Diramakini 24

Diramakini 24 Play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth

Watumishi Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) wajengewa uwezo kuhusu Mfumo wa Usimamizi wa UboraDAR-Ofisi ya Msajili wa Haz...
04/09/2026

Watumishi Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) wajengewa uwezo kuhusu Mfumo wa Usimamizi wa Ubora

DAR-Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) imeendelea na hatua za kuimarisha mifumo yake ya utendaji kwa kuwajengea uwezo watumishi kuhusu Mfumo wa Usimamizi wa Ubora (Quality Management System-QMS), unaolenga kuiwezesha taasisi kufikia viwango vya kimataifa vya ubora.

Mafunzo hayo yametolewa leo Septemba 4, 2026 jijini Dar es Salaam na kampuni ya Amaxon,ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya OTR kuelekea kupata ithibati ya ubora kimataifa (ISO 9001:2015), ambayo inaweka viwango vya kimataifa vya usimamizi wa ubora katika taasisi na mashirika.

Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Msajili wa Hazina,Bi. Lightness Mauki ambaye ni Mkurugenzi wa Usimamizi wa Utendaji wa Taasisi za Kibiashara amesema,utekelezaji wa QMS utasaidia OTR kuimarisha mifumo ya kazi, kuongeza ufanisi na kuhakikisha huduma zinazotolewa zinazingatia mahitaji ya wadau.

“Tunataka kutambulika kimataifa k**a taasisi inayofuata viwango vya ubora wa kimataifa katika utoaji wa huduma,”amesema Bi. Mauki.

Amesema, kufikia kiwango hicho kunahitaji ushiriki wa watumishi wote na utekelezaji wa taratibu zinazoweka wazi namna kazi zinavyopaswa kufanyika, kufuatiliwa na kutathminiwa.

Mafunzo kwa watumishi hao yametanguliwa na programu ya wiki moja ya kuwajengea uwezo QMS Champions kutoka kila idara na kitengo cha OTR, iliyowapa ujuzi kuhusu matumizi ya misingi ya usimamizi wa ubora katika shughuli za kila siku, pamoja na namna ya kufanya ukaguzi wa ndani wa mifumo ya kazi.

QMS Champions hao wanatarajiwa kuwa na nafasi muhimu katika kuhamasisha na kusaidia utekelezaji wa QMS katika maeneo mbalimbali ya kazi, ili kuhakikisha mfumo huo unaeleweka na unatekelezwa ipasavyo katika shughuli za taasisi.

Sheria ya Vipimo ni rafiki kwa wote,muuzaji na mnunuzi-WMA MWANZA-Wakala wa Vipimo (WMA) umesisitiza kuwa ni rafiki wa m...
04/09/2026

Sheria ya Vipimo ni rafiki kwa wote,muuzaji na mnunuzi-WMA

MWANZA-Wakala wa Vipimo (WMA) umesisitiza kuwa ni rafiki wa muuzaji na mnunuzi na kwamba sheria ya vipimo haikuundwa kuwakomoa wafanyabiashara bali kuwasaidia kufanya biashara ya haki.

Kauli hiyo imetolewa leo Septemba 4, 2026 katika Siku ya Nane ya Maonesho ya 21 ya Biashara ya Afrika Mashariki yanayoendelea katika Uwanja wa Furahisha jijini Mwanza.

Wakiizungumza kwa nyakati tofauti na wageni waliotembelea banda la WMA, Wataalamu wa Wakala wamesema lengo la uhakiki wa vifaa vya vipimo ni kulinda pande zote mbili.

"Muuzaji akitumia kipimo sahihi anajenga imani kwa mteja wake na kupata soko la uhakika. Na mlaji naye anapata thamani kamili ya fedha yake. Hapa hakuna mshindi na mshindwa. Sheria ya Vipimo ni msaada, sio adhabu" wamewaeleza wananchi.

Katika siku ya nane ya maonesho hayo, banda la WMA limeendelea kuwa kivutio kwa wafanyabiashara, wazalishaji na wananchi wa kawaida ambapo Wataalamu wameendelea kutoa elimu ya vipimo hususan jinsi ya kutambua vipimo halali pamoja na umuhimu wa kuhakiki vipimo mbalimbali ili kuepuka hasara katika biashara.

WMA imesema ushiriki wake katika maonesho hayo ni sehemu ya mkakati wa kusogezwa kwa huduma kwa umma na kusikiliza changamoto za moja kwa moja kutoka kwa wadau.

Wakala wa Vipimo umewahakikishia wananchi kuwa unaendelea kutoa huduma za uhakiki wa haraka katika Ofisi zao zilizopo mikoa yote ya Tanzania Bara na umewakaribisha kuendelea kutembelea banda lao katika Maonesho hayo hadi Septemba 6, 2026 yatakapofungwa.

Zanzibar yazindua Mwongozo wa Mawasiliano kati ya Mzazi na Mtoto ZANZIBAR-Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwa kushiri...
04/09/2026

Zanzibar yazindua Mwongozo wa Mawasiliano kati ya Mzazi na Mtoto 

ZANZIBAR-Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) imezindua rasmi Mwongozo wa Mawasiliano kati ya Mzazi na Mtoto kuhusu Haki ya Afya ya Uzazi (PCC Toolkit), unaolenga kuimarisha malezi, mawasiliano, ulinzi na ustawi wa watoto na vijana.

Uzinduzi wa mwongozo huo umefanyika jana katika Hoteli ya Verde na kuzinduliwa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Zawadi Amour Nassor kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo, Anna Athanas Paul.

Akizungumza katika hafla hiyo, Zawadi alisema wazazi na walezi wanapaswa kuvunja ukimya katika kujadili masuala ya afya ya uzazi na watoto wao kwa kutumia lugha sahihi, yenye heshima na inayozingatia umri wa mtoto.

Alisema,watoto na vijana wanahitaji kupata taarifa sahihi zinazolingana na umri wao ili kuwasaidia kuelewa mabadiliko wanayopitia, kutambua hatari, kujilinda dhidi ya ukatili na kufanya maamuzi sahihi kuhusu maisha yao.

“Tunapozungumzia afya ya uzazi, hatuzungumzi tu masuala ya kibaolojia, bali pia malezi, maadili, mahusiano yenye heshima, usalama wa mtoto na uwezo wa kusema ‘hapana’ pale inapohitajika,”alisema.

Alisema,wazazi wengi wamekuwa wakihofia kuanzisha mazungumzo hayo, huku watoto wakishindwa kuuliza maswali kwa hofu ya kukemewa au kudhalilishwa, hali inayowafanya baadhi yao kutafuta taarifa zisizo sahihi kutoka kwa marafiki na mitandao ya kijamii.

“Ukimya hauondoi changamoto, bali huacha nafasi kwa upotoshaji,” alisema, akibainisha kuwa PCC Toolkit itawasaidia wazazi kuzungumza na watoto wao kwa uwazi, kusikiliza bila kutoa hukumu na kujenga mazingira ya kuaminiana.

Aidha, alisema utekelezaji wa muongozo huo unahitaji ushirikiano wa Serikali, UNESCO, mashirika ya kiraia, wazazi, walimu, viongozi wa dini na vijana wenyewe, huku akiipongeza UNESCO na wadau mbalimbali, wakiwemo Katibu Mkuu Abeda Rashid Abdallah, Mkurugenzi na Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Watoto Mohamed Jabir, kwa kuchangia maandalizi ya muongozo huo.

Kwa upande wa Umoja wa Mataifa...Soma habari hii kwa kina katika tovuti ya DIRAMAKINI.

TMA:Weather forecast for the next 24 hours for September 5th,2026.
04/09/2026

TMA:Weather forecast for the next 24 hours for September 5th,2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan leo Septemba 4,2026 amefanya uteuzi wa viong...
04/09/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan leo Septemba 4,2026 amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali k**a ifuatavyo...

TMA:Utabiri wa hali ya hewa Tanzania saa 24 zijazo kwa Septemba 5,2026.
04/09/2026

TMA:Utabiri wa hali ya hewa Tanzania saa 24 zijazo kwa Septemba 5,2026.

Mradi wa Maji wa Miji 28:Serikali yafikisha maji Mangaka kwa asilimia 100MTWARA-Hatimaye mji wa Mangaka unaenda kunufaik...
04/09/2026

Mradi wa Maji wa Miji 28:Serikali yafikisha maji Mangaka kwa asilimia 100

MTWARA-Hatimaye mji wa Mangaka unaenda kunufaika na mradi wa maji wa mji 28 uliofanikishwa na Serikali ambapo hali ya upatikanaji wa maji kwa wananchi itakuwa asilimia 100.

Mradi huo ni mahsusi katika kuongeza uzalishaji na kusambaza maji katika mji wa Mangaka na maeneo ya vijijini vya wilaya ya Nanyumbu yanayopitiwa na bomba kuu hivyo kuondoa kabisa changamoto ya upatikanaji wa maji. 

Mradi una uwezo wa kuzalisha maji lita milioni tano (5,000,000) kwa siku na kuhudumia wakazi wapatao 81,000 walioko Nanyumbu mjini na vijiji vinavyopitiwa na bomba kuu. Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji inakuwa asilimia 100 katika mji wa Mangaka.

Thamani ya mradi wa miji 28 Mangaka ni takriban Dola za Marekani USD 16,380,000.59 na Serikali tayari imelipa Dola za Marekani USD 13,497,058.48.

Hivi sasa utekelezaji wa mradi umefika asilimia 96 na kwa kazi zifuatazo. SOMA habari hii kwa kina katika tovuti ya DIRAMAKINI.

Rais wa Somaliland aelekea Marekani katika ziara yake ya kwanza rasmi,huku kampeni ya kutambuliwa kimataifa ikiendeleaNA...
04/09/2026

Rais wa Somaliland aelekea Marekani katika ziara yake ya kwanza rasmi,huku kampeni ya kutambuliwa kimataifa ikiendelea

NA DIRAMAKINI 

RAIS wa Somaliland, Abdirahman Mohamed Abdullahi Irro ameondoka nchini humo kuelekea Marekani kwa ziara yake ya kwanza rasmi ya kikazi tangu aingie madarakani, wakati Serikali ya Hargeisa ikiimarisha juhudi zake za kidiplomasia kutafuta kutambuliwa zaidi kimataifa.

Kwa mujibu wa Ofisi ya Rais wa Somaliland, Irro atasafiri kuelekea Marekani kupitia Falme za Kiarabu (UAE). Hata hivyo, ofisi hiyo haikutoa taarifa kuhusu muda ambao rais huyo atatumia nchini Marekani wala kufafanua kwa kina viongozi, taasisi au maofisa atakaokutana nao wakati wa ziara hiyo.

Ziara hiyo inatajwa na Hargeisa kuwa sehemu muhimu ya juhudi za kuimarisha uhusiano wake na Washington, sambamba na kupanua ushirikiano katika masuala ya usalama na maendeleo ya kiuchumi.

Aidha, Rais Irro anatarajiwa kutumia fursa hiyo kuhamasisha uwekezaji wa kigeni katika Somaliland na kusukuma mbele ajenda ya muda mrefu ya eneo hilo ya kutaka kutambuliwa rasmi k**a taifa huru na jumuiya ya kimataifa.

Taarifa zilizowahi kuchapishwa na Horn Diplomat zilieleza kuwa, Rais Irro anatarajiwa kufanya mazungumzo mjini Washington na New York, yakiwahusisha baadhi ya wajumbe wa Bunge la Marekani pamoja na maofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani. 

Hata hivyo, wakati wa maandalizi ya ziara hiyo, hakukuwa na uthibitisho rasmi kuhusu uwezekano wa kukutana na Rais wa Marekani, Donald Trump.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, ziara hiyo inalenga kujenga juu ya msukumo mpya wa kidiplomasia uliotokana na hatua ya Israel kuitambua Somaliland, huku Hargeisa ikitarajiwa kutumia mazungumzo hayo kuishawishi Marekani na mataifa mengine kuanzisha uhusiano rasmi na Somaliland.

Israel yaitambua Somaliland

Ziara ya Irro nchini Marekani inafanyika wakati mazingira ya kidiplomasia yanayozunguka Somaliland yakitarajiwa kubadilika kufuatia uamuzi wa Israel wa kuitambua Somaliland mwezi Desemba,2025.

Hatua hiyo iliifanya Israel kuwa taifa la kwanza mwanachama wa Umoja wa Mataifa kuitambua rasmi Somaliland k**a...Soma habari hii kwa kina katika tovuti ya DIRAMAKINI.

Rais Dkt.Mwinyi awatakia wananchi wote Jummah Mubarak leo Septemba 4,2026ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Bara...
04/09/2026

Rais Dkt.Mwinyi awatakia wananchi wote Jummah Mubarak leo Septemba 4,2026

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Alhaj Dkt.Hussein Ali Mwinyi leo Septemba 4,2026 amewatakia wananchi wote Jummah Mubarak huku akisisitiza kuwa,busara ni kusema kwa hekima na kutenda kwa heshima.

Waziri Dkt.Nanauka kukutana na wahariri, kueleza fursa na mipango ya Serikali kwa vijana nchiniNA DIRAMAKINIWAZIRI wa Nc...
04/09/2026

Waziri Dkt.Nanauka kukutana na wahariri, kueleza fursa na mipango ya Serikali kwa vijana nchini

NA DIRAMAKINI

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais–Maendeleo ya Vijana, Mhe. Dkt.Joel Arthur Nanauka (Mb) anatarajiwa kukutana na wahariri wa vyombo vya habari nchini kupitia Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), katika kikao kinacholenga kujadili kwa kina masuala ya maendeleo ya vijana na fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali.

Kikao hicho kinatarajiwa kufanyika Septemba 7,2026 kuanzia saa 3:00 asubuhi katika ukumbi wa JNICC, Dar es Salaam ikiwa ni mara ya kwanza kwa Waziri huyo kufanya kikao rasmi na wahariri wa vyombo vya habari nchini tangu kupewa dhamana ya kusimamia masuala ya maendeleo ya vijana.

Pia, kikao hicho kitatoa fursa kwa wahariri kupata uelewa mpana kuhusu majukumu ya Ofisi ya Rais-Maendeleo ya Vijana pamoja na mikakati ya Serikali katika kuwawezesha vijana kiuchumi,kuongeza ajira na kukuza ujasiriamali nchini.

Miongoni mwa mambo yatakayojadiliwa ni mikopo na uwezeshaji wa vijana, ikiwemo fedha zinazotengwa kwa ajili ya kuwawezesha vijana kuanzisha na kuendeleza shughuli za kiuchumi.

Kikao hicho pia kinatarajiwa kuangazia Shilingi bilioni 200 zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya mikopo na uwezeshaji wa vijana.

Aidha, wahariri watapata maelezo kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuandaa na kuimarisha kanzidata (database) ya vijana nchini, ambayo inalenga kuweka mfumo mzuri wa kutambua, kupanga na kuratibu mahitaji pamoja na fursa zinazowahusu vijana.

Ikumbukwe kuwa, katika jitihada za kuongeza uwezeshaji wa vijana, Serikali imeanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Vijana, wenye lengo la kuwawezesha vijana kiuchumi kwa kuwapatia mitaji ya kuanzisha au kuendeleza shughuli mbalimbali za uzalishaji, biashara na utoaji wa huduma.

Kupitia mfuko huo na programu nyingine za uwezeshaji, Serikali inalenga kuongeza ajira kwa vijana, kukuza ujasiriamali na kuchochea ushiriki wao katika shughuli za kiuchumi, hatua inayotarajiwa kuchangia kwa kiasi kikubwa katika ukuaji wa uchumi wa Taifa. SOMA habari hii kwa kina katika tovuti ya DIRAMAKINI.

Address

Ilala
12101

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Diramakini 24 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Diramakini 24:

Shortcuts

Share