Diramakini 24

Diramakini 24 Play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth

SERIKALI YAANZA KUREJESHA MABASI YA MWENDOKASI UBUNGO,KIVUKONI NA GEREZANI WAKALA wa Mabasi yaendayo Haraka Dar es salaa...
28/11/2025

SERIKALI YAANZA KUREJESHA MABASI YA MWENDOKASI UBUNGO,KIVUKONI NA GEREZANI

WAKALA wa Mabasi yaendayo Haraka Dar es salaam (DART) imerejesha huduma za usafiri wa umma katika awamu ya kwanza, kuanzia Ubungo Terminal kuelekea Gerezani, Kivukoni na Muhimbili.

Huduma hiyo imerejea rasmi leo Novemba 28,2025 katika maeneo tajwa ikiwa ni hatua ya mwanzo ya kurejea kwa huduma baada ya uharibifu mkubwa wa miundombinu uliofanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa DART, William Gatambi ameeleza hayo akitoa ufafanuzi wa kuanza kurejea kwa huduma hizo baada ya tathmini iliyofanyika ili kubaini maeneo salama kwa ajili ya kurejesha huduma.

Gatambi amesema, wamefanya hivyo wakati ukarabati katika vituo vilivyoathiriwa ukiendelea kwa awamu ili kuhakikisha mfumo mzima unarejea kikamilifu, huku akikiri kuwa kusitishwa kwa huduma kuliathiri sana wananchi, huku wengi wakilazimika kuhangaika kupata usafiri wa uhakika.

Tanzania Kuendeleza Ushirikiano wa Kidiplomasia na Jumuiya ya KimataifaDAR-Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afri...
28/11/2025

Tanzania Kuendeleza Ushirikiano wa Kidiplomasia na Jumuiya ya Kimataifa

DAR-Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amekutana na kuzungumza na Jumuiya ya Wanadiplomasia wanaowakilisha nchi na taasisi za kimataifa hapa nchini katika Ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo, ambao ni wa kwanza tangu kuundwa kwa Serikali ya Awamu ya Sita kipindi cha pili baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025, ulilenga kuimarisha majadiliano na kueleza msimamo wa Serikali kuhusu masuala ya kitaifa na kimataifa.

Katika mazungumzo hayo, Mhe. Waziri Kombo aliwahakikishia wanadiplomasia hao kuwa Tanzania itaendelea kudumisha na kuimarisha ushirikiano na mataifa yote pamoja na mashirika wanayoyawakilisha.

Kupitia kikao hicho, Mabalozi kutoka nchi mbalimbali wamethibitisha utayari wa nchi na tasisi zao kuendelea kushirikiana na Tanzania, hatua ambayo Waziri Kombo alisema kuwa inaonesha ukomavu wa diplomasia na uhusiano imara baina ya Tanzania na washirika wake wa kimataifa.

Serikali pia ilitumia mkutano huo kutoa taarifa kwa wanadiplomasia kuhusu mwenendo wa uchaguzi mkuu na matukio wakati wa uchaguzi huo na kuelezea hatua zilizochukuliwa na Serikali kurejesha hali ya utulivu, kuhakikisha usalama wa raia na mali zao, na kuendeleza utoaji wa huduma za msingi na shughuli za kiuchumi.

Mhe. Waziri Kombo pia aliwaeleza mabalozi hao juu ya Tume ya Uchunguzi iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuchunguza chanzo cha matukio hayo, pamoja na kupendekeza hatua madhubuti za kuimarisha mifumo ya kitaifa ili kuzuia matukio k**a hayo kutokea tena.

TMA yataja sababu za ongezeko la hali ya joto kali kwa baadhi ya maeneo nchiniNA DIRAMAKINIMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanza...
28/11/2025

TMA yataja sababu za ongezeko la hali ya joto kali kwa baadhi ya maeneo nchini

NA DIRAMAKINI

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa kuhusu kuongezeka kwa viwango vya joto katika maeneo mbalimbali nchini, hususan yale yenye misimu miwili ya mvua kwa mwaka.

Ongezeko hilo limejitokeza katika kipindi cha miezi ya hivi karibuni kutokana na kusogea kwa Jua la Utosi pamoja na upungufu wa mvua katika maeneo husika.

Kwa mujibu wa TMA, vipindi vya Jua la Utosi hufikia kiwango cha juu mwishoni mwa Novemba wakati jua linapoelekea kusini (Tropiki ya Kaprikoni), na hali hii hurudiwa tena Februari jua linapoelekea kaskazini (Tropiki ya Kansa).

Kipindi hiki huambatana na mionzi mikali ya jua inayopelekea ongezeko la joto, kwani uso wa Dunia huwa karibu zaidi na Jua katika eneo husika https://www.diramakini.co.tz/2025/11/tma-yataja-sababu-za-ongezeko-la-hali.html

TMA reports extreme heat in bimodal areas, expects relief in DecemberBY DIRAMAKINITHE Tanzania Meteorological Authority ...
28/11/2025

TMA reports extreme heat in bimodal areas, expects relief in December

BY DIRAMAKINI

THE Tanzania Meteorological Authority (TMA) has issued a statement alerting the public to extreme hot conditions in various parts of the country, particularly in bimodal areas.

The increase in temperatures over the past few months is attributed to the movement of the overhead sun and reduced rainfall in these regions https://www.diramakini.co.tz/2025/11/tma-reports-extreme-heat-in-bimodal.html

Tanzia
27/11/2025

Tanzia

Waziri Kombo apokea magari mawili kutoka QatarWizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imepokea magari ...
27/11/2025

Waziri Kombo apokea magari mawili kutoka Qatar

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imepokea magari mawili aina ya Land Cruiser Prado kutoka Taifa la Qatar kwa ajili ya kuhudumia viongozi wanaokuja kwa ziara za kitaifa na kikazi nchini.

Qatar k**a mshirika wa maendeleo ya uchumi wa Tanzania alikubali ombi na ametoa magari hayo mapya kufuatia ombi la magari na pikikipiki za kuhudumia viongozi wa nje wawapo katika ziara nchini huku wakiendelea na mchakato wa kuleta pikipiki sita.

Akizungumza katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam baada ya kukabidhiwa nyaraka za magari hayo, Mheshimiwa Waziri, Balozi mahmoud Thabit Kombo (Mb.) ameishukuru Qatar kwa kuwa mdau mkubwa wa maendeleo Tanzania na kuahidi kutumia vyema misaada hii ili kuweza kutatua changamoto zinazojitokeza katika kazi.

Akimkabidhi funguo za magari hayo Afisa Usafirishaji Mkuu, Bw. Maulid Mkenda, Mhe. Waziri Kombo amemhimiza kuyatunza magari hayo ili yadumu na kuleta tija na ufanisi.

Qatar pia imekuwa ikitoa ushirikiano katika masuala ya ajira kwa vijana kwa kutoa nafasi za ajira kwa madereva wa Kitanzania nchini Qatar huku nafasi nyingine zikiendelea kuja na kutangazwa.

DIPLOMASIA YA TANZANIA YANGA'RA UNIDOTanzania imechaguliwa kwa kura zote za ndiyo na nchi wanachama wa UNIDO kuwa Mjumbe...
27/11/2025

DIPLOMASIA YA TANZANIA YANGA'RA UNIDO

Tanzania imechaguliwa kwa kura zote za ndiyo na nchi wanachama wa UNIDO kuwa Mjumbe wa Bodi ya Maendeleo ya Viwanda ya UNIDO kwa kipindi cha mwaka 2025-2029 na Mjumbe wa Kamati ya Programu na Bajeti ya UNIDO kwa kipindi cha mwaka 2025-2027 ikiwakilisha Kundi la nchi za Afrika katika Shirika hilo la Umoja wa Mataifa.

Uchaguzi huo ulifanyika wakati wa Mkutano Mkuu wa 21 wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda (UNIDO’s General Conference) unaohitimishwa jijini Riyadh, Saudi Arabia, Novemba 27, 2025.

Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa, Vienna, Mhe. Naimi S.H. Aziz ambaye alimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewashukuru Mabalozi wote wa Ukanda wa Afrika wanaowakilisha nchi zao kwenye Umoja wa Mataifa, Vienna, Austria kwa imani kubwa walioipatia Tanzania katika kuwakilisha mataifa ya Afrika kwenye vyombo hivyo muhimu vya kisera na maamuzi vya UNIDO.

Balozi Naimi alieleza kuwa ujumbe kwenye Bodi ya Maendeleo ya Viwanda na Kamati ya Programu na Bajeti utatoa fursa ya pekee kwa Tanzania kushauri kuhusu sera na programu za shirika zinazohusiana na maendeleo ya viwanda, na kushiriki kikamilifu maamuzi ya mipango na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya UNIDO kwa nchi wanachama.

Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Bi. Felister Mdemu; na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Viwanda wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Bw. Juma Mwampamba.

FUNDI NGUO JELA MIAKA 20 KWA KUMNAJISI MTOTO WILAYANI TEMEKEDAR-Mahak**a ya Wilaya Temeke Jijini Dar es Salaam imemukumu...
26/11/2025

FUNDI NGUO JELA MIAKA 20 KWA KUMNAJISI MTOTO WILAYANI TEMEKE

DAR-Mahak**a ya Wilaya Temeke Jijini Dar es Salaam imemukumu kutumikia kifungo cha miaka 20 jela Rashidi Ruambo mwenye umri wa miaka 56 fundi ushonaji mkazi wa Yombo Makangarawe kwa kupatikana na hatia ya kosa la Shambulio la aibu.

Hukumu hiyo imeitolewa Novemba 25,2025 na Hakimu wa Mahak**a ya Wilaya Temeke Mh. Janeth Kaluyenda akisoma hukumu hiyo amesema kuwa Mahak**a imeridhika na ushahidi uliowasilishwa Mahak**ani hapo ambao pasi na chembe ya shaka umemtia hatiani mtuhumiwa huyo.

Imeelezwa kuwa mnamo mwezi Novemba 24,2024 majira ya saa 06:00 mchana huko maeneo ya Yombo Makangarawe mtuhumiwa akiwa katika duka lake la ushonaji alimuita mtoto wa k**e mwenye umri wa miaka sita mwanafunzi wa chekechea na kuanza kumchezea kwa kumuingizia vidole sehemu zake za uke na kisha mtoto huyo akaenda kumueleza mama yake juu ya kitendo hicho alichofanyiwa.

Address

Ilala
12101

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Diramakini 24 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Diramakini 24:

Share