Anord Msakwa

Anord Msakwa Ukweli na uwazi

30/04/2025

NENO LA SIKU

Na, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira- Kanisa la Efatha.

TAREHE: 30/04/2025

SOMO: BAADA YA MAOMBI KIRI USHINDI.

Marko 11:24 "Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu."

Ukishamaliza kuomba hakikisha unachoongea kila siku kinakubaliana na kile ulichoomba, k**a uliomba Mungu akuondolee umasikini na ufukara basi kuanzia hapo usiongee kwamba mimi sina hela, la! Bali anza kusema Mungu amenibariki sitakufa masikini, nitajenga nyumba nzuri nitakuwa na Maisha mazuri; ongea yale yanayohusu baraka, usianze kuongea unajua mimi sina fedha au sina hiki wala kile; anza kuongea k**a ulivyoomba, usiongee tena k**a mtu ambaye haelewi nini anataka.

Ukishaomba amini ya kwamba Mungu anasikia na ameshasikia kile ulichoomba. Kuanzia hapo ondoa unyonge ya kwamba hakuna mtu anayekupenda, tambua kuwa yupo aliyekufia anakupenda, hata k**a watu hawakupendi Yesu anakupenda na k**a Yeye anakupenda basi hata watu watakupenda.

Hakikisha unatenda k**a mtu aliyejibiwa maombi, acha kuwaza shida zako waza jinsi unavyokwenda kutumia baraka zako. Anza kuchora kitu au kuumba kitu unachokitaka au namna utakavyotumia zile Baraka ulizoomba.

16/11/2024

NENO LA SIKU

Na, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira- Kanisa la Efatha

TAREHE 08/11/2024

SOMO: KIBALI

1 Yohana 3:1 “Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu;..” Kusudi tulilonalo ni ili kufikia lengo la Kibali cha Mungu; maombi tunayoyafanya, mafundisho tunayayoyapata ni ili tuweze kufika mahali pa lengo la kibali cha Mungu. Kibali ni kwa ajili ya wana.

Kibali ni kwa ajili ya Wana wanaokubali kuacha tabia za kitoto ili Mungu apate kuwaamini. Tulipokuwa watoto hakuna maamuzi tuliyoyafanya yaliyosababisha Mungu atufurahie, lakini ukishakuwa Mwana unaweza ukawa na kibali moyoni mwako cha kufanya jambo litakalo mfanya Mungu akufurahie akupe kibali. Yesu hakuchagua kuzaliwa katika hori la ng’ombe, lakini alipofika na kutimiza mapenzi ya Mungu, akachagua kwenda kubatizwa. Akiwa anaomba Mbingu zilifunguka.

Ili uweze kutoka kwenye utoto na kuingia kuwa mwana ni lazima ukutane na watu ambao sio watoto. Ukitaka kuwa dereva mzuri, lazima umpate dereva aliyekuzidi au unataka kuwa tajiri, kaa na matajiri wakuelekeze namna ya kuwa tajiri. K**a unataka kuwa mwana, kaa na wenye uzoefu wa kuwa wana. Kibali cha Mungu kinachokubali ambacho kinaruhusu Nguvu ya Mungu itembee kwa mtu ni pale mtu anapotoka katika utoto, kwa ridhaa yake mwenyewe, nia ya ndani na kwa makusudi ya dhahiri na yeye anasema kwenye akili yake, “Nataka kukua, nataka kuwa watofauti, nataka kujionesha mimi ni mwana, mimi nimeelewa.”

Address

Mufindi
Iringa

Telephone

+255757298730

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Anord Msakwa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Anord Msakwa:

Share