08/03/2026
Katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amemkabidhi mama mzazi wa marehemu Steven Kanumba gari jipya aina ya Toyota Harrier (New Model).
Hatua hiyo imeelezwa kuwa ni sehemu ya kuthamini mchango mkubwa alioutoa marehemu Kanumba katika kukuza tasnia ya filamu nchini na kuenzi alama aliyoiacha katika sanaa ya Tanzania.
Inaelezwa kuwa zawadi hiyo imekuja kufuatia ombi la Mama Kanumba kwa Rais Samia, ambapo alieleza changamoto ya usafiri anayokutana nayo kutokana na umri wake mkubwa.
Akizungumza baada ya kupokea zawadi hiyo, Mama Kanumba alimshukuru Rais Samia kwa moyo wa upendo na kujali, akisema gari hilo litamsaidia kurahisisha shughuli zake za kila siku ambazo hapo awali zilikuwa zikimpa changamoto ya usafiri.