Rubondofm

Rubondofm District radio station
provide News content, sports, music and current affairs.

18/12/2025

Mkuu wa mkoa wa geita Martine Shigela, ameipongeza kampuni ya uchimbaji dhahabu Mkoa wa Geita GGML kwa ufanisi wake katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Geita.Mheshimiwa shigela ametoa pongezi hizo kwenye Kikao cha k**ati ya ushauri ya Mkoa , ambapo pamoja na mambo mengine amebainisha kuwa katika miradi 35 iliyokuwa na changamoto 32 imekamilika kwa ufanisi asilimia 100

18/12/2025
Habari picha na
18/12/2025

Habari picha na

18/12/2025

Umoja wa Vijana wa Nyarugusu Mkoni Geita ambao upo kwa ajili ya kusaidiana umekutana siku ya leo kwa ajili ya kujadili mambo mbalimbali.

Umoja wa UVINYA umemekutana na unaongozwa na Mwenyekiti wake Michael Kajanja.

Hata hivyo Naibu Waziri wa TAMISEMI anayeshughulikia afya Dk. Jafari Seif atakutana na Vijana hao baadaye.

Na

17/12/2025

Mwenyekiti wa kikundi Cha Umoja wa Vijana Nyarugusu UVINYA Michael Kajanja ameeleza kufurahishwa na namna kikundi Cha wenzao Cha Nepa kilichopo Nyarugusu kinavyojitoa kusaidia jamii iliyo na uhitaji.

Kajanja ameeleza hayo wakati akiwa amealikwa na kikundi Cha Nepa katika kikao chake Cha Mwaka pamoja na kushiriki kutoa misaada katika kituo Cha Afya Nyarugusu.

Na

17/12/2025

Kituo Cha afya Cha Nyarugusu kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mkoani Geita kimekishukuru kikundi Cha Nyarugusu Empathetic Partinners (Nepa) kwa kutoa misaada mbalimbali pamoja na uchangiaji wa damu.

Kituo hicho Cha afya kimetoa shukrani hizo kwa kikundi Cha Nepa kupitia kwa Darling Jonja Chiragwile ambaye ni kaimu Mganga Mfawidhi WA kituo baada ya kupokea ujio wa kikundi hicho kituoni hapo.

Mwenyekiti wa kikundi Cha Nepa Morris Julius Morris Sundo amesema kikundi hicho ni Cha kusaidiana wakati wa Majanga na misiba na na kimeamua kuigusa jamii kwa kusaidia wahitaji.

Afisa Mtendaji wa kata ya Nyarugusu Lusekelo Mwaikenda ameeleza kuwa kituo hicho kinahudumia kata tano zikiwemo Bukoli, Nyalwanzaja, Nyaruyeye, Lwamgasa pamoja na Nyarugusu hivyo kina mahitaji mengi.

Afisa Habari wa kikundi hicho Daud Makani amesema kikundi hicho kitaendelea kuigusa jamii katika nyanja mbalimbali.
Na

15/12/2025

Madereva wa mabasi wametakiwa kuzingatia mila na desturi za Kiafrika wanapoweka nyimbo na video ndani ya magari ya abiria, ili kuepuka ukiukwaji wa maadili ya Kitanzania.

Wito huo umetolewa na Mnadhimu wa Jeshi la Polisi, SACP Butusyo Akim Mwambelo, wakati alipokuwa akifanya ukaguzi na kutoa elimu kwa madereva pamoja na abiria katika Kituo Kikuu cha Mabasi, Manispaa ya Geita.

Katika hatua nyingine, SACP Mwambelo amesema kuwa ajali nyingi zinazotokea kwa sasa husababishwa na madereva wa pikipiki maarufu k**a bodaboda, kutokana na tabia ya kuzidisha abiria kinyume na sheria za usalama barabarani.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Geita, SP Lazaro Masembo, amesema jeshi la polisi limeendelea kutoa elimu kwa watumiaji wa barabara ili kupunguza ajali zinazojitokeza mara kwa mara.

Aidha, mmoja wa wasafiri katika kituo hicho cha mabasi amepongeza jitihada zinazofanywa na Jeshi la Polisi katika kutoa elimu kwa umma, akisema kuwa hatua hiyo inasaidia wananchi kutambua haki zao na wajibu wao wanapotumia vyombo vya usafiri.

15/12/2025

b

Afisa mnadhim Kikosi Cha Usalama Barabarani Makao Makuu  Jeshi la Polisi SACP Butusyo Akim Mwambelo ametoa wito kwa made...
15/12/2025

Afisa mnadhim Kikosi Cha Usalama Barabarani Makao Makuu Jeshi la Polisi SACP Butusyo Akim Mwambelo ametoa wito kwa madereva wa Magari ya abiri kuzingatia Mila na desturi za kiafrika wakati wa kuweka nyimbo na video kwaajili ya abiri na kuepuka ukiukwaji wa maadili.

Ametoa wito huo Mkoani Geita akiwa kwenye mwendelezo wa ziara ya ukaguzi wa Magari ya abiria ili kulunguz ajali zinazoweza kutolea kuelekea kipindi Cha mwisho na mwanzo wa mwaka.

Pamoja na hayo amewataka Madereva, Kondakta, Wapigadebe na abiria kuzingatia usalama Sheria za Usalama barabarani ili kuepuka ajali.

13/12/2025

Ziara ya Mbunge wa Jimbo Jipya la Katoro Yaweka Msingi wa Utekelezaji wa Ahadi za Barabara na Afya

Baada ya kugawanywa kwa Jimbo la Busanda na kuundwa kwa majimbo mawili ya Katoro na Busanda, Mbunge wa Jimbo jipya la Katoro, Mhandisi Kija Limbu Ntemi, ameanza rasmi utekelezaji wa ahadi alizotoa kwa wananchi wakati wa kampeni, kwa kuweka kipaumbele katika uboreshaji wa miundombinu ya barabara na huduma za afya, maeneo yaliyokuwa changamoto kwa muda mrefu katika wilaya hiyo.

Alhamisi, Mbunge Ntemi alifanya ziara ya kukagua ujenzi wa mitaro ya kupitisha maji katika maeneo mbalimbali ya Katoro, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kulinda barabara dhidi ya athari za mvua na maporomoko. Mradi huo unaotekelezwa na kampuni ya Jonta Investment Limited ya Mkoa wa Shinyanga, unafadhiliwa na Benki ya Dunia kwa zaidi ya shilingi bilioni 1.299 na unahusisha ujenzi wa mitaro yenye urefu wa kilomita 5.25.

Akiwa katika ziara hiyo, Mbunge wa Katoro aliipongeza Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia katika kutekeleza miradi ya maendeleo, akieleza kuwa ujenzi wa mitaro hiyo utaongeza uimara wa barabara na kuboresha usafiri kwa wananchi. Aidha, aliwataka wakandarasi kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi na kuhakikisha ubora unazingatiwa ili kazi ikamilike kwa wakati uliopangwa.

Wahandisi kutoka TARURA Wilaya ya Geita walieleza kuwa utekelezaji wa mradi unaendelea vizuri, huku wakisisitiza umuhimu wa mkandarasi kuzingatia maelekezo yote ya kitaalamu ili kupata matokeo bora yanayokusudiwa. Wakazi wa Katoro nao walipongeza hatua hiyo, wakisema ni mwanzo wa suluhisho la changamoto ya barabara iliyokuwa ikiwasumbua kwa muda mrefu, hasa wakati wa mvua.

Siku iliyofuata, Ijumaa, Mbunge Mhandisi Kija Limbu Ntemi aliendelea na ziara yake kwa kutembelea Hospitali ya Wilaya ya Katoro, ambapo alipokea changamoto mbalimbali zinazohusu utoaji wa huduma za afya. Miongoni mwa changamoto hizo ni ukosefu wa njia ya watembea kwa miguu (walkway) ndani ya hospitali, hali inayosababisha usumbufu kwa wagonjwa, watumishi na wananchi wanaofika kupata huduma. Mbunge aliahidi kuwasilisha suala hilo kwa viongozi husika ili kupatikane ufumbuzi wa kudumu.

13/12/2025

Mbunge wa Jimbo la Katoro, Mhandisi Kija Limbu Ntemi, amepokea changamoto ya ukosefu wa njia ya watembea kwa miguu (walkway) katika Hospitali ya Katoro na kuahidi kuifuatilia kwa kushirikiana na viongozi husika ili kupata ufumbuzi wa kudumu.

‎Akizungumza wakati wa ziara yake hospitalini hapo, Mhandisi Ntemi amesema amelipokea ombi hilo na ataliwasilisha kwa viongozi wanaohusika ili lipatiwe majibu na hatua stahiki zichukuliwe kwa manufaa ya wagonjwa, watumishi na wananchi wanaotumia huduma za hospitali hiyo.

‎Pamoja na changamoto ya walkway, Mwenyekiti wa Hospitali ya Katoro amemuomba mbunge huyo kusaidia upatikanaji wa jokofu katika chumba cha kuhifadhia miili ya marehemu (maiti), akieleza kuwa ni hitaji muhimu kwa kuboresha huduma za afya na heshima kwa marehemu.

‎Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Katoro amewataka watumishi wa hospitali hiyo kufanya kazi kwa weledi, kutoa huduma bora kwa wagonjwa na kuacha matumizi ya lugha zenye ukakasi, akisisitiza umuhimu wa maadili na utu katika utoaji wa huduma za afya.

‎Aidha, Diwani huyo amempongeza Mbunge wa Katoro kwa kuanza kazi mapema tangu kuanzishwa kwa jimbo hilo jipya, akisema juhudi hizo zitasaidia Jimbo la Katoro kufikia malengo yake ya maendeleo kwa haraka na kwa ufanisi.

12/12/2025

Mbunge wa Jimbo la Katoro Mhandisi Kija Limbu Ntemi amefanya ziara katika Hospitali ya Wilaya Katoro na kugawa zawadi mbalimbali kwa wagonjwa na watumishi wa Hospitali hiyo.

Wakizungumza Baadhi ya Wananchi waliofika hospitalini hapo kupata huduma wakiwemo wakinamama waliojifungua, wamemshukuru Mbunge kwa Msaada aliotoa na kupongeza huduma nzuri waliopata kutoka Kwa wataalam wa Afya.

Baadhi ya wazazi waliofika kwaajili ya kupata huduma ya matibabu ya watoto wao wanaosumbuliwa na changamoto ya utapyamlo wamempongeza mbunge kwa kuwajali pamoja na huduma za madaktari waliojitahidi kuhakikisha watoto wao afya zao Zinahimarika.

Address

BOMANI
Geita
30101

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Rubondofm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Rubondofm:

Share