Rubondofm

Rubondofm District radio station
provide News content, sports, music and current affairs.

Tunaomba radhi kwa adha ulioipata mdau wetu kwa kutokupata maudhui yetu  kwa muda Sasa.Kwa Sasa tunayo furaha kukufahami...
16/03/2025

Tunaomba radhi kwa adha ulioipata mdau wetu kwa kutokupata maudhui yetu kwa muda Sasa.
Kwa Sasa tunayo furaha kukufahamisha kwamba Matangazo yetu yamerejea k**a kawaida.

Je, Ulimis zaidi kipindi gani?

02/03/2025

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Mhe. Dkt. Doroth Gwajima, amesema atatembelea ofisi za Benki ya Stanbic ili kupata ufafanuzi wa takwimu zao kuhusu namna walivyowezesha wanawake kiuchumi kupitia mikopo nafuu. Lengo lake ni kuhakikisha Watanzania wengi wanapata taarifa hizo na kutumia fursa hiyo kuinuka kiuchumi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Kanda ya Ziwa katika Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, Dkt. Gwajima alisema amesikia Stanbic wakieleza kuwa wametoa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wanawake.

Hata hivyo, alibainisha kuwa baadhi ya takwimu alizozisikia kutoka kwa benki hiyo ni mpya kwake, na huenda pia kwa wananchi wengine.

"K**a mimi sijawahi kusikia, basi kuna wananchi wengi pia hawajawahi kupata taarifa hizi. Nitatembelea ofisi za Stanbic ili nipate ufafanuzi wa kina na niweze kuwafikishia wananchi taarifa hizi kwa sababu Rais Samia ameweka mazingira mazuri yanayowawezesha wananchi kunufaika na fursa mbalimbali," alisema Dkt. Gwajima.

Katika maadhimisho hayo, Waziri Gwajima pia alisifu mchango wa Benki ya Stanbic kwa maendeleo ya taifa, akisema kuwa kwa kipindi cha miaka 30 ya uwepo wake nchini, benki hiyo imefanya kazi nzuri.

Kwa upande wake, Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya Stanbic, Bw. Fredrick Max, alisema benki hiyo inaendelea kukua kwa kasi na imeendelea kuwahudumia Watanzania kupitia matawi yake 11, huku matawi mengine sita yakiwa mbioni kufunguliwa mwaka huu, ikiwemo tawi moja mkoani Geita.

"Tuna zaidi ya mawakala 1,500 nchini kote na tunatoa huduma bora za kibenki kidijitali. Ukuaji wetu umeambatana na ongezeko la wafanyakazi, ambapo sasa tuna zaidi ya 600 nchini nzima," alisema Bw. Max.

Aidha, alibainisha kuwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Benki ya Stanbic kwa kushirikiana na benki mama ya Standard Bank Group, imetoa mikopo nafuu kwa Serikali ya Tanzania inayofikia zaidi ya dola bilioni 1 za Kimarekani. Kati ya hizo, dola milioni 600 zimetolewa na Stanbic Tanzania na Standard Bank Group, huku kiasi kingine kikitolewa na washirika wao mbalimbali.

Fedha hizo zimetumika katika miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo sekta za nishati, miundombinu, elimu, maji, na afya.

Pia, Bw. Max alieleza kuwa Benki ya Stanbic imekuwa ikiwezesha biashara za wanawake nchini kwa kutoa mikopo kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati. Katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita, benki hiyo imesaidia zaidi ya biashara 1,000 zinazomilikiwa na wanawake kwa mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 10.

Maadhimisho haya ya Siku ya Wanawake Duniani Kanda ya Ziwa yamekuwa jukwaa muhimu la kujadili masuala ya uwezeshaji wa wanawake kiuchumi na fursa zinazopatikana kupitia taasisi mbalimbali za kifedha k**a Benki ya Stanbic.

Imeandikwa na Gharos Riwa

02/03/2025

Mkoa wa Geita ni miongoni mwa mikoa iliyopata fursa ya kunufaika na mradi wa maji kwa miji 28 nchini, unaofadhiliwa na Serikali ya India kwa masharti nafuu.

Miji miwili ya Geita na Chato imejumuishwa katika mpango huo, jambo ambalo limeelezwa kuwa ni fursa kubwa kwa wakazi wa maeneo hayo.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Chato, Mhandisi Isack Mgeni, amesema kuwa ingawa Tanzania ina miji mingi, Geita imepata bahati ya kupokea mradi huo, na hivyo ni jambo la kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa upendeleo huo.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Taasisi ya Wanawake na Samia, iliyofanyika katika Kata ya Bwanga, Wilaya ya Chato, Mhandisi Mgeni alieleza kuwa utekelezaji wa mradi huo unaendelea bila kusimama kwa kuwa fedha zote zimeshatolewa.

Kwa mujibu wa Mhandisi Mgeni, Mji wa Chato umetengewa shilingi bilioni 39 kwa ajili ya mradi mkubwa wa maji unaotekelezwa katika eneo la Buzirayombo.

Mradi huo unatarajiwa kuzalisha lita milioni 11 za maji kwa siku, huku mahitaji ya mji huo yakiwa wastani wa lita milioni 6 kwa siku, hivyo kutakuwa na ziada ya lita milioni 4.

Aidha, aliongeza kuwa kwa kuunganisha maji yaliyopo yenye uwezo wa kuzalisha lita milioni 4.8 kwa siku, jumla ya ziada itafikia lita milioni 8

Hivyo itawezesha upatikanaji wa maji wa uhakika, huku Mamlaka ikipanga kusambaza maji hayo katika kata mbalimbali za Wilaya ya Chato ili kusaidia juhudi za serikali katika kuboresha huduma za maji kwa wananchi.
Gharos Riwa

01/03/2025

Mbunge wa Jimbo la Chato, Mhe. Dkt. Medard Kalemani, amesema sauti ya wanawake ni sauti ya Mungu na wengi, akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Dkt. Kalemani alitoa kauli hiyo Machi 1, 2025, wakati wa uzinduzi wa Taasisi ya Wanawake na Samia katika Kata ya Bwanga, Wilaya ya Chato, akisisitiza kuwa Tanzania ni nchi yenye utulivu, amani, na mshik**ano mkubwa, hali ambayo imechochewa na uongozi wa Rais Samia.

Alieleza kuwa serikali imewekeza katika maendeleo ya miundombinu mkoani Geita, hususan katika Kata ya Bwanga, ambapo huduma za umeme, maji safi, barabara za lami, na stendi ya mabasi zipo katika hali nzuri.

Mbunge huyo aliwataka wanawake kupitia taasisi hiyo kushiriki kikamilifu katika kueneza mafanikio ya Rais Samia kwa Watanzania wote. "Sauti ya wanawake ni sauti ya Mungu na ya wengi, hivyo ni muhimu kuzungumza mazuri yanayofanywa na serikali," alisisitiza Dkt. Kalemani.

Gharos Riwa

01/03/2025

Kituo cha Afya Bwanga Chato Chatoa Huduma Bora kwa Wajawazito

Kituo cha Afya Bwanga kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Mkoa wa Geita, kimekuwa msaada mkubwa kwa wanawake wajawazito, kikifanya upasuaji wa dharura kwa wajawazito wenye uchungu pingamizi kati ya 40 hadi 45 kila mwezi.

Mganga Mfawidhi wa kituo hicho, Dkt. Remidius Jovin, akizungumza Machi 1, 2025, wakati wa kupokea msaada wa vifaa mbalimbali kwa ajili ya akinamama waliojifungua, kutoka kwa Taasisi ya Wanawake na Samia, alisema kuwa wastani wa wanawake 15 hadi 20 hufika kituoni hapo kila siku kwa ajili ya kujifungua.

"Kwa siku tunafanya upasuaji wa dharura kwa wajawazito 1 hadi 2, na kwa mwezi tunafikia upasuaji wa wanawake 40 hadi 45 kutokana na changamoto mbalimbali za uzazi," alisema Dkt. Jovin.

Aidha, alieleza kuwa kituo hicho kinahudumia wanawake kutoka ndani na nje ya kata hiyo, kikiwa na wodi tatu za wazazi ambazo zina jumla ya wauguzi 15.

Wodi hizo ni ya wanawake wanaosubiri kujifungua, wodi ya wazazi, na wodi ya akinamama baada ya kujifungua.

Alisisitiza kuwa wanawake wote wanapata huduma stahiki, iwe ni kujifungua kawaida au kwa njia ya upasuaji.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Samia, Bi Kabak**a, aliwahimiza wanawake kuendelea kutumia kituo hicho cha afya ambacho kimeboreshwa kwa kupatiwa vifaa tiba muhimu kupitia juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan.

Aidha, alipokuwa kwenye hafla ya uzinduzi katika Shule ya Msingi Bwanga, Bi Kabak**a aliwasisitiza wanaume kuambatana na wake zao wakati wa kujifungua, kwani sasa wodi hiyo ina miundombinu inayoruhusu uwepo wa mwanaume kumsaidia mwenza wake wakati wa kujifungua.

Dkt. Biteko: Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi Wasaidie Kutatua Kero za WalimuWakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri...
27/02/2025

Dkt. Biteko: Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi Wasaidie Kutatua Kero za Walimu

Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini wametakiwa kuanzisha kliniki ndogondogo za walimu ili kusaidia kutatua changamoto zinazowakabili.

Rai hiyo imetolewa leo, Februari 26, 2025, na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Dotto Mashaka Biteko, wakati wa kliniki ya kusikiliza na kutatua kero za walimu iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Nyankumbu, Manispaa ya Geita.

Dkt. Biteko amesema kuwa baadhi ya changamoto za walimu zinaweza kutatuliwa katika ngazi za halmashauri bila kufikishwa kwenye ngazi za juu za serikali, endapo tu walimu watawasilisha kero zao kwa wakati kupitia viongozi wao wa halmashauri.

Akizungumzia mafanikio ya sekta ya elimu katika serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Dkt. Biteko amesema kuwa zaidi ya walimu 10,839 wamepandishwa madaraja, huku shilingi bilioni 4.6 zikitumika kuwalipa madeni na malimbikizo ya mishahara walimu 5,061. Aidha, walimu 876 wamebadilishiwa muundo wa ajira baada ya kujiendeleza kielimu.

Ameongeza kuwa serikali ya awamu ya sita inatambua na kuthamini mchango wa walimu katika maendeleo ya sekta ya elimu, ambapo shilingi milioni 25 zimetumika kwa ajili ya matibabu ya walimu katika Mkoa wa Geita kwa mwaka 2024.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Patrobas Paschal Katambi, amesema serikali imefanya mabadiliko katika sera na sheria za utumishi wa umma, ikiwemo sheria za mifuko ya hifadhi ya jamii PSSF na NSSF, ili kuendana na mahitaji ya sasa na kuondoa kero zinazowakabili watumishi, wakiwemo walimu.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Martin Shigela, amepongeza Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kwa kubuni mbinu bora za kutatua kero za walimu kwa kuwakutanisha na serikali.

Kliniki hiyo imeratibiwa na CWT kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Ofisi ya Rais – Utumishi na Utawala Bora, Wizara ya Fedha, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, pamoja na Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC-HQ).

Imeandikwa na
Na kuhaririwa na

CHATO YAKABILIWA NA UPUNGUFU WA MADAWATI ZAIDI YA  ELFU 26 SHULE ZA MSINGI.Serikali katika wilaya ya chato Mkoani Geita ...
27/02/2025

CHATO YAKABILIWA NA UPUNGUFU WA MADAWATI ZAIDI YA ELFU 26 SHULE ZA MSINGI.

Serikali katika wilaya ya chato Mkoani Geita imewaomba wadau wa elimu kuendelea kushirikiana na serikali ili kutatua upungufu wa madawati kwa wanafunzi wa shule za Msingi na sekondari Wilayani humo.

Rai hiyo imetolewa na katibu Tawala Wilaya ya Chato Thomas Dime wakati akimwakilisha Mkuu wa Wilaya hiyo katika hafla ya kukabidhi madawati, viti pamoja na vifaa tiba kwenye shule ya Msingi Mkuyuni vilivyotolewa na Benki ya Nmb kwa lengo la kutatua changamoto katika sekta ya elimu pamoja na afya.

Dime amesema Wilaya ya Chato inakabiliwa na upungufu wa madawati zaidi ya elfu 26 kwa shule za Msingi pamoja na elfu 6 kwa shule za Sekondari na kuwaomba wadau wa elimu, Serikali kupitia Halmashauri pamoja na wananchi kushirikiana kutatua tatizo hilo.

Meneja wa benki ya Nmb kanda ya ziwa Faraja Raphael Ng'ingo amevitaja vifaa hivyo vilivyotolewa na Benki hiyo vimegharimu kiasi cha shilingi Milioni 29.5 na vitainufaisha Hospitali ya Rufaa kanda ya Chato, shule ya Rubambagwe, Itale, Lumasi pamoja na shule ya Msingi Mkuyuni.

Mbunge wa jimbo la Chato Dk. Medard Matogolo Kalemani na Mwenyekiti wa kijiji cha Mkuyuni Goodluck Phinias wameishukuru Benki ya Nmb kwa msaada wake na kuomba kuendelea kujitoa katika kuchochea maendeleo ya Wilaya ya Chato katika nyanja mbalimbali.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wilaya ya Chato, Serikali kwa kushirikiana na wakala wa misitu TFS wamepanga kutumia misitu iliyopo kutengeneza viti na meza kukabiliana na tatizo hilo.

Imeandikwa na
Na kuhaririwa na

Idara ya Maendeleo Ya Jamii, Halmshauri Ya Wilaya Ya Geita kwa kushirikiana na wadau wa wamendeleo wameendelea kutoa eli...
25/02/2025

Idara ya Maendeleo Ya Jamii, Halmshauri Ya Wilaya Ya Geita kwa kushirikiana na wadau wa wamendeleo wameendelea kutoa elimu katika Kijiji cha Busaka Kata ya Bukondo kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani Machi 8, 2025.Akiongea na wananchi wa Kijiji Cha Busaka Februari 24, 2025 mdau kutoka Smaujata Elizabeth Coster amewataka wanaume kuacha kuwapiga wake zao pale wanapokosea na badala yake wasuluhishe kwa kuzungumza.

Aidha wamewaomba wanawake kutokuwa chanzo cha wanaume wao kuwafanyia ukatili kwani baadhi ya wanawake wamekuwa hawana heshima na pia hawatekelezi majukumu yao k**a wanawake.

Afisa Maendeleo Ya Jamii Kutoka Halmashauri Ya Wilaya Ya Geita Tibezuka John amewaomba wazazi kuwapa muda wa kutosha watoto kujisomea hasa watoto wa k**e badala ya kutumia muda mwingi kuwapa kazi za nyumbani k**a kulima, kuchunga mifugo pamoja na kuwahudumia wadogo zao.

Amesema jukumu la kuhudumia familia ni la mzazi na si la mtoto hivyo ni vyema kusimama katika nafasi zao kwa kuhakikisha watoto wanapata mahitaji yote ya msingi.

Naye Christina Gamba mdau kutoa Shirika Lisilo La Kiserikali La Marafiki Wa Elimu amewaomba wazazi kufuatilia kwa ukaribu marafiki wa watoto wao kwani wengi wameingia kwenye makundi yasiyofaa na kusababisha mtoto kuwa na tabia zisizo nzuri kwa jamii.

Wakizungumza kwa niaba ya wananchi wa Kijiji cha Busaka wamefurahia elimu iliyotolewa na wawezeshaji na kuomba kurudi tena kijijini hapo kuzungumza na wanawake kwani wanawake wengi wamekosa utii lakini pia wamekuwa wakiwapa maneno mabaya watoto kuhusu baba zao.

Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yanatarajiwa kufanyika kitaifa Machi 8, 2025 Jijini Arusha yakibeba kauli mbiu isemayo “Wanawake na Wasichana 2025: Tuimaishe Haki, Usawa na Uwezeshaji”.


Uchimbaji wa madini umekuwa kinara wa uharibifu wa mazingira katika Halmashauri Ya Wilaya Ya Geita kwa asilimia 45 ambap...
25/02/2025

Uchimbaji wa madini umekuwa kinara wa uharibifu wa mazingira katika Halmashauri Ya Wilaya Ya Geita kwa asilimia 45 ambapo juhudi mbalimbali zimekuwepo ikiwa ni pamoja na kila mchimbaji kuhakikisha anapanda miti isiyopungua 100 kwa mwaka.

Hayo yamesemwa na Mkuu Wa Kitengo Cha Maliasiri Na Hifadhi Mazingira Halmashauri Ya Wilaya Ya Geita Hellen Mgini Februari 25, 2025 wakati wa uzinduzi wa zoezi la upandaji miti katika shule ya msingi Mtoni mji mdogo Katoro kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.

Akitoa taarifa fupi kwa Mgeni Rasmi Afisa Maendeleo Ya Jamii Halmashauri Ya Wilaya Ya Geita Rehema Kabanda amesema kuelekea kilele cha maadhimisho hayo idara hiyo imetekeleza shughuli mbalimbali za utoaji elimu, upandaji wa miti 200 pamoja na kufanya utalii katika Kisiwa Cha Taifa Cha Rubondo.

Akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi, Afisa Tarafa Ya Butundwe Kassim Ramadhani ametoa wito kwa halmashauri kuwa na mwendelezo wa upandaji miti katika maeneo yote ya utawala lakini pia wananchi kuwa mabalozi wazuri wa upandaji miti katika maeneo yao.

Peter Deogratius mwenyekiti wa kikundi cha Twigunane Group na Magdalena Kusekwa wamewashauri wananchi wote wa Katoro kupanda miti katika maeneo yao ili kuweka mazingira vizuri.

Nao wanafunzi wa shule ya msingi Mtoni wameahidi kusimamia miti hiyo na kuilinda dhidi ya wanyama waharibifu ili iweze kuwaletea kivuli na hewa nzuri wawapo shuleni.

Maadhimisho ya siku ya wanawake Mkoa wa Geita yanatarajiwa kufanyika Wilayani Bukombe Machi 2, 2025 kwa kongamano na Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Naibu Waziri Mkuu Na Waziri Wa Nishati Dokta Dotto Biteko.


Kukosekana kwa maadili kwa watoto kumechangiwa kiasi kikubwa na malezi yasiyofaa kwa baadhi ya wazazi pamoja na walezi k...
22/02/2025

Kukosekana kwa maadili kwa watoto kumechangiwa kiasi kikubwa na malezi yasiyofaa kwa baadhi ya wazazi pamoja na walezi kwakuwa watoto wengi huiga kinachofanywa na wazazi.

Hayo yameelezwa na Christina Gamba mdau kutoa Shirika Lisilo La Kiserikali La Marafi Wa Elimu katika Kata Ya Bugalama Halmashauri Ya Wilaya Ya Geita Februari 21, 2025 katika muendelezo wa utoaji elimu katika vijiji mbalimbali vya halmashauri hiyo kuelekea siku ya wanawake duniani.

Gamba amesema watoto wengi wamekuwa wakiiga vile wanavyoona kwa wazazi wao kwani kuna baadhi ya wazazi wamekuwa wakiwaagiza watoto pombe, sigara lakini pia kutumia madawa ya kulevya mbele yao.

Kwa upande wake Elizabeth Coster mdau kutoka Smaujata amewasihi wanawake kutowatelekeza watoto kwa sababu ya kutofautiana na waume zao kwani vitendo hivyo vimepelekea watoto wengi kufanyiwa ukatili.

Amesema “wanawake wengi sasa hivi mmekuwa mkiteleza watoto kwa baba zao pamoja na bibi na kukimbilia kuolewa na wanaume wengine bila kujali wale ni watoto wadogo hii imekuwa ikisababisha watoto kujilea wenyewe na kupelekea kufanyiwa ukatili”.

Naye Afisa Maendeleo Ya Jamii Kutoka Halmashauri Ya Wilaya Ya Geita Tibezuka John amewataka wazazi kuwapeleka watoto shule na kufuatilia maendeleo yao ikiwa ni pamoja na kuhudhuria vikao vya shule, kushirikiana na walimu kuhusu ufaulu na chakula shuleni.

Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yanatarajiwa kufanyika kitaifa Machi 8, 2025 Jijini Arusha yakibeba kauli mbiu isemayo “Wanawake na Wasichana 2025: Tuimaishe Haki, Usawa na Uwezeshaji”.

Kukosekana kwa maadili kwa watoto kumechangiwa kiasi kikubwa na malezi yasiyofaa kwa baadhi ya wazazi pamoja na walezi k...
22/02/2025

Kukosekana kwa maadili kwa watoto kumechangiwa kiasi kikubwa na malezi yasiyofaa kwa baadhi ya wazazi pamoja na walezi kwakuwa watoto wengi huiga kinachofanywa na wazazi.

Hayo yameelezwa na Christina Gamba mdau kutoa Shirika Lisilo La Kiserikali La Marafi Wa Elimu katika Kata Ya Bugalama Halmashauri Ya Wilaya Ya Geita Februari 21, 2025 katika muendelezo wa utoaji elimu katika vijiji mbalimbali vya halmashauri hiyo kuelekea siku ya wanawake duniani.

Gamba amesema watoto wengi wamekuwa wakiiga vile wanavyoona kwa wazazi wao kwani kuna baadhi ya wazazi wamekuwa wakiwaagiza watoto pombe, sigara lakini pia kutumia madawa ya kulevya mbele yao.

Kwa upande wake Elizabeth Coster mdau kutoka Smaujata amewasihi wanawake kutowatelekeza watoto kwa sababu ya kutofautiana na waume zao kwani vitendo hivyo vimepelekea watoto wengi kufanyiwa ukatili.

Amesema “wanawake wengi sasa hivi mmekuwa mkiteleza watoto kwa baba zao pamoja na bibi na kukimbilia kuolewa na wanaume wengine bila kujali wale ni watoto wadogo hii imekuwa ikisababisha watoto kujilea wenyewe na kupelekea kufanyiwa ukatili”.

Naye Afisa Maendeleo Ya Jamii Kutoka Halmashauri Ya Wilaya Ya Geita Tibezuka John amewataka wazazi kuwapeleka watoto shule na kufuatilia maendeleo yao ikiwa ni pamoja na kuhudhuria vikao vya shule, kushirikiana na walimu kuhusu ufaulu na chakula shuleni.

Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yanatarajiwa kufanyika kitaifa Machi 8, 2025 Jijini Arusha yakibeba kauli mbiu isemayo “Wanawake na Wasichana 2025: Tuimaishe Haki, Usawa na Uwezeshaji”.


@

MBUNGE MHE. CONSTANTINE KANYASU ATIMIZA AHADI YA KUKABIDHI PIKIPIKI KWA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA GEITA Mbunge wa Jimb...
20/02/2025

MBUNGE MHE. CONSTANTINE KANYASU ATIMIZA AHADI YA KUKABIDHI PIKIPIKI KWA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA GEITA

Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini, Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, ametekeleza ahadi yake kwa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Geita (GPC) kwa kukabidhi pikipiki tatu zitakazorahisisha kazi za uandishi wa habari katika mkoa huo.

Katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika leo, Mheshimiwa Kanyasu amepongeza juhudi za waandishi wa habari katika kuhabarisha na kuelimisha jamii, akisema kuwa mchango wao ni muhimu kwa maendeleo ya taifa.

"Ninatambua kazi kubwa inayofanywa na waandishi wa habari katika kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kwa wakati. Pikipiki hizi zitawasaidia kuwafikia wananchi kwa haraka na kufanya kazi yenu kwa ufanisi zaidi," alisema Mheshimiwa Kanyasu.

Mwenyekiti wa GPC, Bw. Renatus Masuguliko, amepongeza juhudi za Mbunge huyo na kueleza kuwa msaada huo utakuwa chachu ya kuboresha mazingira ya kazi kwa wanahabari wa Geita.

"Tunamshukuru sana Mheshimiwa Kanyasu kwa kutimiza ahadi yake. Pikipiki hizi zitatuwezesha kufuatilia matukio kwa wakati na kuhakikisha habari zinawafikia wananchi haraka," alisema Bw. Masuguliko.

Hafla hiyo imehudhuriwa na waandishi wa habari wa Geita pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya habari, ambao wamesisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana katika kuboresha mazingira ya kazi kwa wanahabari nchini.



JAMII YAELIMISHWA KUHUSU UKATILI WA KIJINSIA,MALEZI BORA NA AFYA KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE.Katika kuelekea kilele cha ma...
20/02/2025

JAMII YAELIMISHWA KUHUSU UKATILI WA KIJINSIA,MALEZI BORA NA AFYA KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE.

Katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani, Halmashauri Ya Wilaya Ya Geita, Idara Ya Maendeleo Ya Jamii kwa kushirikiana na wadau wameanza ziara ya kutembelea vijiji mbalimbali kwa ajili ya kutoa elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia, malezi na makuzi ya mtoto, afya ya akili pamoja na madawa ya kulevya.

Akizungumza na wanakijiji wa kata ya Nyawilimilwa februari 20, 2025, Afisa Maendeleo Ya Jamii Halmashauri Ya Walaya Ya Geita Tibezuka John ameitaka jamii kuzingatia lishe bora kwa watoto na wajawazito na akisisitiza suala la maadili kwa kutowalaza watoto wa k**e na kiume katika chumba kimoja.

“wazazi mjitahidi kunyonyesha watoto miezi sita mfululizo bila kuwapa kitu chochote, mhakikishe mnawapa watoto vyakula kwa kuzingatia makundi ya chakula, kuwapatia chanjo na pia kwenye maadali msiwalaze watoto wak**e na kiume chumba kimoja”, amesema Tibezuka.

Naye Elizabeth Coster mdau kutoka SMAUJATA akizungumzia ukatili amesema si vyema wazazi kuwaadhibu watoto kwa kuwafanyia ukatili k**a wa kuwachoma moto na kuwafanyia vitendo vingine vya ukatili pale wanapokosea kwani huo ni ukatili na sio adhabu.

Mdau kutoka shirika lisilo la kiserikali, Marafiki Wa Elimu, Christina Gamba amesema kutokuwajibika kwa wazazi na walezi kumepelekea watoto wengi kujiingiza katika makundi yasiyofaa hasa ya madawa ya kulevya.

Baadhi ya wananchi waliopata elimu hiyo akiwemo Patrick Kwimba Na Grace James Kazinza wamesema wamenufaika na elimu iliyotolewa hasa kwenye malezi ya watoto na ukatili na kuomba elimu hiyo iwe endelevu.

Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yanatarajiwa kufanyika Kitaifa machi 8, 2025 Jijini Arusha yakibebwa na kauli mbiu isemayo “Wanawake na Wasichana 2025: Tuimarishe Haki , Usawa Na Uwezeshaji.




@105.3rubondofmupdate

GEITA DC YAFIKIA ASILIMIA 58 UKUSANYAJI WA MAPATO YA NDANINa Yohana Shida, Geita.HALMASHAURI ya wilaya ya Geita imefanik...
20/02/2025

GEITA DC YAFIKIA ASILIMIA 58 UKUSANYAJI WA MAPATO YA NDANI

Na Yohana Shida, Geita.

HALMASHAURI ya wilaya ya Geita imefanikiwa kukusanya kiasi cha sh bilioni 4.87 ya mapato ya ndani ambayo ni sawa na asilimia 58.39 ya malengo ya kipindi cha Julai hadi Desemba mwaka 2024.

Aidha halmashauri hiyo hadi kufikia Desemba 2024 imekusanya na kupokea jumla ya Sh bilioni 45.5 sawa na asilimia 54.3 ya lengo la fedha za mapato ya ndani, mishahara na fedha za miradi ya maendeleo.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Geita, Karia Rajabu amesema hayo katika mkutano wa kawaida cha Baraza la Madiwani kwa Kipindi cha Robo ya Pili kwa mwaka wa Fedha 2024/25.

Amesema halmashauri ya wilaya ya Geita kwa mwaka huu wa fedha 2024/25 imepanga kupokea na kukusanya jumla ya sh bilioni 84.3 kwa ajili ya mishahara, ruzuku ya matumizi mengineyo pamoja na miradi ya maendeleo.

Ameongeza kuwa, kwa mwaka wa fedha 2024/25 halmashuri imepanga kusimamia na kutekeleza miradi ya maendeleo yenye thamani ya sh bilioni 17.2 kutoka mapato ya ndani, fedha za wahisani na serikali kuu.

“Hadi kufikia Desemba 2024 kiasi cha Shilingi bilioni 14.8 zimepokelewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kutoka serikali kuu na wadau.

“Kwa upande wa miradi ya mapato ya ndani, halmashauri imehamisha kiasi cha sh bilioni 2.3 iliyopangwa kutekeleza miradi ya msingi", amesema Karia.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Geita, Charles Kazungu amesema suala la ukusanyaji wa mapato linahitaji ushirikiano hivo nguvu ya pamoja inahitajika ili kuvuka malengo ya mwaka huu wa fedha.

"Sisi k**a halmashauri kupitia madiwani, tukiongozwa na k**ati ya fedha tumejipanga, ajenda ya mapato ni ajenda mtambuka kwetu, suala la mapato tumelichukulia kipaumbele cha kwanza", amesisitiza Kazungu.

Kaimu mkuu wilaya ya Geita ambaye ni Katibu Tawala wa wilaya, Lucy Beda ameitaka halmashauri kutobweteka badala yake kusimamia kikamirifu na kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato ya ndani na fedha za ruzuku kutoka serikali kuu.
yohana.jr

GEITA DC YAFIKIA ASILIMIA 95 UTEKELEZAJI ILANI YA CCMHALMASHAURI ya wilaya ya Geita mkoani hapa imeweka wazi kuwa mpaka ...
18/02/2025

GEITA DC YAFIKIA ASILIMIA 95 UTEKELEZAJI ILANI YA CCM

HALMASHAURI ya wilaya ya Geita mkoani hapa imeweka wazi kuwa mpaka kufikia Februari 2025 tayari imefikia asilimia 95 ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020-2025.

Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo, Khadija Said amesema hayo katika mkutano wa Baraza la Madiwani kwa Kipindi cha Robo ya Pili kwa mwaka wa Fedha 2024/25.

Amesema mafanikio hayo ni matokeo ya ushirikiano kati ya madiwani, viongozi na maofisa wa halmashauri ambapo kila mmoja kwa nafasi yake amewajibika kikamirifu kutatua kero za wananchi.

Amesema kupitia fedha zinazotolewa na serikali ya awamu ya sita halmashauri imesimamia kwa uafasaha kuhakikisha kila kata, kijiji na kitongoji kinapata huduma muhimu za kijamii hususani maji, afya na elimu.

“K**a kuna diwani ambaye ameshindwa kutekeleza ahadi alizotoa kwenye kata yake, nitoe wito kwa madiwani wenzangu waendelee kukumbuka zile ahadi alizotoa ili waweze kuondoa adha za wananchi", amesema.

Diwani wa Kata ya Bukoli, Faraji Self amesema kwa upande wa kata hiyo utekelezaji wa ilani umefikia asilimia 93 na juhudi kubwa zinafanyika ili kukamilisha asilimia 100 kabla ya kuvunjwa kwa bunge.

Faraji amedokeza miradi inayoendelea ni ujenzi wa jengo la upasuaji, jengo la zahanati na maabara katika kijiji cha Ntono pamoja na shule mpya ya sekondari.

“Changamoto kubwa iliyopo ni mfumo wa NEST, ambao ndio unatusumbua lakini watendaji tunawapongeza kwa kazi kubwa ambayo wanaendelea kuifanya kwenye miradi hii hakuna hujuma", amesema

Diwani wa kata ya Busanda, Seleman Gamala amesema ndani ya miaka minne kata hiyo imepokea zaidi ya sh billioni mbili kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali sambamba na pesa za mfuko wa jimbo.

“Kata ya Busanda mfuko wa jimbo umetunufaisha sana, tumepokea zaidi ya sh milioni 22 kwa ajili ya ujenzi wa daraja, ofisi za kijiji, mara ya kwanza tulipokea milioni 18, mara ya pili tukapata milioni nne.
yohana.jr

@105.3rubondofmUpdate

Madiwani Geita Wajadili Maendeleo ya Kata kwa Robo ya Pili ya Mwaka 2024/2025MADIWANI wa Halmashauri ya wilaya ya Geita ...
18/02/2025

Madiwani Geita Wajadili Maendeleo ya Kata kwa Robo ya Pili ya Mwaka 2024/2025

MADIWANI wa Halmashauri ya wilaya ya Geita wamekutana leo Februari 18, 2025 katika mkutano wa kawaida wa Baraza la Madiwani kwa Kipindi Cha Robo ya Pili ya Kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025.

Ajenda kuu ya Kikao hicho ni Kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Shughuli za Maendeleo ngazi ya kata kwa kipindi cha Oktoba hadi Desemba, 2024.

Kikao hicho kimeongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Geita, Khadija Said na kuhudhuriwa na wajumbe mbalimbali akiwemo Mbunge wa Jimbo la Busanda, Tumaini Magesa.
yohana.jr
@105.3rubondofmupdate

Serikali Yaimarisha Huduma za Fedha Geita, Yazindua Jengo la Hazina NdogoNaibu Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Mhe. Stan...
17/02/2025

Serikali Yaimarisha Huduma za Fedha Geita, Yazindua Jengo la Hazina Ndogo

Naibu Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Mhe. Stanslaus Nyongo, amezindua rasmi jengo la Hazina Ndogo Geita katika hafla iliyofanyika leo, Februari 17, 2025, katika Kata ya Bombambili, Manispaa ya Geita. Uzinduzi huu ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020, inayolenga kusogeza huduma za serikali karibu na wananchi.

Mhe. Nyongo alisema kuwa kukamilika kwa jengo hilo ni ishara ya dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuboresha utoaji wa huduma serikalini na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora bila kulazimika kusafiri umbali mrefu.

"Serikali inatekeleza Ilani kwa vitendo. Jengo hili ni sehemu ya juhudi za kuboresha mazingira ya kazi kwa watumishi wa umma na kurahisisha huduma kwa wananchi wa Geita," alisema Mhe. Nyongo.

Pamoja na uzinduzi huo, Naibu Waziri aliweka wazi kwamba Wizara ya Fedha itatoa fursa kwa taasisi nyingine za umma ambazo hazina ofisi katika mkoa wa Geita kupata nafasi ya kutoa huduma ndani ya jengo hilo, ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wananchi.

Elimu ya Fedha kwa Umma na Changamoto ya Mikopo Umiza

Katika hotuba yake, Mhe. Nyongo alisisitiza umuhimu wa elimu ya fedha kwa umma, akisema kuwa Wizara ya Fedha inatekeleza mpango wa elimu ya fedha wa mwaka 2021/22 hadi 2025/26. Mpango huo unalenga kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu masuala ya kifedha, hasa katika kuanzisha vikundi vya huduma ndogo za fedha na kupunguza utegemezi wa mikopo isiyo rasmi.

Hata hivyo, alieleza wasiwasi wake kuhusu ongezeko la mikopo umiza inayojulikana kwa majina k**a kausha damu, mikopo kuzimia, chuma ulete, na kuonya kuwa mikopo hiyo inarudisha nyuma maendeleo ya wananchi kwa kuwabebesha mzigo wa riba kubwa.

"Natoa wito kwa taasisi zote za kifedha na k**ati za ulinzi na usalama kufuatilia suala hili kwa karibu. Hatutavumilia watu wanaotoa mikopo kwa masharti kandamizi na bila vibali rasmi," aliongeza.

Mhe. Nyongo alihimiza wananchi kuwa na nidhamu ya fedha kwa kukopa kwa malengo yenye tija, k**a uwekezaji kwenye biashara na uzalishaji mali, badala ya matumizi ya kawaida.



Waziri wa Habari na Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof Palamagamba Kabudi ametoa wito kwa vyombo vya utangazaji kuwa na Ma...
13/02/2025

Waziri wa Habari na Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof Palamagamba Kabudi ametoa wito kwa vyombo vya utangazaji kuwa na Matumizi fasaha ya Lugha ya Kiswahili ili kusaidia kukua kwake.

Mhe Waziri ameyasema hayo Alhamis Februari 13, 2025 kwenye ukumbi wa New Generation Jijini Dodoma ambapo mkutano wa mwaka wa vyombo vya utangazaji unafanyika.

Amewataka Waandishi wa Habari kuandaa vipindi kwa kuzingatia ueledi na ufasaha wa matamshi yanayozingatia matumizi sahihi ya lugha yatakayochochea maendeleo kwa jamii


Address

BOMANI
Geita
30101

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Rubondofm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Rubondofm:

Share