Rubondofm

Rubondofm District radio station
provide News content, sports, music and current affairs.

02/10/2025

Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa –TAKUKURU Mkoa Geita na Viongozi wa dini kwa pamoja wameazimia kuzuia wagombea wa nafasi ya Urais,Ubunge na udiwani kutumia mimbari k**a shemu ya kufanyia kampeni za kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu oktoba 29, 2025.Azimio hilo pamoja na mengine limepitishwa kwenye mkutano maalumu ulioandaliwa na takukuru kwa lengo ya kujadili nafasi za viongozi wa dini katika mapambano dhidi rushwa kuelekea uchaguzi mkuu wa urais ubunge na udiwani Naibu mkuu wa takukuru Mkoa Geita, Alex Mpemba amesema wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu watanzania wanapaswa kuwa na mshik**ano na kuzuia rushwa.

HABARI PICHA; Wananchi wakiwa katika banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kununua majiko ya gesi na majiko bani...
23/09/2025

HABARI PICHA; Wananchi wakiwa katika banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kununua majiko ya gesi na majiko banifu kwa bei ya ruzuku katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini mkoani Geita.

Hatua hiyo inaashiria mwitikio mkubwa wa wananchi kuunga mkono kampeni ya matumizi ya nishati safi na nishati mbadala na kuondokana na matumizi ya nishati ya mazoea ambayo ni kuni na mkaa.

Maonesho ya Nane ya Teknolojia ya Madini yanafanyika katika Viwanja vya Dk Samia mjini Geita ambapo yamefunguliwa rasmi Septemba 22, 2025 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa.

Habari Na .yohana.jr

SERIKALI kupitia Benki Kuu ya Taifa (BoT) imesema itaendelea kununua dhahabu kutoka kwa wachimbaji wa madini kwa bei ili...
23/09/2025

SERIKALI kupitia Benki Kuu ya Taifa (BoT) imesema itaendelea kununua dhahabu kutoka kwa wachimbaji wa madini kwa bei iliyopo katika ushindani wa dunia ili kutoa faida kwa wachimbaji.

Ofisa kutoka Idara ya Masoko ya Fedha BoT, Rehema Kassim amesema hayo mbele ya Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa alipotembelea banda la Benki hiyo katika maonesho ya 8 ya Teknolojia ya Madini mkoani Geita.

Amesema kwa mjibu wa sheria ya madini kifungu cha 59 sura ya 123 ambacho kinaelekeza kila mwenye leseni ya uchimbaji na mchimbaji auze angalau asilimia 20 ya dhahabu yake.

Amesema mtu anayeuza mzigo wake BoT anapata punguzo la malipo katika mrabaha ambapo awali ilikuwa asilimia 6 na sasa ni aslimia 4 na malipo ya ada ilikuwa asilimia moja na kwa sasa ni asilimia sifuri.

Amesema muuzaji anaweza pia kuiuzia BoT asilimia 100 ya mzigo wake kupitia kwenye viwanda vya uchenjuaji wa dhahabu ambavyoni ni Geita Gold Refinery Ltd (GGR), Mwanza Preciuos Metals Co. Ltd pamoja na Eyes of Africa kilichopo Dodoma

Awali meneja mahusiano BoT Vicky Msina amesema BoT inahifadhi kinga ya fedha za kigeni kupitia ununuzi wa dhahabu ambayo inaisaidia nchi kuhifadhi fedha za kigeni kupitia hazina ya dhahabu

Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Majaliwa Kassim Majaliwa amehitimisha kwa kuzitaka taasisi za kifedha chini ya BoT kuendelea kutoa huduma kwa wachimbaji wadogo ili waweze kuwafungulia milango ya uzalishaji wenye tija zaidi.

Habari Na .yohana.jr

Imeelezwa kuwa majiko banifu yanayotolewa kwa bei ya ruzuku na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ni majiko yanayotumia k...
23/09/2025

Imeelezwa kuwa majiko banifu yanayotolewa kwa bei ya ruzuku na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ni majiko yanayotumia kiasi kidogo cha mkaa kulinganisha na majiko mengine ya mkaa.

Hayo yamebainishwa na Wataalam kutoka REA wanaoendelea kutoa elimu kwa wananchi katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Geita.

Aidha, majiko banifu yametengenezwa kwa teknolojia ya kisasa yenye uwezo wa kupunguza sumu ya mkaa (carbon monoxide) hivyo inasaidia kupunguza madhara ya kiafya yatokanayo na nishati ya mkaa.

Halikadhalika, majiko banifu yanasaidia utunzaji wa mazingira, ni rahisi kwa matumizi yanadumu kwa muda mrefu bila kupata changamoto ya kuharibika kwa watumiaji.

Katika mkoa wa Geita kampuni inayosambaza majiko banifu kwa bei ya ruzuku ni Geita Millenium Star Company Limited.

Majiko banifu yanatolewa kwa bei ya ruzuku ya shilingi 6,195 kwa kuwa Serikali imeweka ruzuku ya bei katika majiko hayo ili wananchi waweze kuyatumia na kuyapata kwa urahisi ambapo kabla ya ruzuku yalikuwa yanauzwa kwa shilingi 41,300.

Habari Na .yohana.jr

Habari picha Katika tukio la Uzinduzi wa Kampeni za Jumanne Misungwi ambaye ni Mgombea Udiwani kata ya Ludete kupitia ti...
20/09/2025

Habari picha Katika tukio la Uzinduzi wa Kampeni za Jumanne Misungwi ambaye ni Mgombea Udiwani kata ya Ludete kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM.

Mgombea Ubunge ubunge Jimbo la Katoro kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Eng. Kija Limbu Ntemi yupo katika uzinduzi huo unaofanyika viwanja vya shule ya Msingi Ludete.

Mgeni rasmi ni Nocolaus Kasendamila Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita.

Wananchi wamejitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa kampeni Jimbo la Busanda huku baadhi wakiwa na mabango yenye picha ya...
15/09/2025

Wananchi wamejitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa kampeni Jimbo la Busanda huku baadhi wakiwa na mabango yenye picha ya Mgombea Urais na ubunge kupitia chama Cha Mapinduzi CCM.

Mbali na umati huo Mkubwa pia wasanii kutoka jijini Dar es salaam Madee na Chege wametumbuiza katika uzinduzi huo wa kampeni.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Ccm Mkoa wa Geita amezindua rasmi Kampeni Katika Jimbo la Katoro.Katika uzinduzi huo a...
14/09/2025

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Ccm Mkoa wa Geita amezindua rasmi Kampeni Katika Jimbo la Katoro.

Katika uzinduzi huo amemtambilisha Mhandisi Kija Limbu Ntemi kuwa ndiyo Mgombea wa ubunge wa Jimbo hilo pamoja na kuwatambulisha wagombea udiwani wa kata 11 za Jimbo hilo.

Na mwandishi wetu

Shangwe latawala katika Viwanja vya Nyaseke Kata ya Bulela, Jimbo la Geita Mjini, Baada ya Mgombea Ubunge Jimbo hilo Mha...
14/09/2025

Shangwe latawala katika Viwanja vya Nyaseke Kata ya Bulela, Jimbo la Geita Mjini, Baada ya Mgombea Ubunge Jimbo hilo Mhandisi Chacha Mwita Wambura, kuwasili tayari kwa uzinduzi wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2025.*

*Viongozi, Wananchi na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM), wamefika katika Viwanja hivyo kushuhudia uzinduzi na kusikiliza Sera za Mgombea huyo.

Mbunge mstaafu Jimbo la Busanda, ambalo kwasasa limegawanywa na kuwa Jimbo la Katoro na Busanda, Mhandisi Tumaini Brayso...
14/09/2025

Mbunge mstaafu Jimbo la Busanda, ambalo kwasasa limegawanywa na kuwa Jimbo la Katoro na Busanda, Mhandisi Tumaini Brayson Magesa amewasili katika viunga vya soko la CCM Katoro kumuunga mkono Mgombea wa Jimbo hilo Mhandisi Kija Limbu Ntemi leo tarehe 14 Septemba 2025.

Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Geita imewaonya wanachama wake wanaoendeleza makundi yanayotokana...
12/09/2025

Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Geita imewaonya wanachama wake wanaoendeleza makundi yanayotokana na kura za maoni badala yake washik**ane kuhakikisha wagombea wateule kupitia chama hicho wanashinda kwenye uchaguzi mkuu wa oktoba 29,mwaka huu.

Onyo hilo limetolewa na mwenyekiti wa Jumuiya hiyo wilaya ya Geita, Robert Nyamaigolo alipokutana na viongozi jumuiya hiyo ngazi ya kata ikiwa ni hatua ya kuvunja makundi na kuwaunga mkono wagombea waliopitishwa na vikao halali vya ngazi ya maamuzi ndani ya chama hicho.

Amesema Chama pamoja na Jumuiya havitasita kuwachukulia hatua wanachama wake watakaobainika wanaendekeza makundi ambayo hayana mantiki katika uchaguzi huu.

Awali akimkaribisha mwennyekiti huyo kuzungumza kwenye kikao hicho, Katibu wa Jumuiya hiyo wilaya ya Geita, Ramadhan Ndago amesema lengo la kukutana ni kujadili njia nzuri itakayoleta mafanikio ya wagombea wa CCM kushinda ngazo zote Diwani, ubunge na Rais.

“Kikao hiki ni cha dharula, ni kikao muhimu sana kwenye kipindi hiki cha uchaguzi, muda wowote tunaweza kuwaita, hivyo tuvumiliane lengo ni kuhakikisha tunashik**ana tunaenda pamoja kukipambania chama chetu(CCM) na kinashinda nafasi zote” amesema Ndago.

Habari Na

Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa Takuku Mkoa wa Geita imeendesha mafunzo kwa Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ng...
11/09/2025

Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa Takuku Mkoa wa Geita imeendesha mafunzo kwa Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata, Halmashauri na Maofisa uchaguzi wa Halmashauri ya Manispaa na Wilaya ya Geita, ikiwa ni juhudi za mapambano ya vitendo vya rushwa kuelekea uchaguzi Mkuu wa oktoba 29, 2025.

Pamoja na mambo mengine wamekumbushwa Sheria na wajibu wao wakati wa kutekeleza Majukumu yao ya usimamizi wa shughuli za uchaguzi bila rushwa.

Address

BOMANI
Geita
30101

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Rubondofm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Rubondofm:

Share