Rubondofm

Rubondofm District radio station
provide News content, sports, music and current affairs.

Wadau wa elimu waliosoma katika Shule ya Msingi Monuna, iliyopo Kata ya Nyambureti, Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, wam...
13/01/2026

Wadau wa elimu waliosoma katika Shule ya Msingi Monuna, iliyopo Kata ya Nyambureti, Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, wametoa msaada wa madaftari, kalamu na mabegi kwa wanafunzi wanaotarajiwa kuanza masomo ya sekondari mwaka huu.

Msaada huo umetolewa ikiwa ni sehemu ya jitihada za wadau hao kuhakikisha wanafunzi wanapata haki yao ya msingi ya elimu katika mazingira bora na yenye usawa, bila kujali changamoto za kiuchumi zinazowakabili.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Mwenyekiti wa umoja huo, Joram Agary, alisema msaada huo unalenga kuwapa hamasa wanafunzi hao na kuwasaidia kuanza safari ya elimu ya sekondari wakiwa na vifaa muhimu vya masomo.

“Msaada huu utawasaidia wanafunzi wetu kupata haki ya elimu k**a wenzao na kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa usawa,” alisema Agary.

Alifafanua kuwa wazo la kutoa msaada huo lilianzishwa kupitia kundi la WhatsApp la wadau hao, ambapo wanachama walikubaliana kuchangia kwa pamoja na hatimaye kufanikisha zoezi hilo kwa vitendo.

Katika zoezi hilo, jumla ya wanafunzi 14 wamenufaika, ambapo kila mwanafunzi amepatiwa madaftari tisa kwa ajili ya masomo yao ya sekondari, pamoja na kalamu na mabegi.

Wageni na wanachama wengine waliohudhuria tukio hilo ni pamoja na Josinta Garigo, Sayi Marugu, Maritha Mathayo, Mwajuma Mwita, Juma Kitenge na wengineo.

Baadhi ya walimu wa Shule ya Msingi Monuna wakiongozwa na Mwalimu Mkuu Lukas Kosianga, walitoa pongezi kwa wadau hao kwa juhudi walizozionesha, wakisema ni mfano bora wa ushiriki wa jamii katika maendeleo ya elimu.

Walimu wengine waliokuwepo ni pamoja na Paulo Chacha, Baraka Panyako, Theopista Ngoyani na Joseph Mwashi, ambao kwa pamoja waliwataka wadau wengine wa elimu kuiga mfano huo na kuungana katika kutekeleza ajenda ya elimu kwa vitendo kijijini hapo.

Wadau hao wamesema wataendelea kushirikiana na jamii na uongozi wa shule ili kuhakikisha wanafunzi wanapata msaada unaohitajika kwa maendeleo endelevu ya elimu katika eneo hilo.

13/01/2026

Mwanamke aitwaye Magreth petro, mkazi wa kijiji cha Kayenze, kata ya Nyamwilolelwa wilayani anaishi katika hofu kubwa baada ya mapacha wake watatu kukumbwa na upungufu mkubwa wa lishe.

Magreth petro anasema mapacha hao wote wakiwa ni wavulana walizaliwa miezi mitano iliyopita wakiwa na afya njema lakini hali imebadilika kwa sasa baada ya familia hiyo kushindwa kumudu gharama za kuwatunza.

Kutokana na hali ngumu ya maisha watoto hao wameanza kudhoofika kiafya jambo linalozua hofu kubwa kwa wazazi wao.

Akizungumza kwa uchungu, mama huyo amesema changamoto za kiuchumi zimeifanya familia ishindwe kupata chakula cha kutosha, hali inayohatarisha afya na ukuaji wa watoto hao wachanga.

Kwa upande wake mme wa Magreth Benjamin Chai ameungana na mke wake kuomba msaada kutoka kwa jamii, wasamaria wema pamoja na serikali.

Amesema kazi yake ya vibarua humuingizia sh 5,000 kwa siku, kiasi ambacho hakitoshelezi mahitaji ya familia, hasa ikizingatiwa mahitaji ya lishe ya watoto watatu kwa wakati mmoja.

Habari Na .yohana.jr

12/01/2026

Diwani wa Kata ya Kalangalala, Reuben Sagayika ametoa msaada wa vifaa mbalimbali vya shule kwa wanafunzi zaidi ya 600 wanaotoka katika familia zisizo na uwezo kutoka katika kata hiyo.

Akizungumza katika hafla ya utoaji wa vifaa iliyofanyika January 12, 2025 katika ofisi ya kata hiyo, Sagayika amewaomba wazazi kuhakikisha watoto wanaenda shule kupata haki yao ya msingi hata bila ya kuwa na sare za shule.

Aidha Sagayika amesema zoezi la ugawaji wa vifaa vya shule litakuwa ni endelevu katika kata hiyo.

Kaimu Afisa Elimu Kata ya Kalangalala, Regina Cosmas amesema msaada wa vifaa vilivyotolewa na diwani utasaidia watoto kuwa na mahudhurio mazuri shuleni.

Nao baadhi ya wazazi waliopokea vifaa hivyo Consolata Rwanda na Yohana Benjamin wamempongeza diwani kwa utaratibu huo na kumuomba aendelee kufanya hivyo.

Vifaa vilivyotolewa kwa wanafunzi hao ni pamoja na madaftari, kalamu na penseli hii ikijumuisha wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.

Habari Na

12/01/2026

Takribani wanafunzi 50 wa sekondari na Msingi wamepatiwa mahitaji ya vifaa vya shule na Kanisa la Naioth International church lililopo Maweni Wilayani Chato ikiwa shabaha yake ni kuwawezesha kupata vifaa vya kujifunzia wakati wa masomo Yao.

Mchungaji wa kanisa hilo Ideca Ehembwe amevitaja vifaa walivyokabidhi kwa wanafunzi hao kuwa ni Madaftari, nguo za shule, kalamu pamoja na viatu.

Baadhi ya wanafunzi waliopokea vifaa hivyo wamesema vifaa hivyo wataenda kuvitumia kujifunzia wakati wa masomo.

Katibu wa kanisa hilo Musa Samwel amesema ugawaji wa vifaa hivyo unalenga kuwawezesha wanafunzi kupata elimu huku Mmoja wa wazazi wa wanafunzi Bahati mtachereza akishukuru Mtoto wake kupata vifaa vya shule.

Na

HALMASHAURI ya wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita imeweka wazi kuwa imeandaa miundombinu inayotosheleza kupokea wanafunz...
11/01/2026

HALMASHAURI ya wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita imeweka wazi kuwa imeandaa miundombinu inayotosheleza kupokea wanafunzi 3,056 wa kidato cha kwanza mwaka 2026.

Ofisa Elimu Sekondari wilayani Nyang’hwale, Malemu Tito ametoa taarifa hiyo katika ziara ya mkuu wa wilaya kukagua miundombinu ya elimu kuelekea mwaka mpya wa masomo.

Malemu amesema mpaka sasa tathimini inaonyesha kuwa halmashauri hiyo haina upungufu wa vyumba vya madarasa kwenye shule zote za sekondari hivo kila mwanafunzi atapokelewa.

Amesema ukaguzi uliofanyika umebaini bado kuna upungufu mdogo wa meza pamoja na viti vya wanafunzi ambapo juhudi zinaendelea kuziba pengo kabla ya shule kufunguliwa.

“Matarajio ni kwamba kufikia siku ya kufungua shule upungufu uliopo utakuwa umefanyiwa kazi kwa maana kwamba tunatarajia kutengeneza viti na meza”, amesema.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Nyang’hwale, Ezekiel Ntiriyo amesema maagizo yameshatolewa kwa wakuu wa shule kusimamia ukarabati wa viti na meza vilivyoharibika.

“Wakuu wa shule huwa wanatengewa bajeti ya ukarabati na matengenezo ya miundombinu watazitumia hizo pesa kutengeneza meza, viti na madawati yaweze kurejea kwenye matumizi”.

Amesema pia maagizo yametolewa kwa k**ati za maendeleo ngazi ya kata kushirikisha wadau wa maendeleo kufanya tathimini ya viti, meza na madawati na kuangalia namna ya kutatua tatizo.

Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale, Grace Kingalame amesema tayari amefanya ukaguzi kwenye shule zote 19 za sekondari lengo kuu likiwa ni kujiridhisha utayari wa wilaya kupokea watoto.

Amesema ili kukabiliana na upungufu meza na viti halmashauri imejipanga kutenga kiasi kidogo cha pesa kila mwezi kupitia mapato ya ndani kwa ajili ya kufanya matengenezo na ukarabati.

“Maelekezo ya serikali ni kuhakikisha kila mtoto anakwenda darasani, kuanzia shule ya awali, darasa la kwanza na kidato cha kwanza”, amesema Kingalame.

Habari Na .yohana.jr

MKUU wa wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita, Grace Kingalame ameagiza maofisa elimu kata kusimamia ubora wa madarasa ya a...
11/01/2026

MKUU wa wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita, Grace Kingalame ameagiza maofisa elimu kata kusimamia ubora wa madarasa ya awali ili kujenga mazingira rafiki kwa watoto kujifunza.

Kingalame ametoa maagizo hayo wakati wa ziara maalum ya kukagua miundombinu ya elimu kuelekea kuanza kwa mwaka mpya wa masomo 2026.

Amesema shule zinapaswa kuzingatia muongozo wa sera ya elimu unaoelekeza madarasa yote ya wanafunzi wa awali kuwa na miundombinu bora inayoaksi mafundisho kulingana na umri wao.

“Mahitaji ya madarasa ya awali yapo na yameainishwa, kwa mjibu wa Wizara ya Tamisemi (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa), lazima tuandae madarasa kwa kufuata utaratibu huo.

Kingalame amemwagiza mkurugenzi wa halmashauri hiyo kusimamia ujenzi wa miundombinu ya watoto kujifunza ikiwemo michoro na alama sahihi kwa watoto kujifunza kwa urahisi.

Amesema uwepo wa maiundombinu rafiki kwa watoto siyo tu itarahisisha zoezi la ufundishaji kwa walimu bali pia itawajengea molari watoto kuanza kuipenda elimu pasipo kuwa na adha yeyote.

Ameongeza pia shule zote zinapaswa kuandaa vitendea kazi kwa watoto kujifunza stadi za kazi sambamba na kupata chakula shuleni kwa ilivyoelekezwa na serikali.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Nyang’hwale, Ezekiel Ntiriyo amesema ili kukidhi mahitaji ya watoto kujifunza kila Mwalimu mkuu atapaswa kuainisha mahitaji yake.

Amesema ofisa ya mkurugenzi ipo tayari kufanyia kazi mapungufu yote yatakayowasilishwa na walimu wakuu ili kufanikisha azma ya kuweka miundombinu rafiki kwa watoto kujifunza vizuri.

Takwimu za Ofisa Elimu Mkoa wa Geita, Anthony Mtweve zinaeleza hadi kufikia Januari 2025, Nyang’hwale imefanikiwa kuandikisha wanafunzi wa awali 5,479 sawa na asilimia 74 ya lengo la 7,372.

Amesema kwa darasa la kwanza, halmashauri hiyo imeandikisha 6,585 sawa na asilimia 88 ya lengo la wanafunzi 7,450 na hivo Nyang’hwale ndio kinara ya uandikishaji mkoa wa Geita.

Habari Na .yohana.jr

HALMASHAURI ya Wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita imeanzisha mashamba darasa katika shule zote za msingi na sekondari il...
11/01/2026

HALMASHAURI ya Wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita imeanzisha mashamba darasa katika shule zote za msingi na sekondari ili kuzalisha chakula cha uhakika maalum kwa ajili ya wanafunzi.

Aidha mashamba darasa hayo yameanzishwa ili kutoa fursa kwa wakazi wa Nyang’hwale kujifunza kwa vitendo hatua kwa hatua juu ya kilimo cha kisasa na kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula.

Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale, Grace Kingalame ametoa taarifa hiyo wakati wa ziara maalum ya kukagua miundombinu ya elimu kuelekea kuanza kwa mwaka mpya wa masomo 2026.

Kingalame amesema ili kufanikisha mpango huo halmashauri ilinunua mbegu na kutoa kilo 16 za mahindi na kuelekeza kila shule ilime angalau hekari 2 na zisimamiwe na maofisa kilimo wa kata.

“Lengo letu ni kuwapunguzia adha ya michango wazazi, hii biashara ya mzazi kuchanga gunia la mahindi au mchele, tujikite kwenye mambo mengine ya maendeleo”, amesema Kingalame.

Amesema mpango huo unatarajiwa kuongeza matokeo chanya katika kiwango cha ufaulu kwani wanafunzi watapata chakula shuleni badala ya kupata mapumunziko Kwenda kula nyumbani.

“Kipaumbele chetu ni elimu, kwani elimu ndiyo jambo la msingi kwa jamii yeyote, jamii iliyoelimika inaweza kufanya mambo yake bila kushurutishwa na mtu yeyote”, amesema.

“Yeyote atakayekwenda kinyume, akatumia mahindi haya vibaya, tukitoa viazi lishe akavichukua akaenda kutumia kwa mambo yake atakuwa ametuchokoza”, amesema.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Nyang’hwale, Ezekiel Ntiriyo amesema hatua hiyo ni mpango wa kuinua ufaulu wa wanafunzi kupitia upatikanaji wa chakula kwa shule 74.

Amesema mbali na kilimo cha mahindi pia program hiyo imeambatana na ugawaji wa viazi lishe kuwezesha wanafunzi kupata chakula cha kutosha na chenye kuimarisha afya zao.

Ofisa Elimu Kata ya Shabaka, Laurent Gilindui amesema programu inaendeshwa kwa kushirikisha walimu na wanafunzi na wamejizatiti kusimamia vizuri kuanzia kulima, kuvuna hadi kuhifadhi.

Habari Na .yohana.jr

HALMASHAURI ya Wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita imeunda kikosi kazi kwa ajili ya kufuatilia, kusimamia na kuhamasisha ...
11/01/2026

HALMASHAURI ya Wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita imeunda kikosi kazi kwa ajili ya kufuatilia, kusimamia na kuhamasisha marejesho ya mikopo kutoka kwa makundi maalumu.

Hatua hiyo inalenga kukabiliana na mwitikio hafifu wa urejeshaji wa mikopo ambapo kati ya sh milioni 150 zilizokopeshwa mwaka 2025 hadi sasa sh milioni 102 hazijarejeshwa kwa wakati.

Ofisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya wilaya ya Nyang’hwale Estelina Colman ametoa taarifa hiyo katika hafla ya awamu ya pili ya utoaji wa mikopo kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

Amesema k**ati maalum iliyoundwa inafanya kazi kwa siku mbili za juma kwa kupita na kutembelea vikundi vyote na kisha kufanya tathimini ya maendeleo ya miradi ya vikundi hivo.

“Kila siku ya Jumanne na Alhamis timu inatoka kwa ajili ya Kwenda kufuatilia marejesho, hii timu imesaidia zaidi kwa kushirikiana na maofisa maendeleo ngazi ya kata.

Estelina ameweka bayana kuwa Kundi ambalo limeonekana kuwa na mwitikio hafifu katika urejeshaji ni vijana ambao wengi wao wameonekana kutofautiana katika uendeshaji wa miradi.

Awalia Mratibu wa Mikopo Halmashauri ya wilaya ya hiyo, Yahaya Balasinda amesema kwa awamu pili ya utoaji mikopo ya mkwa huu wa fedha vikundi 40 viliwasilisha maombi ya mkopo.

Amesema kati yake, vikundi 37 viliidhinishwa na kukidhi vigezo na kisha baada ya tathimini ya kina vikundi 34 pekee ndiyo vimeweza kukidhi vigezo vya kukopeshwa jumla ya sh milioni 300.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya Nyang’hwale, Husna Toni amesisistiza kuwa mikopo hiyo inaendelea kutolewa kwa kuzingatia tathimini ya kina ili kuepuka kunufaisha vikundi hewa.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo, Adamu Mtore amewataka viongozi wa halmashauri kufanya utafiti wa kuinua uzalishaji na masoko ya uhakika kwa wajasiriamali hao.

Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale, Grace Kingalame aliagiza idara ya maendeleo ya jamii kuvijengea uwezo vikundi vilivyokosa vigezo ili viweze kunufaika na fursa hiyo ya kujikwamua kiuchumi.

Habari Na .yohana.jr

11/01/2026
10/01/2026

Tume ya Rais iliyoundwa kwa ajili ya kuchunguza matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi wa oktoba Mwaka 2025 imewasikiliza makundi mbalimbali Mkoani Geita yaliyopoteza ndugu, kujeruhiwa pamoja na kuharibiwa biashara.

Mjumbe wa tume hiyo Balozi Ombeni Sefue akizungumza wakati wa zoezi la kuwasikiliza wananchi wa Mkoa wa Geita kuhusu vurugu hizo amesema tume inaendelea kuwasikiliza wananchi huku akisema waliojitokeza ni makundi ya waliopoteza ndugu zao, kujeruhiwa pamoja na kuharibiwa biashara zao.

Sefue ameongeza kwamba tume inapokea maoni ya wananchi kupata mwafaka wa nini kifanyike kwa taifa juu ya vurugu zilizotokea.

08/01/2026

I got over 100 reactions on one of my posts last week! Thanks everyone for your support! 🎉

08/01/2026

Tume ya Taifa ya shirika la elimu, Sayansi na utamaduni UNESCO chini ya ufadhili wa tume ya Taifa ya UNESCO ya nchini Korea imezindua programu ya mradi wa elimu utakaoibua fursa na kuwawezesha vijana kujiajiri na kujitegemea.

Katibu Mtendaji wa tume hiyo Prof. Hamisi Masanja Malebo wakati akizungumza katika uzinduzi rasmi wa mradi huo uliofanyika Ofisi za Kata ya Nzera Halmashauri ya Wilaya ya Geita, ameueleza mradi huo kuwa umebeba matumani kwa vijana kuelekea ajenda ya dunia ya Maendeleo Endelevu ifikapo mwaka 2030.

Prof. Malebo amesema kwamba programu hiyo ya elimu inawalenga Vijana hasa wasichana na makundi maalumu ya kijamii huku ikibeba matarajio makubwa kwa siku za usoni kwa kutengeneza mabilionea, na viongozi wenye uwezo.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri, Jonas Kilave amewataka vijana hao kuonyesha nidhamu ya kujifunza na kuufanyia kazi ujuzi watakaoupata.

Wanufaika wa mradi huo Hapoyness Pastory na Mikael Falima wanasema programu hiyo inaenda kuwasaidia hasa kwa vijana waliopo mtaani bila kazi za kufanya.

Vijana 1,050 kutoka kata 10 wanatarajia kunufaika na programu hiyo itakayoendeshwa kwa
awamu 5.

Na

Address

BOMANI
Geita
30101

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Rubondofm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Rubondofm:

Share