wa mashambulizi hayo, huku mapigano makali yakiendelea katika baadhi ya maeneo huku serikali ikijaribu kurejesha hali ya utulivu.

Tukio hilo linaashiria kuongezeka kwa nguvu kwa makundi ya waasi na kuzidi kuyumbisha mamlaka ya kijeshi ya Mali mbele ya mashambulizi ya ndani.

23/04/2026

Naibu Waziri wa Ujenzi, Godfrey Kasekenya, amesema Serikali imeelekeza timu ya wataalamu kutoka TANROADS mkoa wa Dar es Salaam kutembelea barabara ya Kifuru–Pugu kwa lengo la kubaini na kutatua maeneo korofi yanayosababisha usumbufu kwa wananchi.

Naibu Waziri Kasekenya ametoa kauli hiyo wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Segerea, Agnesta Lambert Kaiza, aliyetaka kujua ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami ili kurahisisha usafiri na shughuli za kiuchumi kwa wakazi wa eneo hilo.

Amesema timu ya TANROADS itafanya tathmini ya kina katika barabara hiyo ili kubaini maeneo yenye changamoto kubwa, hususan yale yanayokatika au kujaa maji wakati wa mvua kubwa zinazoendelea kunyesha, hali inayosababisha wananchi kushindwa kuvuka kutoka eneo moja kwenda jingine.

  Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu anakabiliwa na kesi ya uhalifu iliyoahirishwa kutokana na sababu za kiusalam...
20/04/2026

Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu anakabiliwa na kesi ya uhalifu iliyoahirishwa kutokana na sababu za kiusalama, kulingana na jarida la The Jerusalem Post.

Majaji wa mahak**a ya wilaya ya Yerusalemu, Jumapili, waliamua kusikiliza ushahidi kutoka kwa shahidi mwingine, na hivyo kuchelewesha zamu ya Netanyahu kupanda kizimbani kutoa ushahidi wake.

Uamuzi huo unafuatia ombi la upande wa utetezi wa kusitisha ushahidi wa Netanyahu, ukitoa sababu za kiusalama. Hata hivyo, upande wa waendesha mash*taka walipinga ombi hilo, wakisisitiza kwamba hakuna hoja ya msingi ya kiusalama, na kumtaka Netanyahu afuate kalenda ya mahak**a hiyo kwa maslahi ya umma.

Kesi hiyo ipo katika hatua ya mahojiano na Netanyahu, ambapo alipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Disemba 2024. Netanyahu anashtakiwa kwa makosa ya ufisadi na udanganyifu, kesi iliyofunguliwa Novemba 2019.

Mbali na kesi hiyo, Mahak**a ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) ilitoa hati ya kuk**atwa kwa mwanasiasa huyo Novemba 2024, kwa makosa ya uhalifu wa kibinadamu unaoendelea huko Gaza.

Address

Tabata
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when DIRA YA LEO posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share