ISLAM

ISLAM mwandishi

YESU SI MUNGU: KWA SABABU MUNGU NI MMOJA TU. Baadhi ya Wakristo wanatafuta sababu na udhuru wa kumfanya Yesu kuwa Mungu....
16/12/2024

YESU SI MUNGU:

KWA SABABU MUNGU NI MMOJA TU.

Baadhi ya Wakristo wanatafuta sababu na udhuru wa kumfanya Yesu kuwa Mungu. Kwa mfano husema kwamba Yesu ni Mungu au mwana wa Mungu au Yesu ni Mungu mdogo au Yesu ni nafsi moja ya Mungu. Mambo haya yote ni kufuru tupu iliyovuka mipaka. Kwa sababu sawa na Biblia Mungu ni mmoja tu. Hakuna Mungu mdogo wala Mungu mwana. Biblia inasema:-

1. Wewe naam, wewe peke yako ndiye Mungu wa falme zote za dunia; wewe ndiwe uliyeziumba mbingu na nchi. (2 Wafalme 19:15).

2. Kwa kuwa ndiwe mkuu, wewe ndiwe mfanya miujiza, ndiwe Mungu peke yako. (Zaburi 86:10).

3 Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma, (Yohana 17:3).

Sasa wakati Mungu wa pekee ni mmoja, hivyo Mungu zaidi ya mmoja ni wa uwongo.

4. Mwawezaje kuamini ninyi, mnaopokeana utukufu ninyi kwa ninyi, na utukufu ule utokao kwa Mungu aliye wa pekee hamwutafuti? (Yohana 5:44).

5. ...Hakuna Mungu ila mmoja tu. Kwa maana ijapokuwa wako waitwao miungu, ama mbinguni au duniani; k**a vile walivyoko miungu mingi na mabwana wengi. Lakini kwetu sisi Mungu ni mmoja tu. aliye baba, ambaye vitu vyote vimetoka kwake. (1 Wakorintho 8:4-6).

Sawa na aya hizi hakuna Mungu ila mmoja tu. Ingawa miungu wa bandia wanatajwa tajwa mbinguni na ardhini. Basi sasa ambaye anaamini mungu minghairi ya Mwenyezi Mungu anatoka katika imani na anaingia katika ushirikina kwa sababu ya kuwaita miungu zaidi ya mmoja ambaye ni wa kweli na wa pekee.

6. ..Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye Mungu. (Marko 2:7).

Aya hii inathibitisha kwamba mwenye kufuta na kuondoa dhambi ni mmoja tu ambaye ni Mungu. Yaani hakuna mungu wa pili wala wa tatu wala mwenye kufuta dhambi isipokuwa Mwenyezi Mungu tu. Siyo aya hizo tu, bali tunaposoma Biblia tunakuta msululu wa aya kadhaa ambazo zinataja umoja wa Mungu. Kwa mfano: Kumbukumbu 4:39, 6:4; Nehemia 9:9; Isaya 43:10-11; 44:6-8, 44:5. 45:21-22, 46:9; Marko 12:32; Luka 18:19; Mathayo 4:10; Warumi 3:30; Timotheo 1:17, 2:5.
Hakuna aya hata moja inayosema kwamba Yesu ni Mungu..

Na Mw/Ally Muhammad Kaswezi.

JE KRISTO KAFIA MSALABANI?SOMA KWA FAIDA YA KUELEWA KISA HIKI CHA YESU KUFA PALE MSALABANI. Kikundi cha wanasayansi wa K...
12/12/2024

JE KRISTO KAFIA MSALABANI?

SOMA KWA FAIDA YA KUELEWA KISA HIKI CHA YESU KUFA PALE MSALABANI.
Kikundi cha wanasayansi wa Kijerumani kilikuwa kinafanya utafiti kuhusu sanda ya Yesu kwa muda wa miaka minane iliyopita. Matokeo ya utafiti wao yametolewa hivi karibuni katika vyombo vya habari.

Ile shuka aliyofunikwa Yesu ambayo umri wake ni miaka elfu mbili imegunduliwa katika mji mmoja wa Italia uitwao Turin.

Shuka hiyo ina athari za picha ya mwili wa Yesu. "Wanasayansi hao wamemwarifu Baba Mtakatifu kuhusu uvumbuzi huu. Lakini Baba Mtakatifu hajasema lolote.

Uvumbuzi huu umeifichua siri kubwa ya historia ya kidini ya Kanisa Katoliki. Kwa msaada wa sanaa ya upigaji picha wanasayansi hawa wamejaribu kuhakikisha kwamba ule ufufuo ambao watu waliuhesabu kuwa ni mwujiza kwa muda wa miaka elfu mbili iliyopita, kwa hakika yalikuwa ni matokeo ya kawaida ya utendaji kazi wa mwili wa binadamu au tuseme wa viumbe vyote vyenye uhai.

Wamekubaliana kwa pamoja kwamba Kristo hakufia msalabani. Suala la sanda ya Yesu limekuwa likijadiliwa tangu miaka elfu moja iliyopita. Shuka hii ilipelekwa mjini Constantinople mnamo mwaka 438 kwa kalenda ya Kikristo. Aliyeipeleka huko ni Malkia Endoxi.

Mara ya kwanza kabisa shuka hii ilionekana karibu ya makaburi. Ilibakia mjini Constantinople kwa muda wa miaka mia saba. Hatimaye mtu mmoja aitwae De La Roche aliondoka nayo baada ya mji wa Constantinople kushambuliwa.

Wakati moto ulioziunguza nyumba za mji huo, shuka hiyo ilikuwa ndani ya sanduku la fedha. Kwa sababu ya kuyeyuka kwa sanduku hilo la fedha shuka hiyo ikafifia kidogo. Hata hivyo zile alama za mwili wa Yesu zilikuwa bado zinaonekana".

"Watu wa Ufaransa walipata pesa nyingi sana kwa kuifanyia maonyesho nguo hii. Kutoka Ufaransa shuka hiyo ikapelekwa Turin na ilipofika hapo ikawa inaonyeshwa hadharani baada ya kila miaka thelathini na tatu. Mnamo mwaka 1898 kwa tarehe za Kikristo mwanasheria mmoja wa Kiitalia aliuelekeza ukanda uliotumiwa kuipiga picha shuka hii kwenye mwangaza wa jua na akauangalia.

Alish*tuka kuona kwamba ukanda ule ulikuwa na picha inayoshabihiana kwa kila hali na Yesu Kristo. Wakati picha ilipochapishwa kutokana na ukanda huo, ilionyesha uso wa mtu huyu (Yesu) ambaye hakuna aliyewahi kumwona tangu miaka 1900 iliyopita.

Mnamo mwaka 1931 kwa tarehe za Kikristo nguo hiyo ilionyeshwa tena hadharani, na mpiga picha mmoja aitwae Guisepe Enric aliipiga picha tena nguo hiyo kwa kutumia vishubaka vya umeme wenye nguvu ya volti 6,000 na 20,000 na wakati shughuli hii ikifanyika alikuwepo mtu mmoja ambaye ana cheo cha juu katika kanisa.

Picha hii imefichua ukweli wenye kutia hamasa katika akili ya mtu na kwa mara ya pili imedhihirisha kile ambacho mpiga picha wa kwanza aitwae Pia alikionyesha. Picha hiyo inashabihiana sana na michoro ya kuigiza ya uso na mwili wa Yesu ambayo wanasanaa wa Kikristo walikuwa wakituonyesha kwa muda wa miaka elfu mbili iliyopita.

"Mtu anapoangalia ile picha ambayo imechapishwa ndani ya kitabu kiitwacho DAS LINNEN KURT BERNA A TUL TGART kilichotungwa na Hanas Naber Verlag, anaweza kuelewa Kanisa litajisikiaje kwa kuiona picha hii. Baba Mtakatifu Pius wa 9 alikuwa na maoni haya:-
"PICHA HII HAIKUTENGENEZWA KWA MKONO WA BINADAMU YE YOTE"

Wanasayansi hao wametangaza ya kwamba shuka hiyo pamoja na historia vyote vinathibitisha ya kwamba picha hiyo ni ya Kristo. Utengenezaji pamoja na mfumo wa nyuzi unaonyesha ya kwamba ni namna ya shuka zilizokuwa zinapatikana mahali paitwapo Pompii. Kuonekana kwa picha mbili za mwili wa Yesu katika shuka hiyo kunaonyesha ya kwamba nusu ya shuka hiyo ilitumiwa kwa kufunika kichwa chake. Marahamu yaliyopakwa mwilini mwake pamoja na lile joto la mwili ndivyo vimewezesha athari ya picha ya mwili wa Kristo ichapishwe katika shuka ile.

Damu yenye uhai ya Yesu Kristo ambayo ilinyonywa na nguo hiyo vile vile iliacha alama katika shuka hiyo. Picha hiyo inaonyesha waziwazi alama za taji la miiba chini ya kichwa na kwenye paji la uso wa Kristo na shavu lililovimba. Na alama ya jeraha la mkuki kwenye ubavu wa kulia. Alama ya matone ya damu yaliyochuruzika kutoka katika jeraha hilo pamoja na majeraha ya misumari na vile vile alama za majeraha ya mgongoni yaliyosababishwa na msuguano kati ya mgongo wake na lile bao la msalaba.

Lakini jambo la kushangaza zaidi ni kwamba katika ule ukanda wa kupigia picha, macho mawili ya Yesu ambayo yalikuwa yamefumba yanaonekana kana kwamba yako wazi. "Picha hii inabainisha pia kwamba ile misumari haikupigiliwa katika viganja bali kwenye maungio ya viganja. Jambo lingine linalobainishwa ni kwamba ule mkuki haukuugusa moyo wa Yesu. Bibilia inasema kwamba KRISTO ALIKATA ROHO, lakini wanasayansi hao wanasisitiza kwamba moyo wa Yesu haukuacha kufanya kazi hata mara moja.

"Pia inahojiwa ya kwamba k**a Kristo angalibakia bila ya uhai kwa muda wa saa moja juu ya msalaba, damu yake ingeganda na kukauka. Kwa hiyo matone ya damu yasingalipatikana katika shuka ile. Lakini kwa vile damu ilisambaa katika shuka ile hii inaonyesha ya kwamba Kristo alikuwa hai aliposhushwa msalabani." Ninaweza kuongeza hapa kwa uvumbuzi huu wenye kutia hamasa ambao umefanywa na wanasayansi hawa wa Kijerumani, unathibitisha tu yale ambayo yalisemwa na Kurani Tukufu karne kumi na nne zilizopita. Kurani Tukufu inatangaza ya kwamba Yesu hakufia msalabani. "Na kusema kwao (Mayahudi) Hakika sisi tumemwua Masihi Isa mwana wa Mariamu Mtume wa Mungu; ambapo kwa hakika hawakumwua wala hawakumfisha msalabani isipokuwa tu alifanywa aonekane machoni pao kana kwamba AMEKUFA MSALABANI (ni jambo la uwongo); na wale wanaohitalafiana (na wasemao kweli) kuhusu jambo hili, kwa hakika wamo katika hali ya mashaka mashaka: hawana elimu kamili kuhusu jambo lenyewe ila wanafuata dhana tu, na kwa vyo vyote iwavyo hawawezi kuifanya dhana yao iwe kweli. (Kurani Tukufu 4: 158).

Na Mw/ Ally Muhammad Kaswezi

KUTOKA MAKTBA.KUKIRI KWA WASIO AHMADIYYA JUUYA MWENENDO MWEMA WA JUMUIYYA HII.SEHEM YA KWANZA.1) Khawaja Hasan Nidhami a...
11/12/2024

KUTOKA MAKTBA.

KUKIRI KWA WASIO AHMADIYYA JUU
YA MWENENDO MWEMA WA JUMUIYYA HII.
SEHEM YA KWANZA.

1) Khawaja Hasan Nidhami aliandika:
"Ingawaje mimi sina itikadi ya Kikadiani wala sina maelekeo yo yote kwenye Jumuiya ya Kikadiani, lakini ninakiri kwamba Jumuiya ya Kikadiani inafanya kazi nzuri iletayo athari kwa kushindana na maadui wa dini ya Kiislamu".
(Kitabu: Musalman Maha-Rana, utungo wa Bwana Khawaja Hasan Nidhami wa Delhi).

2) Maulana Abdul Halim Sharar, Mhariri wa gazeti 'Dilgudaz' la Lucknow, aliwahi kukiri:

"Siku hizi Waahmadiyya wanashindana na Mabahai hali hii ya mabishano inaendelea. Lakini tofauti hasa baina ya hao wawili ni kwamba Dhehebu la Ahmadiyya linahubiri Islam na kuieneza likibakiza sheria ya Muhammad katika nguvu na shani hiyo hiyo, ilhali dini, ya Kibahai inaifuta sheria ya Kiarabu (Kiislamu) na kuhubiri kwamba dini hii haifai kuifuata. Kwa kifupi ni kwamba Ubabi umefika kuiangamiza Islam, na Uahmadiyya kuiimarisha Islam. Na kwa ajili ya baraka hiyo yake, juu ya hitilafu chache, Jumuiya Ahmadiyya inaihudumia Islam kikweli-kweli na kwa jazba kubwa ilhali Waislamu wengine hawafanyi."
(Gazeti Dilgudaz', Lacknow, Juni 1926)

3) Maulana Zafar Ali Khan Zafar, Mhariri wa Gazeti la 'Zamindar', Lahore, aliandika hivi:

"Tunawauliza Waislamu kwamba wanafanya juhudi gani kwa kuieneza dini yao tukufu katika dunia? Katika India kuna Waislamu 70,000,000; je, kwa niaba yao hata kituo kimoja pekee cha mahubiri ya Kiislamu kinashughulika katika nchi za Magharibi? Ni rahisi kuwasemea vibaya Waahmadiyya; lakini hakuna awezaye kukataa kwamba hiyo ndiyo Jumuiya iliyowapeleka Wabashiri wake katika Uingereza na nchi zingine za Yoropa."
(Zamindar, Lahore, Desemba, 1926) Ijulikane kwamba gazeti hili lilikuwa ni adui mkali wa Jumuiya ya Ahmadiyya.

4) Katika Dibaji ya Tafsirul-Quran, aliandika Ashraf Ali Thanawii:

"Wazungu wa Ulaya walisaidia kwa fedha na wakaingia nchini India kwa kuchukua ahadi za msaada wa kufululiza, ndipo akasimama Sheikh Ghulam Ahmad wa Qadian na akamwambia Padre na Jumuiya yake: Yesu mnayemtaja alikwisha kufa k**a wanadamu wengine, na yule Yesu aliyeahidiwa kufika ndiye mimi.... Kwa njia hii yeye akawahangaisha sana Wakristo hata waka-shindwa kuepukana naye. Na kwa njia hiyo mapadre wote wa India hadi Ulaya wakashindwa mbele yake."
(Dibacha Tafsirui-Quran. uk. 30).

5) Gazeti "Al-Jazirah" la Jordan liliandika yafuatayo:

"Twaona ni faradhi yetu kukiri kwamba wabashiri wa Jumuiya Ahmadiyya wanatekeleza
wajibu wao kwa bidii na jitihada nyingi, na wanajibidiisha kweli kweli kwa kuieneza Islam. Juhudi zao ziko nyingi zaidi katika Afrika, Afrika ya Kati na Amerika".
(Gazeti "Al-Jazirah" la Oman, Jordan, la tarehe 12 Juni. 1949)

6) Gazeti Al-'Irfaan" (Lebanon) liliandika:

"Juhudi za Jumuiya Ahmadiyya kuhusu kuhubiri na kuieneza Islam zinastahili kushukuriwa. Tunayo yakini kwamba Jumuiya hii inafanya kazi kubwa ya kuishindisha Islam."
(Al-Irfaan. Lebanon, la mwezi wa Dhulkaada, 1358 Hijriyyal

7) Gazeti la Cairo, "Al-Fatha" liliandika:

"Nimeona mwendeleo wa Kikadiani ni kitu kinachostaajabisha. Makadiani wamepaaza sauti yao katika lugha mbali mbali kwa midomo na kimaandishi... Vituo vyao vya mahubiri vimepatikana katika Asia. Yoropa, Amerika na Afrika. ambavyo vinalingana na misheni za Kikristo; lakini katika athari na ufaulu vituo vyao vya mahubiri haviwezi kulinganishwa na misheni za Kikristo, kwani Makadiani wamefaulu sana mno kuliko Wakristo kwa ajili ya ukweli wa Kiislamu na hekima zake."

(Al-Fat'ha, Cairo, la tarehe 20 Jumadal-Akhirah, 1351 Hijriyya)

Na Mw/ Ally Muhammad Kaswezi
Kahama shinyanga Tanzania.
📙📙ELIMU HAINA UMRI📙📙

KUTOKA MAKTABA......HAKIKA TATU NDANI YA MAKUSUDIO MATATU YA UJENZI WA MNARATUL MASIH.Mnamo Tarehe 28 Mei 1900, kwa kuti...
06/11/2024

KUTOKA MAKTABA......

HAKIKA TATU NDANI YA MAKUSUDIO MATATU YA UJENZI WA MNARATUL MASIH.

Mnamo Tarehe 28 Mei 1900, kwa kutimiza kusudio la Hadithi za Mtume, Hudhur Hadhar Mirza Ghuram Ahmad as alipanga kujenga mnara upande wa mashariki wa Masjid Aqsa na akaeleza makusudio yake matatu:
K**a ifuatavyo..........

LA KWANZA

ni kwamba mwadhini akipanda juu yake atoe adhana mara tano kwa sala, na ili jina takatifu la Mungu litangazwe kwa sauti ya juu mara tano katika usiku na mchana, na ili kwa maneno machache mara tano tuwatangazie watu kwamba Mungu wa tangu azali na wa kudumu ambaye wanadamu wote wanapaswa kumwabudu ni Mungu yule tu ambaye Mtume Mteule na Mtakatifu Muhammad Mustafaa anaongoza kwake. Pasipo yeye hakuna Mungu yeyote ardhini wala mbinguni.

LA PILI:

Kusudio la pili la mnara huu litakuwa kwamba kwenye
sehemu ya juu sana ya ukuta wa mnara huu, taa kubwa sana itawekwa... Mwanga huu utaenda mpaka mbali sana kwa kunurisha macho ya wanadamu.

LA TATU:

Kusudio la tatu la mnara huu litakuwa kwamba kwenye sehemu ya juu ya ukuta wa mnara huu, saa kubwa itawekwa, ili wanadamu wathamini nyakati zao na wanadamu waelekee kuzingatia wakati.

Kazi hizo tatu zitakazofanyika kwa mnara huu, ndani yake zimefichika hakika tatu:

YA KWANZA

Ni kwamba adhana itakayotolewa kwa sauti kubwa mara tano, ndani yake ukweli huu umefichika kwamba sasa kwa kweli wakati umewadia kuwa sauti ya

لَا إِلَهَ إِلَّا اللهُ مُحَمَّدٌ رَّسُولُ اللهِ
ifikie kila sikio. Yaani, sasa wakati wenyewe unasema kwamba Mungu wa azali na wa kudumu Aliye hai Ambaye kwake Mtume Mtukufu Muhammad ameongoza, minghairi yake miungu wote waliobuniwa ni batili. Kwa nini ni batili? Kwa sababu wanaowaamini hawawezi kupata baraka yoyote kwao wala hawawezi kuonyesha ishara yoyote.

YA PILI
Taa ile itakayowekwa kwenye ukuta wa mnara huu, ndani yake kuna ukweli huu kwamba watu watambue kuwa zama za mwanga wa kimbingu zimefika. Na k**a vile ardhi ilivyosonga mbele katika uvumbuzi wake, ndivyo mbingu pia ulivyotaka kwamba udhihirishe nuru zake wazi wazi sana, ili kwa watafutao ukweli zije tena siku za kustawi, na kila jicho liwezalo kuona na lione mwanga wa kimbingu, na kwa mwanga huo asalimike na makosa.

YA TATU
Saa ile itakayowekwa kwenye sehemu fulani ya ukuta wa mnara huu, ndani yake ukweli huu umefichika kwamba ili watu watambue wakati wao. Yaani waelewe kwamba wakati Wa kufunguliwa milango ya mbingu umewadia. Tangu sasa jihadi ya kiardhi imefungwa na vita vimekwisha.

(Tablighe Risalat, J. 9, uk. 35-36, Tangazo la 28 Mei 1900)

IMEANDALIWA NA MW/Ally Muhammad Kaswezi
Kahama shinyanga Tanzania.

26/03/2024

Haifai kukasirika pindi ukweli unaposemwa ila ni njia ya muungwana kujikwamua kwenye shimo la maafa.

MASWALI NA MAJIBU KATIKA SOMO LA SABA SUNNA NA HADITHI 1. Njia ngapi za kuongoza? Njia za kuongoza ni tatu:- i. Kurani T...
26/03/2024

MASWALI NA MAJIBU KATIKA
SOMO LA SABA SUNNA NA HADITHI

1. Njia ngapi za kuongoza?
Njia za kuongoza ni tatu:-
i. Kurani Takatifu. ii. Sunna. iii. Hadithi.

2. Maana ya Sunna ni nini?
Maana ya sunna ni desturi, lakini neno hili linapotumika katika Kiislamu mradi wake ni desturi za Mtume Muhammad Mtakatifu.

3. Mradi gani katika desturi za Mtume?
Mradi wake ni vitendo vya Mtume alivyofanya zama za uhai wake kwa kuzifuatia amri za Kurani.

4. Faida ya Sunna ni nini?
Tunajua njia ya kufanya vitendo vingi vya sheria ya Kiislamu na njia ya kusali na kutawadha na njia ya kufunga saumu na vinginevyo, kwa sababu ya Sunna.

5. Vifungu vya Sunna ni vingapi? Vifungu vya Sunna ni viwili:-
Fungu la kwanza ni la lazima, k**a rakaa mbili za sunna ya sala ya asubuhi na sunna za sala zingine. Fungu la pili si la lazima k**a kufunga saumu ya siku sita za Shawwal.

6. Je, kufuata sunna ni lazima? Kufuata Sunna za fungu la kwanza ni lazima, na kufuata Sunna za fungu la pili si lazima, lakini k**a mtu akifuata ni vizuri sana.

7. Hadithi ni nini?
Maana ya Hadithi ni maneno, lakini tamko hili katika Kiislamu hutumika hasa kwa maneno ya Mtume Muhammad Mtukufu.

8. Hadithi zimekusanywa lini, na zimeandikwa katika vitabu lini? Zimeanza kukusanywa hata katika siku za Mtume na zimeandikwa vitabuni baada ya kupita miaka 100 kufariki kwake Mtume Muhammad (s.a.w.).

9. Tunawezaje kutambua Hadithi za kweli na zisizo za kweli?
Hadithi inayokuwa sawa na maneno ya Kurani itakuwa ni sahihi na Hadithi isiyo sawa na maneno ya Kurani itakuwa uwongo, maana Mtume Mtukufu s.a.w. hawezi kusema kinyume cha Kurani.

10. Vitabu vya Hadithi ni vingapi? Vitabu vya Hadithi ni vingi sana lakini vitabu vya Hadithi vilivyo mashuhuri ni sita: i. Sahihil-Bukhari, kimekususanywa na Imam Muhammad bin Ismail Bukhari Imam huyu aliza-liwa miaka 194 AH. Na kitabu chake husifiwa sana na husomwa sana.
ii. Kitabu cha Muslim kimekusanywa na Imam Muslim bin Hajjaj na kitabu hiki husomwa sana.

Address

KAGONGWA
Kahama

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ISLAM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share