Diramakini 24

Diramakini 24 Play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth

Taarifa kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
20/09/2025

Taarifa kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Benki Kuu ya Tanzania kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, huuza Dhamana za Serikali za muda mrefu ...
20/09/2025

Benki Kuu ya Tanzania kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, huuza Dhamana za Serikali za muda mrefu (Hati fungani) ikiwa ni njia ya kukopa fedha kutoka kwa ama taasisi au mwananchi mmoja mmoja.

Dhamana za muda mrefu ni zile ambazo muda wake wa kuiva unazidi mwaka mmoja. Dhamana hizi huuzwa kwenye soko la awali kwa njia ya ushindani kupitia minada na baada ya hapo uuzaji wa dhamana hizo hufanywa kwenye soko la upili.

Mwekezaji atanunua Hati fungani kupitia kwa Mawakala ambao ni benki zote za biashara zilizosajiliwa na kupatiwa leseni ya biashara na benki kutoka Benki Kuu ya Tanzania au Mawakala wa soko la Hisa la Dar-es- Salaam waliopatiwa leseni na kusimamiwa na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana.

Mwekezaji mwenye kiwango cha kuanzia shillingi milioni moja (TZS 1,000,000.00) na kuendelea anaruhusiwa kushiriki katika mnada wa Dhamana za Muda Mrefu (Hati Fungani).

Kabla ya kuwekeza, kila mwekezaji anatakiwa kufungua akaunti maalum ya uwekezaji inayoitwa Central Depository System Account (Akaunti ya CDS).

Akaunti hii ni tofauti na akaunti ya akiba kwa kuwa inatumika kutunza kumbukumbu na taarifa zote za uwekezaji.
Kufungua akaunti hii hakuna gharama yoyote, na mwekezaji atatakiwa kuwasilisha nyaraka za utambulisho k**a vile kitambulisho cha taifa (NIDA), namba ya mlipa kodi (TIN), pamoja na picha mbili ndogo za pasipoti.

Wawekezaji wa dhamana za Serikali hupata malipo ya faida mara mbili kwa mwaka, na Benki Kuu ya Tanzania hulipa moja kwa moja stahiki hizo kupitia akaunti za benki za kila mwekezaji.

TANZIA:MTUMISHI WA MAHAKAMA KUU KANDA YA MWANZA AFARIKI DUNIA MWANZA-Mahak**a Kuu Kanda ya Mwanza inasikitika kutangaza ...
19/09/2025

TANZIA:MTUMISHI WA MAHAKAMA KUU KANDA YA MWANZA AFARIKI DUNIA 

MWANZA-Mahak**a Kuu Kanda ya Mwanza inasikitika kutangaza kifo cha mtumishi wake, Bi.Febronia John Mayala ambaye alikuwa Msaidizi wa Kumbukumbu daraja la I kilichotokea mnamo tarehe 16 Agosti 2025 katika hospitali ya Kamanga Wilaya ya Nyamagana Mkoa wa Mwanza

Kwa mujibu wa Mtendaji wa Mahak**a Kuu Kanda ya Mwanza Bw. Tutubi Mangazeni marehemu Bi. Febronia aliajiriwa mnamo tarehe 21 Septemba, 2015 katika kada ya Msaidizi wa Kumbukumbu II.

Baada ya kuajiriwa alipangiwa Kituo chake cha kwanza cha kazi cha ajira huko Mahak**a ya Wilaya Sengerema na baada ya hapo akahamishiwa Mwanza IJC ambapo alipangiwa Mahak**a ya Wilaya Ilemela na baadaye kuhamishiwa Mahak**a ya Hakimu Mkazi mpaka umauti ulipomfika

Ameajiriwa na elimu ya Stashahada ya utunzaji wa kumbukumbu (Diploma in Record Management) katika Chuo cha Utumishi wa Umma tawi la Tabora

Marehemu Bi. Febronia anatarajiwa kuzikwa Mwanza katika makaburi ya Buhongwa leo tarehe 19 Septemba, 2025.

Bwana ametoa na Bwana ametwaa Jina la Bwana Lihimidiwe.

Vikombe sita,Medali 63:TAKUKURU yafunika SHIMIWI 2025DODOMA-Zawadi zimewasilishwa kwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU zikiju...
19/09/2025

Vikombe sita,Medali 63:TAKUKURU yafunika SHIMIWI 2025

DODOMA-Zawadi zimewasilishwa kwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU zikijumuisha Kombe la Ushindi wa Jumla wa Mashindano, Ushindi wa Jumla wa Riadha, Kombe la Kwanza la Mbio za Baiskeli, pamoja na makombe ya Pili kwa mchezo wa Kuvuta Kamba (wanaume na wanawake) na Kombe la Tatu kwa Mpira wa Miguu. 

Aidha, timu hiyo ilijinyakulia medali 10 za dhahabu katika mbio mbalimbali za riadha na baiskeli, medali 30 za fedha katika kuvuta kamba, na medali 23 za shaba katika mpira wa miguu. 

Ushindi huo umetajwa kuipa heshima na kuitangaza vyema TAKUKURU kupitia vyombo vya habari, huku wanamichezo 63 wakishiriki michezo ya riadha, kuvuta kamba, mpira wa miguu na michezo ya jadi tangu kuanza kwa mashindano hayo Septemba 1, 2025| https://www.diramakini.co.tz/2025/09/vikombe-sitamedali-63takukuru-yafunika.html

Naibu Gavana wa Sera za Uchumi na Fedha wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt.Yamungu Kayandabila, amekutana na kufanya ma...
18/09/2025

Naibu Gavana wa Sera za Uchumi na Fedha wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt.Yamungu Kayandabila, amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Tume ya Taifa ya Mipango ulioongozwa na Naibu Katibu Mtendaji anayeshughulikia Mipango ya Kitaifa, Dkt.Mursali Milanzi, tarehe 18 Septemba 2025 katika ofisi za BoT jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo yalijikita katika kujadili mikakati mbalimbali ya kugharamia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, inayolenga kuifanya Tanzania kuwa taifa lenye maendeleo yanayolingana na nchi zenye uchumi wa kipato cha ngazi ya juu au zaidi.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Naibu Gavana wa Uthabiti na Usimamizi wa Sekta ya Fedha, Bi. Sauda Msemo, pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. Sosthenes Kewe, na viongozi wengine wa Benki Kuu.

TCB Stawi Bond yazinduliwa rasmi,wawekezaji kupata faida asilimia 13.5 kwa mwakaNA GODFREY NNKOBENKI ya Biashara Tanzani...
17/09/2025

TCB Stawi Bond yazinduliwa rasmi,wawekezaji kupata faida asilimia 13.5 kwa mwaka

NA GODFREY NNKO

BENKI ya Biashara Tanzania (TCB) imezindua rasmi Hatifungani ya TCB Stawi Bond ambayo inampatia mwekezaji faida ya mpaka asilimia 13.5 kwa mwaka, inayolipwa kila robo mwaka.

Uzinduzi huo umefanyika leo Septemba 17,2025 jijini Dar es Salaam ukiongozwa na mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw.Elijah Mwandumbya kwa niaba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt.Doto Biteko.

Hatua hiyo imefikiwa, baada ya Mamlaka ya Mitaji na Masoko ya Dhamana (CMSA) kuidhinisha waraka wa matarajio wa programu ya miaka mitano ya hatifungani hiyo yenye jumla ya shilingi bilioni 150.

Pia, katika toleo la kwanza CMSA imeidhinisha TCB Stawi Bond yenye jumla ya shilingi bilioni 50 huku kiwango cha chini cha kuwekeza ikiwa ni shilingi 500,000 https://www.diramakini.co.tz/2025/09/tcb-stawi-bond-yanduliwa-rasmi.html

Kutana na maajabu ya mchanga unaooshwa TangaTANGA-Sekta ya Madini nchini inaendelea kushuhudia mageuzi ya kuongeza thama...
17/09/2025

Kutana na maajabu ya mchanga unaooshwa Tanga

TANGA-Sekta ya Madini nchini inaendelea kushuhudia mageuzi ya kuongeza thamani madini yakiwemo ya ujenzi k**a mchanga na kufungua fursa nyingine mpya kwa wachimbaji wadogo wa mchanga kupitia teknolojia bunifu za usindikaji. 

Katika mkoa wa Tanga, Kampuni ya Muwa Trading Tanzania Limited imewekeza kwenye Kiwanda cha kuosha na kusafisha mchanga kwa maji ili kuondoa udongo na uchafu mwingine k**a mizizi, hatua ambayo imebadilisha kabisa mtazamo wa thamani ya rasilimali hiyo kwa miaka mingi.

“Mchanga unaosafishwa kiwandani hapa umetumika katika miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo ukarabati wa Bandari ya Tanga, ujenzi wa baadhi ya viwanda mkoani hapa, pamoja na utekelezaji wa bomba la mafuta ghafi kutoka Chongeleani,Tanga.

Hatua hii si tu kwamba imerahisisha upatikanaji wa malighafi zenye ubora, bali pia imefungua soko jipya kwa wachimbaji na wafanyabiashara wa mchanga https://www.diramakini.co.tz/2025/09/kutana-na-maajabu-ya-mchanga-unaooshwa.html

Ni Young Africans Sports Club (Yanga SC) ikitwaa Ngao ya Jamii 2025 dhidi ya watani zao Simba Sports Club (Simba SC) leo...
16/09/2025

Ni Young Africans Sports Club (Yanga SC) ikitwaa Ngao ya Jamii 2025 dhidi ya watani zao Simba Sports Club (Simba SC) leo Septemba 16,2025 katika Dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

RC CHALAMILA ATEMBELEA SOKO LA KAWE AMBALO LIMEUNGUA KWA MOTODAR-Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mheshimiwa Albert Chalami...
16/09/2025

RC CHALAMILA ATEMBELEA SOKO LA KAWE AMBALO LIMEUNGUA KWA MOTO

DAR-Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mheshimiwa Albert Chalamila ametembelea soko la Kawe ambalo limeungua moto usiku wa kuamkia leo Septemba 15,2025 kuwafariji wafanyabiashara waliopoteza mali zao kutokana na ajali hiyo ambapo ameelekeza Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kutoa kiasi cha shilingi milioni miamoja k**a mkono wa pole

Akizungumza mara baada ya kutembelea soko hilo lililoteketea kwa moto kwenye eneo la kawe jijini Dar es aalaam RC Chalamila pamoja na kufikisha salam za pole kutoka kwa Rais Dkt.Samia amesema soko hilo sasa litajengwa na Serikali kwa ubora na kwa haraka ili wafanyabiashara waendelee na biashara na kwamba kwa sasa wafanyabiashara wapelekwe eneo la viwanja vya shirika la nyumba NHC Tanganyika Perkas

Aidha, RC Chalamila ameelekeza kuandaliwa takwimu za wafanyabiashara kwenye masoko yote ili yanapotokea majanga kuwe na takwimu sahihi za waathirika ambapo kwa soko hilo la Kawe kulikua na takribani wafanyabiashara elfu moja walioathitika hivyo ametaka Manispaa ya kinondoni kutoa milioni miamoja ya pole mapema Septemba 16, 2025

Kwa upande wake Katibu wa wafanyabiashara wa soko la Kawe,Silvester Chidego ameshukuru Serikali kwa kutoa faraja kwa wafanyabiashara na kwamba fedha hizo milioni miamoja watazigawa kwa wafanyabiashara wote huku mmoja wa wazee wafanyabiashara wa soko hilo akiomba wadau kujitokeza kuwawezesha wafanyabiashara huku akitoa tahadhari kwa vibaka walioiba bidhaa za wafanyabiashara kuwa kuna dua maalum itasomwa

Soko hilo la kawe limeungua usiku wa Septemba 15, 2025 hivyo kuamkia Septemba 16, 2025 RC Chalamila ameagiza k**ati ya kuchunguza chanzo cha moto huo iwe imeundwa na ifanye kazi yake mara moja.

Address

Ilala
12101

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Diramakini 24 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Diramakini 24:

Share