sera media

sera media Follow Sera Media WhatsApp channel

https://whatsapp.com/channel/0029Vb5rTYfLikg6gjHbxi0o

01/08/2025
Ningeambiwa  nitoe maoni yangu k**a ni sahihi kwa kundi la maprofesa kuwania ubunge, ningeanza kwa kuwapongeza na kuwaom...
30/07/2025

Ningeambiwa nitoe maoni yangu k**a ni sahihi kwa kundi la maprofesa kuwania ubunge, ningeanza kwa kuwapongeza na kuwaombea wafanikiwe katika harakati zao ikiwa tu wanaenda kutenda jambo lililo sahihi.

Zamani wakati tunakua, tukisikia mtu fulani ni "profesa" unapata picha ya mtu mwenye akili kubwa kwelikweli, sijui k**a walikuwa na ukubwa huo wa akili tuliokuwa tunafikiri au ni kwasababu tu tulikuwa hatuwaoni kwenye mazingira yetu.

Maprofesa wengi wamekuja kudhihirisha dhana ya ukubwa wa akili kuwa na utata baada ya kujiingiza kwenye siasa. Kwa ufupi wamekuja kwenye mazingira yetu na kujidhihirisha tofauti na mwanzo walipokuwa mbali nasi.

Swali lenye utata linabaki kuwa, je Maprofesa hawana uwezo mkubwa wa akili?

Binafsi bado naamini uwezo wao wa akili ni mkubwa sana ila tatizo wameingia eneo la siasa za Kiafrika ambako unatakiwa kuunga mkono hoja. Tabia ya kuunga mkono kila hoja ili tu ubakie kwenye madaraka ni matusi makubwa sana. Matusi haya hayaishii kwa wasomi walioko madarakani tu bali yanawaumiza hata wasiohusika.

Tumesikia tambo mbalimbali za kukejeli wasomi kutokuwa na msaada sahihi kwenye nchi kwasababu ya michango yao na mamuzi yao yenye utata.

Tatizo siyo kwamba wasomi kwa ujumla wao hawana uwezo, isipokuwa wameamua kuitikia ndiyo mzee ili waepuke kurudishwa majalalani, huko vyuo vikuu pasipo na maslahi.

Nihitimishe kwa kuwaomba wasomi wetu wote bila kujali maprofesa pekee, iokoeni CCM, iokoeni nchi. Simamieni maono yenu yenye maslahi mapana ya nchi, mkiona mnapingwa bila sababu za msingi, lindeni taaluma zenu kwa kurudi vyuoni mkafundishe.

Maoni ya sera media.

Klabu ya Simba imemtambulisha Beki wa Kati, raia wa Afrika Kusini Rushine De Reuck aliyekuwa akikipiga Mamelodi Sundowns...
29/07/2025

Klabu ya Simba imemtambulisha Beki wa Kati, raia wa Afrika Kusini Rushine De Reuck aliyekuwa akikipiga Mamelodi Sundowns.

Mwijaku jina lake halijafanikiwa kupitishwa kwenye idadi ya wagombea wanne waliyopitishwa kuomba ridhaa ya kugombea Ubun...
29/07/2025

Mwijaku jina lake halijafanikiwa kupitishwa kwenye idadi ya wagombea wanne waliyopitishwa kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge katika Jimbo la Mvomero Morogoro kupitia chama cha Mapinduzi CCM.

Chief Godlove jina lake halijafanikiwa kupitishwa kwenye idadi ya wagombea wanne waliyopitishwa kuomba ridhaa ya kugombe...
29/07/2025

Chief Godlove jina lake halijafanikiwa kupitishwa kwenye idadi ya wagombea wanne waliyopitishwa kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge katika Jimbo la Kyela mkoani Mbeya kupitia chama cha Mapinduzi CCM.

Address

Dodoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when sera media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share