Diramakini 24

Diramakini 24 Play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth

*ZANZIBAR KUANZA USAFIRI WA MABASI YA UMEME MWISHONI MWA FEBRUARI 2026*📍 Unguja – ZanzibarUsafiri wa umma wa kutumia mab...
09/01/2026

*ZANZIBAR KUANZA USAFIRI WA MABASI YA UMEME MWISHONI MWA FEBRUARI 2026*

📍 Unguja – Zanzibar

Usafiri wa umma wa kutumia mabasi ya umeme Zanzibar unatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Februari, 2026, ukianzia Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja.
Mradi huu unaotekelezwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) unalenga kupunguza msongamano barabarani, kuboresha uhakika wa safari, na kuimarisha usafiri rafiki kwa mazingira.

Serikali kupitia ZSSF imeingia mkataba na Kampuni ya GRT Limited katika utekelezaji wa mradi huu, utakaotumia vituo vya kisasa na mfumo maalum wa uendeshaji katika barabara za kawaida.

Mradi huu utafanyika kwa awamu tatu, ambapo awamu ya kwanza itaanza Mkoa wa Mjini Magharibi kwa njia za:Uwanja wa Ndege – Malindi,Buyu – Chukwani na Mnazi Mmoja – Malindi.

Kituo cha Kijangwani kitatumika k**a kiunganishi kikuu cha mabasi yote, sambamba na kuwepo kwa vituo ndani ya Uwanja wa Ndege na Bandari ya Malindi.
Mabasi ya umeme yanatarajiwa kuanza kuwasili mwanzoni mwa Februari, 2026.

Juhudi hizi za Serikali ya Awamu ya Nane chini ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt.Hussein Ali Mwinyi zinalenga kuiletea Zanzibar maendeleo kupitia sekta mbalimbali.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa China, Mheshimiw...
09/01/2026

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa China, Mheshimiwa Wang Yi, amewasili Dar es Salaam, Tanzania, kwa ziara ya kikazi ya siku mbili kuanzia tarehe 9 hadi 10 Januari 2026.

Katika Uwanja wa ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Mheshimiwa Wang Yi amelakiwa na mwenyeji wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb), Naibu Mwaziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe na Mhe. James Milya, Katibu Mkuu Balozi Dkt Samwel Shelukindo na viongozi wengine wa Serikali

Ziara hiyo inalenga kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano wa kimkakati kati ya Tanzania na China.

Ziara hiyo pia inalenga kukuza ushirikiano kwa kuendeleza uhusiano wa kiuchumi na kuangazia fursa mpya za ushirikiano katika maeneo yenye maslahi ya pamoja.

Akiwa nchini Mheshimiwa Wang Yi atakuwa na mazungumzo na mwenyeji wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshiniwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo ambayo yatalenga kuendeleza na kuimarisha uhusiano wa kimkakati kati ya Tanzania na China

Mheshimiwa Wang Yi pia atakutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Ikulu jijini Dar es Salaaam ambako pia atawasilisha salamu maalum kutoka kwa Rais wa China Mheshimiwa Xi Jinping

Tanzania na China zimekuwa zikishirikiana katika maeneo mbalimbali ikiwemo biashara na uwekezaji, ambapo kwa mwaka 2024 thamani ya biashara kati ya Tanzania na China ilifikia takriban dola za Marekani bilioni 5.2.

Kampuni za China pia zimeendelea kuwekeza nchini katika sekta za viwanda, kilimo, huduma, usafirishaji, mawasiliano na utalii. Kwa mwaka 2025, Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) ilisajili miradi ya China 343 yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 3.1 na kuzalisha ajira 82,404.

Tanzania na China pia zimekuwa zikishirikiana katika sekta ya miundombinu ya uchukuzi ambapo reli ya TAZARA ni moja wapo ya alama ya urafiki na ushirikiano kati ya nchi hizi mbili. Reli hiyo ina urefu wa Kilomita 1860 ambapo, kilomita 975 zipo Tanzania na kiliomita 885 zipo Zambia.

DCEA yavipongeza vyombo vya habari mapambano dhidi ya dawa za kulevya nchini■Kamishna Jenerali Lyimo amesema, dawa za ku...
09/01/2026

DCEA yavipongeza vyombo vya habari mapambano dhidi ya dawa za kulevya nchini

■Kamishna Jenerali Lyimo amesema, dawa za kulevya ni uhalifu wa kupangwa na unaovuka mipaka, hivyo vyombo vya habari vinapaswa kuendelea kushirikiana na taasisi za serikali na wadau wengine kwa kuzingatia maadili ya uandishi wa habari,ili kuhakikisha taarifa sahihi na zenye tija zinaifikia jamii kwa wakati.

“Bila ninyi hatuwezi kufanya jambo la kuwaelimisha wananchi kuhusu dawa za kulevya, kupitia vyombo vyenu vya habari ndipo Tanzania imefahamika Dunia nzima kufanikisha mapambano dhidi ya dawa za kulevya, awali Tanzania ilifanywa kuwa lango la dawa za kulevya, lakini sasa hilo lango limefungwa.

“Sisi Tanzania, hatutaki kuruhusu madhara ya dawa za kulevya katika Taifa letu, hivyo tunaendelea kushirikiana ili kuhakikisha tunaishinda vita hii kwa pamoja,"amefafanua Kamishna Jenerali Lyimo| https://www.diramakini.co.tz/2026/01/dcea-yavipongeza-vyombo-vya-habari.html

TEA na UNICEF wafungua milango ya miradi ya elimu ZanzibarZANZIBAR-Katika kuendeleza ushirikiano na wadau wa Sekta ya El...
09/01/2026

TEA na UNICEF wafungua milango ya miradi ya elimu Zanzibar

ZANZIBAR-Katika kuendeleza ushirikiano na wadau wa Sekta ya Elimu nchini, Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa kushirikiana na Shirika la Kuhudumia Watoto (UNICEF Tanzania) wamefungua rasmi milango ya utekelezaji wa miradi ya elimu visiwani Zanzibar kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali (WEMA), kwa lengo la kuboresha miundombinu ya elimu.

Kupitia ushirikiano huo, TEA na UNICEF wametenga jumla ya shilingi bilioni 2.5 kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa vyumba vya madarasa, maabara za sayansi pamoja na matundu ya vyoo katika shule 20 ambapo, shule 11 zipo kisiwani Unguja na shule 9 kisiwani Pemba.

Akizungumza wakati wa kikao kazi maalum cha kujadili utekelezaji wa miradi hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Dkt. Erasmus Kipesha alisema, utekelezaji wa mradi unatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Januari na kukamilika kabla ya mwezi wa sita mwaka huu.

Dkt.Kipesha alibainisha kuwa,lengo la mradi huo ni kuwawezesha wanafunzi kusoma katika mazingira bora, salama na rafiki kwa afya zao. Aliongeza kuwa, TEA ni taasisi ya Muungano,hivyo utekelezaji wa miradi ya elimu Zanzibar ni sehemu ya majukumu yake ya msingi.

Aidha, alisisitiza kuwa ushirikiano uliopo kati ya TEA na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar umekuwa nguzo muhimu ya mafanikio ya miradi mbalimbali ya elimu inayotekelezwa na ambayo imekamilika| https://www.diramakini.co.tz/2026/01/tea-na-unicef-wafungua-milango-ya.html

Mheshimiwa Silinde atoa rai kwa wakandarasi wazawa miradi ya umwagiliajiSIMIYU-Serikali imewataka wakandarasi wazawa wan...
09/01/2026

Mheshimiwa Silinde atoa rai kwa wakandarasi wazawa miradi ya umwagiliaji

SIMIYU-Serikali imewataka wakandarasi wazawa wanaotekeleza miradi ya Umwagiliaji nchini kuhakikisha miradi hiyo inaleta tija kwa wakulima na taifa kwa ujumla, ikisisitiza kuwa uzembe au kuchelewesha utekelezaji kutaibua hatua kali za kisheria dhidi yao.

Rai hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb) akiwa katika muendelezo wa ziara yake mkoani Simiyu, wakati wa kukagua maendeleo ya ujenzi wa Bwawa la Umwagiliaji la Kasoli lililopo Kijiji cha Kasoli, Kata ya Kasoli. Bwawa hilo lina ujazo wa takribani mita za ujazo milioni 2.7 na linatarajiwa kuhudumia mashamba yenye ukubwa wa hekta 650.

Mhe. Silinde amesema kuwa uamuzi wa Serikali kuwapa wakandarasi wazawa miradi mikubwa ya kimkakati, ikiwemo ya Umwagiliaji, unalenga kuwajengea uwezo na kukuza ujuzi wa ndani ili wazawa washiriki kikamilifu katika kujenga uchumi wa nchi yao. Amesisitiza kuwa imani hiyo lazima iendane na uwajibikaji, ubora wa kazi na kukamilisha miradi kwa wakati uliopangwa.

“Serikali inawapa nafasi wakandarasi wazawa kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuimarisha uchumi wa ndani. Hata hivyo, ni wajibu wao kuhakikisha miradi hii inaleta matokeo chanya kwa wakulima, kinyume chake hatua zitachukuliwa," amesema Mhe. Silinde| https://www.diramakini.co.tz/2026/01/mheshimiwa-silinde-atoa-rai-kwa.html

DCEA yak**ata tani 9 za dawa za kulevya,Mkenya muuza chai adakwa Sinza C■Pia, Kamishna Jenerali Lyimo amesema, katika Mt...
08/01/2026

DCEA yak**ata tani 9 za dawa za kulevya,Mkenya muuza chai adakwa Sinza C

■Pia, Kamishna Jenerali Lyimo amesema, katika Mtaa wa Wailes uliopo Halmashauri ya Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam mamlaka hiyo ilik**ata pakti 20 za skanka zenye uzito wa kilogramu 20.03 zikiwa zimefichwa ndani ya balo la mitumba na kufichwa kwenye basi aina ya Scania.

Basi hilo lenye usajili wa nchi ya Msumbiji namba AAM 297 CA ni mali ya Kampuni ya King Masai Tours, ambapo huwa linafanya safari zake kati ya Nampula nchini Msumbiji na Tanzania.

"Watuhumiwa waliok**atwa kuhusiana na tukio hilo ni Amasha Idd Mrisho miaka 40, ambaye ni mkazi wa Buza jijini Dar es Salaam na Seleman Juma Ally miaka 32 raia wa Msumbiji https://www.diramakini.co.tz/2026/01/dcea-yak**ata-tani-9-za-dawa-za.html

Address

Ilala
12101

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Diramakini 24 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Diramakini 24:

Share