02/10/2025
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa –TAKUKURU Mkoa Geita na Viongozi wa dini kwa pamoja wameazimia kuzuia wagombea wa nafasi ya Urais,Ubunge na udiwani kutumia mimbari k**a shemu ya kufanyia kampeni za kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu oktoba 29, 2025.Azimio hilo pamoja na mengine limepitishwa kwenye mkutano maalumu ulioandaliwa na takukuru kwa lengo ya kujadili nafasi za viongozi wa dini katika mapambano dhidi rushwa kuelekea uchaguzi mkuu wa urais ubunge na udiwani Naibu mkuu wa takukuru Mkoa Geita, Alex Mpemba amesema wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu watanzania wanapaswa kuwa na mshik**ano na kuzuia rushwa.