Mimi niko ambaye niko

  • Home
  • Mimi niko ambaye niko

Mimi niko ambaye niko Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Mimi niko ambaye niko, MLOLE, .

23/08/2025

IBADA YAKO YA KESHO IKAWE YENYE BARAKA NA MAJIBU KWAKO

NENO LA LEOMWANADAMU WEW NI K**A MAUA LEO UPO KESHO HAUPO CHAGUA FUNGU LILILO JEMA NA FUNGU HILO NI KUMWAMINI BWANA YESU...
23/08/2025

NENO LA LEO
MWANADAMU WEW NI K**A MAUA LEO UPO KESHO HAUPO CHAGUA FUNGU LILILO JEMA NA FUNGU HILO NI KUMWAMINI BWANA YESU KRISTO PEKEE.

WEW NI MAUA TU MPENDWA HATA MIMI PIA NI K**A MAUA LEO TWAONENKANA TUNA PENDEZA JE KESHO YAKO /YANGU INAKUWAJE

UNAIJUWA KESHO YAKO /NINAIJUWA KESHO YANGU?

NIHELI MPENDWA KUACHANA NA YA DUNIA NA KUMWAMINI YESU KRISTO YEYE AMBAYE NI MWOKOZI WETU

USI SHUPAZE SHINGO LAKO KWA KUYAFUATIA YA ULIMWENGU

KUMBUKA KILA KITU KINA PITA JE UTAKUWA MTU WA NANI UTAKUWA MGENI WA NANI KAKA NA DADA YANGU

NI HERI UMKABITHI BWANA NAFASI KATIKA MAISHA YAKO

UPO LEO NI KWA NEEMA TU UMEPEWA NEEMA ILI UWEZE KUKAMILISHA PALE AMBAPO BADO

LAKINI JE K**A UTASHINDWA KUKAMILISHA NA MUDA WAKO UKIISHA UTAJIBU NINI KWAKE?

K**A KUHUBIRI MPAKA MITANDAONI TUMEKUFIKIA KWANINI USIKUBARI KUGEUKA? 😭😭😭

CHAGUA LEO FUNGU JEMA MWANA WA MUNGU.
✍️ 0787 658 269

06/08/2025
π™ˆπ™Šπ™”π™Š π™π™‡π™„π™Š π™…π™€π™π™π™ƒπ™„π™’π˜Ό πŸ•ŠοΈMoyo uliojeruhiwa ni moyo uliovunjika, ulioumizwa na mateso, kukataliwa, huzuni au dhambi. Lakini B...
26/07/2025

π™ˆπ™Šπ™”π™Š π™π™‡π™„π™Š π™…π™€π™π™π™ƒπ™„π™’π˜Ό πŸ•ŠοΈ
Moyo uliojeruhiwa ni moyo uliovunjika, ulioumizwa na mateso, kukataliwa, huzuni au dhambi. Lakini Bwana Yesu haachi mioyo hiyo k**a ilivyo β€” Yeye ni mponyaji wa waliovunjika moyo.

Zaburi 147:3
"Huponya waliovunjika moyo, na kuwafunga jeraha zao."

Usikate tamaa…
Jeraha lako lina maana mbele za Mungu.
Ukimkaribia, atayagusa yale maeneo yanayouma zaidi.
Yupo karibu na wale waliovunjika moyo, na atakufariji kwa upendo wake wa milele.

πŸ™ Mwache Yesu auponye moyo wako leo.
🌿 Maumivu yako si ya bure β€” ni sehemu ya ushuhuda wako utakaokuletea uzima mpya.
0787 658 269

SOMO: π™’π˜Όπ™π™ π™’π˜Όπ™‡π™„π™Š π™„π˜½π™„π™’π˜Ό π™‰π˜Ό π™†π™π™π™€π™†π™’π˜Ό-π™‡π˜Όπ™†π™„π™‰π™„ π˜½π˜Όπ˜Ώπ™Š π™‡π™„π™†π™Š π™π™π™ˆπ˜Όπ™„π™‰π™„Andiko Kuu: Isaya 42:22> β€œLakini watu hawa ni watu walioibiwa ...
26/07/2025

SOMO: π™’π˜Όπ™π™ π™’π˜Όπ™‡π™„π™Š π™„π˜½π™„π™’π˜Ό π™‰π˜Ό π™†π™π™π™€π™†π™’π˜Ό-π™‡π˜Όπ™†π™„π™‰π™„ π˜½π˜Όπ˜Ώπ™Š π™‡π™„π™†π™Š π™π™π™ˆπ˜Όπ™„π™‰π™„
Andiko Kuu: Isaya 42:22
> β€œLakini watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa; wote wamenaswa katika mashimo, wamefichwa katika magereza; wamekuwa mawindo, wala hapana aokoaye; wamekuwa mateka, wala hapana asemaye, Rudisha.”

1. UTANGULIZI

Katika andiko hili, Nabii Isaya anaonyesha hali ya huzuni ya watu wa Mungu waliotumbukia kwenye mateso, kifungo na maangamizi kwa sababu ya uasi wao na kuachana na mapenzi ya Mungu. Hili pia ni onyo na wito wa toba kwa vizazi vyote. Hali hii ya β€œkutekwa na kuibiwa” siyo tu ya kimwili bali pia ni ya kiroho.

2. MAANA YA MANENO MUHIMU

Kuibiwa na kutekwa – Kupoteza vitu vya thamani (neema, baraka, amani, nafasi) kwa sababu ya dhambi au uvamizi wa kipepo.

Wamenaswa katika mashimo – Kutumbukia katika hali ya giza, tamaa, uovu au mateso.

Wamefichwa katika magereza – Kufungwa kiakili, kihisia au kiroho; maisha bila uhuru wa kweli.

Wamekuwa mawindo, hapana aokoaye – Wamekuwa walengwa wa adui, na hakuna wa kuwatetea.

Wamekuwa mateka, wala hapana asemaye 'Rudisha' – Hawana hata wa kusimama kwa maombi au utetezi ili kurejeshewa walichopoteza.

3. HALI ZINAZOCHANGIA KUWA MATEKA

Kuacha njia za Mungu (Zaburi 107:10-11)

Kutotii Neno la Mungu (Yeremia 5:23-25)

Kuishi maisha ya dhambi bila toba (Warumi 6:16)

Kujiingiza kwenye mapepo, laana au ibada za sanamu

Kutokuwepo kwa maombezi na walinzi wa kiroho

4. MATOKEO YA KUWA MATEKA AU MAWINDO YA ADUI

Kupoteza mwelekeo wa maisha

Kuishi maisha yasiyo na tija wala furaha

Kuogopa na kukata tamaa

Kuishi chini ya vifungo visivyoelezeka

Kukosa msaada na tumaini

5. TUMAINI LIPO: YESU NDIYE MWOKOZI

Yesu Kristo alikuja "kuwafungua mateka" (Luka 4:18). Yeye ndiye anayeweza kusema β€œRudisha!” kwa yale yote uliyoibiwa na adui:

Rudisha afya

Rudisha amani

Rudisha ndoa yako

Rudisha huduma yako

Rudisha heshima yako

Rudisha kibali na baraka zako

6. NINI TUFANYE ILI KUREJESHEWA?

βœ… Tubu na umrudie Mungu (Yoeli 2:12-13)
βœ… Omba kwa bidii na shauku ya kweli (Yeremia 33:3)
βœ… Paza sauti kwa imani: β€œRudisha!” (Yoeli 2:25)
βœ… Kaa kwenye Neno la Mungu
βœ… Tafuta msaada wa kiroho – wachungaji, waombezi, watakatifu waaminifu
βœ… Usikubali kukaa kimya – simama k**a mpiga kelele kwa ajili ya wokovu wako

7. HITIMISHO

Isaya 42:22 si tu taarifa ya huzuni, bali ni mwito wa toba, uamsho na vita vya kiroho. Mungu anatafuta mtu mmoja tu atakayesimama katika mwanya na kusema kwa mamlaka ya kiroho:
β€œRUDISHA!”

Usikae kimya, simama kwenye maombi na imani ukidai kurejeshewa chochote kilichoibiwa katika maisha yako, familia yako au huduma yako.

MAOMBI YA MWISHO

Ee Bwana, najua nimepoteza vitu vingi katika maisha yangu, lakini leo ninainuka kwa imani na ninatangaza: Rudisha afya yangu, rudisha furaha yangu, rudisha huduma yangu, rudisha baraka zangu, kwa jina la Yesu Kristo. Amen.
π™ˆπ™–π™¬π™–π™¨π™žπ™‘π™žπ™–π™£π™€ π™₯π™žπ™œπ™–
0787 658 0787 658 269

NAMNA YA KUOMBA UKIWA KWENYE MAJARIBU...  Somo hili Lina part 2 usikose Katika Somo hili kuna mambo kadhaa pia tutayaang...
20/06/2025

NAMNA YA KUOMBA UKIWA KWENYE MAJARIBU...
Somo hili Lina part 2 usikose

Katika Somo hili kuna mambo kadhaa pia tutayaangalia nayo NI k**a hivi yafuatavyo.........
1Nini maaana ya karibu
2Namna ya Majaribu yanavyo kuja
3Lengo la Majaribu.

Tuanze kabisa kuangalia nini maana ya Majaribu πŸ€”
MAJARIBU ➑️Ni Mtihani wa Imani zetu au ,Ni Kipimo cha Imani zetu
K**a Mtu unaye mwamini Kristo Majaribu kwako nikwamba huo NI Mtihani wako WA kupima Imani yako katika Yesu ,kuangalia je Kweli wampenda Yesu au waigiza na je Kweli Huwezi kumuacha na kugeukia kungine mfano,Kwa waganga ,miungu NK

Mfano ,Kwanini shuleni Mwanafunzi hupaswa kupewa Mtihani ?
Nikwa sababu moja Tu kumpima k**a Mwanafunzi anaelewa na kile ambacho mwalimu amekuwa akifundisha Kila SIKU na Mwanafunzi Huyo anapo Fanya vizur ,mwalimu hujisikia vizuri,na kusema kwamba hakika Mwanafunzi Huyu alikuwa anasoma na alielewa vyema Somo.

Kwa mtu ambaye amemwamini Kristo kuwa Bwana na Mwokozi WA MAISHA yake nilazima ajaribiwe ,ili ijulikane Huyu mtu amesimamia wapi!, utaona ata watu wengi walio mcha Mungu walipitia Majaribu mbalimabali hiyo ikionyesha kwamba wanapimwa katika Imani zao

SASA EMBU TUANGALIE JINSI MAJARIBU YANAVYO KUJA AU YANAKO TOKA. (KATIKA SEHEMU TATU 3)
Kwanza kabisa unatakiwa kuelewa kwamba kuna Aina 3 za Majaribu ambavyo yanakuja Lakin WATU wengi tumekuwa tuki SEMA kwamba Majaribu hayo hutoka moja Kwa moja Kwa shetani ,Lakin Leo Naomba tuangalie HAPA ,,

1️⃣MAJARIBU YANA TOKA KWA SHETANI.
Hii ni Njia ya Kwanza ambayo unatakiwa kufahamu kwamba Majaribu hutoka Kwa shetani,na SIKU ZOTE Majaribu yanayo TOKA kwahuyu Shetani sikuzote yanakuja Kwa lengo la kukutenganisha wew na Mungu kuvunja Mahusiano yako kabisa kuharibu mpango WA MUNGU katika MAISHA yako kuharibu Kila KITU
Mfano NI HAPA Kwa Yesu mwenyewe.
Mathayo 4
3 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate.
4 Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.
5 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu,
6 akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
7 Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.
8 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake,
9 akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.
10 Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.

Ukisoma Kwa makini Hapo katika MATHAYO 4;1-10
Utagundua Huyu Shetani analeta jaribu Kwa Yesu Kristo ILI atakapo kubali na kumsikiliza BASI mpango wa MUNGU kukomboa mwanadamu uharibike,Shetani aliona kwamba Yesu amekuja kuharibu KAZI yake kwahiyo kaamua kwenda kumjaribu ILI aone k**a atambahatisha na KAZI ya ukombozi iishie Hapo.

2️⃣MAJARIBU YALETWAYO,AU YASABABISHWAYO NA MWILI WAKO.
Kunamtu atashangaa Sana kwamba inawezekanaje kujaribuwa Kwa mwili wangu?
Lakin Sikia nikwambie ,Kunamajaribu ambayo mwili wako huo ndio husababisha ,na wew USIPO Elewa BASI moja kwamoja unaingia dhambini ,
Mfano ,Unaanzisha Mahusiano wew na Binti/kijana Lakin Muda wa kuona mnaona kabisa bado,mnaanza KUWA na maongezi nyeti yanayo pelekea kuwasha tamaa za miili yenu ,hatimae mnakubaliana na matokeo yake mna sexy ! Je Hapo NI jaribu KUTOKA Kwa shetani au Ni miiliyenu mliyo chochea vitu vya tamaa ?
Yakobo 1
13 Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu.
14 Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.
15 Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.
Naamini Hapo kunakitu umekielewa wew mwenyewe kwamba yawezekana Kabisaaa Majaribu kuletwa na miili yetu tamaa kuwaka ndani yako unatamani kitu usichokuwa na uwezo nacho.

3️⃣MAJARIBU YALETWAYO NA MUNGU MWENYEWE.
Mwana wa MUNGU,nataka nikwambie kwamba Mungu humjaribu Mtumishi wake ,na hata wew Mungu anaweza akawa amekujaribu Kwa jaribu furani,Na jaribu analo kusudia Mungu juu ya MTU ANAKUWA anamaana kubwa Sana kwake
Anakuwa na mpango WA kumtoa Hapo na kumpeleka viwango vingine inawezekana Huyo mtu akaumia Sana akalia ,Lakin Mungu anakuwa na kusudi maarumu,
Mfano.
Yusufu kuuzwa utumwani KULIKUWA jaribu la moja Kwa moja KUTOKA Kwa Mungu,MUNGU AKIWA na mpango WA kumpeleka Yusufu ILI akawe waziri mkuu.
Mwanzo 37
5 Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari, nao wakazidi kumchukia;
6 akawaambia, Tafadhalini, sikieni ndoto hii niliyoiota.
7 Tazama, sisi tulikuwa tukifunga miganda shambani, kumbe! Mganda wangu ukaondoka ukasimama, na tazama, miganda yenu ikazunguka ikainama mbele ya mganda wangu.
8 Ndugu zake wakamwambia, Je! Kweli wewe utatumiliki sisi? Nawe utatutawala sisi? Wakazidi kumchukia kwa ajili ya ndoto yake, na kwa maneno yake.
9 Akaota tena ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake, akasema, Angalieni, nimeota ndoto nyingine; na tazama, jua na mwezi na nyota kumi na moja zikaniinamia.
10 Akawaambia baba yake na ndugu zake; baba yake akamkemea akamwambia, Ni ndoto gani hii uliyoiota? Je! Mimi na mama yako na ndugu zako tutakuja tukusujudie hata nchi?
Hiki ndicho kilicho MFANYA ndugu wa Yusufu kumchukia na kumuuza utumwani Lakin kwake Yusufu lilikuwa jaribu kubwa Sana ,Lakin Lilitokea KWAMUNGU ILI amfikishe alipo kusudia

Mwingine NI Huyu
Mwanzo 22
1 Ikawa baada ya mambo hayo Mungu alimjaribu Ibrahimu, akamwambia, Ee Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.
2 Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.
3 Ibrahimu akaondoka alfajiri, akatandika punda wake, akachukua vijana wawili pamoja naye, na Isaka mwanawe, akachanja kuni kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka, akaenda mpaka mahali alipoambiwa na Mungu.
15 Malaika wa Bwana akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni
16 akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,
17 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako k**a nyota za mbinguni, na k**a mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;
18 na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.
Naamini Hapo umeona ,baada ya kushinda huo Mtihani Mungu anaamua kufunguka juu ya Ibrahim Kwa alicho kufanya juu yake

INAWEZEKANA KUNA MAHALI UNAPITIA NA HILO JARIBU K**A NI LA KIMUNGU HUPASWA KULIKEMEA NA KULIKATAA ISIPOKUWA KUNA NAMNA YA KUOMBA ,MAANA UNAWEZA UKAWA UNAPITIA JARIBU AMBALO MBELEN KUNA BARAKA ZAKO NA KUINUKIA KWAKO SASA UTAKAPO LIKEMEA MAANA YAKE HUTAZIONA HIZO BARAKA ,KWAHYO LITAMBUE JARIBU LAKO K**A LATOKANA NA MUNGU AU SHETANI AU MWILI WAKO KISHA UJUWE NI NAMNA GANI YA KULIOMBEA.

K**A UNAHITAJI MAOMBI ,USHAURI ,MAOMBI NK
NIPIGIE KWA NAMBA HII NAMI NITAKUHUDUMIA
NIMEPEWA BURE NA NINATOA BURE
0787 658 269

19/06/2025

TUISHI KWA UPENDO
0787 658 269

03/06/2025

Hesabu 23
19 Mungu si mtu, aseme uongo; Wala si mwanadamu, ajute; Iwapo amesema, hatalitenda? Iwapo amenena, hatalifikiliza?

Somo letu la Leo .MAMBO YALETAYO BARAKA KWA KILA AMWAMINIYE KRISTO AU KWA KILA ALIYE OKOKA. Bwana Yesu asifiweeee Sana M...
03/06/2025

Somo letu la Leo .
MAMBO YALETAYO BARAKA KWA KILA AMWAMINIYE KRISTO AU KWA KILA ALIYE OKOKA.

Bwana Yesu asifiweeee Sana Mwana wa MUNGU πŸ€—
Leo nataka tukaangalie baadhi ya mambo ambayo yatamfanya MUNGU kuachilia Baraka katika MAISHA YAKO endapo wew utayazingatia na kutembea nayo siku zote.

Kwanza kabisa Jambo namba moja litakalikuwa chanzo cha MUNGU Kukubariki katika maisha yako,au kumfanya MUNGU aachilie Baraka kwako NI

➑️KUMTEGEMEA MUNGU KWA KILA JAMBO.
Wana wa MUNGU hii Njia huwa inamfanya MUNGU kumbariki mtu anaye mtegemea ,na tena amesema mwenyew yakwamba yeye asiye mtegemea melaaniea Lakin Yeye amtegemea amebarikiwa ,SASA hapa yatonyesha wazi kwamba MOJA Kati ya mlango unao tufungulia Baraka NI Kwa kumtegemea MUNGU Kwa kila Jambo.

Yeremia 17
5 Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana.

6 Maana atakuwa k**a fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.

7 Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake.

8 Maana atakuwa k**a mti uliopandwa kando ya maji, Uenezao mizizi yake karibu na mto; Hautaona hofu wakati wa hari ujapo, Bali jani lake litakuwa bichi; Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, Wala hautaacha kuzaa matunda.

πŸ‘‰Huyo MTU anaye mtegemea MUNGU kunakipindi anaweza akapitia kigumu ,kwake kikawa afadhar Sana kuliko Yule ambaye amemuacha Mungu Kwa kuwategemea wanadamu,Kwanza MAISHA yake yatakuwa yamashaka yasiyo na tumaini ,Lakin amtegemea Mungu anakuwa na tumaini la NENO LA Mungu maana Mungu ameahidi Baraka kwake amtegemeae.

Njia ya pili au Jambo la pili linaloweza kumfanya AKUBARIKI NI

➑️UTAKATIFU,KUWA MBALI NA KILA MACHUKIZO KWA MUNGU.
Bwana Yesu asifiweeee
Endapo SASA utaishi MAISHA Ya UTAKATIFU,Yaani mala Kwa mala ukiwa MTU WA hofu ,ukihofu na kuogopa kumtenda Mungu dhambi BASI ,UTAKUWA chanzo cha Yeye Kukubariki
Shika amri zake,Tii NENO lake,sikia sauti yake NA Tenda NENO lako ,BASI Hapo Baraka utaziona.
Kumbukumbu la Torati 28
1 Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;

2 na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.

3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.

4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng'ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.

➑️KUTO KUMSAHAU MUNGU WAKATI WA ,RAHA,MAFANIKIO,AMANI NA KUTAJIRIKA KWAKO.

Hallelujah Mwana wa MUNGU πŸ€—
Hapa WATU wengi wamepigwa Sana kwakumsahau Mungu Baada ya Mungu kuwatendea nao wakamsahau nakumuacha ,ndipo uharibifu ukaanzia Hapo.
Lakin k**a hutaki kupona uharibifu BASI Rudi Leo na utrngeneze mahali palipo bomoka Mwana WA MUNGU.
Kumbukumbu la Torati 8
11 Jihadhari, usije ukamsahau Bwana, Mungu wako, kwa kutozishika amri zake, na hukumu zake, na sheria zake, ninazokuamuru leo.

12 Angalia, utakapokuwa umekula na kushiba, na kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake;

13 na makundi yako ya ng'ombe na kondoo yatakapoongezeka, na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka, na kila kitu ulicho nacho kitakapoongezeka;

14 basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau Bwana, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa;

15 aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji; aliyekutolea maji katika mwamba mgumu,

MWISHO
MUNGU WAMBINGUNI AKUBARIKI SANA KWA KUSOMA MPAKA MWISHO ,SHARE UJUMBE HUU KWA WENGINE,NAPIA USISAHAU KUNIFOLLOW KATIKA ACCOUNT HII ..

KWA MAWASILIANO USISITE KUNIPIGIA ,KWA USHAURI NA MAMBO MENGINE PIGA NAMBA. 0787 658 269
Na Pasta Moses Godwin

11/02/2025

Salamu wafuasi wangu wapya! Nina furaha kuwa nanyi! Agnes Samwel, Paulo Chgu Hm, Evelyne Naliaka, Mfuasi Wa Bwana Yesu, Manase Akyoo, Justina Mkombo, Lindah Lindah, Agatha Rukigwa, Steve Mteule

07/02/2025
07/02/2025

Yohana 3
20 Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa.

Address

MLOLE

Telephone

+255787658269

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mimi niko ambaye niko posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share