20/12/2025
*KINGA RAHISI KWA MTOTO WAKO*
👉 Leo nakuelekeza kinga rahisi sana kutengeneza lakini ni imara sana kwa maadui wa mwanao iwe majini au wachawi.
👉 Tafuta pangaa ya mbaazi na mkilika tu k**a utakosa pangaa tumia mizizi yake, pia utachukua majani yake hiyo miti.
👉 Majani twanga kwenye kinu (sio blender tafadhali) weka maji kisha zima makaa 7 kwa nia za kuzima kila ubaya aliofanyiwa, anaofanyiwa, na atakaofanyiwa popote pale.
👉 Baada ya hapo utamuogesha dawa hiyo mwanao akiwa mlangoni anatazama nje nawe uvae kaniki juu na chini.
👉 Baada ya kumuogesha utakata kipande kidogo sana cha mkilika na mbaazi pangaa au mzizi, kisha chukua kipande kidogo sana cha mkaa ule uliozimia dawa.
👉 Vipande hivyo vyote vifunge katika nailoni ngumu ili visiloane kisha funga katika kitambaa cheusi kwa manuizi ya kuufunga kila ubaya dhidi ya mwanao.
👉 Hakikisha umekaza sana fundo na iwe ndogo tu k**a punje ya choroko.
👉 Baada ya hapo mvalishe mwanao iwe mkononi au kiunoni au shingoni, lakini vizuri avae isionekane na walimwengu.
👉 Kwa wale wasomaji hii unaisomea Yasin moja ila ukifika Mubiyn unatia nia na kupulizia fundo kisha unaanza upya Yaasin mpaka ya Mubiyn ya pili unafanya k**a awali kisha unaanza upya Yaasin mpaka Mubiyn ya tatu unaanza upya, nenda na utaratibu huo mpaka umalize surat Yaasin ndipo umvalishe.
👉 Ndugu yangu huyo mtoto watamwita mchawi au wewe utaitwa mchawi kwa sababu hii;
👉 Inazuia ubaya wowote usimfike mtoto biidhinillah na pia inaua ubaya wowote ambao aliwahi kufanyiwa
👉 K**a mtoto alikuwa haishi kuumwa yaani kila siku anaumwa hapo ndio mwisho
👉 K**a mtoto alikuwa anastuka na kulia sana usiku hapo ndio mwisho
👉 K**a mtoto alikuwa anaogopa sana watu ile hofu isiyo kawaida basi hapo ndo mwisho
👉 K**a mtoto afya imezorota kichawi yaani haumwi lakini hanenepi hapo ndo mwisho
👉 K**a mtoto alikuwa anachukuliwa kichawi hapo ndo mwisho maana kuna watu mnalala na watoto wenu vizuri usiku ukiamka unamkuta mtoto uvunguni na mtoto hatembei wala hatambai