23/12/2025
LIWALE: Mkurugenzi wa kampuni ya Liwale Tabasamu ameahidi kuipatia Shule ya Msingi Ngongowele kompyuta na printa, ili kurahisisha uandaaji wa mitihani na mchakato wa ufundishaji.
Akizungumza k**a Mgeni Rasmi katika mahafali ya darasa la saba ya shule hiyo, Mkurugenzi huyo amesema msaada huo utaambatana na ufungaji wa mfumo wa maji safi shuleni hapo. Ahadi hiyo imekuja kufuatia risala ya mwalimu Taji Mikongo, iliyobainisha uhaba wa vitendea kazi vya kidijitali licha ya shule hiyo kufaulisha wanafunzi wote 59 wa mwaka 2025.
Kwa upande mwingine, Mwenyekiti wa kijiji hicho, Hassan Mbangulila, ameahidi kutoa vifaa vya shule kwa wanafunzi wote waliofaulu kujiunga na Kidato cha Kwanza mwaka 2026 ili kuwapunguzia mzigo wazazi na kuhamasisha elimu kijijini hapo.