English Swahili

English Swahili DIFFERENT COLOURS, ONE LANGUAGE
Learn Swahili language here. JIFUNZE KIINGEREZA kwa njia rahisi

FRANCIS PAUL MAZIKU almaarufu CHELEA MAN ni mmoja wa wasanii wakali waliowahi kutokea Tanzania, wenye uwezo mkubwa wa ku...
22/04/2025

FRANCIS PAUL MAZIKU almaarufu CHELEA MAN ni mmoja wa wasanii wakali waliowahi kutokea Tanzania, wenye uwezo mkubwa wa kutunga na kuimba (bila kubana pua) nyimbo nzuri.
Pale Tip Top palikuwa na vipaji haswa!๐Ÿ”ฅ

"Kampani yetu wote makachaa/
Kuhusu mabitozi hakuna kabisa aa/
Ji-mixx na magansta,baby upate raha aa/
Ooh nachoka kabisa aa/"

"Naomba unipende k**a nilivyo msela aa/
(Usiniache ee)/
Hivi ndivyo mimi nilivyo msela aa/
(Usiniache ee)"
ยฉ Francis Josephat Lwambo (FUJO MASTA)
Aprili 22,2025
Dodoma,Tanzania.

JE WAJUA?Rais wa Upper Volta, Thomas Sankara alibadili jina la nchi hiyo kuwa Burkina Faso (Nchi Ya Watu Wanyoofu) mnamo...
07/04/2025

JE WAJUA?
Rais wa Upper Volta, Thomas Sankara alibadili jina la nchi hiyo kuwa Burkina Faso (Nchi Ya Watu Wanyoofu) mnamo mwaka 1984.

NYIEEE! HUKU KUMECHANGAMKA ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅKabla sijasema mengi,watoto wa buku bee chukueni chandimu mkacheze nje,wakulu tuna jamb...
01/04/2025

NYIEEE! HUKU KUMECHANGAMKA ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ
Kabla sijasema mengi,watoto wa buku bee chukueni chandimu mkacheze nje,wakulu tuna jambo letu.
La, k**a hamko tayari kupitwa na uhondo, KARIBUni mjumuike nasi wakulu USIKU HUU muonje vyenye tulifaidi.
Jamani eee,kumetokea mjadala wa moto ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅndani ya nafsi yangu hadi nikaamua mgogoro huu wa nafsi niulete kwenu.
Kati ya KARIBU ya Seif Shaaban akiwashirikisha Berry Black na Mr Blue,na USIKU HUU ya Mfalme Daudi,hapa simzungumzii Young Dee,namzungumzia Daz Mwalimu a.k.a Daz Baba akiwashirikisha Sajo na Mr Blue,unadhani IPI KALI???
Binafsi nilishajaribu kuziweka katika mzani ngoma hizi mbili nikashindwa kutoa hukumu!
Ukiisikiliza Karibu utaona ndiyo kali zaidi; baadaye ukiisikiliza Usiku Huu utaona ndiyo kali zaidi ๐Ÿค”
Halafu sasa,zote zina kauchawi f'lani hivi: ukianza kuisikiliza Usiku Huu utatamani kuirudia mara alfu lela u lela;vivyo hivyo ukianza kuisikiliza Karibu utatamani kuirudia mara alfu lela u lela!
Halafu sasa,zote "zimevamiwa" na mtoto wa mtaa,Nyani Zee Babylon enzi hizo akiwa tozi tozi kweli ๐Ÿ˜
Binafsi,nazipenda zote ila katika Usiku Huu napenda zaidi vasi ya Daz Baba pamoja na kiitikio:
Nataka niwe na wewe hapo sista duu/
Unapendeza peke yako usiku Huu/
Na mavazi yako yananiweka roho juu/
Kasi ya kucheza toka chini mpaka juu/.
Halafu katika Karibu, Tonya ni balaa, Blue ni balaa lakini humu Berry Black aliua sana.Huwa nafikiri blaza Seif hata angemuuzia Berry Black ngoma hii iwe yake (Berry Black ft Tonya & Blue) .Napenda zaidi kiitikio na vasi ya Berry Black :

Kamata mchuchu wako njoo turuke k**a vipi k**a hujui n'takufunza kucheza/
Ukiweza k**ata machupa ya 'wine' pombe kali punguza kumeza/
Nicheki nilivyo bling bling nilivyo ching ching n'shapagawa k**a kawa napoteza/
'Stage' k**a kawa nawameza/
Wachumba nawafunza kucheza/
Ukiweza/
Chombeza/
Mcheki Marco Chali alivyo-chill ndani ya 'club' yuko na ka-chixx kake katuliii...
Ka-chixx kana 'good shape' kana 'nice lips every song ' kana-swing hakachokiii/
We' niite Berry Black 'real' /
Uki-feel real ndani ya 'club' niki-clap soo kwa 'chart'-iii/
'Welcome move your body like a snake'/
'Slow shawty style in mini-skirt'/
Skiza 'rhymes, you and me galie'/

Oya wee,hawa jamaa walikuwa na unyamwezi mwingi sana na huo nd'o UKWELI๐Ÿ˜๐Ÿซก
Hapo nimejaribu kutafuta mistari ya Berry Black pekee ili niunde 'lyrics' lakini nina uhakika nitakuwa nimechapia sana๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
Haya hebu ngoja nijaribu kufuatishia kiitikio Tonya anapoimba :
Come njoo tu-dance/
Sweet boo/
Sweet bang with me kariiibu(kariiiiii)
Hii nadhani nimeiotea๐Ÿ˜๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
Oya,narudia,Bongo Fleva ya kizazi cha kina Tonya Blue Joseline Mb Dog nk. ilikuwa na unyamwezi mwingi sana (na si kwamba nawadharau wasanii wa sasa,hasha)! Kuna ngoma za Tonya hadi leo huwa naambulia kubahatisha tu maneno kadhaa๐Ÿ˜Pengine labda kwa sababu mimi ni Bush Star ila kwakweli hawa jamaa walikuwa matozi haswa,si uvaaji tu mpaka matumizi ya lughaโ™ฅ๏ธ
Sasa kwa mfano, kwenye 'bridge' ya ngoma ya Mb Dog iliyoitwa Tip Top,pale mwanadada Keisha unaweza kuniambia aliimba nini? Mimi nilikuwa najiimbia tu mradi liende:
Dantoromero,say Tip Top East African soldiers x2๐Ÿ˜‚
Au kile kiitikio cha Ishk Candeni ya Mb Dog:
Ishk Candeni iiiii/
Ishk sholahaaaiii/
Egiyuvamidooo ishkiiiii/
Mhnaaaaaa๐Ÿ˜‚
Bora liende mradi tu na-enjoy utamu wa melody.
MIMI NADHANI KUNA UMUHIMU WA WASANII HAWA (ALHAMDULILLAHI BADO WAPO) WAANDIKE 'LYRICS' ZA NYIMBO ZAO ILI VIZAZI VIJAVYO VIJE VIFAIDI UTAJIRI HUU WA MIZIZI YA BONGO FLEVA.

Turudi kwenye sokosoko letu la leo: kati ya KARIBU ya Seif Shaaban akiwashirikisha Sajo na Mr Blue na USIKU HUU ya Mfalme Daudi a.k.a Daz Mwalimu kura yako inadondokea wapi? Mimi niko juu ya fensi sijui pa kudondokea kwa kweli,wewe je?
Naitwa Fujo Masta.
April 1,2025,
Dodoma Tanzania.

NGUVU YA MITANDAO------_------------_-----------------ANAITWA   ALBERTMangwea? Hapana!Longomba(Awilo)? Hapana!Einstein? ...
31/03/2025

NGUVU YA MITANDAO
------_------------_-----------------
ANAITWA ALBERT
Mangwea? Hapana!
Longomba(Awilo)? Hapana!
Einstein? Hapana!

ANAITWA Albert Ofosu Nketia kutoka mkoani Ashanti,huko Ghana, Afrika Ya Magharibi.
Mwaka 2023 ,akiwa na umri wa miaka Saba(7), video yake ilisambaa duniani kote ikimwonesha akihama kutoka kulia hadi kucheka ndani ya sekunde chache!
Umaarufu wa kipande hicho cha video ulikifanya kitumike na watengeneza maudhui wengi wa video za vichekesho mwishoni mwa video zao ili kuzinogesha.
Video hii ilichukuliwa wakati Albert akililia viazi maana siku hiyo alikuwa hajapikiwa viazi.Akiwa katika kulia,bibi yake akawa anamwimbia wimbo wa kumtuliza lakini mjomba wake alikuwa akichukua video ya tukio hilo kwa simu ili baadaye aitume kwa baba wa Albert.
Baadaye alisahau kuituma hivyo video hiyo ikabaki tu kwenye simu.Alipoiuza simu hiyo kwa mtu mwingine,kuna mtu alijirushia,akaitupia mtandaoni "bhamtu bha mtandaoni bhakaishi nayo". Kilichobaki ni historia!
Hivi sasa Albert ana umri wa miaka kenda (9) na anasumbuliwa na ugonjwa wa tetekuwanga.Watu wa mtandaoni "wenye mapenzi mema" wamechangishana na kupata millioni kadhaa na wanaendelea kuchangia kumsaidia dogo.
NGUVU YA MTANDAO!
Naitwa Fujo Masta
Machi 31,2025
Dodoma,Tanzania.

BREAKING NEWS: LEJENDARI wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania, Michael Francis Mwakatundu almaarufu Mike Tee amzawa...
12/03/2025

BREAKING NEWS:
LEJENDARI wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania, Michael Francis Mwakatundu almaarufu Mike Tee amzawadia msanii mwenzake Francis Josephat Lwambo almaarufu Fujo Masta zawadi mahsusi ya wimbo wake maridhawa "Nampenda Nani" aliowahi kumshirikisha msanii Juma Kassim Kiroboto almaarufu Juma Nature au Sir Nature katika kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Fujo Masta.
Mike Tee ni moja kati ya miamba waliopambana kuifanya aina ya muziki wa kizazi kipya (Bongo Fleva) ukubalike na kusikilizika katika jamii ya Watanzania na hatimaye duniani kote hivyo kupelekea muziki huo kuwa chanzo cha ajira kwa vijana wengi wa Kitanzania.
Mike aliwahi kutamba na vibao vya moto k**a vile "Sintobadilika" aliomshirikisha Abukar Shaaban Katwila(Q-Chilla),"Nyalu Land" aliomshirikisha Judith Wambura Mbibo(Lady Jay Dee),"Kama" na "Je Utanipenda" aliomshirikisha Ahmed Mohamed Kakoyi(Mad Ice).

Ninafanya ' Graphic designing '. Huduma inakufikia popote ulipo duniani.Simu: ๐Ÿ“ž+255-710-509-374
22/02/2025

Ninafanya ' Graphic designing '. Huduma inakufikia popote ulipo duniani.
Simu: ๐Ÿ“ž+255-710-509-374

Designer: ๐Ÿ“ž +255-710-509-374
22/02/2025

Designer: ๐Ÿ“ž +255-710-509-374

Address

Dodoma

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when English Swahili posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share