SOKA LETU Mtaani KWETU

SOKA LETU Mtaani KWETU

MAKALA AGUSTIN OKRAH USAJILI MPYA YANGA⚽👣Agustin okrah magic ni midifilder au mido wa mpira Ambae pia anaweza kucheza na...
03/01/2024

MAKALA AGUSTIN OKRAH USAJILI MPYA YANGA⚽👣

Agustin okrah magic ni midifilder au mido wa mpira Ambae pia anaweza kucheza nafasi ya winga na kuutumi vyema mguu wake wa kushoto

Agustin okrah magic ni mzaliwa wa nchini Ghana ana umri wa miaka 30 akiwa na urefu172cm mghana uyu amekuwa gumzo baada ya kusajiliwa na young African baada ya kuachwa na timu ya Simba sports club na kurudi bechem ya nchini kwao Ghana

Agustin okrah amekuwa na kiwango Bora zaidi kwa msimu uliopita nchini kwao Ghana akitoka na wastan wa mabao 16 kwa nusu msimu ambao ni wastan wa mabao tisa kwa msimu mzima akicheza dk141 akiwa ndie top scorers katika club hiyo

Agustin okrah amecheza vilabu kadhaa vikubwa akianzia maisha ya soka katika club ya rb ya Ghana na kusajiliwa kwa ada ambayo haikuwekwa wazi kwenda asante kotoko ya huko huko Ghana pia amecheza katika club ya al merrikh ya Sudan pamoja na al hilal omrduman ya Sudan pia.

Ikiwa k**a okrah akifanya vizuri YANGA na kurudi katika ubora wake hakuna Ambae hatompenda kwa kuwa ni mcheshi sana k**a walivyo waghana wengi k**a winga wa zamani wa yanga anayekipiga kunako club ya far rabat ya Morocco benard Morrison⚽

Mara kadhaa inasemekana ndugu wawili wakigombana ugomvi uache tu hii ni watani wa jadi yanga na Simba waliibiana au walipeana wachezaji lakini sio kwa furaha ila ni ugomvii mkubwa na huu ndio utani wa jadi itoshe kusema kuwa Agustin okrah ni mchezaji mzurii ila tusubiri muda utaamua

Mimi ni kijana wenu soka letu kitaani KWETU hadi wakati ujao⚽⚽👣

Mimi napenda kumuita Mzee wa VAR Kwa majina yake kamili anaitwa perluigi collina aliyezaliwa mnamo mwaka wa 13 February ...
30/12/2023

Mimi napenda kumuita Mzee wa VAR

Kwa majina yake kamili anaitwa perluigi collina aliyezaliwa mnamo mwaka wa 13 February 1960 hukoo italy mji wa bologna mwenye urefu wa futi 6na inch 2 na mita1.88

Mmmmh kilichonivitutia Leo kuwapa simulizi ni kutokana na vituko vyake uwanjani pamoja na tukio la kikatili linalo nikumbusha fainali za UEFA mnamo mwaka wa 1999 nchini Hispania jijini Barcelona

Naweza kunukuu alichosema official referee mstaafu perluigi collina..siku ambayo niliijua tafsiri ya SOKA ni mchezo uliobeba hisia na wenye maumivu yasio na mfano na ndio sura halisi ya mpira wa miguu.

Ilikiwa ni mnamo mwaka wa 1999 may 26 fainali ya mpira kombe la UEFA nchini Hispania jijini Barcelona ikiwa imesalia dakika 3 tu kati ya nne nilizoziongeza kuumaliza mchezo huu ambao ungeisha kwa goli Moja sifuri na kuupa ushindi timu ya Bayern munichen wakisubiri kipenga changu tu.

Kwa mara ya kwanza ndipo niliijua sura halisi ya mpira wa miguu mnamo dakika ya 92ya mchezo ambapo Manchester united walipo sawazisha ubao na kufanya mambo yabadilike kabisa na kufanya mashabiki wa Bayern munichen waliokuwa na furaha kuzima k**a mshumaa mbele ya mashabiki wa Manchester united walipo guruma k**a Simba na kufanya uwanja mzima uitikie kwa kelele zao.

Ambapo bao la kwanza lilipachikwa na sheigham mnamo dakika ya 91 ukifuatiwa na olegunar solskjaer mnamo dk92 sekunde ya 59..

Ndipo wachezaji wa Bayern Munich walipoishiwa nguvu uku sauti iliyo kuwa ikiskika ni glory man united glory glory man united nilimfuata mchezaji Jeremie alitekuwa kaishiwa nguvu sikuwa na la kufanya zaidi ya kumwambia una sekunde ishirini tu za kupambana.

Ilikiwa ni uchungu sana usio na kifani juu ya tukio lile nisiloweza kulisahau linalonijia mara zote kichwani kwangu k**a jinamizi alihitimisha referee huyo perluigi collina.

Nmeona nimzungumzie kwa ufupi je ungependa nimzungumzie nani Tena ni kijana wenu muandishi wa soka niite SOKA letu mtaani KWETU tukutane makala yajayo

Address

Longido

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Telephone

+255692087834

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SOKA LETU Mtaani KWETU posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to SOKA LETU Mtaani KWETU:

Share