Diramakini 24

Diramakini 24 Play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth

Zimebaki Siku 9:Kuelekea miaka 60 ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
03/06/2026

Zimebaki Siku 9:Kuelekea miaka 60 ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

9 Days Left:Towards 60 Years of the Bank of Tanzania (BoT).
03/06/2026

9 Days Left:Towards 60 Years of the Bank of Tanzania (BoT).

TMA:Utabiri wa hali ya hewa Tanzania saa 24 zijazo kwa Juni 4,2026.
03/06/2026

TMA:Utabiri wa hali ya hewa Tanzania saa 24 zijazo kwa Juni 4,2026.

TMA:Weather forecast for the next 24 hours for June 4th,2026.
03/06/2026

TMA:Weather forecast for the next 24 hours for June 4th,2026.

Mbolea ipo ya kutosha nchini-Waziri ChongoloNA GODFREY NNKOSERIKALI kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA...
03/06/2026

Mbolea ipo ya kutosha nchini-Waziri Chongolo

NA GODFREY NNKO

SERIKALI kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) imewahakikishia wakulima uwepo wa mbolea ya kutosha nchini na itahakikisha inapatikana msimu wote ili waweze kuzalisha mazao ya kutosha.

Hayo yamesemwa leo Juni 3,2026 jijini Dar es Salaam na Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Daniel Chongolo baada ya kufanya ziara ya kukagua maghala ya mbolea ya waagizaji,wazalishaji na wasambazaji wakubwa ikiwemo Kampuni ya ETG,Yara na OCP.

Amesema, lengo la ziara yake hiyo ni kujiridhisha k**a uwepo wa mbolea upo sawa, ambapo ameshuhudia hifadhi kubwa ya mbolea huku ikiendelea kupakiwa kwa ajili ya kusambazwa kwenda maeneo ya mikoa mbalimbali nchini.

“Kwa hiyo, kwanza tumekuja kuwathibitishia wananchi na watanzania kwamba hofu kwamba labda mbolea hamna hayo yalikuwa mashaka tu na yasiyo na sababu.Mbolea nchini ipo, na sasa hivi tupo low season ya kilimo na ndiyo tunafika mwisho, maeneo makubwa ambayo yanaendesha kilimo kwa sasa ndiyo yapo kwenye mavuno.

“Lakini, yako maeneo k**a ya Kilimanjaro, Arusha na sehemu za Manyara sasa hivi wako katikati ya msimu wa kilimo na tumefuatilia kujiridhisha kule mbolea inayohitajika zaidi ni Urea kwa ajili ya kukuzia,hapa wamesema wenyewe na mmesikia mbolea ipo na leo wametoa gari mbili zimepeleka mbolea Kilimanjaro.”

Waziri Chongolo amewahakikishia wananchi kuwa, mbolea ya kutosha kwa ajili ya hatua zote za kilimo nchini ipo ya kutosha na wataendelea kuhakikisha msimu wote wa kilimo inapatikana.

Vilevile amesema kuwa, Serikali itaendelea kutoa mbolea ya ruzuku kwa sababu kumekuwa na changamoto huko duniani ambayo imeathiri mifumo ya usambazaji huku ikiathiri mataifa mengi.

Amesema, maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha wakulima hawakosi pembejeo na hilo wanalisimamia na kulitekeleza kwa ufanisi mkubwa kote nchini.

Pia, amesema waagizaji zaidi ya 18 wa mbolea nchini wana hifadhi ya kutosha ambayo inatoa uhakika wa mbolea ya kutosha hapa nchini.

Waziri Chongolo, pia amewaomba wakulima nchini kuwa watulivu kwani tayari Wizara ya Kilimo imepeleka timu nchi nzima ambayo inafanya tathimini ya mbolea iliyopo.

Dkt.Jingu apongeza ushirikiano wa Wizara ya Katiba na Sheria na Jeshi la Magereza katika kuimarisha upatikanaji wa hakiN...
03/06/2026

Dkt.Jingu apongeza ushirikiano wa Wizara ya Katiba na Sheria na Jeshi la Magereza katika kuimarisha upatikanaji wa haki

NA SSGT MAWAZO MTONDO

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. John Jingu, amepongeza ushirikiano imara uliopo kati ya Wizara ya Katiba na Sheria na Jeshi la Magereza katika kuimarisha upatikanaji wa haki na huduma za msaada wa kisheria kwa Wafungwa na mahabusu kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za nchi.

Dkt. Jingu amesema kuwa, Wizara ya Katiba na Sheria  itaendelea kushirikiana kwa karibu na Jeshi la Magereza katika maeneo mbalimbali, ikiwemo kuwajengea uwezo wataalamu wa sheria, kuimarisha utekelezaji wa vifungo mbadala, utoaji haki pamoja na kuboresha mifumo ya ukusanyaji, uchambuzi na uwasilishaji wa taarifa zinazohusu huduma za msaada wa kisheria na ufuatiliaji wa haki za wafungwa na mahabusu.

Amesisitiza kuwa, lengo la Serikali ni kuhakikisha Magereza yanabaki kuhifadhi wale tu wanaostahili kuwepo kwa mujibu wa sheria, na kutumia ipasavyo fursa nyingine za kisheria kwa wanufaika wanaostahili ili kupunguza msongamano magerezani.

Dkt. Jingu alitoa kauli hiyo leo Juni 3, 2026, katika ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Katiba na Sheria uliopo Mtumba, Jijini Dodoma, wakati wa kikao cha pamoja kati ya viongozi wa Wizara hiyo na Jeshi la Magereza kilicholenga kujadili na kuimarisha ushirikiano katika masuala ya utoaji haki na huduma za msaada wa kisheria magerezani.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkuu wa Jeshi la Magereza, CGP Jeremiah Yoram Katungu, amesema ushirikiano kati ya Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na Jeshi la Magereza ni nguzo muhimu katika kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya taasisi hizo na kufikia malengo ya Serikali ya kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi.

Ameeleza kuwa, maeneo ya ushirikiano yanajumuisha utoaji wa mafunzo kwa maafisa wa sheria, uimarishaji wa huduma za msaada wa kisheria kwa wafungwa na mahabusu, pamoja na kushughulikia changamoto mbalimbali za kisheria zinazowakabili watu waliopo magerezani.

CGP Katungu amesema kuwa, Jeshi la Magereza linaendelea kutekeleza kwa mafanikio mfumo wa Mahak**a Mtandao unaowezesha baadhi ya mashauri kusikilizwa kwa wafungwa na mahabusu wakiwa ndani...

Naibu Waziri ahimiza ushirikiano kusambaza taarifa za hali ya hewa kwa wananchi wa vijijini DODOMA-Naibu Waziri wa Nchi,...
03/06/2026

Naibu Waziri ahimiza ushirikiano kusambaza taarifa za hali ya hewa kwa wananchi wa vijijini 

DODOMA-Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Reuben Nhamanilo Kwagilwa, ameitaka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kuendelea kuimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali ili kuhakikisha taarifa za hali ya hewa zinawafikia wananchi wote, hususan wanaoishi katika maeneo ya vijijini na maeneo ya mbali yanayokabiliwa na changamoto za upatikanaji wa huduma za mawasiliano.

Mhe. Kwagilwa ameyasema hayo alipotembelea banda la TMA wakati wa Ufunguzi wa Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani 2026 yanayofanyika kuanzia tarehe 1 hadi 5 Juni 2026 katika Viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Centre (JKCC), jijini Dodoma, chini ya kauli mbiu isemayo "Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania"

Akizungumza na wataalamu wa TMA, Mhe. Kwagilwa ameipongeza mamlaka hiyo kwa kazi kubwa inayoendelea kufanya katika utoaji wa huduma za hali ya hewa na kusisitiza umuhimu wa kuhakikisha taarifa hizo zinawafikia wananchi wanaozitegemea katika shughuli zao za kila siku, hususan sekta ya kilimo.

“Nawapongeza kwa kazi nzuri mnayoifanya na tunaona matokeo yake. Hata hivyo, kuna umuhimu wa kuhakikisha taarifa hizi zinawafikia wananchi waliopo kwenye maeneo ya mbali ambao wanategemea utabiri wa hali ya hewa katika shughuli zao za kimsimu, hasa kilimo,” amesema Mhe. Kwagilwa.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya TMA na Vituo vya Kijamii vya Uhimilivu dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi (CCCRC) ili vituo hivyo viwe daraja muhimu la kufikisha taarifa za hali ya hewa kwa wananchi ngazi ya jamii na kuwawezesha kupata taarifa sahihi zinazohusu maeneo yao pamoja na mwongozo wa hatua stahiki za kuchukua katika misimu mbalimbali.

Ushiriki wa TMA katika maonesho hayo ni sehemu ya juhudi za Mamlaka  kuendelea kusogeza huduma za hali ya hewa kwa wananchi, kuongeza uelewa wa matumizi ya taarifa za hali ya hewa katika sekta mbalimbali za maendeleo na kuimarisha ushirikiano na wadau

TMA inawakaribisha wananchi, wadau wa mazingira, watafiti, wanafunzi na washiriki wote wa maonesho hayo kutembelea banda la TMA  ili kujifunza zaidi kuhusu huduma.

EWURA yatangaza bei ya mafuta Juni 2026,nafuu kidogo kwa Petroli NA DIRAMAKINI MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati ...
02/06/2026

EWURA yatangaza bei ya mafuta Juni 2026,nafuu kidogo kwa Petroli

NA DIRAMAKINI 

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza bei kikomo za mafuta ya petroli nchini kuanzia Juni 3, 2026 huku zikiendelea kupanda, ikieleza kuwa hali hiyo imesababishwa kwa kiasi kikubwa na vita vinavyoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati pamoja na kuvurugika kwa usafirishaji wa mafuta duniani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na EWURA, mgogoro ulioanza Februari 28, 2026 ukizihusisha Marekani, Israel na Iran umeathiri miundombinu muhimu ya uzalishaji, uhifadhi na usafishaji wa mafuta, hali iliyosababisha kupungua kwa upatikanaji wa mafuta katika soko la dunia na kuongezeka kwa bei za bidhaa hizo.

EWURA imeeleza kuwa,hali hiyo imechangiwa zaidi na kufungwa kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz, njia inayopitisha takribani asilimia 20 ya mafuta yote yanayosafirishwa duniani. 

Kufungwa kwa njia hiyo kumesababisha ongezeko la gharama za usafirishaji, bima za meli za mafuta pamoja na ucheleweshaji wa mizigo, jambo ambalo limeongeza shinikizo la bei katika soko la kimataifa.

Tanzania, ambayo huagiza sehemu kubwa ya mafuta yake kutoka Mashariki ya Kati, imeathirika moja kwa moja na mabadiliko hayo ya kimataifa.

Katika hatua ya kupunguza athari kwa wananchi na uchumi wa nchi, Serikali imeendelea kutoa ruzuku ya takribani shilingi 534.91 kwa kila lita moja ya dizeli ili kusaidia kudhibiti ongezeko kubwa zaidi la bei za mafuta hayo yanayotumika katika sekta za usafirishaji, uzalishaji viwandani na huduma mbalimbali za kijamii.

Kwa mujibu wa bei mpya zilizotangazwa, mafuta ya petroli katika Jiji la Dar es Salaam yatauzwa kwa bei isiyozidi shilingi 4,086 kwa lita, huku dizeli ikiuzwa kwa shilingi 4,333 na mafuta ya taa kwa shilingi 4,685 kwa lita.

Katika Bandari ya Tanga, petroli itauzwa kwa shilingi 4,157 kwa lita, dizeli shilingi 4,404 na mafuta ya taa shilingi 4,756 kwa lita. 

Kwa upande wa Mtwara, petroli itauzwa kwa shilingi 4,193 kwa lita, dizeli shilingi 4,440 na mafuta ya taa shilingi 4,792 kwa lita.

Ikumbukwe kwa mwezi Mei 2026, bei kikomo za rejareja katika mikoa ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara zilikuwa k**a ifuatavyo...

Serikali kuimarisha mifumo ya usimamizi wa maafa MOROGORO-Serikali imeendelea kuimarisha mifumo ya uratibu, kujiandaa na...
02/06/2026

Serikali kuimarisha mifumo ya usimamizi wa maafa 

MOROGORO-Serikali imeendelea kuimarisha mifumo ya uratibu, kujiandaa na kukabiliana na maafa ili kuhakikisha misaada ya kibinadamu inayotolewa inawafikia walengwa kwa wakati, ufanisi na kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.

Hayo yameelezwa leo Juni 2, 2026 na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Kanali Selestine Masalamado, wakati wa ufunguzi wa warsha ya zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wakati wa dharura, mkoani Morogoro.

Amesema utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wa dharura ni nguzo muhimu zinazowezesha kuokoa maisha ya wananchi walioathiriwa na maafa, kupunguza mateso ya waathirika na kuharakisha urejeshaji wa hali za kawaida katika maeneo yaliyoathirika.

“Kwa kutambua umuhimu huo, Serikali imeendelea kuimarisha mifumo ya uratibu, kujiandaa na kukabiliana na maafa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha misaada inawafikia walengwa kwa wakati, ufanisi na kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya utoaji wa huduma za kibinadamu,”amesema.

Vilevile, amelishukuru Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), washirika wote waliohusika katika utekelezaji wa Mradi wa Field-Based Preparedness Project (FBPP), ambapo katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, mradi huo umechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha uwezo wa taifa katika sekta ya utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji.

Amesema Tanzania imefanikiwa kuanzisha Kikosi Kazi cha Kitaifa cha Uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wa dharura mwezi Julai 2025, ambacho kimekuwa jukwaa muhimu la uratibu na ushirikiano baina ya taasisi za serikali na wadau wa kibinadamu.

“Zoezi hili la uigaji limeandaliwa k**a jukwaa la kitaifa la kujifunza, kupima na kuboresha mifumo yetu ya uratibu wa shughuli za usafirishaji na utoaji wa misaada ya kibinadamu,”alieleza.

Katika hatua nyingine, Kanali Masalamado amesisitiza umuhimu wa kuendelea kujumuisha masuala ya uhifadhi wa mazingira na ustahimilivu wa tabianchi katika mipango na shughuli za usafirishaji wa misaada ya kibinadamu.

Dkt.Kiruswa akutana na Balozi wa Australia anayemaliza muda wake nchini Tanzania DODOMA-Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Ste...
02/06/2026

Dkt.Kiruswa akutana na Balozi wa Australia anayemaliza muda wake nchini Tanzania 

DODOMA-Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, leo tarehe 2 Juni, 2026 amekutana na Balozi wa Australia nchini Tanzania anayemaliza muda wake wa uwakilishi, Mhe. Jenny Da Rin, kwa mazungumzo ya kumuaga yaliyofanyika jijini Dodoma.

Katika mazungumzo hayo, Dkt. Kiruswa amempongeza Mhe. Jenny Da Rin kwa kumaliza muda wake wa uwakilishi nchini kwa mafanikio makubwa, huku akitambua mchango wake katika kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Australia, hususan katika maendeleo ya Sekta ya Madini.

Amesema Tanzania na Australia zimeendelea kushirikiana katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ambayo imekuwa na matokeo chanya katika kukuza sekta ya madini na kuchangia maendeleo ya uchumi wa Taifa kwa ujumla.

Dkt. Kiruswa ameeleza kuwa Serikali ya Tanzania imeendelea kuhakikisha wananchi wanapata manufaa ya rasilimali madini kwa kuwashirikisha kikamilifu katika shughuli za madini, huku ikitambua mchango wa wawekezaji wa kimataifa, wakiwemo kutoka Australia, katika maendeleo ya sekta hiyo.

Aidha, amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuimarisha ushirikiano na Australia katika maeneo ya utafiti wa madini, uwekezaji, uhamishaji wa teknolojia na maendeleo ya rasilimali watu ili kuongeza uzalishaji na kuifanya sekta ya madini kuwa na tija zaidi kwa Taifa.

“Sekta ya madini inaendelea kukua kwa kasi na inahitaji uwekezaji wa kutosha katika teknolojia, ujuzi na tafiti ili kuongeza uzalishaji na manufaa ya kiuchumi kwa wananchi na Taifa kwa ujumla,” amesema Dkt. Kiruswa.

Kwa upande wake, Mhe. Jenny Da Rin ameishukuru Serikali ya Tanzania na Wizara ya Madini kwa ushirikiano mkubwa alioupata katika kipindi chote cha utumishi wake nchini.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa Watanzania kutumia kikamilifu fursa za elimu, mafunzo na semina zinazotolewa na Australia, akibainisha kuwa maarifa na ujuzi unaopatikana kupitia programu hizo unachangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya sekta mbalimbali, ikiwemo Sekta ya Madini.

Mhe. Jenny Da Rin ameongeza kuwa moja ya malengo ya ushirikiano kati ya Tanzania na Australia ni kuhamasisha wawekezaji na wafanyabiashara wa Australia kuja kuwekeza nchini Tanzania.

Address

Ilala
12101

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Diramakini 24 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Diramakini 24:

Share