Hon. Amina Mollel

Hon. Amina Mollel We are a content production page that educates the community of Agriculture, farming activities, Politics, Sports and Social issues.

30/07/2025

Mijitu mingine bana, inakeeraaaaaa!!!! Wewe ungefanyaje!? Au adhabu hii inatosha??

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Edward Pastory, Shao Delton, Ezekiel Mai'joh, Barnabas Lu...
30/07/2025

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Edward Pastory, Shao Delton, Ezekiel Mai'joh, Barnabas Lugwisha, Juma Bwanga, Chaa Sheha Mohammed, Solomon Laizer, Khadija Abdallah, Harrison Shange, Elidaima Daniel Pallangyo Mydear, John Mrosso, Gereone Geremonga, Anselm Ngulugulu, Deogratius Shau, Friedrich Mboya, Charles Msama, Roselyn Moshi, Joyceline M Ezek, Loshiva Ole Leikoyo, Emanuel Arteta Edward Shayo, Mahamudu Mwidete, Prisca Mhangwa, Msafiri Supana Maduhu, Mteule Mteule, Yuda Lupoja, Lucas Kimat, Jamal Khatib Ameir, Ombeni Ndege, Mary Fonga, Bahati Michael, Deo Junior, Samwel Nassari, Gidion Lekimbashe, Emmanuel Issack, Priscus August, Beritini Asenga, Justine James, Grace Jacob, Karimu Muhidini, Danieli Sipira, Amina Tiboka, Rhoda Glory Daniel, Issaiah Julius, John Elias, Maglan Samwel, Mwajuma Hassan, Dhambi Inaua Church, Wilbart Miagie, Makaveli Mwakanosya, Joseph Kivuyo

24/07/2025

Ingekuwa wewe ungefanyaje!? Inahitaji akili ya ziada kufanyà maamuzi haya.

23/07/2025

Tujikumbushe Enzi hizo Miaka 14 iliyopita. Amina katika ubora wake. Katika Dunia hii ya Sasa ogopa sana teknolojia inaweza kukuwekea kumbukumbi nzuri au mbaya ambazo zitakifanya uchukie mitandao wakati wote wa maisha yako.

Tukiwa na kumbukumbu nzuri watoto wetu watajifunza mengi kutoka kwako.
Pumzika Kwa Amani Elisha Eliah, Babu wa Loliondo pamoja na Mzee wetu Isdory Shirima aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha wakati huo.

Je babu wa Loliondo anakukumbusha nini!? Tujikumbushe hapa.

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Victor Uiso, Peter Lilayon, Onesmus Nyange Mayuta, Mareka...
23/07/2025

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Victor Uiso, Peter Lilayon, Onesmus Nyange Mayuta, Marekani Thabith, Daniel Akonaay Jr., Rajabu Kun Mary, Nelson James, Dayo Bayo, Steve Shayo, Baraka Mkekena, Bedan Karani, Haruna Kaindoan Murishidi, Mariam Shaibu Sudi, Ally Ngatawila, Ereneo Mweusi Kiria, Naj Kimaro, Simon Matei, Fatma Ally, Hassan Tukwa, Janepher Valley, William Mungaya, Paulo Nela, George Stanley, Hamad Mutembei, Hemed Mwinyi, Shomari Masunga Athuman, Anna Maronga, Subi Kibona, Mejja Marley, Shemngodo Abdulrahman, Said Idd, Lomnyack Saimalie, Hamisa Mmbaga, Rose Ngalai, Richard Waziri, Rebeca Nyagenge, Filbert Shija, Amina Shaban, Furaha Edson, Shaban Mustafha, Edna Sarakikya, Elizabeth Lyimo, Jasmin Douglas, Maria Kailasy, Mackie Yohana, Emanueli Mgheni, Peter Meidimi, Jimmy Chikwedo, Emmy Muk**a, Erick Lutonja

Lemaasa kimbotitoii!! Wapi Ile mutu nasema mie hapana vaa rubega. Jasiri haachi asili yake na huku ndio kwetu. Tunazungu...
21/07/2025

Lemaasa kimbotitoii!! Wapi Ile mutu nasema mie hapana vaa rubega. Jasiri haachi asili yake na huku ndio kwetu. Tunazunguka mjini kutafuta riziki mwisho wa siku narudi nyumbani kwetu Laarusa.

Hili tukio huwa tunakula ngiring,o mbankanacheua yenyewe. Walete wenye Mila Yao Morani na masiangik wao. Napenda sana kabila yangu bila kusahau Kwa mama yangu na watani wetu Murangi.

Halafu sisi wamasai tunaamini ng'ombe wote hapa nchini ni wakwetu, hii kabila nyingine nachukua kutoka kwetu. Mukuje watani wetu tufurahi.

Isome hii Ina fundisho kubwa ndani yake.Mwaka 2008 baada ya kumaliza chuo na kuingia mtaani , kila mtu akipambana na mai...
20/07/2025

Isome hii Ina fundisho kubwa ndani yake.

Mwaka 2008 baada ya kumaliza chuo na kuingia mtaani , kila mtu akipambana na maisha kujikwamua. Ilipofika mwkaa 2015 tukawa na group letu kubwa la darasa la uchumi. Mwezi June 2015 iliingia message ya mchumi mwenzetu Jimmy. Ilisema hivi “wachumi wenzangu mko salama, ninawataarifu ninaumwa snaa, nina kansa stage ya mwisho, natamani walioko dsm mje kunitembelea ocean road, kuna msaada nahitaji”.
Mapema saa saba tulikuwa ocean road classmates k**a 19. Tukaingia kumuona. Baada ya kusalimiana na pole jimmy alizungunza, Alisema hivi “sihitaji mnisaidie kitu mimi, ila mjue mimi nililewewa bila kumjua baba, mama yangu ni mzee huyu mliyemsalimia shikamoo bibi, hana ndugu wala mtoto zaidi yangu mimi, najua sitapona kwa namna yeyote, k**a mkiweza nitunzieni mama yangu”.
Hapo kila mtu na saikolojia yake alimtia moyo na kumwambia atapona asikate tamaa. Na wengine walitoa mawazo ya dawa za mitishamba na ushuhuda wa watu waliopona kwa magonjwa k**a
Hayo.
Jioni ya saa 10 Kwemye group tulikubaliana hapo tumtoe jimmy ili tujadili mchango wa matibabu yake, kweli saa 11 jioni admin alimuondoa kwa muda lakini kumbe alimuondoa milele.
Saa mbili usiku wa siku hiyo hiyo tulipata taarifa Jimmy ameenda kwa muumba wake wakati mchango ukiwa umefika laki 2 tu. Huku wengine walikuwa wakihoji kuwa kumekuwa na wagonjwa wengi na michango mingi hivyo tupeane muda.
Kundi lilizizima na hakuna mtu aliongea kwa masaa 6, mawazo yalikuwa kwa mama Jimmy kuliko kwa rafiki yetu.
Leo ni miaka 10, mama wa jimmy anachangiwa kila mwezi 184x10,000=1,840,000. Na wengine wanatoa zaidi. Anaishi tabora na kila mchumi yeyoye akipita tabora lazima Akamjulie hali. Mama Jimmy kazaa mtoto mmoja na sasa kapata watoto 184, kashindwa kutujua majina wote, tumemwambia atuite pacha inatosha, yani pacha wa moyo wa Jimmy. Tunaamini Jimmy ana amani alipolala na amani iendelee.
Wako kina mama Jimmy wengi kwa wenzetu wanaotangulia mbele za haki . Lakini tunashindwa kuwatambua na kuwapa msaada. Ninakumbusha:
1. Usione aibu kuwaambia rafiki zako shida zilizo nje ya uwezo wako ata k**a hawajakusaidia.
2. ⁠hakuna mtu anayeweza peke yake bila kushikwa mkono
3. ⁠kwenye group mlioko mkumbuke siku moja ya kukutana na siku hii muweke maombi ya wana group waliotangulia kwa kuita familia zao, mtajua mengi tena rahisi kuwasaidia
4. ⁠urafiki unaanzia pale ambapo unayewajibika kwa urafiki wenu hawezi kukurudishia fadhira zako na bado ukawajibika kwake
5. ⁠dunia tunapita ila nyanyua mkono wako kwa uwezo wako kwa ajili ya wengine.
6. ⁠leo iwe siku muhimu kila group kuulizana mama jimyy na watoto wako salama, hakuna kilichoko ndani ya uwezo wetu tunachoweza kuwasaidia kutokea kwenye group letu.
Rafiki mpendwa wa Jimmy

Jasiri haachi asili. Miaka hiyo nikiwa enditoo wenyewe wanaelewa maana ya enditoo, ni hivi vibuyu wakati wote vilijaa ch...
19/07/2025

Jasiri haachi asili. Miaka hiyo nikiwa enditoo wenyewe wanaelewa maana ya enditoo, ni hivi vibuyu wakati wote vilijaa chakula cha asili oloshoroo.

Raha yake umetoka shule mchana wa Jua Kali halafu kibuyu kimoja kina Kulee ya Jana jioni then mix na loshoroo jamani!!!?

Niitieni wale enditoo ambao wakati huo akija morani nyumbani k**a kumepikwa mboga za majani na metii Kule wanajificha. Hivi Bado ipo mpaka Leo!?

Ila Moran waliwabeba rafiki zangu Miaka hiyo, iliniuma sana. Umehitimu TU darasa la Saba morani wanakusubiri njiani unabebwa na ndio tayari mke wa mtu hivyo. Hivi hii tabia Sasa imeisha au bado?

Mkataa kwao mtumwa, nyie enditoo wa wakati ule. Haaaaaaaa penda sana asili yangu.

KIDILE   MWARI KIVIKA. Niitieni wenye Lugha yao Wazaramo.Haya NGOMA  YA  MTOTO IMEFIKA
18/07/2025

KIDILE MWARI KIVIKA. Niitieni wenye Lugha yao Wazaramo.

Haya NGOMA YA MTOTO
IMEFIKA

Ukiyaharibu maisha ya mwenzako kwa Chuki, fitina, kashifa, kumtangazia ubaya Kwa viongozi wake, jirani zake na hata ndug...
17/07/2025

Ukiyaharibu maisha ya mwenzako kwa Chuki, fitina, kashifa, kumtangazia ubaya Kwa viongozi wake, jirani zake na hata ndugu zako huku ukijua kabisa kuwa unayosema ni uongo, na ni kwa chuki zako binafsi Ili aonekane mbaya wakati siyo kweli, tambua kuwa ni suala la muda TU, huo ni Mkopo na Siku Moja utalipa mkopo huo tena kwa maumivu makali.

Ni suala la muda TU ukweli utajulikana sababu mwisho wa Ubaya ni kuona AIBU..

16/07/2025

Hiki kipaji Siyo cha gereji huyu ni lnjinia wa madaraka, huyu ni Mfugale Jr. Aendelezwe atakuja Jenga Madaraja na Magorofa. Mwenyezi Mungu msaidie mtoto huyu atimize ndoto zake.

Tujikumbushe KidogoHome of inspirationACHA  NIKUAMBIE KITU!!Ukimhukumu samaki kwa kushindwa kupanda mti utakua umekosea,...
14/07/2025

Tujikumbushe Kidogo
Home of inspiration

ACHA NIKUAMBIE KITU!!

Ukimhukumu samaki kwa kushindwa kupanda mti utakua umekosea, wewe mtupie kwenye maji uone atakavyo kata mawimbi. Kuna mahali ukiwekwa utafanya vitu vya ajabu mpaka Dunia itashangaa.

Usimpotezee mtu anayejitahidi kukujali. Siku akiondoka ndio utagundua ulikua bize unaokota mawe badala ya dhahabu.

Kwa nini unahangaika na kuumia unaposemwa vibaya na watu wasio kufahamu kiundani? Inamaana hujui kuwa mbwa hum'bwekea mtu asiyemfahamu.

Unapopaka make-up ili upendeze, jitahidi pia kuupendezesha moyo wako kwa kufanya matendo mema maana haina maana kupendeza usoni wakati moyoni ni pachafu.

Usikimbilie kuolewa au kuoa mtu tajiri, olewa au oa mtu mwema maana hakuna tajiri atakayeweza kuununua moyo mwema na moyo mwema ni chanzo cha amani na amani ikiwepo ndo kufurahia maisha sasa.

Hii na wewe chukua na weka akilini kabisa, ukitaka kupunguza matatizo katika maisha yako jitahidi uwe unafuata utaratibu.

Nakwambia ukweli na wewe ndio unamjua, watsap anauwezo wa kuku-block, instagram anauwezo wa kuku-block na facebook anaweza kuku-block lakini kamwe hawezi kuzi-block baraka zako kutoka kwa Mungu zitokako katika Mbingu yake tukufu.

Hivi unawezaje kuuza ng'ombe wako eti tu kwa vile umepata oda ya ngozi. Ukiona mtu anachezea utu wako kaa nae mbali maana watu wengine ni kweli k**a mkaa, asipokuunguza basi atakuchafua.

Hivi, ulishawahi kuona mti uko bize unasumbuka na majani yaliyoanguka? Mti hua bize kutengeneza majani mapya, nawewe kuwa bize kutengeneza na kukaribisha vitu vipya na sio vilivyopita.*

*Swali lenye majibu ya maisha yako yote, Je hicho unachokifanya ndicho Mungu alichokuleta Duniani ukifanye? K**a jibu lako ni hapana, basi unahaki kuendelea ku-struggle bila faida

MWISHO

Address

Chamwino
Dodoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hon. Amina Mollel posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Hon. Amina Mollel:

Share