Simon peter

Simon peter Taarifa sahihi kwa wakati sahihi

Mara ya sita mfululizo. Hongereni wana Yanga🐸Poleni sana Wanamsimbazi🦁
16/09/2025

Mara ya sita mfululizo.
Hongereni wana Yanga🐸
Poleni sana Wanamsimbazi🦁

Ngao ya Jamii  2025/2026Kikosi cha Simba na Kikosi cha YangaNani kuibuka mshindi?
16/09/2025

Ngao ya Jamii 2025/2026
Kikosi cha Simba na Kikosi cha Yanga
Nani kuibuka mshindi?

16/09/2025

MFAHAMU MWANARIADHA ALPHONCE SIMBU.
Alphonce Felix Simbu alizaliwa tarehe 14 Februari 1992 katika mkoa wa Singida.
‎Alianza mbio akiwa kijana, akijulikana kwa uwezo wake wa kukimbia muda mrefu bila kuchoka
‎Alianza kushiriki mashindano ya kimataifa, akiwakilisha Tanzania katika mbio za marathon mwaka 2015–2016

‎Katika Olimpiki ya Rio 2016 Alimaliza nafasi ya 5 kwenye marathon – ushindi mkubwa kwa mwanzo wa mashindano makubwa ya dunia.

‎Mwaka 2017 alishinda medali ya shaba (bronze) kwenye World Championships, London katika mbio za marathon.Hii ilimfanya kuwa mmoja wa wanariadha wa Tanzania waliopata medali kwenye michuano ya dunia.

‎Mwaka 2018–2019: Aliendelea kushindana kwenye marathon kubwa duniani, akijenga jina lake miongoni mwa wakimbiaji bora wa umbali mrefu.

‎Katika mbio za Tokyo zilizofanyika 2021 badala ya 2020 kwa sababu ya Covid-19 Alimaliza nafasi ya 7.

‎Licha ya kuto kushinda,Desemba 2024, Katika Valencia Marathon, alikimbia kwa muda wa 2:04:38 –na hapa alijiwekea rekodi yake bora binafsi (Personal Best)

‎Aprili 2025: Alishiriki Boston Marathon, akimaliza nafasi ya pili na
‎Septemba 2025: Katika World Athletics Championships – Tokyo, ameshinda medali ya dhahabu ya marathon kwa muda wa 2:09:48 akimaliza nafasi ya kwanza.
‎Simbu amekuwa nguzo ya riadha Tanzania na sura ya matumaini kwa kizazi kipya cha wanariadha.

‎Anahesabiwa miongoni mwa wakimbiaji bora wa marathon duniani, akiwa na medali ya dhahabu (2025), shaba (2017) na rekodi binafsi ya kasi.

Anauliza Ayubu Taarifa
15/09/2025

Anauliza Ayubu Taarifa

Klabu ya Simba SC imepokea barua kutoka CAF ambayo inaeleza kupigwa  faini ya Dollar za kimarekani 50,000 (Tshs 123M) pa...
14/09/2025

Klabu ya Simba SC imepokea barua kutoka CAF ambayo inaeleza kupigwa faini ya Dollar za kimarekani 50,000 (Tshs 123M) pamoja na kufungiwa kuingiza Mashabiki kwa mechi moja kwenye michuano ya CAF kuelekea msimu ujao kutokana na vurugu walizofanya mashabiki kwenye mchezo wa CAFCC dhidi ya Al Ahli Tripol mwaka jana.

14/09/2025

Baada ya timu za simba na Yanga kufanya matamasha na kutambulisha wachezaji uelekeo wa sasa ni kwenye ngao ya Jamii.
Nani kuwa bingwa wa ngao ya jamii 2025/2026?

12/09/2025
11/09/2025

‎ Rais wa klabu ya Yanga pamoja na Viongozi wengine wa klabu hiyo wameingia Makubaliano ya kutengeneza AI na Kampuni ya Blackbirds ya Uholanzi ambayo itasaidia kufuatilia perfomance ya mchezaji,kujua Afya yake na kumfanyia Tathmini watakapotaka kumuuza.

11/09/2025

Baada ya kushuhudia tamasha la Simba hapo jana, nimejiridhisha kuwa simba inazidi kuwa bora mwaka hadi mwaka. Hongereni wenye nchi , hongereni viongozi wa simba na wachezaji pia. Kuhusu mashabiki hilo halina kipengere, ile tuzo ya Caf mlistahili.

Kikosi kipya cha Simba msimu wa 2025/2026
10/09/2025

Kikosi kipya cha Simba msimu wa 2025/2026

10/09/2025

MANGUNGU LAWAMA UNAJITAKIA.
Leo ni siku kubwa kwa timu ya simba, ni SIMBA DAY 2025.
Wenzio wote tumevaa jezi za Simba.
Katika zile jezi zenye rangi tatu umekosa hata moja?

26/07/2020

MAIKO 1.

Maiko ni mwanafunzi wa chuo cha Veta Songea akisomea kozi ya umeme wa magari, ni mtoto ambaye hamjui baba ake wala mama ake. Amekuwa akilelewa na mzee Kapinga ambaye alimchukua kwenye kituo cha kulelea watoto yatima peramiho baada ya kumtafuta mtoto wa kiume kwa miaka kadhaa na kushindwa kumpata.

Akiwa na miaka 19 baada ya kumaliza kidato cha nne, London sekondari mzee wake ambaye alikuwa akimlea k**a mwanae alifariki dunia kwa maradhi ya kisukari na ni mwaka mmoja tu baada ya mke wake kufariki. Maisha yalikuwa magumu kwa Maiko ambaye lengo lake la kuwa fundi mkuu wa magari Tanzania yote lilififia.

Dada ake mkubwa, mtoto wa mzee Kapinga aliyeitwa Mage aliyemzidi miaka 15 alijitolea kumlea Maiko kwa sharti la kumtimizia haja zake za kimapenzi,kwa shingo upande Maiko alikubali baada ya maneno ya "mtumikie kafiri upate ujira wako" kupita kichwani mwake.

Maisha yaliendelea hivyo kwa Maiko kufanywa ki ben ten wa Mage, siku moja Maiko akiwa chuo, ulitokea mchango wa Tsh 20000 kwa kila mmoja katika kundi lao ilivwaweze kukamilisha kuitengeneza video iliyokuwa ikielezea namna mfumo wa umeme wa gari aina ya Voxwagen k**a group assignment. Kwa kuwa hakuwa na pesa aliona aikope kwa mwanachuo mwenzie aliyeitwa Clara. Clara alikubali kwa sharti la kulipwa baada ya mwezi mmoja.

Aliporudi nyumbani alimkuta Mage amesharudi kutoka kazini kwake, Mage alikasirika sana kuona Maiko amechelewa kurudi kutoka chuo. Alimnunia bila kujua nini kilikuwa kimetokea chuo. Namna ambavyo Maiko alijaribu kueleza kwa nini amechelewa ndivyo Mage alikasirishwa zaidi.

Siku chache mbele Maiko alimwomba Mage hela kwa ajili ya Matumizi binafsi na kulipa deni kwa Clara. Mage hakujibu chochote na kuwasha gari lake na kuondoka kuelekea kazini kwake. Haikuwa shida sana kwa Maiko kwani alizoea hali ile japo aliona k**a dharau zinazidi kuongezeka. Aliondoka na kuelekea chuoni akitembea kutoka Ruhuwiko mpaka msamala Veta. Alifika kwakuchoka sana huku nguo zake ambazo alikuwa hazibadilishwi na kuu kuu zikibeba vumbi lote la bombambili na matarawe.

Siku moja aliamka mapema na kujaribu tena kuomba pesa za matumizi kwa Mage. Mage aliingia ndani na kutokana kiadi cha shillingi laki mbili. Akiwa anampa alimtamkia maneno kuntu " we mbwa, nakupa hizi pesa,kahonge malaya wako, nikigundua utamfukua mama ako kaburini, huna shukrani hata kidogo, kunguru gani usiyefugika wewe? Alipojaribu kumjibu kwa kushukuru alichapwa kibao ambacho kilimfanya asione mbele, alipepesuka akiwa ameshika zile hela na hatimaye akili ilirudi. Alipoangalia alimuona mage akitoka getini kuelekea kazini kwake.

Kiukweli Maiko aliumia na aliamua kuziacha zile pesa pale pale, aliondoka kuelekea chuo huku akiwaza na kulaani kwa nini hakuwahi kumuona mama ake wala baba ake. Alipokaribia chuo alimuona Clara akinunua chipsi kwa Mudi ambaye alikuwa mchoma chipsi jirani na chuo. Clara alipomuona tu, alimfuata na kumkumbusha hela yake kwa masauti makali. "Nipe hela yangu"

Nitaendelea.....

Address


Telephone

+255764018736

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Simon peter posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share