Kyela Fm Radio

Kyela Fm Radio Kyela Fm Radio Official Facebook Account
96.1 MHZ 📻
Sauti Yako, Mafanikio Yako.

Ungana nasi katika matangazo ya moja kwa moja kutoka katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mbeya Jiji kwenye uzinduzi wa opar...
23/03/2025

Ungana nasi katika matangazo ya moja kwa moja kutoka katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mbeya Jiji kwenye uzinduzi wa oparesheni ya ''No reform', No Election'' ambapo mgeni rasmi ni Mwenyekiti wa Chama hicho Tundu Lissu.
96.1 MHz MBEYA| SONGWE | NJOMBE
Kutizama Live YouTube Bonyeza Link hapo chini 👇👇


Ungana nasi katika matangazo ya moja kwa mja kutoka katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mbeya Jiji kwenye uzinduzi wa oparesheni ya ''No reform'm, No Election''...

Mbivu na mbichi juu ya kuvuliwa uanachama kwa Katibu mwenezi na Wanachama wengine watano wa Chama Cha Demokrasia  CHADEM...
17/03/2025

Mbivu na mbichi juu ya kuvuliwa uanachama kwa Katibu mwenezi na Wanachama wengine watano wa Chama Cha Demokrasia CHADEMA wilaya ya Kyela kujulikana Leo March 17,2025.

Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Kyela Victoria Swebe tupo nae hapa ndani ya la Asubuhi

HOST:
| Mwalwembe


📌
26/02/2025

📌

Kutokana na sababu zilizo nje na uwezo wetu tunatangaza mabadiliko ya ratiba ya kufanyika kwa   Mission ndani Ya Jiji la...
26/02/2025

Kutokana na sababu zilizo nje na uwezo wetu tunatangaza mabadiliko ya ratiba ya kufanyika kwa Mission ndani Ya Jiji la Mbeya Badala yake itafanyika tarehe 1/3/2025- 2/3/2025.

Tumefanya mabadiliko haya ili kupata nafasi ya kuungana na Wanahabari wote tulioguswa na Msiba wa Mwandishi Mwenzetu Simchimba aliyefariki kwa ajali ya baada ya Gari ya kampuni ya CRN lenye namba za Usajili T 599 DZQ na Gari ya serikali aina ya Land Cruiser lenye namba za usajili 6167 zilizogongana uso kwa uso katika eneo la Shamwengo wilayani Mbeya na kusababisha vifo vya watu watatu na wengine saba kujeruhiwa wakiwemo waandishi wa habari wenzetu pamoja na baadhi ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi CCM.

Kyela Fm Radio tunatoa pole kwa Familia,Ndugu,Jamaa, na Waandishi wa habari wote wa mkoa wa Mbeya ambao wameguswa na Vifo hivi na tunawaombea waliopata Majeraha warejee katika hali zao za wakawaida ili waendelee na majukumu ya kulijenga taifa kupitia tasnia hii Habari.

Bwana alitoa na Bwana Ametwaa!!Jina lake lihimidiwe Ameen

17/02/2025

TAARIFA KWA UMMA

Sauti Za Watu Zikiomba Msaada na Ukombozi zilisikika kutoka katikati ya JIJI LA MBEYA na Maeneo Jirani, wakilia kutokana na mateso ya kukosa Uhuru wa Burudani, (KIDNAPPING) kukosa Vipindi Bora kutoka Radio za nyumbani na habari zilizoshiba na hii imewasababishia maumivu kwa wasikilizaji wa radio (TORTURE) Vikosi vingine vyote vilivyotumwa Mbeya Vimeshindwa Kuwakomboa mateka wa Kiburudani (FAILED MISSION), Ndipo Taarifa zimetufikia makomando kutoka Mpakani pembezoni mwa Ziwa Nyasa, Kikosi No 961 KF (INFORMATIVE) Kyela Fm Radio Tunachukua jukumu Hili La UOKOZI (RESCUE MISSION).. Kikosi cha kwanza kitatua Katikati ya JIJI LA MBEYA Siku ya Tar 27-28 February 2025 (ENTER MISSION)
Hivyo wananchi Mkiona makomando wetu katika Maeneo yenu, Ruksa kupiga nao picha na kuvaibuka pamoja kwakuwa UKOMBOZI WA KIBURUDANI NA KIHABARI UMEOATIKANA (MBEYA JIJI RESCUE MISSION 27-28 FEB)


Tunawatakia wasikilizaji wa Kyela Fm Radio na wafuatiliaji wote wa mitandao yetu ya kijamii Sikukuu ya Wapendanao yenye ...
14/02/2025

Tunawatakia wasikilizaji
wa Kyela Fm Radio
na wafuatiliaji wote wa mitandao yetu ya kijamii Sikukuu ya Wapendanao yenye upendo, Amani, na furaha tele. Muwe na wakati mzuri wa kusherehekea upendo na mshikamano na wale mnaowathamini, Upendo Udumu kila Siku .

🛑 Mara Baada ya Kufungwa Jana na Tabora united Msemaji wa Kagera Sugar Manzanzala ameongea na  kuwa Hadi sasa hajaamka k...
12/02/2025

🛑
Mara Baada ya Kufungwa Jana na Tabora united Msemaji wa Kagera Sugar Manzanzala ameongea na kuwa Hadi sasa hajaamka kwa sababu ya uchungu wa kupoteza Mechi Muhimu jana.

Kagera sugar ipo Nafasi ya 15 Mechi 18 Alama 12.

Mara Baada ya Kufungwa Jana na Tabora united Msemaji wa Kagera Sugar Manzanzala ameongea na kuwa Hadi sasa hajaamka kwa sababu ya uchungu wa ku...

🛑 Kijana mmoja mkazi wa kitongoji cha Ushirika kati, kata ya Mpuguso, wilayani Rungwe,Mkoani Mbeya anayekadiriwa kuwa na...
11/02/2025

🛑
Kijana mmoja mkazi wa kitongoji cha Ushirika kati, kata ya Mpuguso, wilayani Rungwe,Mkoani Mbeya anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 20-25 amekutwa akiwa amefariki dunia kwa kujinyonga na kamba ndani ya nyumba yao.

Akizungumza na kituo hiki mapema hii leo February 11,2025 Diwani wa kata ya Mpuguso Japhet Mwakagugu amesema kuwa tukio hilo limetokea siku ya jana jumatatu majira ya mchana.

Kijana huyo aitwaye Ezma Mawazo enzi za uhai wake alikuwa akijishughulisha na biashara ya uchomaji nyama katika eneo la Stand ya ushirika Mjini.

Bado hakijafahamika chanzo cha kijana huyo kuchukua hatua ya kujinyonga kwakuwa hakuna taarifa yoyote aliyoiacha.

Kijana mmoja mkazi wa kitongoji cha Ushirika kati, kata ya Mpuguso, wilayani Rungwe,Mkoani Mbeya anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 20-25 amekutwa a...

🛑 🛑Mabadiliko ya Makocha katika Klabu ya yanga  kumesababisha Wachezaji kutoelewa Mifumo ya Walimu Mapema  hii inaweza k...
11/02/2025

🛑 🛑
Mabadiliko ya Makocha katika Klabu ya yanga kumesababisha Wachezaji kutoelewa Mifumo ya Walimu Mapema hii inaweza kusababisha yanga isichukue Ubingwa wa Ligi kuu Msimu huu.

Benzo Sanga ×

Sikiliza Kyela Fm Radio 96.1 Ukiwa eneo lolote Nyanda za juu Kusini

🛑 🛑Siku kadhaa zimepita tokea kuwepo kwa Taarifa ya mtu mmoja kukutwa amekufa uwanja wa mchaga hapa wilayani Kyela .Hati...
10/02/2025

🛑 🛑
Siku kadhaa zimepita tokea kuwepo kwa Taarifa ya mtu mmoja kukutwa amekufa uwanja wa mchaga hapa wilayani Kyela .
Hatimae amejulikana kuwa ni Frances Mbukwa ambaye ni katibu mwenezi chama Cha Mapinduzi tawi la Mbugani kata Mbugani wilayani Kyela .

Wakizungumza kwa masikitiko makubwa viongozi wa chama na serikali pamoja na majirani wameipokea kwa masikitiko makubwa taarifa hiyo ya Ts jina marufu na kusema kuwa alikuwa ni Mtu wa watu na mwanachama mpiga kazi kwa kitongoji chake na kata kwa ujumla .
Kwa mujibu wa Tarifa kutoka kwa msemaji wa Familia ndugu Ts atazikwa kesho .

Nb.Jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi juu ya kifo Cha marehemu na kwa wenyeji wa Kyela nyumbani kwa marehemu ni karibu na kanisa la kasunga Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya marehemu Amina .

Siku kadhaa zimepita tokea kuwepo kwa Taarifa ya mtu mmoja kukutwa amekufa uwanja wa mchaga hapa wilayani Kyela .Hatimae amejulikana kuwa ni Frances Mbukwa a...

Timu ya Sungura FC Bingwa wa ligi Daraja la Tatu Mkoa wa Mbeya, Kutoka Wilayani Kyela imenyang'anywa ushiriki wa ligi ya...
07/02/2025

Timu ya Sungura FC Bingwa wa ligi Daraja la Tatu Mkoa wa Mbeya, Kutoka Wilayani Kyela imenyang'anywa ushiriki wa ligi ya Mabingwa Wa Mikoa kwa Sababu ya kukosa Vyeti vya usajili wa Timu.

Akizungumza na Kipindi cha ​ hii leo Mwenyekiti wa Chama cha Mpira Mkoa wa Mbeya (MREFA) Ndugu Sadick Jumbe ameeleze kuwa Miongoni mwa Sababu iliyopelekea Sungura FC kutoenda Kushiriki ligi ya Mabingwa Wa Mikoa ni Kukosa cheti cha Usajili ilihali walikuwa na Namba ya usajili Jambo ambalo kanuni za FIFA hazirusu

Timu ya Sungura FC Bingwa wa ligi Daraja la Tatu Mkoa wa Mbeya, Kutoka Wilayani Kyela imenyang'anywa ushiriki wa ligi ya Mabingwa Wa Mikoa kwa Sababu ya kuko...

Kwa unavyoliona Kundi hilo unadhani Tutatoboa Kwenda Hatua inayofuata?1.TANZANIA2.UGANDA3.TUNISIA4.NIGERIAComment tutapi...
28/01/2025

Kwa unavyoliona Kundi hilo unadhani Tutatoboa Kwenda Hatua inayofuata?

1.TANZANIA
2.UGANDA
3.TUNISIA
4.NIGERIA

Comment tutapitia kwenye saa 10:00-01:00 Mchana.

🛑LIVE: Kyela fm Radio Tupo Live kwenye UCHAGUZI MKUU CHADEMA LEO MLIMANI CITY. 🛑 Sikiliza Kupitia   na Tizama Live Kupit...
21/01/2025

🛑LIVE: Kyela fm Radio Tupo Live kwenye UCHAGUZI MKUU CHADEMA LEO MLIMANI CITY. 🛑 Sikiliza
Kupitia na Tizama Live Kupitia Account yetu ya YOUTUBE Bofya 👇

Endelea kutufuatilia Kupitia Kyela Fm DigitalFacebook: KyelafmRadioInstagram: Kyelafmradio

Helloooo MWANAKWETU,👋 Baada ya vikao vya Muda mrefu vya mipango na mikakati Kwaajili ya  Mwaka 2025 Sasa HESABU ZIMEKUBA...
05/01/2025

Helloooo MWANAKWETU,👋 Baada ya vikao vya Muda mrefu vya mipango na mikakati Kwaajili ya Mwaka 2025 Sasa HESABU ZIMEKUBALI✅
Rasmi Kuanzia Juma 3 Hii 06/01/2025 Kyela FM Tumejiandaa vyakutosha Kuhakikisha Tunakupa Kampani MWANAKWETU kwakuwa nawe bega kwa bega katika Safari Yako kuelekea Ushindi.
Tumekubaliana Kuisikia SAUTI YAKO nakuitumia kushiriki Mchakato Wa kujenga msingi wa MAFANIKIO yako Kwa sababu Sasa tumeshaKUWA ZAIDI na safari yetu inasubiri kushiriki nawe HATUA yako nyingine...
Wewe na sisi tukiwa na mdundo mmoja, 2025 HATUA KWA HATUA. 📻

Tuambie Ukweli X-Mass ya mwaka huu Imekukuta Ukiwa Wapi!?
24/12/2024

Tuambie Ukweli X-Mass ya mwaka huu Imekukuta Ukiwa Wapi!?


Jeshi la Polisi Nchini limetoa onyo na kupiga marufuku maandamano yaliyotangazwa na Viongozi wa CHADEMA September 23,202...
13/09/2024

Jeshi la Polisi Nchini limetoa onyo na kupiga marufuku maandamano yaliyotangazwa na Viongozi wa CHADEMA September 23,2024 na kusema Mtu yeyote atakayeingia barabarani atakabiliwa vilivyo kwa mujibu wa sheria za Nchi.

Akiongea Mjini Moshi leo September 13,2024, Msemaji wa Polisi, David Misime amesema “September 11,2024 kupitia Vyombo vya Habari na Mitandao ya Kijamii walisikika Viongozi wa CHADEMA akiwemo Mwenvyekiti wa Chama hicho (Freeman Mbowe), akiwahamasisha Viongozi wa Dar es salaam kuingia barabarani kuanzia September 23,2024, Viongozi hao waliendelea kuhamasisha Wananchi wa Kanda mbalimbali Nchini kukutana Dar es salaam ili kuungana na Wakazi wa Dar es salaam kuingia barabarani”

“Hatua hiyo waliyofikia tunajiuliza na tunaendelea kufuatilia na kuchunguza kwanini wanataka kututoa kwenye reli ya hatua za kiupelelezi zinazoendelea baada ya Rais Samia kuviagiza Vyombo vya Uchunguzi vifanye uchungizi kisha wawasilishe uchunguzi kwake”

“Ikumbukwe mara kadhaa Viongozi na Wafuasi wa Chama hicho wamekuwa wakipanga, kuratibu mikakati mbalimbali na kutoa matamshi yenye lengo la kuleta vurugu Nchini ili kuharibu amani ya Nchi yetu kwasababu wanazozijua wenyewe”

“Jeshi la Polisi linatoa onyo kwa Viongozi wa Chama hicho kuacha kuendelea kuhamasisha Wananchi kujihusisha katika uhalifu huo na yoyote atakayeingia barabarani atakabiliwa vilivyo kwa mujibu wa sheria za Nchi, kwa maana hiyo maandamano hayo yamepigwa marufuku, naomba kurudia kwa maana hiyo maandamano hayo yamepigwa marufuku”

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema vitendo vya utekaji na mauaji vinavyoendelea nch...
13/09/2024

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema vitendo vya utekaji na mauaji vinavyoendelea nchini havikubaliki na yeyote na kuongeza kuwa vitendo hivyo vinafanywa na watu aliowaita ‘genge’ la wasioitakia mema nchi.

Dkt. Nchimbi amesema kutokana na hilo, CCM na vyama vya upinzani vinapaswa kuungana pamoja kupinga vitendo hivyo.
"...tunao wajibu mkubwa sana wa kuhakikisha kwamba tunaacha kunyoosheana vidole tunahakikisha kwamba uchunguzi wa kweli na wa kina unafanyika..."Emmanuel Nchimbi - Katibu Mkuu CCM

Address

Kyela
Mbeya
600

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kyela Fm Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kyela Fm Radio:

Share