30/07/2025
Ningeambiwa nitoe maoni yangu k**a ni sahihi kwa kundi la maprofesa kuwania ubunge, ningeanza kwa kuwapongeza na kuwaombea wafanikiwe katika harakati zao ikiwa tu wanaenda kutenda jambo lililo sahihi.
Zamani wakati tunakua, tukisikia mtu fulani ni "profesa" unapata picha ya mtu mwenye akili kubwa kwelikweli, sijui k**a walikuwa na ukubwa huo wa akili tuliokuwa tunafikiri au ni kwasababu tu tulikuwa hatuwaoni kwenye mazingira yetu.
Maprofesa wengi wamekuja kudhihirisha dhana ya ukubwa wa akili kuwa na utata baada ya kujiingiza kwenye siasa. Kwa ufupi wamekuja kwenye mazingira yetu na kujidhihirisha tofauti na mwanzo walipokuwa mbali nasi.
Swali lenye utata linabaki kuwa, je Maprofesa hawana uwezo mkubwa wa akili?
Binafsi bado naamini uwezo wao wa akili ni mkubwa sana ila tatizo wameingia eneo la siasa za Kiafrika ambako unatakiwa kuunga mkono hoja. Tabia ya kuunga mkono kila hoja ili tu ubakie kwenye madaraka ni matusi makubwa sana. Matusi haya hayaishii kwa wasomi walioko madarakani tu bali yanawaumiza hata wasiohusika.
Tumesikia tambo mbalimbali za kukejeli wasomi kutokuwa na msaada sahihi kwenye nchi kwasababu ya michango yao na mamuzi yao yenye utata.
Tatizo siyo kwamba wasomi kwa ujumla wao hawana uwezo, isipokuwa wameamua kuitikia ndiyo mzee ili waepuke kurudishwa majalalani, huko vyuo vikuu pasipo na maslahi.
Nihitimishe kwa kuwaomba wasomi wetu wote bila kujali maprofesa pekee, iokoeni CCM, iokoeni nchi. Simamieni maono yenu yenye maslahi mapana ya nchi, mkiona mnapingwa bila sababu za msingi, lindeni taaluma zenu kwa kurudi vyuoni mkafundishe.
Maoni ya sera media.