FGA Tv

FGA Tv Official Facebook account for Fountain Gate Academy Online Tv. Get in touch via our social media pl

NIGERIA vs CONGO DR kucheza fainali ili kupata timu moja itakayo ungana natimu zingine kutoka afrika ili kucheza kombe l...
14/11/2025

NIGERIA vs CONGO DR kucheza fainali ili kupata timu moja itakayo ungana natimu zingine kutoka afrika ili kucheza kombe la dunia mwakani..

Endelea kutufuatilia kwa Taarifa Mbalimbali kuhusu Michezo

Umewahi kujiuliza kwanini pete ya ndoa huvaliwa mkono wa kushoto katika kidole cha nne? basi ni hivi uvaaji wa pete ya n...
14/11/2025

Umewahi kujiuliza kwanini pete ya ndoa huvaliwa mkono wa kushoto katika kidole cha nne? basi ni hivi uvaaji wa pete ya ndoa katika kidole cha nne mkono wa kushoto ni kwasababu ya asili yake inatokana na imani za kale , hasa kutoka kwa Warumi na Wamisri wa zamani .

Wamisri waliamini kuwa ndani ya kidole hicho cha mkono wa kushoto kuna mshipa unaoitwa vena amoris. Huku wengine wakienda mbali zaidi na kuita mshipa wa upendo , kwani unatoka katika kidole hicho unakwenda moja kwa moja katika moyo wa Binadamu .

Kwao kuvaa pete kwenye kidole hicho kunamaanisha moyo wa mume na mke umeunganishwa na upendo wa kudumu moyoni . Baada ya Wamisri kufanya hivyo, Warumi nao walirithi imani hiyo na kuifanya kuwa sehemu ya mila zao za ndoa , jambo lililoenea hadi Ulaya na baadaye Dunia nzima ikaiga utamaduni huu .

Hata hivyo kwenye baadhi ya tamaduni na nchi k**a Urusi na India pete ya ndoa huvaliwa mkono wa kulia.

Lakini maana yake hubaki palepale kiapo cha uaminifu wa milele. Kwa ujumla kuvaa pete ya ndoa kwenye kidole cha pili cha mkono wa kushoto , ni ishara ya heshima , mapendo.

Mtaalam wa muziki wa R&B na Pop, The Weekend, ameendelea kurudisha fadhira kwa mashabiki zake kutoa msaada mkubwa kwa wa...
14/11/2025

Mtaalam wa muziki wa R&B na Pop, The Weekend, ameendelea kurudisha fadhira kwa mashabiki zake kutoa msaada mkubwa kwa waathirika wa Kimbunga Melissa kilichotikisa Jamaica hivi karibuni.

Kupitia mfuko wake wa misaada, XO Humanitarian Fund, msanii huyo ametangaza mchango wa takribani dola 350,000, sawa na zaidi ya shilingi milioni 900 za Kitanzania.
Fedha hizo zinapelekwa kwa Shirika la Chakula Duniani (WFP) ili kusaidia familia zaidi ya 200,000 zilizopoteza makazi na chakula kutokana na athari za kimbunga hicho kilichoitwa “Storm of the Century.”

Msaada huo utatumika kununua na kusambaza chakula cha dharura ikiwemo mchele, dengu, samaki na nyama za makopo pamoja na mafuta ya kula.

The Weeknd, ambaye jina lake halisi ni Abel Tesfaye, amekuwa akitumia sanaa yake si tu kwa burudani bali pia k**a jukwaa la kuleta matumaini.

Hatua yake imepongezwa na mashabiki na wadau wa muziki duniani, ikionyesha kuwa wasanii wana nafasi kubwa ya kuleta mabadiliko ya kijamii.

XO Humanitarian Fund ni mfuko wa misaada ulioanzishwa na msanii Abel “The Weeknd” Tesfaye mwaka 2022 kwa kushirikiana na Shirika la Chakula Duniani (WFP). Dhumuni lake kuu ni kupambana na njaa duniani na kusaidia waathirika wa majanga ya kibinadamu.

Kimbunga Melissa kilikuwa mojawapo ya vimbunga vikubwa zaidi vilivyowahi kupiga Jamaica mwishoni mwa Oktoba 2025, kikiwa na upepo mkali wa zaidi ya 185 mph na kuacha uharibifu mkubwa wa miundombinu na maisha ya watu.
Cc

Muigizaji maarufu wa Marekani, Josh Duhamel, aliyezaliwa Novemba 14, 1972, amejijengea jina kubwa katika ulimwengu wa sa...
14/11/2025

Muigizaji maarufu wa Marekani, Josh Duhamel, aliyezaliwa Novemba 14, 1972, amejijengea jina kubwa katika ulimwengu wa sanaa ya uigizaji.

Safari yake ilianza kwenye tamthilia ya televisheni All My Children, ambapo alionesha kipaji cha kipekee na kushinda tuzo ya Emmy.

Umaarufu wake ulipanuka zaidi aliposhiriki kwenye filamu kubwa ya Transformers, akicheza k**a Luteni Kanali William Lennox. Uwezo wake wa kuunganisha uhalisia na mvuto wa kisanii ulimfanya kuwa mmoja wa nyota wanaotambulika sana katika tasnia ya filamu. Mbali na Transformers, Duhamel ameonekana kwenye filamu k**a Safe Haven na Life as We Know It, akionyesha upeo wake wa kuigiza katika aina tofauti za burudani kuanzia mapenzi, vichekesho hadi vituko vya kisayansi.

Kwa mchango wake mkubwa katika sanaa ya filamu na televisheni, Josh Duhamel anabaki kuwa mfano wa msanii aliyejituma na kuacha alama ya kudumu katika burudani ya dunia.

Cc

Unaweza kusema kweli umri ni namba tu, usemi huu unatupeleka kwa kinda wa kimataifa mchezaji wa timu ya taifa wa Ufarans...
14/11/2025

Unaweza kusema kweli umri ni namba tu, usemi huu unatupeleka kwa kinda wa kimataifa mchezaji wa timu ya taifa wa Ufaransa na klabu ya Real Madrid , Kylian Mbappe alizaliwa mnamo tarehe 20 disemba 1998 mpaka sasa anaumri wa miaka 26 tu. Lakini takwimu zake ni zaidi ya umri wake .

Mbappe mpaka sasa kafanikiwa kufunga magori mia nne (400) ndani ya miaka 26 . Na msimu huu pekee mbappe amechangia mabao 28 ndani ya michezo 20 katika timu ya Taifa pamoja na klabu yake ya Real Madrid .

Unaweza sema ,Mbappe anaweza fikia ndoto za Ronald ambaye mpaka sasa ana umri wa miaka 40 akiwa amefikisha idadi ya mabao 953 .

Moja ya namba 10 bora miaka wa hivi karibuni, Kylian Mbappe kutoka Timu ya Taifa ya Ufaransa na klabu ya Real Madrid.

2025 imekuwa na mafanikio makubwa sana kwenye upande wa burudani lakini kwa wale wote waliofunga ndoa na vipenzi vyao, t...
13/11/2025

2025 imekuwa na mafanikio makubwa sana kwenye upande wa burudani lakini kwa wale wote waliofunga ndoa na vipenzi vyao, tukianza na Osmane Dembele baada ya kushinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka duniani upande wa mpira wa miguu, lakini pia kwa Jeremy Doku kukiwasha sana siku hizi akiwa dimban, kufikia Mpaka kwa Bad Man baada ya kufunga ndoa na mwanadada kutoka Nigeria Priscilla, ameanza kung’aa kipande hicho cha Naija.

Hii imekuja baada ya Muimbaji huyo kuandaa tamasha lake binafsi litakalofanyika 18 Desemba mwaka huu, ukweni yaani Nigeria na kuwa Msanii wa kwanza kutoka bongo Tanzania kufanya hivyo, kupitia ukurasa wake wa Instagram ameshare video ya tangazo la tamasha hilo kasha kuandika maneno yafuatayo:

“Upendo na sapoti ambayo ninyi nyote mmenionyesha umekuwa wa ajabu sana! Najisikia k**a niko nyumbani hapa Nigeria. Kila jiji lina mdundo wake, lakini Lagos lina roho. TAREHE 18 DESEMBA, tunakuja kwa ukubwa — tukileta upendo wote, maisha, na urithi pamoja! Kutoka Tanzania hadi Nigeria, moja kwa moja.”

Jux aliongezea kwa kusema: Juma Jux in Lagos si tukio la muziki pekee bali ni mkutano wa kifamilia unaounganisha watu kupitia upendo na positive vibes.

Tutegemee ukubwa wa tamasha na kufungua macho kwa wasanii wengine kuchukua hatua k**a kwa manufaa ya muziki wa Tanzania.

Cc

Golden Landis Von Jones, anayejulikana kwa jina la kisanii 24kGoldn, ni staa kijana anayetikisa muziki wa hip-hop na pop...
13/11/2025

Golden Landis Von Jones, anayejulikana kwa jina la kisanii 24kGoldn, ni staa kijana anayetikisa muziki wa hip-hop na pop duniani. Alizaliwa Novemba 13, 2000 na jina lake la jukwaa linamaanisha “dhahabu safi ya karati 24,” ishara ya ndoto zake zisizo na doa.

Safari yake ya muziki ilianza mwaka 2016, lakini ni mwaka 2019 alipovuma kupitia wimbo “Valentino” uliopata mamilioni ya streams na kumuingiza kwenye chati za Billboard.

Mafanikio makubwa zaidi yalikuja mwaka 2020 kupitia wimbo “Mood” aliomshirikisha Iann Dior, ulioshika nafasi ya kwanza kwenye Billboard Hot 100 na kumfanya kuwa nyota wa kimataifa.

Mwaka 2021, 24kGoldn alitoa albamu yake ya kwanza El Dorado, ikimthibitisha k**a sauti mpya yenye nguvu katika kizazi cha muziki wa trap na pop. Muziki wake unachanganya mitindo tofauti na kuvutia mashabiki kote duniani, hasa kupitia mitandao ya kijamii na majukwaa ya kusikiliza muziki mtandaoni.

Kwa sasa, 24kGoldn anaonekana k**a mfano wa vijana wanaotumia teknolojia na ubunifu kufanikisha ndoto zao. Kutoka mitaa ya San Francisco hadi kilele cha chati za dunia, kijana huyu ameonyesha kuwa muziki ni daraja la kuunganisha tamaduni na vizazi.

Cc

2025 imekuwa na mafanikio makubwa sana kwenye upande wa burudani lakini kwa wale wote waliofunga ndoa na vipenzi vyao, t...
13/11/2025

2025 imekuwa na mafanikio makubwa sana kwenye upande wa burudani lakini kwa wale wote waliofunga ndoa na vipenzi vyao, tukianza na Osmane Dembele baada ya kushinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka duniani upande wa mpira wa miguu, lakini pia kwa Jeremy Doku kukiwasha sana siku hizi akiwa dimban, kufikia Mpaka kwa Bad Man baada ya kufunga ndoa na mwanadada kutoka Nigeria Priscilla, ameanza kung’aa kipande hicho cha Naija.

Hii imekuja baada ya Muimbaji huyo kuandaa tamasha lake binafsi litakalofanyika 18 Desemba mwaka huu, ukweni yaani Nigeria na kuwa Msanii wa kwanza kutoka bongo Tanzania kufanya hivyo, kupitia ukurasa wake wa Instagram ameshare video ya tangazo la tamasha hilo kasha kuandika maneno yafuatayo:

“Upendo na sapoti ambayo ninyi nyote mmenionyesha umekuwa wa ajabu sana! Najisikia k**a niko nyumbani hapa Nigeria. Kila jiji lina mdundo wake, lakini Lagos lina roho. TAREHE 18 DESEMBA, tunakuja kwa ukubwa — tukileta upendo wote, maisha, na urithi pamoja! Kutoka Tanzania hadi Nigeria, moja kwa moja.”

Jux aliongezea kwa kusema: Juma Jux in Lagos si tukio la muziki pekee bali ni mkutano wa kifamilia unaounganisha watu kupitia upendo na positive vibes.

Tutegemee ukubwa wa tamasha na kufungua macho kwa wasanii wengine kuchukua hatua k**a kwa manufaa ya muziki wa Tanzania.

Cc

Watoto wa kisasa wanazidi kung’aa kwa mitindo yao ya kuvutia.Wasichana huvaa jeans kali,short pens na sketi fupi wakimec...
12/11/2025

Watoto wa kisasa wanazidi kung’aa kwa mitindo yao ya kuvutia.Wasichana huvaa jeans kali,short pens na sketi fupi wakimechisha na top maridadi,raba safi na vikoti vya kifashion vinavyo ongeza mvuto wa muonekano wa kisasa na wakishua zaidi wakijiamini na wenye rangi zinazopendeza.

Wavulana nao hawabaki nyuma kwa mitindo ya mavazi Yao wakitupia mikato ya kijanja na yakuvutia zaidi uvalia mkato wa kwenda k**a pens kali,tisheti kali nyeusi ,kofia ya pama au cap ya kawaida ya kwenda.

Wanaonekana nadhifu kwa mtindo wa watoto wa mtaani wenye ladha ya kisasa, kwa ujimla mtindo wa mavazi kwa watoto wa mchanganyiko na ubunifu wakisasa.kila vazi linaeleza utu wao, furaha yao na namna wanavyopenda kupendeza kwa njia ya kipekee.

Dunia ya burudani ilipoteza nguzo muhimu mnamo tarehe 12 Novemba 2018, baada ya kufariki kwa Stan Lee, gwiji wa ubunifu ...
12/11/2025

Dunia ya burudani ilipoteza nguzo muhimu mnamo tarehe 12 Novemba 2018, baada ya kufariki kwa Stan Lee, gwiji wa ubunifu aliyeunda ulimwengu wa mashujaa wa Marvel Comics. Lee, ambaye alifikisha umri wa miaka 95, alifariki akiwa Los Angeles, Marekani, na kuacha urithi mkubwa uliogusa vizazi vingi kupitia kazi zake.

Stan Lee, jina halisi Stanley Martin Lieber, alianza kazi yake katika Timely Comics miaka ya 1940 kabla kampuni hiyo kubadilika kuwa Marvel. Kupitia ubunifu wake, alitoa taswira mpya kwa mashujaa wa komiki mashujaa wenye utu wa kawaida, mapungufu, na hisia k**a binadamu wengine.

Kutoka kwa Spider-Man, Iron Man, The Hulk, Thor, hadi Black Panther, kila mhusika wake aliibeba falsafa ya matumaini, ujasiri, na uthubutu.

Kwa mashabiki wa sinema, Lee alijulikana pia kwa “cameo appearances” zake zile sehemu ndogo ambazo alionekana kwenye filamu za Marvel akicheka au kutoa maneno ya hekima. Hilo likawa alama yake ya kipekee, na kila mashabiki walipomwona, ukumbi mzima ulilipuka kwa shangwe.

Kifo chake kilileta simanzi kwa mashabiki duniani kote, huku mitandao ya kijamii ikifurika salamu za rambirambi kutoka kwa wasanii, waigizaji, na wapenzi wa komiki. Marvel Studios ilimuelezea k**a “moyo wa ulimwengu wa Marvel.”

Leo, miaka kadhaa baada ya kuondoka kwake, jina la Stan Lee linaendelea kuishi kupitia sinema, vitabu, na mamilioni ya mashabiki wanaovaa fulana za mashujaa wake. Urithi wake unabaki kuwa kumbukumbu kwamba ubunifu, unapochanganywa na moyo wa binadamu, unaweza kuunda ulimwengu usio na mwisho wa burudani.

Cc

Mnamo tarehe 12 Novemba 1955, dunia ya muziki ilishuhudia mapinduzi makubwa wakati jarida maarufu la Billboard lilipoanz...
12/11/2025

Mnamo tarehe 12 Novemba 1955, dunia ya muziki ilishuhudia mapinduzi makubwa wakati jarida maarufu la Billboard lilipoanzisha mfumo mpya wa kuchanganua nyimbo maarufu nchini Marekani.

Kwa mara ya kwanza, matokeo ya nyimbo hayakutegemea hisia au upendeleo wa watangazaji, bali data halisi kura kutoka redio, matumizi ya jukebox, na mauzo ya rekodi.

Hatua hiyo ilifungua ukurasa mpya katika historia ya muziki, ikiweka msingi wa kile kinachoitwa leo “Billboard Hot 100”. Mfumo huu uliwawezesha wasanii, watayarishaji na mashabiki kuona kwa uwazi ni nani kweli aliyekuwa juu kwenye chati za mauzo na usikilizaji.

Kabla ya mwaka huo, mafanikio ya msanii yalipimwa kwa maneno ya mashabiki na magazeti ya burudani pekee.

Lakini baada ya 1955, takwimu za Billboard zikawa dira rasmi ya umaarufu, zikisaidia kuzaliwa kwa nyota wakubwa k**a Elvis Presley, The Beatles, na baadaye Michael Jackson.

Kwa miaka mingi, chati hizo zimekuwa kipimo cha ubora na kipenzi cha mashabiki wa muziki duniani. Hata leo, msanii anapopanda kwenye chati za Billboard, ni k**a amepanda kilele cha heshima katika tasnia ya muziki.

Tukio la 12 Novemba 1955 linabaki kuwa kumbukumbu muhimu siku ambayo muziki ulianza kupimwa kwa namba, si maneno.

Cc

Address

P. O. Box 4283
Dodoma
026

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when FGA Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to FGA Tv:

Share