FGA Tv

FGA Tv Official Facebook account for Fountain Gate Academy Online Tv. Get in touch via our social media pl

Luanda Afro ni chapa ya mitindo ya mikufu ya Brazil inayotoa vifaa vya asili vya mitindo ya kiafrika K**a vile mikufu ,v...
11/08/2025

Luanda Afro ni chapa ya mitindo ya mikufu ya Brazil inayotoa vifaa vya asili vya mitindo ya kiafrika K**a vile mikufu ,vidani na heleni vilivyobuniwa kiustadi na kuchanganywa na vitenga vya rangi za kuvutia. Ikiwa na mtazamo mkali wa utambulisho na urithi wa kitamaduni.

Chapa hii inalenga kuhamasisha watu wenye kupenda kuonyesha utambulisho wao Kwa nguvu na rangi, Kila kifaa kinaeleza hadithi ya asili na urithi ukiwa ni njia ya kujivunia asili na kuinua mawasiliano ya kina kupitia mitindo.

Baadhi ya mapambo hayo yameoneshwa hivi karibuni 12 julai 2025, chapa imepewa taarifa kuhusu staili ya kipekee ikiwa ni njia ya kujivunia asili na kuibua mawasiliano ya madili ya kina kupitia mitindo.

✍️

GWIJI wa Klabu ya Al Ahly Reza Abdel-Aal amezungumza kupitia Mtandao wa YouTube akieleza kuwa Kocha Jose Reveiro hastahi...
11/08/2025

GWIJI wa Klabu ya Al Ahly Reza Abdel-Aal amezungumza kupitia Mtandao wa YouTube akieleza kuwa Kocha Jose Reveiro hastahili kuifundisha Timu hiyo.

"Kikosi cha sasa cha Al Ahly kinahitaji kocha mahiri k**a Takis Gonias angesajili kwa ustadi na kuwafundisha vyema. Riveiro hafai kwa kazi hiyo. Kwa nini Dieng yuko kwenye benchi?" Alihoji GWIJI huyo.

Ikumbukwe kuwa Jose Reveiro alichukua kibarua hilo akichukua nafasi Kocha Marcelo Kohler.

MLINDA mlango wa Crystal Palace Dean Henderson ameshangilia ubingwa wa kombe la Ngao ya jamii Kwa mtindo wa aina yake ma...
11/08/2025

MLINDA mlango wa Crystal Palace Dean Henderson ameshangilia ubingwa wa kombe la Ngao ya jamii Kwa mtindo wa aina yake mara baada ya kumkumbuka Baba yake mzazi aliyefariki Mwaka mmoja uliopita.

Dean alichapicha maneno kwenye Mtandao wake wa kijamii akishika kofia alisema "Baba popote ulipo hii ni Kwa ajili yako"

Kisha akaongeza akisema "nafahamu yupo na Mimi wakati wote na kwenye kila mchezo".

Henderson ameisaidia Crystal Palace kutwaa ubingwa wa Ngao ya jamii mbele ya Liverpool ambapo alifanikiwa kuokoa mikwaju miwili ya penati.

KIUNGO wa zamani wa Simba Sadio Kanoute amerejea tena Ligi Kuu Tanzania bara awamu hii akijiunga na Klabu ya Azam. Kanou...
11/08/2025

KIUNGO wa zamani wa Simba Sadio Kanoute amerejea tena Ligi Kuu Tanzania bara awamu hii akijiunga na Klabu ya Azam.

Kanoute amewahi kucheza Simba Kwa msimu kadhaa ya mafanikio kabla ya Msimu uliopita 2024/25 ambapo aliichezea JS Kyblie.

Azam Sasa wanakwenda kuiboresha safu ya kiungo ambayo tayari Ina wachezaji wengine k**a Himid Mao, Sospeter Bajana, James Akaminko na wengineo.



"Ni wakati sahihi mimi kuingilia kati sakata la Sheikh Walid, kuhakikisha kijana anaenda kutimiza ndoto yake ya kucheza ...
11/08/2025

"Ni wakati sahihi mimi kuingilia kati sakata la Sheikh Walid, kuhakikisha kijana anaenda kutimiza ndoto yake ya kucheza Nje ya Nchi.

Naingilia kati kuhakikisha kijana anauzwa kwa thamani yake halisi na sio Bei za kukurupuka ili kukwamisha Biashara makusudi

Haiwezekani kila mchezaji akitaka kuondoka kwenu ianze vita, Kwa Mayele tulijua bahati mbaya kwa Feisali tukasema haitojirudia tena na sasa kwa Walid hii haikubaliki

Kuzuia mtu asitimize malengo yake ni unyonyaji na unapotaja Bei isiyoendana na uhalisia ni lugha iliyojificha ya kumwambia mtu siuzii bidhaa hii

Hili siwezi kulifumbia macho, Tulimnusuru Mayele, tukamkomboa Fei na sasa ni zamu ya Walid

Kwako Walid wewe endelea kuipigania Tanzania, sisi tutapambana nao na mwisho wa siku tutakukabidhi ushindi Insha Allah".

Ahmed Ally Afisa Habari wa Klabu ya Simba. Unakubaliana nae?

Kocha Jose Riveiro amekuwa na mwanzo mbaya ndani ya Klabu ya Al Ahly jambo ambalo linatishia uwezekano wake wa kudumu kl...
10/08/2025

Kocha Jose Riveiro amekuwa na mwanzo mbaya ndani ya Klabu ya Al Ahly jambo ambalo linatishia uwezekano wake wa kudumu klabuni hapo.

Mpaka Sasa ameiongoza Al Ahly kwenye mechi 04 ameambulia sare 03 na kichapo kimoja.

Utakumbuka kuwa Kocha huyo alianza kukosolewa mapema toka kwenye mashindano ya Kombe la Dunia ngazi ya Vilabu ambapo aliambulia alama Mbili tu kwenye mechi Tatu.

Fashion Cds gwiji wa ubunifu katika ulimwengu wa mitindo,anayejulikana Kwa ubunifu unaovunja mipaka na kusisimua macho y...
10/08/2025

Fashion Cds gwiji wa ubunifu katika ulimwengu wa mitindo,anayejulikana Kwa ubunifu unaovunja mipaka na kusisimua macho ya wapenzi wa mitindo.

Hivi karibuni amewasilisha vazi jipya la ubunifu mchanganyiko wa muundo wa vipengele vya mikato ya kisasa vinavyoleta mvuto wa kisasa

Ikiwa sehemu ya maandalizi ya msimu mpya wa mitindo Ambao Fashion Cds anakuja Kwa nguvu mpya na ubunifu usio wa kawaida.

Kupitia vazi hili, anaonyesha dhamira ya kusukuma mbele mipaka ya ubunifu. Kuunganisha Urithi wa mitindo na mtazamo wa kisasa, huku akiwapa wapenzi wa Fashion msukumo wa kujaribu mitindo mipya yenye ujasiri.



USHINDI wa 2-1 mbele ya Madagascar umetosha kuipa nafasi Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars kutinga hatua ya Robo fai...
09/08/2025

USHINDI wa 2-1 mbele ya Madagascar umetosha kuipa nafasi Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars kutinga hatua ya Robo fainali ya michuano ya CHAN 2024.

Magoli ya Tanzania yamefungwa na Clement Mzize aliyefunga yote mawili mapema kipindi cha kwanza.

Taifa Stars Sasa ipo kileleni Kwa Kundi B baada ya kukusanya alama 9 wakisaliwa na mchezo mmoja dhidi ya Afrika ya Kati.

Umekionaje kiwango cha Taifa Stars?



KWENYE Kombe la Shirikisho barani Afrika hizi hapa Mechi za awali baada ya Droo ya Leo Kwa Timu za Tanzania. Rayon Sport...
09/08/2025

KWENYE Kombe la Shirikisho barani Afrika hizi hapa Mechi za awali baada ya Droo ya Leo Kwa Timu za Tanzania.

Rayon Sports ya Rwanda itacheza na Singida Black Stars huku Eli Merriekh Bentiu ya Sudan Kusini itacheza na Azam FC.

Rayon Sports imekuwa na historia kubwa kwenye soka la nchini Rwanda huku barani Afrika pia iliwahi kutinga Robo fainali ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.

Singida Black Stars watatoboa kirahisi?



BAADA ya Droo ya michuano ya Klabu Bingwa barani Afrika Young Africans SC itakutana na Wiliete Benguela SC kutoka Angola...
09/08/2025

BAADA ya Droo ya michuano ya Klabu Bingwa barani Afrika Young Africans SC itakutana na Wiliete Benguela SC kutoka Angola kwenye mchezo wa hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika.

Klabu ya Simba yenyewe itacheza dhidi ya Gaborone United ya Botwasana ambapo mechi hizo Mbili zitapigwa kati ya Septemba 19-21, 2025 na Michezo ya marudiano itapigwa Septemba 26-28, 2025.

Simba na Yanga wote wataanzia Ugenini.

Nani kaokota kibonde hapa?




KIUNGO mshambuliaji Mpya wa Klabu ya Simba Mohamed Bajaber amesema kuwa wakati anapewa taarifa ya yeye kuhitajika na Sim...
09/08/2025

KIUNGO mshambuliaji Mpya wa Klabu ya Simba Mohamed Bajaber amesema kuwa wakati anapewa taarifa ya yeye kuhitajika na Simba alipokea Kwa mshtuko hali ambayo ilimnyima usingizi kabisa.

"Kaka yangu ndiye aliniambia kuwa Simba wananihitaji, Wala sikusita nilimwambia sawa Haina shida huku nikiipokea hali hiyo Kwa mshangao wa furaha kubwa. Usiku huo sikupata usingizi kabisa Kwa sababu Simba ni timu kubwa" Alisema Bajaber kupitia Simba TV.

Bajaber ameisaidia Police FC ya nchini Kenya kuibuka mabingwa wa Ligi Kuu nchini humo msimu wa 2024/25 kabla ya kujiunga na Simba Kwa ajili ya msimu Mpya wa 2025/26.



LEO saa Mbili kamili usiku itapigwa mechi ya Tatu ya michuano ya CHAN 2024 Kwa Taifa Stars ambapo itacheza dhidi ya Mada...
09/08/2025

LEO saa Mbili kamili usiku itapigwa mechi ya Tatu ya michuano ya CHAN 2024 Kwa Taifa Stars ambapo itacheza dhidi ya Madagascar kwenye Dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Stars ndio vinara wa Kundi B wakiwa na alama zao Sita baada ya kushinda 2-0 mbele ya Burkina Faso kisha kuichapa Mauritania 1-0 kwenye mchezo wa pili.

Mechi ya Leo inakuwa tamu zaidi kwani Stars wakishinda wanakuwa wamefuzu Moja Kwa Moja hatua ya Robo fainali ya Kombe la CHAN 2024 huku wakisaliwa na mchezo mmoja dhidi ya Afrika ya Kati.



Address

P. O. Box 4283
Dodoma
026

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when FGA Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to FGA Tv:

Share