OTV MEDIA

OTV MEDIA >Tumekufikia
>Official page Otvmedia �
>Tangaza Biashara yako hapa �>+255687049827au WhatsApp

NGUMU KUAMINI.. NIMEFIWA NA MKE WANGU.
16/07/2025

NGUMU KUAMINI.. NIMEFIWA NA MKE WANGU.

MIAKA 20 JELA KWA KOSA LA KUIBA MALI YA UMMA.Ezbon Mujuni (28) Mkazi wa kijiji cha Bunazi Wilaya ya Missenyi Mkoa wa Kag...
16/07/2025

MIAKA 20 JELA KWA KOSA LA KUIBA MALI YA UMMA.

Ezbon Mujuni (28) Mkazi wa kijiji cha Bunazi Wilaya ya Missenyi Mkoa wa Kagera amehukumiwa kwenda jela miaka 20 kwa kosa la kuchimba na kuiba nguzo (3) za umeme na nyaya zenye thamani ya Tsh.11,536,357/=.11,536,357/=.

Mshtakiwa alitenda kosa hilo tarehe Julai 21,2024 katika kijiji cha Nyakahama Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera na kuk**atwa na Jeshi la Polisi na kufikishwa Mahak**ani Disemba 20,2024.Hukumu imetolewa Julai 15, 2025 mbele ya Mhe.Daniel Nyamkerya Hakimu wa Mahak**a ya Wilayaya Muleba.

“UNAKUFA KATIKA UMRI WA MIAKA 20 UNAZIKWA UKIWA NA MIAKA 60’’Nilikuwa nasoma kitabu kimoja nikakutana na sentensi hii, i...
29/06/2025

“UNAKUFA KATIKA UMRI WA MIAKA 20 UNAZIKWA UKIWA NA MIAKA 60’’

Nilikuwa nasoma kitabu kimoja nikakutana na sentensi hii, ikanifikirisha kidogo.

Nikataka kujua mwandishi wa kitabu hicho alimaanisha nini kusema watu wengi hasa Afrika, wanakufa wakiwa na miaka 20 lakini wanazikwa wakiwa na miaka 60?

Katika kujifunza zaidi nikagundua tabia 08 zinazoweza kuonyesha mtu aliyekufa lakini angali na uhai ndani yake.

1. Kuamka na kulala bila ratiba maalumu.
Hii ni tabia inayowakumba vijana wengi wasomi na wasio wasomi. Utamkuta mtu na familia yake kabisa lakini anaamka asubuhi anajiuliza au anasemezana na mwenzake leo sijui niende wapi, sijui nifanye nini!
Utasikia oyaa! Una mchongo wowote huko?
Akiambiwa hakuna anarudi kulala asubirie chai au ugali wa mchana.

2. Kutoishi katika uhalisia.
Hii ni tabia waliyo nayo vijana wa kitanzania.
Kupenda kumiliki vitu vya kujionesha visivyoendana na uhalisia wa maisha yao.
Mathalani mtu yuko radhi auze mtaji wake wote wa kuku ili amiliki iPhone. Pasipo kujua atapoteza zaidi kuliko kuingiza faida.

3. Kutojua kusudi lako kuwepo duniani.
Kuna watu utasikia anasema “Kikubwa uzima mengine tumwachie Mungu’’
Hiyo ni tabia inayoonesha umekufa lakini una pumzi ndani yako.
Kila mwanadamu hakuzaliwa na nguo, na sio wote walizaliwa wakakuta pesa.
Wengi wamekulia katika mazingira magumu lakini kwa kuwa walijua kusudi lao la kuumbwa wamemiliki mali na wanazidi kuongeza zaidi.
Kumbe tunahitaji kuchukua hatua kila siku, pasipo kukata tamaa, maana mtafutaji hachoki na akishachoka ujue kapata.

4. Kuiga maisha ya wengine.
Utasikia “aisee jamaa kanunua friji na mimi nanunua friji” unachukua mtaji wako wa samaki unanunua pasipo kujua mwenzako kanunua kupitia faida aliyoingiza katika biashara yake.
Utajikuta mpaka unakufa, ulikuwa mtu wa kufukuzia mafanikio ya watu wengine wakati malengo yako na kusudi la Mungu kukuweka duniani haujalitimiza.

5. Kutowajibika katika majukumu yako.
Hapa nirukie kwa wanafamilia.
Wewe ni baba au mama hauwajibiki katika kutunza familia wakati unajua familia ni baraka kutoka kwa Mungu, wewe umekufa angali una pumzi.
Kwa sababu mtu asiye tunza familia ni zaidi ya mchawi.
Familia imetoka kiunoni mwako mwenyewe, unashindwaje kuwapa watoto mavazi na mazingira bora ya Elimu ili hali wewe umesomeshwa na wazazi wako na una mshahara?
Familia yako inapoadhirika jua wazi uko uchi, yaani sehemu zako za siri ziko wazi.
K**a unavyokuwa makini kuzilinda sehemu nyeti za mwili wako ndivyo unavyotakiwa kuwatunza wanao maana wametoka huko.

6. Kung’ang’ania jambo lisilo kupatia faida.
Utakutana na kijana na nguvu zake kabisa anashinda stendi kuokota hamsini hamsini anazotupiwa na makondakta.
Akisha kusanya 1500 ananunua msosi anavutia sigara, siku imeisha.
Akirudi nyumbani harudi na chochote anadai chakula kwa mkewe, pesa hajapeleka anakula analala.
Mtu wa namna hii hayupo katika kundi la watu wanaoishi labda wanaopumua.
Tunamtofautishaje na waliolazwa wakipumulia mashine?

7. Hurka ya matumizi mabaya ya pesa.
“Hebu tutumie tu pesa yote, ya kesho yatajisumbukia au wewe una
uhakika wa
kufika kesho?”
Mtu k**a huyu kwa vyovyote vile huwezi kusema ana maisha ndani yake.
Tabia ya mtu anayejua kusudi la kuishi lazima awe mtunza akiba na nidhamu katika matumizi ya pesa.
Wapo watu wengi wamejikuta wakiishi maisha ya kukimbia nyumba zao kwa sababu ya madeni yaliyozidi kipimo.

8. Kukata tamaa na kupuuzia kila jambo.
Kuna mtu utamshauri fanya hivi, atakujibu mbona hata fulani alijaribu akashindwa, mimi ni nani hata nifanikiwe?
Huyu mtu tayari amejikatia tamaa na hawezi kufika popote tena maana mawazo yake hayapo katika kutafuta njia mbadala za kufikia mafanikio au kujifunza kwanini wale walifeli na yeye atumie njia gani afanikiwe.
Mwingine anasema Mungu mbona unakawia njoo unichukue.
Unampangia Mungu ratiba ndo hakuchukui sasa mpaka unafikia miaka 60 ya kifo chako, umezaa watoto 10 lakini una vyumba viwili na sebule tu.

Tuache kujikatia tamaa, kuona hatuwezi ili hali kila mtu kaumbwa na kaletwa duniani kwa kusudi maalumu.
Kwanini unakata tamaa wakati tunaambiwa kibaiolojia mbegu zaidi ya milioni mia hukimbia kuelekea mfuko wa uzazi, lakini ni moja tu hufaulu na kutengeneza mtoto ambaye ni wewe.

Tafsiri tu ni kwamba umezaliwa kuwa mshindi na unatakiwa ushinde.
Ushindi upo katika kuishi vile unatakiwa kuishi k**a kusudi la Mungu linavyokutaka. Kutobweteka bali kwa kuwajibika ili kujiletea maendeleo
Mungu hakukuumba uwe maskini.
Tambua Fursa, kimbilia fursa.
Ukimbie umasikini kwa mbio kubwa

Dkt. BUSANDA BUSANDA ATAKA KURITHI KITI CHA ENG.MAGESA JIMBO LA BUSANDA GEITA .Dk. Busanda Lucas Busanda , Mwenye  shaha...
29/06/2025

Dkt. BUSANDA BUSANDA ATAKA KURITHI KITI CHA ENG.MAGESA JIMBO LA BUSANDA GEITA .

Dk. Busanda Lucas Busanda , Mwenye shahada ya kwanza ya udaktari wa binadamu ni Moja Kati ya wagombea zaidi ya wanne waliojitokeza Kurithi Kiti Cha aliyekuwa mbunge WA Jimbo hilo Eng. Tumaini Magesa ambaye anagombea Jimbo jipya la Katoro.

Hii ni awamu ya pili kwa Dkt. Busanda Busanda kuwania nafasi hiyo ya Ubunge, ambapo kwa mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2020.

WAKILI MSOMI PATRICK MALOGOI AJITOSA KUCHUANA NA MUSUKUMA JIMBO LA GEITA VIJIJINI.Patrick Stephen Malogoi ambaye ni  wak...
29/06/2025

WAKILI MSOMI PATRICK MALOGOI AJITOSA KUCHUANA NA MUSUKUMA JIMBO LA GEITA VIJIJINI.

Patrick Stephen Malogoi ambaye ni wakili wa serikali ofisi ya mwanasheria Mkuu wa serikali ni Moja Kati ya wagombea wanaowania Kuchuana na Mbunge anayemaliza muda wake kwenye Jimbo hilo Joseph Kasheku Musukuma.

Malogoi alikuwa mshindi wa pili kwenye kura za maoni Katika uchaguzi mkuu WA mwaka 2020.

Dkt. JAFARI RAJAB SEIF AJITOSA KUCHUANA NA VIGOGO UBUNGE JIMBO LA BUSANDA.Daktari wa binadamu ambaye pia ni kijana Kutok...
29/06/2025

Dkt. JAFARI RAJAB SEIF AJITOSA KUCHUANA NA VIGOGO UBUNGE JIMBO LA BUSANDA.

Daktari wa binadamu ambaye pia ni kijana Kutoka kata ya Bukoli amejitosa Kuchuana na vigogo kuwania nafasi ya ubunge Jimbo la Busanda Geita.

Dkt. Jafari amechukua fomu Leo June 29, 2025 Katika ofisi za CCM wilaya Geita.

MHANDISI KIJA NTEMI AINGIA KWENYE MCHUANO WA UBUNGE JIMBO JIPYA LA KATOROMHANDISI Kija Ntemi amechukua fomu ya kuomba ri...
29/06/2025

MHANDISI KIJA NTEMI AINGIA KWENYE MCHUANO WA UBUNGE JIMBO JIPYA LA KATORO

MHANDISI Kija Ntemi amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumteua kugombe ubunge wa jimbo la Katoro Geita.

Mhandisi Ntemi amechukua fomu hiyo Juni 29, 2025 katika ofisi za CCM wilaya ya Geita zilizopo mjini Geita.

Address

Manyara

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when OTV MEDIA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share