14/07/2026
*SIMULIZI ZA WANANCHI WA TABORA NA KIGOMA WAKIELEZEA KUNUFAIKA NA MRADI WA SGR*
Wananchi wa mikoa ya Tabora na Kigoma walioguswa na mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha sita wameeleza kunufaika na fidia kwa njia mbalimbali.
Katika simulizi zao, wameshuhudia masuala kadhaa ikiwemo,
Kujenga au kununua makazi mapya kufuatia maeneo yao kutwaliwa kwa ajili ya mradi.
Baadhi ya waliopokea fidia wamesema mradi huo wa
Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC) umewawezesha
kuanzisha na kupanua biashara, ikiwemo biashara ndogo ndogo, kilimo na ufugaji, jambo lililowasaidia kuongeza kipato cha familia.
Aidha wamesema, mradi umepiga jeki mahitaji ya familia, k**a kulipia ada za watoto na kuboresha maisha ya kaya kupitia matumizi ya fidia kwa shughuli za maendeleo.
Pamoja na hayo wamesema,
mradi umeleta fursa za ajira na biashara zinazotokana na ujenzi wa SGR, ambapo wananchi wa maeneo yanayopitiwa na mradi wamepata kazi za muda na wengine kunufaika kwa kutoa huduma k**a upangishaji wa nyumba, mama lishe na usafirishaji nk.