sera media

sera media Follow Sera Media WhatsApp channel

https://whatsapp.com/channel/0029Vb5rTYfLikg6gjHbxi0o
(1)

Jeshi la Polisi katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Septemba 6, 2025 limeeleza kuwa wameona picha mjongeo inayosamba...
06/09/2025

Jeshi la Polisi katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Septemba 6, 2025 limeeleza kuwa wameona picha mjongeo inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha mwanamke akimnywesha pombe mtoto mdogo jambo ambalo ni ukatili kwa mtoto na ni kinyume cha sheria za nchi.

Jeshi hilo limetoa wito kwa yeyote anayemfahamu mwanamke huyo asisite kutoa taarifa kwa njia yoyote atakayoona inafaa ambayo ni rahisi kwake au kupitia namba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi 0699 998899.

Kwa upande wake, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dk Dorothy Gwajima kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram ametoa wito waliorekodi na kusambaza na wanaoijua familia hii watoe ushirikiano kwa kuwataja badala ya kuendelea kuisambaza.

Mkurugenzi wa Jamii Forum Maxence Melo, amejiuzuru nafasi yake k**a  Mjumbe wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi. aMelo ...
06/09/2025

Mkurugenzi wa Jamii Forum Maxence Melo, amejiuzuru nafasi yake k**a Mjumbe wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi. a

Melo alianza majukumu k**a Mjumbe wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi Disemba 18, 2023.

Akituma taarifa hiyo leo kupitia mitandao ya kijamii Melo ameandika, "Leo, Septemba 06, 2025 nimemuandikia rasmi Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari juu ya uamuzi wangu kujiuzulu ujumbe wa Bodi katika Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi"

"Aidha, naishukuru Taasisi yangu na Bodi ya Wakurugenzi kwa kulipa gharama zote za ushiriki wangu katika vikao vyote na shughuli za Tume kwa takribani miaka miwili."

Ikumbukwe kuwa Jamii Forum iliyokuwa ikisimamiwa na Maxence Melo imesitishiwa na TCRA leseni kwa muda siku tisini.

Jamii Forum imekutwa na kadhia ya kusitishiwa leseni  na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).TCRA imechukua hatua ya ...
06/09/2025

Jamii Forum imekutwa na kadhia ya kusitishiwa leseni na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

TCRA imechukua hatua ya kusitisha Leseni ya Maudhui Mtandaoni ya JamiiForums kwa muda wa siku 90 na kuzuia upatikanaji wa jukwaa hilo kwa maelezo ya kukiuka Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta kuhusu maudhui mtandaoni.

TCRA imesema uamuzi huu umetokana na JamiiForums kuchapisha taarifa ya Mwanasiasa Humphrey Polepole kuhusu Rostam kumiliki mgodi wa makaa ya mawe kwa asilimia 70 na taarifa za uhusiano kati ya Rais wa Tanzania na “Mfanyabiashara” Wicknell Chivayo bila kuzingatia mizania.

Kwa mujibu wa TCRA, JamiiForums ilishindwa kutafuta maoni ya Mamlaka husika/Msemaji wa Rais/Serikali, kuthibitisha uhalisia wa picha (za Rais na Chivayo) zilizotumika, na hivyo kuuaminisha Umma taarifa za upande mmoja.

Aidha, TCRA imeeleza kuwa jukwaa la JamiiForums halikudhibiti maudhui yenye lugha ya matusi, kashfa na kejeli dhidi ya Rais wa Tanzania, na kuendelea kuhifadhi maudhui hayo ambayo bado yanapatikana kwa umma.

TCRA imeongeza kuwa maudhui hayo yanakinzana na mila, desturi na utamaduni wa Kitanzania, hivyo kuhatarisha mshik**ano wa kitaifa, amani na taswira ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

05/09/2025

Address

Dodoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when sera media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share