Lindi News

Lindi News Tumezishika Habari Kidijitali

23/12/2025

LIWALE: Mkurugenzi wa kampuni ya Liwale Tabasamu ameahidi kuipatia Shule ya Msingi Ngongowele kompyuta na printa, ili kurahisisha uandaaji wa mitihani na mchakato wa ufundishaji.

Akizungumza k**a Mgeni Rasmi katika mahafali ya darasa la saba ya shule hiyo, Mkurugenzi huyo amesema msaada huo utaambatana na ufungaji wa mfumo wa maji safi shuleni hapo. Ahadi hiyo imekuja kufuatia risala ya mwalimu Taji Mikongo, iliyobainisha uhaba wa vitendea kazi vya kidijitali licha ya shule hiyo kufaulisha wanafunzi wote 59 wa mwaka 2025.

Kwa upande mwingine, Mwenyekiti wa kijiji hicho, Hassan Mbangulila, ameahidi kutoa vifaa vya shule kwa wanafunzi wote waliofaulu kujiunga na Kidato cha Kwanza mwaka 2026 ili kuwapunguzia mzigo wazazi na kuhamasisha elimu kijijini hapo.

23/12/2025

KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali Katika kutatua tatizo la Maji Taasisi ya Heart to heart Foundation kwa kushirikiana na KOICA imekabidhi visima vitano vyenyewe thamani ya milioni 110 Katika halmashauri ya Mtama Mkoani Lindi

Akizungumza Katika ghafla ya makabidhiano ya visima hivyo iliyofanyika Katika kijiji cha Mtegu huko Halmashauri ya Mtama mwishoni mwa wiki iliyopita Meneja Mradi wa heart to heart Foundation Deodatus Manzi Amesema kuwa visima hivyo ni sehemu ya Utekelezaji wa Mradi wa miaka 3 wa maji Safi na usafi wa mazingira ambao unalenga kufikia Kata 14

Alisema Katika awamu ya Kwanza ya Utekelezaji wa Mradi huo utajikita Katika kusambaza miundombinu ya maji Katika zahanati na vituo vya Afya ambapo mpaka sasa tayari visima 11 vimeshachimbwa

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri hiyo ya Mtama Tasilo Lupapa alisema kupitia Mradi huo Jumla ya wananchi 2987 kutoka Katika Vijiji vya Simama, Ingawali , Mbawala, Litipu na Mtegu watanufaika

Adha Lupapa licha ya kuwashukuru heart to heart kwa msaada huo pia alitoa wito kwa wananchi na jumuoya za watumia maji kuilinda miundo mbinu hiyo ili itumike kwa muda mrefu

Alisema itakuwa ni jambo la kushangaza kuona Miradi hiyo inakwama kiuendelevu na uendeshaji muda mfupi baada ya kukabidhiwa Katika vijiji hivyo.

Mganga mfawidhi wa zahanati ya mtegu Dr. Jacklin Sitta Alisema kuwa kwa kusogezewa huduma ya maji Katika zahanati hiyo kutarahisisha utosji na upatikanaji wa huduma Kwa wagonjwa wanaokuja kupata huduma.

Baadhi ya wananchi wa Mtegu akiwemo ghalia Saidi na Asha swalehe walisema kuwa kwa sasa inapotokea unampeleka mama mjamzito wakati ambao maji yameisha hospialini hapo ulazimika kubeba maji majumbani kwao yatakayowawezesha kuendelea kupata huduma.

Address

Lindi
Lindi
0000

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Lindi News posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Lindi News:

Share