sera media

sera media Follow Sera Media WhatsApp channel

https://whatsapp.com/channel/0029Vb5rTYfLikg6gjHbxi0o
(1)

16/11/2025

leo tarehe 15 Novemba 2025 Baraza la Maaskofu Katoliki  Tanzania na Shura ya Maimamu wametoa matamko ya kulaani mauaji y...
15/11/2025

leo tarehe 15 Novemba 2025 Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania na Shura ya Maimamu wametoa matamko ya kulaani mauaji ya raia yaliyofanyika wakati na baada ya uchaguzi wa tarehe 29 octoba 2025.

Wakionyesha kusikitishwa na mauaji hayo, viongozi hao wa dini wamesema watu waliouwawa wametendewa unyama wakati wakitekeleza takwa la kikatiba la kuandamana ili kudai haki zao. Kutokana na tukio hilo wameomba uchunguzi wa kina ufanyike huku ukihusisha vyombo vya ndani na nje.

Pia viongozi hao wamesema serikali iache kutumia nguvu badala yake ijifunze kusikiliza madai ya watu.

Shura ya maimamu Wakienda mbali zaidi, wamesema kuwa uchaguzi uliofanyika haukuwa huru na wahaki na hawapo tayari kutambua matokeo ya uongozi uliopo.

Ili kuondoa ombwe la dhuluma na upendeleo, viongozi wote wa dini wameitaka serikali kuanzisha mchakato wa katiba mpya itayokubalika na jamii nzima.

Na Godbless Lema Siasa ya ukombozi ni harakati takatifu ya kupigania haki, utu na uhuru wa watu. Haipaswi kabisa kubadil...
13/11/2025

Na Godbless Lema

Siasa ya ukombozi ni harakati takatifu ya kupigania haki, utu na uhuru wa watu. Haipaswi kabisa kubadilishwa kuwa biashara ya udalali au njia ya kujinufaisha binafsi. Ndani yake kuna maumivu, vifo, na mateso ya kweli ya wapigania haki. Ni jambo la kusikitisha kuona watu wanaojitokeza leo wakitafuta uhalali wa kisiasa tena, ilhali jana walishirikiana na watesi na wakatili. Ushirikiano huo hauwezi kufutwa kwa maneno matamu , kwani ni doa katika historia ya ukombozi.

Mtu yeyote ambaye hakusimama upande wa haki wakati ulipohitajika, bali akajitahidi kuzima sauti za waonewa, ni mtesaji na muuaji k**a wale tunaowalaumu leo. Sasa wanarudi kwa mbinu mpya k**a “drones” zinazojaribu kutua kwa ujanja lakini ukweli unabaki pale pale, hawa ni wanafiki wanaojificha nyuma ya kivuli cha siasa.

Ukombozi wa kweli hauwezi kuletwa na walafi wa mamlaka, bali na watu waaminifu kwa misingi ya haki, uadilifu, utu wa mwanadamu. Tunapaswa kukemea tabia hizi, kwani hii haipaswi kuwa tabia ya Nchi yetu na watu wake

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limempitisha Dkt. Mwigulu Nchemba, kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa T...
13/11/2025

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limempitisha Dkt. Mwigulu Nchemba, kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mwigulu amepata kura za Ndio 369 kati ya kura 371 zilizopigwa huku za Hapana zikiwa 0, zilizoharibika zikiwa 2.

leo Bungeni Jijini Dodoma Novemba 13, 2025 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amemteu...
13/11/2025

leo Bungeni Jijini Dodoma Novemba 13, 2025 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amemteua Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Dk. Mwigulu ambaye ni Mbunge wa Iramba Magharibi Mkoa wa Singida anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Kassim Majaliwa ambaye ametumikia nafasi hiyo kuanzia mwaka 2015 hadi 2025.

Baada ya hapo wabunge watampigia kura kumthibitisha Waziri Mkuu aliyependekezwa kwa Azimio litakalopitishwa na Bunge.

Tangu baada ya ‘uchafuzi wenu’ umepoa sana arifee. Unachungulia TL k**a unaaga maiti vile. Hata kutoa pole kwa familia z...
12/11/2025

Tangu baada ya ‘uchafuzi wenu’ umepoa sana arifee. Unachungulia TL k**a unaaga maiti vile. Hata kutoa pole kwa familia zilizopoteza ndugu, jamaa na marafiki umeshindwa? Njoo tujadiliane mlivyolinda kura.

Pole pia kwako kwa kuk**atwa na kutunzwa mahabusu kwa vurugu za baada ya kushindwa huko Kigoma Mjini. Pole kwa wafuasi wako wote waliopewa kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha na kuchoma moto.

Vipi, umefanikiwa kumuona BABA LEVO akiapishwa kuwa mbunge wa Kigoma Mjini? Umeona anatamba kwamba ameangusha mbuyu? CHAWA grade one amekushinda? Amekustaafisha kiroho mbaya.

Tulikueleza ukasema muhuni hasusiwi. Tukakuuliza kivipiii? Ukakaza shingo na kusema piga kura, linda kura. Tulijua, huo ni udalali. Kiko wapi sasa? Hadi kesi mmepewa. Umetumika kuhalalisha uchafuzi haramu.

Anyways, hujachelewa sana braza. Kuna dili la maridhiano feki linazunguka. Bado halijapata expert. Unaweza kuchumpa na kuishi nalo. Biashara ya ubunge imekufa kifo cha mende. Pole sana BRO’

Address

Dodoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when sera media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share