Habari za Zanzibar

Habari za Zanzibar Ukurasa utakaokupa habari mbalimbali kutoka Zanzibar na Ulimwenguni kote.

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari bungeni jijini Dodoma, leo Me...
14/05/2026

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari bungeni jijini Dodoma, leo Mei 14, 2026.

14/05/2026

MSIZUIE WANAFUNZI KUFANYA MITIHANI - DKT. MWIGULU

โ–ช๏ธAsema Serikali itaendelea kuongeza fedha za mikopo ya elimu ya juu

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amezitaka taasisi za elimu nchini kutowazuia wanafunzi kufanya mitihani ya masomo yao kwa kushindwa kulipa ada.

Pia, Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kuongeza fedha za mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na vyuo vya kati ili wanafunzi wengi zaidi wanufaike na mikopo hiyo.

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametoa maelekezo hayo leo (Alhamisi Mei 14, 2026) Bungeni jijini Dodoma katika kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Latifa Khamis Juwakali aliyetaka kujua mkakati wa Serikali kiuhusu wanafunzi wanaozuiwa kufanya mitihani kwa kutokulipa ada.

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na Mhe. Daniel Chongolo, Waziri wa Kilimo, George Simbachawene, Mbunge wa K...
14/05/2026

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na Mhe. Daniel Chongolo, Waziri wa Kilimo, George Simbachawene, Mbunge wa Kibakwe, Hamis Tabasamu, Mbunge wa Sengerema, Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Geita Vijijini na Lucy Mayenga, Mbunge wa Kishapu wakati wa Kikao cha 28 cha Mkutano wa Tatu wa Bunge la 13, Mei 13, 2026 jijini Dodoma.

๐——๐—ธ๐˜. ๐— ๐˜„๐—ถ๐—ด๐˜‚๐—น๐˜‚ ๐—ก๐—ฐ๐—ต๐—ฒ๐—บ๐—ฏ๐—ฎ: ๐—ž๐—ถ๐—ผ๐—ป๐—ด๐—ผ๐˜‡๐—ถ ๐˜„๐—ฎ ๐—ž๐—ฎ๐˜‡๐—ถ, ๐—ž๐—ฎ๐˜€๐—ถ ๐—ป๐—ฎ ๐— ๐˜‡๐—ฎ๐—น๐—ฒ๐—ป๐—ฑ๐—ผ ๐—ฎ๐˜€๐—ถ๐˜†๐—ฒ๐—ฐ๐—ต๐—ผ๐—ธ๐—ฎM***a Saidi-Dar es SalaamKatika kipindi cha siku chac...
13/05/2026

๐——๐—ธ๐˜. ๐— ๐˜„๐—ถ๐—ด๐˜‚๐—น๐˜‚ ๐—ก๐—ฐ๐—ต๐—ฒ๐—บ๐—ฏ๐—ฎ: ๐—ž๐—ถ๐—ผ๐—ป๐—ด๐—ผ๐˜‡๐—ถ ๐˜„๐—ฎ ๐—ž๐—ฎ๐˜‡๐—ถ, ๐—ž๐—ฎ๐˜€๐—ถ ๐—ป๐—ฎ ๐— ๐˜‡๐—ฎ๐—น๐—ฒ๐—ป๐—ฑ๐—ผ ๐—ฎ๐˜€๐—ถ๐˜†๐—ฒ๐—ฐ๐—ต๐—ผ๐—ธ๐—ฎ

M***a Saidi-Dar es Salaam

Katika kipindi cha siku chache tu, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwigulu Nchemba ameendelea kudhihirisha mfano wa uongozi wa vitendo, uchapakazi na kujituma kwa kiwango cha juu katika kuwahudumia Watanzania. Ratiba yake ya kuanzia Mei 8 hadi Mei 13, 2026 imeonyesha wazi namna alivyojitoa kuhakikisha anatimiza wajibu wake wa kitaifa bila kuchoka, bila kusita na kwa uzalendo mkubwa.

Mei 8, 2026 Waziri Mkuu alikuwa mkoani Morogoro ambapo alifanya ziara ya kikazi kwa lengo la kufuatilia utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo na kusikiliza changamoto za wananchi. Ziara hiyo ilikuwa sehemu ya dhamira yake ya kuhakikisha Serikali inawafikia wananchi moja kwa moja na kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi yenye tija kwa taifa.

Kesho yake, Mei 9, Waziri Mkuu aliendelea na ziara yake mkoani Dodoma katika maeneo ya Kibakwe na Mpwapwa ambako alikagua miradi ya maendeleo pamojanna kuzungumza na wananchi na viongozi.

Licha ya ratiba nzito ya mchana kutwa, jioni ya siku hiyo alisafiri kuelekea Dar es Salaam na usiku huo huo akashiriki hafla ya utoaji wa tuzo za wanamichezo, zilizoandaliwa na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) jambo lililoonyesha namna anavyothamini sekta ya michezo na mchango wake katika kuunganisha taifa na kukuza vipaji vya vijana.

Kana kwamba hiyo haitoshi, Mei 10, 2026 Waziri Mkuu aliondoka kuelekea Nairobi nchini Kenya kushiriki Mkutano wa Africa Forward uliowakutanisha viongozi wa Afrika na Ufaransa kujadili masuala ya maendeleo, uwekezaji, biashara na ushirikiano wa kimkakati kwa ajili ya mustakabali wa bara la Afrika.

Katika mkutano huo wa Mei 11 na 12, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba aliupeleka ujumbe wa Tanzania kimataifa, huku Waziri Mkuu aliendelea kuitangaza nchi kimataifa na kutafuta fursa zenye manufaa kwa Watanzania.

Kilichowavutia wengi zaidi ni namna baada ya kurejea nchini Mei 13, 2026, Waziri Mkuu hakupumzika wala kuchelewa, bali aliingia moja kwa moja bungeni kuendelea na majukumu ya kitaifa. Huu ni ushahidi wa wazi wa kiongozi anayeelewa uzito wa dhamana aliyopewa na anayejitoa kwa moyo wote kuhakikisha gurudumu la maendeleo linasonga mbele kila wakati.

Hakika, mwenendo huu wa Dkt. Mwigulu Nchemba ni somo kwa viongozi wengi kuhusu maana halisi ya uongozi wa kuwajibika. Katika nyakati ambazo wananchi wanahitaji matokeo, kasi na uthubutu, Waziri Mkuu ameendelea kuonyesha kuwa maendeleo ya taifa yanahitaji viongozi wanaofanya kazi kwa bidii, wenye uthubutu wa kusafiri, kusikiliza wananchi, kuiwakilisha nchi kimataifa na kurejea kazini bila kuchoka. Uchapa kazi wake ni alama ya uzalendo na dhamira ya kweli ya kulitumikia taifa.

13/05/2026

SURA MPYA SOKO LA SIMU 2000

Serikali iliagiza eneo lililoungua Moto katika Soko la Simu 2000 lililopo Mawasiliano Jijini Dar Es Salaam, lisafishwe ili kuruhusu wafanyabiashara kurejea tena na kuendelea na biashara zao k**a kawaida.

Maagizo haya yaliyotolewa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba.

Baada ya hapo Maagizo haya yalifanyiwa kazi na hatmaye Wafanyabiashara wakarejesha Tabasamu kwa kuendelea na Kazi zao k**a kawaida.

TABASAMU LIMERUDI SOKO LA SIMU 2000

TAZAMA VIDEO HII

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mkurugenzi Mkuu wa Kituo ch...
13/05/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC), Dkt. Jean Kaseya pamoja na Ujumbe wake Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 13 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Kit...
13/05/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC), Dkt. Jean Kaseya pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 13 Mei, 2026.

AFRIKA YAHIMIZWA KUJENGA MUSTAKABALI SALAMA KWA WATOTO.Mke wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bi. Neema ...
13/05/2026

AFRIKA YAHIMIZWA KUJENGA MUSTAKABALI SALAMA KWA WATOTO.

Mke wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bi. Neema Mwigulu Nchemba, ametoa wito kwa viongozi na wadau wa Afrika kuweka kipaumbele katika ulinzi wa watoto dhidi ya ukatili wa kidijitali.

Akizungumza jijini Nairobi, Kenya Mei 12, 2026, katika Mkutano wa Wenza wa Mawaziri wakuu wa nchi za Afrika, uliofanyika Pembezoni mwa Mkutano wa โ€œAfrica-Forward Summitโ€ ukilenga kujenga mazingira salama ya kidijitali kwa watoto wa Afrika katika ulimwengu unaoendeshwa na Akili Unde (AI). Bi.Nchemba alisisitiza kuwa mustakabali wa bara la Afrika hautategemea tu vigezo vya kiuchumi, bali uwezo wa watoto kujifunza na kuvumbua katika nafasi ya kidijitali bila hofu ya unyanyasaji.

Katika hotuba yake, alibainisha kuwa ingawa teknolojia ya Akili Bandia (AI) inatoa fursa kubwa katika sekta za elimu, afya, na ujasiriamali, imeleta pia hatari mpya na halisi. Alitaja changamoto k**a vile uonevu mtandaoni, unyanyasaji wa kijinsia unaochochewa na AI, na ulaghai k**a vitisho vinavyovuruga utu na maendeleo ya watoto barani Afrika.

Ameeleza hatua zilizopigwa na Tanzania, ikiwemo kufanya marekebisho ya Sheria ya Mtoto (Sura ya 13) na kuimarisha utekelezaji wa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015. Aidha, alikumbusha Kampeni ya Kitaifa ya Ulinzi wa Watoto Mtandaoni iliyoanzishwa Februari 2024 na kuundwa k**ati maalum ya wadau mbalimbali ili kuhakikisha mazingira salama kwa watoto.

Mkutano huo, uliandaliwa na Kuongozwa na Mke wa Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mama Rachel Ruto ambapo ulihitimishwa kwa wito wa dharura wa kuimarisha ushirikiano wa kikanda na sheria madhubuti.

13/05/2026

WAZIRI MKUU AREJESHA FURAHA KWA BI. FEDERICA WA KIBAKWE

Mwanamke huyo amemlalamikia mumewe kwa kumtelekeza akiwa na watoto sita huku akiwa hana Kitanda wala godoro.

WAZIRI MKUU PIA ASAIDIA VIJANA WAWILI WALIOSHIRIKI UJENZI WA HOSPITAL YA KIBAKWE KULIPWA FEDHA ZAO PAPO KWA PAPO

TAZAMA VIDEO HII HAPA.

NI TABASAMU LA UTU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Viongozi mbalimbali mara baada ya...
12/05/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam wakati akitokea nchini Uganda ambapo alihudhuria Sherehe za Uapisho wa Rais wa nchi hiyo Mhe.Yoweri Kaguta Museveni, Jijini Kampala,tarehe 12 Mei, 2026.

VIONGOZI WA AFRIKA NA UFARANSA WAJADILI UWEKEZAJI NA MAENDELEOโ–ช๏ธDkt. Mwigulu asisitiza matumizi sahihi ya rasilimali ili...
12/05/2026

VIONGOZI WA AFRIKA NA UFARANSA WAJADILI UWEKEZAJI NA MAENDELEO

โ–ช๏ธDkt. Mwigulu asisitiza matumizi sahihi ya rasilimali ili kujenga uchumi wa Afrika

โ–ช๏ธRais Macron atangaza uwekezaji wa dola bilioni 27 Barani Afrika

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Mei 12, 2026 ameshiriki katika ufunguzi wa Mkutano wa Ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa (Africa Forward: Africaโ€“France Partnership for Innovation and Growth Summit) unaofanyika jijini Nairobi, Kenya.

Mkutano huo umewakutanisha Wakuu wa Nchi na Serikali, viongozi wa sekta binafsi, wadau wa maendeleo pamoja na wawekezaji kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, teknolojia, nishati, afya, Akili Unde (AI), kilimo, uchumi wa buluu pamoja na viwanda.

Akizungumza baada ya mkutano huo, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mkutano huo umekuwa wa manufaa kwa Bara la Afrika na Ufaransa kwa pamoja kwani majadiliano yamegusa namna ya kuzifanya pande hizo mbili ziweze kunufaika na ushirikiano huo.

Amesema rasilimali zinazopatikana barani Afrika zinatosheleza ikiwa zitatumika vizuri katika kujenga uchumi wa Afrika.

โ€œLengo kubwa la jitihada hizi ni kupambana na umasikini lakini pia na kutengeneza ajira kwa makundi makubwa ikiwemo la vijana pamoja na wanawake,โ€ amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amesema maeneo mengi yaliyojadiliwa ni maeneo ambayo yamepewa umuhimu katika Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

โ€œNguzo zote zilizoongelewa kwenye dira lakini pia na maeneo ya kipaumbele yameguswa katika mijadala ya leo,โ€ amesema.

Akizungumza katika mkutano huo, Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mheshimiwa Dkt. William Samoei Ruto, alizitaka nchi za Afrika kutafakari upya mifumo ya kiuchumi kwa kuimarisha ukusanyaji wa rasilimali za ndani, uwekezaji pamoja na ushirikiano wa kikanda ili kuhakikisha kunakuwa na maendeleo ya muda mrefu.

Aidha, Rais Ruto amesema ni wakati wa Afrika kujiweka k**a mdau katika uchumi wa kimataifa badala ya kuwa mnufaika wa misaada ya nje pekee.

โ€œAfrika haiwezi tena kubaki k**a mshiriki asiyekuwa na sauti katika mifumo ya kimataifa ambapo baadhi ya maamuzi muhimu hufanywa bila sauti ya usawa,โ€ alisema.

Kwa upande wake, Rais wa Jamhuri ya Ufaransa, Mheshimiwa Emmanuel Macron, alisema Bara la Afrika linapiga hatua kubwa za maendeleo na ni bara ambalo halisubiri majawabu ya changamoto bali linatoa majawabu ya changamoto mbalimbali lilazokabiliana nazo.

Katika hatua nyingine, Rais Macron alitangaza uwekezaji wa thamani ya dola za Marekani bilioni 27 barani Afrika katika sekta za nishati, Akili Unde, uchumi wa bahari pamoja na kilimo.

โ€œMpango huu utasaidia kutengeneza takriban ajira 250,000 barani Afrika na nchini Ufaransa,โ€ alisema.

Aidha, Rais Macron aliwataka wafanyabiashara wa Afrika kuona fursa zilizopo nchini Ufaransa na kwenda kuwekeza.

โ€œHatuko hapa tu kuja kuwekeza katika Bara la Afrika pamoja nanyi, tunawahitaji viongozi wakubwa wa biashara wa Afrika kuja kuwekeza nchini Ufaransa,โ€ alisema.

Kwa Upande wake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antรณnio Guterres alisema watu wa Bara la Afrika wanapaswa kuwa wa kwanza kunufaika na rasilimali za bara hilo.

โ€œBara hili limebarikiwa rasilimali nyingi, hapa wenyewe ndio wanapaswa wawe wa kwanza kunufaika,โ€ alisema.

Dkt. Mwigulu amemuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano.

Address

Bagamoyo
61305

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari za Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share