Rubondofm

Rubondofm District radio station
provide News content, sports, music and current affairs.

07/06/2026

Mkurugenzi na mmiliki wa Kadama English Medium Primary School Leticia Pastory ametunukiwa tuzo ya Mmiliki Bora wa Shule wa K**e Mkoa wa Geita 2026 (CEO Bora) ikiwa ni kutambua mchango wake katika kuendeleza sekta ya elimu na maendeleo ya jamii.

Tuzo hiyo ilikabidhiwa Juni 6, 2026 na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa na Mbunge Mary Chatanda katika Tamasha la Mwanamke wa Dhahabu (Geita Women Festival 2026) lililofanyika katika Ukumbi wa Golden Social Hall mjini Geita.

Tuzo hizo zimeandaliwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Geita Women and Youth Foundation chini ya Mkurugenzi wake Cecylia Miraji, kwa lengo la kutambua wanawake wenye mchango mkubwa na chanya katika jamii kupitia shughuli mbalimbali za maendeleo.

Habari Na .yohana.jr

07/06/2026

Chama kikuu Cha Ushirika Geita GCU LTD kinavyoendelea kutekeleza sera ya Taifa ya Kilimo.

Fuatilia taarifa hii kwa undani zaidi

05/06/2026

Chama Kikuu Cha Ushirika Geita (GCU LTD) kimefika katika viunga vya Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza Kwa ajili ya kununua zao la Mpunga kwa wakulima

Hatua hii ni sehemu ya jitihada za kuhakikisha malighafi ya kutosha yanapatikana ili kiwanda Cha kuchakata mpunga Cha GCU LTD kilichopo Kasamwa Manispaa ya Geita kinafanya kazi muda wote n kuongeza pato la wakulima na vyama vya Msingi vya Ushirika AMCOS.

Afisa shughuli wa chama Kikuu Cha Ushirika Geita (GCU LTD) Charles Nyasi, akiwa na timu yake katika Kijiji Cha Kalangalala Wilayani Sengerema ameeleza kuwa amefanya ziara ya kutembelea Katibu wa AMCOS wa eneo hilo ili kuona utendaji kazi wake baada ya kuaminiwa na chama ili akusanye mpunga kutoka kwa wakulima.

Bwana Nyasi amesema ameridhishwa na utendaji kazi wa Katibu huyo kwani alipewa shilingi milioni mbili kununua mpunga magunia 20 na mpaka kufikia Sasa tayari amekusanya mpunga magunia 19.

Kwa upande wake Katibu wa AMCOS Kalangalala Wilayani Sengerema bwana Alphonse Mapinduzi John ameipongeza chama kikuu Cha Ushirika Geita GCU LTD kwa kumuamini kufanya kazi hiyo na kuahidi kuwa ataendelea kutekeleza wajibu wake kwa weledi Mkubwa ili kufikia lengo lililokusudiwa.

SHULE ya Royal Family English Medium Primary School imeendelea kung'ara katika sekta ya elimu baada ya kuongoza katika m...
05/06/2026

SHULE ya Royal Family English Medium Primary School imeendelea kung'ara katika sekta ya elimu baada ya kuongoza katika matokeo ya Mtihani wa Mock wa Kanda ya Ziwa, huku wanafunzi wote wa k**e walioshiriki mtihani huo wakifanikiwa kupata wastani wa alama A.

Katika matokeo hayo shule hiyo imeibuka mshindi wa kwanza katika Manispaa ya Geita kati ya shule 91 zilizoshiriki mtihani huo.

Matokeo ya mtihank huo yanaonyesh umla ya wanafunzi 77 wa darasa la saba walifanya mtihani huo, ambapo wanafunzi 76 walipata wastani wa A na mwanafunzi mmoja pekee akipata wastani wa B.

Akizungumza baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo Mkurugenzi wa shule hiyo Mhandisi Lazaro Philipo amesema mafanikio hayo yametokana na ushirikiano mkubwa kati ya walimu, wazazi na wanafunzi pamoja na nidhamu ya hali ya juu katika kufundisha na kujifunza.

Mhandisi Lazaro meishukuru jamii kwa kuendelea kuiamini Royal Family English Medium Primary School na kuahidi kuongeza juhudi zaidi ili kuifanya shule hiyo kuwa kitovu cha elimu bora na maadili mema nchini.

Habari Na .yohana.jr

SERIKALI imekamilisha kwa asilimia 98 mradi wa ujenzi wa mabweni mawili katika shule ya sekondari ya Bukwimba wilayani N...
05/06/2026

SERIKALI imekamilisha kwa asilimia 98 mradi wa ujenzi wa mabweni mawili katika shule ya sekondari ya Bukwimba wilayani Nyang’hwale mkoani Geita kupitia mfumo wa Force Account.

Mradi huo wenye thamani ya sh milioni 260 ulianza kujengwa na Mkandarasi Kampuni ya Ekimart Contractors (T) LTD ambaye alishindwa kuendelea na kazi na kutelekeza mradi ukiwa asilimia 70.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Bukwimba, Zabron Buluba ametoa taarifa hiyo wakati wa ziara ya mkuu wa mkoa wa Geita alipofika kukagua maendeleo ya mradi huo.

Zabron amesema fedha za mradi zilitolewa na serikali katika mwaka wa fedha 2024/25 hata hivyo mradi haukukamilika kwa wakati baada ya mkandarasi kushindwa kuendelea na kazi hiyo.

Amesema kufuatia changamoto hiyo juhudi za kumrejesha mkandarasi zilifanyika bila mafanikio na kuilazimu serikali kuvunja mkataba wake na kisha kuendelea na ujenzi kwa njia ya force account.

Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale Grace Kingalame amesema mabweni hayo yatakuwa msaada kwa shule ya sekondari Bukwimba kwani imepata kibali cha kudahili wanafunzi wa kidato cha tano na sita.

Amesema shule hiyo ni miongoni mwa shule bora zinazofanya vizuri katika mtihani wa taifa wa kidato cha nne hivo ongezeko la miundombinu ni chachu ya kuinua kiwango cha ufaulu zaidi.

Amesema chini ya uongozi wake wilayani humo ataendelea kusimama kidete kuhakikisha sekta ya elimu inapiga hatua zaidi kwa kuendana na kasi ya miundombinu ya elimu inyojengwa na serikali.

Mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigela amepongeza wilaya hiyo kwa kufanikisha ukamilishaji wa mradi huo huku akiagiza halmashauri ianze mchakato wa ujenzi wa uzio shuleni hapo mara moja.

Amesema hatua ya serikali kutoa kibali cha shule ya sekondari Bukwimba kudahili wanafunzi wa kidato cha tano na sita imekuja baada ya kuridhishwa na maendeleo yake na miundombinu iliyopo.

Habari na .yohana.jr

HALMASHAURI ya wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita imeweka mpango maalum wa kushirikisha wadau wa maendeleo ili kumaliza ...
05/06/2026

HALMASHAURI ya wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita imeweka mpango maalum wa kushirikisha wadau wa maendeleo ili kumaliza uhaba wa madawati kwa shule za sekondari.

Mpango huo umeazimia kufikia mahitaji la madawati 3,000 kwa mwaka wa masomo 2026 katika shule za sekondari za serikali 20 ambazo zimepokea wanafunzi wa kidato cha kwanza 3,056.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya hiyo, Husna Toni amesema hayo katika taarifa yake kwa mkuu wa mkoa alipokagua na kupokea madawati 1,200 yaliyopatikana hadi kufikia Mei 2026.

Husna amesema madawati hayo ni mafanikio ya awamu ya kwanza ya mpango huo unaolenga kupata madawati 1,500 ambapo juhudi zinaendelea ili kufikia nusu ya mahitaji yaliyopo.

Amesema upungufu wa madawati umetokana mwitikio mkubwa wa wazazi kupeleka watoto shule baada ya sera ya elimu bila bure inayotekelezwa na serikali ya awamu ya sita.

“Ninaamini utoaji wa madawati haya utaboresha utoaji wa huduma ya elimu kwa wanafunzi wetu, na hatimaye kuongeza ufaulu shuleni”, amesema Husna.

Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale, Grace Kingalame amesema wadau wakubwa walioshirikishwa kuunga mkono mpango huu ni wawekezaji katika sekta ya madini na wameonyesha mwitikio.

Amesema mpango huo ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto na kuendana na kasi ya ujenzi wa madarasa inayotekelezwa na serikali.

Mkuu wa mkoa wa Geita, Martine Shigela amepongeza mpango huo huku akizitaka halmashauri zingine kuiga mfano wa Nyang’wale kuunga mkono juhudi za serikali katika sekta ya elimu.

“Huu ni ujumbe kwa wengine hususani kwa viongozi na watendaji kuhakikisha kwamba wanaiga mfano wa Nyang’hwale katika kuhakikisha kwamba wanafunzi wanapata madawati.

“Shule ambazo zitapokea Samani hizi, ni vyema wakapokea na kuthamini mchango huu, na kubwa zaidi kutunza na kuhakikisha pale panapotokea uharibifu, marekebisho yafanyike”, ameelekeza.

Habari Na .yohana.jr

05/06/2026

Mgogoro kati ya Wachimbaji wa Madini katika Mgodi wa Nyamalapa na Mmiliki wa Mgodi uliopo Wilaya ya Nyang'hwale Mkoani Geita umeanza kutatuliwa baada ya wachimbaji wa Mgodi huo kupiga kambi katika ofisi ya Mkuu wa wilaya hiyo na hatimaye kukutana na Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela.

Wachimbaji hao wa Madini wamefika katika ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Nyang'hwale Grace Kingalame na ndipo baadaye Mkuu wa Mkoa Martine Shigela akafika kuwasikiliza.

Wakitoa Madai yao wachimbaji hao Said Fumbuka katibu wa Mgodi huo na Isack Paul wamesema wanaomba kuruhusiwa kuendelea kuchimba Madini katika Mgodi wa Nyamalapa baada ya kusimamishwa kufanya kazi kwa madai kuwa mkataba wa makubaliano wa kuwekeza katika Mgodi huo umekwisha hivyo wanapaswa kuondoka ili kumpisha Mmiliki aendelee na taratibu zingine.

Meneja wa Mgodi huo Kapunda Makamba amesema shughuli zimesimama kwa Sasa katika Mgodi huo baada ya mkataba na wachimbaji hao kumalizika.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela amesema serikali imeanza kuchukua hatua ili kumaliza mgogoro huo.

05/06/2026

HALMASHAURI ya wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita imeweka mpango maalum wa kushirikisha wadau wa maendeleo ili kumaliza uhaba wa madawati kwa shule za sekondari.

Mpango huo umeazimia kufikia mahitaji la madawati 3,000 kwa mwaka wa masomo 2026 katika shule za sekondari za serikali 20 ambazo zimepokea wanafunzi wa kidato cha kwanza 3,056.

Mkuu wa wilaya ya Nyang'hwale, Grace Kingalame amesema hayo katika taarifa yake kwa mkuu wa mkoa alipokagua na kupokea madawati 1,200 yaliyopatikana hadi kufikia Mei 2026.

Habari Na .yohana.jr

04/06/2026

Wahimbaji wadogo wa Madini katika Mgodi wa Igalula Wilayani Nyang’hwale Mkoani Geita wamesema serikali ina mchango mkubwa katika kuongeza tija katika sekta hiyo kwa kuwa imerahisisha upatikanaji wa zana zinatumika kuchimba madini.

Wachimbaji hao wa madini wameeleza hayo baada ya kuwafikia Mgodini hapo ili waweze kueleza mchango wa serikali katika shughuli zao.

Wachimbaji hao wa Madini akiwemo Saguda Nyerere na Ezekiel Magunguli wamesema serikali ya awamu ya sita ina mchango mkubwa katika sekta ya madini kwa kuwa imerahisisha upatikanaji wa zana za kuchimbia madini.

Viongozi wa mgodi huo kupitia kwa katibu Mkuu wa Mgodi Makamba Lameck wanamesema serikali ina mchango mkubwa katika maendeleo ya mgodi huo huku wameomba kupelekewa umeme.

Shirika la umeme TANESCO wilaya ya Nyang’hwale Mkoani Geita kupitia kwa Meneja Lucas Karoli limetoa ufafanuzi wa kupeleka umeme mgodini hapo.

04/06/2026

Spika wa bunge Musa Azan Zungu amemuagiza katibu wa bunge Baraka Leonard awaandikie barua za kujieleza wabunge wote waliokwenda nchini Moroco bila kibali chake kushuhudia fainali za AFCON kwa vijana chini ya umri wa miaka 17kwa kuwa kufanya hivyo ni kinyume na kanuni za bunge.

Spika ametoa agizo hilo bungeni jijini Dodoma akisema wapo wabunge walioambatana na timu ya Serengeti boys bila kibali rasmi cha ofisi ya Spika na kukiuka taratibu na kanuni za uendeshaji wa bunge.

Aidha amemtaka Katibu wa bunge kuhakikisha wabunge hao wanajibu barua hizo ndani ya siku nne na watakaoshindwa kufanya hivyo wachukuliwe hatua za kisheria kwa mujibu wa kanuni za bunge.

Address

BOMANI
Geita
30101

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Rubondofm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Rubondofm:

Share