02/06/2026
EWURA yatangaza bei ya mafuta Juni 2026,nafuu kidogo kwa Petroli
NA DIRAMAKINI
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza bei kikomo za mafuta ya petroli nchini kuanzia Juni 3, 2026 huku zikiendelea kupanda, ikieleza kuwa hali hiyo imesababishwa kwa kiasi kikubwa na vita vinavyoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati pamoja na kuvurugika kwa usafirishaji wa mafuta duniani.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na EWURA, mgogoro ulioanza Februari 28, 2026 ukizihusisha Marekani, Israel na Iran umeathiri miundombinu muhimu ya uzalishaji, uhifadhi na usafishaji wa mafuta, hali iliyosababisha kupungua kwa upatikanaji wa mafuta katika soko la dunia na kuongezeka kwa bei za bidhaa hizo.
EWURA imeeleza kuwa,hali hiyo imechangiwa zaidi na kufungwa kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz, njia inayopitisha takribani asilimia 20 ya mafuta yote yanayosafirishwa duniani.
Kufungwa kwa njia hiyo kumesababisha ongezeko la gharama za usafirishaji, bima za meli za mafuta pamoja na ucheleweshaji wa mizigo, jambo ambalo limeongeza shinikizo la bei katika soko la kimataifa.
Tanzania, ambayo huagiza sehemu kubwa ya mafuta yake kutoka Mashariki ya Kati, imeathirika moja kwa moja na mabadiliko hayo ya kimataifa.
Katika hatua ya kupunguza athari kwa wananchi na uchumi wa nchi, Serikali imeendelea kutoa ruzuku ya takribani shilingi 534.91 kwa kila lita moja ya dizeli ili kusaidia kudhibiti ongezeko kubwa zaidi la bei za mafuta hayo yanayotumika katika sekta za usafirishaji, uzalishaji viwandani na huduma mbalimbali za kijamii.
Kwa mujibu wa bei mpya zilizotangazwa, mafuta ya petroli katika Jiji la Dar es Salaam yatauzwa kwa bei isiyozidi shilingi 4,086 kwa lita, huku dizeli ikiuzwa kwa shilingi 4,333 na mafuta ya taa kwa shilingi 4,685 kwa lita.
Katika Bandari ya Tanga, petroli itauzwa kwa shilingi 4,157 kwa lita, dizeli shilingi 4,404 na mafuta ya taa shilingi 4,756 kwa lita.
Kwa upande wa Mtwara, petroli itauzwa kwa shilingi 4,193 kwa lita, dizeli shilingi 4,440 na mafuta ya taa shilingi 4,792 kwa lita.
Ikumbukwe kwa mwezi Mei 2026, bei kikomo za rejareja katika mikoa ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara zilikuwa k**a ifuatavyo...