Loko Kontent Digital

Loko Kontent Digital 🏆 Sports | 🎬 Entertainment | 🔥 Trending Stories
Habari za michezo, burudani na matukio mapya kila siku. Follow upate kontent kali zaidi!

USM Algers kutoka nchini Algeria yaichapa Zamalek ya misri katika mchezo wa fainali wa kombe la shirikisho barani Afrika...
16/05/2026

USM Algers kutoka nchini Algeria yaichapa Zamalek ya misri katika mchezo wa fainali wa kombe la shirikisho barani Afrika kwa changamoto ya mikwaju ya penati

Katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliochezwa Algeria USMA alishinda bao moja kwa sifuri na kwenye mchezo wa marudiano uliopigwa nchini Misri zamalek wakahinda moja sifuri na kupelekea mchezo huwo kwenda hatuwa ya penati

Katika hatuwa ya penati zamalek wameshinda penati saba na kukosa moja huku USMA wakipata penati nane wakiwa hawajakosa hata moja na kuwa mabingwa wa mashindano hayo kwa msimu wa 2025/26

Ubingwa huwo unakuwa wapili kwa timu hiyo baada ya kubeba 2021/22 dhidi ya young Africans na sasa wanabeba tena kwa changamoto ya mikwaju ya penati dhidi ya Zamalek

Follow loko kontent

Chama  na Seleman Mwalimu waipa timu yao ya simba ushindi wa mabao matatu kwa sifuri dhidi ya mashujaa katika dimba la l...
14/05/2026

Chama na Seleman Mwalimu waipa timu yao ya simba ushindi wa mabao matatu kwa sifuri dhidi ya mashujaa katika dimba la lake Tanganyika Kigoma kwenye mwendelezo wa ligi kuu Tanzania bara

Ushindi huwo unawafanya simba kusalia nafasi ya pili kwa kuwa na alama 52 nyuma ya alama mbili kwa kinara wa ligi young Africans mwenye alama 54

Katika mchezo huwo Cloutus chama amefunga mabao mawili na kuibuka mchezaji bora wa mchezo akiendeleza alichokifanya may 3 na kuchukuwa tuzo ya mchezaji bora mara nne mfululizo

Chama amebeba tuzo ya mchezaji bora kwenye mchezo dhidi ya Yanga baada ya kufunga goli moja na kutoa pasi ya goli, dhidi ya JKT TANZANIA akifunga bao pekee lililoipa simba ushindi, dhidi ya Tanzania Prisons na leo dhidi ya mashujaa

Pia Ushindi huwo unawafanya mashujaa kupoteza mchezo wao wa kwanza baada ya kucheza michezo 11 pasi na kupoteza mchezo wowote

Mashujaa 0 - 3 Simba

Follow loko kontent

14/05/2026

Cloutus chota chama ameivunja unbeaten ya mashujaa kwa kuwachalaza mabao mawili na kuipa simba uwongozi katika uwanja wa lake Tanganyika Kigoma

Mashujaa 0 - 2 Simba
Game on dakika 81

Follow loko kontent

14/05/2026

Chama aendeleza makali yake kwa kuwatanguliza simba dhidi ya mashujaa lake Tanganyika Kigoma kwa goli la kona goli

Game on
Mashujaa 0 - 1 Simba
HT dakika 13

Video ni mali

Follow loko kontent

Kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania U17 kitashuka dimbani dhidi ya Msumbiji U17 kutupa karata yake ya kwanza ya michuan...
14/05/2026

Kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania U17 kitashuka dimbani dhidi ya Msumbiji U17 kutupa karata yake ya kwanza ya michuano ya Afcon U17 majira ya saa1 usiku katika uwanja wa Mohammed VI football academy

Katika michuano hiyo ya Afcon U17 inayofanyika nchini Morocco kikosi cha Tanzania kipo kundi C pamoja na Angola, Mali, Msumbiji pamoja na Tanzania

Tanzania U17 wanaingia katika mchezo wakiwa wameshinda mchezo mmoja katika michezo mitano iliyopita na kupata sare mchezo mmoja huku wakipoteza michezo mitatu

Nao Msumbiji wanaingia kwenye mchezo wakiwa wameshinda michezo miwili Katika mitano iliyopita na kupoteza mitatu

kontent

Follow loko kontent

14/05/2026

Hali ilivyo mkoani Kigoma kwenye uwanja wa lake Tanganyika kuelekea kwenye mchezo wa Mashujaa dhidi ya Simba utakaopigwa saa10 kamili jioni

Apo videoni wanaonekana vijana wakiingia na magodoro kwaajili ya kukausha maji yalipo uwanjani ili kuruhusu pitch kuwa kwenye hali nzuri ya kuruhusu mpira udunde na kutembea

Video kwa hisani

Follow loko kontent

14/05/2026

Marquinhos mchezaji wa kimataifa kutoka Brazil anaekipiga kunako klabu ya PSG ya Ufaransa amefanikiwa kuwa mchezaji wa kwanza kutoka Brazil kucheza michezo mingi ya UEFA

Marquinhos hadi sasa tayari ameshacheza michezo 121 akimpiku Roberto Carlos aliecheza michezo 120 na kuwa kinara kwa wachezaji wa kibrazil kucheza michezo mingi ya UEFA

Follow loko kontent

14/05/2026

Ndoto za Barcelona kumaliza msimu wakiwa na alama100 zimekufilia mbali baada ya kupokea kichapo cha bao moja kwa nunge kutoka kwa Deportivo Alaves

Kipigo hiko kinawafanya Barcelona kusalia na alama zao 91 huku wakibakisha michezo miwili kutamatisha msimu wa 2025/26 wakiwa mabingwa wa ligi hiyo

Nao Deportivo Alaves ushindi huo unawafanya kufikisha alama 40 kwenye msimamo huku wakiwa wanapambania nafasi ya kusalia kwenye ligi hiyo

Follow loko kontent

14/05/2026

Wakati young Africans wanapambana kuutafuta ubingwa wao watano mfululizo kule Ufaransa kwenye ligue 1 PSG wameweza kufanya hivyo baada ya kutangazwa kuwa mabingwa wa ligi hiyo kwa msimu wa 2025/26

PSG wamebeba ubingwa huwo kuanzia msimu wa 2021/22 hadi msimuu huu wa 2025/26 na kuwa klabu inayoongoza kubeba mataji mengi ya ligi kuu Ufaransa kwa kufanya hivyo mara 14

Swali ni kwamba wakati mabingwa mara nyingi Ufaransa wanaweza kubeba taji mara tano mfululizo, Vipi mabingwa mara nyingi Tanzania yanga wataweza kufanya hivyo??


Follow loko kontent

13/05/2026

Hull City pamoja na Southampton zimetinga hatuwa ya fainali ya mchujo wa kupanda Ligi Kuu England utakaopigwa tarehe 23 mwezi may

Hull City katika hatuwa ya awali waliwaondosha Milwal huku Southampton wakiwaondosha middlesbrough

Wakati timu hizo zikiwania kupanda Ligi Kuu kwa njia ya mchujo, Coventry pamoja na Ipswich wao wamepanda moja kwa moja kwenye ligi ya EPL

Follow loko kontent

Address

Dar Es Salaam
Dar Es Salaam
0000

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Loko Kontent Digital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share