Kemo tv

Kemo tv hot news

Barcelona hawashikiki msimu huu, wamemshushia mtu pigo la umbwa koko...
30/03/2025

Barcelona hawashikiki msimu huu, wamemshushia mtu pigo la umbwa koko...

LAMINE! LAMINE! LAMINE! 1-0 BARΓ‡A! πŸ”΅πŸ”΄
30/03/2025

LAMINE! LAMINE! LAMINE! 1-0 BARΓ‡A! πŸ”΅πŸ”΄

RASHFORD AIPELEKA ASTON VILLA NUSU FAINALI YA FA.Man U. Washtuka, kumbe bado kijana ni wa moto!
30/03/2025

RASHFORD AIPELEKA ASTON VILLA NUSU FAINALI YA FA.

Man U. Washtuka, kumbe bado kijana ni wa moto!

🚨Jack wilshere: to Arsen Wenger,  Mikel Arteta and the arsenal fans
30/03/2025

🚨Jack wilshere: to Arsen Wenger, Mikel Arteta and the arsenal fans

STORY: HOUSE GIRL BIBI {10}NA: ASHROUPH K.A https://youtu.be/7EKvuOen1rM?si=jVxEt-ZNX5Z5cnJCPale pale niliichukua simu y...
07/12/2024

STORY: HOUSE GIRL BIBI {10}

NA: ASHROUPH K.A

https://youtu.be/7EKvuOen1rM?si=jVxEt-ZNX5Z5cnJC

Pale pale niliichukua simu yangu na kumpigia mama yangu. Lakini cha kushangaza, alipokea nakuzidi tu kucheka simuni huku akisema,

"Deo, hivi huyo bibi anakupa nini kikubwa hivyo!? Mbona unampenda kupita maelezo! Eenh..! nidanganye tena kuwa haumpendi. Nidanganye, nidanganye tu baba'angu!".

Maneno hayo ya mama yalizidi kunichanganya maradufu. Nikajua kuwa, rafiki yangu Chichi kani double cross. Lazima mama kautumia udhaifu wa Chichi wa kupenda hela, ili tu anibananishe.

Nilikata simu ile niliyokuwa nimempigia mama yangu, kisha nikaipigia simu ya Chichi muda huo huo, nikakuta Chichi akiwa anatumika. Na nilipojaribu tena nikaambiwa namba haipatikani.

Aloo! Nilizidi kuchemkwa na jasho pale kitini nilipokuwa, na ukizingatia msimu huo ulikuwa ni wa joto kali ndani ya jiji la Dar.

Watu walihisi k**a sipo sawa hivi, maana hata macho yangu yalikosa kabisa utulivu. Nikawa na angaza angaza huku na kule k**a mwizi.

Ndipo Patron akaja pale nilipokuwa nimeketi na kuniletea chupa kubwa ya maji ya Kilimanjaro. Huku akisema,

"Kijana, acha presha. Hii ni graduation sio ndoa, mbona una wenge namna hii!?". Nilimtizama kwa jicho kali na kumsonya, maana huyo naye ni wale wale vibaraka wa mama.

Bhasi, sherehe ili pamba moto, japo kwa upande wangu nilitamani ishe mapema ili nikasikie atakacho kisema mama yangu. Japo sitaki kukuficha, awamu hii niliamua iwe, ubaya ubwela. Maana mama mwenyewe haogopi. Siananichimba chimba ili mradi aniharibie penzi langu kwa Bi. Theodora!?

Ngoja nimkomeshe! Deo nilikata shauri.

Bhasi bhana, tulitunzwa zawadi zakutosha sana. Kisha Mgeni rasmi ambaye alikuwa pia ni mbunge na mfanyabiashara mkubwa wa kampuni la kiteknolojia liitwalo R.Z.J mheshimiwa Kombo Abdallah M. Alituhutubia hotuba nzuri sana. Yote kwa yote akituhimiza tuzipambanie ndoto zetu. Wala tusikubali mtu aturudishe nyuma kwa namna yeyote ile.

Wakati hotuba hii ikitolewa, nilibahatika kugonganisha macho yangu na ya mama. Kisha nikanoti jambo fulani kwa mama huyo. Mara moja nikachukua simu na kumtumia mama ujumbe mfupi wa meseji uliosomeka hivi,

"Mama. Sipo tayari uikwamishe ndoto yangu. Nitapambana hadi kieleweke. Theodora ndiye mke wa chaguo la moyo wangu. Mwambie hata baba naye ajue. Sina shida tena na utajiri wenu, wacha nikatesekee pendo langu!".

Wala hakunijibu. Bali alituma tu emoji ya makopa kopa. Nikazidi kuisoma akili yake.

**

Siku hiyo usiku, baba yangu aliwaalika matajiri wenzake wa maeneo yale ya mbezi beach tulipokuwa tukiishi. Kisha akanunua vinywaji k**a kawaida yake. Akataka sote tunywe kwa kusherehekea matokeo yangu. Lakini, wakati tukiwa katikati ya sherehe, nilishangaa kumuona mwanasheria wa baba akiingia nyumbani hapo na makabrasha kibao ya kisheria. Alafu akamsogelea baba na kumnong'onezana jambo la siri sikioni.

Baba akainuka juu na kusema,

"Aidha, nipende kiitumia siku hii ya leo kumsainisha mwanagu Deogratias k**a mrithi namba moja na namba mbili wa mali zangu zote. Hivyo. Deo mali hizi ni zako sasa!". Baba aliongea, nami nikaitwa mbele ya ukumbi huo wa nyumbani. Nikaonyeshwa sehemu ya kusaini na kuweka fingerprint yangu. Mama akabaki tu amepigwa na butwaa, kwani hakutarajia kuwa, baba angelifanya jambo hilo adhimu kwa siku hiyo.

Mchezo ukawa umekwisha. Alama zote tatu nikazikomba mbele ya macho ya mama yangu. Akawa hana la kunambia tena. Maana alishaitambua nguvu yangu kuanzia hapo.

Deo nikawa rasmi tajiri mtoto. Maana baba alinikabidhi utajiri wenye thamani ya zaidi ya shingingi bilioni kumi za kitanzania.

"Ahsante mungu, kilichobaki nikumsaka Theodora wangu. Ili maisha yaendelee maana k**a ni mali tayari ninayo kibindoni", hovi ndivyo nilivyokuwa nikijiwazia kichwani kwangu kila sekunde. Maana sio siri nilikuwa nikimpenda Theodora kupita kiasi, licha ya umri wake ule mkubwa aliokuwa nao....ITAENDELEA

Chimba dawa, safari iendelee.

Pata full story kwa kulipia Tsh 1000/=

Kwenda namba hizi

Kwetu hadithi ni burudani yenye soma zito ndani yake. Karibu tuelimike.

Malenga mwenye kalamu iliyosahaulika nyikani!

Done deal Awesu Ali Awesu ni πŒππ˜π€πŒπ€.
17/07/2024

Done deal
Awesu Ali Awesu ni πŒππ˜π€πŒπ€.

Saa chache baada ya Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es salaam kuamuru Rais wa Club ya Yanga Hersi Saidi na wenzake k...
17/07/2024

Saa chache baada ya Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es salaam kuamuru Rais wa Club ya Yanga Hersi Saidi na wenzake kuachia ngazi kutokana na kuwepo madarakani bila kufuata katiba ya Club hiyo, hivi ndivyo hali ilivyo nje ya Makao Makuu ya Club hiyo Jangwani.Camera ya Kemo Tv imefika Makao Makuu ya Yanga asubuhi hii kujionea hali ilivyo ikiwa ni asubuhi ya kwanza tangu Wanachama wa Yanga kupata habari za Uongozi wa Club hiyo kutakiwa kuachia ngazi baada ya baadhi ya Wazee wa Yanga kushinda kesi ya madai mbalimbali ikiwemo tuhuma za uwepo wa Hersi na wenzake kuvunja katiba ya Yanga.Uongozi wa Yanga unatarajiwa kuzungumza na Waandishi wa Habari leo saa nane mchana kwenye Makao Makuu ya Club hiyo yaliyopo Jangwani,

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam, imeamuru Uongozi wa Club ya Yanga ukiongozwa na Rais wa Yanga Inji...
17/07/2024

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam, imeamuru Uongozi wa Club ya Yanga ukiongozwa na Rais wa Yanga Injinia Hersi Saidi na wenzake, kuachia ngazi na kuondoka kwenye Club hiyo kwakuwa Katiba ya Yanga haitambui uwepo wao.

Imedaiwa kuwa uamuzi huu wa Mahak**a umekuja baada ya Kundi la Wazee wachache waliowahi kuwa Wazee wa Yanga kipindi cha nyuma, kush*taki Mahak**ani likidai uwepo wa Viongozi wa sasa wa Yanga (Injinia Hersi na wenzake) ni batili na haujafuata Katiba ya Club hiyo.

Kutokana na Wazee hao kushinda kesi hiyo katika Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu, inamaana kuwa Rais wa Yanga Injinia Hersi na Viongozi wenzake wanatakiwa kuachia ngazi na kukabidhi Ofisi kuanzia sasa.

Injinia Hersi alianza kuiongoza Yanga k**a Rais miaka miwili iliyopita baada ya kushinda nafasi hiyo akiwa ni Mgombea pekee July 2022 na kumfanya kuwa Rais wa kwanza wa Yanga SC toka kuanza kwa mfumo mpya wa mabadiliko ambapo alitangazwa kuwa atakuwa madarakani kwa miaka minne ( hadi 2026 ) kwa mujibu wa Katiba ya Club hiyo.

Kemo TV. Habari zetu zimehakikiwa.

OFFICIAL KEMO NEWSWazee wa Yanga wafanikiwa kumng'oa rasmi aliyekuwa Rais wa Yanga Eng. Heris Said.
17/07/2024

OFFICIAL KEMO NEWS

Wazee wa Yanga wafanikiwa kumng'oa rasmi aliyekuwa Rais wa Yanga Eng. Heris Said.

Address

Moshi
Kilimanjaro

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kemo tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category