Sento Flani DiCaprio

Sento Flani DiCaprio SENTOFLANI DICAPRIO
πŸ“° Habari za siasa β€’ Uchambuzi β€’ Mijadala πŸ“ Tanzania πŸ”” Kwanza kupata taarifa za kisiasa

14/07/2026

*SIMULIZI ZA WANANCHI WA TABORA NA KIGOMA WAKIELEZEA KUNUFAIKA NA MRADI WA SGR*

Wananchi wa mikoa ya Tabora na Kigoma walioguswa na mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha sita wameeleza kunufaika na fidia kwa njia mbalimbali.

Katika simulizi zao, wameshuhudia masuala kadhaa ikiwemo,
Kujenga au kununua makazi mapya kufuatia maeneo yao kutwaliwa kwa ajili ya mradi.

Baadhi ya waliopokea fidia wamesema mradi huo wa
Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC) umewawezesha
kuanzisha na kupanua biashara, ikiwemo biashara ndogo ndogo, kilimo na ufugaji, jambo lililowasaidia kuongeza kipato cha familia.

Aidha wamesema, mradi umepiga jeki mahitaji ya familia, k**a kulipia ada za watoto na kuboresha maisha ya kaya kupitia matumizi ya fidia kwa shughuli za maendeleo.

Pamoja na hayo wamesema,
mradi umeleta fursa za ajira na biashara zinazotokana na ujenzi wa SGR, ambapo wananchi wa maeneo yanayopitiwa na mradi wamepata kazi za muda na wengine kunufaika kwa kutoa huduma k**a upangishaji wa nyumba, mama lishe na usafirishaji nk.

Mwaka SGR itakapofika Kigoma... Babu: Enzi zetu safari ya Kigoma ilikuwa ni tukio. Mjukuu:Safari gani babu? Mimi nikiamb...
14/07/2026

Mwaka SGR itakapofika Kigoma...

Babu: Enzi zetu safari ya Kigoma ilikuwa ni tukio.

Mjukuu:Safari gani babu? Mimi nikiambiwa twende Kigoma nafikiri ni k**a kwenda posta tu. πŸ˜‚
Sijui nisemaje tu sio kwa tunavyo isubili Yani siku itimie tu.

13/07/2026




13/07/2026

*KINGU AWEKA WAZI MSIMAMO WAKE KUHUSU TAARIFA ZA NILESH,*
*"SINUNULIKI WALA SITUMIKI"*

Mbunge wa Jimbo la Ikungi Magharibi, Elibariki Emmanuel Kingu, amesema kauli yake kuhusu mfanyabiashara maarufu nchini Nilesh Suchack haikupaswa kutafsiriwa k**a kutetea ukiukwaji wowote wa sheria katika masuala ya biashara, kodi au taratibu za kifedha.

Akizungumza katika mahojiano maalumu, Kingu amesema alichokizungumza kilikuwa katika mtazamo wa kawaida wa uendeshaji wa biashara, hususan kuhusu wafanyabiashara kutumia huduma za benki na mikopo kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao.

Amesema endapo kuna suala lolote la kisheria linalohusu biashara, kodi au miamala ya kifedha, vyombo husika vya Serikali vina wajibu wa kufuata taratibu na kuhakikisha sheria zinafuatwa.

β€œNisieleweke kwamba kauli yangu ilikuwa inataka kusimama upande wa kuzuia k**a kuna mambo mengine ya kisheria au ya kibiashara. Sikumaanisha hivyo,” amesema Kingu.

Mbunge huyo amesema hawezi kuwa mtetezi wa mtu anayekwepa kulipa kodi au anayekiuka taratibu za Serikali, akisisitiza kuwa k**a kuna madeni ya kodi kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yanapaswa kulipwa kwa mujibu wa sheria.

β€œK**a kuna kodi za Serikali zinadaiwa zilipwe katika utaratibu wa kisheria, k**a kuna mikopo kwenye benki ilipwe. Hilo ndilo jambo la msingi,” amesema.

Vilevile Kingu amekanusha dhana kwamba kauli yake ililenga β€œkumclear” mtu, akisema yeye si mbunge wa kutumika kwa maslahi ya mtu binafsi na kwamba maamuzi yake yanatokana na misingi anayoamini.

Amesema msimamo wake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Chama Cha Mapinduzi (CCM) na maslahi ya nchi unafahamika, huku akisisitiza kuwa hasukumwi na mtu yeyote katika kutoa kauli zake.

β€œMimi sinunuliki na situmiki. Mimi ni mbunge ninayejitambua na ninayejiamini. Nitasimama kwenye misingi ya kile ninachokiamini,” amesema Kingu.

Kingu amesisitiza kuwa kauli yake ililenga kuweka uelewa sahihi kuhusu mazingira ya biashara na si kuingilia taratibu za Serikali, akieleza kuwa endapo kuna jambo lolote linalohitaji uchunguzi au hatua za kisheria, vyombo husika vina wajibu wa kulifanyia kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo.

"K**a Mkuu wa nchi kazi yangu ni kulea vyama vyote, nawalea mawakili wa serikali na mawakili binafsi. Rais wa TLS Bonifa...
13/07/2026

"K**a Mkuu wa nchi kazi yangu ni kulea vyama vyote, nawalea mawakili wa serikali na mawakili binafsi. Rais wa TLS Boniface Mwabukusi alikuja kuniona na changamoto zao, nimeanza kutatua, nimepeleka magari mawili ili waongeze nguvu katika Mama Samia Legal Aid Campaign, na mengine nitayatekeleza pole pole" Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

"Kazi ya kutafsiri sheria kwa lugha ya Kiswahili inakaribia kukamilika, mwananchi anapoielewa sheria anaelewa haki zake,...
13/07/2026

"Kazi ya kutafsiri sheria kwa lugha ya Kiswahili inakaribia kukamilika, mwananchi anapoielewa sheria anaelewa haki zake, wajibu wake, mipaka ya uhuru wake na mipaka ya mamlaka ya serikali, na hii ndio maana halisi ya utawala wa sheria" Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

"Nilipopata mwaliko wa kuja kwenye ufunguzi wa mkutano Mkuu wa Chama cha Mawakili wa serikali sikusita kukubali mwaliko ...
13/07/2026

"Nilipopata mwaliko wa kuja kwenye ufunguzi wa mkutano Mkuu wa Chama cha Mawakili wa serikali sikusita kukubali mwaliko huo kwa kutambua uzito na umuhimu wa kazi zinazofanywa na mawakili na maafisa wa sheria wa serikali katika kuimarisha mfumo wa utoaji haki nchini" Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi, Mawakili, wageni m...
13/07/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi, Mawakili, wageni mbalimbali, kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Jijini Arusha tarehe 13 Julai, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya Kitabu cha Falsafa ya Sh...
13/07/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya Kitabu cha Falsafa ya Sheria ya Mama Samia (Mama Samia Doctrine of Law); kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Hamza Johari kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Jijini Arusha tarehe 13 Julai, 2026. Kitabu hicho kinaelezea historia, falsafa na mafanikio ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia

Address

Temeke
Dar Es Salaam
N/A

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sento Flani DiCaprio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category