izack

izack Content actor

Hatua 10 Jinsi ya Kutengeneza Mtoto anayejiaminina Kujitambua Mbele za watu! Sevu au Share isijepotea!Kujiamini siyo kit...
13/07/2025

Hatua 10 Jinsi ya Kutengeneza Mtoto anayejiaminina Kujitambua Mbele za watu! Sevu au Share isijepotea!

Kujiamini siyo kitu ambacho mtoto huzaliwa nacho — ni kitu anachojifunza kwa kupitia malezi, mazingira, na uzoefu wa kila siku. Mtoto anayejiamini huwa jasiri kusema mawazo yake, kuuliza maswali, kuonyesha kipaji chake na kujieleza bila woga mbele za watu. K**a mzazi au mlezi, una nafasi kubwa ya kumjenga mtoto wa aina hii.

(1) Hatua ya Kwanza: Mpe Mtoto Nafasi ya Kujieleza
Usimakatishe mtoto kila mara anapoongea. Mruhusu aseme mawazo yake hata k**a si sahihi. Ukimkata mdomo, atahisi mawazo yake hayana maana.
Mfano wa kufanya:
Badala ya kumwambia “Unasema nini sasa, kaa kimya!” sema “Acha tusikilize kidogo unachotaka kusema.”

(2) Hatua ya Pili: Sifia Juhudi Zake — Siyo Matokeo Tu
Watoto wengi huanza kujiona hawawezi kwa sababu wanasifiwa tu wanapofanya vizuri sana. Sifia hata pale anapojitahidi, sio tu akishinda.
Mfano:
“Umejitahidi sana kufanya hiyo kazi ya shule peke yako, najivunia wewe!”

(3) Hatua ya Tatu: Mpe Majukumu Madogo
Mtoto anapopewa kazi ndogo k**a kumkaribisha mgeni, kutangaza kitu shuleni, au kuongoza wenzake kwenye michezo, hujijengea ujasiri na kujiona ana uwezo.
Anza na majukumu ya familia:
• Kumkaribisha mgeni
• Kuombea chakula mezani
• Kusoma aya ya Quran
Au Mstari wa Biblia mbele ya familia

(4) Hatua ya Nne: Mwonyeshe Mifano Hai ya Kujiamini
Watoto hujifunza kwa kuangalia. Ikiwa wewe mwenyewe una aibu kuongea mbele ya watu, kuwasalimia wageni au kuongea hadharani, mtoto wako naye atakuwa hivyo.
Fanya hivi:
• Muonyeshe jinsi ya kusalimia watu kwa kujiamini
• Ongea naye kwa macho
• Mfundishe jinsi ya kutoa “salamu ya nguvu” (firm handshake)

(5) Hatua ya Tano: Usimlinganishe na Wengine
Kauli k**a “Angalia fulani alivyoongea vizuri mbele ya darasa!” huua kabisa hali ya kujiamini kwa mtoto wako.
Badala yake sema:
“Nilifurahia ulivyothubutu kusimama mbele ya watu, kila mtu alianza hivyo kabla ya kuwa mzuri.”

(6) Hatua ya Sita: Mpe Nafasi ya K

UFANANO WA MWEWE NA B-2 SPIRIT STEALTH BOMBER 1.Ufanano wa Kimuundo:Mwewe na B-2 Spirit wanafanana kwa kushangaza kwa um...
25/06/2025

UFANANO WA MWEWE NA B-2 SPIRIT STEALTH BOMBER

1.Ufanano wa Kimuundo:

Mwewe na B-2 Spirit wanafanana kwa kushangaza kwa umbo la mwili – wote ni aerodynamic, wamesawazishwa ili kupenya hewani kwa kasi na kwa ukimya.

B-2 Spirit ilitengenezwa kwa teknolojia ya hali ya juu sana, lakini ni wazi muundo wake ulivutiwa na ndege wa porini k**a mwewe – viumbe waliobuniwa na maumbile kwa ustadi wa hali ya juu.

2. Kasi, Kimya, na Ushambulizi:

Mwewe anajulikana kuwa ndege mwenye kasi kubwa zaidi duniani, akifikia hadi 390 km/h anaposhambulia mawindo.

B-2 Spirit pia ni ndege ya kimya, inayotumika kwa mashambulizi ya siri (stealth) – haionekani kirahisi na rada.

3. Ufanano wa Majukumu

Mwewe: Anashambulia kimya kimya, anapiga ghafla, na anajua lini pa kushuka.

B-2 Spirit: Inatumwa kwa mashambulizi ya kushtukiza, ikiwa na uwezo wa kubeba silaha nzito zikiwemo za nyuklia, bila kugunduliwa kirahisi.

4. Ujumbe wa Kifalsafa:

🔺 Binadamu na Asili

Picha hii inaonyesha namna ambavyo binadamu anavyojifunza kutoka kwa asili kutengeneza teknolojia – mfano dhahiri wa biomimicry (kuiga maumbile).

Hata baada ya maendeleo ya kisasa ya kijeshi, bado tunarudi kwa viumbe wa asili k**a mwewe kutafuta maarifa.

🔺 Ukali wa Maumbile vs Ukali wa Teknolojia

Mwewe ni mmoja tu, lakini anatosha kutia hofu kwa wanyama wa chini.

B-2 ni mashine kubwa, inahitaji watu kadhaa kuiendesha, lakini kazi yake ni ile ile: kupiga kwa ghafla.

5. Ujumbe wa Mwisho – Uzuri na Hatari

Kuna uzuri wa kimuundo na hatari ya matumizi:

Mwewe ni mzuri, wa ajabu, lakini ni mwuaji wa kipekee.

B-2 Spirit ni muujiza wa uhandisi, lakini huweza kuleta maangamizi makubwa.

Hitimisho

Picha hii ni somo la kuvutia la jinsi teknolojia ya kijeshi inavyoiga maumbile, na inatufundisha kwamba uzuri, kasi, na usiri – vyote vinaweza kutumika kwa ajili ya uhai au uharibifu. Iwe ni mwewe au ndege ya kivita, dhamira iko mikononi mwa anayeendesha.

Simba sc wataenda uwanjani na watawapa Suprise Ambayo hamtaamini Simba sc Amejipanga kwenye huu mchezo kuliko mchezo mwi...
25/06/2025

Simba sc wataenda uwanjani na watawapa Suprise Ambayo hamtaamini

Simba sc Amejipanga kwenye huu mchezo kuliko mchezo mwingine wowote aliowahi kucheza ndani ya hii miaka 4 yaani Juhudi ni kubwa sanaaaa

Na nipo hapa Kuwaambia Baada ya Dakika 90 Yanga sc mtalia kilio cha kusaga Meno

Simba wapo seriously sana na huu mchezo

BADO HUJACHELEWA! HII NI STORY ITAKAYOBADILI MTAZAMO WAKO KUHUSU UMRI NA MAFANIKIO. UNAWEZA BADILI MAISHA UKIWA KATIKA U...
10/05/2025

BADO HUJACHELEWA! HII NI STORY ITAKAYOBADILI MTAZAMO WAKO KUHUSU UMRI NA MAFANIKIO. UNAWEZA BADILI MAISHA UKIWA KATIKA UMRI WOWOTE ULIONAO.

Alizaliwa mwaka 1890 huko Indiana, Marekani. Baba yake alifariki akiwa bado mtoto mdogo, na hivyo alianza kupika kwa ajili ya familia akiwa na miaka 7 tu.

Hakuwa na utoto wa furaha. Alihama shule akiwa na darasa la saba. Alifanya kazi nyingi sana—mtu wa treni, mfagiaji, muuzaji wa bima, dereva wa mashine ya kuchimba barabara. Lakini hakuna hata moja iliyodumu. Aliendelea kufukuzwa kazi au kufeli kila alipojaribu kuanza upya.

Miaka ikaenda. Akiwa na umri wa miaka 40, alianza kuuza chakula cha kukaanga kwenye kituo kidogo cha mafuta alichokuwa anakisimamia. Wageni waliopitia walimpenda sana kwa namna aliyvopika kuku—aliongeza viungo vya kipekee kwa mapishi aliyoyarithi kutoka kwa mama yake. Lakini bado, maisha hayakuwa rahisi.

Wakati akiwa na miaka 65—ndiyo, miaka “65”—serikali ilimkatia pensheni. Alikuwa na dola 105 (sawa na shilingi laki mbili na elfu sabini!) tu mfukoni, hana kazi, hana biashara, hana kitu. Alichoka. Aliona k**a maisha yake hayakuwa na maana tena. Alichukua karatasi na kalamu akaanza kuandika wosia... akiwa amejiandaa kujiua.
Lakini kabla hajatekeleza hilo wazo, kitu ndani yake kilimwambia:

“Sijawahi kutumia kwa nguvu zote kile ninachojua—kupika kuku.”

Akaamka. Akapika kuku kwa ufundi wake ule wa kipekee. Kisha akaanza kupita kwa migahawa mbalimbali, akijaribu kuwashawishi wauze kuku wake kwa mapishi yake.
“Alikataliwa mara 1000” alipoenda katika migahawa tofauti tofauti.
Ndio. Mara “elfu moja”.

Lakini hakukata tamaa. Mwisho wa siku, tajiri mmoja aliyekuwa anamiliki mgahawa mmoja alimkubali. Na hapo ndipo historia ya Kentucky Fried Chicken ilipoanza kubadilika. Alikaanga kuku kwa mchanganyiko wa viungo alivyofanya kuwa ni siri yake. Wateja waliongezeka maradufu, na faida ikapanda mara tatu kwa mwaka. Ndipo akafungua matawi mengine sehemu mbalimbali.

Leo, jina lake linatamkwa katika miji mikubwa, midogo

BY MWALIMU HABELNOAHJM LIBRARYMWANZAMwanamke mmoja alik**atwa na kufungwa gerezani baada ya kukutwa na hatia ya mauaji y...
30/04/2025

BY MWALIMU HABELNOAH
JM LIBRARY
MWANZA

Mwanamke mmoja alik**atwa na kufungwa gerezani baada ya kukutwa na hatia ya mauaji ya mume wake ambaye mwili wake haukuwahi kupatikana.

Baada ya kutumikia miaka takribani kumi (10) gerezani ikaja kubainika yule mwanaume hakufa bali alimtelekeza mkewe na watoto na yeye kwenda kuishi mbali na mchepuko wake.

Ikabidi taratibu za kumtoa gerezani yule mwanamke zifanyike na siku aliyokuwa anatolewa gerezani mume wake alikuwa ni miongoni mwa waliokwenda akiongozana na ndugu zake wengine kwa lengo la kumuangukia mke wake amsamehe kwa kumsababishia matatizo.

Punde yule mwanamke alipotoka getini akiwa amefura na kwa hasira na kukutana uso kwa uso na mumewe alimpokonya mlinzi wa gereza silaha na kummiminia shaba za kutosha mumewe mbele ya ndugu zake na askari wengine asimpe fursa hata ya kufungua mdomo wake mpaka risasi zikaisha. Akawageukia askari akasema "nirudisheni gerezani nikaendelee kutumikia kifungo changu kwa kosa lile lile la kumuua mume wangu. Nimetumikia miaka 10 gerezani bila hatia yoyote sasa narudi tena kwenda kutumikia maisha yangu yote gerezani kihalali"

Akawageukia na wakwe zake waliokuja na mumewe kwa lengo la kumuomba msamaha akawaambia "chukueni mzoga wenu mkazike mlinifunga bila ya kosa hamkutaka kusikia maelezo wala kilio changu nikaacha wanangu wakiwa bado wadogo nashukuru sasa wamekuwa kidogo wanajielewa sitojali km watanihukumu kwa kumuua baba yao sababu baba huyo huyo nilishamuua miaka mingi iliyopita sasa narudi gerezani nikiwa na furaha na amani moyoni.

Unahisi huyo mwanamke alichukua uamuzi sahihi au ungekuwa ni wewe ungefanyaje?

Kijana Asani Mutarika raia wa Malawi anayefanya kazi Afrika Kusini, amerejesha kiasi cha Rand milioni 2 (zaidi ya shilin...
23/04/2025

Kijana Asani Mutarika raia wa Malawi anayefanya kazi Afrika Kusini, amerejesha kiasi cha Rand milioni 2 (zaidi ya shilingi milioni 250 za Kitanzania) alizozikuta kwenye p**a la takataka zilizokuwa kwenye kituo cha biashara cha Olieven Plaza.

Mfanyakazi huyo wa Bustanini alipongezwa na bosi wake kwa uaminifu mkubwa na kupewa zawadi ya vocha ya (Shoprite) yenye thamani ya Rand 500 tu (Zaidi ya 71000/= za Kitanzania) k**a ishara ya kuthamini uaminifu wake.

Tukio hilo limezua hisia tofauti kwa watu, baadhi wakimsifu kwa uaminifu wake, wengine wakimkosoa na kumlaani atakufa masikini.

Ungekuwa ni wewe ungechukua uamzi gani?

Kuna muda tu Wanaijeria wanashindwa kumrate Diamond hadharani k**a moja ya wasanii wakubwa tulionao barani Afrika, wanac...
21/04/2025

Kuna muda tu Wanaijeria wanashindwa kumrate Diamond hadharani k**a moja ya wasanii wakubwa tulionao barani Afrika, wanachojaribu kukifanya ni kulinda zaidi kiwanda chao ila wanakubali kiaina k**a Chid alivyowahi kuimba😂

Wakati Diamond anatua kwenye Ardhi ya Nigeria, siku 4 zilizopita, kuhudhuria harusi ya rafiki yake, Jux, Wa-Nigeria huko X wakaanza kutahadharisha wasanii wao kuwa wanapaswa kuwa makini na projects zao kwasababu kubwa la maadui limetua nchini mwao kusepa na nyimbo zao😁.

Project ya mwisho ambayo Diamond alishambuliwa na WaNigeria, ilikuwa ni Yataniua akiwa na Mbosso, wakidai amesample wimbo wa Asake.

Tazama kwenye comments

UKOMAVU ZAIDI KIAKILI UNAHITAJIKA ILI TUCHEZE FAINALI CAF!🎙” Hii ni michuano ya CAF, Nusu Fainali ilikuwa muhimu sana ku...
21/04/2025

UKOMAVU ZAIDI KIAKILI UNAHITAJIKA ILI TUCHEZE FAINALI CAF!

🎙” Hii ni michuano ya CAF, Nusu Fainali ilikuwa muhimu sana kutoruhusu bao la kufungwa, tulifanikiwa katika hilo na hawakuwa na nafasi za kufunga isipokuwa hatari yao katika mipira mirefu ya kurusha”

“komavu kiakili na ukatili unahitajika kuicheza michezo ya Nusu Fainali kwa sababu unapokwenda ugenini haujui hali itakuwaje, haujui kiwanja kitakuwaje...mfano leo eneo la kuchezea...mvua ilinyesha karibu siku nzima, hatukuweza kucheza kwa uhuru mpira wetu”

“Lakini achilia yote hayo...Mimi nina furaha na kiwango chetu leo (Jana), lakini kiujumla ni muhimu kutambua Ukomavu wetu kimchezo unapaswa kupanda gia za juu zaidi iwapo tunataka kucheza Fainali...”

Fadlu Davids - Kocha Simba SC baada ya Ushindi v Stellies hio jana.

Michuano ya kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC) inaendelea tena leo Aprili 20, 2025 kwa michezo ya mkondo wa kwanza wa ha...
20/04/2025

Michuano ya kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC) inaendelea tena leo Aprili 20, 2025 kwa michezo ya mkondo wa kwanza wa hatua ya nusu fainali ambapo wawakilishi pekee wa Tanzania kwenye michuano hiyo, Simba Sc watatupa karata yao ya kwanza kwenye nusu fainali.

Simba Sc itakuwa mwenyeji wa Stellenbosch ya Afrika Kusini katika dimba la New Amaan Complex, Zanzibar majira ya saa 10:00 jioni ikiangazia kutumia vyema uwanja wa nyumbani kumaliza shughuli kabla ya marudiano wiki ijayo.

Katika mchezo mwingine, Mabingwa mara mbili wa CAFCC, RS Berkane ya Morocco watakuwa wenyeji wa CS Constantine ya Algeria katika dimba la Manispaa ya Berkane kabla ya kurudiana Aprili 27, 2025 katika dimba la Mohamed-Hamlaoui, Algeria.

16:00 Simba Sc 🇹🇿 vs 🇿🇦 Stellenbosch
🏟️ New Amaan Complex, Zanzibar

22:00 RS Berkane 🇲🇦 vs 🇩🇿 CS Constantine
🏟️ Stade Municipal de Berkane

Caen FC Klabu inayomilikiwa na Kylian Mbappé imeshuka daraja kutoka Ligue 2 mpaka Nacional League huko nchini Ufaransa.U...
20/04/2025

Caen FC Klabu inayomilikiwa na Kylian Mbappé imeshuka daraja kutoka Ligue 2 mpaka Nacional League huko nchini Ufaransa.

Upande wa pili pia klabu yake ya Real Madrid C.F. nayo imetolewa UEFA champions league

huyu hapa mpenz mpya wake haji manala
20/04/2025

huyu hapa mpenz mpya wake haji manala

Address

Katoro

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when izack posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to izack:

Share