03/01/2026
Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, kesho inatarajiwa kushuka dimbani kuwania nafasi ya kuendelea mbele katika mchezo wa hatua ya 16 bora ya Mashindano ya AFCON 2025.
Ndoto na matarajio ya Watanzania wengi ni kuiona timu yao ikiibuka na ushindi dhidi ya Morocco, matokeo ambayo yangeiwezesha Taifa Stars kuishangaza dunia na kuonyesha ubora halisi wa soka la Tanzania.
Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa, huku kila timu ikiingia uwanjani ikiwa na dhamira ya kusonga mbele katika mashindano hayo makubwa barani Afrika.